ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 22, 2022

Benki ya CRDB yafuturisha wateja wake jijini Mwanza, yatoa zawadi kwa watoto

 

Benki ya CRDB imewafuturisha wateja wake jijini Mwanza ikiwa ni mwendelezo wa utamaduni wa benki hiyo kuungana na waumini wa dini ya Kiislamu wanaoishiriki mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Hafla ya Iftar hiyo imefanyika Alhamisi Aprili 21, 2022 katika ukumbi wa Gold Crest mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya Ilemela Hassan Masala na kuhudhuriwa pia na viongozi mbalimbali akiwemo Sheikh wa BAKWATA Mkoa Mwanza Hassan Kabeke.

Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta alisema benki hiyo imekuwa na desturi ya kujumuika pamoja na wateja wake katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na kupata Futari ya pamoja na kuimarisha mahusiano miongoni mwa pande zote mbili.

Sitta alitumia fursa hiyo waeleza waumini wa dini ya Kiislamu kwamba benki ya CRDB imeanzisha huduma ya Al-Barakah Banking inayoendana na misingi ya dini hiyo ikiwa ni pamoja na mikopo isiyo na riba na hivyo kuwaepusha kuingia kwenye dhambi ya riba.

Mkuu wa Huduma ya Al-Barakah Banking (Islamic Banking), Rashid Rashid alisema uanzishwaji wa huduma hiyo unadhihirisha kauli mbiu ya namna benki ya CRDB isemayo 'Benki Inayomsikiliza Mteja' ambapo kupitia maoni ya wateja wake iliamua kuanzisha huduma ya Al-Barakah.

Rashid aliongeza kuwa akaunti zinazofunguliwa kupitia huduma ya Al- Barakah zina uangalizi maalum unaohakikisha hazitumiki kwenye miamala inayokinzana na maadili ya imani ya kiislamu ikiwemo riba na kuwaondolea changamoto iliyokuwepo zamani ya kuhifadhi fedha kwenye mabenki yanayokinzana na misingi ya sharia.

Naye Sheikh wa BAKWATA Mkoa Mwanza, Hassan Kabeke aliishukuru benki ya CRDB kwa kuwaondolea waislamu na wasio waslamu dhambi ya kuingia kwenye riba baada ya kuanzisha huduma ya Al- Barakah kwani riba ni dhurma kubwa na watu wengi wamefirisika kutokana na kuingia kwenye dhambi hiyo, akisema "yeyote anayeingia kwenye riba ajiandae kupigana vita na Mwenyezi Mungu, CRDB wametutoa huko".

Sheikh Kabeke aliagiza misikiti, Kata na Wilaya zote za Mkoa Mwanza kutii maelekezo ya Mufti wa Tanzania ya kutaka akaunti zote za BAKWATA nchini kufunguliwa ndani ya huduma ya Al- Barakah. "Tumeanzisha mchakato wa kujenga Vituo vya Afya katika Wilaya zote saba za Mkoa Mwanza, akaunti ambayo tumewaomba waislamu na wasiokuwa waislamu wachangie humo michango yao ni akaunti ya Al-Barakah" alisema Sheikh Kabeke.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Ilemela, Hassan Masala alisema Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na benki ya CRDB katika kuwahudumia watanzania kupitia huduma zake zenye ubunifu ikiwemo Al-Baraka Banking inayowapa wasilamu huduma zinazotimiza matakwa ya dini yao.

"Tunatambua kazi kubwa mnayoifanya, miradi yetu mingi, fedha zetu nyingi na biashara kubwa, Serikali inafanya na benki ya CRDB, lakini mmeanzisha huduma ambazo zinagusa makundi mbalimbali kama hii ya Al-Barakah, kwa kweli tunaiona nia yenu njema" alisema Masala wakati akizungumza kwenye Iftar hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Meneja wa benki ya CRDB Kanda ya Ziwa akizungumza kwenye Iftar hiyo.
Meneja wa benki ya CRDB akizungumza kwenye Iftar iliyofanyika jijini Mwanza.
Mkuu wa Matawi Benki ya CRDB, Boniventure Paul alisema katika kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, lisha ya benki hiyo kujumuika pamoja na wateja wake kwenye futari pia hutoa msaada vyakula/ futari kwenye vituo vya kulelea watoto vyenye uhitaji mkubwa ili kuwawezesha watoto na walezi wao kutekeza vyema ibada ya swaum.
Mkuu wa Islamic Banking (Al-Barakah), Rashid Rashid akizungumza kwenye hafla hiyo.
Sheikh wa BAKWATA Mkoa Mwanza, Hassan Kabeke akizungumza kwenye Iftar hiyo.
Mkuu wa Wilaya Ilemela, Hassan Masala akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya Ilemela, Hassan Masala akizungumza kwenye Iftar hiyo ambayo aliwahimiza pia waislamu kuendelea kutenda matendo mema, kuswali na kujinyenyekeza mbele za Mwenyezi Mungu nyakati zote na si wakati wa Mwezi Mtukufu tu.
Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Hassan Masala akipata riziki ya Iftar iliyoandaliwa na benki ya CRDB jijini Mwanza.
Sheikh wa BAKWATA Mkoa Mwanza, Hassan Kabeke akiwa kwenye Iftar hiyo.
Mkurugenzi Mkuu Hospitali ya Kanda Bugando, Dkt. Fabian Massaga akichukua riziki kwenye Iftar hiyo akiwa ameambatana na wateja mbalimbali wa benki ya CRDB.
Wateja wa benki ya CRDB jijini Mwanza wakipata riziki ya Iftar.
Wateja wa benki ya CRDB jijini Mwanza wakiwa kwenye hafla hiyo.
Viongozi mbalimbali akiwemo Sheikh wa BAKWATA Mkoa Mwanza Hassan Kabeke (katikati) wakipata Iftar iliyoandaliwa na benki ya CRDB jijini Mwanza.
Wateja na wafanyakazi wa benki ya CRDB wakiwa kwenye Iftar hiyo.
Uongozi wa benki ya CRDB umetumia fursa hiyo pia kukabidhi zawadi ya bidhaa mbalimbali za vyakula kwa ajili ya watoto wanaolelewa katika Vituo mbalimbali jijini Mwanza.

Wednesday, April 20, 2022

WAZIRI MBARAWA APANIA UJENZI WA DARAJA KUBWA LA MTO WAMI KUKAMILIKA MWEZI JUNI



 Wazari wa ujenzi wa uchukuzi Profesa Makame Mbarawe wa kulia akigagua mradi wa ujenzi wa daraja la mto wami ambalo limejengwa kwa kiasi cha shilingi bilioni 75.1 kushoto kwake ni balozi wa china nchini Tanzania Mingijian Cheni alipofanya ziara ya kukagua mradi huo.

 


 Balozi wa china nchini Tanznaia Mingijian Cheni wa kulia akizungumza jambo na Waziri wa ujenzi na Uchukuzi wakati walipofanya ziara ya pamoja kwa ajili ya kuweza kukagua mwenendo na maendeleo ya ujenzi wa daraja la mto wami.


 Waziri wa ujenzi na uchukuzi akiwa katika picha ya pamoja na balozi wa china nchini Tanzania sambamba na baadhi ya viongozi wa Tanrods pamoja na wakandarasi wa mradi huo.

 


 Waziri Mbarawa pamoja na balozi wakiwa wanatembea kujionea maendeleo ya ujenzi huo wa mradi mkubwa wa daraja la mto wami.


 Picha ya pamoja na Waziri Mbarawa pamoja na Balozi wa china nchini Tanzania pamoja na watendaji wengine mara baada ya kuutembelea mradi wa ujenzi wa daraja la mto wami.

 NA VICTOR  MASANGU, PWANI

SERIKALI imesema kwamba kukamilika kwa mradi mkubwa wa ujenzi na daraja jipya la mto wami Julai  mwaka huu kutakuwa ni mkombozi mkubwa wa kupunguza wimbi la vifo kwa wananchi ambavyo vimekuwa vikitokana mara kwa mara  kutokana na kukithiri kwa changamoto ya kutokea kwa  ajali za barabarani kutokana na kuwepo  kwa miundombinu finyu katika daraja hilo la zamani.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa ambapo amemuagiza  mkandarasi  wa Power  Construction kukamilisha ujenzi wa daraja hilo ifikapo mwezi Juni mwaka huu badala ya  mwezi  novemba  21 mwaka huu kama ilivyokuwa  katika mkataba.

Pia waziri Mbarawa amemtaka mkandarasi Power Construction kukamilisha ujenzi wa Daraja la Mto Wami ifikapo Juni badala novemba mwaka huu ambapo daraja hilo litagharimu kiasi cha shilingi bilioni 75.1 mara litakapo kamilika.

 

Aliyasema hayo jana kwenye ujenzi wa Daraja hilo jipya lililopo Wami-Chalinze Wilayani Bagamoyo ambapo aliambatana na Balozi wa nchi ya China Ming Jian Chen na kuwa angependa arudi Juni 15 na kupita na gari kwenye daraja jipya na siyo la zamani.

 

Mbarawa alisema kuwa kukamilika kwa daraja hilo kutasaidia kuokoa maisha ya watu ambao walikuwa wakipoteza maisha pamoja na mali kuharibika kutokana na ufinyu wa barabara hiyo kwani magari hayawezi kupishana tofauti na daraja jipya ambalo litakuwa na urefu wa mita 500.

 

"Daraja la zamani limejengwa mwaka 1959 ni jembamba na ni la njia moja ningefurahi kuona muda mliopanga kukamilisha Julai usifike mmalize Juni ijapokuwa mwanzo ilipangwa kukamilika Novemba mwaka huu kwani watu wengi wamekuwa wakipata shida kwenye daraja la zamani,"alisema Mbarawa.

 

 

Kwa upande wake Balozi wa china nchini Tanzania amesema kwamba wataendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania katika miradi mbali mbali ya maendeleo na kwamba daraja hilo la mto wami litasaidia kupunguza kasi ya ajali kwa  wananchi  mbali mbali  wa Dar es salaam, Pwani pamoja na nchi nyingine za jirani.

Aidha balozi huyo alifafanua kuwa mradi huo wa Maendeleo unaunganisha Mji wa Kibiashara wa Dar es Salaam na mikoa ya Kaskazini na kuleta maendeleo na nchi yake itaendelea kushirikiana bega kwa began a serikali ya Tanzania katika kusaidia miradi mbali mbali ya ya maendeleo.

 

Naye Mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANRODS) Injinia  Hussen Mativila amebainisha kwamba  mradi wa daraja hilo ambalo lina urefu wa mita 5.15  limegharimu kiasi cha shilingi bilioni 75.1 na kwamba daraja la zamani ni chakavu na nifinyo  kutokan ana na magari kupita kwa shida kwani limejengwa tangu manamo  mwaka 1959.

Kadhalika mtendaji huyo mkuu wa Tanrods alisema kuwa mradi huo unagharimiwa na serikali na unatumia Teknolojia ya madaraja marefu kuna nguzo nne ambapo mbili zina urefu wa mita 19 nyingine ikiwa na urefu wa mita 37 na huku moja ikiwa na urefu wa mita 44.

 

 

Kukamilika kwa  mradi wa ujenzi  wa daraja hilo jipya la mto wami  lililopo katika halmashauri ya Chalinzi Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani kutaweza kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi pamoja na kupunguza wimbi za  ajali ambazo zimekuwa zikijitokeza mara kwa mara na kupoteza maisha ya watu.

                                                

WAFANYABIASHARA IRINGA WALALAMIKIA KUTOZWA KODI KUBWA

 

Moja ya barua ambazo wafanyabiashara waliopanga katika jengo la Halmashauri ya Iringa wakituma malalamiko kwa mkuu wa wilaya juu ya kutosikilizwa na ofisi ya mkurugenzi.
Hii ni barua kutoka kwa mkurugenzi akiwaalika wafanyabiashara kwenye kikao cha maridhiano juu ya bei zao



Na Fredy Mgunda,Iringa.

WAFANYABIASHARA waliopanga katika jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Iringa lililopo karibu na Stendi ya zamani ya Mabasi ya Mkoani wamelalamikia kutozwa kodi kubwa kutoka ofisi ya Halmashauri hiyo.

Wakizungumza na waandishi wa habari wafanyabiashara hao walisema kuwa wanalipishwa kodi kubwa kuliko biashara ilivyo katika eneo ambalo kwasasa halina wateja kama ilivyokuwa awali.

Walisema kuwa wamekuwa na majadiliano ya mara kwa mara na ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri hiyo lakini wamekuwa hawapati ushirikiano wa kutosha kutatua changamoto hiyo.

Raphati kaberege ni mfanyabiashira aliyepanga katika jengo hilo alisema kuwa wameandika barua ya kuomba kukutana na viongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa toka mwaka 2017 na hawajawahi kujibiwa.

“Kwa kweli mamlaka hawajahi kutupa ushirikiano licha ya kuwaandikia barua, Pia tumewahi kuwaalika katika eneo la biashara lakini hawajahi kufika, na ukiangalia mazingira ya biashara hayaridhishi kwani vyoo wakati mwingine vimejaa na mitaro imeziba jambo linalohatarisha afya zetu”alisema kaberege

Alisema kuwa wameitwa na mkurugenzi ili kufanya kikao cha majadiliano lakini mkurugezi hakufanikiwa kufika katika kikao hicho ambacho ofisi yake ilikiitisha kwa ajili ya majadiliano.

Kaberege alisema kuwa vyumba vya biashara ambavyo vinapangishwa na halmashauri ya Manispaa ya Iringa na vyumba vya biashara vya CCM Iringa ni gharama nafuu Zaidi kuliko halmashauri ya wilaya ya Iringa.

“Mfano CCM wanalipa wanatoza kiasi cha shilingi 50,000 hadi 70,000 na maeneo mengine yanayotazamana na jengo hilo wafanyabiashara wanalipa kwa gharama ya shilingi laki moja (100,000) hadi laki moja na nusu (150,000) kwa mwezi,tofauti na sisi” alisema kaberege

Isaack Steven ni Miongoni mwa wapangaji katika jengo hilo amesema kuwa kwa wafanyabiashara waliopanga milango ya mbele wanalipa shilingi laki tatu na nusu (350,000) huku waliopanga milango ya nyuma wakitozwa kodi ya shilingi laki Moja (100,000).

Alisema kuwa kodi hizo ni kubwa sana kwa kuwa eneo hilo kwa sasa halina mzunguko wa biashara baada ya standi kuhamishiwa eneo la igumbilo ambapo pia mazingira ya jengo hilo siyo rafiki kwani choo wanachotumia wanatozwa fedha nyingi.

Mfanyabiashara Alice Ngwale alisema kuwa licha ya kuchajiwa fedha kubwa ya pango ya mwezi pia wanashindwa kuendesha biashara zao kwani wamekuwa wakitoa fedha katika vyanzo vingine vya mapato ili waweze kulipia majengo hayo.

Wapangaji hao kwa kauli moja waliamua kuondoka katika Ofisi za Siasa ni kilimo baada ya Mkurugenzi wa halmashauri kushindwa kufika katika kikao hicho huku wakiiomba serikali kuwawekea utaratibu mzuri wa kulipa kodi kila mwezi au kila baada ya miezi mitatu na siyo kila baada ya miezi 6 jambo ambalo linawafanya washindwe kumudu gharama hizo.

 

 

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Stephen Mhapa alisema kuwa kama wanaona kuwa kodi waliyopangiwa ni kubwa bora wakaachia vyumba hivyo kwa kuwa wanafanya biashara sio kutoa huduma kwa wananchi.

Mhapa alisema kuwa hata ukienda kwa watu binafsi inaendana na gharama ambazo halmashauri inapangisha kwa wafanyabiashara waliopanga katika jengo hilo.

Alisema kuw malalamiko ya kushuka kwa biashara hayana mashiko kwa kuwa changamoto hiyo ipo na bado wafanyabiashara wengine wa jirani wanafanya biashara kwanini wawe wao.

Mhapa alimazia kwa kusema kuwa kama kuna changamoto ya kutosikilizwa basi wanapaswa kurudi tena kwenye ofisi yake ili watafutiwe njia mbadala ya kujibiwa kero hizo.