ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, November 2, 2012

BAHATI CHANDO ON THE WAY TO MISS EARTH BEAUTY QUEEN

'Tanzanian Bahati Chando left Mwalimu Julius Kambarage Nyerere International Airport in Dar es Salaam,Tanzania to represent Tanzania in Miss Earth beauty queen in Manila,Philippines.The competition will be held on 24th November 2012 and beautiful Bahati Chando will be in Manila representing  Tanzania.

MABADILIKO KWA BAADHI YA MAKAMANDA WA MIKOA NA VIKOSI



                                          JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
                                                               WIZARA YA MAMBO YA NDANI
                                                                JESHI LA POLISI TANZANIA


Anuani ya Simu “MKUUPOLISI”
Ofisi ya  Inspekta  Jenerali wa Polisi,
Simu : (022) 2110734 
Makao Makuu ya Polisi,
Fax Na.(022)2135556 
S.L.P. 9141,
Unapojibu tafadhali taja:
DAR ES SALAAM.



02 Septemba 2012

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


MABADILIKO KWA BAADHI YA MAKAMANDA WA MIKOA NA VIKOSI.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IJP Said Mwema, amefanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa Polisi wa mikoa na vikosi.

Mabadiliko hayo ni pamoja na aliyekuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani SACP Ernest Mangu anayekwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza kuziba pengo la marehemu ACP Liberatus Barlow, ACP David Misime aliyekuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Temeke kwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma kuchukua nafasi ya SACP Zelothe Steven anayestaafu. Vilevile, aliyekuwa kamanda wa Polisi Viwanja vya Ndege ACP Ulrich Matei anakwenda kuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani.

Aidha, wengine ni kutoka Makao Makuu ya Polisi na Makao Makuu Idara ya Upelelezi ambapo ACP Engelbert Kiondo kutoka makao makuu Idara ya Upelelezi  anakwenda kuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Temeke, ACP Rashid Seif kutoka Makao Makuu ya Polisi Kwenda kuwa Kamanda wa kikosi cha Tazara, ACP Deusdedit Kato kutoka Makao Makuu ya Polisi kwenda kuwa Kamanda wa Polisi Viwanja vya Ndege, ACP Shaban Hiki kutoka Kamanda wa Kikosi cha Ufundi kwenda Makao Makuu ya Polisi na ACP Lucas Mkondya kutoka Makao Makuu ya Polisi kwenda kuwa Kamanda wa Kikosi cha Ufundi.

Mabadiliko hayo pia yamehusisha aliyekuwa Afisa Mnadhimu wa kikosi  cha Usalama Barabarani  ACP Johansen Kahatano anayekwenda kusimamia  Mradi wa SMARTER Traffic ambapo nafasi yake itachukuliwa na aliyekuwa RTO mkoa wa Pwani ACP Swalehe Mbaga. Uhamisho huo pia umewahusisha baadhi ya Wakuu wa Operesheni wa Mikoa, Wakuu wa Vikosi vya Kutuliza Ghasia vya Mikoa, Wakuu wa Polisi wa Wilaya na Wakuu wa Upelelezi wa Wilaya.

Uhamisho huo ni wa kawaida kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi.


Imetolewa na:
 Advera Senso-ASP
 Msemaji wa Jeshi la Polisi (T).

MATUKIO YA UJAMBAZI WA KUTUMIA SILAHA BADO YAITESA POLISI MWANZA

Siku 18 tangu lilipotokea tukio la mauaji ya aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa wa mwanza liberatus barlow, usiku wa kuamkia leo majira ya saa 8:00 za usiku katika eneo la Nyegezi watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamevamia makazi ya Wakili wa kujitegemea Elias Hezron na kumpigwa risasi  ya tumbo kisha kumpora kompyuta yake ya mkononi (laptop), simu tatu ikiwemo moja ya mkewe na kutokomea kusikojulikana.

Wakili Elias Hezron wa kampuni ya uwakili ya JURISTIC LAW CHAMBER inayo milikiwa na Hon. Justice Nchalla, Outa & Hezron, Partiner Advocte ya jijini Mwanza ambaye amelazwa katika hospitali ya rufaa ya Bugando chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) ambapo hali yake inadaiwa kuwa mbaya hivyo madaktari wanaendelea kumpatia tiba ili kuokoa maisha yake.

Akizungumza na Clouds kwa njia ya simu kaka wa wakili huyo George Hezron ameeleza kuwa tukio hilo lilitokea usiku wa Novemba 2 mwaka huu majira ya usiku baada ya muda mfupi kukatika kwa umeme ambapo wakili huyo akiwa na mkewe walisikia kishindo cha kuvunjwa geti na hatimaye mlango kisha watu wawili wasiotambulika sura zao waliingia ndani  huku wengine wakionekana nje ya nyumba na kumtaka Bw. Elias kuwapatia kompyuta yake ya mkononi, simu zake zote naye kukaidi agizo la watu hao.

"Baada ya kumuamuru na yeye kukataa  kutii kuwapatia kompyuta ndipo mmoja wa watu hao aliamua kumpiga na kitu kizito (nondo) kichwani naye kumkaba mwenzake hali iliyopelekea purukushani na kumzidia nguvu jambazi, ndipo mwenzake alipoamua kutoa silaha na kumfyatulia risasi tumboni kisha kupora vitu walivyohitaji na kumwamuru mke wa wakili huyo pia kuwapatia simu yake ya mkononi na kisha wakatokomea kusikojulikana" Alieleza kwa masikitiko kaka wa wakili huyo.

Bw. George amefafanua kuwa baada ya kupora kompyuta hiyo na simu hizo watu hao walitokomea bila kuchukuwa kitu kingine huku kompyuta iliyochukuliwa ikionekana kuwa na kumbukumbu na nyaraka za kesi mbalimbali ambazo wakili huyo amekuwa akizisimamia kwenye mahakama za mkoa wa Mwanza na mikoa ya jirani hali inayoonyesha kuwa watu hao walikuwa wamekusudia kupora nyaraka hizo.

Kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza Bi. Lilian Matola amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na tayari polisi wanaendelea na uchunguzi wa kina na chanzo cha tukio ikiwa ni pamoja na kuwasaka kwa udi na uvumba watu walio husika. 

FM ACADEMIA KUTOA BURUDANI KWA WAKAZI WA MWANZA JUMAMOSI HII TAREHE 3/11/2012


 JOKERS LIVE PUB ILIYOPO ILOGANZALA PASIANSI JIJINI MWANZA IKISHIRIKIANA NA BIA YA SERENGETI PREMIUM LAGER INAKULETEA WAZEE WA 'NGWASUMA' 
FM ACADEMIA.

WAKISINDIKIZWA NA HILL WAY BAND 'VIJANA WA JUU KWA JUU', FM ACADEMIA WATAMWAGA MVUA YA BURUDANI KWA WAKAZI WA JIJI LA MWANZA 

JUMAMOSI YA TAREHE 3 NOVEMBA 2012 
MUDA KUANZIA SAA 2:00 USIKU HADI MANANE
KIINGILIO NI TSH. 15,000/=
uSiKoSe...

Thursday, November 1, 2012

TOTO YALAMBISHWA SUKARI GURU NYUMBANI

NA ALBERT G. SENGO:MWANZA

 Ikicheza nyumbani Timu ya Toto Africans ya jijini Mwanza leo imefungwa mabao 2-1 na Kagera Sugar toka Bukoba mkoani Kagera katika mchezo wa kiporo ligi kuu soka Tanzania bara ulioahirishwa kuchezwa siku ya jumatano kufuatia mvua kubwa kunyesha na hali ya uwanja wa CCM Kirumba kuwa tete.

Toto ilionyesha uhai kwenye dakika za mwanzo za mchezo na kufanikiwa kupata bao dakika mbili tu tangu kipyenga cha kuanza mchezo kilipo pulizwa mfungaji akiwa ni Peter Mtabuzi.

Dakika ya kumi ya kipindi hicho cha kwanza tayari Kagera Sugar walikuwa wamelifikia lango la Toto na kusawazisha  kupitia Temu Felix.

Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Toto 1, Kagera Sugar 1, goli la ushindi kwa Kagera Sugar lilipatikana mnamo dakika ya 56 mfungaji akiwa ni Daudi Jumanne.

Kocha wa Kagera Sugar Abdalah king Kibadeni amezungumza na Sports Xtra na haya ndiyo aliyosema bofya play hapo chini....
Abdalah Kibadeni

MKUTANO WA VIONGOZI WA MAENEO YANAYOLIMA PAMBA ULIOFANYIKA JIJINI MWANZA LEO

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akitoa mchango wake kwenye mkutano wa viongozi wa maeneo yanayolima zao la pamba uliofanyika jijini Mwanza katika ukumbi wa chuo cha benki kuu leo.

Msimu wa kilimo wa 2011/12, utekelezaji wa kilimo cha mkataba katika maeneo yote yanayolima pamba ambapo asilimia 72 ya wakulima wanaokadiriwa kuwa 500,000 walifunga mikataba na wenye viwanda.

Uzalishaji wa pamba kwa msimu huu unatarajiwa kufikia tani 350,000 hadi tarehe 29 octoba 2012, jumla ya pamba tani 339,000 zimekwishanunuliwa na ununuzi unaendelea katika wilaya za Bariadi, Maswa na Meatu. Hili ni ongezeko la asilimia 50 ikilinganishwa na kiwango cha uzalishaji wa tani 225,000 zilizopatikana msimu wa ununuzi wa 2011/12.
Mkuu wa mkoa mpya wa Simiyu akizungumza na wakulima wa zao la pamba.

Pichani mkulima mwezeshaji Bw. Masalu Mazoya kutoka Magu, akichangia kwenye kusanyiko hilo kutetea wakulima kuendelea na kilimo cha mkataba kwani mnamo Tarehe 20 Octoba 2012, TCA na TACOGA waliamua Kilimo cha mkataba kisitishwe kutokana na matatizo mbalimbali yaliyojitokeza msimu unaomalizika.

Uamuzi huo ulistua Bodi ya Pamba na tarehe 25 Octoba 2012 Baraza la Wakurugenzi liliitisha kikao cha dharula na kuamua kuitisha mkutano baina ya Bodi na viongozi wa maeneo yanayolima pamba, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika na Vyama vya Ushirika uitishwe haraha ili kujadili kwa undani utaratibu utakaotumika kuwafikishia wakulima wa pamba pembejeo katika msimu huu wa kilimo.
Moja kati ya maazimio ya mkutano huo baina ya viongozi wa serikali, ushirika, wakulima na bodi ya pamba ni kuwa Kilimo cha mkataba ndiyo njia ya kuinua uzalishaji na ubora wa pamba hivyo suala hilo liunganishwe na juhudi za kuimarisha Ushirika.

Meza kuu ikizungumza na kusanyiko hilo lililohusisha wakuu wa mikoa na wilaya mbalimbali kanda ya ziwa walioketi pamoja na wakulima wa zao la pamba

Mmoja kati ya wakulima wa zao la pamba akichangia kwenye kusanyiko hilo.

Bodi ya pamba Tanzania imeanza kusambaza mbegu mpya aina ya UKM 08 kwenye magereza na kwa wakulima wa zao la pamba waanze kuitumia katika msimu wa kilimo mwaka huu baada ya mbegu hiyo kufanyiwa utafiti wa kina na kuthibitishwa kufaa kwenye Chuo cha Utafiti a Kilimo cha Ukiliguru kilichopo wilayani Misungwi mkoani Mwanza.

Mkurugenzi mkuu wa Bodi ya Pamba Tanzania Bw. Marco Mtunga akieleza wajumbe wa kikao cha wadau wa pamba kutoka wilaya zinazolima zao hilo kwenye ukumbi wa Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania jijini Mwanza, amesema kuwa hivi karibuni mbegu hizo mpya za pamba zisizokuwa na manyoya kutoka Ukiriguru zilizofanyiwa utafiti tangu mwaka 2008 na kuthibitishwa kuwa na ubora zitaanza kutumiwa na wakulima katika baadhi ya maeneo yakiwemo Gereza la Malya, Magu na Mahango ili kuongeza uzalishaji wa mbegu hizo kwa nia ya kufikia malengo
Bw. Mtunga amesema kuwa baadhi ya makampuni ambayo yamekuwa hayapeleki kwa wakati pembejeo za kilimo kwa wakulima na kusababisha wakulima kushindwa kuendana na kalenda ya kilimo kwa wakati, Bodi ya Pamba itachukuwa hatua.

BALOZI WA KINYWAJI CHA HENNESSY KUTEMBELEA DAR ES SALAAM TAR 13 NA 14

Kampuni ya Hennessy leo imetangaza ujio wa balozi wake, Bwana Cyrille Gautier Auriol hapa Dar es Salaam tarehe 13 na 14 ya mwezi huu.
Bwana Auriol anakuja Dar es Salaam kwa matukio kadhaa ya kukutana na wapenzi wa kinywaji cha Hennessy, lakini pia ataongoza uonjaji wa kinywaji hicho, chakula cha usiku na ufunguzi wa club mpya ya Hennessy 327.

SHINDANO LA UNIQUE MODEL 2012 LAZINDULIWA RASMI @HOLIDAY IN HOTEL JIJINI DAR


SHINDANO LA UNIQUE MODEL LAZINDULIWA KWA KISHINDO HOLIDAY INN JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Shindano la kumsaka mwanamitindo mwenye vigezo vya kipekee nchini Tanzania(unique model) linaloandaliwa na Unique Entertainment limezinduliwa leo jumatano kwa kishindo katika hoteli ya Holiday Inn iliyopo katika ya jiji la Dar es salaam mbele ya waandishi wa habari. 

Akizungumza na waandishi wa habari hao katika ufunguzi huo mkurugenzi wa shindano hilo Bw. Methuselah Magese amesema kuwa mchakato wa shindano umefunguliwa rasmi ili kutoa fursa ya wadhamini kujitokeza kwa wingi kudhamini shindano hilo ambalo litakuwa na mvuto wa aina yake kwa msimu huu wa pili.

Pia wanamitindo wenye sifa za kimataifa wameombwa kujitokeza kwa wingi katika usaili utakaofanyika tarehe 18 novemba katika hoteli ya Lamada Apartments.

 Tumeboresha shindano kwa kiwango cha hali ya juu tofauti na ilivyokuwa hapo awali,lengo ni kulifanya shndano hili liwe la heshima,hadhi na linalotimiza lengolake la kuvumbua na kuinua vipaji vya wanamitindo wa kchipikizi.

Tunaomba wabunifu wadogo kwa wakubwa wajitokeze kuja kuonyesha umahili wao katika shindano hili ambapo mwaka huu tutakutanisha wabunifu wengi wa mavazi nchini Tanzania katika shindano moja kwa lengo la kuwainua wabunifu wadogo na kuendelea kuwatangaza wabunifu wenye majina makubwa katika tasnia ya mitindo hasa katika kipindi hiki maridhawa cha mwisho wa mwaka” alisisitiza Magese.

Katika msimu huu wa pili wa unique model kutakuwa na nyongeza ya mataji mengine madogo matatu amabayo ni “model photogenic2012”,”model talent 2012” na “model with good manner 2012” ambapo mataji hayo yatakuwa chini ya taji kuu la “Unique model of a year 2012”.

Fainali za shindano la Unique model 2012 zitafanyika mwishoni mwa mwezi Desemba ambapo kamati ya maandalizi imedhamilia kufanya onyesho lenye hadhi kuanzia ubora wa washiriki wenye vigezo vya uanamitindo ambao wataleta mabadiliko katika tasnia ya mitindo nchini.

Shindano la Unique model lilianzishwa mwaka 2010 ambapo kwa mwaka huu ni mara ya pili kufanyika,Asia Dachi ndiye mwanamitindo anaeshikilia taji hilo mpaka sasa.

Wito umetolewa kwa makampuni kujitokeza kuchukua mabalozi ambao ni wanamitindo washiriki kwa lengo la kufanya nao kazi za kutangaza bidhaa ama huduma inayotolewa na kampuni husika kwa lengo la kutoa ajira kwa wanamitindo hao wanaochipukia katika tasnia.

Unique model 2012 imedhaminiwa na Dtv,Gazeti la Tanzania Daima,Mashujaa investment ltd, Sophernner Investment co ltd, K.d.surelia, Young don records, Kiu investment ltd, Oriental bureau de change,100.5 Times fm,J’s professional ltd, Lamada apartments hotel, na Unique entertainment blog.

Wednesday, October 31, 2012

MTOTO ALIYEANGUKIWA NA UKUTA AKIWA NA WAZAZI WAKE AFARIKI DUNIA

Mwenyekiti wa mtaa wa Ngara Kirumba eneo la mlimani 'B' Bw. Thadeo Katalala akisimulia tukio hilo.


Mtoto  Asfati Mslam amefariki dunia leo majira ya saa 9 na dakika kadhaa alasili katika hospitali ya mkoa wa Mwanza, Sekou Toure alikokimbizwa yeye na wazazi wake mara baada ya kuumizwa vibaya kwa kuangukiwa na ukuta wa nyumba yao kupitia mawe yaliyoporomoka kutoka kwenye msingi wa nyumba iliyo eneo la juu mlimani jijini Mwanza. 

Kuangukiwa nyumba hiyo ni tukio lililotokea leo hii majira ya asubuhi saa 5:45 katika nyumba wanayoishi kilima cha Sabato mtaa wa Ngara eneo la Mlimani 'B' Kirumba jijini Mwanza ambapo pamoja na kwamba ni majira ya mchana watu hao  mke na mume walikuwa wamejipumzisha chumbani wakiwa na mtoto wao, (yawezekana kutokana na hali ya hewa kwa mvua inayoendelea kunyesha leo tangu asubuhi hadi muda huu tunakupa taarifa) ndipo wakakutana na ajali hiyo.

 Msingi wa nyumba iliyo eneo la kimo cha juu toka nyumba iliyovunjwa ukuta na kutokea ajali.


 Wananchi wakiwa wameizingira nyumba liyovunjwa ukuta na kusababisha dhahma hiyo iliyo ondoa uhai wa mtoto Asfati Mslam huku wazazi wake wakiwa katika hali taabani hospitali ya Sekou Toure jijini Mwanza.

 Hii ndiyo nyumba ambayo kuta zake zilibomolewa na mawe ya msingi wa nyumba iliyo juu yake.


 Mashuhuda wakiwa wameambatana na mwenyekiti wa mtaa wa Ngara Kirumba eneo la mlimani 'B' Bw. Thadeo Katalala.


Kaburi la Asfati.
Mtoto  Asfati Mslam amezikwa leo jioni kwenye makaburi ya waislamu Ngara Kirumba eneo la Mlimani 'B'.

WATUHUMIWA KESI YA MAUAJI KAMANDA WA POLISI MWANZA WAFIKISHWA MAHAKAMANI LEO

Zoezi la utambuzi wa wahusika wa mauaji.
Watuhumiwa watano wa mauaji ya aliyekuwa kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Liberatus Barlow leo majira ya mchana saa 8:55 wamefikishwa mahakamani chini ya ulinzi mkali kusomewa mashitaka yanayowakabili.

Watu hao ni Muganyizi Michael Peter (36), Chacha Waitare Mwita (50), magige Mwita Marwa (48), Bugazi Edward Kusuta pamoja na Bhoke Marwa Mwita (42).

Akisoma mashitaka mbele ya Hakimu mfawidhi wa serikali Kastus Ndamugobi amesema kuwa watuhumiwa hao wanakesi ya jinai la Mashitaka ya mauaji namba 30 kifungu cha 196 na 197 cha kanuni ya adhabu ya sheria iliyofanyiwa marekebisho ya mwaka 2002, kwani mnamo October 13 usiku walishirikiana kumuua mtu mmoja aitwaye Liberatus Barlow katika eneo la Minazi Mitatu Kitangili wilayani Ilemela jijini Mwanza.

Mwendesha mashitaka huyo akitaja kuwa upelelezi bado ungali ukiendelea ameiomba mahakama kuahirisha kesi hiyo.

Ombi hilo limekubaliwa na sasa kesi hiyo imepangwa kusomwa tena tarehe 15 November 2012.  

Watuhumiwa hao waliondoka eneo hilo la mahakama chini ya ulinzi mkali huku wakiwa wamemshikilia huku na huku mtuhumiwa mwenzao Muganyizi Michael Peter (aliyetajwa na wenzie kuwa ndiye aliye mpiga risasi na kumuua Kamanda Barlow) anayetembea kwa taabu.

BANK OF AFRICA TANZANIA SASA KUSHIRIKIANA NA AIRTEL TANZANIA KATIKA KUTOA HUDUMA YA AIRTEL MONEY NA UTOAJI MIKOPO KWA WASAMBAZAJI WAKUBWA WA HUDUMA YA AIRTEL MONEY

Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando (kushoto) akiongea wakati  wa uzinduzi wa ushirikiano wa kampuni ya simu za Mkononi ya Airtel na Bank of Afrika katika kutoa huduma ya Airtel money kupitia matawi ya bank hiyo yote yaliyopo Tanzania. Uzinduzi huo ulifanyika jana katika Makao makuu ya Airtel Morocco Jijini Dar es Salaam. pichani kulia ni mkuu wa kitengo cha IT Bank of Afrika bwn. Willington Munyanga , akifatiwa na  Mkuu wa huduma za kibenki Mwanahiba Mzee  na anayefatia ni Meneja Airtel Money John Ndunguru.


Meneja Airtel Money John Ndunguru na Mkuu wa huduma za kibenki Mwanahiba Mzee  kwa pamoja wakikabidhiana mikataba mara baada ya makubaliano ya ushirikiano  wa Airtel na Bank of Afrika katika kutoa huduma ya Airtel money kupitia matawi ya bank hiyo yote yaliyopo Tanzania. Makabidhiano hayo yalifanyika jana katika Makao makuu ya Airtel Morocco Jijini Dar es Salaam. wakishuhudia Katikati ni Mmoja ya wakala mkubwa wa Airtel money kutoka kampuni ya Connexions bwn Shyamkumar Balakrishnan (katika) na kushoto ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando

Meneja Airtel Money John Ndunguru na Mkuu wa huduma za kibenki Mwanahiba Mzee wakipitia mkataba mara baada ya makubaliano ya ushirikiano  wa Airtel na Bank of Afrika katika kutoa huduma ya Airtel money kupitia matawi ya bank hiyo yote yaliyopo Tanzania.


BANK OF AFRICA TANZANIA SASA KUSHIRIKIANA NA AIRTEL TANZANIA KATIKA KUTOA HUDUMA YA AIRTEL MONEY NA UTOAJI MIKOPO KWA WASAMBAZAJI WAKUBWA WA HUDUMA YA AIRTEL MONEY

Dar es Salaam, 30 Oktoba 2012

Huduma bora na ubunifu wa huduma mpya zinazokidhi matarajio ya wateja ni moja ya silaha muhimu katika kukuza wateja waliopo pamoja nakuongeza idadi ya wateja wapya, Kutokana na msingi huu BANK OF AFRICA TANZANIA ina furaha kuanzisha ushirikiano na AIRTEL TANZANIA katika kutoa huduma ya Airtel money kupitia matawi yake yote yaliyopo Tanzania.
Ushirikiano huu wa kibiashara unatoa fursa kwa wasambazaji wa huduma za Airtel Money kupata PESA za mtandao pasipo usumbufu wowote. Katika tukio la leo baina ya BANK OF AFRICA na AIRTEL TANZANIA tunapenda pia kutangaza uanzishwaji wa mikopo kwa wasambazaji wa Airtel money ili kukuza mitaji itakayowawezesha kulikabili soko  shindani la biashara hii.
Makubaliano haya yanayotiwa saini leo yanaendelea kuboresha huduma za kifedha zitolewazo kupitia mitandao ya simu za mkononi kupitia BANK OF AFRICATANZANIA. Ushirikiano huu wa Huduma ya Airtel money unawalenga mawakala wakubwa na wa kati pamoja na wasambazaji wadogo  wa Airtel Money  katika kupata pesa za mtandao zitakazowawezesha kuendesha biashara zao kwa ufanisi zaidi, sambamba na hilo pia Mawakala na wasambazaji wa Airtel Money watapatiwa mikopo itakayowawezesha kukuza biashara zao, mikopo hiyo itakuwa kati ya shilingi  Millioni 10 hadi 100.

Kwa upande wake Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Airtel Money Godfrey Mugambi amesisitiza kwamba  ushirikiano wa Airtel Tanzania na BANK OF AFRICA TANZANIA  ni moja ya mkakati wa kampuni yake katika kuendelea kuboresha na kufikisha huduma za kifedha nchini kote. Hii ni njia rahisi sasa itakayowawezesha wasambazaji wetu wa Airtel Money wakubwa kuwafikia mawakala wengi na kuokoa muda na  gharama walizokuwa wanazipata kutafuta  pesa za mtandao. Airtel inatambua ongezeko la mahitaji ya huduma za kifedha zenye usalama, uhakika, katika soko la Tanzania na ni kwa sababu hizi  Kampuni ya Airtel imeingia makubaliano na BANK OF AFRICA TANZANIA kutoa huduma ya Airtel Money  nakurahisha zaidi upatikanaji wa huduma hii kwa wateja.

Huduma za Airtel Money  zitawawezesha  makundi yote nchini yaani yale yaliyofikiwa na taasisi za kifedha kama mabenki  na yasiyo fikiwa na mabenki kupata huduma za kifedha kwa  urahisi Kupitia mtandao wa simu ya mkononi.

Aidha Huduma ya Airtel Money inatoa fursa kwa taasisi, mashirika mbalimbali, kujenga uwezo wa matumizi makubwa ya teknologia ikiwa ni pamoja na kurahisisha huduma za mfumo wa malipo kwa ajili ya bidhaa au huduma mbalimbali.

Huduma za Airtel Money zinapatikana nchi nzima kwa wateja wote wa malipo ya kabla na ya baadaye,  Airtel money ina  mawakala zaidi ya elfu 20,000 nchi nzima  wakitoa huduma mbalimbali ikiwemo kuwaunganisha  Wateja na huduma ya Airtel Money bure bila ya malipo ya uandikishwaji.

Historia Fupi ya BANK OF AFRICA
BANK OF AFRICA ilifungua milango yake kwa wateja kwa mara ya kwanza mnamo mwaka  1982 ikiwa na makao yake makuu  Bamako, Mali. Kwa sasa kundi hili la mabenki lina wafanyakazi wapatao  4,000  ambao wanafanya kazi  katika nchi  15 .

BANK OF AFRICA kwa sasa inafanya shughuli zake  katika nchi za Africa   na barani Ulaya  zikiwemo  Benin, Burkina Faso, Burundi, Djibouti, DRC, France, Ghana, Ivory Coast, Kenya, Madagascar, Mali, Niger, Senegal, Tanzania pamoja na  Uganda. BANK OF AFRICA imejipanga na inatambulika zaidi kwa ubora wake katika maeneo yafuatayo 

  • Huduma bora kwa wateja
  • Wafanyakazi hodari na wanaofikika kwa Urahisi
  • Uimara wa mtaji
  • Mtandao wa matawi unaokua kwa kasi
  • Utaalamu wa  uboreshaji wa huduma za kifedha
  • Wawekezaji wa uhakika

BANK OF AFRICA ina wawekezaji  wa uhakika ambao ni pamoja na  BMCE Bank (Banque Marocaine du Commerce Exterieur - BMCE), PROPARCO, IFC (International Finance Corporation), West African Development Bank, Netherlands Development Finance (FMO), Belgium Investment Company for Developing Countries (BIO) and investment fund AUREOS. 
BANK OF AFRICA TANZANIA  ina mtandao wa matawi 17  ambapo  10 yanapatikana mkoani Dar es Salaam na   mengine 7 katika mikoa ya  Arusha, Mwanza, Kilimanjaro (Moshi), Morogoro (Morogoro mjini na  Mtibwa), Mbeya na Tunduma.

PATA HABARI ZA KAJUNASON BLOG KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI KWA SMS, TUMA NENO KB KWENDA 15678

Wakati ndiyo huu kwa wasomaji wa KAJUNASON BLOG (www.kajunason.blogspot.com), Pata Habari Moto Moto kutoka Kajunason Blog kupitia simu yako ya Mkononi (SMS). Kujiunga Tuma neno KB KWENDA 15678. NAWASHUKURUNI SANA KWA WALE AMBAO TAYARI WAMEJIUNGA. HUDUMA ITAANZA HIVI PUNDE. UKISIKIA HABARI NJEMA HII MJULISHE NA MWENZAKO.

JIWE LACHOMOKA TOKA MLIMANI MWANZA NA KUANGUKIA NYUMBA


Watu watatu akiwemo mtoto mdogo wamekimbizwa hospitali ya mkoa Sekou Toure mara baada ya kuumizwa vibaya kwa kuangukiwa na ukuta wa nyumba yao kupitia jiwe lililoporomoka kutoka mlimani jijini Mwanza.

Waliokumbwa na ajali hiyo ni Bw. Msalam Husein(30) ambaye ni  dereva  na mkewe Bi. Nadia Grecian(25) ambaye ni mama wa nyumbani  pamoja na kichanga wao Asfati Mslam (aliyechini ya umri wa mwaka).

Tukio hilo limetokea leo hii majira ya saa 6:00 mchana katika nyumba wanayoishi kilima cha Sabato mtaa wa Ngara eneo la Mlimani B Kirumba jijini Mwanza ambapo pamoja na kwamba ni majira ya mchana watu hao  mke na mume walikuwa wamejipumzisha kitandani, (yawezekana kutokana na hali ya hewa kwa mvua inayoendelea kunyesha leo tangu asubuhi hadi muda huu tunakupa taarifa) ndipo wakakutana na ajali hiyo.

Kwa mujibu wa  Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya jinai wilaya ya Ilemela  (OC-CID) Afande Magesa amesema kuwa hali ya Msalam Husein ni mbaya kwani amekimbizwa hospitali akiwa ajitambui huku mkewe akiwa akilia kwa maumivu makali kufuatia ajali hiyo.

Taarifa ya tukio hilo ilichelewa kufika polisi kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha lakini hata hivyo polisi walifika eneo la tukio na kutoa msaada kwa kuwakimbiza hospitalini wajeruhiwa hao.

Tunaendelea kufuatilia tukio hilo kwa karibu kujua hali za watu hao.




Tuesday, October 30, 2012

13 WAFARIKI KUTOKANA NA KIMBUNGA SANDY




Mojawapo ya vimbunga vikubwa zaidi kuwahi kupiga Mashariki mwa Pwani ya Marekani kimesababisha mafuriko makubwa katika baadhi ya sehemu za mji wa New York.
Maeneo mengi mjini yamewachwa katika giza baada ya huduma za umeme kukatizwa.
Kimbunga hicho kilipiga ardhi kwenye Pwani ya New Jersey karibu na mji wa Atalanta muda mfupi jana usiku/Dhoruba kali kutoka mjini Florida hadi nchini Canada imepiga Mashariki mwa Marekani na kusababisha mawimbi makali mjini New York.

Maji yamefurika kwenye barabara na katika njia za reli pamoja, maeneo ya kuegesha magari na katika eneo la Ground Zero, eneo ambalo mashambulizi ya Septemba kumi na moja yalitokea.

Sehemu kubwa za mji wa New York ziko kwenye giza baada ya milingoti ya umeme kuharibiwa.

Wagonjwa waliondolewa kwenye hospitali moja baada ya umeme kukatika.
Zaidi ya watu milioni tano walisemekana kukosa umeme katika eneo la Pwani baada dhoruba kali huku takriban wengine milioni moja wakishauriwa kuhama nyumba zao. Athari za kimbunga hicho labda huenda zikajulikana baadaye leo.

 CHANZO: bbc swa

MAOFISA WAKUU WAANDAMIZI WA JESHI LA POLISI WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO NCHINI UJERUMANI

Mmoja wa Maofisa wa Polisi akielekeza jambo kwa Kamanda Wa Kikosi cha Usalama Barabarani, SACP Mohamed Mpinga (tatu shoto) ,ACP Kilonzo kutoka makao makuu ya jeshi la Polisi (mwenye miwani) pamoja na ASP Msuyale ( wa tatu mstari wa nyuma) wote kutoka nchini Tanzania,kuhusiana na mambo ya usalama barabarani.

Maofisa hao wakuu waandamizi wa jeshi la polisi kutoka nchini Tanzania walikuwa nchini Ujerumani kwa ziara ya mafunzo ya wiki moja (21/10 - 27/10/20120),katika jimbo la Lower Saxon,ambapo pia walitembelea Mji mkuu wa jimbo hilo Hannover, Neunberg, na Gottingen. 

Aidha ziara hiyo ilihusisha mambo mbalimbali ya usalama barabarani ikiwemo kuangalia upimaji mwendo kasi kwa kutumia mtambo maalum unaopiga picha, na rader ya kawaida, ukaguzi wa malori ya mizigo na mambo mengine mengi..
Mmoja wa Maofisa wa Polisi (mwenyeji) akiwaelekeza jambo kwa Kamanda Wa Kikosi cha Usalama Barabarani,SACP Mohamed Mpinga,ACP Kilonzo  pamoja na ASP Msuyale (wote watatu pichani kati) namna ya matumizi  mbalimbali ya usalama barabarani.
Mmoja wa Maofisa wa Polisi akimuelekeza Kamanda Wa Kikosi cha Usalama Barabarani, SACP Mohamed Mpinga namna ya kuangalia upimaji mwendo kasi kwa kutumia mtambo maalum unaopiga picha kuhusiana na uendeshaji magari barabarani.
Kamanda Wa Kikosi cha Usalama Barabarani,SACP Mohamed Mpinga,ACP Kilonzo  pamoja na ASP Msuyale wakielekezwa namna ya leseni za madereva zinavyokuwa. 
Maofisa wa juu wa kutoka jeshi la polisi nchini Tanzania, Kamanda Wa Kikosi cha Usalama Barabarani,SACP Mohamed Mpinga,ACP Kilonzo  pamoja na ASP Msuyale (wote watatu pichani kati) wakiwa katika picha ya pamoja na wenyeji wao.Picha zote kwa hisani ya SACP Mohammed Mpinga - CO Traffic.