ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, July 21, 2012

MAMIA WASHIRIKI KUMZIKA MCH. JAMES KWAKA OLIMO

Mamia ya wananchi toka sehemu mbalimbali leo wamejitokeza kwa wingi katika kijiji cha Kiabakari mkoani Mara kumzika Mchungaji Mstaafu kipenzi cha watu James Kwaka Olimo wa Kanisa la Menonite mkoa wa Mara aliyefariki dunia mnamo jumamosi ya wiki iliyopita tarehe 13july2012 katika Hospitali ya Rufaa Bugando ambako alikuwa akipatiwa matibabu na kuzikwa leo tarehe 21july2012.

Watoto na ndugu wa marehemu katika picha ya pamoja nje ya kanisa la Menonite jimbo la Musoma mjini ambapo ibada ya kuuaga mwili wa marehemu mchungaji mstaafu Olimo ilifanyika.


Wachungaji wakiwakilisha kanda mbalimbali nchini wamehudhuria ibada hii takatifu.


Huzuni na majonzi vilitawala ndani ya kanisa la Menonite Musoma Mjini pale watoto wa marehemu walipokaribia mwili wa mpendwa baba yao kwaajili ya kutoa heshima za mwisho.


Waumini ndani ya Kanisa la Menonite Musoma mkoani Mara wakishiriki ibada hiyo.


Wachungaji na Maaskofu zaidi ya 50 toka makanisa mbalimbali nchini wameshiriki ibada hiyo hii leo.


Wachungaji na Maaskofu wakiwa wameubebe mwili wa mpendwa wao kutoka kanisani tayari kwa safari kuelekea Nyumbani kwa ukoo wa marehemu eneo la Kiabakari kwa ajili ya maziko.


Mwili wa marehemu Mchungaji Mstaafu Olimo, uliwasili kijiji cha Kiabakari majira ya saa nane hivi na kukutana na Ummati mkubwa wa waombolezaji.


Marafiki na wazee wa kaya mbalimbali eneo la Kiabakari.


Mwili wa marehemu Mchungaji Mstaafu James Kwaka Olimo ukishushwa kaburini kwa heshima na taratibu za kanisa wahusika wakiwa ni wachungaji waliohudhuria toka makanisa mbalimbali.


Marafiki wakishuhudia yanayojiri kwa safari ya mpendwa wao.


Kamera yako haikupata jukwaa kuonyesha picha kamili ya Umma ulioshiriki maziko hayo lakini ilipenya na kuona japo engo hii.


 Kamera yako  iliwasihi Mabinti hawa wa marehemu 'japo watabasamu' kwani baba yao waliyempenda katwaliwa na yule aliyemleta mara baada ya kumaliza kazi yake duniani, nao wakatabasamu kujifariji.


Picha ya pamoja na mzee mkongwe wa ukoo.


Wakufunzi wa Chuo Cha Ualimu  Bunda ambao ni mashabiki namba moja wa www.gsengo.blogspot.com nao walihudhuria mazishi hayo, kutoka kulia Alex Mwingira, Emmanuel Mandango, Jublet Shuma, Hilary Majimbe na Tumaini Mnale.


Kutoka kushoto ni Edgar Mapande, G. Sengo na Mr Ben.

BIKINI YAMREJESHA JORDIN SPARKS KATIKA KURASA ZA MBELE GAZETI LA SHAPE

"I've always felt cute, but now I feel sexier," she told People at the time. Twenty more pounds down, she's even happier, telling SHAPE: "I've never felt sexier!"

Jordin Sparks
Wow! Fans of American Idol alum Jordin Sparks are no doubt aware that the 22-year-old singer has been losing weight over the past couple of years.

However, her stunning appearance in a bikini on the August issue of SHAPE leaves no doubt as to how hard she's worked on her figure.

Sparks, who was 17 and a size 14 when she won the sixth season of Idol, tells the magazine she's lost an impressive 50 pounds total. She first decided to get in shape at age 21, claiming she felt tired, sick, and just plain lousy overall.

"I just wanted to be healthy," she notes. "I remember thinking, 'I'm in my prime. I should be happy and fit.' That was the moment I decided that changes needed to be made."
Sparks tells SHAPE she started out slowly, beginning with simple walks around her neighborhood. Once she felt a bit stronger, she joined a gym for Zumba classes and began adjusting her diet. By June of 2011, she was 30 pounds lighter and down to a size 8, leading her to try out her first-ever bikini shoot with People.

MASHINDANO YA NGOMA ZA ASILI YA BALIMI KUANZA KESHO MUSOMA


Na. Shommy Binda
Mashindano makubwa ya ngoma za asili ambayo hufanyika kila mwaka katika mikoa ya kanda ya ziwa kwa kudhaminiwa na kampuni ya TBL kupitia bia yake ya Balimi yatafanyika kesho kwa upande wa Mkoa wa Mara katika ukumbi wa bwalo la Mageraza huku jumla ya vikundi vikitarajiwa kushiriki mashindano hayo.

Akizungumza na Mwandishi wa blogu hii hii leo Mjini Musoma meneja wa TBL Mkoa wa Mara Polycalipo Makunja,amesema taratibu zote kuhusiana na mashindano hayo ikiwemo kuwasiliana na vikundi vyote kutoka katika wilaya zote za Mkoa wa Mara zimekwisha kamilika kilichobakia ni kuona ni kikundi gani kinaibuka washindi hapo kesho na kwenda kuuwakilisha mkoa wa Mara katika mashindano ya kanda yatakayofanyika Julai 28 Jijini Mwanza.

Poly amesema awali mashindano hayo yalikuwa yafanyike jumamosi Julai 21 lakini wameamua kuyasogeza mbele kwa siku moja baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete kutangaza siku tatu za maombolezo kufuatia ajali ya meli ya MV Karama kuzama katika bahari ya Hindi ikiwa njiani kuelekea visiwani Zanzibar.

Amesema vikundi 10 kati ya 12 vilivyojitokeza kushiriki mashindano hayo vitakuwa na nafasi ya kupata zawadi kutokana na maandalizi mazuri ambayo yameboleshwa kwa mashindano ya mwaka huu.

Meneja huyo wa TBL Mkoa wa Mara amesema mshindi wa kwanza katika mashindano hayo ataondoka na kitita cha shilingi laki sita,shindi wa pili laki tano,mshindi wa tatu laki nne na mshindi wa nne shilingi laki tatu.

Ameongeza kuwa kuanzia mshindi wa tano hadi wa kumi kila mmoja ataondoka na kifuta jasho cha shilingi laki moja na nusu huku burudani mbalimbali zikitarajiwa kusindikiza mashindano hayo.

Kwa upande wake Meneja wa Kanda wa kampuni ya TBL Andrew Mbwambo amesema mashindano ya ngoma za asili ya Mwaka huu yanatarajiwa kuwa na upinzani mkubwa kutokana na vikundi kupewa maandalizi ya muda mrefu na kuongezeka kwa zawadi za washindi.

Mbwambo ameongeza kusema kuwa kutakuwa hakuna kiingilio chochote katika kushuhudia mashindano hayo hivyo kila mmoja anaruhusiwa kwenda kushuhudia katika ukumbi wa bwalo la magerza mjni Musoma ni ngoma gani ya asili ya Mkoa wa Mara itakayoibuka kidedea na kwenda kuwakilisha katika mashindano ya kanda jijini Mwanza julai 28.

BODI YA MASHINDANO MISS UTALII YACHUKUA MAAMUZI MAZITO - YAFUTA SHINDANO


BODI ya Taifa ya Miss Tourism Tanzania Organization (MTTO), imelifuta shindano la Miss Utalii Kanda ya Ziwa 2012, lililo fanyika New Mwanza Hotel, juzi, huku taifa likiwa kwenye maombolezo ya siku tatu kutokana na msiba mkubwa wa ajali ya meli ya Mv Skagit, mjini Zanzibar na kupoteza uhai wa watu wengi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa katika vyombo vya habari jana jijini Dar es Salaam na kutiwa sahihi na Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa Miss Utalii Tanzania, Abubakari Omary Bakari, ilisema shindano hilo limefanyika kimakosa na matokeo yake hayawezi kutambuliwa kwa namna
moja ama nyingine.

Alisema uamuzi wa serikali ni wa mwisho, hivyo hawajaunga mkono kufanyika kwa shindano hilo wakati nchi ina majonzi ya kupoteza ndugu na jamaa wao.

“Shindano limefanyika bila kuzingatia misingi ya kiubinadamu na uzalendo kwa Taifa, hivyo Bodi imeamua kulifuta na waandaaji watafuata tena utaratibu mwingine.

“Miss Utalii ni shindano lenye uzalendo, hivyo inapotokea matatizo kama haya na agizo la maaombolezo kutoka kwenye serikali nadhani kuna kila sababu ya kuliafiki,” ilisema taarifa hiyo.

Shindano hilo limeandaliwa na Fania Beauty Salon, chini ya Mkurugenzi wake Fania Hassan, ambaye sasa ana changamoto nyingine ya kujiweka sawa katika jamii, ukizingatia kwamba Taifa lilikuwa kwenye maombolezo ya siku tatu.
--
Miss Tourism The Symbol Of National Heritage

RAJABU MAOJA AMTISHIA MAISHA GOTTLIEB NDOKOSHO WA NAMIBIA

Gottlieb Ndokosho kushoto akiwa kazini.

Mtanzania Rajabu Maoja bondia mzoefu katika ngumi za kulipwa kutoka mkoa wa Tanga atapanda ulingoni Septemba 1 kupimana ubavu na bondia Gottlieb Ndokosho bingwa wa ngumi nchini Namibia.
Mpambano huo unaofanyika katika jiji na Windhoek, nchini Namibia unawakutanisha mabondia wawili ambao wanazimudu vizuri ngumi ulingoni. Hii ni mara ya kwanza kwa bondia wa Kitanzania kugombea mkanda wa IBF katika bara la Afrika nje ya nchi tangu mpambano katia ya Iraq Hudu na Ali Said wa Kenya ulivyofanyika jijini Mombasa mwaka 2000.

Wawili hao wataumana kwenye mpambano uliopewa jina la “The Battle for the Kalahari Desert” (Vita ya Jangwa la Kalahari) na waandaaji wa mpambano huo ambao ni Kinda Boxing Promotion chini ya promota Simon Nangolo wa nchi ya Namibia. Namibia iko Kusini Magharibi mwa bara la Afrika ikikingana na Afrika ya Kusini, Botswana na Angola.

Mtanzania Rajabu maoja anatokea katika jiji la tanga na ni mkali aliyejijengea umaarufu mkubwa katika masumbi hapa nchini. Maoja ni kati ya mabondia wachache wenye majina yanayotishia maisha baadhi ya mabondia wenzake katuka bara la Afrika.

Katika uhai wake wa ngumi Maoja amepigana mapambano 31 akishinda 18 na kupoteza kwa kiduchu mapambano 10 ambayo mengi sio yenye hadhi yoyote ya kumharibia historia yake kwemey ngumi na kutoka sare mapmbano matatu (3)

Naye bondia Gottlieb Ndokosho ambaye ni bingwa wa Namibia amepigana pambano 15 na kushinda 11 wakati amepoteza mapambano 3.

Mpambano huo uliopewa jina la The Battle for the Kalahari Desert (Vita ya jangwa la Kalahari) utasimamiwa na Rais wa Shirikiso la ngumi la Kimataifa bara la Afrika, Mashariki ya kati na Ghuba ya Uajemi Mtanzania Onesmo Ngowi. Aidha Ngowi ndiye Rais w kamiehsni ya Ngumi za Kulipwa nchini (TPBC) na mkurugenzi wa ngumi wa baraza la Ngumi la Jumuiya ya madola.

Watanzania, tumuezi mwenzetu rajabu maoja anapopeperusha bendera ya Tanzania. Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.

Imetumwa na;
Onesmo Ngowi

Rais wa IBF bara la Afrika, Mashariki ya Kati na Ghuba ya Uajemi

Friday, July 20, 2012

MASHINDANO YA FA WILAYA YA ILEMELA KUANZA KUTIMUA VUMBI KESHO MWANZA



Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mh. Amina Masenza anatarajiwa kufungua mashindano ya ligi ya soka FA kwa wilaya hiyo yatakayoanza kutimua vumbi kesho kwenye dimba la CCM kirumba jijini Mwanza.

 Kwa mujibu wa Katibu wa Chama cha soka Wilaya ya Ilemela Juma Msaka amesema kuwa timu zitakazoshiriki michuano hiyo ni zile zote zenye usajili unaotambulika na msajili wa vyama vya vilabu vya michezo nchini na timu ambazo hazina usajili kwani michuano hiyo ya FA haina kanuni ya kukataza timu zisizosajiliwa kushiriki michuano hiyo.....

Katibu mkuu wa chama cha soko wilaya ya Ilemela James Msaka (katikati) akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani..
    
Taarifa zaidi bofya hapa kusikiliza.


Mdau wa IDFA akionyesha Tshirt za mashindano.

MFALME ANAYEKUJA ANAVYOTISHIA MAISHA YA MABONDIA WENGI AFRIKA!

Mtanzania Ramdhani Shauri atapanda ulingoni siku ya Idd pili kupambana na bondia Sande Kizito kutoka Uganda kugombea mkanda wa IBF katika bara la Africa katika uzito wa unyoya (Featherweight).
Shauri anayefanya mazoezi yake Ubungo, maeneo ya Mabibo na anafundishwa na kocha mzazi anayetamba kuwa na mabondia wenye nidhamu na vipaji vya hali ya juu.

Ramdhani Shauri ni bondia chipukizi mwenye umri wa miaka 19 na historia yake ya ngumi inafurahisha kila anayeisoma na kuisikia. Ana haiba nzuri inayovutia na anafananishwa na bondia Sugar Ray Leonard wa Marekani kutokana na haiba yake na upiganaji wake.

Sugar Ray Leonard alitamba katika miaka ya 70 na 80. Shauri ni Mfalme anayekuja na hivi sasa anatishia maisha ya mabondia wengi katika bara la Afrika.

Ramadhani Shauri ana nidhamu ya hali ya juu na maisha yake katika ngumi yanafurahisha kwa jinsi anavyoishi kwa nidhamu na kufanya mazoezi ya kujijenga katika ngumi. Katika maisha yake anajiepusha sana na matatizo ambayo vijana wengi wametumbukia kama vile uvutaji wa bangi, ngono zembe na mambo mengine yasiyo na malengo katika maisha.

Huyu ndiye kweli Mfalme anayekuja katika ngumi za kulipwa na nchi yetu imepata bahati kubwa sana kuwa na kipaji cha bondia kama huyu.
Mpambano wa Shauri umepewa jina la “The Rumble in the City of Heaven’s Peace” (Vurumai katika Jiji la Amani)
Watanzania, tumuezi mwenzetu Ramadhani Shauri anapopeperusha bendera ya Tanzania. Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.

Imetumwa na; Onesmo Ngowi
Rais wa IBF bara la Afrika, Mashariki ya kati na Ghuba ya Uajemi
Rais wa kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Nchini (TPBC)

MENEJA MELI ILIYOZAMA ZANZIBAR AKAMATWA : TAIFA LAOMBOLEZA


Bendera zikipepea nusu mlingoti katika jengo la makao makuu ya CCM mkoani Mwanza ishara ya maombolezo.

VIFO VYA FIKIWA WATU 63, SERIKALI YATANGAZA SIKU TATU MAOMBOLEZO
 Waandishi Wetu
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Omari Hassan Mnkhon ambaye ni Meneja wa boti ya Mv Skagit, kwa ajili ya mahojiano baada ya kubainika kwamba kumekuwa na kasoro za kumbukumbu katika taarifa za hiyo.Wakati Jeshi hilo likimshikilia meneja huyo, hadi jana jioni saa 10:30, vikosi vya uokoaji vilifanikiwa kupata maiti 63, huku 29 kati yao ikiwa imetambuliwa majina namba za tiketi na sehemu wanakotoka marehemu.

Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa meneja wa boti Mkoa wa Dar es Salaam, anashikiliwa ili kuweza kusaidia jeshi la polisi kupata taarifa za kina kuhusu za meli hiyo.

Kova alisema tukio hilo linagusa maeneo mengi ikiwa ni pamoja na Mkoa wa Dar es Salaam ambako safari za meli hiyo huanzia na kuongeza kwamba, wanamshikilia meneje huyo baada ya kukosekana taarifa muhimu juu ya safari za boti hiyo.



Wananchi wakiwa kwenye foleni katika viwanja vya Maisara mjini unguja Zanzibar jana kwa ajili ya kwenda kutambua miili ya ndugu zao waliofariki kwenye ajali ya meli MV Skygat, iliyozama eneo la chumbe Zanzibar juzi. Picha na Fidelis Felix

Maiti zilizotambuliwa
Hadi saa 10 jioni jana, maiti 63 zilikuwa zimepatikana na watu 145 kuokolewa wakiwa hai. Hata hivyo kati ya maiti hizo zilizopatikana, matiti 34 zilichukuliwa na ndugu zao.

Baadhi ya maiti waliotambuliwa pamoja na umri wao na maeneo wanayoishi katika mabano ni Anita Emanuel (42, Kibamba -Dar es Salaam), Rukiya Issa Muombwa (miezi 2, Meli nne –Fuoni Zanzibar ), Halima Ali Khamis (23, Mtopepo- Zanzibar), Kolin Krispin (miezi 9, Kunduchi - Dares Salaam) na Rahma Ali Abdalla (miaka 52, Mfenesini - Zanzibar).

Maiti wengine ni Said Jumanne Masanja (miaka 9, Nzega Tabora), Sauda Abdalla Omar (22, Ole Pemba), Said Juma Said (36, Arusha), Amina Abdalla Tindwa, (miezi 6, Fuoni), Halima Ramadhani Kilimo, (53, Morogoro), Khadija Omar Ali (58), Amina Hamir Bakari (39, Chukwani - Zanzibar), Mwanahamisi Mshauri (42, Kibandamaiti), Ali Hamdu Othman (35, Mkwajuni) na Mohamed Said Salum (40, Magomeni Mikumi - Dares Salaam).

Wengine ni Amina Ahmed Ramadhani (21, Michenzani zanzibar ), Mgeni Juma Halfani (25, Daraja Bovu), Khadija Rajab Kibune (22, Fuoni), Maua Ramadhani Feruzi (29, Mwembeladu), Hussein Ali Khamis (4, Mwanakwerekwe) na Sabiha Heri Mbarouk (25, Mgeleme, Chakechake-Pemba).

Pia wamo Halima Ali Mohamed (35, Kiwengwa- Zanzibar), Asia Juma Khamis (29, Kiembe Samaki), Yusuf Hasan Yusuf (7, Chamanzi, Dar es Salaam), Batuli Abrahmani Amir (20, Jang'ombe), Fatma Said Sultani (54, Msasani Dar es Salaam), Juma Jafari Shajak (Miezi 6, Kimaneta - Tanga) na Mohamed Ali Ngombe (41, Buguruni - Dares Salaam).



Serikali yatangaza siku
tatu za maombolezo

Kufuatia msiba huo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imetangaza siku tatu za maombolezo kuanzia Julai 19 hadi Julai 21 mwaka huu.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohammed Shein alisema bendera zote zitapepea nusu mlingoti na shughuli zote zinazoambatana na sherehe na burudani zimefutwa kwa muda huo lakini kazi na shughuli za Serikali zitaendelea kama kawaida

Nayo Serikali kupitia kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi ilitangaza siku tatu za maombolezo kufuatia msiba huo mkubwa uliolikumba taifa.

Rais Shein amewahakikishia wananchi na hasa waliopoteza jamaa zao kuwa Serikali itabeba gharama zote za mazishi na huduma za matibabu kwa majeruhi.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadick alisema kutokana na maagizo ya Waziri Mkuu aliyoyatoa Bungeni Mkoa wa Dar es Salaam ndio umepewa jukumu la kushuhulikia suala hilo. Alisema kwa sasa mkoa Umepanga kutoa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya kuhifadhi mili ya watu waliofariki katika ajali hiyo. “Watu wote ambao wanajua kuwa ndugu zao walisafiri na meli hiyo wafike katika bandari ya Dar es Salaam kwa ajili ya utambuzi,” alisema na kuongeza kuwa ambayo haitatambuliwa Serikali itachukua jukumu la kuizika.

EU yatoa ndege ya uokoaji
Katika kuonyesha kuguswa na ajali hiyo, Umoja wa Ulaya (EU) umetoa ndege maalum kusaidia juhudi za utafutaji na uokoaji katika eneo la ajali.

Balozi wa Uingereza hapa nchini Diane Corner aliwaambia waandishi wa habari mjini Zanzibar kuwa wameamua kutoa msaada wa ndege hiyo ambayo iliwasaili Zanzibar usiku wa kuamkia Julai 19, kitokea katika visiwa vya Ushelisheli. “Nawapa pole watu wa Zanzibar kwa msiba huu, nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana, hasa nilipoziona maiti saba za watoto wadogo. Moyo wangu umeumia sana,” alisema huku akibubujikwa machozi.

Wabunge wachangia maafa
Katika hatua nyingine, wabunge wote watakatwa posho ya siku moja kuchangia maafa ya kuzama kwa boti hiyo huku Bunge likiahirishwa kwa siku moja kuomboleza maafa hayo.

Posho hizo za wabunge zitawezesha kupatikana kwa Sh24.6 milioni kutoka kwa Wabunge wa sasa 352 ambao kila mmoja atachagia Sh70,000.

Wakizungumza baada ya ajali hiyo, baadhi ya wabunge waliitupia lawama Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), kwa kile walichodai kuwa ilishindwa kutoa taarifa ya tahadhari kwa watumiaji wa usafiri wa majini.

Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde alisema mamlaka hiyo inabeba lawama kwa kushindwa kutoa ushauri kwa vyombo husika na badala yake wanafanya kazi ya kutabiri mvua tu.

Mbali na Mamlaka ya Hali ya hewa, lakini mbunge huyo alitaka pia wakaguzi wa vyombo vya majini kuwajibika kwa kushindwa kukagua uimara wa vyombo hivyo.

TMA watoa kauli
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), Dk Hamza Kabelwa alisema kuwa, kupitia ofisi yao iliyopo bandarini Dar es Salaam walitoa taarifa kwenye vyombo vya usafiri wa majini juu ya upepo mkali uliokuwa ukivuma baharini kwa kasi ya kilometa tatu kwa saa kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 5:00 asubuhi. “Tulipogundua hali hiyo tulitoa taarifa kwa wahusika wa vyombo vya usafiri wa majini tu,” alifafanua Dk Kabelwa.
Meli ya Skagit ilitengenezwa mwaka 1989 nchini Marekani na ilikuja nchini 2008.
SOMA ZAIDI GAZETI LA MWANANCHI

SHUGHULI ZA KUTAMBULIWA MAITI ZILIZOOKOLEWA KATIKA AJALI YA MELI ZILIENDELEA ZANZIBAR JANA



Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli ya Skagit iliozama hapo jana zikitambuliwa na Ndugu zao na kuruhusiwa Kuzichukuwa kwa ajili ya Kufanya taratibu za mazishi hapo katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar jana.

Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli ya Skagit iliozama hapo jana zikitambuliwa na Ndugu zao na kuruhusiwa Kuzichukuwa kwa ajili ya Kufanya taratibu za mazishi hapo katika Viwanja vya Maisara Mjini Zanzibar.


Balozi wa Marekani Nchini Tanzania Learnhat Alfonso wakatikati akionekana na huzuni Baada ya kuziona Maiti zilizookolewa katika Meli iliozama hapo jana katika Bahari ya Chumbe Zanzibar.Balozi alifika katika Viwanja vya Maisara ili kuona namna shughuli za kushughulikia maiti zinavyoendelea.

Waziri wa Mamboya ndani wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Emanuel Nchimbi alifikakatika Eneo lililohifadhiwa Maiti wa Ajali ya Meli ya Skagit ili kutambuliwa na Ndugu zao na Kupata maelezo kwa Daktari Kiongozi hayupo pichani Hapo katika Viwanja Vya Maisara Zanzibar.

Baadhi ya Maiti zilizookolewa kutoka katika Meli iliozama na kukosa watu wake zikipelekwa kuzikwa na Serikali katika Eneo la Kama lililotayarishwa makusudi kwa ajili hio.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete mwenye koti nyeusi akiwa na Makamu wapili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Seif Ali Idi wakihudhuria katika Eneo la Maisara ili kuona namna shughuli za kutambuliwa kwa Mati zilizookolewa katika Meli iliozama ya Skagit zinavyoendelea na kujuwa hatuwa za kuchukuwa.
CHANZO www.fullshangwe.blogspot.com

Thursday, July 19, 2012

DAGAA WADODA SOKO LA MWALONI KIRUMBA

Soko la dagaa kwa mwalo wa Kirumba jijini Mwanza linaonekana kudoda mara baada ya mizigo mingi ya bidhaa hiyo kuonekana sokoni hapo bila kuwa na wanunuzi kama ilivyokuwa nyakati za nyuma kwa soko hilo kushamiri wanunuzi na wachuuzi toka pande mbalimbali Afrika Mashariki.

Ni msimu wa mauzo na gunia moja linauzwa shilingi 50,000/= lakini kwa sasa mali yote imedoda sokoni hapa ukilinganisha na mwaka jana ambapo gunia moja liliuzwa shilingi 100,000/= na bidhaa zilikuwa zikitoka kwa kasi licha ya bei hiyo kuwa juu.

wafanyabiashara bado hawaridhishwi na mfumo uliopo sasa ambao umeshindwa kuwabana/kuwazuia wageni kutoka Kenye na kongo kwenda kununua dagaa moja kwa moja kwa wavuvi.
Waandishi wa Habari walio maliza mafunzo ya kuripoti Habari za biashara na uchumi wakifanya mahojiano na baadhi ya wafanyabiashara soko la kimataifa Mwaloni kirumba Mwanza.

Wafanyabiashara wakisubiri wanunuzi katika soko la Kimataifa Mwaloni kirumba jijini Mwanza.

Kadri wanavyoendelea kukaa kwenye soko dagaa hushuka thamani hivyo bei nzuri ni kwa wale dagaa wapya.

Mwanahabari Florah Magabe akipata ufafanuzi kuhusu bidhaa za dagaa soko la Kimataifa Mwaloni kirumba jijini Mwanza ikiwa ni sehemu ya mafunzo ya uripoti habari za Uchumi na Biashara.

Mwisho wa siku wafanyabiashara hao 'waliungishwa' na waandishi hao kwa kununuliwa bidhaa zao.

Picha ya pamoja kwa washiriki mafunzo ya Uchumi na Biashara pamoja na mwalimu wetu Mr. Mnaku (aliyesimama kulia mwenye begi mgongoni).

MH MKONO ATIMIZA AHADI YAKE YA KUPELEKA MADAWATI KATIKA SEKONDARI YA BUTUGURI

Gari kutoka Halmashauri ya Musoma likiwa linapakia madawati yaliyotengenezwa na TASAF tayari kurudishwa kwenye Halmashauri


Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondary Butuguri Godfrey Robert


Moja ya Madawati yaliyotengenezwa na Mh Mkono


Wadau wakiangalia baadhi ya Madawati yaliyotengenezwa na TASAF
MUSOMA
Na
MBUNGE wa Jimbo la Musoma Vijijini Nimroadi Mkono amekamilisha ahadi yake ya kupeleka Madawati mapya katika shule ya sekondari Butuguri baada ya kubainika kuwa madawati yaliyotengenezwa na mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika shule hiyo hayana ubora.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupokea awamu ya kwanza ya Madawati zaidi ya 50,diwani wa kata ya Butuguri Mwita Charles alimpongeza Mbunge huyo kwa kukamilisha ahadi hiyo huku akitoa wito kwa viongozi wengine kuiga mfano huo.

Diwani huyo alisema kuwa Madawati yaliyotengenezwa na TASAF hayana ubora na hivyo anaunga mkono kauli ya Mh Mbunge kuyarudisha Madawati hayo katika Halmashauri ya Musoma.

Kuhusu wale wote waliohusika katika ubadhilifu huo diwani huyo alisema kuwa wanatakiwa kuchukuliwa hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa viongozi wengine ambao wapo kwa masilahi yao.

Naye Mwalimu mkuu Wa Shule hiyo Godfrey Robert alisemshukuru Mbunge huyo na kusema kuwa amesaidia kupunguza mzigo kwa wazazi katika kukabiliana na upungufu wa madawati uliokuwepo shuleni hapo.

Amesema Madawati yaliyokuwepo hayatoshi ikilinganishwa na idadi ya wanafunzi waliopo katika shule hiyo,na hivyo mwaka huu walikuwa na mpango wa kutengeneza madawati hayo.

Aidha madawati yote yaliyotengenezwa na mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF tayari yamerudishwa katika halmashauri ya Musoma Vijijini kutokana na kutokuwa na kiwango kinachokubalika

Hivi karibuni akifanya ziara shuleni hapo mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini Nimrodi Mkono aliyakataa madawati zaidi ya 1000 yaliyotengenezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kutokana na kutokuwa na kiwango chenye ubora

CASTLE LAGER SUPER FAN YASHIKA KASI NCHINI TANZANIA

Tairosy Augustino Masangula mkazi wa Iringa Tanzania akishangilia mara baada ya kufanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kushindania nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye kuunda timu ya Castle Lager Supafan ya Afica Afica United Team itakayokuwa nchini Afrika ya kusini kushangilia mashindano ya Africon mwakani.


Keneth Gwivammkazi wa Iringa Tanzania akishangilia mara baada ya kufanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kushindania nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye kuunda timu ya Castle Lager Supafan ya Afica Afica United Team itakayokuwa nchini Afrika ya kusini kushangilia mashindano ya Africon mwakani.


Happy Chatanda Mshindo Iringawa Iringa Tanzania akishangilia mara baada ya kufanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kushindania nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye kuunda timu ya Castle Lager Supafan ya Afica Afica United Team itakayokuwa nchini Afrika ya kusini kushangilia mashindano ya Africon mwakani.


Philipo Kidongososi wa Iringa Tanzania akishangilia mara baada ya kufanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kushindania nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye kuunda timu ya Castle Lager Supafan ya Afica Afica United Team itakayokuwa nchini Afrika ya kusini kushangilia mashindano ya Africon mwakani.


Stanley godfrey wa mwanjelwa Tanzania akishangilia mara baada ya kufanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kushindania nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye kuunda timu ya Castle Lager Supafan ya Afica Afica United Team itakayokuwa nchini Afrika ya kusini kushangilia mashindano ya Africon mwakani.


Keneth mwaiselo wa Airport mbeya Tanzania akishangilia mara baada ya kufanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kushindania nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye kuunda timu ya Castle Lager Supafan ya Afica Afica United Team itakayokuwa nchini Afrika ya kusini kushangilia mashindano ya Africon mwakani.


Michael Rocky manyoni wa singida Tanzania akishangilia mara baada ya kufanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kushindania nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye kuunda timu ya Castle Lager Supafan ya Afica Afica United Team itakayokuwa nchini Afrika ya kusini kushangilia mashindano ya Africon mwakani.


David Kihenge wa Mtwara Tanzania akishangilia mara baada ya kufanikiwa kuingia katika kinyanganyiro cha kushindania nafasi ya kuwakilisha nchi kwenye kuunda timu ya Castle Lager Supafan ya Afica Afica United Team itakayokuwa nchini Afrika ya kusini kushangilia mashindano ya Africon mwakani.
Picha zote kwa Hisani ya Intellectuals Communications Limited