ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 16, 2025

RAIS SAMIA AFANYA KWELI KIBAHA TC ATOA PIKIPIKI 37 KWA MAAFISA UGANI

 
NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

 
Halmashauri ya Kibaha mji imepokea jumla ya pikipiki zipatazo  37 kutoka serikalini kupitia Wizara ya kilimo kwa lengo la  kuwawezesha maafisa ugani wa kilimo kutoka kata zote 14 kwa ajili ya  kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa weledi na  ufanisi zaidi katika suala la kuwahudumia wakulima na kuleta matokeo chanya katika sekta ya kilimo.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha  Nickson John  wakati wa halfa ya kukabidhi pikipiki hizo 37 kwa maafisa ugani hao na kuwatka kuhahakikisha kwamba wanaweka misingi ya kuwa na mikakati kabambe katika kuwa  na  kilimo cha kisasana chenye kuleta tija kwa wakulima.
Mkuu huyo alisema kwamba lengo kubwa la serikali ni kuhakikisha wanaendekea na kufanya juhudi za hali na mali za kuhakikisha inaendelea kuwasajili wakulima wote waweze katika mfumo ambao unatambulika ikiwemo sambamba na kuwapatia pembejeo za kilimo ambazo zitaweza kuwasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao.

"Tunapenda kumshukuru kwa dhati Rais wetu wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuongeza bajeti katika sekta ya kilimo pamoja na kutoa vitendea kazi hivi amabvyo ni boda boda 37 kwa maafisa ugani kwa lengo la kuweza kuongeza ufanisi na tija  zaidi katika suala zima la kuwahudumia wakulima waweze kuwa na kilimochenye tija katika maeneo yao,"alisema Simon.
Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amebainisha kwamba nia kubwa ya serikali ni kushiikiana bega kwa bega na maafisa ugani katika kuweka mippango endelevu ya kufanya kilimo cha kisasa ambacho kitakuwa ni mkombozi mkubwa kwa wakulima pamoja na wananchi kwa ujumla katika sekta ya kilimo.

Katika hatua nyingine amewaagiza maafisa ugani pamoja na wataalamu wakilimokuhakikisha kwamba wanazitumia vizuri pikipiki hizo kwa kuwafikia walengwa ambao ni wakulima na kwamba dhima kubwa ya serikali ni kuona  kunatokea mabadiliko  zaidi katika maeneo mbali mbali ya Kibaha mji.
 
Pia Mkuu huyo amemshukuru kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezeha vyombo hivyo vya usafiri ambavyo vitaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kutimiza majukumu ya maafisi ugavi hao  ikiwemo pamoja na kuongeza kiwango cha mapato.
Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kibaha mji Dkt. Rogers Shemwelekwa amebainisha kwamba kwa sasa kuna jumla ya watumishi wa ugani wa kilimo wapatao 41 ambao wanatoa ushauri wa ugani kwa wakulima 7, 528 katika mitaa yote  73 kutoka kata 14.
Pia mkurugezni huyo amebainisha kwamba  kwa sasa halmashauri ya mji Kibaha lina eneo linalofaa kwa kilimo lenye ukumbwa wa wastani wa Hekta zipatazo 7, 750 na kwamba wakulima 3,600 tayari wameorodheshwa katika mfumo wa mbolea na mbegu  za ruzuku katika msimu kwa mwaka 2024/2025 na wanapata mbolea na mbegu za ruzuku.

Pia amesema kuwa Halmashauri ya mji Kibaha kuna fusa mbali mbali na kwamba kuna wakulima wapatao  191 wa zao la korosho  wamefaanikiwa kupata  ruzuku kwa ajili ya zao hilo, ambapo pia wakulima wapatao 6, 709 ni wale wa mbogamboga , na wakulima 628 ni wa mazao ya matunda.
Nao baadhi ya maafisa Ugani katika Halmashauri ya Kibaha mji wamempongeza Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwawezesha vitendea kazi hivyo vya pikipiki zipatazo 37 ambazo zitaweza kuwasaidia katika suala zima la utekelezaji wa majukumu yao ya kuwahudumia wakulima katika maeneo yao.

Wamebainisha kwamba hapo awali walikuwa wanakabiliwa na changamoto kubwa ya usafiri na kupelekea kushindwa kufika kwa urahisi kwa wakulima lakini kwa sasa wataweza kufanya kazi zao kwa uafanisi mkubwa na kuwafikia  wakulima wao kwa urahisi na kutekeleza maelekezo ya serikali ya kuwahudumia wakulima na kuwa na kilimo chenye tija.

YANGA YAFUNGA DIRISHA DOGO KWA USAJILI WA JONATHAN IKANGALOMBO KAPELA.

 KLABU ya Yanga imemtambulisha winga wa kulia, Jonathan Ikangalombo Kapela kutoka AS Vita Club ya kwao, Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuwa mchezaji wake mpya wa pili dirisha hili dogo.

Anamfuatia beki wa kulia, Israel Patrick Mwenda anayeweza kucheza kama winga wa kulia pia na kiungo, aliyesajiliwa kwa mkopo wa hadi mwisho wa msimu kutoka Singida Black Stars.

SIMBA KUIKABILI CS CONSTANTINE UWANJA MTUPU BILA MASHABIKI

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeifingia klabu ya Simba kuingiza watazamaji katika mechi zake mbili za Kombe la Shirikisho Afrika baada ya vurugu zilizotokea kwenye mechi dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia Desemba 15, 2024 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Siku hiyo, Simba SC ilitoka nyuma na kushinda 2-1 kabla ya vurumai kuibuka na mashabiki wake kushambuliana na mashabiki wa wageni kwa kurushiana viti walivyokuwa wanang’oa uwanjani.

Maana yake Simba hawatakuwa na watazamaji katika mchezo wao wa mwisho wa Kundi A Kombe la Shirikisho dhidi ya CS Constantine Jumapili.

Tuesday, January 14, 2025

MSIGWA ALIONEWA CHADEMA NDIYO AKAAMUA KUTIAMKIA CCM

 NA ALBERT G.SENGO

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Jumanne, Januari 14, 2025.

LEMA AMTEMA MBOWE HADHARANI AMSHAURI KUPUMZIKA NA KUMWACHIA LISSU UENYEKITI.

 NA ALBERT G.SENGO

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini, Godbless Lema amemshauri mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe kusikiliza ushauri wa familia yake wa kumtaka kutogombea tena nafasi hiyo. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mapema hii leo Jumanne, Januari 14, 2025 Lema amesema anamheshimu Mbowe kutokana na kazi kubwa ya kukijenga chama hicho, lakini kwa sasa asikilize zaidi ushauri wa familia yake. Lema amesema Mbowe mara kadhaa amekuwa na nia ya kupumzika na kuwaachia nguvu mpya vijana kuendeleza mapambano, lakini watu wanaoitwa wanachama wamekuwa wakimshauri kuendelea kuwa mwenyekiti.

Monday, January 13, 2025

VIONGOZI KUTOKA CHATO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO TFS - SHAMBA LA MITI SAOHILL

 

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Dkt Linda amewapongeza kwa kuchagua kuja kutembelea na kujifunza kuhusu uhifadhi wa misitu utunzaji mazingira na ukusanyaji wa mapato katika Wilaya ya Mufindi kwani ni eneo sahihi kwao. Salekwa 
Viongozi mbalimbali kutoka Halmashauri ya Chato wakipa elimu ya uhifadhi wa miti na faida zake kutoka shamba la miti Sao Hill
Viongozi mbalimbali kutoka Halmashauri ya Chato wakipa elimu ya uhifadhi wa miti na faida zake kutoka shamba la miti Sao Hill

Na Fredy Mgunda, Iringa.

VIONGOZI kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chato Mkoani Geita wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe. Peter Bura, Katibu Tawala wa Wilaya pamoja na madiwani wa halmashauri hiyo wamefanya ziara ya mafunzo  Shamba la Miti Saohill lililopo Wilayani  Mufindi Mkoa wa Iringa.

Akizungumsha wakati wa ukaribisho wa Viongozi hao Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Dkt Linda Salekwa amewapongeza kwa kuchagua kuja kutembelea na kujifunza kuhusu uhifadhi wa misitu utunzaji mazingira na ukusanyaji wa mapato katika Wilaya ya Mufindi kwani ni eneo sahihi kwao.

"Tunapozungumza habari ya uhifadhi wa  misitu, na ukusanyaji wa mapato ya halmashauri na serikali kwa ujumla, Wilaya ya Mufindi imepiga hatua kubwa sana na hii inatokana na uwepo wa Shamba la Miti la serikali la Saohill" Amesema Dkt. Linda Salekwa

Ameongeza kuwa kupitia elimu inayotolewa na wahifadhi kuhusu utunzaji wa mazingira kwa kupanda miti imechangia uwepo wa rasilimali kubwa ya misitu hali iliyopelekea kuwepo kwa viwanda vingi vinavyochakata mazao ya misitu  na hivyo kuongeza pato la mwananchi mmojammoja  na taifa na hii ni kutokana na uuzaji na  ushuru unaokusanywa kupitia mazao ya misitu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe. Peter Bura amesema kuwa lengo la ziara hiyo ni kujifunza ni kwa namna gani Wilaya ya Mufindi kupitia Shamba la Miti Saohill wamefanikiwa  katika uhifadhi wa misitu na ukusanyaji wa mapato ili nao waweze kuona ni hatua gani watazichukua katika kufanikisha hilo katika Wilaya ya Chato.

"Katika Wilaya ya Chato tunalo Shamba la Miti Silayo hivyo tumekuja kujifunza ni kwa namna gani wenzetu wa Mufindi wananufaika vipi kimazingira na kimapato ili na sisi kupitia Shamba la Miti Silayo tuone namna tutakavyoshirikiana na TFS katika kuleta tija  wilayani kwetu kupitia Shamba lile" Amesema Mkuu wa Wilaya ya Chato

Kwa upande wake Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Saohill PCO Tebby Yoramu amesema kuwa Shamba limefanikiwa kufika hatua iliyopo kwa sasa kutokana na kuwepo kwa programu mbalimbali zinazolenga kujenga mahusiano mazuri na jamii zinazolizunguka shamba ikiwemo kutoa ajira za kutwa kwa wananchi, elimu ya uhifadhi pamoja na kusaidia shughuli za maendeleo katika sekta ya elimu, afya na miondombinu ya barabara hali inayopelekea kuwepo kwa uhusiano chanya baina ya shamba, taasisi na wananchi.

Katika ziara hiyo Viongozi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Chato waliweza kujifunza juu ya shughuli mbalimbali za ufugaji nyuki, uzalishaji wa miche katika bustani, pamoja na shughuli za uvunaji wa utomvu katika misitu ya kupandwa.

Sunday, January 12, 2025

Kamwe asema Yanga yaweza kumaliza kinara kwenye kundi lao

 “Sisi tunaweza kumaliza pia tukiwa kinara kwenye hili kundi” maneno ya Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe akilichambua kwa undani kundi lao kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL).

Kamwe pia ameuchambua mchezo wao wa leo dhidi ya Al Hilal huku akimtaja Kocha Florent Ibenge. Kamwe amesema wachezaji wa Yanga wanaogelea pesa kutokana na motisha ambayo amekuwa akiitoa Mfadhili na Mdhamini wao Ghalib Said Mohamed (GSM) #YangaSafarini #YangaMauritania #AlHilal #YangaSC #AlHilalYanga #CAFCL #CAFChampionsLeague

SERIKALI YASISITIZA UMUHIMU WA MAFUNZO YA UFUATILIAJI NA TATHIMINI KWA MAENDELEO YA MIRADI YA SERIKALI

 

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) imezitaka halmashauri, taasisi, na wadau mbalimbali wanaonufaika na mafunzo ya ufuatiliaji na tathmini kutumia vyema fursa hizo. Imepongeza ushirikiano uliopo baina ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, ambacho kimeendelea kutoa mafunzo wakishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuongeza ufanisi wa kufuatilia na kusimamia maendeleo ya miradi ya serikali.


Kauli hiyo imetolewa leo Januari 10, 2024, na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, na Uratibu, John Bosco Quman, wakati wa kufunga mafunzo ya uelewa kwa watumishi wa serikali ngazi ya halmashauri. Quman amehimiza washiriki kushiriki kikamilifu hatua zote tatu za mafunzo ili kuimarisha usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aidha amekipongeza Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Quman amesema chuo hicho kimefanya kazi nzuri katika kutoa mafunzo ya ufuatiliaji na tathmini, bila malalamiko yoyote kuhusu utekelezaji wa mpango huo unaosimamiwa na serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu.


Kwa upande wake, mwezeshaji wa mafunzo hayo kutoka Chuo Kikuu Huria, amesema mpango huo unalenga kuwajengea uwezo wafanyakazi wa serikali. Hadi sasa, mikoa yote nchini  imefaidika na mafunzo hayo katika ngazi ya kwanza. Ameongeza kuwa washiriki 67 kutoka halmashauri mbalimbali wamepata maarifa ya kutafsiri miongozo, kusimamia utekelezaji wa miradi, na kuandaa miongozo inayosaidia kutatua changamoto za kijamii katika mafunzo yaliyotolewa Mkoani Morogoro .

Naye, Caroline Marila, mshiriki wa mafunzo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa, amesema mafunzo hayo yataboresha utekelezaji wa miradi ya serikali na usimamizi wa rasilimali fedha, hivyo kuleta mabadiliko chanya katika utoaji wa huduma kwa jamii.

Mafunzo haya, yaliyoanzishwa na serikali kupitia Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, yalianza mwaka 2024 kwa lengo  la kuwajengea uwezo watumishi wa umma katika kufuatilia na kutathmini miradi ya maendeleo ili kuongeza uwajibikaji na ufanisi wa matumizi ya rasilimali.