ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 9, 2012

KARIBU USIKU WA LEO NDANI YA GOLD CREST

 Kutoka kushoto ni Hellen, G. Sengo na mwanamuziki Barnaba ambaye kwa usiku wa leo akiwa sambamba na Lady Jay Dee & Machozi Band watafanya perfomance kwa wakazi wa jiji la Mwanza ndani ya Ukumbi wa Nyerere Gold Crest..

 Mwanamuziki Lady Jay Dee akiwa kwenye mazoezi na Machozi Band.

Wahi siti yako mapema kwani mpango mzima ni 20,000/= tu.......!!!

USIKU WA KUZINDUA 101.7 MAGIC FM MWANZA WAFANA

 
 Daimond the Platnum akiwa na wasafi.



Kula Video.

Mtangazaji wa |Magic Fm Salma Msangi akiwa na msanii tok Rock City Jitah Man

Kutoka kushoto ni Producer Man Walter, Salma Msangi na Lulu.

Ze swaggaz one

Ze swaggaz 2.

Three.

Rastafarian hewani na Magic fm

Mr Chegeni.

Miss Mwanza 2011-2012 akiwa na Salma.

Ze Style.com

Katika picha ya pamoja wasanii wa Uchekeshaji kikundi cha Babatan kutoka Mwanza kinachorusha michezo yake kupitia Chanel Ten 

 Interview na Platnum.

 Watu pipoooo na sapoti....

 Ze nyomi mbele ya stage.

MawunoZ''

Friday, June 8, 2012

ALIYEKUWA NA MATUNDU MA3 KWENYE MOYO AFARIKI

Marehemu  Neema (kushoto) enzi za uhai wake alipotembelewa na  Albert G. Sengo aliyefika nyumbani kwa bibi wa mtoto huyu eneo la Butimba mkoani Mwanza kwa ajili ya kuchukuwa taarifa za kuomba msaada.
Mtoto Neema George (16) amefariki dunia leo asubuhi majira ya saa moja huko wilayani Sengerema ambako ndiko wazazi wake wanaishi. 

Mtoto huyu aliyetajwa kuwa na matundu matatu kwenye moyo (kwa mujibu wa vipimo) hivi karibuni akiwa na wazazi wake walijitokeza katika blogu hii na kuomba wasamaria wema kujitokeza kumchangia fedha ili akapate matibabu ya moyo nchini India.

Taarifa za kiuchunguzi zinasema kuwa moyo wa marehemu Neema ulifikia hali ya kushindwa kutambua na kutofautisha kati ya damu safi na damu chafu na kama inavyojulikana kuwa kazi ya moyo ni kusukuma damu safi kwenda sehemu mbalimbali za mwili, pia damu chafu kuifanya ikasafishwe kwenye kibofu, ini na mapafu basi zoezi lote hili lilikuwa limefeli kwenye moyo wa mtoto huyo.

Marehemu Neema anatarajiwa kuzikwa kesho wilayani Sengerema.

Japo imeshindikana kunusuru maisha ya mwanae, baba wa marehemu aitwaye George Lenatus Mugunga amewashukuru wasamaria wema waliojitokeza kumsaidia.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

DIAMOND KESHATUA MWANZA KUZINDUA MAGIC LEO

Video at Mwanza Airport.

Diamond Platnum akiwa na densaz' wake hapa akizungumza na waandishi wa habari Mwanza mara baada ya kutua jijini humo kwa ajili ya kuwa sehemu ya burudani ya uzinduzi wa Radio Magic Fm Mwanza leo usiku ndani ya Villa Park.
"Mara baada ya kuipeperusha vyema bendera ta Tanzania ndani ya Big Brother Africa sasa niko Mwanza inshort nimepania kufanya kitu classic" asema.

Time to show love: Kutoka kushoto ni Producer Man Water aka Man Maji, G. Sengo, Muslim na Olest Kawau.

Crew.

Jikoni at Villa Park Mwanza kumepambwa na ma fish na minyamanyama namuna hii.

Wengine wakisubiri oda zao wengine saa mingi wako sahanini.

MWAKYEMBE: NIMEMNG'OA bosi ATCL KWA UFISADI

Na. Fidelis Butahe wa Gazeti la Mwananchi
SIKU nne baada ya kung’olewa aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Paul Chizi, Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ameamua kuanika tuhuma za ufisadi zinazodaiwa kufanywa na kigogo huyo.Miongoni mwa tuhuma hizo ni kuingia mkataba wa kununua ndege bila kumhusisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG) na kununua sare 15 za watumishi wa ndege kwa dola 50,000 za Marekani. 
Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akizungumza katika mkutano na na wafanyakazi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) uliofanyika Dar es Salaam jana. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi mpya wa ATCL, Milton Lazaro na Mkurugenzi Rasilimali Watu, Judith Ndaba. Picha na Rafael Lubava


Juni 5, Dk Mwakyembe alitengua uteuzi wa Chizi na kumteua rubani wa muda mrefu, Kapteni Lusajo Lazaro kukaimu nafasi hiyo, akisema uteuzi ulikiuka Sheria za Utumishi wa Umma.

Mbali na kutengua uteuzi huo, pia alitangaza kuwasimamisha kazi vigogo wengine wanne wa shirika hilo, hatua ambayo ilianza kuibua malalamiko kutoka kwa baadhi ya wafanyakazi kwamba hatua hiyo ilitokana na majungu na ukabila.

Waliosimamishwa kazi na Dk Mwakyembe ni Kaimu Mkurungenzi wa Uhandisi, Jonh Ringo, Mwanasheria  ,Amini Mziray, Kaimu Mkurugenzi wa Fedha, Justus Bashara na Josephat Kagirwa ambaye alikuwa Kaimu Mkurugenzi wa Biashara.

Jana, waziri huyo wa uchukuzi aliamua kufafanua tuhuma moja hadi nyingine zinazomhusu kigogo huyo na wenzake na kusema, mbali ya tuhuma za Chizi, wakurugenzi wawili wa shirika hilo walikwenda kushonesha sare 15 za wahudumu wa ndege nchini China kwa gharama ya dola 50,000 za Marekani (karibu Sh80 milioni).

Akizungumza na wafanyakazi wa shirika hilo katika Uwanja wa Ndege wa zamani (Terminal One) jijini Dar es Salaam, Dk Mwakyembe alisema kutokana na hali hiyo, ameagiza kujazwa kwa nafasi zilizo wazi na kuwaonya watakaozichukua, kuhakikisha wanachapa kazi ili ATCL ipige hatua na kama wakishindwa watakuwa wamejiondoa wenyewe.

Dk Mwakyembe alitoa miezi mitatu kwa shirika hilo kuanza kujiendesha kwa faida, ikiwa ni pamoja na kupata fedha za kuwalipa wafanyakazi wake.

“Kwa kasi niliyoanza nayo watu kama Chizi ni lazima wakae pembeni, ni mtaalam katika masuala haya, lakini tatizo lake hakuwa muwazi,” alisema Dk Mwakyembe.Chizi hakupatikana jana kuzungumzia tuhuma hizo, wakati wote Mwananchi ilipompigia simu yake ya kiganjani, ilikuwa imezimwa.

Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, alitumia Saa 1:17 kuzungumza na wafanyakazi hao na kufafanua kwamba Serikali imechoka kutoa fedha za kuliendesha shirika hilo, akihoji iweje mashirika mengine ya ndege yaweze kusimama yenyewe, lakini  ATCL iishindwe.

“Tunaipenda ATCL iendelee na tunachukua hatua za kila aina ila tukiona tunashindwa tutaachana nalo ili, fedha zinazotumika hivi sasa zipelekwe kufanyia mambo mengine ya maendeleo,” alisema Dk Mwakyembe.

Tuhuma
Akichambua tuhuma moja hadi nyingine za ukiukwaji wa sheria na taratibu, Dk Mwakyembe alianza kwa kutolea mfano mkataba tata baina ya shirika hilo na Air Bus ambao umeifanya nchi kudaiwa Sh69 bilioni na kusisitiza kuwa, kutokana na hali hiyo Serikali haikuwa tayari kufumbia macho mambo mengine ya ovyo yaendelea katika shirika hilo.

Alisema wafanyakazi wote wa ATCL ambao wananung’unika baada ya kutengua uteuzi wa Chizi wako huru kuondoka katika shirika hilo, huku akionya atawatimua wengi watakaofanya mambo kinyume.

“Nilipoteuliwa kuwa waziri wa uchukuzi siku chache baadaye nilisikia ATCL wanaleta ndege mpya, nilimwita Katibu Mkuu wa wizara anipe ufafanuzi wa jambo hilo, lakini, akaniambia hafahamu lolote,” alisema Dk Mwakyembe.

Aliongeza, “Ndege hiyo ilikodishwa na kutua nchini kwa mara ya kwanza mwezi uliopita kutokana na iliyokuwapo kuanguka mkoani Kigoma. Ndege hiyo aina ya Boeing 737-500 imekodishwa kutoka Kampuni ya Aero Vista ya Dubai.”

Dk Mwakyembe kwa sauti ya ukali alisema, “Niliamua kuwaita wakurugenzi wa ATCL ofisini kwangu saa 3 asubuhi, lakini wakaja saa nne na nusu, pamoja na hayo walinieleza kuwa jambo hilo liko safi na limeshafika kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.”

Alisema baada ya siku moja, alipata taarifa kutoka ofisi ya AG ikieleza kwamba hawana mkataba huo.

“Nikaona jambo zito kidogo, nikaamua kukutana na wale wawekezaji ambao walinionyesha mkataba ule ambao ulipitishwa bila wizara kujua, jambo hilo nililihoji pia…, nawambia ukweli mkataba huu niliuona upande wa pili sio kwa viongozi wa shirika,” alisema Dk Mwakyembe.

Alisema hivi sasa mchakato wa kuchunguza mikataba hiyo umeshaanza na kusisitiza kuwa, hiyo ndio ilikuwa moja ya sababu ya kumng’oa Chizi.


Dk Mwakyembe alisema, “nchi haiwezi kuendelea kwa kukiukwa kwa sheria za ununuzi na ajira. Hata Kapteni Lazaro naye ameponea chupu chupu maana kabla ya kuwang’oa wakurugenzi tulipitia mafaili yao.”

“Msitegemee kubebwa ndugu zangu, nawaomba mchape kazi, mishahara yenu sio mizuri, lakini mkiweza kusimama mtakuwa na uwezo wa kujipangia hata mishahara,” alisema Dk Mwakyembe.

Alisema kwa kutambua mchango wa ATCL, Serikali imepata Sh4.9 bilioni kwa ajili ya matengenezo ya ndege ya shirika hilo na kuwataka kuzitumia kwa ufanisi fedha za shirika hilo.“Hivi sasa inatakiwa kila baada ya miezi mitatu tunakutana na kuzungumza,” alisema Dk Mwakyembe.

Kapteni Lazaro aahidi ushirikiano
Kwa upande wake, Kapteni Lazaro aliahidi kuyazingatia yote yaliyozungumzwa na waziri huyo, huku akiomba shirika hilo kuongezewa muda zaidi kwa kuwa miezi mitatu ni michache ili liweze kujitegemea.


Kupanda/kushuka  ATCL
ATCL ni kampuni iliyoanzishwa baada ya Shirika la Ndege la Tanzania ATC kuingia ubia na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) mnamo mwaka 2002.

ATCl ni moja ya mashirika ya ndege yaliyoonyesha kukua kwa kasi miaka ya 1980 na 1990, lakini lilianza kuyumba kutokana na uendeshaji mbovu na hali ikawa mbaya zaidi baada ya kuingia ubia na SAA.

Serikali iliingia mkataba wa ubia na SAA mwaka 2002 kwa matumaini kwamba itakua na kuwa moja ya mashirika makubwa ya ndege Afrika, lakini hali ikawa kinyume chake.

Kwenye mkataba huo, Serikali ikibakia na hisa 49 huku SAA ikiwa nazo 51, ambazo zilimfanya mbia huyo kuwa na nguvu ya kuamua mambo mengi.

Serikali ilivunja mkataba na SAA Septemba 2006, baada ya kubaini kuwa ATCL inazidi kudidimia kiuchumi huku madeni yakiwa yanaongezeka kadri muda ulivyokuwa unaenda.

Thursday, June 7, 2012

VIGEZO NA MASHARTI TUPA KULE....!!!!

Wakati wabongo wengine nchini wanavaa viatu vya kuanzia laki moja kwenda juu, wengine wanatembea peku mpaka miguu inaota magwambala aka machacha yenye kukuwezesha hata kuficha sarafu.. Kabla ujajiuliza kuhusu hatma za vyandarua na mashuka vipi kama utalala mzungu wa nne na ndugu huyu kisha ikatokea akapitisha kwa bahati mbaya unyayo wake usoni kwako yaaani ile raaaa!! (ya kuparura) uTajisIKiAJE?

NASIBU RAMADHAN V/S FADHILI MAJIA ULINGONI 9/6/2012

FADHILI MAJIA(pichani) ANAMKABILI NASIBU RAMADHAN katika pambano la ubingwa wa WBO la raundi kumi azito wa fly weight, siku ya jumamosi 9/06/2012 katika ukumbi wa friends corner hotel-manzese.

Akilizungumzia pambano hilo katibu mkuu wa TPBO IBRAHIM KAMWE ”BigRight” ambao ndio wasimamizi wa pambano hilo amesema kuwa maandalizi yote yamekwisha kamilika na mabondia wote wapo katika hali nzuri kiafya na morali wa kulisubiria kwa hamu pambano hilo kubwa.

Amsema kuwa katika siku hiyo pia kutakuwepo na mapambano kadhaa ya utangulizi kama vile ABDALLAH MOHD’ Prince Naseem’ atakayemenyana na YOHANA MATHAYO, JUMA FUNDI v/s SHABAN MADILU, VENANCE MPONJI v/s JONAS GODFREY na mapambano mengineyo mengi.

Pia katibu huyo wa TPBO akaongeza kuwa jopo lake limejipanga vyema kwa kuwa na marefa pamoja na majaji wenye uzoefu na ngumi, "Siku zote huwa tunasimamia mchezo kwa haki na kufuata sheria na taratibu za ngumi hakuna upendeleo wa upande wowote hivyo tunawaomba mashabiki waje kwa wingi kutizama ngumi zenye ufundi wa hali ya juu na ushindani mkubwa" alisema

"Nimehakikishiwa na promota Kaike na akanionesha vielelezo vyote vya polisi kuwa ulinzi na usalama utakuwa wa hali ya juu na sehemu ya kuegeshea magari ipo ya usalama" aliongeza katibu huyo.

LADY JAY DEE NA MACHOZI BAND AND BARNABA KUSHUSHA BURUDANI JUMAMOSI HII YA TAREHE 9 JUNI NDANI YA GOLD CREST MWANZA

Sipati Picha.....Jumamosi hii hapa atasimama Lady Jay Dee na Machozi Band na pale atasimama Barnaba na Bendi yake.
Narudia ni jumamosi hii ya tarehe 9 june 2012 kuanzia saa 2 usiku ndani ya Nyerere Hall Gold Crest Hotel jijini Mwanza kwa kiingilio cha shilingi 20,000/= tu!!!
Ladies njooni mkiwa mmependeza tucheze muziki, tupate pix kwa Blogs, Face book na Twitter 
Na wanaume tujumuike kucheza muziki mkali wa Barnaba huku tukipaza sauti za kiitikio cha Magube-gube....tehe teeeee!!
TIKETI ZINAPATIKANA SASA
PIGA SIMU NAMBA 0754074152 
 Machozi Band Live na Usiusemee moyo.

SUPER D AENDEREA KUWAFUA MABONDIA WA KAMBI YA ILALA KWA AJILI YA MPAMBANO WA 10BORA JUNE 15


Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kulia akimwelekeza jinsi ya kutupa makonde bondia Said Mtitu wakati wa mazoezi yanayoendelea katika Kambi ya Ilala Dar es salaam jana ya kujitaharisha na mashindano ya kumi Bora yatakayofanyika june 15 katika ukumbi wa Panandi Panandi Ilala Bungoni.

Wednesday, June 6, 2012

HAPPY BIRTHDAY 2 PHILBERT KABAGO

Siku kama ya leo miaka kadhaa iliyopita amezaliwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, mwenyekiti wa Mwanza Kwanza ambaye ni mtangazaji wa Passion Fm Mwanza 91.0 

Umezaliwa pamoja na Alexander Sergeyevich Pushkin (June 6 1799–February 10 1837) was a Russian Romantic author who is considered to be the greatest Russian poet and the founder of modern Russian literature. Pushkin pioneered the use of vernacular speech in his poems and plays, creating a style of storytelling—mixing drama, romance, and satire—associated with Russian literature ever since and greatly influencing later Russian writers.

Born in Moscow, Pushkin published his first poem at the age of fifteen, and was widely recognized by the literary establishment by the time of his graduation from the Imperial Lyceum in Tsarskoe Selo. Pushkin gradually became committed to social reform and emerged as a spokesman for literary radicals; in the early 1820s he clashed with the government, which sent him into exile in southern Russia. While under the strict surveillance of government censors and unable to travel or publish at will, he wrote his most famous play, the drama Boris Godunov, but could not publish it until years later. His novel in verse, Eugene Onegin, was published serially from 1825 to 1832.

DIAMOND KUZINDUA MAGIC NDANI YA MWANZA

Mpango mzima kutakuwa na usakaji vipaji Mwanza, Burudani kusanukishwa na Diamond Platnum & on the One + Two  Pro 24 Dj.
Video Habari.

Dj Tass wa Magic Fm na Pro 24 Djs ...mapemaaaa ndani ya Rock City
 D Mango ambaye ni mratibu wa Uzinduzi Magic Fm jijini Mwanza (aliyevaa miwani )akizungumzia uzinduzi huo mbele ya waandishi wa habari (walioketi kulia) huku Dj Tass toka Magic Fm na Pro 24 Djs (kushoto) akisikiliza kwa umakiini.

D Mango ambaye ni mratibu wa Uzinduzi huo jijini Mwanza akizungumzia uzinduzi huo mbele ya kamera ya blog hii.
Magic Fm Mwanza kuzinduliwa rasmi Ijumaa hii ya tarehe 8/06/2012 ndani ya Villa Park Mwanza. Shindanola kusaka vipaji kufanyika mshindi kurekodi Studio za Combination Sound chini ya Producer Man Walter aka Man Maji.
 Diamond Platnum kutoa burudani..
Ngoma zitaanza kugengeshwa kuanzia saa 2 usiku kiingilio ni shilingi 10,000/=

WAREMBO WA MISS DAR INTERCOLLEGE 2012 WATAMBULISHWA WAKATI WA UZINDUZI WA BENDI YA SKYLIGHT NDANI YA MAFIAN LOUNGE JIJINI DAR



















Mratibu wa Shindano la Miss Dar Intercollege 2012, Dina Ismail akiwanadi warembo watakaoshiriki shindano la Miss Dar Intercollege 2012 wakati wa uzinduzi wa bendi ya SkyLight ndani ya Mafian Lounge jijini Dar es Salaam wikendi iliyopita.

Warembo wakionesha umahili wao wa kupita jukwani.

Wakipita wa mwendo wa twiga...

Wakifunguliwa shampeni kwa nderemo na vifijo.


Baadhi ya Warembo wa Miss Dar InterCollege wakiwamejipanga mbele ya wadau na wadhamini katika uzinduzi wa bendi ya SkyLight iliyofanyika  Mafian Lounge iliyopo Masaki, bendi hiyo inamilikiwa na mmoja wa wadhamini wao Ndege Insurance.

ZE NEWz
Mratibu wa Shindano hilo Dina Ismail alisema kwamba warembo watakaoshiriki shindano hilo wanaendeleza na mazoezi kwenye hoteli ya Lamada jijini Dar es Salaam chini ya ukufunzi wa Marylidya Boniface, huku kwa upande wa shoo wakinolewa na Bob Rich.

Alisema mpaka sasa warembo 15 kutoka vyuo vya Biashara (CBE), Uandishi wa Habari (DSJ) na Time, Ustawi wa Jamii na kile cha Usimamizi wa Fedha (IFM) wamesharipoti kambini.Dina aliwataja warembo hao kuwa ni pamoja na Hilda Edward, Nancy Maganga, Saada Seleman, Neema Nashon, Rose Muchunguzi, Fina Revocatus, Jane Augustino,Theresia Issaya na Natasha Deo.Taji la kitongoji hicho linashikiliwa na Rose Msuya kutoka IFM.

Kwa upande mwingine, mratibu huyo ameyaomba makampuni mbalimbali kujitokeza kudhamini shindano hilo ambalo linatarajiwa kuwa la aina yake na hasa ikizingatiwa kuwa washiriki wake wana vigezo vya hali ya juu.

“Tunaomba makampuni mbalimbali yajitokeze kudhamini shindano letu…mpaka sasa wadhamini tulionao ni pamoja na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Redd’s, Lamada Hotel, Ndege Insurance, Dodoma Wine na Clouds Fm.

Tuesday, June 5, 2012

MWANZA YAONGOZA KWA USAFI MWAKA WA 7

Tuzo zilizotangulia ofisi za jiji la Mwanza
Jiji la Mwanza kwa mwaka wa saba mfululizo limefanikiwa kuibukamshindi wa kwanza kwa usafi wa mazingira na zfya katika majiji nchini.

Awali Taarifa za matokeo zilitolewa na Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii kuweendea makatibu Tawala wa mkoa iliyoshiriki ambapo hatimaye leo kwenye kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira mjini Kilimanjaro, Mwanza imekabidhiwa rasmi Kombe lake la ushindi wa kwanza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete ambaye alikuwa mgeni rasmi.
Wilson Kabwe.
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Bw. Wilson Kabwe ameeleza kufurahishwa kwake na rekodi hiyo ya  ushindi mfululizo akiwataka wafanyakazi wa kitengo cha usafi pamoja wanasiasa, wauguzi wa afya na wananchi kwa ujumla kutobweteka na ushindi huo bali kuiunga mkono kwa dhati kampeni hiyo ili kuhakikisha jiji linakuwa safi muda wote.

Majiji ya Tanzania yaliyoshindanishwa kwenye mchakato huo ni pamoja na jiji la Dar es salaam, Tanga, Arusha na Mbeya
Kulia Naibu Waziri Ofisi ya Makamau wa Rais mh. Charles Kitwanga akipata maelezo toka kwa Bi Arafa Maggid mhandisi mazingira Bonde la pangangi kuhusu vifaa vya kupimia ubora wa maji, alipotembelea banda la hilo leo katika maonyesho ya wiki ya mazingira mkoani Kilimanjaro.

Kauli mbiu ya siku ya mazingira 2012 ni Hifadhi Mazingira Jikite Kwenye Uwekezaji Endelevu.

KAMERA YETU

 Duka la dalali wa viwanja, mashamba na nyumba KISESA.

 Kiwanda na duka la majiko na makarai IGOMA .

Chanzo cha maji kwa watu wa eneo mojawapo katika kijiji cha KISESA wilayani Magu.

Mkoko wa juu ya mawe.

 Mizani ya mabondo aka vyuma chakavu na plastiki.

 Mchana kweupeee vijana nguvu kazi kwa taifa inatumika kwenye pool table katika eneo la KISESA.

Tizama mifereji kisha tulalamike kuhusu mafuriko...
Mitaro ya maji machafu imegeuka kuwa mashimo ya taka.
Moja ya hoja binafsi iliyo wasilishwa majuzi na kuungwa mkono na madiwani wote kwenye Baraza lao lililofanyika hivi majuzi ni kuwa kila kata ianze kuwatumia vijana wasio na ajira kuzibua mitaro kwa vifaa maalum na kulipwa na halmashauri hiyo kwa lengo la kukabiliana na changamoto ya ajira nchini, hoja iliyowasilishwa na diwani wa kata ya Nyamagana Bhiku Kotecha, kiukweli hoja hiyo itakuwa na manufaa kwa jamii hata kutuepusha na mafuriko.