ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 10, 2021

MAKUMI YA WAFUNGWA WATOROKA GEREZANI DR Congo

 


Makumi ya wafungwa kutoka gereza la Boma magharibi mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wametoroka.


Wafungwa hao walitumia fursa ya muziki wa sauti ya juu uliokuwa ukipigwa katika eneo la mazishi ili kuwavuruga walinzi.


Wafungwa tisa walikamatwa karibu na gereza hilo na mmoja kujeruhiwa wakati walinzi wakifyatua risasi hewani, Radio Okapi iliripoti.


Wafungwa wengine 19 bado wako hawajapatikana, kulingana na redio hiyo. Gereza la Boma hapo awali lilikuwa na matukio ya utoro wa wafungwa.


Wenyeji wanasema gereza hilo linahitaji kufanyiwa marekebisho kama lilijengwa miaka ya 1900.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.