ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 9, 2024

MABANGO NA UJUMBE MAADHIMISHO SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MISUNGWI MKOANI MWANZA.

aaaa
Mamlaka ya Usimamizi wa wanyamapori Tanzania TAWA - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii

Shirika la Umeme Tanzania - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Wizara ya \Uchukuzi na Huduma za Meli - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Wadau Halmashauri ya Misungwi - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Idara ya Uhamiaji Mwanza - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
TAHEA MWANZA - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii.
Wizara ya utamaduni, sanaa na Michezo - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu NIMR - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii
Mahakama ya Tanzania Kanda ya Mwanza - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii.
Mamlaka ya maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali - Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii

 Wekeza kwa wanawake Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii

WANAWAKE SF GROUP WAMWAGA MISAADA SHULE YA SEKONDARI KOKA, WATOTO YATIMA NA HOSPITALI YA LULANZI

 
VICTOR MASANGU,KIBAHA 

WANAWAKE wa kampuni ya SF group ya Jijini Dar es Salaam wameadhimisha kilele  cha siku ya mwanamke duniani kwa kufanya matendo ya huruma kwa kutoa msaada katika maeneo mbali mbali ya Jimbo la Kibaha mjini.

Wanawake hao wa SF group  wameweza kutembelea katika nyanja mbali mbali ikiwemo sekta ya elimu,afya pamoja ya mambo kuwatembelea watoto wenye mahitaji maalumu.

Katika maadhimisho hayo wanawake wa SF Group ambayo ndani yake kuna makampuni mbali mbali ambayo  yamekuwa mstari wa mbele katika kusaidiana na jamii.
Mkurugenzi wa Rasirimali watu wa SF Group Maria Faustine ambaye aliongoza jopo la wanawake hao walikwenda kutoa msaada wa vifaa mbali mbali  katika shule ya sekondari Koka.

Mkurugenzi huyo alibainisha kwamba wameamua kwenda kutoa vifaa katika shule hiyo ya Koka ikiwa ni katika kuwasaidia wanafunzi7 kupata mahitaji yao hususan kwa upande wa  wanawake.

"Tumeungana wanawake wote wa SF Group katika kuadhimisha kilele cha siku ya wanawake duniani kwa kutembelea maeneo matatu  ikiwemo shule ya Koka,watoto yatima pamoja na hospitali ya Lulanzi,"alisema Mkurugenzi Goleti.

Kadhalika aliongeza kuwa katika kuunga mkono juhudi  za serikali awamu ya sita katika kuboresha sekta ya elimu wameamua kutoa zawadi kwa msichana mwanafunzi aliyefanya vizuri katika masomo yake.
Pamoja na hayo walikwenda kutembelea kituo cha watoto yatima cha Buloma kilichopo kata ya Picha ya ndege na kutoa msaada wa mahitaji mbali mbali ya msingi ikiwemo vyakula mbali mbali kama sukari,unga pamoja na  sabuni,madaftari na mambo mengine ya msingi.

Kadhalika sambamba na hayo waliweza kutembelea katika Hospitali ya Wilaya ya Lulanzi ambapo pia waliweza kutoa msaada wa vitu mbali mbali  kwenye wodi ya wazazi.

Mkurugenzi Faustine alibainisha kuwa lengo kubwa la kwenda kutoa msaada katika maeneo matatu ni kwa ajili kuonyesha ushirikiano wa dhati kati ya wanawake wa SF Group pamoja na jamii.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule ya Koka Sekondari Magreth William aliwashukuru kwa dhati wanawake hao wa SF Group kwa msaada huo pamoja na Mbunge wa Jimbo hilo Silvestry Koka kwa sapoti katika mambo mbali mbali.

Kadhalika nao  baadhi ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika kituo hicho cha Buloma walitoa shukrani zao za dhati kwa msaada huo kutoka kwa wanawake wa SF Group.
Nao badhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) ambao walishiriki katika zoezi  hilo la ugawaji  hawakusita kutoa shukrani zao za dhati kwa wanawake  hao wa SF group.


SF Group imetumia kilele cha maadhimisho ya siku ya mwanamke duniani kufanya matendo ya Huruma katika sehemu tatu.shule ya Sekondari Koka.kituo cha watoto yatima Buloma na wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wilaya Lulanzi.

Thursday, March 7, 2024

BARRICK YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KWA KUTOA MSAADA WA MASHINE YA PATIENT MONITOR HOSPITALI YA RUFAA MWANANYAMALA

 

Afisa Mawasiliano wa Barrick, Neema Ndossi (kulia) akikabidhi msaada wa mashine ya Patient Monitor, kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala,Dkt. Zavery Benella.Wengine pichani ni Wafanyakazi wa Barrick alioongozana nao.
Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Wafanyakazi Wanawake wa kampuni ya Barrick kutoka ofisi ya Dar es Salaam wametembelea hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, na kukabidhi msaada wa mashine ya kudhibiti maendeleo ya kiafya ya watoto waliozaliwa na matatizo (Neonatal Patient Monitor).

Akiongea wakati wa kukabidhi kifaa hicho kwa uongozi wa hospitali hiyo, Afisa Mawasiliano wa Barrick, Neema Ndossi, aliyeambatana na baadhi ya Wafanyakazi Wanawake wakiungwa mkono na wafanyakazi wenzao Wanaume alisema “Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake, mwaka huu tumeona tutoe fadhila ya msaada wa Patient Monitor kwa ajili ya kusaidia watoto wachanga wanaozaliwa na matatizo katika hospitali hii.”

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt. Zavery Benella, ameishukuru Barrick na wafanyakazi wake kujitolea muda wao kutembelea hospitali na kutembelea wagonjwa katika wodi ya watoto.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala,Dkt. Zavery Benella, akiongea na baadhi ya wafanyakazi wa Barrick waliotembelea hospitali hiyo.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala Dkt. Zavery Benella (kushoto) akitoa maelezo ya huduma za hospitali hiyo kwa wafanyakazi wa Barrick walipotembelea wodi ya watoto.
Mwonekano wa mashine ya Patient Monitor iliyokabidhiwa katika hospitali ya Mwananyamala.
Wafanyakazi wa Barrick katika picha ya pamoja na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, Dkt. Zavery Benella.

Wednesday, March 6, 2024

DAWASA YAFANYA KWELI KUWASHA MITAMBO YA RUVU CHINI MUDA WOWOTE


VICTOR MASANGU BAGAMOYO

Mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inatarijia  muda wowote  kuwasha  baadhi ya pamp ambazo zilikuwa zimezimwa  kutokana na kukabiliwa na changamoto ya maji  kujaa tope katika baadhi ya maeneo kwenye  mtambo wa Ruvu chini uliopo Wilaya ya Bagamoyo.

Hayo yamebainishwa na Kaumu Mkurugenzi wa Dawasa Kiula Kingu wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufanya ziara kwa ajili ya kugagua na kujionea mtambo wa Ruvu chini.
Kadhalika amebainisha kwamba kutokana na hali hiyo wamelazimika kutumia zaidi ya mapipa  makubwa 97  ya lita 200 kwa siku  kwa ajili ya kusafishia maji hayo yaweze kuwa safi na salama kwa wananchi.

"Kwa kweli maji yapo ya kutosha lakini changamoto kubwa ni machujio yaliyopo katika mtambo wa ruvu juu kujaa na matope mengi hivyo kusababisha hata maji kubadilika rangi yanakuwa kama vile ya udongo ",alifafanua Kiula.
Kadhalika alifanua kwamba hali ya kuwepo kwa maji mengi ni kutokana na uharibifu wa mazingira na kupelekea kujaa matope katika chujio.

Pia alifafanua kuwa kuwepo kwa tope kunapelekea kwa kiasi kikubwa kupungua kwa uzalishaji wa maji  katika baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam na Pwani.

"Kwa hiyo tuliomba masaa 36 kwa wananchi wetu lakini lengo kubwa lilikuwa ni kwa ajili ya kufanya marekebisho katika baadhi ya machujio yetu ya maji,"alibainisha Kiula.
Alisema kwamba kwa sasa mafundi wapo kazini kwa ajili ya kuhakikisha wanarekebisha katika maeneo ambayo yalikuwa yamejaa tope ili huduma ya maji iweze kurudi kwa wananchi  muda wowote kuanzia leo.


Alisema kwamba baada ya kufanyika kwa matengenezo hayo wananchi watarajie kupata maji ya kutosha ambayo pia yatakuwa katika kiwango cha usafi.
Katika hatua nyingine Kingu alisema kwamba mtambo wa ruvu chini unazalisha maji kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kwa kiwango cha asilimia 75 huku akisema kwa sasa kiwango kimeshuka kwa asilimia 20 kutokana na changamoto hiyo ya tope.

 Hivi karibuni Dawasa  walitoa tangazo la kukosekana kwa  huduma ya kukata maji kwa kuzima kwa pampu na kukosekana na huduma ya maji kwa  kipindi cha zaidi ya masaa 36.

Sunday, March 3, 2024

UONGOZI WA CCM KIBAHA MJI WAMSAIDIA MAGONGO KIJANA ALIYEVUNJIKA MGUU KWA AJALI

 


NA VICTOR MASANGU KIBAHA 



Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini  Issack Kalleiya ametimiza ahadi yake kwa vitendo kwa kutoa msaada wa magongo  kwa kijana mmoja anayeishi katika kata ya Msangani.

Kijana huyo ambaye anajulikana kwa jina la John William amepatiwa msaada huo baada ya kupata ajali ya kupushiwa na Lori hivi karibuni na kupelekea mguu wake wa kulia kuvunjika kwa chini.

Katibu huyo wa CCM alike da kutoa msaada huo akiwa ameambatana na viongozi mbali mbali wa chama sambamba na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kibaha mji Mwalimu Mwajuma Nyamka pamoja na baadhi ya wananchi wengine.

Katibu huyo alisema kwamba alipokea kwa masikitiko makubwa juu ya taarifa hiyo ya kijana wa CCM kupata ajali hivyo aliahidi kwenda kumuona pamoja na kumpatia msaada huo wa magongo.

"Kwa kweli mimi kama kiongozi niliguswa sana na tukio hili la kijana wetu wa ccm ambaye kwa kweli nikaona kuna umuhimu kumsaidi kwa hali na mali magongo ambayo yataweza kumsaidia katika kufanya mazoezi ya kutembea,"alifafanua Katibu huyo.

Kadhalika alisema kwamba  kijana huyo amekuwa mstari wa mbele katika kushirikiana na vijana wenzake kwa lengo la kukilinda na kukiimarisha chama katika mambo mbali mbali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Kibaha mji Mwalimu Mwajuma Nyamka naye  alifika nyumbani kwa kijana huyo kwa ajili ya kumona na kumfariji.

Naye Kijana huyo John William aliyepata ajali alimshukuru kwa dhati Katibu wa CCM kwa moyo wake wa upendo wa kumpatia magongo hayo na kuwashukuru viongozi wote wa CCM waliokwenda kumjulia hali na kumpa pole.