ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 29, 2024

TRAORE ATAIFANYA UFARANSA KUWA MASKINI WANAMUWINDA WAMUUE PUTIN NAYE ANANG'ATIWA VIDOLE

 Mpenzi mtazamaji wa IBM CHANNEL endelea kutufuatilia kwa ajili ya kupata elimu zaidi ya uzalendo, ukombozi wa kifkira na ukuu wa Mwaafrika hapa hapa. tunakupa pia makala mbalimbali zinazohusiana na ulimwengu tunaoishi na taarifa zetu ni za ukweli na uhakika sio za uongo. karibu tuendelee kuwa pamoja. kama hauja-subscribe tafadhali fanya hivyo ili usipitwe na chochote.

Friday, June 28, 2024

KATIBU CCM PWANI-WAGOMBEA WATAKAOTEULIWA NA VIKAO VYA CHAMA KWENYE CHAGUZI WATENDEWE HAKI



NA VICTOR MASANGU, PWANI


Chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu kimejiwekea mipango kabambe  ya kuhakikisha  kwamba wanapata wagombea wazuri  na wenye sifa ambao wanakubalika katika jamii  na kuweza kusabisha kuweza kuibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi huo.

Hayo yamebainishwa na Katibu wa (CCM)  Mkoa wa Pwani Bernad Ghathy  wakati wa kikao cha Halmashauri kuu ya (CCM) Mkoa ambapo amesema kuwa lengo kubwa la chama ni kuweka misingi imara ya kuwapata viongozi wazuri ambao watakwenda kuipeperusha vyema bendera ya chama kwa kushinda katika mitaa yote ndani ya Mkoa wa Pwani.

Katibu Ghaty alisema kwamba kikao hicho cha Halmashauri kuu kimeelekeza kwamba katika vikao vyote vya  uteuezi  vitakavyofanyika katika ngazi ya chama  vihakikishe kwamba vinatenda haki bila upendeleo wowote  katika kuwapata viongozi ambao watagombea katika uchaguzi huo wa serikali za mitaa.

"Tumekutana katika kikao cha Halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani na hiki kikao ni cha kikatiba kabisa na  tumeweza kuzungumzia mambo mbali mbali ya utekelezaji wa ilani pamoja na kupokea taarifa ya serikali ya Mkoa ikionyesha kazi na miradi mbali mbali ambayo imetekeleza katika sekta tofauti, ikiwa sambamba na kujadili hali ya kisiasa katika Mkoa wa Pwani,"alisema Katibu Ghathy.

Aidha Katibu huyo alifafanua kwamba Halmashauri hiyo imempongeza kwa dhati Mwenyekiti wa (CCM) Taifa ambaye pia ndiye Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwatumikia wananchi katika nyanja mbali mballi za miradi ya maendeleo ikiwemo elimu, wananchi kuweza kupata huduma ya maji safi na salama, miundombinu ya barabara sambamba na uboreshawaji wa huduma ya afya.

Kadhalika hakusita kutoa pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge pamoja na wasaidizi wake kwa kuweza kuhakikisha kwamba wanajitahidi kupambana kuboresha miundombinu ya barabara ili iweze kupitika kwa urahisi hata katika kipindi cha mvua zinaponyesha.

Pia amebainisha  kuwa chama cha mapinduzi Mkoa wa Pwani wanajivunia kupata Mwenyekiti wa Taifa ambaye ni msikivu na shupavu kwani ameweza kufanya mambo makubwa mbali mbali ya kukisaidia chama ikiwemo kuchangia katika mradi wa jengo la kitega uchumi ambalo linatarajiwa kuzinduliwa ifikapo Julai 30 mwaka huu na kuanza kutumika.

Katika hatua nyingine amesema kuwa mikakati ambayo wamejiwekea ni kuendeleza sera ya chama ya kuweka mifumo ya kujiimarisha kichumi kuanzia ngazi za chini kwa kushirikiana bega kwa bega na wanachama wote wa chama cha mapinduzi lengo ikiwa ni kuweza kuletaa mabadiliko chanya ya kimaendeleo kupitia vitegaa uchumi vilivyopo.

MAMA AANGUA KILIO MOCHWARI BAADA YA KUMUONA MWANAWE ALIYEPIGWA RISASI KWENYE MAANDAMANO.


 Mama akilia nje ya chumba cha kuhifadhia maiti cha City (l). Waandamanaji wakifanya ishara kwa mikono wakati wa maandamano (r). 

Mwanamke mmoja ni miongoni mwa Wakenya wanaoumia baada ya mpendwa wake aliyejitokeza kwa maandamano hayo kuathiriwa na dhuluma za polisi.

Je Rex Mmasai alikufa vipi? 

Katika kisa sawia, Rex Masai, kijana kutoka kaunti ya Nairobi, alidaiwa kuuawa na afisa wa polisi alipokuwa akiandamana kupinga Mswada wa Fedha wa 2024.

Kijana huyo alipopigwa risasi, alikimbizwa katika Kituo cha Matibabu cha Bliss katikati mwa jiji, na baba yake, aliyetambulika kama Chrisphine Odawa, akaenda kumtazama. 

Cha kusikitisha alipoteza maisha na Chrisphine ambaye alihuzunika sana alieleza kuwa kifo cha mwanawe kilikuwa hasara kubwa kwa familia. 

Nini kingine unahitaji kujua kuhusu maandamano ya kupinga Muswada wa Fedha Baadhi ya Wakenya walionyesha kufadhaika baada ya Rais William Ruto kuwashukuru polisi waliojibu maandamano hayo.

Nyumba ya Mbunge wa Molo Kimani Kuria ilichomwa moto na waandamanaji waliokuwa na hasira.

Charlene Ruto aliwakumbusha Wakenya kuzingatia Mswada wa Fedha wa 2024 kufuatia hotuba ya rais Mwigizaji.

 Lupita Nyong'o aliwapongeza Gen Zs kwa kushiriki maandamano ya amani na kuitaka serikali kuwasikiliza waandamanaji.

Thursday, June 27, 2024

DC KIBAHA AMPA KONGOLE RAIS SAMIA UJENZI WA DARAJA LA MTO MPIJI

HABARI NA VICTOR MASANGU/PWANI. SAUTI YA ALBERT G. SENGO Jeshi la nchi kavu limekabidhi rasmi daraja la muda la mto Mpiji linalounganisha Wilaya.mbili za Kibaha Mkoa wa Pwani na Manispaa ya Ubungo kwa mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Saimon ambaye naye amelikabidhi kwa uongozi wa Tarura.

VIDEO: KILICHOJIRI NCHINI KENYA ASUBUHI YA LEO BARABARA KADHAA ZIMEFUNGWA

 

 

 William Ruto Apata Pigo Jingine Huku Mahakama Ikipiga Breki KDF Kutumiwa Kuzima Maandamano ya Gen Zs 

Rais William Ruto amekumbwa na msukosuko mkubwa katika mpango wake wa kupeleka wanajeshi wa Kenya badala ya polisi kuzuia ghasia katika maeneo mbalimbali nchini.

Mnamo Jumatano, Juni 26, Chama cha Wanasheria nchini (LSK) kilishtaki Waziri wa Ulinzi Aden Duale na Bunge la Kitaifa kuhusu kutumwa kwa KDF kufuatia maandamano ya kupinga Mswada wa Fedha. LSK iliiomba mahakama kusitisha uamuzi huo kusubiri kusikilizwa na kuamuliwa kwa kesi hiyo. 

Mahakama iliamuru pande zote kufika kwa ajili ya kusikilizwa kwa muda mfupi ombi hilo, ambalo liligombanisha LSK dhidi ya Serikali na Waziri wa Ulinzi. 

Katika stakabadhi zilizowasilishwa kortini, LSK inasema kwamba Rais William Ruto hajatangaza hali ya hatari chini ya Kifungu cha 58 cha Katiba katika kutekeleza mamlaka yake ya kikatiba chini ya Kifungu 132 (4) (d) cha Katiba. 

Wednesday, June 26, 2024

DC KIBAHA AMPONGEZA RAIS SAMIA NA MBUNGE KOKA UJENZI WA DARAJA JIPYA LA MTO MPIJI


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Saimon amempongeza Rais kwa kuweza kutoa fedha  kiasi cha shilingi bilioni 4  kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa  daraja jipya la kudumu katika  mto mpiji ambalo litaweza kuwa mkombozi kwa wananchi kuvuka bila shida hasa katika kipindi cha mvua.

Darala hilo la mto mpiji ambalo kwa sasa limejengwa kwa muda  limekuwa ni kiunganishi na mkombozi mkubwa  kwa wananchi kutoka   Wilaya mbili za Kibaha Mkoa wa Pwani pamoja na Wiyaya ya Ubungo ya Jijini Dar es Salaam

Mkuu huyo wa Wilaya ametoa pongezi hizo wakati wa halfa fupi ya kukabidhiwa daraja la muda kutoka kwa kaimu mkuu wa mafunzo na operesheni wa Jeshi la la nchi kavu Brigadia Jenerali Stanley Mjelwa halfa ambayo imehudhuliwa na viongozi wa serikali,chama,wananchi na Tarura.
Nikson amebainisha  kwamba pia   amemshukuru kwa dhati kwa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe. Silvestry Koka kwa kuwa  mstari wa mbele katika kulipambania kwa hali na mali ujenzi wa  daraja hilo liweze kujengwa ili wananchi waweze kupita kwa urahisi.

Amesema  kwamba Mbunge Koka amepambana na kuwasemea wananchi wa Pangani juu ya adha wanayoipata ndio maana Rais Samia  ameweza kuwa msikivu na kukubali   kutoa fedha hizo  kwa ajili ya ujenzi wa ujenzi wa daraja hilo la kudumu.

  Mkuu huyo  amefafanua kwamba kwa sasa daraja ambalo limejengwa na Jeshi la nchi kavu  litatumika kwa muda na baada ya hapo litajengwa daraja lingine jipya la mto mpji  kwa fedha ambazo zimetolewa na Rais  Samia kiasi cha shilingi bilioni 4
"Kwa kweli nimshukuru sana Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutupatia fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja la kudumu katika mto mpiji licha ya kutoa fedha zingine zaidi ya milioni 250 kwa ajili ya kukarabati daraja la muda nimshukuru sana"

"Pia Mbunge wetu wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka kwa kuwa mstari wa mbele katika kuomba fedha na kuchangia michango mbali mbali katika daraja la muda ambalo limekabidhi kwangu leo hii ni juhudi za Mbunge Koka ili wananchi waweze kupata daraja hilo,"alisema Nickson.

Pia amesema kwamba anawashukuru Tarura pamoja kwa juhudi zao pamoja na Jeshi la nchi kavu kwa kuweza kukamilisha ujenzi huo wa daraja la muda katika mto mpiji.

Naye Kaimu wa mkuu wa mafunzo na operesheni wa Jeshi la nchi kavu Brigedia Jenerali Stanley Mjelwa ameitaka Tarura kuhakikisha wanalifanyia ukarabati daraja hilo ili liweze kuharibika mapema.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa barabara za vijijini na mijini (TARURA) Wilaya ya Kibaha mjini Injinia Samwel Ndoveni amesema kwamba daraja hilo la awali limeweza kufanyiwa marekebisho ili kuweza kuwapa fursa wananchi wa Wilaya ya Kibaha na Wilaya ya Ubungo waweze kupita kwa urahisi zaidi.

Nao baadhi ya wananchi wa kata ya pangani hakusita kuzungumzia jinsi ya Mbunge wa Jimbo lao alivyoweza kuwa na wananchi bega kwa bega katika ujenzi wa daraja hilo la mto mpiji.

Wamesema kwamba Mbunge Koka tangu mwanzoni ameshirikiana na diwani wa kata ya Pangani pamoja na wananchi kwa ajili ya kuweza kuhakikisha daraja hilo la muda  linakamili na kupitika kwa urahisi.

VIJANA WENYE BUNIFU MBALIMBALI TANGA KUPATIWA FURSA ZA RUZUKU

 

Mwakilishi wa Shirika la Botnar Foundation Philotheusy Mbogoro akizungumza wakati akifungua mafunzo maalumu ya ufundi na Udereva wa Bajaji za Mfumo wa Umeme yaliyoanza leo kwenye Shule ya Sekondari Tanga School ambapo vijana zaidi ya 40 wanapata mafunzo hayo.
 Mmoja kati ya Washirika na Wafanyakazi wa Tanzania Open Innovation Organization na Robotech Abdulwahab Issa akizungumza  wakati akifungua mafunzo maalumu ya ufundi na Udereva wa Bajaji za Mfumo wa Umeme yaliyoanza leo kwenye Shule ya Sekondari Tanga School ambapo vijana zaidi ya 40 wanapata mafunzo hayo.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) Shaukatali Hussein akizungumza na baadhi ya madereva Bajaji wakati wa mafunzo hayo
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization (TOIO) Shaukatali Hussein akizungumza na baadhi ya madereva Bajaji wakati wa mafunzo hayo
Afisa Vijana Jiji la Tanga Fadhili Secha  kulia akisisitiza jambo wakati wa mafunzo hayo


Na Oscar Assenga, TANGA.

VIJANA wanaofanya shughuli za Ubunifu Jijini Tanga wamewekewa bayana uwepo wa mambo mazuri kwao ikiwemo fursa za kupatiwa ruzuku ili waweze kufanya bunifu ambazo zinaweza kuwaingiza wenzao kwenye ajira na maisha bora zaidi.

Hayo yalisemwa leo na Mwakilishi wa Shirika la Botnar Foundation Philotheusy Mbogoro wakati akifungua mafunzo maalumu ya ufundi na Udereva wa Bajaji za Mfumo wa Umeme yaliyoanza leo kwenye Shule ya Sekondari Tanga School ambapo vijana zaidi ya 40 wanapata mafunzo hayo.

Alisema kwamba kupitia Tanga yetu ipo kwa ajili ya kusaidia vijana wenye ubunifu mkoani humo kwa ajili ya kuwawezesha kunufaika kupitia Taasisi mbalimbali ikiwemo TOIO, Project Inspire Sterm Park na wengine wanawawezesha bajeti ya kuweza kuwasaidia.

Kati ya vijana hao 35 ni kutoka chuo cha Ufundi Veta na wengine ni kutoka mitaani wenye kutakuja kuwa ufundi wa Bajaji ambapo mafunzo hayo yanaendeshwa na Kampuni ya Robotech Labs kwa kushirikiana na Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organization chini ya ufadhili wa Tanga Yetu.

Mafunzo yaliyotolewa ni namna ya kuweza kutumia vyombo hivyo kwa urahisi, ufungaji ikiwemo uunganishaji wa bajaji kwa kila sehemu kabla ya kukamilika na kuwa chombo kamili ambayo itawasaidia kujua hata jinsi ya kufanya marekebisho yake.

Alisema kwamba wao wanawasaidia kupata ruzuku hizo ili kuwawezesha vijana wengi waweze kutumia fursa zilizopo Jijini Tanga na kuweza kujikwamua kiuchumi.

Alisema vijana hao wanapaswa kutumia fursa hizo zilizopo ikiwemo kujitahidi kuwa wabunifu na wasilale kutokana na uwepo wa vitu vingi vya kufanya ambavyo vinaweza kuwaondoa kukaa kijiweni kutokana na kukosa kitu cha kufanya.

Aidha alisema umuhimu wa mafunzo hayo yanatoa fursa kwa vijana wengi kuweza kupata ujuzi wa kuweza kuwasaidia kujiajiri na kufanya shughuli zao ziwe bora kupitia nyanja mbalimbali ikiwemo ufungaji wa samaki, uvuvi, kilimo, ufungaji wa kuku hivyo wanawataka vijana kuwa mabalozi wazuri kujifunza

Akizungumzia mafunzo ya Bajaji za umeme alisema kwamba zinawapa fursa ya kuunganisha bajaji za umeme ambazo wanaweza kupata biashara ya kuziunganaisha, kufanya matengenezo, vituo vya kuzifanya marekebisho.

“Lakini pia zinatoa fursa wengine kuchaji, kuziuza na fursa za ajira ambazo zinakwenda kwa vijana ni wengi kupitia bajaji na pikipiki za umeme zinazokuja na hata magari umeme kwa hiyo wamekuwa kuwa na teknolojia hiyo uwezo mkubwa wa kukamata biashara ya kuhudumia bajaj,pikipiki na hata magari ya umeme itakuwa mikono mwenu hivyo mzingatie mafunzo haya”Alisema

Awali akizungumza katika mafunzo hayo ni Mmoja kati ya Washirika na Wafanyakazi wa Tanzania Open Innovation Organization na Robotech Abdulwahab Issa alisema kwamba wapo kwenye mafunzo ya bajaji wao waona namna gani bajaji zinazounganishwa zikiwa zimetoka kutoka kiwandani.

Alisema pia waweze kuona mifumo ya umeme na mota vinavyofanya kazi lengo kubwa na mahususi vijana hao waweze kuona na kupata uelewa namna vyombo hivyo vinavyoweza kufanya kazi na wao jinsi gani ya kuweza kuwasaidia katika maisha yao ya kila siku na kuokoa kipato.

Alisema bajaji hiyo inaweza kutembea kwa umbali wa kilomita 80 mpaka 100 kwa kutumia chaji ya asilimia 100 kwa bajaji iliyochajishwa kwa sh 3000 hivyo inaweza kuokoa kipato cha matumizi kuokoa mafuta kuhamia huko kwa sababu ya masuala ya kimazingira.

Awali akizungumza katika mafunzo hayo Afisa Vijana Jiji la Tanga Fadhili Secha alisema wamekuwa wakishirikiana na vijana na wadau wa maendeleo kuwatumia vijana kutoka sehemu mbalimbali kuwaunganisha na wadau kuweza kupata vitu mbalimbali vinavyoendelea na Ubunifu wa Teknolojia.

“Ujio wa Bajaji za Umeme hapa vijana wamepata fursa muhimu kwa sababu ni teknolojia mpya ni itawasaidia kuepukana na gharama kubwa kuepukana na matumizi ya petroli ambayo ni gharama na kuweza kupata faida”Alisema

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa Bajaji Mkoa wa Tanga Rahim Makange alisema bajaji za umeme ni fursa kubwa kwa vijana wa Jiji hilo na wamepata elimu nabajaji hizo zinarahisisha mambo mengi na hazina gharama kutokana na kwamba gharama zake ni umeme hakuna kuingia sheli.

Alisema kwamba wameelewa umbali betrii ikichajiwa ikijaa inaweza kutoka Jijini Tanga hadi Korogwe kwa kuchaji lakini petroli ingekuwa ni gharama kubwa na hiyo itawaondolea ugumu wa maisha hivyo vijana wachangamkie fursa hiyo muhimu.

MBAO FC WAANZA UPYA NA KOMBE LA MBUZI

 NA ALBERT GSENGO/MWANZA

Mbunge wa jimbo la Ilemela Angeline Mabula anatajwa kuwa mgeni rasmi wa fainali itakayofanyika Jumatatu ya tarehe 1 July 2024 katika viwanja vya Sabasaba Ilemela jijini Mwanza.

Tuesday, June 25, 2024

BUNGE LASHIKA MOTO HUKU WAANDAMANAJI WAKIKABILIANA NA POLISI

 Sehemu ya Bunge la Kenya imechomeka moto huku waandamanaji wa kupinga Mswada wa Sheria ya Fedha 2024 wakivamia jengo hilo.

Maafisa wa polisi waliokuwa wamejipanga kuzunguka bunge walifurika haraka huku umati ukiharibu lango lake. 

Baada ya muda mfupi wa milio ya risasi kushamiri hewa kutoka kwa maafisa wa usalama, umati wa watu ulipata ufikiaji wa Jumba hilo.

Monday, June 24, 2024

NILITOROSHWA KIPINDI CHA MAPINDUZI |NILIPANDISHWA MELI YA NG’OMBE|NILIKUTANA NA MUME WANGU MSIKITINI

 Aunty Asha ameeleza safari ya maisha yake kutoka Zanzibar mpaka kufika Marekani

Kipindi cha mapinduzi aliweza kuondoka kuelekea Dubai kupitia meli ya kusafirisha Ng’ombe ambako alitumia miezi mitatu baharini mpaka kufika Dubai. Alienda kusoma India na baadae kuendelea na masomo nchini Marekani ambapo alikutana na mume wake msikitini ambako alikua akifundisha Quran. Kwasasa ni Mkurugeni katika sekta ya afya na kua miongoni mwa Mkurugenzi wa kwanza wa kiafrika katika mahala anafanyia kazi. Subscribe to her YouTube channel ili kujifunza kuhusu Afya na kisukari ‪@ashafaulkner‬ Thank you Aunty Asha for allowing this to be online www.oda.international

CCM KIBAHA MJI YATOA TAMKO LA KULAANI VITENDO VYA MAUAJI YA BODA BODA

 


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Chama cha mapinduzi Wilaya ya Kibaha mjini (CCM) kimelaani vikali vitendo vya  matukio ya mauaji ya madereva wa boda boda yanayoendelea katika maeneo  mbali mbali.

Akitoa tamko hilo katika kikao cha halmashauri kuu ya chama Mwenyekiti wa (CCM) Mwalimu Mwajuma Nyamka alisema kwamba wameamua kwa pamoja kutoa tamko hilo kutoka na kukithiri kwa matukio hayo.

Nyamka alisema kwamba matukio hayo ya unyang'anyi wa kuporwa pikipiki na kufanya mauaji yanafanywa na kikundi cha majambazi.

Alifafanua kuwa hivi karibuni kumetokea tukionla Katibu wa CCM tawi la Miswe kata ya Mbawa ambapo ndugu Sitaki Pazi kuporwa pikipiki na kuuwawa.

Pia Mwenyekiti Nyamka alisema kwamba chama pia kinalaani vikali mauaji ya kikatili aliyofanyiwa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi (Albino)  Asimwe Novat mwenye umri wa miaka miwili na nusu.



Katika hatua nyingine chama cha mapinduzi kimetoa pongezi kwa Jeshi la Polisi kwa hatua ambazo limeanza kuzichukua na kuwatia mbaroni baadhi ya watuhumiwa na kuomba waongeze kasi ili hali hiyo itoweke kabisa nchini.

Pia katika tamko hilo limempomgeza kwa dhati Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe.Silvestry Koka kwa kuweza kusaidia familia yenye watoto wawili wenye ulemavu wa ngozi(Albino).

Alisema kwamba Mbunge Koka amewasaidia watoto hao wawili kwa kuwavutia huduma ya maji safi na salama kutoka Dawasa pamoja na kuwapatia jiko la gesi.

Nyamka alisema kwamba Mhe.Mbunge ameguswa kwa kuinarisha ulinzi kwa familia zenye uhitaji maalumj na watu wenye ulemavu wa ngozi.

Pia aliongeza kuwa siku zote chama cha mapinduzi kinaubiri amani na utulivu hivyo wanaliomba jeshi la polisi kuebdelea kuimarisha ulinzi kwa wananchi pamoja na mali zao.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka alisema kwamba atahakikisha anaweka mipango ya kuwalinda na kuwatunza watu wenye ulemavu wa ngozi.

Koka alisema kwamba ataendelea kuwasaidia kwa hali na mali watu wenye ulemavu ili waweze kuishi katika mazingira ambayo ni rafiki na katika hali ya ulinzi na usalama.

Aidha Koka alitoa wito kwa wananchi wa Jimbo lake kuwa na umoja na kutoa taarifa kwa vyombo vya dola endapo wakibaini watu ambao wanahusika katika matukio ya mauaji.

Sunday, June 23, 2024

VIJANA, WAKINA MAMA TANGA WATANGAZIWA FURSA YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI


Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organazation (TOIO) Shaukatali Hussein akiwaonyesha wanahabari ambao hawapo pichani bajaji inayotumia umeme walioyoitengeneza

Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organazation (TOIO) Shaukatali Hussein akikagua moja ya bajaji ambazo zinatarajiwa kuunganishwa na baadae kutengenezwa kwa ajli ya kutumia umeme

Na Oscar Assenga, TANGA

VIJANA na Wakima mama waliopo katika Jiji la Tanga wametangaziwa fursa za kuchangamkia mafunzo ya namna ya kuviunga, kuvirekebisha na kutengeneza Bajaji za Umeme, Pikipiki, na Baiskeli hatua itakayowawezesha kujikwamuaa kiuchumi.

Hayo yalisemwa leo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organazation (TOIO) Shaukatali Hussein wakati akizungumza kuhusu namna walivyojipanga kuendelea kuiwezesha jamii ya wakazi wa Jiji hilo.

Alisema kwamba ili kufikia lengo hilo wameona waanze kutoa mafunzo ya kuunga vitu vya umeme na mafunzo hayo yatatolewa June 26 na 27 mwaka huu jinsi ya kuunga bajaji za umeme na kuanzia saa 4 asubuh hadi saa nane mchana .

“Kwa sasa tumeona njia nzuri ya kuweza kuwakwamua kiuchumi wakina mama na vijana ni kuwapa mafunzo hayo na tunaamini watakapomaliza watapata mwanga mzuri wa kuona namna ya kuzichangamkia fursa hizo”Alisema

Aidha alisema mafunzo ya vijana na wakina mama jinsi ya kuviunga na kuvitengeneza na kuvirekebisha na namba ya kuviendesha kwani hiyo ni fursa mpya ambazo zinaweza kuinua uchumi wao.

Hata hivyo alitumia fursa hiyo kuwataka vijana waliopo mtaani kutumia fursa za kidigitali mpya wanapoelekea pikipiki za umeme na bajaji za umeme,baiskeli zinaingia mtaani.

TFS WAPONGEZWA UHIFADHI WA MISITU NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

 

Mmoja ya viongozi wa shamba la miti Sao Hill wilaya ya Mufindi mkoani Iringa akisoma taarifa kwa viongozi wa mwenge wa uhuru kitaifa  Mwenge wa uhuru ukiwa ukiwa katika shamba la miti la Sao Hill wilaya ya Mufindi mkoani Iringa 
Shangwe za Mwenge wa uhuru katika shamba la miti Sao Hill wilaya ya Mufindi mkoani Iringa 

 Na Fredy Mgunda, Iringa.


Mwenge wa Uhuru 2024 watembelea na kukagua shughuli za uhifadhi wa misitu na utunzaji wa mazingira Shamba la Miti SaoHill

Mbio za Mwenge wa Uhuru zimepita na kukagua mradi wa Uhifadhi na Utunzaji wa Mazingira TFS - Shamba la Miti Sao Hill uliopo Tarafa ya Pili ya Shamba Ihefu katika Safu ya Nyololo Wilayani Mufindi.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2024 Ndg.Godfrey Eliakimu Mnzava amewapongeza Wakala wa Huduma Misitu Tanzania -TFS kwa kazi kubwa ya utunzaji wa Shamba la Saohill kwani limekuwa chanzo kizuri cha mapato kwa serikali na wananchi.

"Tunaelekea katika biashara ya hewa ukaa naamini kupitia msitu huu biashara hiyo itakuwa kubwa" Amesema Ndg Mnzava

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe Dkt Linda Salekwa amesema kuwa Shamba la Miti Saohill limekuwa ni msingi mkubwa katika shughuli za utunzaji wa mazingira na pia limekuwa likichangia kutatua changamoto za ajira kwani wananchi wengi wanafanya kazi katika msitu huu. 

Akiwasilisha taarifa ya mradi huo Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira Wilaya ya Mufindi Ndg. Gilbert Ngailo amesema kuwa Shamba la Miti Saohill limekuwa mchango mkubwa katika utunzaji wa uhifadhi wa mazingira kwani limekuwa likichangia katika utoaji wa elimu ya uhifadhi kwa wananchi na pia limekuwa likiandaa vitalu vya miche ya miti, upandaji wa miti pamoja na usimamizi dhidi ya majanga ya moto.

"Mbali na kuchangia mapato makubwa katika Serikali kuu na Halmashauri Shamba hili linatoa ajira kwa wananchi, kuhifadhi mazingira, kuelimisha wananchi juu ya ufugaji wa nyuki, kukarabati miondombinu ya barabara na kuchangia shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mabweni na ugawaji wa madawati katika shule mbalimbali" ameongeza.

Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024 zinaongozwa na kauli mbiu isemayo "Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu"