ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 3, 2024

MWENYEKITI CCM KIBAHA MJI AMFAGILIA RAIS SAMIA KUSIMAMIA ILANI YA CHAMA KWA VITENDO


 VICTOR MASANGU,KIBAHA


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini  Mwalimu Mwajuma Nyamka amempongeza Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza Ilani ya chama kwa vitendo kutekeza miradi  pamoja na kuwatumikia wananchi katika nyanja mbali mbali.

Akizungumza na mwandishi wa habari katika mahojiano maalumu kuhusiana na maadhimisho ya miaka 47 ya kuzaliwa kwa chama cha mapindu CCM.

Mwalimu nyamka akitolea ufafanuzi zaidi alisema kwamba wananchi na wanachama wanatakiwa kutambua kwamba chama chama cha mapinduzi kimetokana na muunganiko wa chama cha TANU kwa upande wa Tanzania bara  na chama cha ASP kwa upande wa Zanzibar.

"Kwa hiyo vyama hivi viliweza kuungana kwa pamoja ndipo vikaunda chama cha mapinduzi kwa hivyo ni vizuri watu wakaelewa zaidi kupitia maadhimisho haya ya miaka 47 ya kumbukizi ya CCM,"alifafanua Mwalimu Nyamka.

Kadhalika alisema kuwa baadhi ya watu hawafamu chama cha mapinduzi kimetokana na nini hivyo kupitia maadhimisho haya ya miaka 47  wataweza kuelewa zaidi kuhusiana na CCM ilipotoka na hadi ilipo kwa sasa.

"Unapozungumzia chama cha TANU kipindi kile kirefu chake ni Tanganyika African Nation Union ambacho kilikuwa kinaongozwa na hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere,"

Kadhalika Nyamaka aliongeza kwamba chama cha mapinduzi kimeunganishwa mnamo tarehe 5 mwezi wa 2 mwaka 1977 ambapo sasa chama ndio kinatimiza miaka 47,"alifafanua Mwalimu Nyamka.

Pia alisema kwamba katika kipindi chote cha miaka 47 chama cha mapinduzi kimeweza kufanya mambo mengi sana ikiwemo katika suala la utawala pamoja na utekelezaji wa Ilani.

"Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha mapinduzi CCM ni moja ya mkataba na wananchi katika kusimamia mambo mbali mbali na kwamba ilani inasimamiwa vizuri sana na Mama yetu Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan,"alisema Nyamka

Katika hatua nyingine Mwalimu nyamka alipongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza ilani ya CCM kwa vitendo pamoja na kuwatumikia wananchi wake kuanzia kwa mtu mmoja mmoja hadi makundi kwa njia tofauti.

Aliongeza kwamba Rais Samia ameweza kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ya kimaendeleo ikiwemo Afya,Elimu,umeme,miundombinu ya barabara,maji pamoja na maeneo mengine amefanya mambo makubwa hivyo anastahili pongezi.

Katika kutekeleza Ilani ya chama kwa vitendo Rais Samia ameweza kuwakomboa wakinamama kuondokana na kutembea umbari mrefu kwa ajili ya kutafuta huduma ya maji na kupelekea kutimiza dhamira yake ya kumtua mama ndoo ya maji kichwani.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo alisema katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa ambao utafanyika mwaka huu watahakikisha wanashinda kwa kishindo na kwamba watatembea kifua mbele kutokana na kuwa na sababu za msingi za kuwaeleza wananchi.

Maadhimisho ya kuzaliwa kwa miaka 47 ya   chama cha mapinduzi (CCM) yameambatana na shughuli mbali mbali za kijamii ambazo zimefanyika katika maeneo mbali mbali ya Mkoa mzima wa Pwani.

Thursday, February 1, 2024

MADIWANI KIBAHA MJI WAITAKA DAWASA KUSHUGULIKIA KERO YA MAJI HOSPITALI YA LULANZI

 VICTOR MASANGU,PWANI.

 
HOSPITALI ya Wilaya iliyopo katika  Halmashauri ya Kibaha mji kwa sasa inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa huduma ya maji safi na salama hali ambayo inawapa wagonjwa kero na usumbufu mkubwa hasa kwa wakinama wajawazito wanapojifungua.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kibaha mji Mussa Ndomba wakati akitoa taarifa ya changamoto ya maji  katika kikao cha baraza la madiwani robo ya pili na kuiomba Dawasa kuelekeza nguvu zaidi kupeleka maji katika hospitali hiyo.

Wateja Benki ya CRDB kuzawadiwa zawadi za Sh. Milioni 470 kampeni ya Benki ni SimBanking

 

 
Dar es Salaam. Tarehe 31 Januari 2024:  Katika jitihada zake za kuhamasisha  matumizi ya mifumo ya kidijitali nchini, Benki ya CRDB imezindua msimu wa tatu wa kampeni ya ‘Benki ni SimBanking’ na kutenga jumla ya zawadi zenye thamani ya Shilingi milioni 470 mamilioni kwa wateja wake mwaka huu.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Wateja wadogo na wakati wa Benki ya CRDB, Bonaventure Paul amesema lengo la kampeni hiyo ni kujenga utamaduni wa matumizi ya kidijitali katika huduma za kifedha ili kuendana na kasi ya maendeleo na kuondokana na matumizi ya fedha taslimu.
“Maendeleo ya sayansi na teknolojia yanaihamisha dunia kutoka kwenye miamala ya fedha taslimu kwenda ile isiyohusisha fedha taslimu yaani cashless economy. Tanzania hatupaswi kuachwa nyuma, ni lazima twende na mabadiliko hayo tena kwa kasi inayostahili,” amesema Bonaventure.

Kushiriki na kujiwekea nafasi ya ushindi katika kampeni hiyo mteja anatakiwa kutumia SimBanking kufanya miamala yake yote ya kibenki ikiwamo kulipia ankara za maji, umeme au visimbusi vya television, ada, malipo ya manunuzi, kutuma pesa, kulipia kodi, mikopo ya kidijitali, kutoa fedha kwa ATM au CRDB Wakala, kulipia bima ya vyombo vya moto, na huduma nyenginezo.
“Kwa kadri mteja atakavyokuwa akifanya miamala mingi zaidi ndivyo atakavyojiwekea nafasi ya ushindi,” amesema Bonaventure huku akibainisha kuwa katika kampeni hiyo itakayoenda hadi mwisho wa mwaka, kutakuwa na washindi wa gari aina ya Toyota Dualis watakaopatikana kila baada ya miezi mitatu, huku zawadi za  bajaj na pikipiki zikitolewa kwa mshindi wa kwanza na wa pili kila mwezi.

Aidha, katika msimu huu wa tatu wa kampeni ya ‘Benki ya SimBanking’, Benki ya CRDB imetenga zawadi za kompyuta mpakato kufikia 10 kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo vikuu, zawadi za simu janja, pamoja na fedha taslimu.

Pamoja na zawadi hizi Benki hiyo pia imetenga kiasi cha Shilingi milioni 200 zitakazotolewa kupitia Tembo Points ambazo mteja atakuwa akikusanya kila anapofanya muamala. Wateja wataweza kubadili Tembo Points zao kuwa fedha na kuzitumia kulipia huduma au bidhaa.
Bonaventure amewakumbusha wateja wa  Benki ya CRDB ambao hawajakamilisha usajili wa huduma za SimBanking kukamilisha mchakato huo ili wakidhi vigezo vya kujishindia moja kati ya zawadi zilizotangazwa na kuwakaribisha wananchi wengine kufungua akaunti kwa vigezo nafuu sana na kuunganishwa na SimBanking ili kufurahia huduma zilizoboreshwa zaidi.

Benki imeendelea kuiboresha huduma yake ya SimBanking ili kutoa huduma zenye viwango vya kimataifa na uzoefu ulio bora zaidi kwa wateja.  Mwaka jana, tulizindua SimBanking App iliyoboreshwa ambayo inatumia akili mnemba (Artificial intelligence), ianyoiwezesha kuwa na uwezo mkubwa katika utambuzi wa tabia na mahitaji ya mteja pindi anapotumia.

Mapema mwaka huu Benki ya CRDB imeongeza huduma mbili mpya ndani ya SimBanking ikiwamo  huduma ya malipo kupitia Msimbomilia wa Taifa (TANQR) ikimuwezesha mteja kufanya malipo kwa watoa huduma wote wa Benki ya CRDB na hata mitandao ya simu. Huduma nyengine ni ile ya kujitengenezea Tembo Virtual Card mahsusi kufanikisha miamala ya kieletroniki popote pale duniani kwa kushirikiana na Union Pay.











Wednesday, January 31, 2024

PICHA ILIYO ACHA ALAMA JIJINI MWANZA


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Dkt.Samia Suluhu Hassan akizungumza na kusalimiana na Katibu wa NEC itikadi,uenezi na mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Paul Makonda wakati wa uzinduzi wa ugawaji wa boti za kisasa pamoja na vizimba vya kufugia samaki kwaajili ya wavuvi wa kanda ya ziwa.


Hafla hiyo imefanyika jana jijini Mwanza ambapo vitendea kazi hivyo vimegaiwa kwa wavuvi kwa mkopo usiokuwa na riba ili kustawisha maisha ya wavuvi na kukuza biashara ya samaki.

MADIWANI HALMASHAURI YA MJI KIBAHA WAIOMBA SERIKALI KUWAPATIA MAMLAKA YAO YA MAJI


NA VICTOR MASANGU KIBAHA


Baraza la madiwani katika Halmashauri ya mji Kibaha limeiomba serikali kuwaundia mamlaka yao ya maji safi ambayo itasaidia kwa kiasi kikubwa kuwahudumia wananchi kwa urahisi zaidi na kuondokana na changamoto zinazowakabili.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Kibaha  Mhe Mussa Ndomba kwa niaba ya madiwani wenzake wakati wa kikao cha baraza la madiwani kipindi cha robo ya pili.
Mhe.Ndomba alisema kwamba kwa sasa katika baadhi ya maeneo kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama hali ambayo inawapa wakati mgumu wananchi kupata huduma hiyo.

Alifafanua kwamba katika halmashauri ya mji kibaha kuna Hospitali ya Lulanzi ambayo ni ya Wilaya lakini nayo inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji hususa kwa wakinamama wanaojifungua kupata shida sana.
"Kutokana na hali hii ya changamoto ya maji tunaiomba serikali kutusaidia katika halmashauri ya Kibaha tuwe na mamlaka yetu ya maji ambayo itakuwa ni msaada mkubwa kwa wananchi wetu ukizingatia maji yote yanatokea kwetu Kibaha,"alifafanua Ndomba.

Aidha Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa endapo Kibaha ikiba ikiwa na mamlaka yake itaweza kusaidia kuwapunguzia wananchi  adha ambayo yamekuwa wakiipata.
Pia alisema kwamba kwa sasa halmashauri ya mji Kibaha imetenga kiasi cha shilingi milioni 60 kwa ajili ya kuhakikisha inaboresha miundombinu ya maji ili iweze kufika katika Hospitali ya Lulanzi ili wagonjwa waondokane na kuangaika katika suala la maji.

Kadhalika Mwenyekiti huyo aliziomba taasisi wezeshi zote kuwa na ushirikiano wa pamoja katika masuala ya kutekeleza miradi mbali mbali  ya kimaendeleo ili kuepusha usumbufu unaokuwa ukijitokeza katika utekelezaji wa miradi.

 Mwenyekiti huyo alimpongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kulifuta shirika la Elimu kibaha na kumuomba awapatie ardhi kutoka eneo hilo kwa ajili ya kulipanga na matumizi mengine ya kimaendeleo.

"Kiukweli Rais wetu amesikia kilio chetu cha siku nyingi kwa kuamua kulifuta shirika la elimu Kibaha na sisi siku nyingi kama madiwani tulikuwa tunaomba kupatiwa eneo kwa lengo la shughuli mbali mbali lakini hatukuweza kulipata,"alibaisha Ndomba.

Katika hatua nyingine Ndomba aliwataka watumishi na watendaji kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kwa kusimamia kumaliza  migogoro ya ardhi.

"Kero nyingi zinazokuja ni kuhusiana na migogoro ya ardhi ya wakati mwingine unakuta mkurugenzi anashughulikia migogoro hiyo ya ardhi ya asilimia 90 kitu ambacho kilitakiwa kimalizike katika ngazi za chini sio hadi ifike kwa mkuu wa Wilaya au mkuu wa Mkoa,"alisema Ndomba.
 Nao baadhi ya madiwani aliohudhuria katika kikao hicho walisema katika maeneo yao kumekuwa na uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara hasa katika kipindi cha mvua hivyo mamlaka husika zinapaswa kufanya matengenezo.

Aidha waliongeza kuwa suala la changamoto ya maji bado ni tatizo katika maeneo yao hivyo kuanzishwa kwa mamlaka yao kutaweza kuwa ni mkombozi mkubwa kwa wananchi.

Kikao cha baraza la madiwani katika halmashauri ya mji Kibaha kimekutana katika robo ya pili kwa ajili ya kujadili mipango mbali mbali ya kimaendeleo katika sekta tofauti,changamoto zilizopo pamoja na kuweka mikakati ya kuzitafutia ufumbuzi kupitia serikali pamoja na taasisi wezeshi.

Tuesday, January 30, 2024

RASIMU YA TAARIFA YA TATHMINI YA USHIRIKI WA WATANZANIA KATIKA MIRADI YA KIMKAKATI NCHINI KUJADILIWA

 

 Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Anderson Mutatembwa akifungua kikao kazi cha wataalam cha kujadili Rasimu ya Taarifa ya Tathmini ya Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati Uwekezaji inayotekelezwa nchini kilichofanyika Mkoani Singida, tarehe 29 Januari, 2024.


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Anderson Mutatembwa (Kulia) na Mkurugenzi Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi, Kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Condrad Millinga wakifuatilia jambo, katika kikao kazi cha wataalam cha kujadili Rasimu ya Taarifa ya Tathmini ya Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati Uwekezaji inayotekelezwa nchini kilichofanyika Mkoani Singida, tarehe 29 Januari, 2024.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uboreshaji wa Mifumo ya Masoko nchini Bw. Charles Ogutu akizungumza wakati wa kikao kazi cha wataalam cha kujadili Rasimu ya Taarifa ya Tathmini ya Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati Uwekezaji inayotekelezwa nchini kilichofanyika Mkoani Singida.

Baadhi ya Watalaam katika kikao kazi cha kujadili Rasimu ya Taarifa ya Tathmini ya Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati Uwekezaji inayotekelezwa nchini kilichofanyika Mkoani Singida.

(HABARI NA PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)







NA; MWANDISHI WETU – SINGIDA
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Anderson Mutatembwa, ameongoza kikao kazi cha wataalam kujadili Rasimu ya Taarifa ya Tathmini ya Ushiriki wa Watanzania katika Miradi ya Kimkakati Uwekezaji inayotekelezwa nchini kilichofanyika Mkoani Singida Tarehe 29 Januari, 2024.

Bw. Mutatembwa, alisema dhana ya Ushiriki wa Watanzania katika miradi ya kimkakati yaani (Local content) ni dhana inayolenga katika kuhakikisha kuwa thamani ya ziada inayopatikana kwenye uchumi kutokana na utekelezaji wa miradi ya kimkakati na uwekezaji inabaki nchini na kuchangia ukuaji wa uchumi pamoja na kunufaisha Watanzania na Taifa kwa ujumla.

Aliendelea kusema kuwa, Serikali inatekeleza dhana hii kwa kuhakikisha ajira kwa watanzania zinapatikana, uanzishwaji wa kampuni za ubia, matumizi ya malighafi zinazopatikana nchini katika uzalishaji na utoaji wa huduma, manunuzi ya bidhaa na huduma zinazozalishwa au zinazotolewa na kampuni za Kitanzania na uhawilishaji wa teknolojia.

Aidha aliongeza kusema kuwa, dhana hiyo inahakikisha uwepo wa ushiriki wa kampuni za kitanzania, na ushirikishwaji wa jamii zinazoishi katika maeneo ya uwekezaji au miradi inapotekelezwa.

Akiongea na waandishi wa habari baada ya ufunguzi wa kikao kazi hicho, Mkurugenzi Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi, Kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Condrad Millinga alisema moja ya eneo linalofanyiwa kazi katika kikao kazi hiki ni kuona watanzania watashiriki vipi hasa katika eneo la ajira za ndani kwa kuwajengea uwezo waweze kushiriki kwa maana ya wenye ujuzi na wasiokuwa na ujuzi, aidha kuangalia eneo la matumizi ya malighafi na rasilimali zilizopo nchini katika miradi mikubwa.
“Tunauzalishaji unaotumika lakini kwa kiwango kidogo sana kulinganisha na mahitaji halisi, kumbe tunahitaji wenyewe kujipanga ndani lakini pia kushirikiana na wenzetu wanaotoka nje ili kuzalisha kulingana na mahitaji katika maeneo ya Uwekezaji,” Alisisitiza

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uboreshaji wa Mifumo ya masoko Nchini Bw. Charles Ogutu alisema mapitio ya rasimu hiyo yatahakikisha kwamba wanatanzania wanashirki kikamilifu na kunufaika na miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa nchini.

“Bila kusahau kwamba hakuna mradi mkubwa ambao hautegemei kilimo kwa hiyo tunakitazama kilimo kama ndiyo sekta mama inayobeba sekta zote kwa hiyo ni vizuri sana mazingira ya kibiashara na mazingira yote katika sekta ya uwekezaji zijumuishe sekta ya Kilimo.” Alibainisha

Akiongea katika kikao kazi hicho kilichohusisha wataalam kutoka Serikali kuu,Taasisi, MDA’s na sekta binafsi mtaalam wa uwekezaji wa Kimataifa (FDI) na Uchumi mkubwa Dkt. Juma Makaranga alisema ni muhimu kwa makampuni ya ndani kufanya biashara na makampuni makubwa ya nje kwa kusaidiwa kutengenezwa na kuwainua kiteknolojia, usimamizi na kitaaluma.

KISHINDO KIKUBWA KUWEKWA WAKFU NA KUSIMIKWA KWA ASKOFU JOVITUS MWIJAGE WA JIMBO LA BUKOBA

 

Askofu mwijage (katikati) mwenye fimbo akiwa na baadhi ya maaskofu waliohudhuria ibada hiyo
Askofu Mwijage akikabidhiwa fimbo na Kardinali Rugambwa wa Jimbo Kuu la Tabora katika ibada hiyo.
Msemo wa kihaya usemeo “Tikiliwa Igamba”ambalo tafsiri yake ni “tukio ambalo litabaki simulizi” ulidhihirika wakati wa tukio kubwa la kihistoria la kuwekwa wakfu na kusimikwa kwa Askofu Jovitus Francis Mwijage, wa jimbo la Katoliki la Bukoba, lililofanyika mjini Bukoba mkoani Kagera.

Mikimiki na shamrashamra za maandalizi ya tukio hilo kubwa la kihistoria katika jimbo la Bukoba ilianzia kwenye ngazi za familia za wakristo, Vigango, Parokia mpaka jimboni ambako ilihitimishwa na misa takatifu iliyofanyika katika uwanja wa Kaitaba ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Naibu Waziri Mkuu wa Waziri wa Nishati, Mh. Doto Biteko, aliyemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh.Samia Suluhu Hassan.

Misa hiyo iliyoongozwa na Kardinali Protace Rugambwa, Askofu Mkuu wa jimbo kuu la Tabora akisaidiana na aliyekuwa Msimamizi wa Kitume jimbo la Bukoba, Askofu Methodius Kilaini na Askofu Almachius Rweyongeza wa Jimbo la Kayanga, ilihudhuriwa na maaskofu kutoka majimbo mbalimbali nchini, viongozi wa Serikali mkoani Kagera wakiongozwa na Mkuu wa mkoa Fatma Mwassa ,watawa wa kiume na kike, viongozi wa maadhehebu mbalimbali , maelfu ya waumini kutoka parokia mbalimbali za jimbo Katoliki la Bukoba na majimbo jirani waliojawa na bashasha na furaha ya kumpata Askofu mpya.
Kwaya mbalimbali zikitumbuiza wakati wa kumkaribisha Askofu Mwijage katika makazi yake yaliyopo Ntungamo Bukoba.

Pia ibada hiyo ilihudhuriwa na Balozi wa Baba Mtakatifu nchini Tanzania, Askofu Mkuu Angelo Acattino.

Vikundi mbalimbali vya kwaya kuanzia za watu wazima mpaka za watoto zilizoimba katika ibada hiyo zingine kwenye maandamano kwenye sehemu za barabara alizopita Askofu Mwijage kutoka Rwamishenye hadi kanisa kuu la jimbo zilileta shamrashamra ya pekee katika mji wa Bukoba na vitongozi vyake bila kusahau wananchi wengi waliojipanga misururu barabarani kumshangilia bila kujali mvua iliyokuwa inanyesha katika maeneo mbalimbali mjini humo.

Pia kulikuwepo na tukio la mkesha wa ibada ya Masifu ya jioni iliyoongozwa na Askofu Flavian Kassala, wa Jimbo Katoliki la Geita, ambayo ulihudhuriwa na waumini wengi wakiwa wanasubiri tukio hili muhimu la kihistoria kwa shauku kubwa.
Askofu Mwijage akikaribishwa katika makazi yake yaliyopo Ntungamo Bukoba.
Askofu Mwijage akikaribishwa katika makazi yake yaliyopo Ntungamo Bukoba.

Akiwasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mh.Samia Suluhu Hassan, katika ibada hiyo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mh.Doto Biteko, alisema Serikali itampa ushirikiano Askofu Mwijage na kanisa Katoliki ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Dk.Biteko, alisema Rais Samia amehimiza umuhimu wa kujenga Taifa lenye uhuru na haki kwa kuwa haki ulijenga Taifa na kusisitiza kuwa zipo changamoto zinazotukabili kama Taifa ambazo ili kuziondoa kunahitaji kuwepo na ushirikiano miongoni mwetu licha ya kutofautiana kwa mawazo na mitizamo.

Akizungumzia utendaji wa Akofu Mwijage, Dk. Biteko, alisema waumini wa Katoliki wa Bukoba wamempata kiongozi wa kiroho, Mchumi, mlezi na mbunifu anayetegemewa na wengi kuwafundisha na kuwaelekeza katika njia sahihi za kiroho na kimwili.

Awali akizungumza kabla ya kumweka wakfu, Kardinali Rugambwa, amemkubusha askofu Mwijage, kuzingatia nafasi aliyokabidhiwa kuwa ni mali ya Kristo hivyo aishi kwa wito kutekeleza utume wake kwa kumsikiliza Kristo.

“Wapende pia watawa wa kiume na wa kike ukiwaamini na kukuza mchango muhimu katika utume hapa Bukoba, wapende waamini na walei ukiwaalika na ukiwahamasisha kushiriki kikamilifu katika maisha, utume wa kanisa ili jimbo la Bukoba lipate sura ya kisinodi ya kutembea pamoja, ”alisema.

Akiongea katika ibada hiyo, Askofu Mwijage ambaye amechukua nafasi ya Askofu Desderius Rwoma aliyestaafu mwaka 2022 ,aliahidi kushirikiana na mapadri kuendeleza pale alipoacha mtangulizi wake “Kwa mapadri, watawa wa kike na wa kiume wote nawaita kuendeleza jimbo letu,watanguzi wetu walifanya kazi nzuri iliyotukuka ninawaomba tuunganishe vipaji vyetu kuendeleza jimbo kiroho na kiuchumi”,alisisisitiza.

Tukio hilo la kihistoria katika kanisa kwenye jimbo Katoliki la Bukoba liliambatana na habari ya kustaafu kwa aliyekuwa Msimamizi wa Kitume jimbo la Bukoba, Askofu Methodius Kilaini ambaye amelitumikia kanisa kwenye nafasi mbalimbali kwa uadilifu mkubwa kwa kipindi cha zaidi ya miaka 50.
Kwaya mbalimbali zikitumbuiza wakati wa kumkaribisha Askofu Mwijage katika makazi yake yaliyopo Ntungamo Bukoba.
Askofu Mwijage akikaribishwa katika makazi yake yaliyopo Ntungamo Bukoba.

Askofu Mwijage alizaliwa Bukoba, Desemba 2, 1966, baada ya masomo ya kipadre, Julai 20, 1997 alipewa daraja takatifu la la upadre.

Amefanya kazi katika parokia mbalimbali katika jimbo la Bukoba ikiwemo kuwa mwalimu na mlezi katika seminari ndogo ya Rubya.

Kuanzia mwaka 2005 hadi 2011 alitumwa na jimbo la Bukoba kwa ajili ya kujiendeleza kwa masomo ya juu na hivyo kupata shahada ya uzamivu kwenye historia ya kanisa mwaka 2011.

Kati ya mwaka 2011-2012 alikuwa jaalimu wa historia ya Kanisa Seminari Kuu ya Segerea. Mwaka 2012 hadi 2023 aliteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mashirika ya Kimisionari ya Kipapa, PMS, Tanzania.
Kuanzia mwaka 2012 hasi uteuzi wake Oktoba 19 mwaka jana,alikuwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja waMapadre Wazalendo Tanzania (UMAWATA) na kuanzia mwaka 2020 ni Mjumbe wa Kamati ya Kimataifa ya Uchumi ya Mashirika ya Kimisionari ya Kipapa, PMS.

Monday, January 29, 2024

BENKI YA CRDB YAZINDUA LIPA NAMBA INAYOPOKEA MALIPO KUTOKA MITANDAO YOTE

 


Katika kuongeza urahisi wa kufanya malipo, Benki ya CRDB imezindua Lipa Namba iliyounganishwa na Msimbomilia wa Taifa (TANQR) ili kuwaruhusu wateja wa mtandao wowote kulipia bidhaa au huduma kutoka kwa mfanyabiashara yeyote.

Kwa muda mrefu, benki za biashara na taasisi nyingine za fedha pamoja na kampuni za simu zilikuwa zinatoa msimbomilia unaojitegemea lakini serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imefanya jitihada kuiunganisha misimbomilia yote ili kumpa mteja unafuu.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa Lipa Namba hiyo, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mifumo ya Malipo (BoT), Lucy Charles Shaidi aliyepaswa kuwa mgeni rasmi, Meneja Mradi wa BoT, Mutashobya Mushumbusi amesema kasi ya mabadiliko yatokanayo na maendeleo ya sayansi na teknolojia kwenye huduma za fedha inazidi kuongezeka duniani hivyo serikali inachukua hatua muhimu kuhakikisha Tanzania haiachwi nyuma kwa kuwawezesha wananchi wake kuendana na hali iliyopo.

“Kati ya vingi vinavyofanywa na serikali yetu kupitia Benki Kuu ya Tanzania ni kuweka sera na miundombinu madhubuti ili kuchochea ujumuishi wa kifedha nchini.

Huduma jumuishi za fedha huchangia katika maendeleo ya mtu mmoja mmoja, biashara na uchumi wa Taifa kwa ujumla. Katika mazingira yanayoendelea kubadilika ya huduma za kifedha, maendeleo ya teknolojia yamepelekea Benki Kuu kutathmini na kubuni upya mbinu za usimamizi ili kuongeza ufanisi, uwazi na kukuza mazingira yanayohimiza uvumbuzi wa bidhaa na huduma,” amesema Mushumbusi.

Mwaka 2014 serikali ilifanya mabadiliko makubwa yaliyoiweka kwenye historia baada ya kuruhusu mteja wa mtandao mmoja wa simu kumtumia fedha mteja wa mtandao mwingine (interoperability) hali iliyorahisisha utumaji miamala kupitia simu za mkononi.

Mpaka mwaka huo, mteja wa kampuni moja ya simu alikuwa hawezi kumtumia fedha mteja wa mtandao mwingine lakini sasa inawezekana.

“Kwa muongo mmoja sasa, tumejijengea uwezo na kupata uzoefu wa kutosha katika eneo hilo.

Tarehe 12 Agosti 2022 Benki Kuu ya Tanzania ilitoa mwongozo kwa watoa huduma za fedha wote nchini kuhusu kuanzishwa na kutumika kwa Msimbomilia wa Taifa Tanzania 2022 (Circular on the establishment of Tanzania Quick Response CodeStandard - TANQR Code Standard 2022). Mwingiliano huu tunaamini utasaidia kuongeza kasi ya ulipaji wa kidijitali hivyo kupunguza matumizi ya fedha taslimu.

Nawapongeza Benki ya CRDB kwa kuwa wa kwanza kutekeleza maelekezo ya Benki Kuu ya Tanzania,” amesema Mushumbusi.

Kwa upande wake, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa amesema siku zote ubunifu ndio nguzo kuu ya huduma za taasisi hiyo kubwa zaidi ya fedha nchini.

“Tunajivunia ubunifu ambao Benki yetu imefanya katika eneo hili.

Tulikuwa wa kwanza nchini kubuni na kuingiza sokoni huduma za TemboCard, SimBanking, SimAccount, internet banking, CRDB Wakala na malipo kupitia msimbomilia yaani QR Code. Hivi sasa zaidi ya asilimia 90 ya miamala ya wateja wetu inafanyika kupitia mifumo hii ya kidijitali,” amesema Raballa.

Hata katika uzinduzi huu wa msimbolia wa pamoja, Raballa amesema ni fahari kwa Benki ya CRDB kuonyesha njia kwa watoa huduma wengine wa fedha kutekeleza mwongozo uliotolewa na Benki Kuu ya Tanzania juu ya matumizi ya Msimbomilia wa Taifa (TANQR) kwani tayari baadhi ya wafanyabiashara wanaotumia LIPA NAMBA na msimbomilia wamehamia kwenye mfumo huo lakini bado wanaweza kuwahudumia wateja wao tu kwa kuwa kampuni nyingine bado hazijahamia huko.

Benki ya CRDB inao wafanyabiashara zaidi ya 30,000 wanaopokea malipo kwa mfumo wa LIPA NAMBA na msimbomilia.

Kwa maboresho yaliyofanywa, ukiacha wateja wa kampuni nyingine wanaotaka kulipa kupitia LIPA NAMBA na msimbomilia, hata wage na watalii wanaotumia huduma za kampuni za kimataifa wataweza kulipa kwa urahisi hali itakayoongeza miamala kwa wafanyabiashara watakaokuwa na mfumo huo rafiki wa malipo.

TAASISI YA LIONS CLUB YAKABIDHI MATANKI NANE YA MAJI KWA AJILI YA KUWASAIDIA WANAFUNZI WA VIGWAZA

 

NA VICTOR MASANGU,VIGWAZA


TAASISI ya Lions Club inayojishughulisha na masuala mbali mbali  ya kijamii imekabidhi matenki nane kwa ajili ya kuhifadhia maji katika shule zilizopo kata ya Vigwaza Halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Matanki hayo yanakwenda kusaidia kutunza maji safi na salama kwa ajili ya wanafunzi wakiwa shuleni na kuondokana na adha ya watoto kubeba maji pindi yanapokuwa yamekatika.

Akisoma taarifa ya makabidhianao ya matanki pamoja na vyakula kwa ajili ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu Muntazir Bharwani alisema wametoa msaada huo baada ya kupokea maombi kutoka kwa Diwani wa Vigwaza Mussa Gama.

Bharwani ambaye alisoma taarifa hiyo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Lions Host Kaniz Naghavi alisema hafla hiyo ya makabidhiano iliambatana na kumkaribisha Gavana wa Tanzania District 411C Happiness Nkya katika shughuli ya chama .

Aliwaomba wakazi wa Vigwaza kuhifadhi na kuyatumia vizuri matanki hayo Ili yaweze kuwasaidia wanafunzi na kuwaondoa katika tatizo la kukosa maji wakiwa shule.

"Lions Clubs imepata ufadhili huu kutoka kwenye kampuni ya Refuelling Solutions (T) Limited na wadau wengine na wanachama wa taasisi hii wamechangia kuleta vyakula kwa watoto yatima Vigwaza," alieleza.

Taasisi hiyo imetoa hamasa kwa taasisi nyingine kutoa huduma na misaada kwa wanafunzi  wa Shule za hapa nchini kutokana na uhitaji wa vitu vingi utaratibu ambao utasaidia kuboresha masuala ya elimu, afya na michezo.

Gavana wa Taasisi hiyo  Hapiness Nkya alisema kwasasa wapo wanachama 620 na club 23 huku 14 zikiwa Dar es Salam wamekuwa wakitoa misaada kwenye maeneo mbalimbali ambayo wanashiriki moja kwa moja na mingine kuomba kwenye makampuni.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze Ramadhani Poss, Afisa Elimu awali na Msingi wa Halmashauri hiyo aliishukuru taasisi hiyo kwa misaada ambayo inaitoa kupunguza vikwazo kwa wakazi wa Vigwaza.

Diwani wa Vigwaza Mussa Gama ameishukuru Taasisi hiyo huku akieleza kwamba umekuwa ikisaidia mambo mbalimbali ya maendeleo katika Kata hiyo kwa kutoa vifaa kwenye Zahanati, daftari kwa wanafunzi na sasa matenki na vyakula kwa yatima.

" Hawa Lions wamekuwa ni watu wa karibu wanaomsaidia kutafuta matatizo kwenye kata yetu naomba wadau wengine wajitokeza kutupatia misaada ya fedha na vitu kwenye sekta za afya na elimu," alisema Gama.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ruvu Darajani Samwel Mjema alisema matanki hayo yanakwenda kuwasaidia kutunza maji pindi yanapokatika huku akiahidi kuyatunza Ili yadumu kwa muda mrefu na kuwa msaada kwa wanafunzi.

Shule nane zilizonufaika na matanki hayo ni pamoja na Msilale, Chamakweza,Sekibwa, Ruvu, Kitonga na Kwazoka zote za Msingi na Sekondari ni Mnindi na Ruvu na hivi karibuni matanki mengine mawili yataletwa na kukabidhi a shule husika.