ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, March 30, 2018

IJUMAA KUU NJEMA KUTOKA JEMBE FM.

Ni yeye yule aliyetuonyesha njia, Amekwenda kitambo nyumbani kwa baba kutuandalia makao lakini bado anaishi mioyoni mwetu, Jina lake liking'ara daima dumu. 

Twakutakia IJUMAA KUU njema!...!!

HATIAMAYE BOMBARDIER YA TANZANIA ILIYOZUILIWA NCHINI CANADA YAACHILIWA.

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewathibitishia wananchi kuwa ndege yake aina Bombardier Q400 iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada imearuhusiwa kuondoka nchini humo na muda wowote kutoka sasa itawasili hapa Tanzania.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa leo Machi 30, 2018 kupitia ukurasa wake wa Twitter huku akiweka picha zilizokuwa zikionesha ndege hiyo wakati wa matengenezo ya mwisho kabla ya kuruhusiwa kuondoka.

“Ndege yetu aina ya Bombardier Q400, iliyokuwa imezuiliwa nchini Canada ilikwishaondoka Canada kuja Tanzania. Pia ndege kubwa nyingine tatu (2 Bombardier CS300 kutoka Canada na  1 Boeing 787-8 Dreamliner) kutoka Marekani, zitawasili baadaye mwaka huu. Nawatakia Ijumaa Kuu njema”, amesema Msigwa.

Aidha, Msigwa amesema hawajajua tarehe maalumu ya kutua ndege hiyo katika ardhi ya Tanzania kutokana na baadhi ya vitu kuwa vinamaliziwa.

Thursday, March 29, 2018

POLISI WAIMARISHA ULINZI MAHAKAMANI, KESI YA VIONGOZI WA CHADEMA,


Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limeimarisha ulinzi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili kudhibiti umati wa watu wanaodhaniwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao wamekusanyika nje ya mahakama, wasiingie kusikiliza kesi inayowakabili mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe na viongozi wenzake watano.

Mbowe na wenzake wameshafikishwa mahakamani hapo wakitokea mahabusu ya Segerea wakikabiliwa na mashtaka manane yakiwemo kufanya maandamano yaliyosababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline, Februari 16, mwaka huu, uasi na kuhamasisha chuki.
Lowassa.

Baadhi ya wabunge wa Chadema, wafuasi wa chama hicho na wananchi wengine waliofika mahakamani kufuatilia kesi hiyo ni  Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Prof. Abdallah Safari, Mbunge Joseph Haule ‘Prof. Jay.

RC MASENZA AWAPONGEZA RDO KWA KUTATUA TATIZO LA MAJI KWENYE BAADHI YA VIJIJI VYA WILAYA YA MUFINDI NA KILOLO

 Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Nandala alipokuwa ameenda kuzindua mradi wa maji ambao utasaidia kupunguza changamoto ya maji na kuchochea maendeleo kwa wananchi ambao watakuwa wananufaika na mradi huo ulifadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania ambao makao makuu yao yapo Mdabulo Mufindi.

 Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akimtusha ndoo ya maji mmoja ya wananchi walihudhulia uzinduzi wa mradi maji ulifadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania

 Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akiwa na mkurugenzi mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania Fidelis Filipatali wakibadilisha mawazo juu ya mradi huo ambao umegharibukiasi cha shilingi milioni tisini na tano,laki tano na elfu tatu mia moja ( 95,503,100)

 Hapa ndio tank kubwa la mradi wa maji unaofadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania na
umegharibukiasi cha shilingi milioni tisini na tano,laki tano na elfu tatu mia moja ( 95,503,100)

Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Nandala alipokuwa ameenda kuzindua mradi wa maji ambao utasaidia kupunguza changamoto ya maji na kuchochea maendeleo kwa wananchi ambao watakuwa wananufaika na mradi huo ulifadhiliwa na shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania ambao makao makuu yao yapo Mdabulo Mufindi.

 Na Fredy Mgunda,Iringa.
 
MKUU wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amelipongeza shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania kwa kufanikisha kupatikana kwa maji katika baadhi ya vijiji vya wilaya ya Kilolo na Mufindi ambayo itakuwa njia moja wapo ya kuchochea maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Nandala’ Masenza alisema kuwa amefurahishwa na mfumo ambao unatumiwa na shirika hilo kwa kutoa huduma ya maji kwa kushirikiana na wananchi wa maeneo husika.

“Mradi wowote ule ukiwa na ushirikiano mkubwa na wananchi mara nyingi wananchi wanautunza mradi huo kwa kuudhamini na kuulinda,hivyo nawapongeza RDO kwa kufanya maamuzi sahihi ya kubuni mradi huo pamoja na wananchi” alisema  Masenza

Masenza alisema kuwa mradi huo wa maji utatoa huduma kwa wananchi wengi na taasisi binafsi nyingi hivyo wananchi wanatakiwa kuutunza na kuudhamini ili udumu kwa muda mrefu na kuondoa tatizo la maji ambalo limekuwa kero ya muda mrefu.

Nimesikia kwenye risala yenu kuwa mradi huu utahudumia kata zifuatazo Ifwagi,Mdabulo,Ihanu,Luhunga,Mtitu na Kising’a na vijiji vitakavyopata huduma hiyo ni Igonongo,Ludilo,Kidete,Ikanga,Nandala,Ibwanzi,Isipii,Mkonge,Lulanzi,Luhindo,Barabara mbili na Isele hivyo ukiangala utagundua kuwa mradi huu ni mkubwa na upaswi kupuuzwa kwa maendeleo kwa wananchi wa maeneo ambayo mradi huo umepita.

“Jamani wananchi ambao mmepata bahati ya kupitiwa na mradio huu mkubwa wa maji mnapaswa kuulinda na kuudhamini kwa kuwa ni mmoja ya mradi mkubwa ambao unapunguza adha ya upatikanaji wa maji ambayo hapo awali ilikuwa kero kubwa” alisema Masenza

Kwa upande mkurugenzi mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Tanzania Fidelis Filipatali alisema kuwa mradi huo umegharibukiasi cha shilingi milioni tisini na tano,laki tano na elfu tatu mia moja ( 95,503,100) ambao ndani yake kuna pesa zilizochangwa na wananchi kwa ajili ya kusaidia kupata huduma ya maji.

“Sisi kama RDO ambao ndio wafadhili namba moja wa mradio huu wa maji tumechangia kiasi cha shilingi milioni themenini na sita,laki nane ishirini na moja elfu (86,821,000) na wananchi walichanga kiasi cha shilingi milioni nane,laki sita themenini na mbili na mia moja (8,682,100)” alisema Filipatali

Filipatali  alisema kuwa mradi huo wa maji  utazaliza ujazo wa lita 776  kwa vijiji vyote ambazo vinatumia huduma hiyo ya maji na pia wananchi watakao pata huduma hiyo ni 10,874 kwa vijiji vyote vilivyopitiwa na mradi huo na jumla ya taasisi 18 nazo zitanufaika na huduma hiyo.

“Mkuu wa mkoa sasa ukiangalia kwa ujumla ndio utagundua kuwa ni mradi ambao utakuwa unakomba wananchi wengi waliokuwa wanapata tabu juu ya kupata maji hivyo naomba pia nisisitize wananchi kuutunza na kuchangia kwa malipo kidogo kwa ajili ya ukarabati wa mashine na mitambo mingie inayosukuma maji hayo ili isihalibike” alisema Filipatali

Filipatali alisema kuwa mradi huo unakabiliwa na changamoto zifuatazo baadhi ya watumiaji maji kutochangia, viongozi kutotimiza majukumu yao kama kutohudhuria mikutano ya mapato na matumizi,watumiaji maji kutotilia mkazo elimu wanayopewa na wataalamu wa maji,siasa kuingia mfumo mzima wa mradi huu na baadhi ya serikali za vijiji kuchukulia mapato ya miradi ya maji kama sehemu ya mapato ya serikali  kitu ambacho sio kweli mfano kjiji cha Lidilo

“Hizi changamoto zimekuwa kero sana kwenye miradi ambayo imekuwa inatekelezwa kwenye maeneo husika hivyo niwaombe viongozi wa kiasa wawe wa kwanza kutoa elimu juu ya miradi ambayo inafaida na kutatua changamoto za wananchi kwenye maeneo yao” Filipatali

Wednesday, March 28, 2018

BancABC YATEKELEZA SERA YA FEDHA YA BoT

 Mkurugenzi mtendaji wa BancABC Dana Botha akizungumza na waandishi wa habali katika ofisi zao Leo Jijini Dar es Salaam,kuhusu punguzo la tozo  ya mikopo mbali mbali kwa wateja wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa BancABC Dana Botha kulia,kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Hazina BancABC Barton Mwasamengo pamoja na Mkurugenzi wa kitengo cha wateja binafsi na wafanyabiashara wa BancABC Joyce  Malai katikati wakishika bango linaloonyesha punguzo la tozo za Mikopo.


BENKI ya BancABC  imesema imetekeleza Sera ya fedha  ya Benki  Kuu ya Tanzania(BoT) kwa kutangaza kutoa punguzo kwa wateja  wake wapya kuwezesha  kukopa kuanzia Aprili 1 mwaka huu.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji was BancABC Dana Botha amesema benki hiyo ni  sehemu ya Atlasi Mara iliyosajiliwa  katika soko la hisa la Londan ikiwa na lengo la kujitanua ili kuwa kinara katika masuala ya kifedha katika ukanda wa Sahara kwa kutumia uzoefu wake na uwezo wa kukuza mitaji.

Hivyo Botha amesema watapungunza riba kwa wateja wao katika mikopo ya masharti ambayo itakuwa ni huduma ya Over draft pamoja na  ya nyumba na kufafanua mwaka jana benki nyingi zilipita katika wakati mgumu wa ukwasi.

"Hivyo kufanya uwezo wa kukopesha kuwa mdogo.Kwa miezi kadhaa sasa,Serikali kupitia BoT imekuwa ikisisitiza kuhusu punguzo la riba hiyo kwa kupunguza masharti kama vile kiwango cha  chini cha fedha kwa mabenki,"amesema Botha.

Ameongezea viwango vya punguzo,hati fungani za hazina na kukopesha 
mabenki kwa viwango vya chini na hiyo imewezesha ukopeshaji kwa watu binafsi na kampuni mbalimbali ili kuimarisha biashara zao na hatimaye kuboresha uchumi. "Na tunajivunia kuwa kati ya benki za kwanza kutangaza wazi kuhusu punguzo hili."

Aidha Mkuu wa kitengo cha Hazina BancABC Barton Mwasamengo amesema kuwa benki hiyo inahudumia wateja zaidi ya 60,000 ambao wanamiliki bidhaa tofauti za kibenki

Mwasomengo amesema fursa hiyo itawawezesha kuwashawishi wateja kupata mikopo ya Nyumba ambayo ilikuwa changamoto kubwa hasa kwa wananchi wa Daraja la kati na chini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kitengo cha wateja binafsi na wafanyabiashara wa BancABC Joyce Mlai amemalizia kwa kusema katika kujenga nyumba wanaungana na Serikali kuwapa fursa ya kuwapatia mikopo ya Nyumba  wafanyakazi wa aina zote sekta binafsi,serikalini pmoja na wafanya biashara.

HIZI NDIZO SALAMU ZA PASAKA TOKA IGP SIRRO

Inspekta Jenerali wa Polisi, Simon Sirro. 


Milioni 260 za Tatumzuka kunyakuliwa katika ‘Jackpot’ ya Pasaka

 Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano  Sebastian Maganga akizungumza na Waandishi wa Habari mapema leo jijini Dar akielezea kuhusu Tatumzuka kuungana na wateja wake kwa kutangaza fursa ya kushinda kitita cha shilingi 260 ambacho lazima kitolewe jumapili ya Pasaka.

Tatu Mzuka, mchezo wa namba unaongoza hapa nchini unawapa fursa Watanzania kushinda kitita cha Shilingi milioni 260 katika droo itakayofanyika jumapili ya pasaka na kuonyeshwa moja kwa moja saa 3:30 usiku

 Taifa linapojiandaa na sherehe za Pasaka, Tatumzuka imeungana na wateja wake kwa kutangaza fursa ya kushinda kitita cha shilingi 260 ambacho lazima kitolewe jumapili ya Pasaka.

Kitita hicho kinono cha milioni 260 ambacho hakijawahi kutolewa kwa mtu katika historia ya nchi hii sasa kitatolewa kwa mshindi mmoja atakayebahatika kwenye ‘PasakaMzukaJackpot’ siku ya tarehe 31/3/2018.

Bwana Sebastian Maganga, Mkuu wa kitengo cha mawasiliano wa Tatumzuka, ameuelezea umma namna ilivyo rahisi kuingia katika droo. “Wiki hii ukiwa na shilingi 500 tu, kwa kutumia; Mpesa, Tigo pesa au Airtel Money, ingiza namba ya kampuni ambayo ni 555111, kisha weka namba zako tatu za bahati na hapo utakuwa umeingia rasmi kwenye droo ya milioni 260 za PasakaMzukaJackpot” alielezea Maganga

Hicho sio kitu pekee ambacho Tatumzuka inatoa msimu huu wa sikukuu, pia una nafasi ya kushinda milioni 10 kila siku na milioni 6 kila saa.“Ukinunua tiketi moja ya shilingi 500, Tatumzuka inakupa nafasi ya kuingia katika droo 3 tofauti na hivyo kukuongezea nafasi za kushinda tofauti na michezo mingine ya namba” Maganga alisisitiza

Tatu Mzuka pia imetumia fursa hiyo kuwatambulisha washindi wa wiki iliyopita ambao walitokana na droo ya 34 ya Tatumzuka jackpot.Bi Hanifa kutoka Magomeni, Dar es Salaam alijishindia milioni 5. Bwana Juma Mkombozi kutoka Magomeni, Kagera alijishindia milioni 7. Bwana Prosper Munuo kutoka Bunju A alijinyakulia milioni 5 na Magreth Nkwabi wa Kahama, Shinyanga alipata milioni 3.

Washindi wote wakiwa wenye furaha baada ya ushindi walisisitiza kwamba wataendelea kucheza kujaribu bahati zao kwenye dau la kihistoria la milioni 260 jumapili hii.‘Droo hii ya kihistoria itaonyeshwa moja kwa moja kupitia ITV, Clouds TV na TV1 jumapili hii saa 3:30 usiku’ Bwana Maganga aliufafanulia umma.
 Mmoja ya washindi akikabidhiwa mfano wa Hundi yake yenye thamani ya shilingi milioni tano na la  Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Sebastian Maganga.
 Washindi wa Tatu Mzuka Jackpot wa wiki iliyopita kwa pamoja wakifurahi

JICHO LA SERIKALI KATIKA USIMAMIZI WA FEDHA NCHINI TANZANIA





FMOs Wakumbushwa Utendaji wao
Na. Atley Kuni, OR TAMISEMI
Maafisa Usimamizi wa Fedha (Finance Management Officers - FMOs) kutoka Sekretarieti za Mikoa yote ya Tanzania Bara wamesisitizwa kuwa jicho la usimamizi wa fedha za Halmashauri na kutoa taarifa kwa Katibu Tawala (RAS) pamoja na ngazi ya Wizara ili kuwa na taarifa sahihi za kifedha kuanzia ngazi ya Halmashauri, Mkoa na Wizara.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Idara ya Serikali za Mitaa Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Charles E. Mhina wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya Mfumo wa Kielektroniki wa Ufuatiliaji wa Fedha zinazopelekwa Mamlaka za Serikali za Mitaa (Fiscal Transfer Tracking Monitoring(FTTM) – Web Portal)  yanayowakutanisha FMOs kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara kuanzia tarehe 27-28 Machi, 2018 kwenye ukumbi wa Maabara ya Kompyuta uliopo katika jengo la Sokoine OR TAMISEMI, mjini Dodoma.

Dkt. Mhina amewahimiza Wataalam hao kuwa eneo la utoaji wa taarifa ni muhimu sana ili kuwa na taarifa sahihi zitakazosaidia kufanya maamuzi sahihi na kwa wakati.

“Tulichobaini kama Wizara kuna umuhimu wa kuimarisha daraja la mawasiliano kati ya FMOs na Halmashauri. FMOs mmekuwa mkitoa taarifa kwa RAS na Wizara, huku mkisahau kwamba nyinyi kama wataalam mnatakiwa kuzisimamia na kuzijengea uwezo Halmashauri pia.” amesema Dkt. Mhina na kuongeza kuwa changamoto zilizopo zianishwe na kutumika kama chachu yakuleta mabadiliko.

“Changamoto ya matumizi sahihi ya mfumo wa FTTM – Web Portal kutokana na ukosefu wa mafunzo imekuwepo toka 2015. Sasa tumieni fursa hii ya mafunzo mtakayoyapata kikamilifu ilimtakapo ondoka hapa mlete mabadiliko chanya katika usimamizi wa fedha. Wataalam wetu wa TEHAMA na FEDHA kutoka OR TAMISEMI wapo tayari na wamejipanga kuwaelekeza kikamilifu.” alisema Dkt. Mhina.

Pamoja Wataalam hao kusisitizwa juu ya mfumo wa FTTM-Web Portal, Mkurugenzi wa Idara ya TEHAMA OR TAMISEMI, Ndg. Erick Kitali  hakusita pia kuwakumbusha Wataalam hao kuwa ifikapo Julai Mosi, 2018 Mamlaka zote za Serikali za Mitaa zitumie  toleo jipya la 10 la Mfumo wa Malipo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa  (Epicor 10) ili kwenda sambamba na mahitaji ya sasa.

Ndg. Kitali amewaambia wataalam hao kuwa OR TAMISEMI katika utendaji wake wa kazi hutegemea sana ushauri wa Wataalam kutoka ngazi za msingi ambapo ndipo walipo wananchi. Hivyo, aliwataka Wataalam hao kuzingatia mafunzo yatakayotolewa ili kutekeleza majukumu yao kwa weledi.

Maafisa Usimamizi wa Fedha (Finance Management Officers - FMOs) kutoka Sekretarieti za Mikoa hutumika kama wataalam washauri katika ngazi ya Mkoa ili kuzisaidia Halamashauri juu ya taarifa mbali mbali za kifedha sambamba na kumshauri katika katibu Tawala pamoja na Wizara juu ya mwenendo wa kifedha katika mkoa husika.

WATAALAM WA MADINI YA DHAHABU NCHI ZA UKANDA WA MAZIWA MAKUU (ICGLR) WAKUTANA ARUSHA

 Baadhi ya Waratibu wa Mkutano wa Wataalam wa Madini ya Dhahabu kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ICGLR wakifuatilia majadiliano kwenye mkutano huo Jijini Arusha. Kulia ni Mkurugenzi wa Demokrasia na Utawala Bora- ICGLR, Balozi Ambeyi Ligabo akifuatiwa na Mwenyekiti wa Mkutano, Service Julie kutoka Congo.
 Wataalam wa Madini ya Dhahabu kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ICGLR wakiendelea na majadiliano.
 Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa Wataalam wa Madini ya Dhahabu kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ICGLR wakifuatilia majadiliano
 Mwenyekiti wa mkutano, Service Julie kutoka Congo (wa pili kulia) akizungumza wakati wa Mkutano wa Wataalam wa Madini ya Dhahabu kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ICGLR.
 Washiriki kutoka Tanzania wakifuatilia majadiliano kwenye mkutano huo. Kutoka kulia ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kaskazini, Adam Juma akimwakilisha Kamishna wa Madini, Prof. Shukran Manya na Mhandisi Fadhili Kitivai (kutoka Wizara ya Madini).
Wataalam wa Madini ya Dhahabu kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ICGLR wakiendelea na majadiliano Jijini Arusha.

Wataalam wa Madini ya Dhahabu kutoka Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ICGLR wamekutana Jijini Arusha ili kujadili masuala mbalimbali yanayohusu madini hayo kwa maslahi mapana ya nchi hizo.

Mkutano huo wa siku mbili ulifunguliwa jana Machi 27, 2018 na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ambapo alisisitiza kuwa Nchi Wanachama wa ICGLR wanao wajibu wa pamoja kuhakikisha malengo waliyojiwekea yanafikiwa kwa manufaa ya wanachama wote.

Gambo alizungumzia changamoto mbalimbali zinazozikabili Nchi Wanachama ambazo ni uvunaji haramu wa madini, utoroshwaji wa madini, uharibifu wa mazingira, ukosefu wa teknolojia na baadhi ya Nchi kuwa na changamoto za Kiusalama.

Hata hivyo alisema changamoto hizo zisiwe sababu ya kurudi nyuma badala yake juhudi za pamoja, mshikamano wa dhati unahitajika ili kukabiliana na changamoto hizo na kuhakikisha ufumbuzi unapatikana kwa maslahi mapana ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu.

Nchi Wanachama ni Tanzania, Angola, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Congo (Kinshasa), Congo (Brazzaville), Kenya, Rwanda, Sudan Kusini, Sudan Kaskazini, Uganda na Zambia.

Tanzania imekuwa Mwanachama rasmi wa ICGLR Mwaka 2008 na tangu wakati huo imeendelea kutekeleza malengo ya mpango wa ICGLR ili kufanikisha udhibiti wa uvunaji haramu wa madini na kuhakikisha manufaa ya pamoja ya rasilimali husika yanapatikana.  

Tuesday, March 27, 2018

VIDEO:- STARS YAIBAMIZA CONGO 2-0,


Nahodha wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta alivyowainua vitini mashabiki.


Shiza Kichuya akiiandikia Stars bao la pili kwa mkwaju mkali wa chini chini. Litazame

MICHUANO YA COPA COCA-COLA UMISSETA 2018 YAZINDULIWA MKOANI DODOMA

Waziri Jafo akigawa zawadi ya mipira kwa baadhi ya shule za sekondari zitakazoshiriki. Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo akihutubia wakati wa uzinduzi huo.
Meneja wa chapa ya Coca-Cola, Sialouise Shayo, akiongea wakati wa uzinduzi huo. Waziri Jafo akikagua moja ya timu na kugawa vifaa kwa baadhi ya shule za sekondari
Waziri Jafo katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa UMISSETA baada ya uzinduzi.

Wakazi wa Dodoma walijitokeza kushuhudia uzinduzi.

Mashindano ya shule za sekondari ya UMISSETA ngazi ya mkoa yamezinduliwa mkoani Dodoma, na mgeni rasmi katika uzinduzi huo alikuwa ni Waziri wa TAMISEMI,Selemani Jafo.Uzinduzi huo pia ulihudhuriwa na wanafunzi wa shule za sekondari,walimu, viongozi mbalimbali wa mkoa na michezo.

Mbali na uzinduzi,Waziri alikabidhi vifaa vya michezo kwa timu za sekondari zilizokuwepo kwenye uzinduzi huo.Vifaa hivyo vya michezo vimetolewa na kampuni ya Coca-Cola ambayo ni mdhamini mkuu wa mashindano haya,ambapo mwaka huu imepanga kutoa vifaa vya michezo kwa shule 4,000 za sekondari zilizopo sehemu mbalimbali nchini.

Waziri Jafo, alisema kampuni ya Coca-Cola kwa kudhamini mashindano hayo kutafanikisha jitihada za kuendelea kuibua vipaji vya wachezaji chipukizi wa michezo ya soka ,mpira wa kikapu na pia kupitia mashindano haya kutaibuliwa vipaji vya wanariadha watakaotamba katika kipindi cha miaka ijayo.

“Nafahamu kuwa udhamini wa Coca-Cola wa mashindano haya unamalizika mwishoni mwa mwaka huu,lakini natoa ombi maalum iangalie uwezekano wa kuendelea kuongeza kipindi cha kutoa udhamini .Mashindano haya ya UMISSETA ni tanuru ya kuibua vipaji na rekondi ipo ya wachezaji wazuri wa soka waliofanya vizuri na wanaoendelea kufanya vizuri katika michezo mbalimbali,vipaji vyao viliibuliwa katika mashindano haya wengi pia wamechezea baadhi ya klabu kubwa za soka za Yanga na Simba”alisema.

Waziri Jafo,alitoa wito kwa makampuni mengine kujitokeza kudhamini mashindano ya michezo kuanzia ngazi za chini,na kusisitiza kuwa sekta ya michezo inazidi kukua ambapo hivi sasa lengo lake sio burudani bali ni biashara kubwa na ushahidi wa suala hili upo wazi.

Jafo pia alishauri kamati ya maandalizi ya mashindano haya ya UMISSETA ,kwa miaka ijayo ihakikishe uzinduzi wake ngazi ya kitaifa unafanyika mkoani odoma badala ya mkoani Mwanza ili yaendane na mkakati wa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli ya kuhamishia shughuli za serikali katika mji wa makao makuu ya nchi.

Kwa upande wake Meneja wa chapa ya Coca-Cola, Sialouise Shayo,alisema kampuni ya Coca-Cola inajivunia kuwa mdhamini wa mashindano haya kwa kipindi cha miaka 3 mfulilizo na inaamini vipaji vingi vimeibuliwa na vitaendelea kuibuliwa .”Udhamini wetu katika mashindano haya tumejikita katika kutoa vifaa vya michezo kwa wachezaji wanaoshiriki kuanzia ngazi ya mkoa hadi ngazi ya taifa,kutoa mafunzo kwa makocha wanaofundisha timu na zawadi kwa timu zinazofanikiwa kufanya vizuri”,alisisitiza

Shayo alisema mbali na uzinduzi wa UMISSETA ngazi ya mkoa uliofanyika mkoani Dodoma utafanyika katika mikoa ya Kagera,Tanga,Mtwara,Singida na Zanzibar ambapo uzinduzi kwa ngazi ya taifa utafanyika mkoani Mwanza ambapo pia mashindano haya yatafanyika.

MTOTO WA RAIS WA ZAMANI WA ANGOLA AZUIWA KUONDOKA NCHINI KWA TUHUMA ZA UFISADI.

Mtoto wa rais wa zamani wa Angola azuiwa kuondoka nchini kwa tuhuma za ufisadi
Mtoto wa kiume wa rais wa zamani wa Angola, Jose Eduardo dos Santos amezuiwa kuondoka nchini kutokana na tuhuma za ufisadi zinazomuandama.
José Filomeno dos Santos anatuhumiwa kuhamisha kiasi cha dola milioni 500 za Marekani kutoka hazina ya taifa aliyokuwa akiiongoza, hadi kwenye akaunti binafsi.
Duru za habari zinasema, mtoto huyo wa rais wa zamani wa Angola alihamisha fedha hizo kutoka Benki Kuu ya Taifa hadi kwenye akaunti ya Benki ya Credit Suisse iliyoko nchini Uingereza.
Luís Benza Zanga, Mwanasheria Mkuu wa Angola jana Jumatatu aliwaambia waandishi wa habari mjini Luanda kuwa, chama tawala cha MPLA kilihusika pakubwa katika ubadhirifu huo mkubwa wa fedha za umma.
Amesema Valter Filipe, aliyekuwa Rais wa Benki Kuu ya nchi hiyo pia anachunguzwa katika kashfa hiyo ya ufisadi wa kiuchumi.



Angola, moja ya wazalishaji wakubwa wa mafuta inakabiliwa na tuhuma za ufisadi

Rais wa sasa wa Angola, João Lourenço  Januari mwaka huu alimfuta kazi mtoto huyo wa kiume wa mtangulizi wake, kuwa mkuu wa hazina hiyo ya kistratajia ya serikali yenye zaidi ya dola bilioni 5.
Nafasi hiyo ilijazwa na Carlos Alberto Lopes, Waziri wa Fedha wa zamani wa nchi hiyo.
CHANZO/Parstoday swahili

KIJUE KIWANDA CHA MAZIWA KINACHOWANUFAISHA KIUCHUMI WAFUGAJI 2000



 Baadhi ya Wafanyakazi na Viongozi wa Kiwanda cha Maziwa cha The Grande Demam wakihakiki ufungashaji wa bidhaa za maziwa zinazozalishwa kiwandani hapo
Baadhi ya Viongozi wa kiwanda cha maziwa cha  The Grande Demam wakinywa maziwa yanayozalishwa na kiwanda hicho
 Baadhi ya Viongozi wa kiwanda cha maziwa cha  The Grande Demam wakinywa maziwa yanayozalishwa na kiwanda hicho
Uongozi wa kiwanda cha maziwa cha  The Grande Demam

Na Woinde Shizza ,Arusha.
Wilaya ya Meru ni moja kati ya Wilaya maarufu zinazoongoza kwa uzalishaji mkubwa wa maziwa mkoani Arusha,maziwa ambayo huuzwa maeneo ya miji ikiwemo viunga vya Jiji la Arusha na nje ya jiji hilo.
Licha ya uzalishaji huo wa maziwa bado wafugaji hao wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa masoko ya uhakika ya kununua maziwa hayo hivyo kupelekea maziwa wanayoyazalisha kuharibika baada ya kukaa muda bila kununuliwa.
Kufuatia Changamoto  hiyo  Moja kati Daktari wa Mifugo Dokta Deo aliona changamoto hiyo kama fursa ya uwekezaji kwani malighafi ya maziwa inapatikana kwa wingi ,kwa kuwa wafugaji walikua wakiyamwaga maziwa yao yaliyokua yakiharibika kwa kukosa soko la uhakika  na hawakua na namna yoyote ya kuongeza thamani maziwa hayo ili yaweze kukaa kwa muda bila kuharibika.
Dokta Deo aliacha kazi ya kuajiriwa mwaka 2001 na kuamua kufuga ng`ombe 1  baadae  wawili ambao walikua wakitoa  lita 40 kila siku huku yeye na familia yake wakitumia lita 1 hivyo maziwa mengine kuharibika baada ya kukaa kwa muda.
Suala hili lilimfikirisha sana Dokta Deo ambaye alimtafuta mtaalamu kutoka nchini Kenya  atakayemfundisha jinsi ya kuongeza thamani maziwa yake ,kuyafungasha na kuyauza .Mtaalamu huyo alimfundisha ndipo akaianza kazi ya kuongeza thamani maziwa hayo nyumbani kwake.
Baada ya muda majirani zake wafugaji walianza kuvutiwa na jinsi anavyoongeza thamani maziwa yake na walimletea maziwa ili ayaongeze thamani ndipo alipoanza kununua maziwa na kuongeza thamani takribani lita 100,150 mpaka 200 kwa siku.
Baada ya hapo akafungua kiwanda kidogo ambacho kilikua na uwezo wa kusindika lita 200  kwa siku huku wafugaji wakileta maziwa  mengi zaidi  ndipo alipoongeza uzalishaji na kwa sasa anazalisha lita 2000 kwa siku.
Kutokana na ongezeko hilo lauzalishaji kwa sasa Dokta Deo pamoja na Wakurugenzi wenzake wa kiwanda hicho cha The Grande Demam wameongeza wigo na kununua maziwa zaidi kwa wafugaji ambao walikua wakiteseka kupata masoko na wakati mwingine kumwaga maziwa yao yanayoharibika kwa kukaa muda mrefu bila kununuliwa.
Kiwanda hicho kinanunua maziwa bora kutoka kwa wafugaji na kuyaongezea thamani ikiwa ni pamoja na kuyafungasha vyema.
“Maziwa ambayo hayajaongezwa thamani hukaa kwa muda wa masaa 13 lakini maziwa yaliyoongezwa thamani yanaweza kukaa hadi mwezi mmoja jambo ambalo linaleta unafuu hasa kwa kipindi kifupi kabla hayajafika sokoni” Alisema Dokta Deo
Dokta Deo anaeleza kuwa maziwa yaliyosindwa ni maziwa mazuri kwa afya ya binadamu yamekua yameondolewa bacteria hatarishi na kuongezewa bacteria rafiki kwa afya.
Mtu anayetumia Maziwa ambayo hayajasindikwa anakua yuko hatarini kupata magonjwa mbalimbali ikiwemo Tb,Typhoid na Brusela.
Pia maziwa yaliyosindikwa kiwandani yanasaidia kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa yanayoweza kuambukizwa kutoka wanyama kwenda kwa binadamu.
Mkurugenzi wa kiwanda hicho Dokta Deo amesema kuwa maziwa ni bidhaa yenye faida kubwa sana katika mwili wa binadamu ikiwemo virutubisho aina ya Protini,Madini,Fat pamoja na wanga.
Dokta Deo anashauri kinywaji wa maziwa uhamasishwe kwa wingi katika jamii ili kuwa na jamii yenye afya bora inayoweza kushiriki katika shughuli za uzalishaji.
Anaeleza kutokana na ubora wa maziwa yanayozalishwa na kiwanda hicho wateja wamekua wakiyafurahia hivyo wanafirikiria kuongeza uzalishaji na kuboresha zaidi ili kuwafikia wateja wengi zaidi.
“Tuna mpango wa kuzalisha mpaka lita laki moja kwa siku ,uzalishaji huu utaleta tija kwa kiwanda pamoja wafugaji ambao tumekua tukinunua maziwa kwao tutanunua maziwa mengi zaidi hivyo kukuza kipato cha wafugaji waweze kunufaika na shughuli zao za ufugaji” Alisema Dokta Deo
Ni vyema Watanzania wakajifunza kunywa maziwa  haya bora yanayozalishwa nchini badala ya kunywa maziwa kutoka nje kwani kwa kufanya hivyo utakua unainua uchumi wa nje.
Biashara hiyo ya maziwa imesaidia vijana wengi  waliojiriwa na kiwanda hicho katika sekta ya uzalishaji na usambazaji jambo ambalo linaonyesha mnyororo wa wanufaika wa kiwanda hicho unavyoongezeka.
Kwa sasa  bidhaa za maziwa,Yogat na Siagi za The Grande Demam imefika katika mikoa ya Dar es Salaam ,Manyara ,Tanga na Morogoro.
Mshauri wa  Masuala ya Biashara katika Kiwanda Peter Ojukwu  hicho amesema kuwa kiwanda hicho kinaweza kuwanufaisha watu zaidi ya 4500 kutokana na mzunguko wa uzalishaji mpaka kumfikia mlaji.
Anaeleza kuwa licha ya kiwanda hicho kujikita na uzalishaji wa maziwa bado kinatoa huduma za ushauri wa ufugaji bora,matibabu ya mifugo pamoja na madawa ili waweze kufanya ufugaji wenye tija.
Pia anashauri serikali na taasisi binafsi kuunga mkono juhudi za Wawekezaji wanaowekeza kwenye viwanda ikiwamo kiwanda cha maziwa kwani kinagusa maisha ya watu wengi moja kwa moja.
“Kama unavyojua katika maziwa hakuna kinachosalia unatoa maziwa,siagi,yogati,samli,mtindi  hivyo hakuna kinachotupwa kila kitu kina thamani kubwa” alisema Mshauri huyo
Nassari na ni moja kati ya Wafugaji ambao maziwa yao yananunuliwa na kiwanda hicho wamesema kuwa tangu kuanzishwa kwa kiwanda hicho wamekua wakipata soko la uhakika la maziwa yao hivyo kuondokana na tatizo la maziwa kuharibika  kwa kukosa soko.
Anaeleza kuwa uwepo wa kiwanda hicho umewasaidia wafugaji wengi ambao walikua hawana pa kuyapeleka maziwa yao lakini kwa sasa wanafika katika kiwanda hicho na kuyapeleka maziwa yao.