ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 22, 2014

KUELEKEA KOMBE LA DUNIA BRAZIL YAZINDUA MPANGO WA USALAMA.

Brazil imetangaza kwamba wameongeza maafisa wa kulinda usalama 70,000 zaidi watakao toa huduma za usalama katika fainali ya Dimba la Kombe la Dunia mwaka huu.
Idadi hii iliyoongezwa ni katika jitihada za kukabiliana na tishio la usalama na maandamano .
Idadi iliyopendekezwa hapo mbeleni ya maafisa 100,000 .
Kwa ujumla maafisa wa usalama wapatao 170,000 watatumika katika miji 12 itakayoandaa mashindano hayo.
Jumatano wiki hii Rais wa Brazil Dilma Rouseff alisema kwamba jeshi litajumuishwa kwenye mpango huo dhabiti wa usalama iwapo kutaibuka wimbi lingine la maandamano.
Hatua hii inafuatia visa vya ghasia zilizoshuhudiwa katika miji tofauti tangu mwezi Juni mwaka uliyopita wakati Brazil ilipoandaa mchuano wa Kombe la Mashirika.
Mkuu wa Usalama wa Shrikisho la Soka Duniani FIFA amesema kuwa ana uhakika kwamba Brazil itaandaa mchuano wenye usalama.
Kati ya idadi hiyo ya maafisa wa usalama, 150,000 watachaguliwa kutoka katika vikosi vya Polisi na mashirika mengine ya usalama huku wengine 20,000 watatoa huduma usalama ndani ya viwanja vyote 12.
Vikosi vya jeshi la wanamaji pia litazindua mazoezi ya kwanza kwa matayarisho ya dimba la Kombe la Dunia.
Operesheni hiyo maalum ya kupambana na ghasia inawahusisha wanajeshi 20,000, meli 60 na ndege 15 za kivita
CHANZO:BBC SWA.

SAFARI YA MWISHO YA MWENYEKITI WA CCM MTAA WA PWANI KATA YA KUNDUCHI BENEDICT TIBEHENDERWA

Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mtaa wa Pwani Kata ya Kunduchi Benedict Tibehenderwa umeagwa leo na mamia ya watu  na kuzikwa nyumbani kwao Tegeta jijini Dar es salaa.
Mjane wa marehemu (aliyejitanda kanga katikati) akiwa na mwanae (aliyebeba picha ya marehemu) wakiwa na ndugu jamaa na marafiki katika hospitali ya Muhimbili ambako waliufuata mwili wa marehemu kwaajili ya hatua nyigine kukamilisha safari hiyo ya mwisho ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM mtaa wa Pwani kata ya Kunduchi marehemu Benedict Tebehenderwa.
Rodha Tibehenderwa ambaye ni Mama mzazi wa marehemu (aliyeshika fimbo ya kutembelea ) akiwa na dada zake katika sehemu ya kuusubiri mwili wa marehemu hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaa.
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mtaa wa Pwani kata ya Kunduchi marehemu Benedict Tibehenderwa ukitoka mochuari ya hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaa kuelekea nyumbani kwake Tegeta kwaajili ya hatua nyingine.
Gari lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mtaa wa Pwani kata ya Kunduchi marehemu Benedict Tibehenderwa.
Vijana wa CCM wakiliongoza gari lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mtaa wa Pwani kata ya Kunduchi marehemu Benedict Tibehenderwa kutoka katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaa..
Kisha msafara ulielekea nyumbani kwa marehemu.
Makamanda na mwili wa kamanda wao.
Mjane wa marehemu aliwa na baadhi ya viongozi waandamizi wa CCM.
Kutoka kushoto ni Edgar Mapande ambaye ni mdogo wake marehemu, Oliver Sengo, Owen (mtoto wa kwanza wa marehemu), Hamza Iddy na Jafari Magege. 
Histori ya marehemu ikisomwa.
Jumuiya ya wananchi walio hudhuria.
Mstari wa mbere uliongozwa na safu hii.
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kunduchi akitoa wasifu wa marehemu.



KAMPUNI ZA KINYONYAJI ZAIBUKA MIGODINI YA TANZANIA.

CHAMA CHA WAFANYAKAZI MIGODINI (NUMET),CHAISHAURI
SERIKALI IWACHUNGUZE WAGENI.
NA PETER FABIAN.
MWANZA.
KUMEKUWEPO Makampuni  ya Kitapeli na kinyonyaji yaliyoibuka kama Uyoga nayotumiwa na waajiri Migodini, kuajiri wafanyakazi na kuwapeleka kufanya kazi katika baadhi ya Migodi ya Dhahabu, Almasi, Tanzanaite na Madini mengine ikiwemo Makaa ya Mawe, Mafuta na Gesi asilia kwa ujira mdogo, ikidaiwa kuwa chini ya kima cha chini cha ujira wa Migodini hapa nchini.

Imebainika Pia, bado kumekuwepo baadhi ya wageni wasiokuwa na ujuzi (kutoka nje ya nchi), kuendelea kufurika kwe migodi mbalimbali hapa nchini wakifanya kazi za kawaida zinazopaswa kufanywa na wananchi  wazalendo ambao wanazosifa na uwezo wa kufanyakazi kwenye migodi hiyo lakini hawapewi nafasi na zaidi kumekuwa na urasimu wa Menejimenti za watu wa mataifa ya nje wanaoendesha migodi.

Taarifa ya risala iliyosomwa wakati wa uzinduzi wa Chama cha Wafanyakazi wa Nishati na Madini (NUMET) juma lililopita kwenye Uwanja wa mkongwe wa Nyamagana Jijini Mwanza.

Akisoma risara ya NUMET kwa Waziri wa Nishati na Madini ambaye hakuwepo kwenye uzinduzi huo, Katibu Mkuu wa chama hicho, Nicomedes Kajungu, alisema kwamba serikali inapoteza mapato mengi kutokana na ‘michezo michafu’ inayofanywa migodini na wafanyakazi wanaochangia baadhi yao kukosa au kupoteza haki zao.  

Katibu Kajungu (NUMET) alisema moja ya changamoto inayoikabili Chama chake ni kuibuka kwa Mawakala katika sekta ya ajira katika Migodi  mbalimbali hapa nchini (Third part employment agent) ambayo yanatumiwa na waajiri migodini kuajiri wafanyakazi na kuwapeleka kufanya kazi kwa ujira mdogo wa chini ya kima cha chini cha ujira wa migodini, taratibu na kisheria.

Baadhi ya Mawakala hao ambao ni baadhi ya Makampuni (ambayo hata hivyo hakuyataja) yasiyokuwa na mitaji ya kulipa ujira, lakini yenyewe yamekuwa yanalipwa fedha nyingi na wenye migodi  huku yenyewe yakilipa ujira mdogo wafanyakazi hao na hivyo kunufaika na asilimia ya fedha yanazookoa kutokana na kuwapunja wafanyakazi wao.

“Waajiri kwa kufanya hivi wanakwepa wajibu wao wa kuwapa haki zao kama vile likizo na marupurupu mengine pia wafanyakazi wanashindwa kujua ni yupi mwajiri waoa halisi maana makampuni hayo ya kinyonyaji hayana mitaji ya kulipa ujira.” Alisema na kulalamika.
“Serikali  imekuwa inapoteza Mapato mengi ya Kodi kwa mchezo huo na wafanyakazi kuajiriwa kwa Mikataba mifupi ili wasidai maslahi yao na kuvifanya vyama vya wafanyakazi vikose fursa ya kujadili nyongeza ya mishara, hili ni janga linalohitaji juhudi za pamoja baina ya wafanyakazi , wanachama na serikali kuliangamiza.”

Aidha aliidai kuwa , janga kubwa jingine lililopo migodini ni kufurika kwa wageni wasiokuwa na ujuzi toka nje ya nchi ambao wanafanya kazi za kawaida, wageni hao wengi hawana vibali vya kufanyakazi nchini au vibali vyao vimekwisha lakini bado wapo.

“Maeneo yetu ya kazi kuna tofauti kubwa ya ajira, wafanyakazi wazalendo bila kujali uzoefu wala weredi wao, wamekuwa wakiambulia kazi za mitulinga tu (ya kutumia nguvu nyingi sana)na kuwaachia wageni kazi za kitaalamu za maofisini na zinginezo.” Alieleza.

Aliongeza kwamba “Mtanzania mwenye shahada ya kwanza ya Uhandisi wa Miamba akipewa kazi ya kitaalamu, analipwa ujira usiozidi Dola za Kimarekani 800 kwa mwezi wakati mfanyakazi kama huyo wa kigeni analipwa ujira usiopungua dola za kimarekani 8,000 yaani mara kumi zaidi japo wanafanya kazi sawa.”alisisitiza kwa kuhoji hapa usawa uko wapi.

Alieleza kwamba pengo hilo la kipato kwa hali yoyote ni kubwa sana na ni changamoto kwa wafanyakazi, waajiri, vyama vya wafanyakazi na taifa kwa ujumla kwani madhara yake ni pamoja na kuwepo matabaka mahala pa kazi, migogoro na kuikosesha mapato makubwa serikali iwapo viwango hivyo havitarekebishwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza aliyekuwa amuwakilishe Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muongo, Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza, Mhandisi Wambura Sabora alisema kuwa ni ajabu wageni wenye ujuzi sawa na wazawa (watanzania) kupata mishahara mikubwa mara kumi zaidi ya wazalendo hivyo atahakikisha atalifikisha suala hilo serikalini.

Mhandisi Sibora alisema  kufatia risala hii iliyosomwa na Katibu, ambayo imeeleza mambo mengi nami niwahakikishie NUMET  na kuwashukuru na kuikumbusha na kuiamsha serikali pale inapoonekana imelala hivyo ijikite katika misingi ya uanzishwaji wake na kuwa suluhisho la wanachama wake bila kuwa chanzo cha migogoro katika sekta ya Nishati na Madini kwenye migodi iliyopo hapa nchini.

HOME SHOPPING CENTRE SASA YAFUNGUWA RASMI TAWI LAKE JIJINI MWANZA

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa mwanza Christopher Fuime (kushoto) akifanya matembezi katika duka la Home Shopping Centre kujionea uwekezaji uliofanyika sambamba na mali za majumbani zinazo patikana dukani humo, kulia ni Mkurugenzi wa Home Shopping Centre Ahmed Ally Said.
Ni baadhi ya bidhaa za makapeti zinazo patikana ndani ya Home Shopping Centre
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa mwanza Christopher Fuime (kushoto) akifanya matembezi katika duka la Home Shopping Centre kujionea uwekezaji uliofanyika sambamba na mali za majumbani zinazo patikana dukani humo, kulia ni Mkurugenzi wa Home Shopping Centre Ahmed Ally Said.
Pajama kwa ajili ya watu warika zote. 
Mavazi ya watoto na bidhaa nyingi full kiwango ziko hapa.
Mataulo, mashuka na bidhaa nyingi nyingi zenye viwango full cotton sasa zinapatikana Home Shopping Centre Mwanza.
Vitanda vya kisasa, makabati ya kileo, mashuka, mapazia na thamani mbalimbali za ndani ziko hapa Home Shopping Centre Mwanza.
Makochi na furniture za aina zote utapata.
Vitanda.
Mashuka, mapazia, na kadhalika.
Furniture full house.
Makapeti ya sampuli zote.
Litapendezesha ama nyumba yako au ofisi yako.
Home Shopping Centre inaibadilisha sebule yako.
Bidhaa zote.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa mwanza Christopher Fuime (kushoto) ameusifu uwekezaji huo kwa kusema kuwa utawarahisishia wakazi wa Mwanza kuondokana na adha ya kutembea maduka mengi wakipoteza rasilimali muda kutafuta bidhaa kukamilisha manunuzi, smabamba na kuwapatia bidhaa zinazodumu zenye viwango. Hakika Home Shopping Centre imenuia kubadilisha mazingira ya nyumba za wakazi wa Mwanza.
Mkurugenzi wa Home Shopping Centre Ahmed Ally Said akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza kuhusiana na uwekezaji wake uliofanyika.
Akijiamini kwa kuwekeza katika bidhaa bora pichani mbele ya kamera ni Mkurugenzi wa Home Shopping Centre Ahmed Ally Said.
Bidhaa madhubuti.
Hapo vipi?
Vipi sebule yako ikiwa na maandari kama hii?
Mashuka na vyombo vya majumbani kwa bei nafuu kabisa.
Home Shopping Centre Mwanza inapatikana barabara ya Makongoro kribu na daraja la Mto Mirongo karibu na ofisi za Mamlaka ya Maji safi na maji taka jijini Mwanza (MWAUWASA).

Thursday, February 20, 2014

KUBANJULIWA KWA ARSENAL, JE NI KIELELEZO CHA MSIMU WA KUCHEMSHA KWA TIMU ZA UINGEREZA UEFA?

Wojciech Szczesny of Arsenal fouls Arjen Robben of Bayern Muenchen
TIMU za Uingereza zimezidi kuandikisha matokeo mabaya katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Arsenal ilipigwa mabao mawili kwa bila na Beyern Munich ya Ujerumani katika mchuano wa robo fainali. Arsenal ililazimika kuwachezesha wachezaji kumi pekee uwanjani baada ya mlinda lango wake kuonyeshwa kadi nyekundu.
Mesut Oezil of Arsenal misses from the penalty spot
Kukosa umakini: Ozil alikosa penati iliyomsababisha kucheza chini ya kiwango hadi mwisho wa mchezo.
Mchezaji Mesut Ozil alipoteza penalti ya Arsenal katika kipindi cha kwanza sawa na David Alaba aliyeshindwa kufunga penalti ya Bayern Munich.
Hii inatokea baada ya Manchester City kuchapwa mabao mawili kwa bila Jumanne na Bercalona ya Uhispania. Timu nyingine za Uingereza ambazo ziko katika kinyang'anyiro hicho ni Chesea na Manchester United ambazo zitacheza michuano hiyo baadaye mwezi ujao.
Katika mechi nyingine iliyochezwa hapo jana Atletico Madrid ya Uhispania iliishinda AC Millan ya Italia bao moja kwa bila na ikiwa itasonga mbele hii itakuwa mara ya kwanza Atletico Madrid kuingia robo fainali tangu mwaka 1997.