ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 19, 2017

SHAKA ASIFU UZALISHAJI WA ZAO LA KARAFUU, ASEMA SERIKALI ILINDE ASILI YA ZAO HILO

Zao la Karafuu

Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg Shaka Hamdu Shaka akipanda miti aina ya Mikoko Kwa ajili ya kutunza Mazingira wakati wa ziara yake katika eneo la Mwambe Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba

Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg Shaka Hamdu Shaka akiwasili katika eneo la Mwambe Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba kwa ajili ya kujionea hali ya upandaji miti aina ya Mikoko unavyoendelea.
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg Shaka Hamdu Shaka akizungumza jambo na Mdhamini wa Shirika la Bodi ya Taifa ya Biashara Zanzibar mara baada ya kutembelea ofisi hizo kujionea hali ya ukusanyaji wa zao la karafuu Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi.
Zao la Karafuu likiwa limehifadhiwa ghalani chini ya Shirika la Bodi ya Taifa ya Biashara Zanzibar
Vijana wakijishughulisha na shughuli za ubabeji mizigo katika ghala la kuhifadhia zao la Karafuu, Wilaya ya Mkoani, Kusini Pemba
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg Shaka Hamdu Shaka akisikiliza maelezo mbalimbali ya Mdhamini wa Shirika la Bodi ya Taifa ya Biashara Zanzibar mara baada ya kutembelea ofisi hizo kujionea hali ya ukusanyaji wa zao la karafuu Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi.
Na Mathias Canal, Pemba

Zanzibar ni maarufu kwa uzalishaji wa karafuu ulimwenguni kwa zaidi ya  karne mbili sasa. Uzalishaji huo ulikuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka na kufikia tani 35,000 mwaka 1830 na kumiliki soko la karafuu duniani kwa asilimia 90.

Iliongoza katika uzalishaji wa zao hilo kuanzia mwaka 1830 hadi 1940 kabla ya nafasi hiyo kuchukuliwa na Indonesia.Tathmini iliyofanywa hivi karibuni ya Sensa ya Miti (Woody Biomass Survey 2013) imeonesha kwamba Zanzibar kwa sasa ina idadi ya mikarafuu 4,131,783, ambapo Unguja pekee ina zaidi ya mikarafuu 277,196 na Pemba zaidi ya mikarafuu 3,854,587.

Tathmini ya mwaka 1997 ilionesha idadi ya mikarafuu 790,400 kwa  Unguja na mikarafuu 5,042,700 kwa upande wa Pemba, ikifanya idadi ya mikarafuu yote kuwa ni 5,833,100

Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Ndg Shaka Hamdu Shaka amelitaja zao la karafuu kuwa ni zao muhimu kwa uchumi wa taifa ambalo huongeza kwa kiasi kikubwa kipato kwa wananchi.

Alisema katika kuimarisha zao la karafuu Zanzibar, pamoja na kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi kuna haja ya kupandwa mikarafuu na minazi maskulini, ili wanafunzi waweze kupata uwelewa zaidi wa kutunza na kulienzi zao hilo, kwa maslahi yao na taifa kwa ujumla.

Shaka alisema hayo wakati alipotembelea na kupanda miti aina ya Mikoko Kwa ajili ya kutunza Mazingira ili kuhuisha uoto wa asili na kuepuka mmomonyoko wa ardhi katika eneo la Mwambe lenye asili ya Watumbatu Wilaya ya Mkoani na Mkoa Ni Kusini PEMBA .

Pia aliwasisitiza wananchi kuhusu kupanda miche ya mikarafuu na minazi na kutotupa taka ovyo ili kuzuia mmomonyoko wa ardhi.

Alisema kuwa serikali inajukumu kubwa la kuhakikisha kuwa inaandaa sheria kali itakayokuwa maalumu kwa kuwachukulia hatua wananchi wanaokata miti ovyo kinyume na utaratibu.

Katika hatua nyingine Shaka alitembelea shirika la Taifa la Biashara Zanzibar kujionea hali ya ununuzi wa zao la karafuu ambapo alimpongeza Mdhamini wa wa shirika hilo Ndg Seif Suleiman Kassim kutokana na kiwango kikubwa cha ukusanyaji wa zao hilo ambapo katika msimu huu hadi kufikia Mwezi Julai 13, 2017 tayari 2203 sawa na Kilogramu 99180.0 zilikuwa zimehifadhiwa kwa ajili ya kupelekwa Unguja.

Alisema uzalishaji wa zao la karafuu, katika Wilaya ya Mkoani unaongoza kwa zaidi ya asilimia 60 ya uzalishaji wa zao hilo kwa zanzibar, na amewataka wananchi kuendelea kutunza mikarafuu, kwani ndio pato la Taifa.

Zanzibar ni visiwa vinavyosifika kwa uzalishaji wa karafuu bora duniani. Katika miaka 30 ya nyuma pia ilisifika kwa uzalishaji karafuu nyingi, wastani wa tani 8,605 zilikuwa zikizalishwa kwa mwaka.

Jamii ya wakati huo walikuwa wakizijali, wakizithamini na wakizipenda sana karafuu ukilinganisha na kizazi cha sasa. Walihakikisha karafuu zao wakiuza vituoni tena zinakuwa safi, zimekauka vizuri na zinapata daraja la kwanza.

MWISHO

Friday, August 18, 2017

HASFU BARBERSHOP YA JIJINI MWANZA YATIMIZA MWAKA MMOJA

 Ile barbershop 'matata' jijini Mwanza inayokwenda kwa jina la Hasfu Barbershop, inayopatikana pande za Misheni Kirumba jijini Mwanza barabara ya Penda hatimaye imetimiza mwaka mmoja sasa.

Wadau wafanyakazi wa barbershop hiyo wamekutana katika hafla fupi iliyofanyika The Cask jijini hapa na kupata chakula, muziki mkaliii toka Jembe DjZ, mvinyo kidogo na ku-share matukio kadhaa muhimu kwa kumbukumbu ikiwa ni pamoja na kuhamasishana kuendeleza moto wa kuwahudumia kwa wateja kwa kiwango cha juu kama ilivyo jadi.
 Wafanyakazi wa Hasfu Barbershop wakikata keki.
 Kata kata......
 Woyoooooo........!!
 Mkurugenzi wa Hasfu Barbershop Mr. Hamis akilishwa keki na mmoja wa mamemba wa naohudumiwa na kitega uchumi chake hicho kinachotimiza mwaka sasa katika utoaji huduma.
 One of the sisters......
 Nawe onja utamu wake.
 Nyakati za mboga saba na kujisevia.
 Chakula kitamu pande za The Cask Mwanza Tanzania.
 The menu mezani.
 Hafla ilifana sana.
 Ikisaotiwa na mazingira mazuri hafla ilinoga sana.
 Ni mwendo wa kugonga glass...
 ChiaaaaaaaaaZ.....!!
 Flowers.
Huduma zikiendelea na utunzaji wa kumbukumbu ulifanyika 'haflani'

HAPPY BIRTHDAY HASFU BARBERSHOP

UCAF YASAINI MKATABA NA AIRTEL KUPELEKA MAWASILIANO VIJIJINI.


 Afisa Mtendaji Mkuu (CEO), wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Mhandisi. Peter Ulanga, (kushoto), na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel, Bi. Beatrice Suingano Malya wakisaini mkataba wa Mradi wa sita wa kupeleka mawasiliano kwa wote. UCSAF imesaini makubaliano na makampuni yote ya simu nchini yenye lengo la kuhakikisha mawasiliano ya simu yanawafikia watanzania wote hadi vijijini na hafla hiyo imefanyika kwenye makao makuu ya Mfuko huo jijini Dar es Salaam, Agosti 18, 2017.
 Afisa Mtendaji Mkuu (CEO), wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Mhandisi. Peter Ulanga, (kushoto), na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel, Bi. Beatrice Suingano Malya, wakibadilishana hati baada ya kusaini mkataba wa sita wa kepeleka mawasiliano ya simu kwa wote. UCSAF imesaini makubaliano na makampuni yote ya simu nchini yenye lengo la kuhakikisha mawasiliano ya simu yanawafikia watanzania wote hadi vijijini na hafla hiyo imefanyika kwenye makao makuu ya Mfuko huo jijini Dar es Salaam, Agosti 18, 2017.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, (kulia), akimpongeza Mwakilsh wa Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel, Bi. Beatrice Singano Malya, mara baada ya Airtel kusaini mkataba wa sita wa Mradi wa kupeleka mawasiliano ya simu kwa wote na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote, (UCAF), jijini Dar es Salaam, Agosti 18, 2017

UCSAF wasaini makubaliano na Airtel kupeleka mawasiliano vijijini

UCSAF imesaini makubaliano na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanznia PLC  pamoja na makampuni mengine ya simu nchini kwa lengo la kuhakikisha mawasiliano ya simu yanawafikia watanzania wote hadi vijijini. Hafla ya makubaliano hayo imefanyika leo kwenye makao makuu ya Mfuko wa mawasilano kwa wote jijini Dar es Salaam,

"Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano Mallya alisema "Airtel tunasaini mkataba huu kwa lengo la kuendelea kutimiza dhamira yetu ya kutoa huduma za mawasiliano kote nchini zentye ubora na ubunifu wa hali ya juu”

Singano alisema kuwa "uwepo wa mawasiliano haya vijijini utasaidia hasa kutimiza malengo mbalimbali ambayo serikali imejiwekea katika kupanua uchumi wa nchi kwa ujumla katika Nyanja mbalimbali zikiwemo elimu, afya, uboreshwaji wa shughuli za kilimo pamoja na huduma za kibenki kwa maeneo ambayo yako pembezoni mwa nchi.Tunaimani maswala ya uslama kwa watanzania waliopo mipakani yataweza kutatuliwa kwa hara na ufanisi mkubwa kupitia mawasiliano.”  

WAZIRI MKUU A CONGO-BRAZZAVILLE AJIUZULU, MATATIZO YA KIUCHUMI YATAJWA.

 
Waziri Mkuu wa Congo-Brazzaville ametangaza kujiuzulu wadhifa wake huo, huku mgogoro wa kiuchumi unaoikabili nchi hiyo ukitajwa kuwa sababu ya kujiuzulu kwake.

Clément Mouamba amejiuzulu baada ya Rais Denis Sassou N'Guesso kusema kuwa, kuna haja ya kupatikana serikali mpya itakayoweza kukabiliana na matatizo ya kiuchumi ya nchi hiyo. Jumanne iliyopita, Rais Sassou N'Guesso alitangaza kuwa, nchi yake inakabiliwa na matatizo makubwa ya kiuchumi na ana wasi wasi wa kuendelea hali hiyo. 

Akizungumzia kuwa mgogoro wa kiuchumi uliibuka kufuatia matatizo ya kifedha na kwamba leo umekuwa suala la kijamii linaloikabili sekta ya kiuchumi, alisema kuwa hata vyanzo vya bajeti na uwekezaji vimeendelea kupungua kila uchao nchini Congo-Brazzaville.
Rais Denis Sassou N'Guesso wa Congo-Brazzaville.
Hata hivyo alipongeza juhudi zilizochukuliwa katika kuzuia kufilisika kwa taifa hilo kutokana na mgogoro huo wa kiuchumi. Hii ni katika hali ambayo Shirika la Fedha la Duniani limetangaza ongezeko la deni la Congo-Brazzaville na kwamba nchi hiyo ilikuwa pia imelificha shirika hilo kuhusiana na baadhi ya madeni yake. 

Mbali na matatizo ya kiuchumi, serikali ya Brazzaville inakabiliwa pia na matatizo ya kisiasa ambayo yanatokana na upinzani mkubwa wa baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa dhidi ya rais huyo, upinzani ambao umepelekea kuzaliwa kwa makundi ya waasi likiwemo kundi maarufu la Ninja ambalo limehusika na mauaji ya askari wengi wa serikali.

AL-SHABAAB YAWAKATA VICHWA WATU WA 3 KAUNTI YA LAMU, KENYA

Kwa akali watu watatu wameuawa kwa kukatwa vichwa na wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabab katika kaunti ya Lamu, pwani ya Kenya.

Kamishna wa kaunti hiyo, Gilbert Kitiyo amethibitisha kutokea mauaji hayo yaliyofanyika katika kijiji cha Maleli, eneobunge la Witu, Lamu Magharibi. Kadhalika magaidi hao wameteketeza kwa moto nyumba kadhaa katika eneo hilo.

Hata hivyo kamishna huyo hajatoa maelezo zaidi kuhusu tukio hilo, ingawaje anasema maafisa usalama wametumwa katika eneo hilo kudhibiti mambo.

Hii si mara ya kwanza kwa genge hilo la Kiwahabi kushambulia kaunti ya Lamu na kutorokea katika msitu wa Boni ulioko katika kaunti hiyo.
 
Wanachama wa al-Shabab katika msitu wa Boni, Lamu 
 Mapema mwezi uliopita wa Julai, wanachama wengine wa al-Shabab waliwauwa kwa kuwakata vichwa watu 9 katika shambulizi lililofanyika katika kijiji kimoja cha kaunti hiyo ya Lamu, siku chache baada ya wanamgambo wa kundi hilo la kigaidi kuua polisi watatu katika kijiji jirani cha Pandanguo na baadaye wakaua wanafunzi wanne na polisi wanne katika kijiji cha Kiunga, kaunti hiyo ya Lamu.
 
Aidha mwezi Mei mwaka huu, maafisa saba wa polisi ya utawala waliuawa baada ya gari lao kukanyaga bomu lililotegwa kando ya barabara katika kaunti ya Lamu, kusini mashariki mwa Kenya.

HAYA HAPA MAJINA YA MAKOCHA WANAOWANIA TUZO YA KOCHA BORA WA MWAKA 2017.

Shirikisho la mpira wa miguu duniani (FIFA) limetangaza majina ya makocha kumi watakaowania tuzo ya kocha bora wa mwaka 2017.

Katika kinyang’anyiro cha kuwania tuzo makocha kutoka ligi kuu England (EPL) wameongoza kwa kutajwa kwa majina manne, Ligi kuu ya Hispania (La Liga) Hispania majina matatu, Ligi kuu Ujerumani (Bundesliga) imetoa majina mawili huku Ufaransa na Italia ikitoa jina moja moja.

1- Massimiliano Allegri-Juventus

2- Carlo Ancelotti-Bayern Munich

3- Antonio Conte-Chelsea

4- Luis Enrique-Hispania

5- Pep Guardiola-Manchester City

6- Leonardo Jardim-AS Monaco

7- Joachim Low-Ujerumani

8- José Mourinho-Manchester United

9- Mauricio Pochettino

10- Diego Simeone-Atletico Madrid

11– Tite-Brazil

12- Zinédine Zidane-Real Madrid

Upigaji kura unaanza Agosti 21 na kufungwa Septemba 7 mwaka huu, kura zitapigwa na Makocha wa timu za Taifa, Manahodha, baadhi ya Wawakilishi kutoka vyombo vya Habari mbalimbali vitakavyoteuliwa pamoja na Mashabiki kwa Mujibu wa FIFA.

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI HUU.


 Rais John Pombe Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jonh Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa viongozi mbali mbali akiwemo Mkuu wa chuo kikuu cha Ardhi.

Taarifa rasmi iliyotolewa na Ikulu jijini Dar es salaam inasema Rais Magufuli amemteua Prof. Evaristo Liwa kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi, kuchukua nafasi ya Prof. Idrissa B. Mshoro ambaye amestaafu.

Wakati huo huo Rais Magufuli amewateua Prof. Abdulkarim Khamis Mruma kuwa Mwenyekiti wa kampuni ya kuhifadhi mafuta (TIPER), ambaye kabla alikuwa ni Mtendaji Mkuu wa wakala wa Jiologia Tanzania, na Prof. Joseph Buchweshaija kuwa Mwenyekiti wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania LTD.

Prof. Buchweshaija alikuwa Naibu Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es salaam (DUCE).