ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, January 16, 2025

SIMBA KUIKABILI CS CONSTANTINE UWANJA MTUPU BILA MASHABIKI

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeifingia klabu ya Simba kuingiza watazamaji katika mechi zake mbili za Kombe la Shirikisho Afrika baada ya vurugu zilizotokea kwenye mechi dhidi ya CS Sfaxien ya Tunisia Desemba 15, 2024 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Siku hiyo, Simba SC ilitoka nyuma na kushinda 2-1 kabla ya vurumai kuibuka na mashabiki wake kushambuliana na mashabiki wa wageni kwa kurushiana viti walivyokuwa wanang’oa uwanjani.

Maana yake Simba hawatakuwa na watazamaji katika mchezo wao wa mwisho wa Kundi A Kombe la Shirikisho dhidi ya CS Constantine Jumapili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.