ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 2, 2017

BREAKING NEWS; ANTHONY DIALLO AMBWAGA MECK SADICK UENYEKITI CCM MKOA WA MWANZA.

Breaking News Dr Antony Mwandu Diallo Ameshinda Nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza akimpiku Aliekuwa Mkuu wa mkoa wa Dar na Moshi Meck Sadick , Dr Diallo anarejesha kiti chake mara Nyingine Tena Dr Antony Diallo Kura 555 Mh Meck sadick KURA 520 #Jembefm 93.7 Updates

RUNZEWE ACADEMY FC YAJINYAKULIA USHINDI KWA MARA YA PILI KWENYE MICHUANO YA DOTO CUP 2017

Kombe la mashindano ya Doto Cup likiwa mezani kabla ya kumpata mshindi.

Mchezo wa pikipiki pia ulihusika katika kusindikiza michuano ya Doto Cup.

Vikosi vya Karate vikiwa uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017.

Mgeni Rasmi ambaye ni Katibu mkuu wa baraza la michezo Tanzania (BMT) Mohamed Kiganja akiwasili kwenye viwanja vya shule ya sekondari ushirombo  ambapo ndipo michuano ya Doto cup ilikuwa ikifanyika,na kushoto Mbunge wa jimbo la Bukombe Doto Biteko akimpokea mgeni rasmi. 

Mbunge wa Bukombe,Doto Biteko akiteta jambo na Katibu mkuu wa baraza la michezo Tanzania (BMT) Mohamed Kiganja wakati wa michuano ya Doto Cup. 

Vikosi vya wakimbia kwenye magunia wamama vikiwa uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Fainali Doto Cup 2017

Kikosi cha wafukuza kuku wakifukuza kuku wakati wa michuano ya Doto Cup 2017.

Mashabiki na wanachama wa Simba na Yanga wanawake wakipimana nguvu  uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017.

Meza kuu ikiongozwa na Mgeni Rasmi ambaye ni Katibu mkuu wa baraza la michezo Tanzania (BMT) Mohamed Kiganja

Mashabiki na wanachama wa Simba na Yanga wanaume wakipimana nguvu  uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017




 Timu ya Runzewe Academy Fc katika Picha ya Pamoja kabla ya mchezo kuanza wa Fainali ili kumpata mshindi  wa  Ligi ya Doto Cup 2017.

 Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Mohamed Kiganja,Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb),Mwenyekiti wa CCM(W) Daniel Machongo na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe wakiwa na kwenye picha ya pamoja na waamuzi wa michuano ya Doto cup 2017.
Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Mohamed Kiganja,Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb),Mwenyekiti wa CCM(W) Daniel Machongo na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe wakiwa na wachezaji wa Timu ya Chui Fc kutoka Bugerenga katika Picha ya Pamoja kabla ya mchezo kuanza wa Fainali ili kumpata mshindi  wa  Ligi ya Doto Cup 2017.







(Picha na Consolata Evarist.)



Mashindano ya  Doto cup 2017 yamemalizika huku timu ya Runzewe Academy ikiibuka na ushindi wa matuta zidi ya timu ya Chui FC.

Michuano hiyo ambayo inaandaliwa na Mbunge wa jimbo la  Bukombe mkoani Geita  Doto  Biteko  kwa lengo la kuibua vipaji husuani kwa vijana yalianza kutimua vumbi mwezi wa tisa huku timu 45 zikishiriki kwenye mashindano hayo.  

Akizungumza na mtandao wa maduka online ,Kocha wa Runzewe academy Ramadhani Mgoi alisema kuwa huu ni msimu wa pili wa mashindano hayo na kwamba wao ni mala ya pili wanachukua Kombe hilo  na kwamba njia ambazo wanatumia kupata ushindi ni kujituma kwenye mazoezi na wachezaji kuwa na nidhamu.

Hata hivyo Kocha Mgoi ameobgeza kwa kumshukuru Mbunge kwa kuendelea kuwa karibu na vijana na kuibua vipaji kwenye Wilaya hiyo.

Katibu mkuu wa baraza la michezo Tanzania (BMT) Mohamed Kiganja ambaye alikuwa mgeni rasimi kwenye fainali hizo   amehaidi mwakani kufanya   mabadiliko ya mashindano hayo ikiwa ni pamoja na  kuleta wataalamu ili wawachague wachezaji kuchezea timu ya Taifa.

“ Ili mashindano haya yaweze kufanikiwa nilazima wapunguze umri wa wachezaji kutoka miaka 15 mpaka 17 na pia natoa wito kwa halmashauri zote zilizopo nchini kutenga maeneo ya  michezo kwasababu michezo  ni ajila hivyo tukiwa na viwanja vingi kwanza vitasaidia mapato kwenye halmashauri husika”Alisema Kiganja.

Kwa upande wake Mwandaaji wa michuano hiyo ,Mh Doto Biteko alisema kuwa matarajio ni kuona vijana wa Wilaya ya Bukombe wanatoka kwenye michezo na kufika nafasi ya juu zaidi ikiwa ni pamoja na kutoa timu ambayo itapanda daraja na kuchenza fainali kubwa zinazoendelea hapa Nchini.

Imeandaliwa na Mtandao wa Maduka Online.

WATOTO 1,300 WALIOPOTEA POLISI WAANDA KUWASAKA.


JESHI la Polisi mkoani Pwani, limesema limeanza kuwasaka wanafunzi 1,300 wanaodaiwa kutoweka wilayani Kibiti.
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya gazeti dada la hili la MTANZANIA kumnukuu Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali (IGP) Simon Sirro, akisema kuwa taarifa za kutoonekana kwa watoto hao zimetoka Idara ya Elimu na Wazazi.

IGP Sirro ambaye alizungumzia suala hilo alipokuwa katika ziara ya kikazi mkoani Pwani mapema wiki hii, hata baadaye alipozungumza na chumba hiki cha habari alisisitiza kuwa

“Kama mtoto humwoni shuleni wala nyumbani ni lazima uripoti.”

Jana MTANZANIA Jumamosi, lilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jonathan Shana, ambaye alisema msako wa watoto hao utafanywa kwa kushirikiana na walimu pamoja na wazazi wao.

Kamanda Shana pamoja na kuwataka baadhi ya watu kupingana na hisia kwamba watoto hao wamejiunga na vikundi vya kigaidi, alisisitiza kuwa Jeshi la polisi litakuja na majibu sahihi kuhusu mahali walipo watoto hao.

“Tumekubaliana kufanya operesheni ili kuhakikisha watoto hao wanapatikana, taarifa hii inashtusha kwa kuwa wapo watu ambao wanahusisha kupotea kwa watoto hao na ugaidi, wanadhani wamejiingiza katika vikundi hivyo jambo ambalo si kweli,” alisema Kamanda Shana.

Alisema operesheni hiyo pia itawagusa watoto ambao wanashindwa kuhudhuria masomo yao kwa sababu  ya mashinikizo ya wazazi ikiwemo kuwafanyisha kazi za nyumbani.

“Watoto ambao hawaendi shule tumepanga kushirikiana na walimu kupita nyumba hadi nyumba kuhakikisha tunawashurutisha wazazi kuwaamrisha watoto wao waende shule kama sheria inavyotaka, sheria ipo wazi katika hilo,” alisema Shana.

Taarifa za kupotea kwa watoto hao katika kipindi cha kati ya mwaka 2016 na Julai mwaka huu, zilipatikana juzi wakati IGP Sirro alipofanya ziara ya kikazi wilayani Kibaha, Pwani.

Katika ziara hiyo, IGP Sirro alizungumza na wazazi, walimu, viongozi wa mashirika ya umma, wazee maarufu, wastaafu mbalimbali na kamati ya ulinzi na usalama mkoani Pwani kuhusu taarifa hizo.

Kupitia mkutano huo, IGP Sirro, alieleza taarifa ya wanafunzi zaidi ya 1,300 mkoani humo ambao hadi sasa hawajulikani walipo na hawajaonekana shule wala katika familia zao.

IGP Sirro alisema huenda watoto hao ni watoro, hivyo aliwataka wazazi washirikiane na Jeshi la Polisi kujua walipo.

Pia aliwataka wazazi kusaidiana na walimu wa shule za msingi na sekondari, ambazo wanafunzi walikuwa ni watoro ama hawajaripoti shule kwa miezi kadhaa, kutoa taarifa kwani wapo baadhi ya watoto wanaotumika kufundishwa uhalifu hata wa kutumia silaha na watu wasio wema.

Kutokana na utata wa taarifa hizo, gazeti la MTANZANIA la jana lilizungumza na IGP Sirro, ambaye alisema taarifa za kutoonekana kwa watoto hao zinatokana na Idara ya Elimu na wazazi.

“Ni taarifa ya muda mrefu, kipindi cha mwaka jana na mwaka huu, ni zaidi ya mwaka mmoja niliipata Wizara ya Elimu kule, ndiyo maana nimeelekeza wazazi ambao hawawaoni watoto wao kutoa taarifa.

Hadi sasa haijaelezwa wanafunzi hao waliopotea ni wa shule za msingi au sekondari.

Taarifa hizo zimekuja katika wakati ambao hali ya usalama katika wilaya ya Kibiti na Rufiji imeimarika tofauti na miezi kadhaa iliyopita, lilipoibuka kundi la wahalifu ambao walikuwa wakiua watu wakiwamo askari polisi.

Mauaji yaliyotikisa wilayani humo yalisababisha si tu hofu bali baadhi ya watendaji kukimbia vituo vyao vya kazi.

Hivi karibuni IGP Sirro alisema hali ya usalama imerejea katika maeneo hayo yaliyokumbwa na mauaji na zaidi alisisitiza kuwa wahalifu waliokuwa wakitekeleza vitendo hivyo vya kinyama wamekimbilia katika nchi jirani ya Msumbiji.

Chanzo Mtanzania

Friday, December 1, 2017

JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LAKANUSHA SUMU UKUMBI WA MKUTANO UVCCM.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
 JESHI LA POLISI TANZANIA
TELEGRAMS:   POLISI,  
TELEPHONE: 2500712                                                   
KAMANDA WA POLISI,
Fax: 2502310                                                   
MKOA WA MWANZA,

E-mail: mwapol@yahoo.com                                                                                     
S.L.P. 120,          
rpc.mwanza@tpf.go.tz                                                                                
MWANZA.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA KWA VYOMBOVYA HABARI LEO TAREHE 30.11.2017 

KAMANDA   WA   POLISI   MKOA   WA   MWANZA   AMEKANUSHA   TAARIFA   ILIYOPOKATIKA GAZETI LA MWANANCHI LA TAREHE 30/11/2017.

LEO TAREHE 30.11.2017 KAMANDA WA POLISI MKOA WA MWANZA NAIBU KAMISHINA WAPOLISI AHMED MSANGI, AMEKANUSHA TAARIFA ILIYOPO KATIKA GAZETI LA MWANANCHILA TAREHE 30/11/2017, TOLEO NAMBA 6334, UKURASA WA TATU, INAYOSEMA KUWAAMETHIBITISHA  JUU  YA KUWEPO HEWA  YA SUMU  NDANI  YA UKUMBI WA  CITY MALL AMBAPO KULIKUWA KUKIFANYIKA MKUTANO MKUU WA UCHAGUZI WA VIJANA WA CCM(UVCCM) MKOA WA MWANZA.

AIDHA KAMANDA MSANGI ANASEMA, UKWELI NI KUWA ALIPIGIWA SIMU NA MWANDISHIWA   GAZETI   HILO   TAREHE   29/11/2017   MAJIRA   YA   SAA   15:00   MCHANA   ALIYETAKAKUTHIBITISHIWA TAARIFA YA KUWEPO HEWA YA SUMU NDANI YA UKUMBI WA CITY MALLAMBAPO   KULIKUWA   KUKIFANYIKA   MKUTANO   TAJWA   HAPO   JUU.   

KAMANDA   ALIMJIBUKUWA   HANA   TAARIFA   NA   HAWEZI   KUTHIBITISHA   KWANI   HAJAPATA   TAARIFA   YEYOTE KUHISIANA NA YALIYOTOKEA KATIKA MKUTANO HUO, NA YEYE YUPO KWENYE KIKAO CHAKAMATI YA ULINZI NA USALAMA OFISI YA MKUU WA MKOA.

PIA   KAMANDA   HAKUFIKA   ENEO   TAJWA   KAMA   TAARIFA   HIYO     INAVYOSEMA,   HIVYOINAONEKANA MWANDISHI WA TAARIFA HIYO ALIAMUA KUANDIKA MANENO HAYO KWA MANUFAA YAKE BINAFSI HIVYO JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINAOMBA GAZETIHUSIKA KUREKEBISHA. 

PIA ANAOMBA WAELEWE KUWA MATUKIO YA AINA KAMA HIYOYANAHITAJI   YAWE   NA   MAJIBU   YA   KITAALAMU   TOKA   KWA   WANASAYANSI   PINDIYANAPOTOKEA.

 AIDHA JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINANAEDELE KUOMBA USHIRIKIANO TOKAKWA WAANDISHI WA HABARI KWA KUFANYA KAZI KWA PAMOJA ILI KUWEZA KUENDELEAKUDUMISHA   USALAMA   NA   ULINZI   KATIKA   MKOA   WETU.  

 PIA   JESHI   LINAWAOMBAWAANDISHI   WA   HABARI   KUFANYA   KAZI   KWA   KUFUATA   TAALUMA   YA   UANDISHI   WAHABARI, UWELEDI NA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI ILI KUEPUSHA HABARI ZA AINAKAMA HII AMBAZO ZINALETA PICHA MBAYA KWA JESHI NA MKANGANYIKO KWA JAMII.

IMETOLEWA NA;DCP: AHMED MSANGIKAMANDA WA POLISI (M) MWANZA

Thursday, November 30, 2017

WANAFUNZI WANAOSOMEA UDAKTARI CHUO CHA SAYANSI YA AFYA BUGANDO WAJA NA HILI ZURI KUADHIMISHA MAADHIMISHO SIKU YA UKIMWI DUNIANI



Kuelekea siku ya maadhimisho ya Ugonjwa wa ukimwi Duniani wanafunzi wa chuo kikuu cha sayansi ya afya na tiba cha Bugando (CUHAS) mkoani Mwanza kimejitolea kutoa huduma ya upimaji wa virusi vya Ukimwi bure pamoja na kutoa ushauri nasaha ili kuongeza hamasa kwa wananchi kupima afya zao.

Timon Steven.
Akizungumza chuoni hapo rais wa wananfunzi wa chuo kikuu  cha sayansi ya tiba cha Bugando (CUHAS ) Mkoani Mwanza Timon Steven anaeleza lengo la kutoa huduma ya upimaji wa virusi siku ya Ukimwi.


NAGMA GIGA- AWATAKA WAZAZI KUPINGA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA.

 IMG-0287-NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Zanzibar ,  Nagma Giga akifungua mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Jumuiya hiyo uliofanyika Amani Unguja.
 

 BAADHI ya wajumbe wa Mkutano huo wakisikiliza kwa makini hotuba ya ufungunguzi ya mgeni rasmi.
BAADHI ya wajumbe wa Mkutano huo wakisikiliza kwa makini hotuba ya ufungunguzi ya mgeni rasmi.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Amani, Abdi Ali Mzee “Mrope” akiwasalimia wajumbe wa mkutano huo wa uchaguzi jumuiya ya wazazi Mkoa wa Mjini.
 

 BAADHI ya wajumbe wa Mkutano huo wakisikiliza kwa makini hotuba ya ufungunguzi ya mgeni rasmi.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mjini Mohamed Omar Nyawenga(kushoto) Naibu katibu Mkuu wa Jumuiya ya wazazi Zanzibar Nagma Giga (katikati) na viongozi wengine wa jumuiya ya wazazi.

Na Is-haka Omar, Zanzibar.

NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Nagma Giga amewataka wazazi na walezi kuunga mkono juhudi za serikali na wanaharakati katika kupinga vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto nchini.

Kauli hiyo ameitoa wakati akifungua mkutano Mkuu wa uchaguzi wa Wazazi katika Mkoa wa Mjini, uliofanyika Amaani Unguja.

Alisema wazazi ndio walezi na waangalizi wa malezi ya makundi yote katika jamii hivyo ni lazima wawe mstari wa mbele kupinga vitendo vyote vinavyoensda kinytume na maadili, mila desturi na utamaduni visiwani humo.

Alifafanua kwamba ushindi dhidi ya vitendo vya udhalilishaji itafanikiwa endapo jamii itakuwa tayari kushirikiana na Serikali na vyombo vingine vya kisheria ili kudhibiti uhalifu huo unaochafua heshima na sifa ya nchi kitaifa na kimataifa.

"Hii ni vita yetu sote kila mzazi amuone mtoto wa mwenziwe kama wake hapo ndipo tutakapoweza kuwalinda watoto wetu ili wakue katika malezi bora yasioyokukuwa na vikwazo vya kukatisha malengo yao ya baadae.

Wanawake na watoto wengi wamekuwa ni wahanga kubakwa,kulawitiwa na kutelekezwa hali inayosababisha wengi wao kuathirika kisaikolojia ” Alieleza  kwa uzuni Nagma.

Pia aliwasihi wazazi, viongozi wa dini na wanasiasa nchini kuhakikisha wanakemea kuporomoka kwa maadili kwa baadhi ya vijana wanaovaa nguo zinazokwenda kinyume na utamaduni sambamba na kutumia lugha zisizofaa katika jamii.

Akizungumzia Uchaguzi wa Mikoa mbali mbali ya jumuiya hiyo, Nagma aliwasisitiza wajumbe wa mikutano hiyo kuwachagua viongozi imara na wenye dhamira ya kweli katika kuleta mabadiliko ya kimaendeleo ndani ya jumuiya na Chama Cha Mapinduzi kwa ujumla.

Aliwasisitiza wasimamizi wa uchaguzi huo kutenda haki na wapiga kura kuwa na uadilifu wakati wa kutekeleza wajibu wao wa kidemokrasia kwa kuchagua viongozi wanaowataka bila ya kufanya vurugu.

Naibu Katibu Mkuu huyo, alisema Jumuiya hiyo ina majukumu mawili makubwa ya kuhakikisha CCM inashinda na kubakia madarakani kupitia uchaguzi mkuu wa Dola sambamba na kusimamia mwenendo wa elimu, malezi, utamaduni na mazingira kwa jamii.

Alisema nchi zilizoendelea Ulimwenguni ni zile zilizowekeza katika sekta ya elimu inayozalisha wataalamu wa fani mbali mbali za kuleta maendeleo ya haraka katika kukuza uchumi wa nchi kupitia mfumo wa uzazilishaji mali katika sekta za viwanda vinavyotegemea mfumo wa sayansi na teknolojia.

“Kila wana CCM anatakiwa kuchukua jukumu la kuwaelimisha vijana wetu wasome kwa bidii ili Chama na jumuiya zetu ziwe na wanachama wengi wenye uwezo mzuri wa kitaaluma watakaoweza kusimamia maslahi ya taasisi zetu bila kuyumba.

Mikakati hiyo itafanikiwa kama tutapata viongozi makini kupitia uchaguzi huu ambao ni wapambanaji wasiochoka wala kukata tama katika uwanja wa kisiasa.” Alifafanua Naibu Katibu Mkuu Giga.

Naye Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Amani ambaye ni mjumbe wa Mkutano huo, Abdi Ali Mzee ‘’Mrope’’ alisema wakati umefika wa Chama cha Mapinduzi na jumuiya zake kuwa na ajenda moja ya kutumia vizuri rasilimali zinazomilikiwa na Chama kuanzisha miradi mikubwa itakayozalisha kipato na kutoa ajira za kudumu kwa vijana.

Kwa upande wake mjumbe wa Mkutano huo, Salma Abdi Ibada aliwashauri viongozi watakaochaguliwa kupitia uchaguzi huo wawe mfano wa kuigwa katika  kuleta maendeleo ndani ya jumiya na kupiga vita vitendo vya rushwa na makundi ya kuhatarisha uhai wa Chama.

Uchaguzi huo umefanyika katika mikoa yote jumuiya ya Wazazi nafasi ambazo zinagombewa ni Wenyeviti wa Mikoa,  nafasi ya Mkutano mkuu taifa /Baraza la wazazi taifa, nafasi mkutano mkuu wa CCM mkoa, pamoja na nafasi za Baraza kuu la wazazi Mikoa kutoka kila Wilaya.

WCF YAPATA HATI SAFI KATIKA UKAGUZI WA TAARIFA YA FEDHA ULIOFANYWA NA CAG


 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, akifafanua baadhi ya mambo wakati viongozi wa Mfuko walipokuwa wakiwasilisha taarifa za utendaji wake kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mwaka wa Wadu kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC, jijini Arusha leo Novemba 30, 2017.

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, ARUSHA

MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF) umepata hati safi katika taarifa ya hesabu zake za fedha katika kipinmdi cha mwaka 2015-2016 ikiwa ni mwaka mmoja tu tangu kuanzishwa kwake.

Katika taarifa hiyo mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2016 (mwaka wa kwanza tangu kuaza kufanya kazi zake), thamani ya Mfuko ilifikia shilingi bilioni 65.68 na mfanikio haya yaliweza kufikiwa kutokana na ubunifu na ushirikiano mkubwa kati ya Mtendaji Mkuu wa Mfuko na Bodi ya Udhamini, Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Mfuko huo, Bw.Bezil Kwala, aliwaambia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Wadau wa Mfuko huo unaoingia siku yake ya pili nay a mwisho kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC jijini Arusha, wakati akiwasilisha taarifa hiyo ya fedha leo Novemba 30, 2017.
Amesema Mfuko umekuwa ukiaandaa hesabu zake kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya uaandaji wa hesabu za fedha na kwa mujibu wa sheria CAG ndiye mwenye mamlaka ya kufanya ukaguzi na Hati Safi ni uthibitisho wa taarifa ya fedha za Mfuko kuonyesha hali halisi na kutokuwa na dosari ya aina yoyote.
Amesema katika ukaguzi huo, CAG alishirikiana na kampuni ya PricewaterhouseCoopers (PwC). Mwakilishi wa kutoka Ofisi ya CAG, Bw…….. amethibitishia wajumbe usahihi wa taarifa hiyo ya fedha ya WCF.
Mkutanmo huo ambao umeanza Novemba 29, 2017 na kubeba kauli mbiu isemayo, "Mafao ya Fidia: Haki ya Mfanyakazi na chachu katika kukuza uchumi wa viwanda”, pia ulipokea taarifa ya mipango ya uwekezaji ambapo Bw. Kwala aliwaambia wajumbe kuwa, katika kipindi kati ya mwaka 2017/18 – 2021/22, Mfuko umepanga kuwekeza kwenye miradi mbalimbali itakayoleta faida kwa mujibu wa tathmimi za kitaalamu zitakazofanyika.
“Maeneo tuliyoyaanisha katika uwekezaji kwenye sekta ya viwanda ni pamoja na kiwanda cha Grape Processing Factory kwa ushirikiano kati ya  GEPF na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, kiwanda cha Madawa mkoani Simiyu kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na Kiwanda cha Morogoro Canvas Mills kwa kushirikiana na mifuko ya WCF, NSSF, PSPF, GEPF, na LAPF”. Alifafanua.
Akifafanua zaidi kuhusu umuhimu wa Mfuko kuwekeza, Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw.Masha Mshomba alisema, fedha zitokanazo na michango ya Wanachama ni kidogo ukilinganisha na mahitaji halisi ya ulipaji Mafao ya fidia na kwa hali hiyo, ni muhimu Mfuko kuwekeza ili kupanua wigo wa kuongeza mapato na hivyo kuendelea kutoa Mafao ya Fidia bila ya shaka yoyote.
 Baadhi ya Wakurugenzi na Wakuu wa Idara wa WCF wakiwa kwenye mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, akizungumza
 Mkurugenzi wa Fedha WA WCF, Bw.Bezil Kwala, akiwasilisha ripoti ya fedha ya Mfuko kwa mwaka wa 2015-2016.
 Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Ofisi ya Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Johanes Joel Kisiri, akisikiliza uwasilishaji wa taarifa hiyo ya fedha.
 Mkuu wa Kitengo cha Sheria cha WCF, Bw.Abraham Siyovelwa, akitoa mada kuhusu Sheria juu ya kuanzishwa kwa Mfuko na jinsi unavyofanya kazi zake. Pamoja na mambo mengine Bw. Siyovelwa aliwaambia wajumbe kuwa,   Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ni taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoazishwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Sura Na. 263 (Marejeo ya 2015) na kuanza kazi rasmi tarehe 1 Julai 2015. Lengo la kuazishwa kwa Mfuko ni kushughulikia masuala ya fidia kwa wafanyakazi waliopo katika sekta rasmi (Binafsi na Umma) Tanzania bara ambao wataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi
 Mkurugenzi wa Uendeshaji wa WCF, Bw. Anslem Peter, akiwasilisha taarifa ya uendeshaji ya Mfuko katika kipindi cha uahai wake, ambapo alisema Mfuko umekuwa ukifanya vizuri ikiwa ni pamoja na usajili wa wanachama " katika kipindi cha kuanzia mwaka 2015-2017 jumla ya Waajiri 5,178 walisajiliwa ikiwa ni asilimia 71.92 ya lengo la kusajili waajiri 7,200

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Dkt.Irene Isaka.
 Kiongozi wa chama cha Waajiri nchini (ATE), Bw. Aggrey Mlimuka, akizungumza kwenye mkutano huo.
 Bw. Hiroshi Yamabana kutoka Shirika mla Kazi Duniani, (ILO), akiuliza masuala mbalimbali kuhusu upembuzi juu ya usalama mahala pa kazi
 Tommie Dounball, kutoka kampuni ya Argen ya Afrika Kusini, akizungumzia uzoefu wa masuala ya Mfuko wa Fidia kutoka nchini kwake

 Bw. Mshomba (kushoto), akizungumza jambo wakati wa mkutano huo. Kulia ni Bw.Tommie Dounball, kutoka kampuni ya Argen ya Afrika Kusini,

 Mbunge wa jimbo la Mlalo Mkoani Tanga, Mhe. Rashiud Shangazi, (kushoto), akimsikiliza Meneja Uhusiano wa PPF, Bi. Lulu Mengele. Wote hao ni miongoni mwa wadau walioalikwa kushiriki mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wdhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, (kulia), akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Taifa wa Bima ya Afya, (MHIF), Bw. Afya, Bw. Bernard Konga.
Mkurugenzi wa Matekelezo na Uandikishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Lightness Mauki