NA ALBERT G.SENGO
Katika kuhakikisha jitihada za kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (HIV), kuondoa unyanyapaa, na kupunguza vifo kufikia mwaka 2030, jamii imetakiwa kuendelea kuchukua tahadhari kwa kuacha ngono zisizo salama na kutumia kinga ili kuepukana na ugonjwa huo. Akiongea wakati wa kukabidhi vyeti vya pongezi kwa mashujaa wa kampeni ya GGML Kili Challenge waliopanda Mlima Kilimanjaro kwa miguu na baiskeli kupitia njia ya Machame inayofadhiliwa kwa pamoja na mgodi wa Geita Gold Mining Limited (GGML) na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw.Nurdin Babu ameikumbusha jamii kuwa ugonjwa huo bado upo. #mountkilimanjaro #samiasuluhuhassan #habariSaturday, July 26, 2025
Friday, July 25, 2025
Rais Dkt. Samia] Ashiriki Maadhimisho ya Mashujaa Kitaifa katika viwanja vya Mashujaa, Mtumba Jijini Dodoma



JAMII YATAKIWA KUENDELEA KUCHUKUWA TAHADHARI DHIDI YA UKIMWI
Katika kuhakikisha jitihada za kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (HIV), kuondoa unyanyapaa, na kupunguza vifo kufikia mwaka 2030, jamii imetakiwa kuendelea kuchukua tahadhari kwa kuacha ngono zisizo salama na kutumia kinga ili kuepukana na ugonjwa huo.
![]() |
| Sehemu ya wapanda mlima Kilimanjaro baada ya kupokelewa waliposhuka katika Kili Challenge kwa ajili ya kuchangia watu wenye Virusi vya Ukimwi na Ukimwi. |
![]() |
| Sehemu ya wapanda mlima Kilimanjaro baada ya kupokelewa waliposhuka katika Kili Challenge kwa ajili ya kuchangia watu wenye Virusi vya Ukimwi na Ukimwi. |
WATAALAMU WA AFYA MUHIMBILI MLOGANZILA WATAKIWA KUZINGATIA KWA WELEDI MATUMIZI YA VIFAA TIBA
NA VICTOR MASANGU
Wednesday, July 23, 2025
JIBRIL SILLAH WA AZAM FC AJIUNGA NA ES SETIF YA ALGERIA

ALIYEKUWA winga wa Azam FC ya Dar es Salaam, Gibril Sillah raia wa Gambia amejiunga na ES Setif ya Algeria.
Setif ilipost juzi kumtambulisha na kumkaribisha mchezaji huyo aliyeondoka Azam FC baada ya kumaliza mkataba wake.
Sillah aliwasili Azam FC katika dirisha dogo Januari 7, mwaka 2023 akitokea Raja Casablanca ya Morocco baada ya awali kuchezea timu nyingine nchini humo, JS Soualem.


Alijiunga na Raja Agosti 27 mwaka 2021 akitokea Teungueth ya Senegal, lakini Januari 24 mwaka 2022 akapelekwa kwa mkopo JS Soualem alikocheza hadi anasajiliwa Azam FC.
Kabla ya kwenda Teungueth Julai 1, mwaka 2017 alichezea Samger FC na Fortune FC za kwao, Gambia.
YANGA SC YAMSAJILI CASEMIRO WA ZENJI, ABDULNASIR MOHAMED ABDALLAH

Huyo anakuwa mchezaji mpya wa tatu Yanga kuelekea msimu ujao – baada ya kiungo raia wa Guinea, Balla Mousa Conte kutoka Sfaxien ya Tunisia na winga mzawa, Offen Francis Chikola kutoka Tabora United.
Casemiro ni mchezaji ambaye amekipambanua vyema kipaji chake ndani ya misimu michache ya kucheza soka ya Zanzibar kiasi cha kuwa tegemeo kwenye klabu yake na timu ya taifa ya visiwani humo.
Mshindi huyo wa Tuzo Mwanasoka Bora kijana msimu wa 2024-25 katika tuzo za Farafa Zanzibar – aliiwezesha Mlandege kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya PBZ Zanzibar na kuiwezesha pia Zanzibar Heroes kutwa Kombe la Mapinduzi Januari mwaka huu.
INEC YAWANOA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI MKUU WA MIKOA YA MWANZA,MARA YAWATAKA KUZINGATIA SHERIA NA TARATIBU

Jaji wa Mahakama Kuu na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Asina Omari akizungumza kwenye mafunzo.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi Hidaya Gwando akielezea lengo la mafunzo.

…………….
Na Hellen Mtereko, Mwanza
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetoa mafunzo kuhusu Sheria,kanuni,maelekezo mchakato na taratibu za uchaguzi kwa waratibu wa uchaguzi wa mikoa,wasimamizi wa uchaguzi,wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Jimbo,maafisa uchaguzi na maafisa ununuzi 110 kutoka mikoa ya Mwanza na Mara.
Mafunzo hayo ya siku tatu yamefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Benki Kuu Jijini Mwanza.
Akizungumza kwenye mafunzo hayo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Hidaya Gwando amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa na uwezo wakusimamia shughuli za uchaguzi watendaji wa uchaguzi walioteuliwa ili waweze kuifanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
“Mafunzo haya yanafanyika katika awamu mbili awamu ya kwanza yakifanyika Julai 15 hadi 17 julai 2025 katika vituo saba vya mikoa ya Dodoma,Geita,Iringa,Kagera,Kasikazini unguja,Kigoma,Kilimanjaro,Kusini Unguja,Lindi,mjini Magharibi,Morogoro,Mtwala,Njombe,Ruvuma,Singida,Tabora na Tanga”, Amesema Gwando.
Aidha, kwa sasa Tume ipo katika awamu ya pili ambapo katika awamu hiyo mafunzo yameanza leo Julai 21 na yatamalizika Julai 23 mwaka huu.
“Awamu hii itahusisha Mikoa ya Arusha, Dar es salaam,Kasikazini Pemba,Katavi,Kusini Pemba,Mara,Mbeya,Pwani,Rukwa,Shinyanga,Simiyu,Songwe na Mkoa wa Mwanza”
Awali akifungua mafunzo hayo Jaji wa Mahakama Kuu na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Asina Omari ametoa maelekezo nane kwa watendaji hao akiwataka kuzingatia maelekezo yatakayotolewa na tume badala ya kufanya kazi kwa mazoea na wazingatie kuwa baadhi ya mambo yamekuwa yakibadilika mathalani kumekuwa na mabadiliko makubwa ya sheria ya uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani.
“Vishirikisheni vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote zenye kuzingatia matakwa ya sheria na katiba ya tume,”amesema Jaji Asina
Jaji huyo pia amewataka kushirikisha wadau wa uchaguzi hususani katika maeneo ambayo kwa mujibu wa Katiba,sheria,kanuni miongozo na maelekezo yatakayotolewa na tume yanatakiwa kushirikishwa huku pia wakitakiwa kufanya utambuzi mapema wa vituo vya kupigia kura na kuhakikisha kunampangilio mzuri na unazozingatia watu wenye ulemavu.
Wanchoke Chinchibera ni msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Ukerewe amesema tofauti na zamani katika awamu hii, majina ya wasimamizi wa majimbo yamechapishwa kwenye mfumo na gazeti la serikali hali itakayoondoa malalamiko yaliyokuwa yanatokea kipindi cha nyuma na hivyo kuufanya uchaguzi kuwa huru na haki.
“Tumeaminiwa na sisi tunaporudi kwenye majimbo yetu tunaenda kutenda haki na kutoleta migogoro miongoni mwa vyama na wadau wa siasa walioko kwenye maeneo yetu kwakuwa sisi tunakuwa sehemu ya utekelezaji wa sheria mpya ya uchaguzi na sio kusababisha migogoro,” amesema Chinchibela.
Kwa upande wake Mohamed Chande, Msimamizi wa uchaguzi wilaya ya Magu amesema baada ya mafunzo hayo wataenda kusimamia haki ya makundi mbalimbali na kukahakikisha kwamba uchaguzi unakuwa huru na waki.
Tuesday, July 22, 2025
DED HALMASHAURI WILAYA YA MBEYA KUCHELE ASHUSHA NONDO BABU KUBWA KWA WATUMISHI WAPYA 119
Na Mwandishi wetu,Mbeya
RAIS DKT. SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA BANDARI KAVU YA KWALA JULAI 31 KIBAHA PWANI
Na Victor Masangu,Pwani
MUDATHIR YAHYA AJITIA KITANZI YANGA SC HADI 2027
KIUNGO wa Kimataifa wa Tanzania, Mudathir Yahya Abbas (29) amesaini mkataba mpya wa miaka miwili kuendelea kuichezea klabu ya Yanga ya Dar es Salaam.Yanga wameposti video ya Mudathir akiwa anasaini na kuambatanisha a maelezo kwamba mchezaji huyo ni mali yao hadi mwaka 2027.
Mudathir Yahya Abbas aliyezaliwa Mei 6, 1996 huko Jang’ombe, visiwani Zanzibar alijiunga na Yanga Januari mwaka 2023 akitokea Azam FC na katika misimu miwili na nusu ya kuwa wana Jangwani hao amejijengea heshima kubwa kwa uhodari wake kwenye eneo la kiungo.
Kisoka Muda aliibukia katika akademi ya Azam FC mwaka 2012 kabla ya kupandishwa timu ya wakubwa chini ya Kocha Muingereza, Stewart John Hall na kufanikiwa kuwa mchezaji muhimu.
Hata hivyo, mara mbili Muda alikwenda kucheza Singida Black Stars baada ya kupoteza nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Azam FC na mar azote alirejeshwa baada ya kufanya vizuri, kabla ya kuhamia Yanga Januari 2023.DC CHIRUKILE AZINDUA MAFUNZO YA MAAFA SUMBAWANGA ASISITIZA UTAYARI MAPEMA
*Na Mwandishi wetu- RUKWA
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga na Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Maafa ya Wilaya, Mhe. Nyakia Ally Chirukile, amezindua rasmi mafunzo ya usimamizi wa maafa kwa wajumbe wa kamati za wilaya hiyo, akisisitiza umuhimu wa kuwa tayari kabla ya majanga kutokea.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, yaliyofanyika tarehe 21 Julai, 2025 kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Waziri Mkuu – Idara ya Menejimenti ya Maafa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Mhe. Chirukile amesema kuwa maafa kama maporomoko ya ardhi, mlipuko wa kipindupindu, radi na ajali za majini yameathiri jamii na uchumi wa wilaya hiyo.
> “Kuchukua hatua kabla ya majanga ni nafuu zaidi kuliko kushughulika na athari. Mafunzo haya ni nyenzo ya kuongeza ufanisi wetu katika kuzuia na kukabili majanga,” alisema Mhe. Chirukile.
Kwa upande wake, Kanali Selestine Masalamado kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Idara ya Maafa, amesema mafunzo hayo ni utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya mwaka 2022, na yana lengo la kuwawezesha viongozi wa serikali za mitaa kuwa mstari wa mbele wakati wa dharura.
Naye mwakilishi wa UNDP, Bi. Clara Peter Maliwa, amepongeza Wilaya ya Sumbawanga kwa kujitoa kikamilifu kushiriki mafunzo hayo na ameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuboresha mifumo ya kukabili majanga nchini.
Mafunzo haya yamewaleta pamoja wajumbe wa Kamati Elekezi ya Maafa ya Wilaya na Kamati ya Wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, wakiwa na lengo la kujifunza mbinu bora za kupanga, kukabili, na kurejesha hali baada ya majanga.
AWAMU YA PILI YA MAFUNZO YA UFUATILIAJI NA TATHIMINI (M&E) KWA WATUMISHI WA UMMA YAFUNGULIWA JIJINI DODOMA

Na mwandishi wetu Dodoma
Awamu ya Pili ya Mafunzo ya Ufuatiliaji na Tathmini kwa Watumishi wa Umma, yamefunguliwa leo tarehe 21 julai, 2025 na Bi. Sakina Mwinyimkuu — Mkurugenzi wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kuimarisha Ufuatiliaji na Tathmini ili kujenga utamaduni wa uwajibikaji na utendaji unaotegemea matokeo katika Serikali yetu.

Mafunzo haya, yanayofanyika jijini Dodoma, yamewakutanisha washiriki kutoka wizara, idara na taasisi mbalimbali za Serikali, kwa lengo la kuongeza uwezo wao katika usimamizi wa matokeo, matumizi ya taarifa na takwimu, pamoja na ufuatiliaji wa utekelezaji wa mipango.
RC BALOZI,DKT BATILDA BURIAN ATOA AGIZO KWA WAKANDARASI MRADI WA UBORESHAJI HUDUMA YA MAJI TANGA WA HATIFUNGANI YA KIJANI
Na Oscar Assenga,TANGA
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi,Dkt Batilda Burian amewataka wakandarasi watakaohusika katika utekelezaji wa mradi wa hatifungani ya kijani kwa ajili kuboresha huduma ya maji katika Mkoa wa Tanga kuhakikisha wanautekeleza kwa ufanisi mkubwa na ukamilike kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma lengwa.

RC Batilda aliyasema hayo Jumatatu ya Tarehe 21 July 2025 wakati akipokea vifaa ambayo vinakwenda kuboresha huduma za maji katika mkoa wa Tanga na wilaya ya Tanga na Jiji la Tanga ambavyo ni mabomba na viungo yenye urefu wa kilomita 55 na kati ya mabomba yenye urefu wa kilomita 170 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa hati fungaji ya kijani.

Vifaa hivyo vinakwenda kutumika katika kutekeleza na kuendelea mradi wa uboreshaji wa hali ya upatikanaji wa huduma ya maji Tanga katika awamu ya tatu unaogharimu kiasi cha zaidi ya Bilioni 6 ambao utaongeza wigo na fursa ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi.
Maeneo yanayokwenda kutumika na vifaa hivyo katika uboreshaji wa Maji ni Muheza,Pangani na Mkinga ambapo alisema huo ni ubunifu ambao sio mamalaka nyingi za maji mjini zinaweza kwenda wilaya karibia tatu hivyo aliwapongeza kwa kuwa mamlaka ya mfano Tanzania nzima.
“Tunawapongeza sana na tumetayarisha nishani tuwapatie kwa kuendelea kutuheshimisha mkoa wa Tanga katika tasnia ya maji najua mlipewa zawadi siku ya maji katika bara la afrika kama mnatambulika Kimataifa na Afrika na wao kama mkoa watakuwa watu wa ajabu wasipotambuaa mchango wao naa jutihada”Alisema
Alisema kwamba lazima wakandarasi ambao watakaotekeleza mradi huo kuhakikisha wanafanya kazi kwa waledi mkubwa ambao utakuwa chachu ya kukamilika kwa wakati na hivyo wananchi kuweza kunufaika na huduma hiyo muhimu jambo ambalo linawezesha kuondokana na changamoto walizokuwa wanakumbana nazo awali
“Leo hii ni siku muhimu tunapokea mabomba haya na viungio vyake hivyo niwatake wakandarasi wote ambao wanahosuka kwenye utekeleza wa mradi kuhakikisha mradi unatekeleza kwa ufanisi mkubwa na unakamilika kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma lengwa”Alisema RC huyo.
Aliongeza kwamba fedha hizo zimetokana na ubunifu mkubwa uliofanywa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga Uwasa) katika kupata hati fungani ya gharamai ya Bilioni 53.12 ambayo imewezea shughuli hizo kuweza kufanyika na kuleta tija kubwa katika utekelezaji wa miradi.
Aidha alitumia fursa hiyo kuhimiza ushirikiano katika utekelezaji wa mradi huo kutokana na upekee wake kwenye bara la ulimwengu kutokana na kwamba uwekezaji wake na waliowekeza hisa kwa sasa wameshaanza kupewa gawio kila kota wanapata gawio.
“Huu ulikuwa ni ubunifu mkubwa na mafanikio yanaonekana kwa mtu mmojammoja na mkoa umekuwa salama kuwa sababu kukosekana kwa maji ni jambo la kiusalama hivyo tuendeee kuhakikisha maeneo yenye uvujaji wa maji mnaendelea kuyazibiti ili kupunguza upotevu wa maji “Alisema RC Balozi Batilda.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa aliipongeza Tanga Uwasa kwa jitihada zao kubwa za kuongeza upatikanaji na ubora wa maji na kuangalia vyanzo vya maji na mipango na mikakakti ya kupanda miti mingi kwa kuwashirikisha wananchi waliopo kwenye vyanzo vya maji ikiwemo kuendelea kutoa vifaa lakini kuwasaidia katika shughui zao mbalimbali ili waendelea kuwa walinzi wazuri na wajue kwamba vyanzo hivyo vinathamani na wanathamni mchango wao katika kuvilimda.
Aliongeza kwamba mkoa huo unathamani mchango unaofanywa na Wizaraa ya maji chini ya Waziri Jumaa Aweso na ameendelea kufanya makubwa Kitaifa na kimkoa ndio maana hata watendaji wa Maji mkoa ikiwemo mameneja hawajamuangusha ndio wamesimama kidete kuelezea umma ilani ya CCM imetekelezwa kwa asilimia 100 na katika miji yetu asilimia 95 ya maji imewezeka kufikiwa.
Awali akizungumza katika halfa hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo alisema kutokana mradi huo anaona mamlaka ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa asilimia 100 kwa muda mfupi ujao hivi sasa wapo asilimia 95 na kukamilika kwa mradi huo asilimia hiyo wameuvuka na mradi huo wanatarajia mpaka utakapofika mwezi Octoba mwaka huu utakuwa umekamilika kama mambo yote yatakwenda sawa.
Alisema kwamba hakuna sababu kwanini yasiende sawasawa kwa leo wamepokea mabomba kontena 11 bado 8 na vitafika kwa muda ambao umewekwa hivyo wanaiona Tanga Uwasa ikitatua shida ya maji katika wilaya hizo nne ambazo ni wilaya ya Tanga,Muheza,Mkinga na Pangani na hawaoni kama kuna shida na wapo wapi tayari hata wakiambiwa wasogee wilaya nyengine ikiwemo Korogwe uwezo wanao kutokana na utalaamu walionao
Aidha alisema kwamba hiyo ni awamu ya nne ya mradi huo na awamu ya kwanza walipanua mtambo wa kusafisha maji na awamu nyengine kusogeza maji kwenye wilaya ambazo wameongezewa na awamu ya tatu ni mkopo kutoka benki ya TIB wakatanua zaidi huduma zao katika awamu tofauti tofauti ikiwemo kurekebisha mitambo ambayo ni ya muda mrefu eneo la usafishaji Maji Mowe na awamu ya nne ni kusambaza huduma ya maji katika maeneo ya miji.
Naye kwa upande wake Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly alisema wana jambo kubwa la kupokea baadhi ya mabomba kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa hati fungaji ya kijani ambayo kwa sasa yana kilomita 55 na lengo la mabomba yote yana kilomita 170 ni thamani ya zaidi Bilioni 6.3 .
Alisema mradi huo unalengo la kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya Maji katika wilaya ya Tanga, Mkinga Muheza na Pangani utakapokamilika wananchi 555,000 watanufaika kwa namna mbalimbali wapo ambayo hawajafikiwa na maji watafikiwa na wale ambao miundombinu ulikuwa chakavu itaboresha.
Aidha alisema wanategemea mwisho wa mradi huo hali ya upatikanaji wa maji itakuwa ni nzuri sana lakini pia watajenga miundombinu mikubwa na wanaongeza chanzo cha maji kutoka uwezo wa lita Milioni 42 kwenda Lita Milioni 72 lakini na mtambo wa kusafisha maji kutoka lita milioni 45 hadi Lita Milioni 60 kwa hiyo maji hayo yatasaidia kwenda kwenye hizo wilaya bila shaka yoyote.
Mwisho.













.jpg)
.jpg)
.jpg)















