ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, August 5, 2024

VIDEO;- CHADEMA KIMEWAKA WENJE ATANGAZA KUMNG'OA TUNDU LISSU NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI

NA ALBERT GSENGO/MWANZA

Joto la uchaguzi ndani ya CHADEMA limeanza kupamba moto, baada ya Ezekia Wenje kutangaza nia ya kuwania nafasi ya makamu mwenyekiti wa chama hicho Bara. Wenje ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Kanda ya Victoria CHADEMA yenye mikoa ya Mwanza, Kagera na Geita, anakusudia kujitosa kuomba ridhaa ya nafasi hiyo ambayo kwa sasa inashikiliwa na Tundu Lissu. Mbunge huyo wa zamani wa Nyamagama, Mkoa wa Mwanza amesema hayo leo Jumatatu Agosti 5, 2024 alipozungumza na waandishi wa habari juu ya kusudio lake hilo, akisisitiza ameamua kuwania nafasi hiyo, ili kuongeza ufanisi wa kazi na uwajibikaji.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.