ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 15, 2017

TAIFA STARS SARE NA RWANDA 1-1 CCM KIRUMBA MWANZA.

TIMU ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeshindwa kutamba katika uwanja wa nyumbani baada ya kukubali sare ya bao 1-1 dhidi ya Rwanda ‘Amavubi’ katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza

Amavubi ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika ya 17 kupitia kwa Domicique Nshuti dakika ya 18 kabla ya Himid Mao kuisawazishia Taifa Stars dakika ya 34 kwa mkwaju wa penalti.


Matokeo hayo yanaipa wakati mgumu Taifa Stars, kwani inatakiwa kushinda katika mchezo wa marudiano utakaochezwa Jumamosi ijayo jijini Kigali Rwanda.


Taifa Stars ikifanikia kushinda katika mchezo huo wa marudiano itasonga mbele katika hatua nyingine ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Mataifa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN) zitakazofanyika Kenya mwakani.































HUYU HAPA BINTI ALIYEONGOZA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA.

Sophia Juma, mwanafunzi wa St Marry’s Mazinde Juu ya Tanga ameibuka kidedea katika matokeo ya kidato cha sita yaliyotangazwa leo Jumamosi, Julai 15, akishika namba moja kitaifa.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk Charles Msonde imeeleza kuwa nafasi ya pili imeshikwa pia na msichana, Agatha Julius Ninga wa Tabora Girls. Wote walikuwa wakichukua masomo ya mchepuo wa Sayansi (PCB).

Kadhalika taarifa hiyo imeeleza kuwa wasichana wameongoza kwa ufaulu ambapo kati ya wasichana 28,731 (38 asilimia) waliofanya mtihani, waliofaulu ni 27,577 (sawa na asilimia 97.21).

Jumla ya watahiniwa 75, 116, walifanya mtihani huo Mei mwaka huu.

 Kwa upande wa watahiniwa wavulana, waliofaulu walikuwa ni 42,975 (sawa na asilimia 95.34) kati ya 46,385.

“Mchanganuo wa ufaulu katika madaraja unaonyesha kuwa watahiniwa walipata daraja la 1-11  umepanda  kwa asilimia 0.59 kutoka asilimia 93.13 mwaka 2016 hadi 93.72 mwaka huu,” imesema taarifa hiyo na kuongeza;

“Pia ufaulu katika madaraja kwa upande wa wasichana umepanda ikilinganishwa na wavulana. Ubora wa ufaulu kwa wasichana ni asilimia 94.07 ikilinganishwa na asilimia 93.49 ya wavulana.”

Shule zilizoongoza

Katika matokeo hayo, Shule ya Wasichana ya Feza Girls ya Dar es Salaam imeibuka kinara kwa watahiniwa wake 67 kufaulu kwa kupata daraja la kwanza na la pili.

Shule nyingine zilizoibuka kidedea katika matokeo hayo ni Marian Boys (Pwani) iliyoshika nafasi ya pili, Kisimiri (Arusha) imeshika nafasi ya tatu na Ahmes (Pwani) imeshika nafasi ya nne.

Shule nyingine  ni  Marian  Girls (Pwani) iliyoshika nafasi ya tano, Mzumbe (Morogoro) nafasi ya sita, St Marry Mazinde Juu (Tanga) nafasi ya saba, Tabora Boys (Tabora) nafasi ya nane, Feza Boys (Dar es Salaam) nafasi ya tisa na Kibaha ya Pwani iliyoshika namba kumi.

Shule zilizoshika mkia

Shule zilizoshika mkia ni Kiembesamaki ya Unguja, Hagafilo (Njombe), Chasasa (Pemba), Mwenyeheri Anuarite (Dar es Salaam) na Ben Bella (Unguja). Nyingine zilizotajwa kushika mkia ni Meta (Mbeya) na Mlima Mbeya (Mbeya).

Nyingine ni Shule ya Sekondari ya Al-Ihsan Girls (Unguja) na St Vicent(Tabora).

Waliofutiwa matokeo

Kadhalika taarifa ya Necta imeeleza kuwa watahiniwa 10 walifutiwa matokeo kwa makosa ya kufanya udanganyifu.

Taarifa ya Dk Msonde imeeleza kuwa kati ya watahiniwa hao kumi, saba ni wa shule na watatu ni wa kujitegemea.

Pamoja na hao kumi, watahiniwa wengine 15 hawakufanya mitihani ya baadhi ya masomo kutokana na  matatizo mbalimbali ikiwamo ya kiafya na hivyo kushindwa kufanya mitihani hiyo.

‘Watahiniwa hao wamepewa fursa ya kufanya mitihani ya kidato cha sita, Mei 2018 kama watahiniwa wa shule,” imesema taarifa ya Dk Msonde.

Pia, wapo watahiniwa 69 wa shule ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mitihani yote yote, wamepewa fursa ya kufanya mitihani hiyo, Mei 2018.



TOVUTI YA BARAZA LA MITIHANI TANZANIA (NECTA)


MATOKEO KIDATO CHA SITA (ACSEE) 2017


MATOKEO YA DIPLOMA YA UALIMU (DSEE) 2017


MATOKEO YA CHETI CHA UALIMU (GATCE) 2017

KOCHA WA TIMU YA TAIFA YA RWANDA AIFANANISHA PEACH YA UWANJA WA CCM KIRUMBA NA MATUTA YA VIAZI.

Kushindwa kupata ndege ya kuunganisha moja moja toka Kigali nchini Rwanda hadi Mwanza, kunasababisha wachezaji wa Rwanda Amavubi, kuwasili jijini humo kwa mafungu.

Ni wachezaji 11 na kocha wao ndiyo wamewasili mkoani hapa majira ya saa 2 asubuhi kwaajili ya kipute hicho huku wengine 7 wakisalia jijini Dar es salaam wakitaraji kutinga jijini hapa na ndege ya usiku.

Kocha Mkuu wa timu hiyo Antoine Hey analazimika kulishushia lawama shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) kwa kupanga mchezo huo CCM Kirumba badala ya Uwanja wa Taifa Dar es salaam na kisha anaongeza malalamiko yake kwa shirikisho kushindwa kutumia fair play kulisogeza mbele pambano hilo dhidi ya Taifa Stars.

 Kocha Hey ameiponda peach ya dimba la CCM kirumba akiifananisha na matuta ya viazi lakini yote tisa TFF wanasema mchezo uko pale pale.

Mimi ni Albert G Sengo wa Gsengo Tv.

Friday, July 14, 2017

RC GAMBO AWAONYA WAGEUZAO SHULE KUWA MATAWI YA SIASA.

Mkuu wa mkoa wa ARUSHA,MRISHO GAMBO,ameonya shule kutogeuzwa kuwa matawi ya siasa na walimu wakuu kuacha kuruhusu hali hiyo na iwapo watabainika kukiuka agizo hilo watachukuliwa hatua za kisheria.

Gambo anatoa onyo hilo wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa wakuu wa shule za sekondari ARUSHA-TAHOSA-na kutoa angalizo kuwa shule ni eneo kwa ajili ya kutoa elimu kwa wanafunzi na si kitovu cha siasa.

Amesema kuna tabia imeanza kuibuka ya baadhi ya shule kugeuzwa vijiwe vya siasa na kuyataka mashirika yasiyo ya kiserikali endapo yanalengo la kusadia wanafunzi wanaopata mimba mashuleni ni vyema wakaweka mawakili wakuwaadhibu watu wanaowapa ujauzito wanafunzi.

Wakuu hao wa shule wametaja kuwa mkutano huo kuwa ni mojawapo ya jitihada mbalimbali wanazozifanya kuboresha elimu katika shule za sekondari mkoani ARUSHA

KANDA YA ZIWA KUNEEMEKA NA MIKOPO YA TADB

 Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella (kulia) akizungumza na viongozi kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) walipomtembelea Ofisini kwake jijini Mwanza. Viongozi hao walikuwa kwenye ziara rasmi ya kukabidhiwa jengo litakalotumiaka kama Ofisi ya TADB Kanda ya Ziwa. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Matutu Chacha na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (wapili kushoto).
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (kulia) akizungumza na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella (hayupo pichani) wakati wa ziara rasmi ya kukabidhiwa jengo litakalotumiaka kama Ofisi ya TADB Kanda ya Ziwa.
 Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella (mwenye kofia) akifuatana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (aliyevaa) kuelekea kwenye makabidhiano ya jengo litakalotumiaka kama Ofisi ya TADB Kanda ya Ziwa. 

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (mbele kulia) akipokea funguo za  kukabidhiwa jengo litakalotumiaka kama Ofisi ya TADB Kanda ya Ziwa  kutoka kwa Meneja wa Wakala wa Majengo ya Serikali mkoa wa Mwanza, Mhandisi Yohana Mashausi (kushoto). Wanaoshuhudia ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella (mwenye kofia) na Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Matutu Chacha (kulia).

Kanda ya Ziwa kuneemeka na Mikopo ya TADB
Na Mwandishi wetu,
Katika kutimiza ahadi ya Mhe. Rais Dkt. John Magufuli, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imedhamiria kuwaneemesha wakulima wa Kanda ya Ziwa kwa kufungua Ofisi ya Kwanza ya Kanda yenye lengo la kuwapatia mikopo yenye gharama nafuu wakulima wa Kanda ya Ziwa.

Akizungumza wakati wa makadhiano ya jengo litakalotumika kama Ofisi ya TADB Kanda ya Ziwa, Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella alisema kuwa Benki ya Kilimo ikiwa ni taasisi ya umma ina wajibu kusaidia juhudi za Serikali katika kuinua ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini nchini Tanzania hasa katika kuchagiza mapinduzi na maendeleo katika Sekta ya Kilimo, ambayo inaajiri zaidi ya asilimia 75 ya watu wenye uwezo wa kufanya kazi nchini na pia kutoa kiasi cha zaidi ya  asilimia 65 cha mali ghafi kwa ajili ya viwanda vya nchi.
“Uanzishwaji wa TADB unatokana na Serikali kutambua umuhimu wa uwekezaji wenye tija kwenye maeneo yote ya sekta ya Kilimo na kuleta mapinduzi ya dhati ya Kilimo ili kuwezesha upatikanaji wa mikopo na mitaji ya riba nafuu  ikiwa ni pamoja na kuhamasisha mabenki na taasisi zingine za fedha nchini kutoa mikopo zaidi kwenye sekta ya Kilimo,” amesema.
Mhe. Mongella alisema kuwa Kanda ya Ziwa ina utajiri mkubwa kwenye uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara ambayo ni mojawapo wa minyororo ya thamani ya mwanzo inayopatiwa mikopo kwa ajili ya uongezaji wa thamani mazao mbalimbali na Benki ya Kilimo.
Aliongeza kuwa maendeleo ya sekta ya kilimo inahitaji msaada mkubwa wa uwezeshwaji wa mikopo kutoka TADB kwa kuzingatia kuwa ni chombo cha serikali kilichoanzishwa ili kusaidia upatikanaji wa utoshelezi na usalama wa chakula ambao ni endelevu nchini Tanzania.
“Kwa kutambua jukumu kubwa la TADB katika kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka   kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini, Ofisi ya Mkoa wa Mwanza iliona kuna umuhimu wa kuipatia Benki hii jengo hili iweze kuwafikia wakulima wa Kanda ya Ziwa na maeneo ya jirani,” aliongeza.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis Assenga alisema Benki ya Kilimo imedhamiria na kujizatiti kuhakikisha inachangia kwa kiasi kikubwa katika  kuleta Mapinduzi yenye tija katika Sekta ya Kilimo nchini kwa kusaidia upatikanaji na utoaji wa fedha ikiwa ni pamoja sera nzuri zitakazosaidia maendeleo ya kilimo nchini.
Bw. Assenga aliongeza kuwa TADB imejipanga kutekeleza malengo ya Serikali katika kuanzisha Benki hiyo ili kusaidia kukabiliana na mapungufu hayo na kuhuisha upatikanaji wa mikopo katika sekta ya kilimo ili kuleta mapinduzi katika  kilimo nchini.
“Kanda ya Ziwa ni eneo la kimkakati hivyo ujio wetu ni kutimiza dhamira ya dhati ya serikali katika kutatua changamoto za ufinyu mkubwa wa upatikanaji wa fedha mikopo kwa ajili ya maendeleo ya kilimo nchini unachangiwa kwa kiasi kikubwa na mikopo mingi kutoka taasisi za fedha kuelekezwa zaidi kwenye upande wa biashara za bidhaa; riba kubwa kwenye mikopo ya kilimo; mikopo ya muda mfupi; masharti magumu ya kukopa bila kuzingatia hali halisi ya sekta ya kilimo  na mazao ambayo inaathiriwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya hali ya hewa,” alisema.
Aliongeza kuwa Benki ya Kilimo imejipanga kushirikiana na Serikali, wabia wa kimkakati na wadau wengine katika kuendeleza sekta ya kilimo, hasa kuboresha na kutekeleza na juhudi zozote sera zinazohusiana na kuhisha ushiriki wa wananchi kwenye mifumo ya kifedha.

TANAPA YAMPATIA DK JANE GOODALL TUZO YA UTAFITI WA MIAKA 60 YA MAISHA YA SOKWE TANZANIA


 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (kushoto) akimkabidhi  Dk. Jane Goodall tuzo maalumu kwa kutambua mchango wake wa utafiti wa miaka 60 wa maisha ya Sokwe  pamoja na uhifadhi wa wanyama wengine kwenye hifadhi ya Gombe, mkoani Kigoma  katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Tuzo hiyo iliandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa). Habari zaidi zitaletwa punde. (NA  RICHARD MWAIKENDA-KAMANDA WA MATUKIO BLOG)


Na Richard Mwaikenda
Jane ambaye ni raia wa Uingereza alianza utafiti katika Hifadhi ya Gombe mnamo miaka ya 60 akiwa na umri wa miaka 26.

Katika utafiti wake amegundua mambo mengi ikiwemo jinsi Sokwe wanavyojitambua, kuwa na hisia na jinsi wanavyoishi kwa ushirikiano kama walivyo binadamu.

Akizungumza katika hafla hiyo jane anasema wakati anaanza kufanya utafiti ilikuwa vigumu Sokwe hao kumkaribia kwani walikuwa wanamuogopa na ilikuwa ni mara ya kwanza kwao kumuona mtu mweupe, lakini alifanya jitihada hadi wakamzoea na kuanza kumsogelea na kumuona mtu wao wa karibu.

Anasema alitumia mbinu mbalimbali kama vile kuwapatia ndizi na vyakula vingine hadi wakamzoea.

Wakati wa hafla hiyo iliyofanyika katika Chuo cha Utalii katikati ya jiji la Dar es Salaam, viongozi na wageni waalikwa walipata wasaa wa kuangalia picha mbalimbali za matukio ya sokwe wakiwa na Jane Goodall.

Katika utafiti wake amefanikiwa kuanzisha chuo na kutunga vitabu pamoja na video zinazoelezea maisha yake na Sokwe katika Hifadhi ya Gombe mkoani Kigoma.

Katika hafla hiyo walihudhuria Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, Mwenyekiti wa Bodi ya Tanapa, Mkuu wa Majeshi mstaafu, Jenerali George Waitara, Mwanasiasa Mkongwe, Getrude Mongela, Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Goodall, Lembeli, Balozi wa Uingereza nchini, mabalozi mbalimbali pamoja na waalikwa.
Dk. Jane akikabidhiwa cheti cha kutambua mchange wake kwa Tanzania kwa kuhifadhi Sokwe na wanayama wengine


 Jane akipatiwa pia zawadi ya kinyago cha Sokwe
 Jane akikabidhiwa picha ya Sokwe
 Mama Mongela akimvisha Jane zawadi ya vitenge
 Dk Jane akitoa maelezo kuhusu maisha ya Sokwe
 Waziri Maghembe akipata maelezo kuhusu maisha ya Sokwe yalivyo
 Wasanii wa Tanapa wakitumbuiza kwa wimbo 


 Mwenyekiti wa Bodi ya Tanapa, Mkuu wa Mjeshi Mstaafu, Jenerali Waitara akitoa shukrani nyingi kwa Dk Jane kwa kazi kubwa aliyoifanya na kuiletea Tanzania sifa lukuki duniani
 Wageni waalikwa wakisikiliza kwa makini wakati Waziri Maghembe akihutubia katika hafla hiyo, ambapo alisema kuwa Dk. Jane ambaye wakati anaaza utafiti yeye alikuwa darasa la pili, lakini utafiti wake umeiletea sifa kubwa Tanzania na utakuwa ni urithi wa kipekee maishani
 Wageni waalikwa wakisikiliza kwa makini

 Profesa Magembe akihutubia katika hafla hiyo ya kumpatia tuzo Dk. Jane
 Baadhi ya mabalozi waliohudhuria hafla hiyo
 Dk Jane akielezea historia yake na jinsi alivyofanikiwa kufanya utafiti huo wa sokwe


 Lembeli akitoa neno la shukrani
 Jane akiwa katika picha ya pamoja na mabalozi waliohudhuria hafla yake pamoaja na viongozi mbalimbali


 Jane akiwa katika picha ya pamoja na wanahabari baada hafla kumalizika