ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 10, 2024

Friday, August 9, 2024

KILA ABIRIA ATAKAYEPANDA NDEGE UTAPANDWA MTI JIJINI MWANZA NA VIA AVIATION


 NA ALBERT GSENGO/MWANZA

Utafiti umebaini kuwa viumbehai wa kuvutia kama ndege, mimea na wanyama siku moja wanaweza kufutika katika uso wa dunia kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira unaofanywa na binadamu ambao hivi sasa umeleta mabadiliko ya tabia nchi. Wataalam wanasema mabadiliko ya tabianchi yanatokana na tabia ya watu kukata miti hovyo na kuiacha ardhi ikiwa uchi hivyo kuongeza hewa chafu ya ukaa angani ambayo uzalishwa na viwanda, vyombo vya usafiri nchi kavu, majini na angani pamoja na uchomaji taka hivyo kuleta athari kubwa kwa viumbehai wote ambao wanakuwa katika hatari ya kutoweka katika uso wa Dunia. Kwa kuliona hilo wadau wa maendeleo taasisi isiyo ya kiserikali inayotoa huduma mbalimbali za ndege VIA AVIATION Mwanza inakuja na kampeni ya 'MTI MMOJA KWA KILA HUDUMA' yaani kila mteja atakaye kata tiketi ya ndege kupitia wakala ya kampuni hiyo basi utapandwa mti kwaajili ya kutunza mazingira

WAPIGA KURA WAPYA LAKI NNE KUANDIKISHWA SHINYANGA NA MWANZA

 

Mwenyekiti Wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe.Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele, akizungumza wakati akifungua mkutano wa siku moja wa Tume na Wadau wa Uchaguzi uliofanyika leo Agosti 09, 2024 mkoani Mwanza.Wadau hao ni pamoja na Viongozi wa vyama vya siasa, Viongozi wa Dini, Wawakilishi wa Asasi za Kiraia, Wahariri wa Vyombo vya habari, Waandishi wa habari, Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri, Wawakilishi wa Makundi mbalimbali ya Vijana, Watu wenye ulemavu, Wanawake na Wazee wa Kimila.
Mwenyekiti Wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe.Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele, akizungumza wakati akifungua mkutano wa siku moja wa Tume na Wadau wa Uchaguzi uliofanyika leo Agosti 09, 2024 mkoani Mwanza.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima, R.K  akiwasilisha mada kuhusu maandalizi ya Uboreshaji. 

Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe.Jaji Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk, akizungumza wakati akifungua mkutano wa siku moja wa Tume na Wadau wa Uchaguzi uliofanyika leo Agosti 09, 2024 mkoani Mwanza.Wadau hao ni pamoja na Viongozi wa vyama vya siasa, Viongozi wa Dini, Wawakilishi wa Asasi za Kiraia, Wahariri wa Vyombo vya habari, Waandishi wa habari, Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri, Wawakilishi wa Makundi mbalimbali ya Vijana, Watu wenye ulemavu, Wanawake na Wazee wa Kimila.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Kisheria wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Seleman Mtibora akiwasilisha mada kwa niaba ya Mkurugenzi wa Uchaguzi mkoani Shinyanga. 
****************
Na. Mwandishi wetu, Mwanza
Uoreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mkoani Mwanza na Shinyanga utafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 21 hadi 27 Agosti, 2024 ambapo jumla ya wapiga kura wapya 400,082 wanatarajiwa kuandikishwa. 

Hayo yamesemwa leo tarehe 09 Agosti, 2024 kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Wadau wa Uchaguzi iliyofanyika mkoani Mwanza na Shinyanga.

Mkoani Mwanza mkutano wa wadau umefunguliwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele na mkoani Shinyanga mkutano umefunguliwa na Makamu Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk.  

Viongozi hao wa Tume wamewataka wadau hao wa uchaguzi kuhamasisha wananchi na wapiga kura kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao ili zoezi lifanyike kwa ufanisi.
 
Katika mikutano hiyo mada ya Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Bw. Kailima Ramadhani imebainisha kuwa mkoani Shinyanga wapiga kura wapya 209,951 wataandikishwa na mkoani Mwanza wapiga kura wapya 190,131 wataandikishwa na kufanya jumla ya wanaotarajiwa kuandikishwa kuwa 400,082. 

“Kwa mkoa wa Mwanza Tume inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 190,131. Hii ikiwa ni ongezeko la asilimia 10.3 ya wapiga kura 1,845,816 waliopo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

 Hivyo, Tume inatarajia baada ya uandikishaji Mkoa wa Mwanza utakuwa na wapiga kura 2,035,947,” amesema Bw. Kailima. 

“Kwa mkoa wa Shinyanga Tume inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 209,951. Hii ikiwa ni ongezeko la asilimia 21 ya wapiga kura 995,918 waliopo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.

 Hivyo, Tume inatarajia baada ya uandikishaji Mkoa wa Shinyanga utakuwa na wapiga kura 1,205,869,” amesema Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Kisheria wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Seleman Mtibora ambaye amewasilisha mada kwa niaba ya Mkurugenzi wa Uchaguzi mkoani Shinyanga. 

Bw. Kailima amefafanua kuwa idadi hiyo inatokana na makisio yaliyofanywa kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 na kwamba inaweza kuongezeka. 

Uzinduzi wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ulifanyika mkoani Kigoma tarehe 20 Julai, 2024 ambapo ulienda sambamba na kuanza kwa mzunguko wa kwanza wa uboreshaji kwenye mikoa mitatu ya Kigoma, Tabora na Katavi na kufuatiwa na mzunguko wa pili umejumuisha mikoa ya Geita na Kagera. 

Kwa sasa, uboreshaji wa Daftari unaendelea kwenye mikoa hiyo ya Kagera na Geita hadi tarehe 11 Agosti, 2024 ambapo vituo vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
Viongozi na wawakilishi wa vyama mbalimbali vya siasa wakishiriki katika mkutano huo



Wadau mbalimbali wa Uchaguzi kutoka mkoa wa Mwanza wakiwa katika mkutano huo.
 
Wadau mbalimbali wa Uchaguzi kutoka mkoa wa Mwanza wakiwa katika mkutano huo.

Wadau mbalimbali wa Uchaguzi kutoka mkoa wa Shinyanga wakiwa katika mkutano huo.

Wadau mbalimbali wa Uchaguzi kutoka mkoa wa Mwanza wakiwa katika mkutano huo.

NISHATI SAFI YA KUPIKIA AJENDA YA KITAIFA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy akielezea ufanisi wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa wananchi waliotembelea Banda la Wakala, Nzuguni Jijini Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewaasa wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuokoa gharama na muda, kulinda mazingira na afya zao hasa ikizingatiwa kuwa teknolojia sasa imeboreshwa na gharama yake ni nafuu ikilinganishwa na nishati zingine. 


Mhandisi Saidy ametoa rai hiyo Agosti 8, 2024 mbele ya wananchi waliotembelea Banda la REA katika Maonesho ya Siku Kuu ya Wakulima (Nane Nane), Nzuguni Jijini Dodoma. 

"Tunaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia kwani ni salama, rafiki na gharama yake ni nafuu kwani teknolojia sasa imeboreshwa," amesema Mhandisi Saidy. 


 Mhandisi Saidy amesema ipo dhana ambayo imejengeka katika jamii kuwa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ni ghali na si salama na pia chakula kinachopikwa kutokana nayo hakina ladha suala ambalo alisisitiza halina kweli. 


"Ninawathibitishia Nishati Safi ya Kupikia ni salama kuliko nishati zingine tulizozizoea, niwatoe wasiwasi katika hili na tunaendelea kutoa elimu kuhusu usalama na umuhimu wa nishati hii bora," amesema Mhandisi Saidy.

Akizungumzia upatikanaji wa Nishati Safi ya Kupikia kwa wote, amesema Serikali imetoa ruzuku katika usambazaji wa Mitungi ya Gesi (LPG) na Majiko Banifu ili kuvutia wawekezaji wengi na pia kumuwezesha kila mwananchi aweze kumudu gharama zake. 


"Serikali imekuja na mfumo wa kumrahisishia kila mwananchi hususan yule mwenye kipato cha chini kumudu gharama ya Nishati Safi ya Kupikia kokote aliko ili aachane na matumizi ya nishati nyingine," amefafanua Mhandisi Saidy. 


Amesema Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipatia REA jukumu la kuhakikisha inasimamia vyema utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034 ili kufikia 2034 asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia Nishati Safi ya Kupikia. 

"Tunamshukuru Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutuamini na kutupatia jukumu hilo kubwa na tayari kwa kushirikiana na wadau tumeanza utekelezaji wake na tunakwenda vizuri," amefafanua Mhandisi Saidy. 


Amesema hatua inayoendelea sasa ni kuibua na kuwawezesha wazalishaji wengi wa vifaa vya Nishati Safi ya Kupikia ili kuongeza umahiri sambamba na kuwawezesha kutengeneza bidhaa nyingi kwa gharama nafuu na kwa ubora wa kimataifa," amesema. 


Amesema kwa kufanya hivyo kutakuwa na ongezeko la matumizi ya nishati safi ya kupikia, ongezeko la ajira na hivyo kukuwa kwa uchumi.

Monday, August 5, 2024

VIDEO;- CHADEMA KIMEWAKA WENJE ATANGAZA KUMNG'OA TUNDU LISSU NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI

NA ALBERT GSENGO/MWANZA

Joto la uchaguzi ndani ya CHADEMA limeanza kupamba moto, baada ya Ezekia Wenje kutangaza nia ya kuwania nafasi ya makamu mwenyekiti wa chama hicho Bara. Wenje ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Kanda ya Victoria CHADEMA yenye mikoa ya Mwanza, Kagera na Geita, anakusudia kujitosa kuomba ridhaa ya nafasi hiyo ambayo kwa sasa inashikiliwa na Tundu Lissu. Mbunge huyo wa zamani wa Nyamagama, Mkoa wa Mwanza amesema hayo leo Jumatatu Agosti 5, 2024 alipozungumza na waandishi wa habari juu ya kusudio lake hilo, akisisitiza ameamua kuwania nafasi hiyo, ili kuongeza ufanisi wa kazi na uwajibikaji.

CRDB Bank Marathon Congo yakusanya Dola 50,000 kusaidia wodi ya watoto Hospitali ya Jason Sendwe DRC

 

Gavana wa Jimbo la Haut-Katanga, Jacques Kyabula (katikati) akimkabaizi mfano wa hundi yenye thamani ya Dola za Marekani 50,000 Waziri wa Afya, Joseph Nsambi Bulanda wa Haut-Katanga (watatu kulia), zilizokusanywa katika CRDB Bank Marathon Congo iliyofanyika leo Agosti 4 2024 katika jiji la Lubumbashi DRC. Wengine pichani ni Balozi wa Tanzania nchini DRC, Said Mshana (wapili kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Kundi la Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay (watatu kushoto), Mwenyekiti wa Bodi wa CRDB Bank DRC, Dkt. Fred Msemwa (wapili kushoto), Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Benki ya CRDB, Bruce Mwile (wakwanza kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank DRC, Jessica Nyachiro.
Lubumbashi – CRDB Bank Marathon imefanyika leo kwa mara ya kwanza nje ya mipaka ya Tanzania katika jiji la Lubumbashi ambapo zaidi ya wakimbiaji 1,000 wameshirikina kufanikisha lengo la kukusanya USD 50,000 kwa ajili ya kusaidia wodi ya watoto katikaHospitali ya Jason Sendwe.

Mgeni rasmi katika mbio hizo ambazo zimewekahistoria katika marathon ambazo zimewahikufanyika katika jiji la Lubumbashi alikuwa ni Gavana wa Jimbo la Haut-Katanga Mhe. Jacques Kyabula ambaye aliambatana na mawaziri 10 wa Jimbo hilo wakiongozwa na Waziri wa Michezo, pamoja na Waziri wa Afya.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mbiohizo za hisani zilizobeba kaulimbiu isemayo‘Tabasamu Limevuka Mipaka’ Gavana Kyabulaameipongeza Benki ya CRDB kwa kuwaletapamoja WaCongo pamoja na washiriki kutoka mataifa ya jirani kuja kuchangia kuboreshahuduma za afya kwa watoto na kukuza ustawi wa jamii.

"Tunaishukuru CRDB Bank Marathon kwa kusaidia jitihada za Serikali kuboresha huduma za afya kwa wananchi. Serikali yetu inatoakipaumbele kikubwa katika afya, na tunafurahishwa na jitihada zinazofanywa na Benki ya CRDB katika kusaidia kuboresha afyaya watoto," alisema Gavana Kyabula.
Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchiniDRC, Balozi Said Mshana aliipongeza Benki ya CRDB kwa juhudi zake za kukuza mahusianoya kimataifa na kuimarisha umoja na mshikamano katika jamii. Balozi Mshanaalisema mbio hizo zilizozaliwa Tanzania zinaonyesha ubunifu ambao taasisi za kitanzania zinaweza kupeleka nje ya nchi katikakusaidia kukuza ustawi wa jamii.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Bank DRC, Dkt. Fred Msemwa alieleza kuwa marathon hiyoni sehemu ya mkakati wa Benki kusaidia juhudiza serikali katika kukuza ustawi wa watu wa Congo. "Marathon hii si tu inahamasishamichezo, bali pia inajenga utamaduni wa kujitolea kwa jamii.

Benki yetu inaamini kwa kuwaleta watu pamoja tunaweza kuyafikiamakundi mengi kwa urahisi na hivyo kukuza ustawi wa jamii kupitia programu bunifu kama CRDB Bank Marathon, lakini pia kupitia huduma na bidhaa zetu bunifu tutaweza kusaidia jitihadaza kukuza ujumuishi wa kifedha na kiuchumi," alisema.
Akitangaza matokeo ya mbio hizo, MkurugenziMtendaji wa CRDB Bank Congo, Jessica Nyachiro, aliwashukuru washirika wa mbio hizoAfricell, Orange, Ogowe Cleaning, Kin Marche, Policlynique Delta, Shalina, Vinmart Foundation, SUNU Insurance, na Dukan. “Pamoja na kuwahuu ni mwaka wa kwanza kwa mbio hizi lakinimwitikio umekuwa mkubwa sana. Tunawashukuru sana washirika wetu na wakimbiaji wote mlioungana nasi kusambazatabasamu kwa watoto.”

Marathon iliyofanyika leo Lubumbashi ni ya kwanza kati ya tatu ambazo zimepangwakufanyika mwaka huu nchini DRC, Burundi, na Tanzania. Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation ambao ndio waandaji wa mbio hizo, Tully Esther Mwambapa ameeleza furaha yakebaada ya mbio hizo zilivyopokelewa vizuri sana nchini DRC.

Tully amewashukuru Watanzania ambaowamejitokeza kwa wingi kushiriki mbio hizo za DRC ikiwamo kuwashukuru washirika wakuu wa mbio hizo Sanlam, CRDB Insurance Company, na Clouds Media. "Nitumie nafasi hiikuwakaribisha watu wote kuendelea kujisajilikwa mbio za Burundi tarehe 11 Agosti na Tanzania tarehe 18 Agosti," aliongezea.

Papy Kayombo, mshindi wa mbio za Kilometa21 katika CRDB Bank Marathon Congo, ameeleza furaha yake ya kushiriki katika mbiohizo na kusema ushindi wake ni sehemu ya kusambaza tabasamu kwa watoto ambaowatapata matibabu katika hospitali ya Jason Sendwe.

Kayombo alisema, "Katika jiji la Lubumbashi utamaduni huu ni mpya na ninaonautasaidia sana kujenga mshikamano katikajamii. Naipongeza sana Benki hii yetu ya CRDB, imeonyesha upendo mkubwa sana kwa watotowetu na sisi tunaahidi kuiunga mkono."

Viongozi hao pia waliambatana na Balozi wa Tanzania nchini DRC, Balozi Said Mshana, Balozi wa Burundi nchini DRC, pamoja viongozimbalimbali wa Benki ya CRDB wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, na Kaimu MkurugenziMtendaji wa Benki ya CRDB, Bruce Mwile.




PROFESA ASSAD ATAKA USHIRIKIANO UJENZI WA HOSPITALI YA KIISLAMU TANGA

 

Na Oscar Assenga, TANGA.

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) wa zamani Profesa Mussa Assad amesema ni umuhimu kuwepo kwa ushirikiano wa pamoja ili kuhakikisha ujenzi wa Hospitali ya Kiislamu Mkoani Tanga unakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma.

Profesa Assad aliyasema hayo mwishoni mwa wiki Jijini Tanga wakati aliposhiriki kwenye Kongamano la tathimini ujenzi wa Hospitali ya Kiislamu Mkoa wa Tanga lililokwenda sambamba na kufanyika kwa harambee ya kuchangia ujenzi wake huku akieleza ni ushirikiano ni lazima wawe wamoja katika kufanikisha hilo.
Harambee hiyo ilikwenda sambamba na uliokwenda sambamba na kukagua eneo la Ujenzi wa Hospitali hiyo lililopo Kata ya Masiwani, Kupanda miti ya Matunda pamoja na kuweka jiwe la Msingi.

Alisema kwa sababu jambo ambalo linafanyika ni la kuokoa maisha na ukiokoa maisha ya mtu mmoja utakuwa umeokoa maisha ya watu wote kwani hata vitabu vitakatifu vya Mungu (Quran) vimeandikwa hilo.

“Hata vitabu vitakatifu vya Mwenyezi Mungu vinaeleza kumtibu mtu mmoja na kuyaokoa maisha yake ni sawa utakuwa umeuokoa umma nzima lakini tatizo ambalo analiona ni ajizi kwamba wanafikiria hawawezi leo kufanya jambo hilo labda wasubiri kesho itawezakena na mwisho miaka inapita anzeni sasa”Alisema.

“Hilo ni tatizo kubwa la ajizi hivyo tuondoe ajizi tulifanye kazi hi kwa ushirikiano mkubwa ili kuweza kutimiza malengo tuliojiwekea ya kuhakikisha ujenzi wa eneo hilo unaendelea “Alisema

“Leo nimefurahi kwa sababu kuna kazi kubwa imefanywa na amesikitika hatua zake zimekwenda taratibu mno na nimekuwa nikipita sana kwenye eneo hilo kila mwezi kwenda Tongoni na wala sijasikia kuwepo wa shughuli hizi pia kinachomsikitisha zaidi ni kumetolewa nondo 72 katika ujenzi huu”Alisema

Aidha alisema maana yake hawajali vitu vyao wenyewe hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wakifanya vitu hapo vilindwa ili kuepusha kuibiwa na wezi jambo ambalo litapelekea kuepukana na vitendo hivyo.

“Lakini niwasihi katika jambo hilo tuwe pamoja na kuongeza mshikamano ili kulifanikisha jambo hilo na mwakani mungu akipenda kutakuwa wamepandisha jengo pia tutaendelea kuona namna wadau mbalimbali wanaweza kuchangia kwenye ujenzi huu”Alisema

Kwa makadirio ya Fedha za ujenzi wa Hosptali hiyo unakadiriwa kuwa ni zaidi ya Sh.Bilioni 2.4 sio fedha ndogo hivyo ni lazima waone namna ya wao wenyewe wajipange wafanya juhudi kubwa za kuanza kazi hiyo na wao waanze wenyewe na wao watakaoona hivyo wanaweza kuona namna ya wadau wengine kuwaunga mkono.

“Lakini niwaambie kwamba Mwenyezi Mungu akijalia nikirudi Dar nitahamasisha wenzangu kuona namna nzuri ya kuliendelea jengo hlo lianze haraka sana kutokana na umuhimu mkubwa lilikokuwa nalo”Alisema

Alisema kwamba Mwenyezi Mungu amewajalia neema nyingi waislamu hivyo ni vema wajiulize wameifanyia nini hiyo neema ya umri wamekaa miaka miwili jengo hilo hivyo maana yake wamefanya ajizi na hawakufanya hima ya kutekeleza kazi hiyo.

“Jambo la muhimu ni kujikumbusha kwamba tumepewa neema ya umri siku zinavyokwenda tujipime namna gani tumefanya kazi hizo inshallah Mwenyezi Mungu ajalie tukae pamoja juhudi hizi ziendelezwe ili mwakani tusiwe na msingi tuwe tumepanda kama sio ghorofa moja itakuwa ghorofa mbili na hilo tutaliweza kama tutakuwa wamoja”Alisema

Awali akizungumza kuhusu mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali inayozingatia maadili ya Kiislamu Mjumbe wa Halmashauri Kuu wa Baraza la Waislamu Taifa (Bakwata) Sheikh Khamis Mataka alisema kwamba MwenyeziMungu atalipa nguvu jambo hilo ili litimie na uwezo huo wanao.

Alisema kwamba uwezo wa kulitimiza jambo hilo upo ndani yao wao wenyewe wakiondokana na matatizo na changamoto walizojiwekea wao wenyewe wataona namna suala hilo litakavyopata mafanikio.

Naye kwa upande wake Dkt Ally Fungo alisema kwamba mradi huo wa kimkakati umedhamiria kutatua tatizo la kimkakati kama halitatatuliwa litaadhidhiri dhamira ya jamii ya kiislamu kwa kwa maana hapo watakuwa na kituo cha afya cha kutoka tiba kinachzingtia maadili ya kiislamu ambayo ni ya kibinadamu.

Alisema kwamba hospitali hiyo haitakuwa ya waislamu pekee bali wote lakini haiwezekani wakina mama wakatibiwa na daktari mwanaume hiyo ni hospitali ya kimkakati kutatua kimkakati hospitali ya waislamu wenyewe kwa fedha zao wenyewe.

“Hospitali hii itakuwa na majengo sana kuanzia Jengo la Utawala, Jengo la Madaktari,Wodi za Wakina Mama, Kina Baba, Maabara, Mochwari na nyenginezo na gharama zake kwa awali tungetumia Bilioni 1.5 lakini kipindi kimepita miaka mitatu iliyopita”Alisema

Hata hivyo alisema kutokana na uchumi duniani kuadhirika hivyo sasa wamefanya ufuatiliaji vitu vimebadilika na bei ya vitu imeongezeka na hivyo watalazimika watumie bilioni 2.4 hilo sio jambo dogo ni kubwa hivyo watashirikiana na wadau wote kufanikisha.










Sunday, August 4, 2024

WAZIRI MKENDA AZINDUA BODI YA USHAURI CHUO CHA ADEM BAGAMOYO

NA VICTOR MASANGU/BAGAMOYO

SAUTI NA ALBERT GSENGO

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Pro Adolfu Mkenda amezindua Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu - Adem ambapo ameitaka Bodi hiyo kuhakikisha inafanya Tafiti na kusimamia Kwa weledi Mkubwa Ili kuweza kuisaidia Serikali Kupitia Wizara ya Elimu

Akizungumza Wakati wa hafla hiyo fupi ya uzinduzi wa Bodi hiyo amewahimiza kufanya Tafiti mbalimbali pamoja na kuwasaidia Walimu wanaofundiasha hasa katika kukidhi haja ya mitaala mpya ya Elimu ambayo imeanza kutolewa mashuleni.