ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 17, 2015

KAGERA SUGAR YANYWEA MBELE YA MBEYA CITY 0-1 UWANJA WACCM KIRUMBA MWANZA

Mwamuzi wa mchezo akirusha shilingi kupiga kura timu gani ianze kulisukuma gozi, mchezo wa Ligi Kuu soka Tanzania bara kati ya Kagera Sugar na Mbeya City, uliochezwa kwenye dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza. Mbeya City waliibuka wababe kwa kuikunjua Kagera Sugar bao 1-0. 
Watangazaji wa Kasibante Fm walirusha live mchezo huo.
Kagera wakijifua.
Mbeya City wakijifua.
Kikosi cha Mbeya Citykilichoshuka dimbani kupepetana na Kagera Sugar, dimba la CCM Kirumba jiini Mwanza.
Dakika ya 25 kipindi cha kwanza hakuna kipya bao 0-0
Dakika 90 zinamalizika Kagera wamelowa 0-1 dhidi ya Mbeya City. 
SIKILIZA SAUTI YA SPORTS XTRA KUJUA KIPI KILICHOJIRI 

Friday, January 16, 2015

AMAVUBI KUTUA MWANZA JANUARY 21 KUPEPETANA NA TAIFA STARS

Timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi) itawasili Mwanza, Tanzania Januari 21 mwaka huu kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Taifa Stars Maboresho itakayochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini humo.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Boniface Wambura, Amavubi yenye msafara wa watu 26, wakiwemo wachezaji, benchi la ufundi na viongozi itawasili kwa ndege ya RwandAir na siku hiyo hiyo jioni itafanya mazoezi kwenye Uwanja wa CCM Kirumba. Timu hiyo itafikia kwenye hoteli ya JB Belmont.
Baada ya kocha Mdachi, Mart Nooij kutaja kikosi, Stars inaingia kambini keshokutwa (Januari 18 mwaka huu), na siku inayofuata itakwenda Mwanza tayari kwa ajili ya mechi hiyo itakayofanyika Januari 22 mwaka huu.
Kikosi hicho cha Kocha Mart Nooij ambacho ni sehemu ya maandalizi ya mechi za mchujo za michuano ya Afrika kwa Wachezaji wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN) kinaundwa na wachezaji 26.

SKYLIGHT BAND WAZIDI KULITIKISA JIJI LA DAR WASAJILI VIFAA VIPYA AKIWEMO JOHN MUSIC

Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 akitoa burudani kwa mashabiki wa Skylight Band Ijumaa iliyopita kwenye kiota cha Thai Village Masaki jijini Dar.
Kifaa kipya ndani ya Skylight Band John Music akiimba kwa hisia kaliii huku akipewa sapoti na Wenzake wa kwanza kushoto ni Baby na wa pili kutoka kushoto ni Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 na kulia ni Jessie.
Wanaume wa shoka wa Skylight Band kutoka kushoto ni Joniko Flower, Sony Masamba na Sam Mapenzi wakionyesha mbwembwe zao za kulisakata sebene kwa mashabiki wao, ambapo jioni ya leo watakuwepo kama kawaida kwenye kiota cha maraha Thai Village
Wanaume wa shoka wa Skylight Band kutoka kushoto ni Joniko Flower, Sony Masamba na Sam Mapenzi wakionyesha mbwembwe zao za kulisakata sebene kwa mashabiki wao, ambapo jioni ya leo watakuwepo kama kawaida kwenye kiota cha maraha Thai Village
Jessie(katikati) akiimba kwa raha zakee ndani ya Thai Village akipewa sapoti na Baby pamoja na Aneth Kushaba AK47.
John Music akiiendelea kutoa burudani ya nguvu huku akipewa sapoti na Wenzake wa kwanza kushoto ni Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 na wa pili kutoka kushoto ni Baby na kulia ni Jessie
Sam Mapenzi akiimba Naija Flava njoo leo umshuhudie kwa macho yako...Skylight Band ndio kila kitu huna haja ya kwenda disco unapata kila kitu hapa hapa.
Kikosi kazi cha Skylight Band kikiongozwa Meneja wa Band Aneth Kushaba AK47, Sam Mapenzi na Sony Masamba kwa pamoja wakiwapa raha mashabiki wa bendi hiyo (hawapo pichani) kwenye kiota cha maraha cha Thai Village Masaki jijini Dar Ijumaa iliyopita ambapo leo wataendelea kutoa kuwaburudisha mashabiki wake kama kawaida kuanzia saa tatu usiku.
DSC_0021
Mashabiki wa Skylight Band wakiburudika na muziki safi kabisa wa ladha na vionjo vya kila aina ikiwemo Reggae, Kwaito, Naija Flava, R&B, Zouk na zingine kibao bila kusahau sebene pale kati Joniko Flower anahusika sana sambamba na Sony Masamba.
Mashabiki wa Skylight Band wakiburudika na muziki safi kabisa wa ladha na vionjo vya kila aina ikiwemo Reggae, Kwaito, Naija Flava, R&B, Zouk na zingine kibao bila kusahau sebene.

Thursday, January 15, 2015

BALOZI WA UINGEREZA NCHINI TANZANIA AKUTANA NA VIJANA WA SOKA WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU MWANZA

Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose (kushoto) akikabidhi msaada wa jezi na bukta zake kwa mtoto Sunday Hassan ambaye alisimama kwa niaba ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanaosimamiwa na kituo cha kulea na kukuza vipaji vya soka cha TSC Academy cha jijini Mwanza, kulia ni Rais wa TSC Altaf Hirani ambaye pia ni Mkurugenzi wa MOIL akifanya usaidizi kwa makabidhiano.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose (kushoto) akikabidhi msaada wa jezi na bukta zake kwa mtoto Sunday Hassan ambaye alisimama kwa niaba ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanaosimamiwa na kituo cha kulea na kukuza vipaji vya soka cha TSC Academy cha jijini Mwanza, kulia ni Rais wa TSC Altaf Hirani ambaye pia ni Mkurugenzi wa MOIL akifanya usaidizi kwa makabidhiano.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose amesema kuwa shughuli za kusimamia watoto wanao taabika wakiishi kwenye mazingira magumu ni muhimu sana kwa jamii yote kwani watoto hao wakikosa misingi mizuri kama elimu, maadili, chakula, afya na makazi ya kueleweka wanaweza kuwa na madhara makubwa kwa Taifa.

Hivyo amewataka Watanzania wazalendo na wale wageni wenye mapenzi mema, vituo mbalimbali, makampuni na watu binafsi kuitikia wito kwa kuwasaidia watoto hao katika kufanikisha ndoto zao.

Wakisikiliza kwa umakini (walioketi) hawa ni baadhi ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanaosimamiwa na kituo cha kulea na kukuza vipaji vya soka cha TSC Academy cha jijini Mwanza.
Wakisikiliza kwa umakini huku wengine wakichukuwa kumbukumbu.
Watoto wanaoishi katika mazingira magumu wenye umri wa chini ya miaka 12 wanaosimamiwa na kituo cha kulea na kukuza vipaji vya soka cha TSC Academy cha jijini Mwanza, wakijumuika kwenye mazoezi chini ya kocha wao Nyangi Kilacha.
Kocha Nyangi Kilacha akitoa maelekezo kwa timu ya vijana wa chini ya miaka 14 ambao ni sehemu ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanaosimamiwa na kituo cha kulea na kukuza vipaji vya soka cha TSC Academy cha jijini Mwanza, waliojumuika kwenye mazoezi hii leo na kuupokea ubalozi wa Uingereza uliowatembelea. 

Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose akiwa na Rais wa TSC Altaf Hirani aka Dogo ambaye pia ni Mkurugenzi wa MOIL katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu mabingwa wa Kombe la Dunia la vijana wa mitaani TSC Academy waliolinyakuwa mjini Rio De Jeneiro nchini Brazil 2014.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose na TSC.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose katika picha ya pamoja na golikipa bora wa mabingwa wa Kombe la Dunia la vijana wa mitaani TSC Academy waliolinyakuwa mjini Rio De Jeneiro nchini Brazil 2014.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose akiwa na Rais wa TSC Altaf Hirani aka Dogo ambaye pia ni Mkurugenzi wa MOIL katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu mabingwa wa Kombe la Dunia la vijana wa mitaani TSC Academy waliolinyakuwa mjini Rio De Jeneiro nchini Brazil 2014.
Licha ya kuishi katika mazingira ya ushawishi na hatarishi katika malezi, Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Dianna Melrose amesihi vijana hao kuzingatia mafunzo wanayopewa yakiwemo yale ya kuishi  na kumjua Mungu huku wakijiepusha na vishawishi vitakavyo waingiza katika majaribu yanayoweza kufifisha ndoto zao za mafanikio.

Ili kuweza kukuza vipaji na kuwa na mfumo endelevu wa kuendeleza vijana hao ambao watakuwa na manufaa na mabadiliko chanya kwa taifa katika medani ya mchezo wakandanda nchini 
Rais wa TSC Altaf Hirani aka Dogo amesema kuwa endapo Serikali ya mkoa wa Mwanza itatimiza ahadi yake ya kukipatia kituo hicho eneo la michezo kama ahadi yake maendeleo makubwa katika mchezo wa soka yatapatikana.

"Mwaka jana tuliporudi toka Brazil tukiwa mabingwa wa Kombe la Dunia la vijana waishio Mazingira magumu, katika sherehe aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Injinia Evarist Ndikilo pamoja ofisi ya Halmashauri ya jiji kupitia Meya wake Stanslaus Mabula waliahidi kutupatia eneo ambalo litatumika kujenga kituo cha michezo ahadi ambayo mpaka sasa bado haijatekelezwa lakini ninaimani Serikali haitotuangusha kwa hili na nina imani watatupa sapoti ya kutosha" 

"Katika kutimiza ndoto zetu sisi kama kituo tayari tumeshakamilisha taratibu zote za awali kwani tumeshapeleka barua kwa Halmashauri husika, hivyo kikubwa tunasubiri majibu kutoka kwao kwani wawekezaji toka nje wameonyesha nia ya kutusaidia na wapo tayari kwa ajili ya mpango wa ujenzi wa kituo hicho cha michezo" Alisema 
Altaf Hirani.  

Albert G. Sengo
albertgsengo@yahoo.com
+255 754 074 152

THT KUADHIMISHA MIAKA KUMI TOKA KUANZISHWA KWAKE


THT kuadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake, tarehe 31/1/2015, Escape 1

·        Kufungua kampuni ya ushonaji na ubunifu wa mavazi

Kituo cha kuzalisha na kukuza vipaji, Tanzania House of Talent, kinatarajia kuadhimisha miaka kumi toka kuanzishwa kwake hapo tarehe 31/1/2015 Escape 1 jijini Dar es Salaam.

THT ilianzishwa mwishoni mwa mwaka 2005 kwa lengo la kuwasaidia vijana wenye vipaji, lakini wasio na uwezo wa kujiendeleza wenyewe, kwenye sekta ya sanaa hapa nchini, na toka wakati huo kituo kimekuwa na mafanikio makubwa na mchango wa pekee kwenye kukuza sanaa ya muziki nchini.

Akizungumza wakati wa kuzindua maadhimisho hayo ambayo yatakuwa kwa mwaka mzima, Meneja Mkuu wa Kituo hicho, Mwita Mwaikenda alisema ni heshima kubwa kuweza kusherehekea miaka kumi toka imeanzishwa kwani wameweza kufanikisha mambo mengi makubwa.

‘Tulianzisha kituo hiki miaka kumi iliyopita kwa hakika tukiwa hatuna chochote zaidi ya imani yetu kwenye vipaji vya vijana, na tulianza hatuna hata sehemu ya maana, lakini leo miaka kumi baadaye vijana zaidi ya 3000 wamefaidika na kituo hiki kwa namna moja au nyingine na wameweza kumudu maisha yao na familia zao kutokea kuwa watoto wa mitaani’ alisema Mwita.

THT ikiwa imeanzishwa kama kituo cha kusaidia watoto wa mtaani wenye vipaji, imeweza kukua kwa kipindi cha miaka kumi, na sasa sio tu inazalisha na kukuza vipaji bali imekuwa ikitoa huduma zote kuanzia kuratibu matamasha, kuandaa mpangilio wa burudani, kutengeneza matangazo ya radio na televisheni pamoja na makala na vipindi vya televisheni.

‘THT imeweza kuratibu burudani ya matamasha mbalimbali kama FIESTA, Mkutano wa Smart Partnership, Sensa ya mwaka 2013, Sherehe za miaka 50 ya Muungano pamoja na mikutano na matamasha kadha wa kadha’ alisema Meneja Masoko wa THT, Michael Nkya.

THT imeendelea kukua kwa kuweza kuanzisha studio yake ambayo imeweza kurekodi matangazo, nyimbo za wasanii wote wa THT pamoja na wengine wengi kama Mdogomdogo na Number One Remix ya Diamond, Me and You ya Ommy Dimpoz, Prokoto ya Victoria Kimani na nyingine nyingi.

Kwa sasa THT inatengeneza vipindi mbalimbali vya televisheni kama 69 Records, na vingine vingi vinavyorushwa chaneli za nje huku pia ikijivunia kuwa na maktaba ya nyimbo kubwa zaidi nchini.

‘Shukrani zetu za dhati kwa kweli ni kwa serikali, hasa hasa Mheshimiwa Rais Kikwete, ambaye toka mwanzo alikubali wazo na akaamini mziki unahitaji elimu ya peke yake, lakini pia makampuni mbalimbali ambayo wamekuwa wakitupa kazi pamoja na vyombo vyote vya habari kwa kutuunga mkono siku zote’ alisema Bwana Nkya.

Akielezea kuhusu mwelekeo wa kituo baada ya miaka kumi, Mwita alisema anaamini kituo kimefanya kazi yake tayari kwa kuweza kuchagiza sanaa ya muziki nchini, na sasa ni wakati wa kuendelea kusaidia wadau au vituo vingine kama Mkubwa na Wanawe kufika THT ilipofika.

‘Kimsingi mwaka huu ndio mwaka wa mwisho kuendela kupokea wanafunzi wapya wa kuimba, na mpango wetu ni kuendelea kukuza kituo kwa kuanzisha kampuni ya ushonaji na ubunifu wa nguo kwa kutumia kitenge ambao tunaamini utatoa ajira kwa vijana wengi zaidi hapa nchini’ alisisitiza Mwita.

Kampuni ya ubunifu na ushonaji kwa kutumia vitenge, tayari ishaanza mchakato wake kwa kuhusisha wadau wa biashara ya vitenge, na mbunifu mahiri Ally Remtullah, mwanamitindo Flaviana Matata wakiwa ndio walezi na wasimamizi wa mradi ambao utaanza na wabunifu wanaochipukia Neyonce pamoja na Adam Mchovu.


‘Kwa kuanza mradi utapeleka wabunifu nchini China ili wakajifunze zaidi juu ya ubunifu na kuongeza ubora kwenye kazi zao, wakirudi tunaamini wataweza kuwafundisha vijana wengi zaidi, na kutimiza lengo letu la kuwasaidia vijana kujiajiri’ alimaliza Mwita.

AIRTEL YATOA VITABU VYA SAYANSI SEKONDARI BARIADI SIMIYU

Mkuu wa wilaya ya  Bariadi Bw. Erasto Sima akisoma Hotuba katika makabidhiano ya msaada wa vitabu vya masomo ya sayansi kwa shule ya sekondari Bariadi uliotolewa na kampuni ya Airtel Tanzania
Mkuu wa shule ya sekondari ya Bariadi Bw. Pawa Lutema akipokea msaada wa vitabu vya sayansi kutoka kwa mkuu wa wilaya Bariadi, Vitabu hivyo vyote vinathamani ya sh milioni 6 na ni vya masomo ya sayansi kutoka kampuni ya simu ya Airtel kupitia mradi wake wa kusaidia elimu wa Airtel Shule yetu.
Meneja wa Airtel Simiyu Bw. Ezekiel Nungwi akikabidhi msaada wa vitabu vya sayansi vyenye thamani ya milioni 6 kwa Mkuu wa wilaya ya Bariadi Bw. Erasto Sima, vitabu hivyo ni sehemu ya msaada wa Airtel kupitia mradi wake wa Airtel shule yetu.
AIRTEL YATOA VITABU VYA SAYANSI SHULE YA SEKONDARI BARIADI SIMIYU.  
                        
·         Airtel yaahidi kukabidhi vitabu mikoa ya Kilimanjaro na Arusha mwezi huu

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imepiga jeki jitihada za serikali za kuhamasisha masomo ya sayansi kwa kutoa msaada wa vitabu vya sayansi kwa shule ya sekondari ya Bariadi iliyopo Mkoani Simiyu.

Msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni 6 unahusisha vitabu vya fizikia, hisabati, baiolojia na kemia kwa ajili ya wanafunzi wanaosoma masomo hayo shuleni hapo.

Akipokea msaada huo mkuu wa wilaya ya Bariadi Bw. Erasto Sima amesema shule nyingi wilayani humo zimekuwa zikikabiliwa na changamoto ya upungufu wa vitabu vya masomo ya sayansi licha ya kwamba kuna uhaba pia wa walimu wa masomo hayo.

“Ni kweli kwamba uhaba wa vitabu unakwamisha kwa kiasi kikubwa wanafunzi kujifunza kwa ufasaha masomo ya Sayansi wilayani Bariadi hali inayorudisha nyuma ukuaji wa elimu ya sayansi wilayani hapa”. Alisema Bwana Sima.

“uhaba wa vitabu ni moja ya changamoto, lakini uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi ni kikwazo kikubwa kwa utoaji wa elimu ya sayansi kwa wanafunzi wetu hapa Bariadi” aliongeza Bwana Sima.
  
Aidha Bw. Sima ameishukuru kampuni ya simu ya airtel  kwa kuona umuhimu wa kuboresha masomo ya sayansi ambayo  ufaulu wake umekuwa mdogo hali ambayo inayotoa fursa kwa wanafunzi kujifunza kwa umakini zaidi.

“Msaada huu utaongeza hamasa kwa wanafunzi wetu kujifunza masomo ya sayansi hivyo tunawashukuru sana Airtel kwa kuona umuhimu wa kusaidia shule hii na hasa vitabu vya sayansi” alimalizia Bwana Sima.

Kwa upande wake mkuu wa shule ya sekondari Bariadi Bw. Pawa  Lutema akipokea vitabu hivyo, amesema hatua hiyo ni sehemu ya utatuzi wa changamoto ya vitabu vya sayansi na kisha kuahidi kuvitunza ili viwe msaada kwa wanafunzi watakaosoma shuleni hapo.

 Awali  meneja wa Airtel Mkoani Simiyu Bw. Ezekiel Nungwi  akikabidhi  msaada huo wa vitabu  amesema kuwa kampuni yake inaendelea tena katika mwaka huu wa 2015 na mpango wake wa kutoa msaada wa vitabu kwenye shule mbalimbali nchini kwa lengo la kusaidia ukuaji wa elimu nchini.

Msaada huo wa vitabu vya masomo ya hisabati,kemia,fizikia na Bailojia utasaidia kupunguza uhaba wa vitabu vya sayansi kwenye shule hiyo.

Airtel pia kupitia mfuko wake huo wa Airtel Shule yetu mwezi huu imejipanga kukabidhi vitabu katika mikoa mingine miwili ikiwemo Kilimanjaro na Arusha ambapo inatarajiwa kuzifikia zaidi ya shule zingine sita.

HARUSI YA JULLY NA SUMAI ILIVYOFANA NCHINI AFRIKA YA KUSINI (PARTY ONE)

Bwana harusi Jully Iluga Mbwembwe akiwa na Bi. Harusi wake Sumai Kazi mara baada ya kufunga ndoa takatifu nchini Afrika ya Kusini.
Pozi la Bi. Harusi Sumai Kazi.
Bustanini.
Baba wa Bi. Harusi Mr. Kazi akitinga eneo la kanisa na Bi. Harusi kwaajili ya kumkabidhi. 
Wow...
Pete ya harusi.
Signature.
Cheti cha ndoa.
Uwepo wa Mungu na baraka zake kwa ndoa.
"Yes I do...."
Si wawili tena bali ni mwili mmoja.
WapambeZ.
Time 4 pix.
Brothers walio hudhuria.
Pix na Maharusi.
Clean.
'Fresh'
Tukioni.
Bustanini.
Nice.
With family friends.
Good.
Maharusi na akinamama wawakilishi.
Maharusi with Sisterz. 
Maharusi with Brotherz.
Wow.
Yes.
WaoOo...!!
Sisterz with Mrs. Kazi.
ITAENDELEA....