ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 13, 2020

OCODE YAMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI KWA KUWAJENGEA DARASA JIPYA WANAFUNZI WA KIBWEGERE

 Mkurugenzi wa shirika la Ocode Joseph Jackson wa kati kati akiwa na Mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya ubungo Beatrice Dominic  wa kushoto pamona na Afisa elimu wa manispaa hiyo  kulia wakiwa wameshikilia upete kwa ajili ya kuukata ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa darasa moja la wanafunzi wa elimu ya awali Kibwegere ambalo limetolewa na shirika la  Ocode kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Baadhi ya wanafunzi wanaosoma katika shule ya msingi Kibwegere elimu ya awali wakiwa wameketi katika madawati ambayo yametolewa kwa msaada wa shirika la Ocode katika halfa ya makabidhiano yaliyofanyika katika viwanja vya shule hiyo manispaa ya ubungo Jijini Dar es Salaam/(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Mkurugenzi wa Shirika la Ocode Joseph Jackson akizungumza na baadi ya walimu, wanafunzi wa shule ya msingi Kibwegere hawapo pichani wakati wa halfa ya makabidhiano ya uzinduzi wa darasa jipya ambalo limejengwa kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya awali kwa ajili ya kuwasaidia waweze kusoma katika mazingira ambayo ni rafiki.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Ubungo Beatrice Dominic akifafanua jambo kwa walimu na wanafunzi ambao walihudhulia katika halfa fupi ya makabidhiano ya chumba cha darasa jipya ambacho kimejengwa kwa ajili ya kusomea watoto wa elimu ya awali.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Mkuu wa Shule ya Msingi Kibwegere Charles Kulemba akisoma Risala mbele ya mgeni rasmi wakati wa halfa ya uzinduzi huo wa darasa jipya mablo limejengwa mahusus kwa ajili ya watoto wadogo wanaossoma katika ngazi ya awali.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Mmoja wa walimu ambao wanawafundisha wanafunzi wa elimu ya awali Bi. Eunice Matembo akisoma Risala yake kwa mgeni rasmi amabye ni  Mkurugenzi mteandaji wa Manispaa ya Ubungo hayupo picha wakati wa halfa hiyo ya makabidhiano ya madawati, viti pamoja na uzinduzi rasmi wa darasa hilo la wanafunzi wa awali.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Ubungo Beatrice Dominic wa katikati akijadiliana  jambo na mwalimu mkuu wa Shule hiyo ya Kibwegere pamoja na watumishi wengine wa Ocode na serikali wakati wa halfa hiyo ya makabidhiano wa misaada mbali mbali ikiwemo meza pamoja na viti kwa ajili ya kukalia walimu.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Msingi Kibwegere wakiwa wanasikiliza hotuba ambayo ilikuwa inatolewa na Mkurugenzi wa shirika la Ocode Joseph Jackson hayupo pichani wakati wa sherehe ya uzinduzi wa darasa  jipya ambalo limejengwa kwa ajili ajili ya kuwasaidia watoto wa elimu ya awali.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Baadhi ya watendaji wa Shirika la Ocode wakiwa wameketi kwa utulivu wakifuatilia hotuba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Beatrice Dominic hayupo pichani wakati wa halfa hiyo ya uzinduzi wa darasa moja jipya lililojengwa kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya awali.(PICHA NA VICTOR MASANGU)

Pichani ni kibao ambacho kinaonyesha shule ya msingi Kibwegere iliyopo katika Manispaa ya Ubungo iliyopo Jijini Dar es Salaam.abpo shule hiyo imepatiwa msaada wa madawati, 39 viti 13 vya walimu pamoja na kukabidhiwa darasa jipya kwa ajili ya watoto wa elimu ya awali lililotolewa na shirika la Ocode na kughalimu kiasi cha shilingi milioni 24 (PICHA NA VICTOR MASANGU)
NA VICTOR MASANGU, UBUNGO
SEKTA ya elimu hapa nchini licha ya serikali ya awamu ya tano kuweka  sera ya kutoa elimu bure lakini bado katika baadhi ya maeneo ya shule za msingi na Sekondari zilizopo katika Manispaa ya Ubungo Jijini Dar es Salaam zinakabiliwa na changamoto mbali mbali ya upungufu wa matundu ya vyoo pamoja  na uhaba na uchakavu wa  miundombinu ya madarasa hivyo kusababisha wanafunzi wengine kusoma katika mlundikano mkubwa.
Katika kuliona hilo Shirika lisilokuwa la kiserikali la Organization Community Development (OCODE)  limeamua kumuunga mkono Rais wa awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli katika kuboresha sekta ya elimu kwa kutoa msaada wa madawati 39,ya wanafunzi, viti 13 vya kukalia walimu pamoja na kukabidhi rasmi chumba cha darasa moja jipya  kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya awali katika shule ya msingi Kibwegere.
Akizungumzia kuhusiana na msaada huo Mkurugenzi wa Shirika la Ocode Joseph Jackson amesema kwamba kwa sasa wana tekeleza mradi wa elimu ambao utakuwa wa  kipindi cha miaka mitano ambao umeanza kufanyika tangu 2019- 2023 kwa lengo la kuwez kuwasaidia watoto wa shule za awali na msingi katika kuwawekea mazingira mazuri katika suala zima la upatikanaji wa kupata elimu iliyo bora kwa manufaa yao ya baadae.
 Aidha Mkurugenzi huyo alibainisha kwamba katika mradi huo umeweza kugusa ujenzi wa darasa hilo jipya la wanafunzi wa elimu ya awali ambalo mpaka kukamilika kwake limegharimu kiasi cha shilingi milioni 26 na kwamba wana imani kuwa watoto hao kwa sasa waliokuwa wanakabiliwa na changamoto ya kukaa kwa mlindikano watasoma katika mazingira ambayo ni rafiki kwao

“Shirika letu la Ocode kwa sasa linaendelendea kutekeleza program ya mradi wa elimu ambao utakuwa unazigusa baadhi ya shule za msingi ambazo zipo katika maeneo mbali mbali ya Jiji la Dar es salaam, maana nia yetu ni kuwasaidia watoto hawa kuanzia elimu ya awali na kwamba kwa sasa tutajikita zaidi kwa wanafunzi wa daras ala kwanza na darasa la pili pamoja na wale wanafunzi wa ngazi ya awali ili kuweza kuwajengea uwezo wa kupata elimu bora,”alisema Mkurugenzi huyo.
Pia alibainisha kwamba katika kipindi cha utekelezaji wa mradi huo kwa kipindi cha miaka mitano watahakikishwa kwamba wanashirikiaa bega kwa began a serikali ya awamu ya tano pamoja na wadau wengine wa maendeleo ili kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kupitia elimu kuanzia ngazi za chini na kuendelea.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Kibwegre  akisoma risala kwa mgeni rasmi katika halfa ya makabidhdiano ya madawati na  uzinduzi wa  darasa hilo amebainisha kwamba kwa sasa wanafanya kazi katika mazingira magumu sana kutokna na ukosefu wa ofisi za walimu na vyumba vya madarasa ambapo wakati mwingine inawalazimu walimu kufanyia kazi zao wakiwa wamekaa chini ya miti hivyo msaada huo ambao umetolewa na Ocode utakuwa ni mkombozi kwa upande wao.
“Shule yetu ya Kibwegere kwa kweli tunapenda kutoa shukrani zetu za kipekee kwa Shirika ili la Ocode kwani wameweza kutuona na kutusaidia katika mambo mbali mbali  ya kutujengea darasa moja, kutupa viti, pamoja na madawati ya wanafunzi hii kwa upande wetu ni moja ya hatua, kwani hapo awali hali ilikuwa ni ngumu kutokana na miundombinu yenyewe ya madarasa pamoja na ofisi za walimu, hivyo napenda kushukuru sana,”alisema Kulemba.
Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Ubungo Beatrice Dominic ambaye alikuwa mgeni rasmi katika halfa ya makabidhiano amesema kwamba pamoja na juhuzi zinazofanywa na serikali lakini amekiri bado kunachanagmoto kubwa ya miundombinu ya madarasa kwa shule ya msingi na sekondari na anatambua walimu wanafanya kazi zao katika mazingira magumu sana hivyo amelipongeza shirika la Ocode kwa kuamua kushirikiana na serikali katika kuboresha sekta ya elimu kuanzia ngazi ya awali.
SHULE ya msingi Kibwegere iliyopo katika Manispaa ya Ubungo nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam  kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 1741 ambao wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo upungufu wa walimu, uhaba wa miundombinu ya madarasa, ofisi za walimu, pamoja na matundu ya vyoo.
                                                          MWISHO .

BENKI YA CRDB YAZINDUA MPANGO MAALUMU WA KUWAWEZESHA WANAWAKE KUSHIKA NAFASI ZA UONGOZI

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa tatu kulia) akiwakiwaonyesha wakurugenzi wengine wa Benki hiyo, moja ya tuzo zenye jumbe mbalimbali, wakati wa uzinduzi wa program maalumu ya kuwawezesha Wanawake (Mentoring Program for empowering Women) ili waweze kushika nafasi mbalimbali za uongozi, iliyofanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Johari Rotana, jijini Dar es salaam jana.


Benki ya CRDB imezindua mpango maalum wa kuwawezesha wafanyakazi wanawake katika nyanja mbalimbali ili  waweze  kushika nafasi za uongozi.

Akizindua mpango huo katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Abdulmajid Nsekela alisema, Mpango huo ni mahususi katika kuwawezesha wanawake wa CRDB Banki ili waweze kuwa viongozi katika nyanja mbalimbali pamoja na kuwafanya waweze kujiamini na kukamata fursa zilizopo.

Mpago huo ni mwendelezo wa maadhimisha ya siku ya Wanawake Duniani, ambapo Benki ya CRDB imeamua kuadhimisha kwa kuzindua program maalum na kuwapa semina wanawake wa Benki ya hiyo.


Aidha Nsekela alisema mpango huo utakuwa endelevu kwani Benki ya CRDB sio tu kuwa inaamini katika nafasi sawa yaani 50/50, bali imeona ni vema kuwa na mpango maalumu kwa kuwafanya wanawake wawe na wigo mpana zaidi kuweza kupambana kwa kujiamini na kushika nafasi na nyazifa mbalimbali za uongozi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Benki hiyo wakati wa uzinduzi wa program maalumu ya kuwawezesha Wanawake (Mentoring Program for empowering Women) ili waweze kushika nafasi mbalimbali za uongozi, iliyofanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Johari Rotana, jijini Dar es salaam jana.
Afisa Biashara Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Benki hiyo wakati wa uzinduzi wa program maalumu ya kuwawezesha Wanawake (Mentoring Program for empowering Women) ili waweze kushika nafasi mbalimbali za uongozi, iliyofanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Johari Rotana, jijini Dar es salaam jana.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa (kulia) akizungumza wakati wa mdahalo ulioenda sambamba na uzinduzi wa program maalumu ya kuwawezesha Wanawake (Mentoring Program for empowering Women) ili waweze kushika nafasi mbalimbali za uongozi, iliyofanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Johari Rotana, jijini Dar es salaam jana.



Wednesday, March 11, 2020

Tuesday, March 10, 2020

UKEREWE WAZINDUA ZOEZI LA KUNYUNYIZIA DAWA YA UKUKO KUPAMBANA NA TISHIO LA MALARIA


Katika tafiti za viashiria vya ugonjwa wa malaria zilizofanyika hivi karibuni mwaka 2017, Mkoa wetu wa Mwanza bado umeonekana kuwa na kiwango kikubwa cha maabukizi ya ugonjwa wa malaria kwa asilimia 8.1. Kiwango hiki kiko juu ya kiwango cha Taifa ambacho ni asilimia 7.3. Aidha matokeo ya upimaji wa vimelea vya malaria kwa watoto wa Shule za Msingi uliofanyika mwaka 2017 na 2019,Wilaya ya Ukerewe ilionekana kuwa na kiwango kikubwa cha watoto wenye vimelea vya malaria kwa asilimia 51 mwaka 2017 na asilimia 44.2 mwaka 2019. Takwimu za Afya zinazotokana na mfumo wa Wizara ya Afya, katika kipindi cha miaka mitatu mfurulizo Wilaya ya Ukerewe imeonekana kuwa na kiwango kikubwa cha wagonjwa waliothibitika kuwa na vimelea vya ugonjwa wa malaria, yaani asilimia 52.6 ya wagonjwa waliotumwa maabara kupima malaria mwaka 2017 walikutwa na vimelea vya malari, asilimia 51.4 kwa mwaka 2018 na asilimia 51.1 kwa mwaka 2019. Kwa hali hiyo ya ukubwa wa tatizo la ugonjwa huo katika Wilaya ya Ukerewe, serikali imeamua kupambana kuongeza afua za kudhibiti malaria katika Wilaya hiyo ambapo safari hii Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella mguu kwa mguu anafanya ziara ya kazi wilayani humo na kushiriki uzinduzi wa zoezi la uangamizaji wa viluviluvi wa Mbu waenezao Malaria kwa kutumia viuadudu vya dawa maarufu ya UKOKO.

RC MWANGELA AAGIZA WAKANDARASI WAWEPO MASAA 24 KATIKA BARABARA ZILIZO HARIBIKA

 Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Songwe wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela kukagua miundombinu ya barabara kufuatia mvua zinazoendelea kunyessha ambapo amewaelekeza wakandarasi wawepo maeneo yote korofi ili kufanya marekebisho ya haraka.
 Eneo la Kanga ambalo miundombinu ya barabara imeharibiwa kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha na kusababisha maji kujaa barabarani, aidha mkandarasi Sanka Building and Civil Engineering ameelekezwa kufanya marekebisho kwa kujaza mawe ili eneo hilo lipitike kwa urahisi.
 Eneo la Kanga ambalo miundombinu ya barabara imeharibiwa kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha na kusababisha maji kujaa barabarani, aidha mkandarasi Sanka Building and Civil Engineering ameelekezwa kufanya marekebisho kwa kujaza mawe ili eneo hilo lipitike kwa urahisi.
Eneo la Kanga ambalo miundombinu ya barabara imeharibiwa kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha, aidha mkandarasi Sanka Building and Civil Engineering ameelekezwa kufanya marekebisho kwa kujaza mawe ili eneo hilo lipitike kwa urahisi.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela amewaagiza wakandarasi  kuwepo masaa 24 katika maeneo yote ya barabara yaliyoharibika kufuatia mvua kubwa zinazoendelea ili kufanya marekebisho ya haraka pale inapobidi.
Akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa, Brig. Jen. Mwangela ametoa agizo hilo mara baada ya kukamilisha kwa ukaguzi wa barabara zote za Mkoa wa Songwe zinazosimamiwa na Wakala wa Barabara Mijini (TANROADS) ili kufanya tathmini ya hali ya barabara Mkoani hapa.
“Barabara zote zina wakandarasi waliokuwa wanaendelea na matengenezo ila walisitisha kufuatia mvua kubwa hivyo nawaagiza wapepo masaa 24 katika maeneo yote korofi kuhakikisha tatizo linapotokea wanarekebisha haraka na barabara ziweze kuendelea kutumika.”, amesisitiza Brig. Jen. Mwangela.
Amesema mpaka sasa mvua bado ni tishio kwakuwa baadhi ya maeneo miundombinu ya barabara imeharibika vibaya huku TANROADS wakishindwa kufanya ukarabati kufuatia mvua hizo hivyo wakandarasi wajikite katika kuweka mawe ili ziweze kutumika na baada ya mvua matengenezo yaendelee.
Brig. Jen. Mwangela ametoa tahadhari kwa watumiaji wa barabara Mkoani Songwe kuwa endapo watakuta maji yamejaa barabarani wasivuke mpaka watakapo jiridhisha kina cha maji hayo huku akitaja baadhi ya maeneo korofi kuwa ni Nkanga Halmashauri ya Wilaya ya Songwe na Msangano  halmashauri ya Wilaya ya Momba.
Ameongeza kuwa wazazi na walezi wasiwaruhusu watoto kucheza, kuvuka au kuogelea katika mito bila usimamizi wao kwakuwa mvua zinazoendelea kunyesha zimepelekea maji kuongezeka katika mito na baadhi ya maeneo ya makazi ya watu.
Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini (TANROADS) Yohani Kasaini amesema kufuatia agizo la Mkuu wa Mkoa watawaita wakandarasi wote haraka na kuwapatia maelekezo hayo pia watahakikisha wanawasimamia.
Kasaini amesema TANROADS kwa kushirkiana na Maafisa Kilimo na Mazingira wamejipanga kutoa elimu kwa wananchi hususani wakulima kuacha kulima pembezoni mwa mito na kuharibu kingo za maji kama walivyofanya katika mto Zila Uliopo Wilayani Songwe na kupelekea kuharibika kwa barabara eneo la Nkanga.
Msimamizi wa Kampuni ya Sanka Building and Civil Engineering Lutufuyo Anyambilile Mwaikeke amesema wamepewa kazi ya kutengeneza barabara ya Chang’ombe-Patamela lakini kutokana na changamoto ya Mvua watafuata agizo la Mkuu wa Mkoa na kujikita katika eneo Nkanga ambalo limeharibika vibaya.
Mwaikeke ameongeza kuwa baadhi ya madereva wamekuwa wabishi kusikiliza maelekezo yao wanapo wakataza kuvuka barabara pindi maji yanapo jaa na hivyo kuleta usumbufu mara wanapokwama.
Naye Mkazi wa Chitete Wilaya ya Momba Thomas Siwiti amesema serikali ijitahidi kuboresha miundombinu ya barabara hususani maeneo ya madaraja kwakuwa yameonyesha kushindwa kuhimili wingi wa maji kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

CHADEMA YAPATA PIGO.

Madiwani wawili wa CHADEMA Jijini Mbeya wamehamia Chama cha Mapinduzi (CCM), Madiwani hao ni Lucas Mwampiki wa Kata ya Mwakibete ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Madiwani wa CHADEMA na Diwani wa Kata ya Itagano, Hussein Wasoha.

VIONGOZI WA CHEDEMA WAHUKUMIWA KULIPA FAINI JUMLA YA SH. MILIONI 350 AU KIFUNGO CHA MIEZI MITANO KWA KILA KOSA


Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu imewahukumu viongozi wanane wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kulipa faini ya jumla ya shilingi milioni 350 au kifungo cha miezi mitano kwa kila kosa baada ya kuwakuta na hatia ya mashtaka 12.

Wabunge John Mnyika, Salum Mwalimu, Ester Matiko na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt Vicent Mashinji, kila mmoja anatakiwa kulipa faini ya Shilingi Milioni 30, na huku, John Heche, Peter Msigwa, Halima Mdee na Ester Bulaya wakitakiwa kila mmoja kulipa Milioni 40.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, yeye akitakiwa kulipa Shilingi Milioni 70 au kwenda jela miezi mitano.

Monday, March 9, 2020

WAWANAWAKE TUGHE PWANI WACHANGIA MSAADA WA CHAKULA KWA WALIOPATWA NA MAFURIKO RUFIJI

 Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi wanawake  wa serikali na afya (TUGHE) Mkoa wa Pwani Catherine Katele kulia akimkabidhi msaada wa magunia ya mahindi Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji Maria Katemana kwa ajili ya kuwapatia wananchi waliopata maafa ya mafuriko kutoka na mvua zilizonyesha hivi karibuni.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Baadhi ya wanawake wa Chama cha Tughe Mkoa wa Pwani wakiwa wanatoa msaada wa mahindi kwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji akiwa ameongozana na viongozi mbali mbali wa serikali kwa ajili ya kuwapatia wananchi ambao mazao yao yamesombwa na maji na wengine nyumba zao kuzingirwa kutoka na mafuriko yaliyotokea.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Wanawake wa chama cha Tughe Mkoa wa Pwani wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbali mbali wa serikali wakiongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji mara baada ya halfa fupi ya kukabidhi magunia ya mahindi lengo ikiwa ni kuwapatia wananchi ambao wamekumbwa na maafa ya mafuriko na kusababisha mazao yao kusombwa na maji.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji Maria Katemana akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wa wanawake wa Tughe Mkoa wa Pwani walipofika ofisini kwake kwa ajili ya kujitambulisha na kutoa msaada wa magunia ya mahindi pamoja na vyakula mbali mbali wa wananchi ambao wanamahitaji kutokana na kupata mafuriko.(PICHA NA VICTOR MASANGU.)
 Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi wanawake wa serikali na afya (TUGHE) Mkoa wa Pwani Catheline Katele akifafanua jambo kwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji hayupo pichani kuhusiana na ujio wao wa kufanya ziara maalumu yenye lengo la kutoa msaada wa vyakula mbali mbali ikiwemo magunia ya mahindi kwa ajili ya wahanga wa mafuriko.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
  Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji Maria Katemana akiwa na wanawake wa Tughe Mkoa wa Pwani wakiwa wanatembea kwa furaha mara baada ya kumalika kwa sherehe ya kutoa msaada wa vyakula mbali mbali ikiwemo magunia ya mahindi ambayo yametolewa kwa ajili ya kuwasaidia wananchi waliokumbwa na mafuriko(PICHA NA VICTOR MASANGU)
 Baadhi ya viongozi wa Tughe Mkoa wa Pwani wakiwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji wa kati kati wakipiga makofi ikiwa ni ishara ya kufurahi mara baada ya kumaliza kutoa msaada wa magunia ya mahinda kwa waananchi waliokubwa na maafa ya mafuriko.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Baadhi ya wanawake wa Tughe Mkoa wa Pwani wakiwa wanaimba nyimbo maalumu mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Rufiji kwa ajili ya halfa ya kukabidhi mahitaji mbali mbali kwa wananchi ambao walipatwa na mafuriko na mazao yao kusombwa na maji na wengine nyumba zao kuzingirwa na maji.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
VICTOR MASANGU, RUFIJI
Baadhi ya wananchi Wilayani Rufiji Mkoa wa Pwani wamekosa makazi ya kuishi kutokana na nyumba zao pamoja na maduka  kuzingirwa na maji  ikiwemo wengine kukumbwa na changamoto ya mazao yao mbali mbali  zaidi ya hekta 4000 kusombwa na maji kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha na kusababisha maafa  hayo ambayo yamepelekea wananchi kuishi katika mazingira magumu  hivyo kupelekea kuishi katika mazingira magumu.
Hayo yalibainishwa  na wananchi hao wakati wa ziara ambayo imefanywa na Wanawake wa  chama cha wafanyakazi wa serikali na afya (TUGHE) Mkoa wa Pwani  yenye lengo la kutembelea  baadhi ya maeneo ambayo yamekumbwa na maafa ya mafuriko  kwa ajili ya  kutoa msaada wa vyakula kwa walengwa.
Wananchi hao wakizungumza kwa nyakati tofauti akiwemo Shamte Ally na Said Salumu walisema walidai kwamba  mvua  ambazo zinaendelea kunyesha kwa kipindi hiki zimewaletea hasara kubwa ya mazao yao, mifugo, pamoja na makazi kuzingirwa na na maji hivyo wameimba serikali ya awamu ya tano kuwasaidia  msaada wa kupata chakula  pamoja na sehemu  kwa ajili ya  kuishi.
Aidha waliongeza kuwa kwa sasa kutokana na kuwepo kwa hali hiyo baadhi ya bidhaa ya vyakula katika maeneo mengine zimepanda bei hivyo wengine kutokana na kipato chao kuwa cha chini wanashindwa kumudu gharama kwa ajili ya kununua vyakula hivyo wameomba wadau mbali mbali kwa kushirikiana na serikali kuliangalia suala hilo kwa jicho  la tatu katika kuwasaidia kuondokana na hali hiyo.
“Kwa kweli ndugu waandishi kwanza tunashukuru sana hawa wakinamama wa Tughe Mkoa wa Pwani kwa kuweza kuja mpaka uku katika maeneo ya Rufiji, kwani kwa sasa tupo katika hali ngumu sana kutokana na mazao mbali mbali ya chakula ambayo ndio tulikuwa tunayategemea sisi pamoja na watoto wetu yote wamesombwa na maji, lakini pia tunashukuru kupatiwa msaada huu lakini bado tunahitaji zaidi ili tuweze kujikimu,” walisema wananchi hao.
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Rufiji Maria Katemana alikiri  kuwepo kwa maafa hayo na kubainishwa kwamba  hadi sasa zaidi ya hekta 4000 za mazao ya aina mbali mbali ikiwemo mahindi mpunga,  yamesombwa na maji ambapo  pia kuna baadhi ya shule nne  za msingi zimefungwa kwa muda kutokana na  kuwepo kwa hali hiyo ya mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
“Kwanza kabisa napenda kutoa shukrani zangu kwa niaba ya serikali ya Wilaya ya Rufiji kwa msaada huu wa chakula cha mahindi ambao umetolewa na Wanawake wa Tughe Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuwasaidia baaadhi ya wananachi amabao wamekumbwa na mafuriko hayo ambayo kwa kweli yamesabisha hekta  zaidi ya 4000 za mazao kusombwa na maji na kuna maeneo mengine ya shule bado maji yapo, hivyo tunaendelea kujitahidi kwa hali na mali ili wanafunzi waweze kuendelea na masomo yao, alisema Maria.
Kufuatia kutokea kwa  maafa hayo ya mafuriko Wanawake kutoka chama cha wafanyakazi wa serikali na afya (TUGHE) Mkoa wa Pwani  wameguswa na tukio hilo na kuamua kwenda kutoa msaada wa vyakula mbali mbali ikiwemo mahindi kwa wananchi ambao wamekubwa na maafa ya  mafuriko hayo kwa lengo la kuwasaidia kuweza kupata chakula ikiwemo kupata mbegu kwa ajili ya kupanda tena kutokana na mazao yao yaliyosombwa na maji.
Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi wanawake  wa serikali na afya (TUGHE) Mkoa wa Pwani Catherine Katele alisema kwamba waliamua kwenda kutembelea baadhi ya maeneo ambayo yamekumbwa na mafuriko  na kutoa msaada wa vyakula kama mahindi ambayo yatawasaidia wananchi kuweza kupata chakula na mengine kuyatumia kwa ajili ya  kupanda mazao mengine ambayo yamekwenda na maji.
“Sisi kama wanawake wa tughe Katika Mkoa wa Pwani kwa kweli tumegiswa sana na jambo hili la wenzetu wa Rufiji kupata maafa ya mafurikio, hivyo ktukaona ni vema tufunge safari ya kuja mpaka huku na kweli tumjionea jinsi ya nyumba mbali mbali ambanzo zimezingirwa na maji na mazao ambayo yamesombwa na maji kwa hiyo kwa hiki kidogo tulichokitoa cha msaada wa mahindi kitaweza kuwasaidia kwa namna moja hama nyingine na pia tutazidi kuendelea kutoa misaada mbali mbali kwa watu wenye mahitaji, “alisema Katele.
Wilaya ya Rufiji iliyopo Mkoa wa Pwani ambayo ina jumla ya kata zipatazo 13 imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya maafa ya mafuriko hasa katika kipindi cha mvua zinaponyesha kutokana na baaadhi ya maeneo kuwepo pembezoni mwa mto Rufiji hivyo kupelekea baadhi ya mazao kusombwa na maji na nyumba nyingine kuzingirwa na maji na kusababisha wananchi kuishi katika mazingira magumu.

'UKIPENDA SKETI ZA SHULE MSHONEE MKEO' MISUNGWI WATIA FORA MAADHIMISHO SIKU YA MWANAMKE DUNIANI 2020



Katika kilele cha Siku ya wanawake duniani Machi 8 mwaka 2020, kilichofanyika Viwanja vya Shule ya Sekondari Sanjo, Usagara wilayani Misungwi mkoani Mwanza, Wanawake nchini wametakiwa kuonyesha kivitendo uwezo na usawa kijinsia kwa kugombea udiwani na ubunge badala ya kubanana kwenye nafasi za viti maalum huku wanawake wengine wakitakiwa kuwaamini na kuwapigia kura wanawake wenzao ili kuleta mapinduzi makubwa.
Mmoja wa waanzilishi wa Shirika la kutetea haki za wanawake na watoto la jijini Mwanza KIVULINI Yusta Ntibashima akizungumza na kusanyiko lililojitokeza kwenye maadhimisho ya Siku ya Mwanamke Duniani wilayani Misungwi.
Huenda umeshuhudia siku ya Wanawake Duniani ikitajwa kwenye Vyombo vya Habari au kusikia kwa marafiki .
Lakini kwa nini? Lini? Je ni sherehe au maandamano? na Je kuna siku kama hiyo ya kimataifa kwa Wanaume?
Kwa zaidi ya karne sasa, watu duniani wamekuwa wakisherehekea siku hii.

1. Ilianzaje?

Siku ya wanawake duniani ilianza kutokana na jitihada za wanawake 15,000 mwaka 1908 walipoandamana mjini New York Marekani wakidai kupunguziwa muda wa kufanya kazi, ujira wa kuridhisha na haki ya kupiga kura.Kilikuwa chama cha kisoshalisti cha Amerika kilichotangaza kuwa ni siku ya kwanza ya kitaifa ya wanawake, mwaka mmoja baadae.
Wazo la kuwa siku ya kimataifa lilianzishwa na mwanamke kwa jina Clara Zetkin.+1+0
Alipendekeza wazo hilo mwaka 1910 katika mkutano wa kimataifa wa wafanyakazi wanawake huko Copenhagen Denmark.
Kulikuwa na wanawake 100 hapo kutoka nchi 17 na wakakubaliana kwa pamoja.
Kwa mara ya kwanza ilisheherekewa mwaka 1911, Austria, Denmark,Ujerumani na Switzerland.
Sherehe ya 100 ilifanyika mwaka 2011, hivyo mwaka huu ni sherehe ya 107 ya wanawake duniani.
2.Ilikuwalini?
Tarehe 8 mwezi Machi. Wazo la Clara Zetkin la Siku ya kimataifa ya wanawake duniani halikuwa na tarehe maalum na haikuwa rasmi mpaka kipindi cha vita ya mwaka 1917 wakati wanawake wa kirusi walipodai Amani na kufanyia kazi tatizo la upungufu wa chakula (Waliimba Amani na Mkate).
Siku nne za mgomo, zilifanya watawala wa Urusi kuwapa wanawake haki ya kupiga kura.Tarehe ambayo mgomo ulianza ulikuwa kwenye kalenda ya Julian, ambayo ilikuwa ikitumika Urusi wakati huo, ilikuwa siku ya Jumapili tarehe 23 Mwezi Februari.
Siku hii katika kalenda ya Gregoria ilikuwa tarehe 8 mwezi Machi.
3.Je kuna siku ya wanaume?
Ndio ipo, tarehe 19 Novemba. Lakini iliadhimishwa tangu miaka ya 90 na haitambuliwi na Umoja wa Mataifa.Watu huiadhimisha katika nchi zaidi ya 60. Lengo la siku hii ni kutazama afya za wanaume na wavulana, kuimarisha mahusiano ya jinsia,usawa wa jinsia na kutathimini jinsia ya kiume kama watu wa mfano wa kuigwa.Kauli mbiu ya mwaka 2017 ilikuwa 'kuwaadhimisha wanaume na wavulana'

OCD wa Misungwi Shabu B. Shabu akitoa darasa.
Kauli mbiu inayoendesha kampeini ya siku ya kimataifa ya wanawake duniani mwaka huu ni usawa kwa sawa #EachForEqual, ambayo inaangazia usawa wa papoja.
"Sote ni sehemu ya dunia moja," kampeini hiyo inasema. "Mchango wetu wa kibinafsi, mtazamo, tabia na fikira zetu zinaweza kubadili jamii kwa ujumla.
"Kwa pomoja, tunaweza kuleta mabadiliko. Kwa pamoja, kila mmoja wetu anaweza kuchangia upatikanaji wa usawa wa kijinsia duniani."
Meneja CRDB Misungwi Deogratius Kessy amefunguka kuhusu unyanyasaji wa kiuchumi kwa ufasaha haswaa..

Katika miaka miaka michache iliyopita wanaharakati wa kutetea haki za wanawake walipiga hatua kubwa. Mwezi Oktoba 2017, mamilioni ya wanawake walianza kapeini ya #MeToo katika mitandao ya kijamii ili kupinga unyanyasaji na dhulma za kingono.
Mwaka In 2018, kampeini ya #MeToo ilipata umaarufu duniani, huku mataifa kama vile India, Ufaransa, China, na Korea Kusini yakijiunga na kampeini hiyo kushinikiza mabadiliko.
Nchini Marekani, wanawake walivunja rekodi katika uchafuzi wa katikati ya mhula.
Mwaka jana utoaji mimba ulihalalisha Ireland Kaskazini huku sheria inayodhibiti mavazi ya wanawake nchini Sudan ikifanyiwa mabadiliko.

Sunday, March 8, 2020