ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, June 23, 2024

VIJANA, WAKINA MAMA TANGA WATANGAZIWA FURSA YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI


Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organazation (TOIO) Shaukatali Hussein akiwaonyesha wanahabari ambao hawapo pichani bajaji inayotumia umeme walioyoitengeneza

Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organazation (TOIO) Shaukatali Hussein akikagua moja ya bajaji ambazo zinatarajiwa kuunganishwa na baadae kutengenezwa kwa ajli ya kutumia umeme

Na Oscar Assenga, TANGA

VIJANA na Wakima mama waliopo katika Jiji la Tanga wametangaziwa fursa za kuchangamkia mafunzo ya namna ya kuviunga, kuvirekebisha na kutengeneza Bajaji za Umeme, Pikipiki, na Baiskeli hatua itakayowawezesha kujikwamuaa kiuchumi.

Hayo yalisemwa leo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Open Innovation Organazation (TOIO) Shaukatali Hussein wakati akizungumza kuhusu namna walivyojipanga kuendelea kuiwezesha jamii ya wakazi wa Jiji hilo.

Alisema kwamba ili kufikia lengo hilo wameona waanze kutoa mafunzo ya kuunga vitu vya umeme na mafunzo hayo yatatolewa June 26 na 27 mwaka huu jinsi ya kuunga bajaji za umeme na kuanzia saa 4 asubuh hadi saa nane mchana .

“Kwa sasa tumeona njia nzuri ya kuweza kuwakwamua kiuchumi wakina mama na vijana ni kuwapa mafunzo hayo na tunaamini watakapomaliza watapata mwanga mzuri wa kuona namna ya kuzichangamkia fursa hizo”Alisema

Aidha alisema mafunzo ya vijana na wakina mama jinsi ya kuviunga na kuvitengeneza na kuvirekebisha na namba ya kuviendesha kwani hiyo ni fursa mpya ambazo zinaweza kuinua uchumi wao.

Hata hivyo alitumia fursa hiyo kuwataka vijana waliopo mtaani kutumia fursa za kidigitali mpya wanapoelekea pikipiki za umeme na bajaji za umeme,baiskeli zinaingia mtaani.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.