ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 31, 2024

KIKOSI CHA SIMBA DHIDI YA AL HILAL YA SUDAN

 

FUNGA Agosti 2024 Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Fadlu Davids inashuka Uwanja wa KMC Complex kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Al Hilal ya Sudan.

Hiki hapa kikosi cha Simba kinachoanza:-

Manula.

Kapombe

Nouma

Che Malone

Chamou

Kagoma

Kibu

Fernades

Ateba

Chasambi

Awesu

Kwa wachezaji wa akiba ni:-

Hussen

Duchu

Kazi

Kijili

Hamza

Mzamiru

Omary

Okejapha

Mutale

Karabaka

Mashaka

CCM KIBAHA MJI YATEMA CHECHE ZAKE KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

 
Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini kimewataka viongozi wa CCM  kuanzia katika ngazi za Kata, Wilaya na Mkoa kutoingilia kabisa  maamuzi ya wana ccm pamoja na wananchi katika suala zima la  kuwachagua viongozi wanaowapenda katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu kwani wao ndio wanawafahamu  vizuri uwezo wao wa kuchapa  kazi.
 
Kauli hiyo imetolewa na  Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) mwalimu Mwajuma Nyamka wakati wa kikao cha Halmashauri kuu  CCM Wilaya ya Kibaha mji ambacho kimefanyika kwa lengo la kuweza  kupitisha utekelezaji wa Ilani kwa kipindi cha kuanzia Januari  hadi mwezi Juni mwaka 2024 na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na chma.


Nyamka amebaainisha kwamba lengo  kubwa la chama cha mapinduzi ni kuhakikisha inaweza kushinda kwa kishindo katika mitaa yote hivyo ni wajibu wa viongozi wote wa CCM  kuanzia ngazi za mashina na matawi kushikama kwa pamoja na kwamba kutokana na kazi nzuri ambayo imefanywa na Rais Samia Suluhu Hassan katika miradi mbali mbali ya maendeleo watatembea kifua mbele katika kuomba kura kwa wananchi.


Kadhalika Mwenyekiti huyo aliwapongeza madiwani wa Halmashauri ya mji Kibaha pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka kwa kuweza kushirikiana bega kwa bega katika suala zima la utekelezaji wa miradi mbali  mbali ikiwa sambamba na kutatua kero na changamoto  za wananchi.

"Pamoja na juhudi kubwa ambazo zinafanywa na CCM kusimamia utekelezaji wa Ilani lakini bado kuna baadhi ya watendaji wa mitaa,na kata wamekuwa ni kama tatizo kubwa kwa wananchi kiasi cha kupelekea kuwakwaza kwa kiasi kikubwa kutokana na kutoa lugha zisizokuwa na staha kabisa na kwamba hawataweza kuwawafumbia macho hata kidogo  watendaji wa namna hiyo kwani watatupunguzia kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa,"alisema Nyamka.

Pia katika Katika kikao hicho Mwenyekiti Nyamka amesema kwamba  wameiagiza Halmashauri ya mji Kibaha kuhakikisha kwamba wanaitunza miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo imemalizika hususan katika miundombinu ya barabara.

"Tumepitisha utekelezaji wa Ilani kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu wa 2024, lakini kitu kikubwa tumeagiza halmashauri yetu ya mji kuitunza miundombinu ya barabara hasa katika maeneo yenye lami kwani kumukuwa na changamoto ya kutozitunza maana utakuta maeneo  mengine nusu kifusi cha mchanga na nusu lami,"alibainisha Nyamka.

Aidha Mwenyekiti huyo amebainisha kwamba kuna baadhi ya halmashauri nyingine wameweka mikakati ya kuzitunza barabara zao kwa kuzifanyia usafi na kuzifagia lakini kwa upande wa Halmashauri ya kibaha mjini jambo hilo linakuwa ni vigumu hivyo linapaswa kufanyiwa utekelezaji.

Pia Mwalimu Nyamka amesema kwamba  kumekuwepo na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara ambao unafanywa na baadhi ya madereva kupitisha magari ya mchanga yenye uziti mkubwa ambayo ndio yamekuwa ni moja ya chanzo cha kufanya barabara ziweze kuharibika kwa haraka.
 
Kwa upande wake Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mji  Issack Kalleiya ametumia kikao hicho kutoa pongezi kwa mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya mji Kibaha kwa kuweza kubuni vyanzo vipya amabvyo vimepelekea kuongeza zaidi ukusanyaji wa kasi ya kuongeza mapato.

Kadhalika Katibu kalleiya amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, madiwani,pamoja na Mbunge kwa kuweza kushikamana kwa pamoja katika kutekeleza Ilani ya chama kwa vitendo ikiwa sambamba na kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo katika nyanja mbali mbali ikiwemo sekta ya afya, elimu, maji, miundombinu ya barabara pamoja na huduma nyingine za kijamii.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon amemshukuru na kumpongeza Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutenga fedha nyingi katika Halmasshauri ya mji wa Kibaha ambazo zimeweza kuleta matokeo chanya katika suala zima la kuwasaidia wananchi katika miradi mbali mbali za maendeleo.

Aidha Mkuu huyo alisema kwamba kwa ushirikiano mkubwa ambao anaupata kutoka kwa viongiozi wa chama cha mapinduzi (CCM) Madiwani wote pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini,mkurugenzi wameweza kutekeleza Ilani ya chama kwa kiwango kikubwa ikiwemo kumsaidia Rais katika utekelezaji wa majukumu yake.

DIWANI KAMBI AFANYA KWELI ATOA MSAADA WA PHOTOCOPY MASHINE SHULE YA MSINGI VISIGA

 


VICTOR MASANGU, KIBAHA

Diwani wa kata ya Visiga katika Halmashauri ya mji Kibaha Mhe. Kambi Legeza katika kuunga mkono na  kuchagiza  chachu ya maendeleo katika sekta ya elimu ameamua kutoa msaada wa mtambo  maalumu wa kusaidia  kutolea nakala mbali mbali za karatasi  'Photocopy mashine'  katika shule ya msingi visiga kwa ajili ya kuwasaidia walimu na wanafunzi kuondokana na adha waliyokuwa nayo.

 Kambi ametoa msaada wa mashine hiyo wakati  sherehe ya  mahafali ya shule ya msingi Visiga ambayo imeandaliwa kwa ajili ya kuweza kuwaaga wanafunzi waliomaliza wa darasa la saba wapatao 248 ambao wamefanikiwa kuhitimu katika hatua hiyo ngazi ya msingi  na kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali, wakiwemo wa  chama, wazazi , walimu,  walezi pamoja  na wazazi.

Kambi amesema  kwamba amesema kwamba ameamua kutoa msaada huo kutokana na  kubaini katika shule hiyo kuna uhitaji mkumbwa kupeleka mashine hiyo ambayo itakuwa ni mkombozi mkubwa katika kuwasaidia walimu na wanafunzi ambao wamekuwa wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma hiyo kutumia gharama kubwa hivyo itaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwa upande wao.

"Mimi kama Diwani wa kata ya Visiga nimebaini kuna changamoto kubwa na wazazi na walezi kuchanga michango mbali mbali kwa ajili ya kutoa nakala za mitihani hivyo kunatumika gharama nyingi sana kwa hivyo nikaona kuna umuhimu mkubwa kupitia mahafali haya niweze kutoa mashine hii ya Photocopy ambayo  nina amini itaweza kuleta mageuzi makubwa katika shule hii ya msingi Visiga,"alisema Mhe. Kambi  

Pia aliongeza kwamba lengo lake kubwa ni kuweza kuweka mikakati kabambe kwa ajili ya kumsaidia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo hivyo ameahidi kuendelea kutoa sapoti katika shule nyingine zilizobaki ili kuweza kukuza na kuboresha sekta ya elimu kwa ngazi ya msingi na Sekondari  katika Kata ya Visiga.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya  shule ya Visiga Kasmir Komba amempongeza kwa dhati Diwani huyo kwa kuweza kutoa mashine hiyo ambayo itaweza kwenda kupunguza changamoto ya siku nyingi ambayo ilikuwa inawakabili katika suala zima la kutoa nakala mbali mbali hasa katika kipindi cha kutolea mitihani na mambo mengine ya muhimu.

Mwenyekiti huyo aliongeza kwamba shule hiyo ambayo imeaanzishwa  mnamo  mwaka 1992 imekuwa ikifanya vizuri  kwa wanafunzi wake katika mitihani mbali mbali  japo inakabiliwa na baadhi ya changamoto mbali mbali zikiwemo uhaba wa madawati, pamoja na uchakavu wa madirisha kwa baadhi ya madarasa.

Nao baadhi ya wazazi ambo wamehudhuria katika mafali hayo akiwemo Zainabu Abdalah hawakusita kutoa pongezi zai za dhati kwa Diwani wa kata ya Visiga ambaye ameweza kuondoa kero ya michango mbali mbali ambayo walikuwa wakichangishwa na walimu kwa ajili ya kutoa nakala za mitihani hivyo mashine hiyo itawaondolea kabisa baadhi ya michango.

Alifafanua kwamba kabla ya kutolewa kwa mashine hiyo hapo awali wazazi na walezi walikuwa wanachangia kiais cha shilingi elfu 1200 ili mtoto aweze kupata huduma ya kufanya mitihani jambo amabalo lilikuwa ni usumbufu mkubwa kutokana na hali ya kipato na uchumi waliyonayo lakini kwa kitendo alichokifanya diwani huyo kinafaa kuigwa kwa viongozi wengine.

KULA CHUMA HICHO TOKA KWA EXTRA MUSICA

 

 

Extra Musica Nouvel Horizon - EN FORCE ( clip officiel )

MKE WA MBUNGE JIMBO LA KIBAHA MJI KULETA MAGEUZI YA ELIMU SHULE YA MSINGI MKUZA


 NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Mke wa Mbunge la Jimbo la Kibaha mjini Mama Selina Koka katika kuboresha sekta ya elimu ameahidi kuzivalia njuga   baadhi ya changamoto mbali mbali zinazoikabili shule ya msingi Mkuza.

Mama Koka ametoa ahadi hiyo wakati wa sherehe za mahafali ya  kuhitumu wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Mkuza iliyopo katika Halmashauri ya mji Kibaha.

Alisema kwamba dhamira yake kubwa ni kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kupambana na kuboresha sekta ya elimu.


"Mimi kama mke wa Mbunge nitajitahidi kwa hali na mali pamoja na familia yangu kusaidia mahitaji mbali mbali kwa upande wa wanafunzi pamoja na walimu wa shule hii ya mkuza,"alisema Mama Koka.

Aliongeza kwamba anatambua shule hiyo inakabiliwa na changamoto mbali mbali na kuongeza kuwa ataanza kusaidia mahitaji mbali mbali ya msingi ikiwemo mtambo maalumu wa kutolea nakala 'Photocopy mashine' ambayo itawasaidia katika kuendeshea kazi zao mbali mbali.

Kadhalika alimpongeza Rais  Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutenga fedha nyingi ambazo zimeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo katika Jimbo la Kibaha mjini.


Katika hatua nyingine Mama Koka alitoa zawadi mbali mbali kwa wanafunzi wa shule hiyo ambao wameweza kufanya vizuri katika masomo yao ikiwa pamoja na kuwapatia zawadi ya vitenge wazazi pamoja na walimu kwa kufanya kazi nzuri ya kuwatunza na kuwalea watoto.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ya msingi Mkuza amempongeza kwa dhati Mama Selina Koka kwa jitihada zake za kushirikiana na walimu katika kuboresha sekta ya elimu.

Aidha Mwalimu huyo pamoja na hayo hakusita kueleza baadhi ya changamoto zinazowakabili zikiwemo uhaba wa vyumba vya madarasa,uhaba wa matundu ya vyoo,pamoja na uhitaji wa tenki la kuhifadhia maji.

Alimuomba pia asaidiwe kutatuliwa changamoto hizo ikiwemo kuboresha miundombinu ya majengo ya madarasa ili wanafunzi waweze kusoma katika mazingira rafiki.

PEPFAR YAUPONGEZA MKOA WA TANGA KWA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA VVU

 

 




Na Oscar Assenga, KOROGWE
JUMLA ya vijana 134 wenye umri kati ya miaka 15 hadi 25 wamejiandikisha kwenye kliniki ya tiba na matunzo ya VVU katika Hospitali ya Mji wa Korogwe huku asilimia 90 ya vijana hao wakifanikiwa kufubaza makali ya VVU.

Hayo yalibainishwa wakati wa ziara ya waandishi wa habari mkoani Tanga walipotembelea hospitali ya wilaya ya Korogwe (Magunga)na Kituo cha Afya cha St.Raphael  vinayowezeshwa na Shirika la THPS kupitia Mradi wa Afya Hatua unaofadhiliwa na Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kupambana na UKIMWI (PERFAR), kupitia Kituo cha Kudhibiti  na Kuzuia Magonja cha Marekani (U.S. CDC).

Kwa mujibu wa Kaimu Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI (RACC) mkoani Tanga, Bi. Judith Kazimoto, THPS kupitia mradi wa Afya Hatua, kwakushirikiana na timu za usimamizi wa Afya za Mkoa na Wilaya, wanatekeleza afua mbalimbali za kupambana na VVU, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa huduma rafiki kwa vijana katika vituo 67 vya afya vilivyopo mkoani humo, ikiwemo Hospitali ya Mji wa Korogwe.

Ili kuhakikisha huduma bora za kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, kina mama wajawazito wanaoishi na VVU hupatiwa huduma zote muhimu, na mara baada ya kujifungua, Watoto wao husajiliwa na kuchukuliwa vipimo vya VVU mapema.

Kupitia mradi wa Afya Hatua, watoa huduma katika kituo cha Afya cha St. Raphael huhakikisha usajili wa Watoto hao unafanyika na wanachukuliwa sampuli za damu ili kufanyiwa kipimo cha VVU ndani ya wiki sita baada ya kuzaliwa kwao na kuhakikisha wanapatiwa huduma stahiki.

“Kwa kipindi cha kuanzia Oktoba 2023 hadi Julai 2024, jumla ya wapokea huduma za VVU wajawazito 26 walijifungua katika kituo hicho. Watoto waliozaliwa na kina mama hawa walisajiliwa ndani ya siku saba baada ya kujifungua. Kati ya hao, 24 (93%) walichukuliwa vipimo na wote (100%) na matokeo yalionesha wote walizaliwa bila maambukizi ya VVU”, alisema Bi. Kazimoto.

Katika kipindi cha miaka 21 iliyopita, serikali ya Marekani kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI (PEPFAR) imewekeza zaidi ya dola bilioni 7 nchini Tanzania kwa ajili kukabiliana na janga la VVU. 

Kwa mujibu wa Mratibu wa PEPFAR nchini Tanzania, Bi. Jessica Greene, PEPFAR ilipoanza kazi hapa Tanzania, mwaka 2003, kulikuwa na watu wasiozidi 1,000 tu ambao waliokuwa kwenye matibabu ya VVU.  

“Hivi sasa, PEPFAR inasaidia zaidi ya watu milioni 1.5 waliopo kwenye huduma ya tiba na matunzo.  Vifo vinavyotokana na UKIMWI nchini vimepungua kwa 76% na maambukizi mapya yamepungua kwa 58%, tangu 2003”, alisema Bi. Greene.

Bi. Greene alisema ingawa lengo la kutokomeza VVU/UKIMWI ifikapo mwaka 2030 ni kubwa lakini linaweza kufikiwa. 

“Serikali ya Marekani inajivunia kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika jitihada za kufikia malengo ya UNAIDS 95-95-95 ifikapo mwaka 2025, ambayo yanalenga 95% ya watu wanaoishi na VVU kufahamu hali zao, 95% ya waliogundulika kuwa na VVU wapate matibabu, na 95% ya wale walio kwenye matibabu waweze kufubaza VVU”, alisema. 

 Utafiti wa hivi karibuni wa Athari za VVU Tanzania 2022-2023 (Tanzania HIV Impact Survey 2022-2023) umeonesha kuwa jitihada za kupambana na VVU mkoani Tanga zimefanikisha kufikia viwango vya juu vya kufubaza VVU kwa 93.5%. 

“Tunaupongeza mkoa ya Tanga kwa hatua hii nzuri na tunaamini wataendelea kudumisha mafanikio hayo tunapoelekea kuyafikia malengo ya UNAIDS 95-95-95”, alisema Bi. Greene


Friday, August 30, 2024

RUMBA YA UKWELI KUTOKA KWA WANAMUZIKI WA ZAMANI WALIOTOKA KWA WERRASON

 

 

 - Fabregas le Métis Noir ft. Deplick Pomba - La La La

DC ARUMERU ASISITIZA UHAKIKI KUKAMILISHWA KATIKA HALMASHAURI ZOTE ZA WILAYA HIYO

 

NA MWANDISHI WETU, WHMTH, ARUSHA.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, ameiomba Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kuwezesha zoezi la Uhakiki wa Taarifa za Anwani za Makazi katika Halmashauri ya Meru baada ya kukamilisha zoezi hilo katika Halmashauri nyingine za mkoa wa Arusha.

Mhe. Kaganda amesema hatua hiyo itasaidia mkoa mzima kuwa na takwimu safi za Anwani za Makazi na hivyo kuwezesha masuala yote muhimu yakiwemo ya upangaji wa mipango ya maendeleo kufanyika kwa ufanisi.
Ametoa wito huo tarehe 30 Agosti, 2024 wakati akizungumza na timu ya Wataalamu wa Anwani za Makazi na Mradi wa Tanzania ya Kidigitali iliyo chini ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari waliofika ofisi kwake pamoja na mambo mengine kumpa mrejesho wa zoezi hilo la uhakiki lilivyofanyika katika Halmashauri ya wilaya ya Arusha.

Mhe. Kaganda ametoa msisitizo huo kwa Mratibu wa Anwani za Makazi Taifa Mhandisi Jampyon Mbugi na Mratibu wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali (DTP) Bw. Bakari Mwamgugu kuhakikisha zoezi la uhakiki linafanyika katika Halmashauri ya Meru ikizingatiwa kuwa ni zoezi muhimu kwa Halmashauri.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Seleman Msumi ameipokea timu ya waratibu hao ofisini kwake na kupongeza zoezi la uhakiki lilivyoendeshwa katika Halmashauri yake na kwamba wataendelea kuunga mkono kwa kushirikiana na waratibu wa Wilaya.
Mhandisi Mbugi na Bw. Bakari wakizungumza na viongozi hao kwa nyakati tofauti wameeleza umuhimu wa kuendelea kushirikiana na waratibu wa Wilaya pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa Anwani za Makazi na namna zinavyochangia kukuza uchumi hususan uchumi wa kidijitali.

Zoezi la uhakiki wa taarifa za Anwani za Makazi ni zoezi muhimu linalotekelezwa na Serikali ya Tanzania kupitia Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.

Thursday, August 29, 2024

UWT KIBAHA MJI YATEMA CHECHE KONGAMANO LA KUMPONGEZA RAIS SAMIA

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

 
Umoja wa wanawake Wilaya ya Kibaha mjini (UWT) katika kuunga mkono juhudi zinazofanywa  na Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika  kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo  imeamua kufanya  kongamano kubwa la kumpongeza kwa dhati kutokana na kutenga fedha ambazo zimekwenda kuwasaidia kwa kiasi kikubwa kutekeleza  miradi mbali mbali ya maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza katika kongamano hilo  ambalo limehudhuliwa  na viongozi mbali mbali wa chama  na serikali pamoja na jumuiya zake Mwenyekiti wa UW T Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja amebainisha kwamba lengo lubwa ni kumpongeza Rais  kwa kazi nzuri ambazo amekuwa akizifanya za kuwasaidia wananchi  hususan kumtua mama ndoo kichwani.


"Sisi kama umoja wa wanawake UWT Kibaha mjini tumeungana kwa pamoja na kuandaa kongamano hili kwa lengo kubwa la kumpongeza Rais wetu Mama Samia kwani ameweza kufanya mambo makubwa katika nyanja mbali mbali ikiwemo  kuboresha huduma ya afya, ujenzi wa miundombinu ya barabara, elimu sambamba na kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama ambayo imepelekea kumtua mama ndoo kichwani,"alisema Mgonja.

Mgonja alisema kwamba Rais Samia kwa kipindi chake cha miaka mitatu na nusu tangu alipoingia madarakani ameweza kuendelea kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo  katika Jimbo la Kibaha  pamoja na Mkoa mzima wa Pwani ambayo baadhi yake imeanza kufanya kazi na kuwasaidia wananchi katika maeneo tofauti  sambamba na kuongeza kasi ya kuleta  uchumi.

Katika hatua nyingine hakusita kumshukuru kwa dhati Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka , Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mkurugenzi wa Kibaha mjini, Mlezi wa UWT Selina Koka,Mke wa mbunge wa Jimbo la Mkuranga Mariam Ulega , pamoja na madiwani wote kwa  kushirikiana bega kwa bega katika kuhakikisha kongamano hilo linafanikiwa kwa kiasi kikubwa.



Kwa upande wake Mlezi wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Selina Koka ambaye pia mke wa  Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini amesema kwamba amemshukuru Rais Samia kwa kuweza kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo kwa vitendo katika Jimbo la Kibaha mjini ambayo imeweza kuleta chachu ya kuwasaidia wananchi katika nyanja tofauti tofauti.

Mama Koka amesema kwamba katika Jimbo la Kibaha mjini Rais Samia ameweza kuleta mageuzi makubwa katika  nyanja mbali mbali kwenye kata zipatazo 14  ikiwemo sekta afya, katika kuboresha miundombinu ya zahanati, vituo vya afya, Hospitali, elimu, huduma ya maji safi na salama,nishati ya umeme  pamoja na miundombinu ya barabara.
 
Naye mgeni rasmi katika Kongamano hilo Mariamu Ulega ambaye pia ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Mkuranga amewapongeza wanawake wa UWT kwa kuweza kuandaa kongamano hilo kwa lengo la kumpongeza Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwasaidia wananchi katika mambo mbali mbali ikiwemo kuwasogezea huduma za kijamii ikiwemo vituo vya afya, elimu, maji pamoja na mahitaji mengine.

Aliongeza kwamba wanawake wa UWT wameweza kufanya kitendo cha kiugwana kutokana na kutambua umuhimu na mchango mkubwa ambao ameufanya na Rais Samia katika kutekeleza ilani ya chama kwa vitendo kwa kushirikiana bega kwa bega na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini ikiwemo kutenga fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.



Umoja wa wanawake wa UWT Kibaha mjini katika kongamano hilo limeweza kugusia mambo muhimu ambayo yamefanywa na Rais ikiwemo utoaji wa vifaa vya Tehama,utoaji wa elimu bila malipo,kuboresha fursa za watoto wa kike katika elimu,stahiki za walimu,uboreshaji wa afya, huduma ya maji, pamoja na miundombinu ya barabara.

Wednesday, August 28, 2024

DAWA ZA ASILI ZILIZO HAKIKIWA KUTIBU NGUVU ZA KIUME ZAPAMBA MAONESHO YA TIBA ASILI JIJINI MWANZA

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA

Aneth Chambo ni Meneja Masoko wa Kampuni ya IPhytos Tanzania Co. LTD kutoka jijini Arusha, kampuni inayojihusisha na Utafiti, Uchunguzi wa mimea tiba ambayo ni sahihi kwa utengenezaji wa dawa asili za binadamu ambazo zinatengenezwa kwa njia ya teknolojia ya Sayansi ya Computer. #nguvuzakiume #tibaasili #FurahishaMwanza #mwanza #samiasuluhuhassan

Tuesday, August 27, 2024

Benki ya CRDB, Visa kutoa punguzo la asilimia 22 kwa abiria wa Qatar Airways wanaolipa kwa Tembocard Visa

Dar es Salaam. Tarehe 26 Agosti 2024: Benki ya CRDB kwa kushirikiana na wabia wake wa kimkakati ambao ni kampuni ya Visa International imetangaza kutoa nafuu ya nauli ya asilimia 22 kwa abiria wa Shirika la Ndege la Qatar wanaolipia tiketi zao kwa kutumia kadi za Tembocar Visa. 

 Nafuu hiyo inajumuisha punguzo la asilimia 12 litakalotolewa na kampuni ya Visa International pamoja na asilimia 10 ya fedha taslimu itakayorudishwa kwenye akaunti ya mteja wa Benki ya CRDB baada ya kulipia tiketi yake. 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa wakati wa kuzindua kampeni hiyo itakayodumu kwa miezi sita, Kaimu Mkurugenzi wa Wateja wa Awali na Kati wa Benki ya CRDB, Muhumuliza Buberwa amesema ushirikiano huu unalenga kujunga utamaduni kwa wateja kutumia kadi kufanya malipo na kuachana na matumizi ya fedha taslimu. 

 “Punguzo hili la asilimia 22 ni sehemu ya motisha kwa wateja kujenga utamaduni wa kutumia kadi kufanya malipo. Nitumie nafasi hii kuwakaribisha wateja wetu wanaotaka kusafiri kutumia ndege za Shirika la Ndege la Qatar ili kunufaika na punguzo hili ili. ,” amesema Paul huku akibainisha kuwa punguzo hilo pia linatosha kwa abiria kununua zawadi kwa ajili ya wapendwa wao pindi wawapo safarini.
Kaimu Mkurugenzi huyo amesema ushirikiano wa Benki ya CRDB, Visa International na Shirika la Ndege la Qatar unazijumuisha taasisi mbili kubwa zenye ubora unaotambulika ndani na kimataifa uliozifanya zitunukiwe tuzo za aina tofauti.

Tangu mwanzoni mwa miaka ya 2000, Paul amesema Benki ya CRDB imetunukiwa takriban tuzo 200 a ndani na kimataifa ikiwamo tuzo za utoaji wa huduma bora za Visa, wakati Shirika la Ndege la Qatar likishinda tuzo ya shirika bora la ndege zinatolewa na kampuni ya Skytrax mara nane kati ya mwaka 2011 mpaka mwaka 2024.

 Shirika hilo pia limeshinda tuzo ya shirika lenye daraja bora la biashara duniani (world’s best bisness class), ukumbi bora wa daraja la biashara duniani (world’s best business class lounge) na shirika bora la ndege ukanda wa Mashariki ya Kati.

 “Benki ya CRDB na Shirika la Ndege la Qatar pia tunafanana kwenye ubunifu. Benki yetu ndio kiongozi katika ubunifu wa huduma na bidhaa zinazokidhi mahitaji na matarajio ya wateja wetu vivyo hivyo kwa Shirika la Ndege la Qatar ambalo limeshinda tuzo za kimataifa kutokana na ubunifu wake. Vilevile, sisi sote wawili tunajali na kuyatunza mazingira,” ameeleza Buberwa. 
Meneja Mkazi Shirika la Ndege la Qatar, Isaack Wambua amesema ndege zao zenye makao makuu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad uliopo jijini Doha ambao umeshishinda tuzo ya uwanja bora wa ndege duniani mara tatu kuanzia mwaka 2021, zinatua katika viwanja vingine 170 duniani kote hivyo kuwapa abiria wao uhakika wa kufika popote wapatakapo huku Benki ya CRDB ikiwahakikishia kukamilisha safari zao kwa gharama nafuu. 
 “Punguzo hili la Benki ya CRDB litakalodumu mpaka Desemba mwaka huu, linawahusu wateja wetu wote wanaotumia kadi za Tembocard Visa ambao ni zaidi ya milioni nne.

 Kwa kuwa tunatambua kwamba wanazo biashara nje ya nchi na huwa wanasafiri kwa malengo tofauti, tunaamini wataitumia fursa hii kusafiri na ndege za Shirika la Qatar kwenda wanapopataka,” amesema Wambua.








REA YAMTAKA MWENDELEZAJI WA MRADI WA KUFUA UMEME WA MAGUTA MKOANI IRINGA KUONGEZA KASI


Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Lung'ali Natural Resources Co. Ltd alipotembelea Mradi wa kufua umeme wa Maguta kwa kutumia maporomoko ya maji


Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage akielekeza jambo alipotembelea Mradi wa kufua umeme wa Maguta kwa kutumia maporomoko ya maji.


 Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Lung'ali Natural Resources Co. Ltd alipotembelea Mradi wa kufua umeme wa Maguta kwa kutumia maporomoko ya maji


 Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage (kushoto) akikagua miundombinu ya Bwawa la mradi wa kufua umeme wa Maguta.

 


Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage akielekeza jambo alipotembelea Mradi wa kufua umeme wa Maguta kwa kutumia maporomoko ya maji.


Na Mohamed Saif- Iringa

Serikali imemtaka Mwendelezaji wa Mradi wa kufua umeme kwa kutumia maporomoko ya maji wa Maguta  uliopo katika Kijiji cha Masisiwe Wilayani Kilolo Mkoani Iringa kuukamilisha kwa wakati.

Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage ametoa maelekezo hayo Agosti 26, 2024 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo ambao umefikia asilimia 95.

Mradi unatekelezwa na Mkandarasi ZECO ambaye Makao Makuu yake yapo Nchini Italia. Mwendelezaji ametakiwa kuhakikisha makubaliano ya utekelezaji wa mradi kati yake na  ZECO yanatekelezwa kwa wakati ili mradi ukamike ifikapo Desemba 2024.

"Hatua iliyofikiwa inaridhisha; hakuna kikwazo kinachosababisha mradi uchelewe, Mkandarasi anapaswa kuhakikisha ifikapo Desemba mwaka huu awe amekamilisha na umeme umeingia kwenye Gridi ya Taifa," ameelekeza Mhandisi Advera.

Mhandisi Advera amefafanua kuwa mradi umesanifiwa kuzalisha Megawati 2.4 na kwamba unatekelezwa kwa awamu ambapo awamu ya kwanza inayoendelea hivi sasa itazalisha megawati 1.2.

Amesema licha ya kuongeza umeme kwenye Gridi ya Taifa, mradi utazalisha ajira kwa wananchi wa eneo la mradi, utapunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa, ni rafiki kwa mazingira, utaimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwenye maeneo mengi na hivyo kuleta chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa Kilolo na maeneo mengine.

"Kukamilika kwa mradi huu kutakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa maeneo haya na maeneo mengine pia; umeme ni injini ya uchumi hivyo tunatarajia kuona maendeleo makubwa baada ya kuanza uzalishaji wa umeme," amesema.

Mhandisi Advera amebainisha kuwa mradi unatumia Nishati Safi na Salama kutokana na maporomoko ya maji hivyo ili uwe endelevu ametoa wito kwa kila mwananchi kulinda na kutunza mazingira ya maeneo ya vyanzo vya maji.

"Umeme unaokwenda kuzalishwa hapa ni wa maporomoko ya maji, sasa tusipolinda mazingira yanayozunguka hivi vyanzo vya maji yaani hii Mito tutasababisha mradi ushindwe kutupa matokeo tunayoyatarajia," amesisitiza Mhandisi Advera.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi kwa ujumla, msimamizi wa mradi ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Lung'ali Natural Resources Co. Ltd inayosimamia mradi huo kwa niaba ya Kanisa Katoliki-Parokia ya Jimbo la Iringa, Padri Luciano Mpoma ameishukuru Serikali kwa mchango wake katika kuhakikisha mradi unakamilika.

Amesema mradi unatekelezwa kwa ufadhili wa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuendeleza Mitaji kwa ajili ya Maendeleo (UNCDF).

"REA imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mradi unafanikiwa na unaleta manufaa yanayokusudiwa. Mara zote wamefika hapa kukagua na kutushauri tunawashukuru sana," amepongeza.

Miongoni mwa majukumu ya msingi ya REA ni pamoja na kuwezesha ujenzi wa miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia nishati Jadidifu ambayo ni Nishati Safi na Salama.