ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 17, 2024

RC BATILDA AWAONYA WATAKAONG’OA ORODHA YA WAPIGA KURA

 


Na Oscar Assenga, TANGA.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amesema kwamba mkoa huo umejiandaa kikamilifu kuelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa huku akiwaonya watu wenye tabia ya kung’oa orodha ya wapiga kura wasisubutu kufanya hivyo.

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu ambapo alisema watakaojaribu kufanya hivyo hawatasalimika badala yake watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo faini ya Laki tatu,kifungo cha miezi 12 au vyote vya pamoja

Balozi Batilda aliyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuelezea maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Mkoa huo ambapo alisema hawataki kuona vitendo hivyo vinatokea kwenye mkoa huo.

Alisema kwa sababu orodha hiyo imewekwa maalumu kwa ajili ya kuwawezesha wapiga kura wa eneo Fulani kuweza kuhakiki majina yao ili waweze kushiriki kwenye uchaguzi huo hivyo wanapotokea watu wanang’oa ni uvunjifu wa sheria.

“Lakini pia kutoa taarifa za uongo ili uweze kugombea nafasi ya za uongozi pamoja na wale ambao watajiandikisha zaidi ya mara moja anatoka sehemu moja hadi nyengine hao nao wakibainika watachukuliwa hatua kali”Alisema

Aidha alisema kwamba pia wale ambao watabainika wamepiga kura zaidi ya mara moja au kutishia wapiga kura ni kosa na watachukuliwa hatua za kisheria sambamba na wale ambao watafanya kampeni wakati wa uchaguzi.

“Lakini kwa wale ambao wataonyesha ishara au kuvaa mavazi yanayomuashiria mgombea hayo mabango yakionekana wakati wa uchaguzi ni kosa na watakaobainika watashughulikiwa”Alisema

Onyo hilo pia alilitoa kwa wale wenye tabia ya kuwazuia wasimamizi wa Uchaguzi kutekeleza majukumu yao wakati wa zoezi la watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Kuhusu ukomo wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Alisema kwamba viongozi hao ukomo wao utakuwa ni Octoba 25 mwaka huu kwa viongozi wa Serikali za Mitaa na Vijiji na siku saba za ukaguzi na kuanzia Octoba 1 mpaka 7 utakuwa ni muda wa kuchukua fomu na kurudisha na Octoba 8 na 9 utakuwa uwasilishaji pingamizi kuhusu uteuzi na kuanzia Octoba 20-26 itakuwa ni kipindi cha kampeni.

“Kwa mkoa wa Tanga tunatarajia kuwaandikisha wapiga kura wasiopungua chini ya asilimia 80 na kuendelea kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu.

Hata hivyo alisema nafasi zinazogombewa katika uchaguzi huo hutegemea aina ya Halmashauri inayofanya uchaguzi kama ni Mamlaka ya Wilaya au Mji kwa upande wa mkoa wa Tanga wana maeneo ya utawala yanayohusika kwenye uchaguzi ni mamlaka ya mji mdogo ni tatu,Kata 245,mitaa 270,vijiji 763 na Vitongoji 4,531.

RAS PWANI ATEMA CHECHE AWATAKA WAZAZI KUWALINDA NA KUWATUNZA WATOTO WAO

NA VICTOR MASANGU/PWANI. SAUTI YA ALBERT G. SENGO. Serikali Mkoani Pwani imewahimiza wazazi na walezi kuhakikisha wanaweka misingi imara katika kuwalinda na kuwatunza watoto wao katika mambo mbali mbali ikiwemo kukomesha kabisa vitendo vya ukatili wa kijinsia, kulinda usalama wao pamoja na maadili lengo ikiwa ni kupata vijana ambao watakuwa wazalendo na Taifa lao.

Monday, September 16, 2024

RC GEITA AOMBWA KUINGILIA KATI MGOGORO WA MIRATHI

 

 

Na Oscar Assenga. Korogwe.


Mkuu wa mkoa wa Geita, Martine Shigela ameombwa kuingilia kati mgogoro wa mirathi ya mwanamke mkongwe, Kabula Seni aliyefariki na kuacha nyumba iliyopo mtaa wa Msalala Road miti mirefu mjini Geita.


Mgogoro huo unadaiwa kuibuliwa na Diwani wa viti maalumu Geita, Khadija Mfuruki anayedaiwa kushinikiza fedha zitokanazo na mauzo ya nyumba hiyo zigawanywe kinyume na makubaliano ya vikao vya familia.


Ombi hilo limetolewa na Lulu Msemakweli ambaye ni msimamizi wa mirathi hiyo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Korogwe.


Amesema ameamua kumuomba Mkuu wa mkoa wa Geita kuingilia kati mgogoro huo kwa sababu Diwani huyo amekuwa akitumia madaraka yake kuvuruga mchakato wa mirathi.


Amesema chanzo cha mgogoro huo ni baada ya familia kuamua kuiuza nyumba na kupatikana mnunuzi ambaye aliweza kutoa malipo ya awali ya nyumba hiyo ndipo alipojitokeza na kulazimisha fedha zitumike kuwanunulia nyumba nyingine wajukuu wawili licha ya kuwa marehemu aliacha wajukuu 30.


"Amefikia hatua ya kumuamuru mteja anayenunua nyumba hiyo ya urthi asilipe awamu iliyobaki mnunuzi ameingia woga sana,tusichokubaliana naye ni kitendo cha kuamuru wajukuu wawili tu wajengewe nyumba na hawa wengine 28 watajisikiaje?", amesema Lulu.


Lulu ambaye amesema ni miongoni mwa watoto watatu walioachwa na mama yao wakiwamo wanaume wawili amesema kupitia mahakama alipitishwa kuwa msimamizi wa mirathi na kwamba anachohitaji ni maamuzi ya mgawanyo wa mirathi yafanywe na wanafamilia na siyo kutoka nje.


"Diwani amevuruga mno mchakato wa mirathi yetu ningeomba Mkuu wa mkoa aingilie kati ili muafaka upatikane.... natarajia kwenda ofisini kwake kumpa ombi letu hili", amesema Lulu.


Akizungumza kwa njia ya simu, Diwani Mfuruki amesema siyo kweli kwamba ameingilia kati mirathi ya familia hiyo lakini kwa sababu yeye ni kiongozi hana budi kurekebisha pale anapolalamikia kuhusu haki ya wananchi katika eneo lake.


"Sijaingilia kati mirathi ifahamike kuwa mimi ndo niliyesaidia hata mchakato wa kesi mahakamani hadi wakashinda,yapo mengi ambayo si ustaarabu kuweka hadharani,ninachotaka ni kuhakikisha usawa pande zote... kila upande upate haki"amesema Diwani huyo.

WAZIRI MAVUNDE AIPONGEZA TUME YA MADINI KWA KUVUNJA REKODI YA UKUSANYAJI WA MAPATO

 


Waziri wa Madini Anthony Mavunde akizungumza leo wakati akifungua kikao kazi na Menejimenti ya Tume ya Madini Jijini Tanga 
Naibu Waziri wa Madini Dkt Steven Kiruswa akizungumza wakati wa kikao hiho
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Mhandisi Yahaya Samamba akizungumza wakati wa kikao kazi hicho
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akizungumza




Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI wa Madini Anthony Mavunde ameipongeza Tume ya Madini kwa kuvunja rekodi kukusanya kiasi cha Sh Bilioni 196 kwa kipindi cha siku 75 huku akieleza jambo hilo ni kubwa na inaonyesha wamedhamiria kuifanya sekta ya madini inachangia kwenye uchumi wa nchini.

Mavunde aliyasema hayo leo Jijini Tanga wakati akifungua kikao kazi na Menejimenti ya Tume ya Madini Jijini Tanga ambapo alisema kiwango hicho kimepokelewa mpaka leo 15 Septemba ndani ya miezi miwili ya mwaka huu na hilo linatokana na .

Alisema kiwango hicho kimeifanya kuvunja rekodi ya makusanyo ilihali mwaka 2015/2016 ilichukua mwaka mzima kukusanya Bilioni 161 lakini leo ndani ya siku 75 tume hiyo imeshakusanya kiasi hicho na hivyo kuvunja rekodi kwani waliojiwekea makusanyo ya Bilioni 60 mpaka Bilioni 65 kwa kila miezi na mwili iliyopita mmekusanya Bilioni 83 kila mwezi mmevuka malengo yao.

“Niwatie moyo na wakikaza buti na kuendelea na usimamizi huo mzuri na makusanyo wakifika mwakani mwezi wa saba watakuwa mmeandika historia kubwa”Alisema

Katika hatua nyengine Waziri Mavunde amewataka maafisa madini wakazi wa mikoa kuhakikisha wanashughulikia migogoro kwenye maeneo yao kwa haraka inapojitokeza badala ya kusubiri mpaka wafike viongozi wakubwa ikiwemo Waziri.

Alisema haiwezekani wao wapo kwenye mikoa na wanashindwa kutatua migogoro iliyopo hivyo wabadilike wahakikishe wanaishughulia na utatuzi wake unapatikana haraka bila kumuonea mtu.

Alisema anajisikia vibaya kuona mgogoro inapotokea mpaka aende waziri au Naibu Waziri wakati wapo maafisa madini wakazi mpaka umshinde ndio uvuke uende ngazi lakini kazi yenu hya kwanza ni utatuzi wa migogoro labda mniembie nyie ni sehemu ya migogoro lakini kama sio sehemu ya migogoro tatueni migogoro,

“Niwaambieni kipimo chenu cha kazi kitakuwa ni namna mnavyotatua migogoro tatueni na sio mpaka msubiri ufike hatua ya juu anzeni nao lakini mtatue migogoro katika haki asionewe mtu simamieni haki ndugu zangu”Alisema Waziri Mavunde

Udhibiti wa Utoroshwaji wa Madini

WAZIRI Mavunde aliwataka maafisa hao kuhakikisha wanadhibiti utoroshwaji wa madini katika maeneo yao hususani ile ya mipakani

“Mmeona hivi karibuni kuna kesi nyingi sana zinapelekwa mahakamani na juzi tumewakamata watu Bandari Dar na kilo 15 za dhahabu na tumezitaifisha ela dhahabu na wanakwenda mahakamani,huko kwenye maeneo yenu hakikisheni mnashirikiana kwenye task force kudhibiti hili lisitokee”Alisema Waziri Mavunde

Aidha Waziri Mavunde aliutaja Mkoa wa Madini wa Kahama ndio unaongoza kwa shughuli za za utoroshaji wa madini na mbinu hivi sasa zimebadilika wanasikie wale ambao wanakwenda kuuziana kwenye mashine za Mpunga ambapo alimtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa huo kuhakikisha anaimarisha eneo hilo.


Katika hatua nyengine Waziri Mavunde amewataka maafisa madini wakazi wa mikoa kuhakikisha wanashughulikia migogoro kwenye maeneo yao kwa haraka inapojitokeza badala ya kusubiri mpaka wafike viongozi wakubwa ikiwemo Waziri.

Mavunde alitoa agizo hilo leo Jijini Tanga ambapo alisema haiwezekani wao wapo kwenye mikoa na wanashindwa kutatua migogoro iliyopo hivyo wabadilike wahakikishe wanaishughulia na utatuzi wake unapatikana haraka bila kumuonea mtu.

Alisema anajisikia vibaya kuona mgogoro inapotokea mpaka aende waziri au Naibu Waziri wakati wapo maafisa madini wakazi mpaka umshinde ndio uvuke uende ngazi lakini kazi yenu hya kwanza ni utatuzi wa migogoro labda mniembie nyie ni sehemu ya migogoro lakini kama sio sehemu ya migogoro tatueni migogoro,

“Niwaambieni kipimo chenu cha kazi kitakuwa ni namna mnavyotatua migogoro tatueni na sio mpaka msubiri ufike hatua ya juu anzeni nao lakini mtatue migogoro katika haki asionewe mtu simamieni haki ndugu zangu”Alisema Waziri Mavunde

Udhibiti wa Utoroshwaji wa Madini

WAZIRI Mavunde aliwataka maafisa hao kuhakikisha wanadhibiti utoroshwaji wa madini katika maeneo yao hususani ile ya mipakani

“Mmeona hivi karibuni kuna kesi nyingi sana zinapelekwa mahakamani na juzi tumewakamata watu Bandari Dar na kilo 15 za dhahabu na tumezitaifisha ela dhahabu na wanakwenda mahakamani,huko kwenye maeneo yenu hakikisheni mnashirikiana kwenye task force kudhibiti hili lisitokee”Alisema Waziri Mavunde

Aidha Waziri Mavunde aliutaja Mkoa wa Madini wa Kahama ndio unaongoza kwa shughuli za za utoroshaji wa madini na mbinu hivi sasa zimebadilika wanasikie wale ambao wanakwenda kuuziana kwenye mashine za Mpunga ambapo alimtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa huo kuhakikisha anaimarisha eneo hilo.



“Lakini pia nimemwambia Katibu Mkuu waifanye Kahama kama Kanda Maalumu kwa maana dhahabu nyingi inatoroshewa kupitia Kahama nimekuona RMO mara mbili mara tatu mnatoka mnakamata endeleee na mikoa mingine hasa mikoa ya Mipakani”Alisema Waziri huyo.

Waziri huyo aliwataka maafisa hao kila mmoja katika eneo lake ahakikishe anakuwa sehemu ya udhibti wa utoroshaji wa madini kwa maana utoroshwaji huo unasababisha kupoteza mapato mengi.

Hata hivyo Waziri huyo aliitaka Ofisi ya Kamishna wa Madini kushirikiana na RMO kuwalea wachimbaji wadogo na kuwaendeleza katibu mkuu pale wizara wawekezaji wakubwa wana meneja wake ndani ya wizara wa kuyasimamia katibu mkuu kupitia Ofisi ya Kamishna natoa maelekezo tengenezeni utaratibu kushirikiana na RMO kuwaibua watanzania wawekezaji wa sekta ya madini kupitia ofisi ya Kamishna wawelee nao wagraduate kutokana na kwamba hivi sasa wenyewe hawana muangalizi.

Alisema ili siku moja waweze kutengeneza mabilioni wengi kupitia wachimbaji wadogo hivyo wakikaa nao na kuwasaidia kama wanavikwazo waone namna ya kuyatatua ili kuweza kuongeza mapato.

Katika hatua nyengine Waziri Mavunde aliwataka kuhakikisha wanadhibiti upotevu wa mapato waende wakazibe mianya na makusanyo yaweze kuongezeke huku akieleza hiyo ni sehemu ya kazi yako ya msingi.

“RMOs kila mtu amewekewa malengo ya kuwafikia kwa mwaka wa fedha huu kama unahisi kwako unashindwa kufikia malengo kwa jambo ambalo halihusiani na wewe ni tatizo la kimfumo,kimundo lipo nje ya uwezo

Sunday, September 15, 2024