ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, December 11, 2021

VIKOSI:- SIMBA V/s YANGA TAREHE 11/12/2021

 

PABLO Franco, Kocha Mkuu wa Simba anatarajiwa kukiongoza kikosi chake leo kwenye mchezo wa dabi dhidi ya Yanga.

Hiki hapa kikosi chake rasmi ambacho kitaanza Uwanja wa Mkapa:-

Aish Manula

Shomar Kapombe

Hussein

Onyango Joash

Mkude Jonas

Kibu Dennis

Kanoute

Kagere

Morrison

Hassan Dilunga

 

Akiba

Kakolanya

Israel

Kennedy

Nyoni Erasto

Mzamiru

Banda

Bocco

Bwalya

Mhilu

LEO ni Desemba 11,2021 saa 11:00 jioni mchezo wa ligi kati ya Simba na Yanga unatarajiwa kuchezwa.

Hiki hapa kikosi cha Yanga ambacho kinatarajiwa kuanza:-

Diarra Djigui

Djuma Shaban

Dickson Job

Kibwana Shomari

Bakari Mwamnyeto

Jesus Moloko

Bangala Yannick

Aucho Khalid

Feisal Salum

Fiston Mayele

Said Ntibanzokiza

Akiba
Johora
Yassin
Bryson
Mauya
Makambo
Kaseke
Yusuf
Farid

Friday, December 10, 2021

MHE. RAIS SAMIA NA MHE. RAIS KENYATA WAKIZUNGUMZA NA VYOMBO VYA HABARI

 Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Uhuru Muigai Kenyatta wakizungumza na vyombo vya Habari na kushuhudia utiaji wa Saini wa Hati za Makubaliano na Ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Kenya leo tarehe 10 Desemba, 2021 katika viwanja vya Ikulu, Jijini Dar es Salaam

MRADI WA JNHPP KUTEKELEZWA KWA WELEDI, UFANISI, WAKATI NA GHARAMA ZILIZOPANGWA – WAZIRI MAKAMBA

 

Na Dorina G. Makaya – Rufiji, Pwani.

Waziri wa Nishati Mhe. January Yusuf Makamba amesema Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la kuzalisha umeme wa  maji la Julius Nyerere (JNHPP) unatekelezwa kwa weledi, ufanisi, wakati na gharama zilizopangwa

Waziri Makamba ameyasema hayo tarehe 07 Novemba 2021, akiwa kwenye ziara ya kikazi na Waziri wa Nyumba, Huduma na Makazi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri Mhe. Mhandisi Assem Hafez El Gazar walipotembelea Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere (JNHPP)  tarehe 07 Desemba, 2021.


Ameeleza zaidi kuwa, Serikali kupitia Wizara ya nishati inasimamia mradi huo mkubwa wa Ujenzi wa Bwawa la kuzalisha umeme wa maji la Julius (JNHPP) na kuwa mradi huo unagharamiwa kwa fedha za Watanzania shilingi trilioni 6.558 na utazalisha umeme wa Megawatt 2,115.

Waziri Makamba pia amekumbushia kuwa, Ujenzi wa Bwawa la kuzalisha umeme wa  maji la Julius Nyerere (JNHPP),  ni muhimu na ni mradi mkubwa wa kimkakati kwa nchi yetu. “Sisi kama wasimamizi tumepewa jukumu na Rais wetu Mhe Samia Suluhu Hassan la kuhakikisha kwamba mradi huu unatekelezwa kwa weledi, ufanisi, wakati na gharama zilizopangwa” alisema Waziri Makamba.



Alikumbushia kuwa, wakandarasi wa mradi huu wametoka katika nchi ya Misri na kuwa ziara hiyo ya Waziri wa Nyumba, Huduma na Makazi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri Mhe. Mhandisii Assem Hafez El Gazar, aliyepewa dhamana ya kusimamia Ujenzi wa Bwawa la kuzalisha umeme wa maji la Julius (JNHPP), inaonyesha namna ambavyo Serikali ya Jamhuri ya Kiarabu ya Misri ilivyochukulia kwa uzito wa hali ya juu katika kuhakikisha kwamba Mradi unatekelezwa kwa weledi, ufanisi, wakati na gharama zilizopangwa


“Tumekuja hapa leo kukagua maendeleo ya mradi, kuangalia tulipofikia, kuangalia kama kuna changamoto kwa upande wa Serikali ya Tanzania na Serikali ya Misri ili tuweze kutatua na kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huu.” Alisema Waziri Makamba.




Waziri January Makamba amesema, baada ya kutembelea mradi, wameona mradi unaendelea vizuri pamoja na changamoto chache zilizopo za Mradi kutokwenda kwa kasi kama iliyokuwa imepangwa. Lakini, alieleza kuwa si jambo la ajabu kutokea kwa miradi mikubwa kama huo kuchelewa kukamilika.

Amesema, jambo jema ni kuwa, mradi uko katika hatua nzuri ya utekelezaji na iwapo italazimu kuongeza muda basi utakuwa ni muda unaokubalika na hakutakuwa na gharama za ziada.

“Sisi tumepewa kazi ya kuhakikisha kwamba mradi unatekelezwa na kukamilika kwa kuzingatia usalama na ubora na kutuhakikishia upatikanaji wa umeme wa uhakika. alisisitiza Waziri Makamba.

Waziri Makamba ameeleza zaidi kuwa, Wizara ya Nishati ingependa pakiwa na changamoto zo zote basi zijadiliwe kidugu kwa kuzingatia matarajio ya viongozi wakuu. wa nchi zote mbili pasipo kuviziana, kushtakiana na kuingiza madai ya kisheria na kuwa  nia iwe kumaliza tofauti ndogo ndogo zozote zilizopo kwa maelewano.

Nae Waziri wa Nyumba, Huduma na Makazi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mhe. Mhandisi Assem Hafez El Gazar amesema, Mradi wa JNHPP ni muhimu sana kwa nchi zote mbili za Tanzania na Jamhuri ya Kiarabu ya Misri.


Amebainisha kuwa, wakati alipoteuliwa kushika nafasi hiyo ya Uwaziri wa Nyumba, Huduma na Makazi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, maelekezo ya kwanza aliyopewa na Raisi Al Sisi ni kusimamia utekelezaji wa Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere (JNHPP)

Waziri El Gazar ameuelezea Mradi wa Kufua Umeme wa Maji wa Julius Nyerere (JNHPP) kuwa ni mradi utakaosaidia kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizo mbili na kuwa, ukitekelezwa vizuri utajenga imani kwa watanzania kuwa. Jamhuri ya Kiarabu ya Misri ni nchi yenye uwezo wa kutekeleza miradi mingine mikubwa ambayo Tanzania itatazamia kuijenga baadaye.

Aidha, Waziri huyo wa Nyumba, Huduma na Makazi wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri Mhe. Mhandisi Assem Hafez El Gazar, amewataka wakandarasi wajitahidi kukamilisha mradi huo kwa wakati na ubora unaokubalika. 


BREAKING NEWS: ASKARI AUA MWENZAKE KWA RISASI KISA PIKIPIKI

 


Askari wa jeshi la polisi aliyetambulika kwa jina la PC Joseph amemuua askari mwenzake Onesmo Joseph wakiwa kwenye kazi ya kulinda tawi la benki ya CRDB wilayani Ruangwa mkoani Lindi.

Kamanda wa polisi mkoani Lindi, Mtatiro Kitinkwi amesema askari hao walikuwa wakigombania pikipiki na tayari PC Joseph amefutwa kazi na atafikishwa mahakamni muda wowote kuanzia sasa.

MAKUMI YA WAFUNGWA WATOROKA GEREZANI DR Congo

 


Makumi ya wafungwa kutoka gereza la Boma magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wametoroka.


Wafungwa hao walitumia fursa ya muziki wa sauti ya juu uliokuwa ukipigwa katika eneo la mazishi ili kuwavuruga walinzi.


Wafungwa tisa walikamatwa karibu na gereza hilo na mmoja kujeruhiwa wakati walinzi wakifyatua risasi hewani, Radio Okapi iliripoti.


Wafungwa wengine 19 bado wako hawajapatikana, kulingana na redio hiyo. Gereza la Boma hapo awali lilikuwa na matukio ya utoro wa wafungwa.


Wenyeji wanasema gereza hilo linahitaji kufanyiwa marekebisho kama lilijengwa miaka ya 1900.

RAILA ODINGA KUTANGAZA IWAPO ATAWANIA URAIS 2022

 Aliyekuwa waziri mkuu nchini Kenya Raila Odinga hii leo anatarajiwa kuzindua azma yake ya urais katika uchaguzi mkuu wa 2022.


Raila ambaye atakuwa anawania wadhfa huo kwa mara ya tano, anatarajiwa kutoa uamuzi wake iwapo atajibwaga katika kinyanganyiro hicho katika sherehe kubwa inayofanyika katika uwanja wa Kasarani.


Baadhi ya viongozi wa kimataifa wakiwemo wale walioteuliwa humu nchini wanatarajiwa kushiriki katika hafla hiyo itakayoshuhudiwa na maelfu ya Wakenya waliosafiri hapo jana kutoka maeneo mbalimbali nchini.



Azma ya Raila kutangaza kuhusu kuwania uchaguzi inajiri baada ya kupata uungwaji mkono kutoka kwa viongozi na wafanyabiashara wa eneo la mlima Kenya – eneo ambalo rais Uhuru Kenyatta anatoka.


Hatahivyo baadhi ya viongozi walioshirikiana naye katika muungano wa Nasa katika uchaguzi mkuu uliopita huenda wasihudhurie hafla hiyo licha ya kualikwa.


Huku baadhi yao wakitofautiana naye kisiasa , wengine wamejipata katika shughuli za kitaifa katika mataifa ya kigeni.


Hii leo kuanzia mwendo wa saa moja uwanja wa kitiafa wa kasarani jijini Nairobi umekuwa eneo la shughuli nyingi baada ya wafuasi wa chama cha ODM nchini Kenya kuwasili katika uwanja huo tayari kwa mkutano huo wa Azimio la Umoja.

MADUKA YA DAWA MARUFUKU KUWEKA MATANGAZO YA USHAURI NASAHA- SERIKALI


 Bi Elisabeth Shekalaghe, akitoa taarifa mbele ya waandishi wa habari jiji Dodoma


Baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa wanafatilia taarifa iliyotolewa na Msajili wa baraza la Famasi nchini, Bi Elizabeth Shekalaghe

Bi Elisabeth Shekalaghe, akitoa taarifa mbele ya waandishi wa habari jiji Dodoma

Na Atley Kuni, WAMJW- DODOMA

 

Serikali imepiga marufuku kuweka matangazo ya ushauri nasaha kwenye maduka ya uuzaji wa dawa za binadamu kwani ni kinyume na kifungu namba 34 (c) kinacho simamia usajili wa maduka.

 

Akiongea na waandishi wa Habari leo jijini Dodoma, Msajili wa Baraza la Famasi Bi. Elizabeth Shekalaghe amesema maduka ya dawa sio hospitali hivyo kuweka matangazo ya kutoa ushauri wa kitabibu ni kukiuka taratibu za vibali vya usajili wa maduka hayo.

 

“Nitoe wito kwa watu wote wenye maduka ya dawa, ni marufuku kuweka matangazo ya kujinadi kwamba unatoa ushauri nasaha na picha ya Daktari umeiweka hapo ukutani, nirudia kusema, kawaambieni hili halikubaliki na yeyote atakaye kwenda kinyume na utaratibu uliowekwa kwenye maduka ya dawa Sheria itachukua mkondo wake”. Amesema Shekalaghe.

 

Bi. Shekalaghe, ameonya pia wale wote wanaoendesha maduka ya dawa bila kujisajili (Maduka bubu), ambapo amesema katika siku za hivi karibuni kumeibuka tabia ya baadhi ya wenye maduka ya dawa wasio waaminifu kwenda kinyume na seria na kujianzishia maduka bila kufuata utaratibu wa usajili, kufanya hivyo ni kosa kisheria.

 

amewaomba wananchi kutoa ushirikiano pindi waonapobaini biashara duka la dawa inaendeshwa kwa kuuza dawa bila ya kuwa na usajili wala kuwa na Nembo ya Msajili ambayo kimsingi inapaswa kubandikwa kwenye duka husika.

 

Shekalaghe amewakumbusha wananchi faida za matumizi sahihi ya dawa ambayo yanaweza kupunguza uwezekano wa kujenga usugu kwa vimelea vya magonjwa, kupunguza madhara/ maudhi ya dawa na hupunguza gharama za matibabu kwa mgonjwa na Serikali.

 

Baraza la Famasi ni taasisi ya Serikali iliyo chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, iliyoundwa na Sheria Na.1 ya Famasi Sura 311 ikiwa na jukumu kubwa la kusimamia taaluma ya famasi nchini, hususani usajili wa wanataaluma wa fani ya famasi na kusimamia utendaji wao, usajili wa majengo yanayotoa huduma za dawa pamoja na utambuzi wa vyuo vinavyofundisha fani ya famasi.


Thursday, December 9, 2021

VIKOSI MBALIMBALI VYA JESHI KATIIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 60 Ya UHURU WA TANZANIA BARA

 










Vikosi mbalimbali vya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ vikipita Kikakamavu mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika Sherehe zilizofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam leo tarehe 9 Desemba, 2021. PICHA NA ISSA MICHUZI.

MABULA APONGEZWA NA WANANCHI WA MGOGORO WA NYANDOTO KWA KUWASAIDIA.


Wananchi waathirika wa mgogoro wa maeneo ya Nyandoto wamemwagia sifa Naibu waziri nyumba maendeleo na makazi,Angelina Mabula kwa kuingila kati mgogoro wao baina ya halmashauri ya mji wa Tarime.

Mgogoro huo umeendelea kufukuta licha ya kuwa Naibu huyo aliutolea majibu pindi wananchi hao walipofika Mjini Musoma Agost mwaka 2020 akiwa katika ziara ya kikazi na kumtaka kuwasaidia ambapo alisema nimesikiliza pande zote mbili nimegundua kuwa halmashauri ilipima maeneo hayo bila kuwashirikisha walengwa.


 

Katika mazungumzo hayo na Wananchi hao Mabula aliongeza kuwa baada ya kuwasikiliza,natoa maelekezo halmashauri irudi ipime maeneo hayo upya kwa upimaji shirikishi kwa kutumia wataalamu wa serikali na wananchi wa maeneo hayo wapewe kipaumbele kulipia gharama za upimaji na atakaye shindwa kulipia hatua zaidi zitachukuliwa.


Mmoja wa wananchi hao,Anna Nguru alisema kwenye mkutano wa hadhara uliowashirikisha watu wa halmadshauri na Polisi kuwa wahanga hao walienda Musoma kumuona Naibu waziri akiwa katika ziara ya kikazi walipofika na kutoa kilio chao,Mabula aliwasikiliza na kutoa majibu,baya hapo akawaahidi kwenda kuongea na watu wahalmashauri ya Mji wa Tarime na kuwapa maelekezo hayo  aliyoyatoa cha ajabu agizo halikutekelezwa ambapo watu wa halmashauri walidai kuwa Naibu huyo kama aliwarudishia maeneo yao ingebidi awape barua kama sivyo  wanaendelea na mchakato wao wa awali wa kugawa viwanja kwa atakaye hitaji kununua.


Neema Timothy aliuliza swali la kutaka kujua kama kweli halmashauri inadai maeneo niyao kwasababu gani wanakuja na dola kwa maana ya polisi wakiwa na silaha wakati wa zoezi la kugawa viwanja na kwenye mikutano ya wananchi wanahofu gani na mali niyao.


Pia Neema aliongeza kuwa kama halmashauri inadai Naibu waziri aliwapa barua ya maelekezo tofauti na walioambiwa mkutanoni Musoma halmashauri ingepaswa kutoa barua hiyo na kuwasomea hadharani wananchi ili  kujiridhisha lakini wanasema kwa maneno matupu kuwa Mabula aliwabariki kuendelea na zoezi ila wawape kipaumbele wananchi wapale kwa kuwagawia kiwanja kwanza.


Naye Butebi Moya awali alisema kuwa wananchi hao wanania nzuri na halmashauri yao cha msingi wanaomba kupimiwa na viwanja vitakavyo patikana wagawane kwa kufuata uwiano na pia walitoa mda mrefu tangu mwaka 2014 mgogoro ulipoanza na wamefika kila Ofisi ya serikali wakilalamika bila kusaidiwa mdipo wakaamua kwenda kwa Naibu Waziri nyumba maendeleo na makazi ambapo aliwasaidia lakini cha ajabu halmashauri inakaidi ambapo sasa  tayari wameweka zuio la kutaarifu halmashauri Tarime mji kuwa wanataka kwenda kuishitaki mahakamani.


Samo Nyang’anyi ambaye ni mwenyekiti wa mtaa wa Nyagesese alisema kwenye kikao hicho kuwa mgogoro huo umedumu kwa mda mrefu na halmashauri wakati inafanya mchakato wote hawajawahi kumshirikisha kama mwenyekiti wa eneo husika ambapo jana alitangaza  kutoshiriki katika zoezi lolote la halmashauri katika mgogoro huo na kuwa halmashauri wafanye wenyewe.


Mwenyekiti huyo alitumia nafasi hiyo kushukuru serikali iliyopo madarakani chini ya Mama Samia Suluhu Hassani ambapo alitumia nafasi hiyo  kumwambia kaimu mkuu wa kituo cha polisi Tarime Mjini aliyefika katoka kikao hicho kuwa ni bora amefika katika kikao hicho amejionea hali halisi baina ya halmashauri na wananchi wa mgogoro wa Nyandoto.


Mwenyekiti huyo alitupia halmashauri lawama ya kuto mshirikisha na kutokuwa karibu na wananchi wanaokaa na kumiliki maeneo hayo ambapo alisema kama halmashauri ina ushahidi kuwa wanawashirikisha kila zoezi je nilini walikuja na kuwatangazia wananchi kuwa viwanja vilivyopimwa ni vingapi na atakaye kuwa anahitaji kununua au kumilikishwa anatakiwa kufuata taratibu gani hilo halijawahi kutokea alisema.


Kwa upande wake mwanasheria wa halmashauri hiyo,Haruna Matata alisema kuwa halmashauri imeandaa utaratibu wa kugawa viwanja kwa watakao hitaji kununua huku kipaumbele kikiwa cha watu 33 waliokutwa na ramani na kuwa watu hao watapewa bure kiwanja bila kutozwa hata shilingi moja,


Mwanasheria huyo aliongeza kuwa halmashauri imepanga Desemba 14,2021 itaenda kuwaonyesha viwanja waliokwisha lipia na kuwaonyesha wenye uhitaji wa kununua kwa hali hiyo wanaomba ushirikiano.


ASP Maskamo Petro alisema kuwa wananchi hao hawana vielelezo vinavyoonyesha kuwa maeneo wanayoyalalamikia niyao badala yake wanavielelezo vya magazeti na TV na kuwa hivyo havitambuliki.


ASP Maskamo aliongeza kuwa katika mkutano huo police hawakujan kuwatisha badala yake wamekuja kwa swala la kisheria kulinda Raia na mali zake na kuwa wapo kisheria na mtu yeyote akiwahitaji kisheria wanaenda bila kujali ambao aliwaomba kutii sharia bila shuruti.

Wednesday, December 8, 2021

RADI YAPIGA WAPENZI WAKIZINI, YAUA MMOJA.

Mkazi wa Kijiji cha Masweya Kata ya Mtunduru Wilaya ya Ikungi, Vaileth Hassan Mtipa (32) amefariki dunia baada ya kupigwa na radi wakiwa wanazini na mume wa mtu kwenye pagale la nyumba.


Tukio hilo ambalo linadaiwa kughubwikwa na usiri tangu lilipotokea mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu lakini baadaye limeanza kuzungumzwa huku ndugu wakikiri kutokea tukio hilo.


“Tukio lipo na tumeshamzika lakini uliza viongozi watakuambia, na hadi sasa mwanaume aiyekuwa na marehemu bado anaugulia maumivu kwani alijeruhiwa vibaya miguuni na radi hiyo,” alisema shuhuda wa tukio hilo.


Inadaiwa siku ya tukio hilo, Vaileth alikuwa na mpenzi wake Hassan Nzige na wakati wanafikwa na majanga hayo kwenye pagale walikuwa wakiendelea kufanya mapenzi.


Shuhuda anaeleza kuwa baada ya kupatwa na mkasa huo, Nzije alishindwa kusimama ndipo akaanza kupiga yowe kwa nguvu kwa ajili ya kuomba msaada ndipo watu wakamkuta akiwa hajiwezi wakati mwenzake akiwa amepoteza maisha tayari.


Baadhi ya wanakijiji wa Masweya walimchukua Nzige aliyejeruhiwa miguu yake na kumkimbizwa zahanati ya Ndulungu, kwa matibabu ambapo inadaiwa kuwa kwa sasa anaendelea vizuri.


Mwenyekiti wa Kijiji Masweya, Saidi Hongoa amekiri kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 23, 2021 jioni muda mfupi kabla mvua haijaanza kunyesha.


“Radi ilipiga kabla mvua kuanza kunyesha, wakati huo wapendanao hao wakiwa kazini (wakifanya mapenzi) na wote wawili walikimbizwa katika zahanati ya kijiji cha Ndurungu wakati mwanamke akiwa ameunguzwa vibaya shingoni na mgongoni na mwanaume alikuwa ameunguzwa miguuni, lakini walipofikishwa waliambiwa mwanamke alikuwa amepoteza maisha tayari”, amesema Hongoa.


Amesema baada ya kutokea kwa tukio hilo, juhudi zilifanyika katika kumjulisha mume wake marehemu Violeth, Manase Nkungu aliyekuwa mbali na eneo hilo lakini aliposikia alilipokea kwa masikitiko.


Diwani wa kata ya Ndurungu, Theresia Daudi amsema kuna kila dalili kwamba marehemu Vailenth alifariki papohapo kwa vile aliunguzwa sehemu nyeti za mwili wake japo ni vigumu kueleza.


Mume wa marehemu, Manase Nkungu akiwa na masikitiko amesema hakutegemea kuwa angepata pigo kubwa la ghafla namna hiyo katika kipindi ambacho alimwamini mkewe.


Nkungu alisema mkewe amemwachia watoto wanne hivyo inampa wakati mgumu wa namna gani anavyoweza kujipanga kwa namna ya kuwalea na kuwajenga kisaikolojia wanawe kutokana na historia ya kifo cha mkewe hata watakapokuwa wakaubwa.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, ACP Stella Mutabilirwa alipoulizwa na Mwananchi juu ya tukio hilo, amesema taarifa hiyo haikumfikia akidai wahusika huenda waliamua kulimaliza kwa kuchukua hatua za mila huko kwani namna lilivyo hakuna anayetuhumiwa kwa mauaji hayo.


ZAIDI YA 100 WAUAWA KATIKA MAPIGANO YA DARFUR MAGHARIBI MWA SUDAN.

 

Zaidi ya watu 100 wameuawa kufuatia mapigano ya kikabila katika jimbo la Dafur Magharibi nchini Sudan.


Mapigano kati ya Waarabu na wapiganaji wa Kiafrika kutoka jamii ya Masalit inayoungwa mkono na waasi wa zamano yamekuwa yakiendelea kwa siku kadhaa sasa.


Mapigano katika eneo la Kreinik yamesababisha maelfu ya watu kutoroka makwao, wengine wakivuka mpaka na kuingia nchi jirani ya Chad, Umoja wa Mataifa unasema.


Mmoja wa manusura wa ghasia hizo anasema wanaume waliyojihami walishambulia vijiji vyao magharibi mwa Kreinik, na kuanza kupiga risasi kabla ya kuchoma moto nyumba zao.


Pia waliweka vizuizi katika barabara kuu kuwazuia watu kutoroka.


Waliyojeruhiwa hawana njia ya kupata matibabu ya dharura.


Mapigano mapya ya kikabila yalianza Jumapili kati ya jamii hizo mbili, karibu watu 55 wameuawa.


Miili zaidi ilipatikana msituni na kuongeza idadi ya vifo hadi zaidi ya 100. Makumi ya wengine hawajulikani waliko.


Mwezi uliopita, watu 43 waliuawa katika sehemu tofauti ya Darfur Magharibi.


Mapigano ya kikabila pia yameripotiwa kusini mwa eneo hilo lenye machafuko.


Serikali imetuma kikosi cha pamoja cha vitengo vya kijeshi, jeshi na polisi huko Darfur Magharibi na Kusini ili kujaribu kuzuia ghasia.

WAFUNGWA 38 WAFARIKI HUKU 69 WAKIJERUHIWA KATIKA MKASA WA MOTO WA GEREZA BURUNDI.

 


Takriban wafungwa 38 wamefariki dunia na wengine 69 kujeruhiwa katika moto ulioteketeza gereza kuu la mji mkuu wa Burundi City Gitega mapema Jumanne.

Haijabainika ni nini kilisababisha moto huo.





Kumi na wawili kati ya waliofariki walisakamwa na moshi huku 26 waliosalia wakipata majeraha ya moto, kulingana na makamu wa rais wa Burundi, Prosper Bazombanza, ambaye alitembelea kituo hicho na hospitali ambapo wengi wa majeruhi wanatibiwa.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa majeruhi 34 waliopata majeraha ya moto ya wastani na zaidi wamepelekwa hospitali huku wengine wakipatiwa matibabu katika eneo la gereza.

"Wafanyikazi wa afya wametupa hakikisho kwamba watapona", alisema.

Afisa huyo pia alitangaza bili yao ya matibabu italipwa kikamilifu na serikali.

Chanzo cha moto huo bado hakijabainika. Inasemekana kuwa moto huo ulizuka mwendo wa saa 10 asubuhi kwa saa za Burundi, na kuwashtukiza wafungwa wakiwa usingizini. Mashahidi wamethibitisha kwa shirika la habari la AFP kwamba waliona moto mkubwa ukitokea na kuteketeza kabisa sehemu za jengo la gereza.

Mmoja wa wafungwa ambaye ameweza kuongea kwenye simu amesema alipiga kelele "tutachomwa moto tukiwa hai, lakini, ameongeza, polisi walikataa kufungua milango ya sehemu tulikuepo, wakisema" haya ni maagizo ambayo tumepokea ". Wafungwa wenzake waliteketea kwa moto akisuhudia kwa macho yake.
Hali mbaya ya usalama ilifanya iwe rahisi kwa moto huo kuenea haraka katika gereza ambalo awali lilikusudiwa watu 400 lakini sasa lilikuwa na wafungwa zaidi ya 1500.

Kiwango kamili cha uharibifu kilikuwa bado hakijajulikana.

RAS TANGA AWATAKA WAAJIRI WENYE MALIMBIKIZO MICHANGO NSSF KUTUMIA FURSA YA MISAMAHA KUIONDOA

 

KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Manyema akizungumza wakati akifungua mkutano wa wadau wa NSFF katika mkoa wa Tanga uliofanyika leo


Meneja wa NSSF Mkoa wa Tanga Audrey Claudius akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa NSSF Jijini Tanga leo

Meneja wa NSSF Mkoa wa Tanga Audrey Claudius akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa NSSF Jijini Tanga leo


AFISA Mwandamizi Mkuu wa NSSF Mkoa wa Tanga Abubakar Mshangama Soud akizungumza wakati wa mkutano huo
AFISA Mwandamizi Mkuu wa NSSF Mkoa wa Tanga Abubakar Mshangama Soud akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo

AFISA Mwandamizi Mkuu wa NSSF Mkoa wa Tanga Abubakar Mshangama Soud akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo


Afisa kazi Mkoa wa Tanga Janeth Omolo akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo


Mansoor Ramadhani


Sehemu ya Washiriki kwenye mkutano huo
Sehemu ya washiriki kwenye Mkutano huo wakifuatilia matukio mbalimbali
Sehemu ya Washiriki wa mkutano huo



NA OSCAR ASSENGA, TANGA

KATIBU Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Manyema amewataka waajiri wenye malimbikizo ya michango katika Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSFF) kutumia fursa ya misamaha ya adhabu iliyotolewa na mfuko huo kuondoa malimbikizo waliokuwa wakidaiwa.

Pili aliyasema hayo leo wakati wa mkutano wa wadau wa NSFF katika mkoa wa Tanga ambapo alisema mkutano huu ni muhimu ambao dhumuni kubwa ni kutoa elimu juu ya shughuli za kiutendaji za mfuko NSSF, Sheria ya Hifadhi ya Jamii pamoja na kutatua changamoto zilizopo kwenye kufanikisha malengo ya kiutendaji mfuko na waajiri.

Alisema amefarijika sana uwepo wa mkutano huo kwani kufanya hivyo kutasaidia kuondoa yale malimbiko yaliyokuwa wanadaiwa huku akiwataka waajiri fursa hiyo muhimu kwa sababu kama walikuwa wanadaiwa tozo lakini kutokana na umuhimu wa kuwapunguzia.

Katibu Tawala huyo ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Adam Malima alisema ni muhimu kuitumia ili kuweza kuona yale malimbikizo ya michango ya wanachama yanawasilishwa kwa wakati.

Alisema kwani michango hiyo mwisho wa siku inawasaidia wanachama wakati wanapokuwa wakistaafu kazi na inatia uchungu mwajiriwa anapostaafu anaanza kuhangaika na mafao yake kuwa sababu mwajiri hajawasilisha michango,

“Nitumie fursa hii mfuko wa NSSF kutoa punguzo kwenu kwa asilimia 75 ukipiga mahesabu utaona ni ela nyingi utakuwa umeiokoa hivyo utajipima mwenyewe kuona ..Lakini nafahamu zipo changamoto zinazowakabili waajiri kupitia changamoto hizo ni wajibu kuhakikisha michango inawasilishwa kwa wakati “Alisema

“Kwani michango hii itakwenda kuwasadia waajiriwa wanapostaafu hivyo naamini kupitia mafunzo hayo ambapo kwa sasa dunia imehama kutoka Analojia kwenda Digitali hivyo mtakapopata mafanzo hayo yatakwenda kuimarisha utendaji kazi kenye maofisi yao na kuondoka kwenye utendaji kazi wa mafaili na kwenda kutumia Tehama “Alisema

Hata hivyo aliwataka kutumia elimu waliyayapata kufikisha kwa wasaidizi wenu kwa sababu sisi ni binadamu tunaweze kupata changamoto kutokuwepo hivyo kukosekana kwenu kusikwamishe utendaji kazi katika ofisi zenu.

“Nikuombe Meneja wa Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga mafunzo hayo yawe endelevu kwa kuandaa mkutano kufanya tathimini kwa mfumo mlioanzisha ambao utakuwa na manufaa”Alisema

Hata hivyo Katibu Tawala huyo alisema mfuko huo umeanzisha huduma mbalimbali za kidigitali ili kurahisisha huduma kwa wadau wake huku akieleza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga ina imani kwa ushirikishaji wa maoni ya wadau kwa sekta mbalimbali.

“Niwapongeze Ofisi ya NSFF Mkoa kwa mkutano huo kwani utaimarisha huduma za Hifadhi ya Jamii kwa mkoa na nchi kwa ujumla kwani Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu haipo nyuma kwenye kuongeza ustawi wa wananchi mmoja mmoja kwa sekta binafasi kwa ujumla”Alisema

Awali akizungumza wakati wa mafunzo hayo Meneja wa NSSF Mkoa wa Tanga Audrey Claudius alisema wamefanya mkutano na waajiri wasiopungua 900 na wamefanya kwa waajiri 120 wanashukuru mwitikio umekuwa mkubwa lengo likiwa ni kutoa elimu juu ya matumizi ya mfumo wa Tehama wanataka kuhama kutoka analogia kwenye kidigitali.

Alisema wameona watoe elimu kwa waajiri na zoezi hilo litakuwa endelevu ambapo wanataka kuona waajiri wote kuanzia mwezi Januari mwakani kutumia mifumo hiyo kufanya shughuli zao za kila siku au kuandikisha wanachama wapya kupata taarifa za wanachama.

“Lakini pia kulipa michango na wanapotumia mifumo hiyo wanajitahaidi kuhakikisha wanakuwa na data safi kwa sababu mifumo hiyo inawasaidia kupunguza data chafu na kupata taafisa sahihi za wanachama na wajiri wao,

Alisema wakishakuwa na taarifa sahihi watakuwa na data basee nzuri watakaohifadhi taarifa za wanachama wao na itawasaidia kutoa huduma bora baadae kwani mwanachama anapokuja kufuatilia mafao yake taarifa zake zitakuwa sahihi na hivyo kuweza kufanikisha.

Aidha alisema mwezi Octoiba Mosi mwaka huu wametoa taarifa kwamba watakuwa na punguzo za tozo kwa waajiri waliochelewa kulipa michango ya nyuma na tozo ilikuwa kwa awamu tano ambao hawajalipa michango kuanzia Octoba 1 hadi 31 walisamahewa tozo hizo asilimia 100.

Alisema sasa kwa awamu wa pili wamesahewa asilimia 75 ya tozo hivyo wanatumia mkutano huo kuwasihi waajiri wote watumie fursa hiyo kwani tozo hizo zitaisha Januari 31 mwakani watasamehe kwa asilimia 90 baada ya hapo haitakuwepo tena na taratibu wa kisheria zitafuata maana mchango wa NSSF ipo kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake Afisa kazi Mkoa wa Tanga Janeth Omolo alisisitiza waajiri wanapo kuwa wakiajiri wanapaswa kuwa na mikataba ya kazi lengo kuu ni kuboresha mahusiano kati ya mfanyakazi na mwajiri.