ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, August 25, 2022

JAPAN: MKUU WA POLISI AJIUZULU KUTOKANA NA KIFO CHA SHINZO ABE


Itaru Nakamura amesema ameamua kuwajibika juu ya dosari za Usalama ambazo uchunguzi ulionesha Jeshi halikumlinda ipasavyo Waziri Mkuu wa zamani, Shinzo Abe aliyeuawa Julai 8, 2022

-
Taarifa hiyo inakuja wakati ripoti ya Uchunguzi iliyotolewa leo ikionesha kulikuwa na udhaifu mkubwa ndani ya Jeshi la Polisi juu ya kupanga ulinzi katika eneo ambalo Abe alishambuliwa
-
Ingawa Nakamura hajasema ni lini ataondoka Ofisini, ombi la kujiuzulu kwake linatarajiwa kuidhinishwa katika mkutano wa Baraza la Mawaziri Agosti 26, 2022.

WABUNGE WAPYA KENYA KUFIKA BUNGENI KWA ZIARA YA UTAMBULISHO KABLA YA VIKAO KUANZA.

Wabunge wapya waliochaguliwa kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9 wanatazamiwa kupata mwelekeo wa Bunge kabla ya kufunguliwa tena kwa bunge mwezi ujao. Wabunge wakijadili hoja katika Bunge la Kitaifa Kenya. 

 UGC Katika notisi, karani wa Bunge la Kitaifa Serah Kioko alifahamisha wabunge hao kwamba ziara ya utambulisho itafanika leo na kesho. 

Vikao elekezi vitajumuisha usajili wa Wanachama, ukusanyaji wa taarifa za bio-data, utoaji wa vitambulisho vya ubunge, kutoa taarifa kuhusu matumizi ya mfumo wa upigaji kura bungeni. 

Katibu wa Bunge alisema kuwa itahusisha pia ziara ya Majengo ya Bunge na maelezo mafupi ya Ofisi ya Karani kuhusu mambo muhimu ya kisheria, pamoja na mambo mengine. 

Kioko alidokeza kuwa Wabunge Wateule watafahamishwa mara tu Rais Uhuru Kenyatta atakapotangaza tarehe watakayokutana kwa kikao cha kwanza. 

Watatembezwa kwenye Majengo ya Bunge na pia watapewa taarifa pamoja na mambo mengine huduma na vifaa vinavyopatikana kwa ajili ya Wajumbe. 

Wabunge wapya pia watawezeshwa kujiandikisha kwa huduma na vifaa ikiwa ni pamoja na bima ya matibabu na huduma zingine zinazohusiana. 

Wednesday, August 24, 2022

FCC YAWAPIGA MSASA WADAU WA KAHAWA MKOANI KAGERA

NA ALBERT G.SENGO. Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Albert Chalamila ametoa maelekezo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Kagera kubaini vikundi au makundi yanayojihusisha na uzalishaji mali vinavyohudumiwa na Serikali ili kulinda bidhaa ya Mtumiaji wa kahawa. Mhe. Albert Chalamila ametoa maelekezo hayo wakati akifungua semina ya masuala ya Ushindani na Udhibiti wa bidhaa bandia kwa wadau wa Sekta ya Kahawa Mkoani Kagera, Semina hiyo iliyoandaliwa na FCC imefanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera ikivijumuisha vyama vya ushirika vya vya wakulima na wazalishaji wa zao Kahawa Wilayani Karagwe na Mkoani Kagera (KDCU na KCU) ikiwa ni pamoja na wakulima, wazalishaji na wadau wa zao hilo kwa ujumla. " Tunazungumzia kahawa ya hapa kwetu Kagera yenye ubora mzuri lakini michakato ya kuivuna na maandalizi ya kupata zao lenyewe bado inatumia mchakato wa kizamani na kufanya watumiaji kuacha kahawa yetu na kutumia kahawa nyingine" amesema Mhe. Chalamila.

WALIO LALA GESTI, MAHOTELI, WATOTO WA MITAANI NA WAKAZI KIRUMBA WAHESABIWA

 

 

NA ALBERT G. SENGO
Kirumba ni moja ya kata zenye mishemishe na pilika pilika nyingi jijini Mwanza.

Mbali ya kuwa na soko kubwa la Kimataifa la Biashara ya Samaki lililopo Mwaloni, pia katika kata hiyo kuna jengo kubwa la kisasa la biashara lenye maduka ya huduma mbalimbali kubwa na ndogo ndogo nazungumzia Rock City Mall, ambapo humo ndimo kuna ile bar maarufu ya burudani na vyakula vya kitalii The Cask Bar and Grill.

Uwanja maarufu Afrika Mashariki uliochukuwa jina la kata hiyo (Kirumba Stadium) unapatikana Kirumba.

Kata ya Kirumba pia ni maarufu kwa huduma za Gesti, Hotels na chocho za mengineyo yanayowafanya watu kukesha. 

SENSA iliyoanza usiku wa saa 6:01 kuamkia Tarehe 23 imegusa vipi maeneo hayo...?

"NDIYO MAANA HUFANIKIWI": PASTA AWAONYA WANAUME DHIDI YA KURAMBA NYETI ZA WANAWAKE.


Mchungaji mmoja kutoka nchini Nigeria Ebuka Obinna amewasuta wanaume wanaolamba sehemu za siri za wanawake kuthibitisha kuwa wanawapenda. 

Mchungaji Ebuka Obinna alisema wanaume wengi wanaopenda kuramba nyeti za wanawake hawafanikiwe. 

 Pasta huyo alifedheheshwa na kitendo hicho na kudai kuwa ndiyo sababu vijana wengi hawaoni mwanga maishani. 

Kulingana na Ebuka, kuweka mdomo katika sehemu ya siri ya mwanamke kunaweza kumleta bahati mbaya mwanamume na watoto wake endapo akajaaliwa.

 "Acha kuweka mdomo wako kwenye sehemu ya siri ya mwanamke, unataka kufanikiwa vipi, kinywa hicho hicho, ambapo biblia inasema nguvu ya uzima na mauti iko kwenye ulimi wako, unabeba mdomo wako na kuusimika ndani ya sehemu ya siri ya mwanamke. 

 "Angalia wavulana wanaopenda kufanya hivyo, laana ndogo ndogo huwafwata. Kutoka mahali mwanamke anavuja damu, akiona hedhi yake ya kila mwezi, unaweka mdomo wako kwa madai ya 'kuthibitisha kwamba unapenda' aibu kwako!" Alisema. Mhubiri huyo alibainisha kuwa kitendo hicho ni kinyume cha maadili na ndiyo sababu ya baadhi ya vijana hawana pesa. 

"Ndio maana hupati pesa. Kuanzia wakati huo, ulimi wako umechafuliwa. Kuweka mdomo kwenye sehemu ya siri ya mwanamke kunaweza kuletea masaibu mabaya," aliongeza. Katika makala mengine tofauti, mhubiri alizua ucheshi miongoni mwa wanamitandao, baada ya kufoka kwa nguvu akiwahubiria kina dada, na kuwaonya dhidi ya kukubali kuolewa na wanaume waliofuga nywele za rasta. 

Pasta huyo alionekana kumlenga mwanamume mwenye 'dreadlocks' aliyepita kando yake akihubiri, akiwa amendamana na kipusa alishangiliwa na wafuasi wake kwa kusema hivyo. "Wacha nirudie tena nyinyi wasichana musiolewe na marasta. Marasta hawafanyangi kazi ni majamaa ya kuzunguka akiuliza wasichana unanipenda... Usiolewe na rasta, kataeni marasta," mtumishi huyo alisema. 

TUME YA UCHAGUZI KENYA KUPELEKA USHAHIDI MAHAKAMANI.


 Tume ya Taifa ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ya Kenya, leo mchana Agosti 24, 2022 inatarajia kufikisha vielelezo vya fomu namba 34 ambazo zilitumika kwenye uchaguzi.

Fomu namba 34A, 34B na 34C zilitumika kwenye Uchaguzi Mkuu wa Kenya uliofanyika Agosti 9, 2022 kwa ajili ya kurekodi matokeo ya urais, ubunge na ugavana wa kila kituo nchini humo.

Tume ambayo kwa sasa imekuwa kwenye mgogoro wa ndani tangu makamishna wanne wakiongozwa na Naibu Mwenyekiti Juliana Cherera kujitoa kuhusika na matokeo yaliyotangazwa Agosti 15,2022 na Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati ambayo yalimpa ushindi wa urais William Ruto aliyepata kura milioni 7.1 dhidi ya kura milioni 6.9 alizopata Raila Odinga.

Mara baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Odinga aliyapinga akidai kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi zilizofanywa na Chebukati huku akiwataka wafuasi wake watulie kwa kuwa tafuata mfumo wa kisheria kudai haki.

Odinga amefungua kesi ya kupinga ushindi wa Ruto katika Mahakama ya Juu ya Milimani ambako shauri hilo linaendelea na kama mahakama ikithibitisha kulikuwa na ukiukaji wa taratibu inaweza kufuta matokeo ya urais.

Hii ni mara ya pili kwa Odinga kwenda mahakamani kupinga matokeo ya urais ambapo mwaka 2017 alifanya hivyo na mahakama ilifuta matokeo yaliyompa ushindi Rais Uhuru Kenyatta na kuagiza IEBC iitishe uchaguzi mwingine wa urais.

Tuesday, August 23, 2022

MBUNGE KOKA ASHIRIKI ZOEZI LA SENSA NA MKEWE NYUMBANI KIBAHA

  Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka akiwa pamoja na mke wake Selina Koka nyumbani kwao mtaa wa Vigaeni Wilayani Kibaha na Kalani wa sensa na mjumbe wa shina la Mkoani 'A'

Na Victor Masangu,Kibaha

Mbunge wa Jimbo la  Kibaha .mjini Silvestry Koka leo mapema akiwa na  mke wake Selina Koka  wameshiriki kikamilifu zoezi la Kuhesabiwa huku akiwasisitiza wananchi wa Jimbo lake kutoa ushirikiano kwa mawakala wa Sensa ambao wanapita kwa lengo la kujua taarifa mbali mbali ambazo zinawahusu wananchi.


Koka ameshiriki kuhesabiwa zoezi hilo la sensa ya watu na makazi akiwa na mke wake nyumbani kwao katika mtaa wa Vigaeni kata ya Tumbi Wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani Sambamba akiwa na familia yake.


Mbunge huyo baada ya kuhesabiwa alisema kwamba zoezi hilo limefanyika salama na kubainisha kuwa taarifa zote ambazo ameulizwa ameweza kuzijibu ipasavyo kwa kalani wa sensa ambaye alifika nyumbani kwake kwa lengo la kufanya zoezi hilo.


"Tunashukuru zoezi hili limefanyika vizuri na mm nimeweza kupata fursa ya kuweza kuhesabiwa nikiwa pamoja na mke wangu na familia yangu na kikubwa naweza kusema zoezi kimemalizika salama na tumetoa ushirikiano wa kutosha katika zoezi hili,"alisema Koka.


Pia Mbunge huyo alibainisha kuwa umuhimu wa zoezi hilo la kuhesabiwa kutaweza kuisaidia serikali kupata takwimu halisi ya wananchi wake lengo ikiwa ni kuweka mipango madhubuti kwa ajili ya kuleta maendeleo.


Kadhalika Koka alimpomgeza Rais wa Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuleta chachu ya maendeleo katika sekta mbali mbali ikiwemo Sambamba na kuwahimiza wananchi kujitokeza katika suala zima la kuhesabiwa.


Naye mmoja wa makalani wa zoezi hilo la sensa Mariam Mohamed amesema kuwa zoezi hilo limeanza tangu asubuhi japo kulikuwa na changamoto ya mvua lakini wananchi wamekuwa na hamasa katika kuhesabiwa.


"Zoezi la sensa ya watu na makazi tumelianz mapema ya asubuhi na tumepita katika maeneo mbali mbali ikiwemo kwa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini ambaye tumemkuta nyumbani kwaki mtaa wa Vigaeni akiwa pamoja na mke wake na ametupa ushirikiano wa kutosha,"alisema Kalani huyo.


Katika hatua nyingine mke wa Mbunge huyo Selina  Koka ameeleza kuwa ameshiriki kikamilifu katika kuhesabiwa na kwamba zoezi hilo limekwenda vizuri na wamehesabiwa yeye pamoja na familia yake.


Pia mama Koka alisema kwamba matarajio yake makubwa katika zoezi hilo la sensa ni kuwa litaweza kusaidia katika kufahamu idadi ya wananchi ili serikali iweze kupanga mambo yake ya kimaendeleo


Mjumbe wa shina namba tatu kutoka mkoani 'A' Jestina Lewis alisema kwamba wananchi wa Jimbo la Kibaha wameonekana kutoa ushirikiano wa kutosha kwa makalani ambao wamekuwa wakipita katika maeneo mbali mbali.


Kadhalika amemshukuru Mbunge wa Jimbo kwa kuweza kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo Sambamba wa kuwahimiza wananchi wake kuweza kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo.


Katika Jimbo la Kibaha mjini pamoja na maeneo mengine ya Wilayani Kibaha wananchi wake tangu asubuhi wameonekana kuhamasika katika kushiriki katika zoezi hilo la sensa ya watu na makazi.

DC JERRY MURO AHESABIWA

Mkuu wa wilaya ya Ikungi Mhe. Jerry C. Muro ameshiriki zoezi la sensa ya watu na makazi kwa kuhesabiwa akiwa katika makazi yake ikungi singida 


Zoezi la kuhesabiwa limeongozwa na  karani wa sensa ya watu na makazi Bi. Scovia mkempia deus akiwa pamoja na mwenyekiti wa kitongoji cha gairo kijiji cha ikungi Bw. Justin juma mghwai 



Dc Muro ametimiza takwa la kisheria la kuhesabiwa na ametoa ushirikiano kwa kujibu maswali yote 100 ipasavyo na watu wa kaya yake


Dc Muro pia amewapongeza sana waratibu na wasimamizi wa zoezi hilo wakiwemo karani na mwenyekiti kwakufanya kazi yao kwa uadilifu na umakini mkubwa uku wakiwa wakarimu na waungwana katika uulizaji wa maswali 


Dc Muro ametoa rai kwa wananchi wote wa ikungi kuendelea kuwapokea na kuwapa ushirikiano wa kutosha makarani wetu wa sensa ili waweze kuifanya kazi hii kwa uaminifu na uadilifu mkubwa katika zoezi hili la sensa ya watu na makazi 2022

Monday, August 22, 2022

TIMU YA NEWS GENERATION YATWAA UBINGWA SAMIA SULUHU CUP KIBAHA.

 


Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Sarah Msafiri akimkabidhi nahodha wa timu ya New generation  kombe baada ya kuutwa ubingwa huo.

Na Victor Masangu,Kibaha

Timu ya soka ya New generation Leo imeweza kuibuka kidedea kwa kuutwa ubingwa wa michuano ya kombe la 'Samia Suluhu Cup' baada ya kuichapa timu ya Palasupalasu kwa mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa katika dimba la mwendapole Wilayani Kibaha.


Katika mchezo huo wa fainali ambao ulikuwa wa vuta ni kuvute kutokana na timu zote mbili kuonyesha kandanda la aina yake katika kipindi chote cha dakika 90 na kuhudhuliwa na umati wa mashabiki kutoka maeneo mbali mbali ya Wilaya ya Kibaha na maeneo mengine ya jirani.


Mchezo huo ambao ulikuwa unasubiliwa kwa hamu na shauku kubwa na wapenzi wa mpira wa kandanda ulihudhuliwa pia na viongozi mbali mbali wa dini,serikali,pamoja na wadau wa viongozi wa chama Cha mpira wa miguu wilaya ya Kibaha (KIBAFA)


Mabingwa katika mchezo huo ndio waliokuwa wa kwanza kuzifumania nyavu za wapinzani wao katika kipindi Cha kwanza ambapo bao lao la kwanza lilifungwa kwa njia ya kawaida na bao la pili lilifungwa kwa njia ya mkwaju wa penati.


Katika kipindi c ha pili wapinzani wao waliweza kupata bao la kufutia machozi ambalo lilipatikana kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji wao kufanyiwa madhambi katika eneo la hatari.


Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Sarah Msafiri ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika kilele Cha michuano hiyo ambapo alisema lengo kubwa ya kuandaa mashindano hayo kupitia sekta ya michezo ni kwa ajili ya kuhamasisha zoezi la sensa ya watu na makazi.


"Tunashukuru mashindano haya ya Samia Suluhu Cup' katika Wilaya yangu ya Kibaha yamemalizika salama na kikubwa ilikuwa ni kuwakutanisha wanamichezo kuwahamasisha kushiriki katika sensa na tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa ,"alisema Msafiri.


Aidha Mkuu huyo alisema kwamba katika michuano hiyo imeweza kusaidia kwa kiasi kubwa tangu ilipoanza kufanyika na imeleta matokeo chanya katika kuwaimisha wananchi na wanamichezo umuhimu wa kuhesabiwa katika sensa.


Msafiri aliwapongeza wachezaji wa timu mbali mbali ambao wameweza kujitokeza katika mashindano hayo ya Samia Suluhu Cup' na kwamba yatakuwa yanafanyika kila mwaka lengo ikiwa pia ni kukuza vipajj.


Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya mji Kibaha Injinia Mshamu Munde amebainisha kwamba Maandalizi yote kwa ajili ya sensa yanaendelea vizuri na kwamba hamasa na mwamko kwa wananchi no mkubwa.


Munde aliongeza kuwa mashindano ya michezo ambayo yameandaliwa maalumu kwa ajili ya kuhamasisha sensa ya watu na makazi yameleta matokeo chanya katika suala zima la kuwapa fursa wanamichezo kutambua umuhimu wa kuhesabiwa.


Kivumbi Cha michuano hiyo Cha kombe la Samia Suluhu Hassan kimemalizika ambapo timu za soka kuanzia mshindi wa kwanza hadi mshindi wa nne zimeoatiwa zawadi mbali mbali ikiwemo mipira,jezi, medani pamoj vikombe.

WAZIRI JAFO AWAHIMIZA WANANCHI KUJITOKEZA KATIKA SENSA.

 Waziri Selemani Jafo akizungumza Wilayani Kisarawe wakati wa zoezi maalumu kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kushiriki katika sensa ya watu na makazi.

 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge akizungumza na wananchi juu ya umuhimu wa kuhesabiwa katika sensa.


Na Victor Masangu,Pwani

MJUMBE  wa Kamati ya Sensa kitaifa  na Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira  Dk Selemani Jafo amewataka wananchi kutowabughudhi makarani wa sensa na badala yake kuwapa ushirikiano wafanikishe shughuli hiyo 


Aidha Dk Jafo amesema kamati imeridhika na maandalizi ambayo yamefanyika kwa makarani na vifaa vinavyohitaji.


Dk Jafo aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza kwenye Tamasha la sensa lililoandaliwa na mkoa wa Pwani kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhesabiwa ambalo limefanyika Kisarawe.


Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kisarawe alisema makarani wa sensa wananchi wanatakiwa kutoa ushirikiano kwa kuwapa taarifa zinazotakiwa makarani wa sensa badala ya kuwabughughi.


" Tuwape ushirikiano kwa kila wanachohitaji tusipowqpa ushirikiano itakuwa haina maana kutokana na maandalizi yaliyofanyika katika shughuli hii ya sensa, na tutambue kujua idadi itarahisisha serikali katika kwenye utekelezaji wa miradi" alisema


Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakari  Kunenge  ametoa onyo kwa wanaotaka kutumia sensa kuhalifu kwamba watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.


Kunenge alisema hali ya usalama imeimarishwa hivyo wananchi waondoe hofu kwani yeyote atakayejaribu kuharibu shughuli ya sensa  hatua zitachukuliwa.


Kwa mujibu wa Kunenge maandalizi ya mkoa huo yamefikia asilimia 96, na uhamasishaji umefanyika kwa njia tofauti ikiwemo ya michezo na matamasha mbalimbali kwenye wilaya za mkoa huo.


ONYO KWA WATAKAOKWAMISHA ZOEZI LA SENSA

 DC Ilemela, Waziri Mabula wafunguka.

Saa zinahesabika kufikia siku ya SENSA ya Tanzania 2022.

Siku nne kabla yaani Ijumaa ya tarehe 19 Agosti Mkuu wa wilaya ya Ilemela pamoja na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula walikutana na wenyeviti wa kata mbalimbali za wilaya ya Ilemela nia ni kutia msisitizo wa mwisho na kukazia elimu ya SENSA iliyotolewa kwa vipindi tofauti.

#SENSA #mwanza #SENSABIKA