ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, March 29, 2018

POLISI WAIMARISHA ULINZI MAHAKAMANI, KESI YA VIONGOZI WA CHADEMA,


Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limeimarisha ulinzi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili kudhibiti umati wa watu wanaodhaniwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao wamekusanyika nje ya mahakama, wasiingie kusikiliza kesi inayowakabili mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe na viongozi wenzake watano.

Mbowe na wenzake wameshafikishwa mahakamani hapo wakitokea mahabusu ya Segerea wakikabiliwa na mashtaka manane yakiwemo kufanya maandamano yaliyosababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline, Februari 16, mwaka huu, uasi na kuhamasisha chuki.
Lowassa.

Baadhi ya wabunge wa Chadema, wafuasi wa chama hicho na wananchi wengine waliofika mahakamani kufuatilia kesi hiyo ni  Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Prof. Abdallah Safari, Mbunge Joseph Haule ‘Prof. Jay.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.