ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, October 4, 2024

Simba SC 2-2 Coastal Union | Highlights | NBC Premier League 04/10/2024

 Coastal Union imelazimisha sare ya 2-2 dhidi ya Simba katika mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania Bara uliopigwa kwenye Dimba KMC Complex, Dar es Salaam.

Simba wametangulia kwa magoli mawili kipindi cha kwanza kutoka kwa Mohamed Hussein Zimbwe Jr. na Lionel Ateba kwa penati , lakini Coastal wakacharuka kipindi cha pili na kupata magoli mawili kupitia kwa Abdallah Hassan na Hernest Malonga....

Thursday, October 3, 2024

VIJIJI VYOTE MTWARA VIMEFIKISHIWA UMEME SASA NI ZAMU YA VITONGOJI



📌BILIONI 16.7 KUSAMBAZA UMEME VITONGOJI 150


📌KUNUFAISHA KAYA 4,950

Baada ya kukamilisha usambazaji wa umeme katika vijiji vyote 785 Mkoani Mtwara, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 16.7 wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 150 utakaonufaisha kaya 4,950 mkoani humo.

Mhandisi Msimamizi wa Miradi ya Umeme REA Kanda ya Kusini, Mhandisi Deogratius Nagu amebainisha hayo Oktoba, 02, 2024 Wilayani Masasi Mkoani Mtwara mbele ya Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Kanali Patrick Sawala wakati wa kumtambulisha Mkandarasi atakayetekeleza mradi huo Kampuni ya Northern Engineering Works Ltd ya Arusha.

“Tunamshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutuwezesha kukamilisha utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme kwenye vijiji vyote 785 mkoani hapa kwa asilimia 100 na sasa ni zamu ya vitongoji ambapo kiasi cha shilingi 16,717,407,821.65 kitatumika kutekeleza mradi wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 150,” alisema Mhandisi Nagu.

Tukio hilo lilishuhudiwa na viongozi wa Mkoa na Wilaya wakiwemo Wakuu wa Wilaya za Nanyumbu, Mtwara na Tandahimba, Kamati za Usalama Mkoa wa Mtwara na Wilaya ya Masasi, Madiwani kutoka Kata mbalimbali Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. 

Akizungumza wakati wa utambulisho wa mkandarasi huyo, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala alizipongeza REA na TANESCO kwa kuendelea kushirikiana kuhakikisha dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea maendeleo wananchi wake kupitia Nishati linatimia.

“Wana Mtwara tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko kwani kwa sasa hapa kila Kijiji kina umeme na sasa wanahakikisha umeme unafika vitongojini,” alisema.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi wa kufikisha umeme vitongojini, Mhandisi Nagu alisema kati ya vitongoji 3,427 vilivyopo Mkoani humo, vitongoji 2,200 vimefikishiwa umeme ambayo ni sawa na asilimia 64 na kwamba vitongoji 150 ambavyo vitapata umeme kupitia mradi huo vitaongeza idadi ya vitongoji vyenye umeme katika Mkoa wa Mtwara.

Aidha, alibainisha kuwa mradi huo ambao mkandarasi wake ametambulishwa, utatekelezwa kwa muda wa miezi 24 na hivyo kukamilika ifikapo Septemba 2026 na kwamba vitongoji vitakavyobaki vitaendelea kupatiwa umeme kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mhandisi Nagu alisema mradi utatekelezwa katika majimbo 10 katika wilaya za Mtwara, Tandahimba, Newala, Masasi na Nanyumbu na kwamba katika kila Jimbo Vitongoji 15 vitanufaika.

“Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kutekeleza miradi mbalimbali katika Mkoa wa Mtwara ikiwa na lengo la kuwapatia huduma za Nishati wananchi ili kuboresha huduma za jamii maeneo ya vijijini na vijiji-miji,” alisema Mhandisi Nagu.

Kwa upande wake Mkandarasi aliyeshinda zabuni hiyo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Northern Engineering Works Ltd, Samwel Lema alimuhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa mradi utatekelezwa kwa ubora unaotakiwa na utakamilika ndani ya muda kama ilivyo katika mkataba.

UWT KIBAHA MJI WACHARUKA WALAANI VIKALI VITENDO VYA KUCHOMA PICHA ZA RAIS SAMIA

 


NA MWANDISHI WETU, KIBAHA

 
Jumuiya ya umoja wa  wanawake wa Chama cha mapinduzi (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini imeungana na Mwenyekiti wao wa Taifa Mary Chatanda kupinga na kulaani vikali kwa baadhi ya wanawake  wanaodaiwa kuwa ni wa chama cha demokrasia na maendeleo  Chadema (BAWACHA) kuchoma vitenge ambavyo vilikuwa na picha ya  Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hasssan kitendo ambacho sio cha uzalendo katika Taifa la Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari  wakati wa kutoa tamko juu ya tukio hilo Mwenyekiti wa (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja  amesema kwamba  wanawake wote kwa umoja wao wamesikitishwa sana kuona vitenge vyenye picha ya Rais vinachomwa hadharani na picha zake kusambaza katika  baadhi ya mitandao kitendo ambacho sio cha kiungwana hata kidogo.

Mgonja alibainisha kwamba kitendo hicho ni  utovu mkubwa wa nidhamu  kwani kufanya hivyo ni ukosefu wa maadili ya nchi  na  kwamba kundi la wanawake hao  wameamua kuvunja heshima  baada ya  kusema maneno ya  uwongo  ambayo yanaweza kuleta  uchonganishi mkubwa  baina ya wananchi pamoja na  Rais Samia.

Mwenyekiti huyo alifafanua kwamba Rais wa waamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kufanya mambo  makubwa katika miradi mbali mbali ya maendeleo na hivyo maneno ambayo yamesemwa na baadhi ya wanawake hao hayana ukweli kabisa hata kidogo hivyo amewaomba watanzania wote kuwa na uzalendo na nchi yao na kuachana kabisa na maneo ya kashfa kwa Rais Samia.

"Sisi kama Jumuiya ya wanawake wa umoja (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini tunapinga vikali kabisa na kulaani kitendo hicho kilichofanywa hivi karibuni na  baadhi ya wanawake wanaodaiwa kuwa wa (Bavicha) kuchoma vitenge vyenye picha ya Rais Samia huu ni ukosefu mkubwa wa utovu wa nidhamu na maadili kwa hivyo jambo hili limetuumiza sana na alipaswi kufumbiwa macho hata kidogo,"alisema  Mwenyekiti  Mgonja.

Katika hatua nyingine aliviomba vyombo vya dola ambavyo vinahusika na usalama kuwakamata na  kuwachukulia hatua kali za kisheria wale  wanawake wote ambao wamehusika kwa makusudi kuchoma kitenge chenye picha ya Rais  Samia Suluhu Hassan na kwamba wangekuwa wazalendo na nchi  yao wasingefanya tukio kama hilo ambalo wao kama wanawake hawawezi kulifumbia macho hata kidogo.

Kadhalika alisema kitendo walichokifanya ni uchochezi na ni uvunjifu wa amani hivyo wanapaswa kukamatwa kwani wameshindwa kuheshimu mamlaka na madaraka aliyonayo Rais  Samia Suluhu Hassan  na kwamba wameahidi kuendelea kumlinda na kumtetea kwa hali na mali kwani amefanya mambo makubwa kwa wananchi wa Tanzania katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo pamoja naa ili mikubwa ya kimkakati.

Wednesday, October 2, 2024

RC PWANI AUNGURUMA AAHIDI NEEMA KWA WAZEE WA KIBAHA MJI


VICTOR  MASANGU, KIBAHA  


Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaj Abubakari Kunenge  amewahimiza wazee kuhakikisha kwamba wanaweka misingi mizuri na imara  kwa ajili  ya kuweza kumsapoti   Rais wa awamu wa sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumlinda, kumtunza  na kumtetea katika shughuli mbali mbali anazozifanya ikiwemo kuwatumikia wananchi  wa Tanzania sambamba na kutekeleza miradi  ya maendeleo katika sekta tofauti .

Kunenge ameyasema hayo wakati wa  kilele cha maadhimisho wa siku ya wazee Duniani ambayo katika ngazi ya Wilaya yamefanyika katika Halmashauri ya Kibaha mji na kuhudhuliwa na wazee  mbali mbali kutokana kata zote 14 za Kibaha mji  pamoja na viongozi wa serikali, viongozi wa dini pamoja na viongozi wa vyama vya siasa.


Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani amesema kwamba anatambua mchango mkubwa uliofanywa na wazee wa Mkoa wa Pwani hivyo ana imani  wanaweza kumsemea mazuri Rais Samia kwa mambo mazuri  ambayo ameyafanya kwa weledi mkubwa katika  kuboresha sekta mbali mbali ikiwemo kuifanya Pwani kuwa na miradi mingi ya kimikakati ambayo itakuwa ni mkombozi mkubwa kwa wananchi.

"Mimi kama Mkuu wa Mkoa wa Pwani nimefarijika sana kukukutana katika siku hii muhimu ya maadhimisho ya wazee lakini kitu kikubwa ninachowaomba tumpe ushirikiano wa kutosha Rais wetu na kuhakikisha kwambaa tunamlinda na kumtetea kwa yale yote mazuri ambayo amekuwa akiyafanya katika nchi hii kwani ameweza kutenga fedha nyingi ambazo zimeweza kuleta matokeo chanya katika Mkoa wetu wa Pwani ikiwemo kuongoza kwa  viwanda nchi nzima,"Kunenge.  

Kunenge pia alisema lengo la serikali ya awamu ya nne ni kuweka mikakati madhubuti  ya kuendelea kuboresha huduma ya afya hususan kwa wazee ikiwa pamoja na kuwapatia vitambulisho maalumu ambayo vitaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa katika suala zima la kutambulika pindi wanapokwenda kupatiwa matibabu na huduma nyingine za msingi wanazostahili.


Kadhalika alifafanua kwamba wazee wa Mkoa wa Pwani wana busara nyingi hivyo wanapaswa kama wazazi na walezi kuweza kumpa amani na faraja Rais wao ili aweze kuendelea kuwatumikia wananchi wa Tanzania ikiwa pamoja na kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuboresha huduma mbali mbali kwa wananchi  na kuwaahidi kuwatembeza katika mirida ya kimikakati ili  waweze kujionea na kujifunza mambo makubwa aliyoyafanya Rais Samia.

Kwa upande wake Mganga mkuu wa Halmashauri ya Kibaha mji Catherine Saguti amesema kuwa  kwa sasa kuna jumla ya wazee wapatao 12,724 na kwamba wameweka mipango ya kuhakikisha wazee wote wanatambuliwa kwa lengo la kuweza kuwabaini ili kuweza kuwabaini na kuwapatia mahitaji yao ya msingi ikiwemo kuwapa kipaumbele zaidi katika mahitaji yao muhimu.

Dkt. Catherine aliongeza kwamba wanaendelea kutekeleza sera ya wazee ya mwaka 2003 ya kuwawezesha wazee wenye umri wa miaka 60 na kuendelea kupatiwa  fursa ya huduma ya matibabu pasipokuwa na vikwazo vyovyo vile hususan kwa wale  wasiokuwa na uwezo wa kumudu ya kuchangia gharama  mbali mbali za matibabu.

Pia alifafanua kwamba Halmashauri ya mji Kibaha katika kuwajali wazee hao imeendelea kutengeneza vitambulisho kwa ajili ya msamaha wa kuweza kupata matibabu bila malipo ambapo wameweza kuwafikia jumla ya wazee wapatao 8,540 ambao tayari wameshatengenezewa vitambulisho hivyo na kukabidhiwa.


Naye Afisa maendeleo ya jamii Halmashaauri ya Kibaha mji  Rea Lwanji akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kibaha amebainisha kuwa siku ya wazee dunianiaa inalenga kuleta mabadiliko makubwa katika suala zima la uboreshaji  wa maisha pamoja na kuwapatiaa huduma stahiki kwa ustawi wao wa siku za baadae.

Alisema kwamba serikali ya Wilaya ya Kibaha itakuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kwamba inaboresha zaidi huduma kwa wazee wote na kwa kuzingatia utekelezaji wa sera ya mwaka 2003 ya kuwapatia wazee hao vitambulisho vya msamaha wa matibabu lengo ikiwa waweze kupatia huduma ya matibabu bila ya vigwazo vyovyote na kuwaweka katika mazingira ambayo ni rafiki katika maisha yao.


Nao baadhi ya wazee hao akiwwemo Rose Lwanda ambaye ni katibu wa baraza la wazee katika Halmashauri ya Kibaha mji ameishukuru serikali japo bado wanakabiliwa na  changamoto ya kutoingizwa kwenye mfumo wa Tasaf hivyo wameiomba serikali kuliangalia jambo hilo  kwa jicho la tatu ili kuweza kuwasaidia waweze kupata fursa hiyo.

Kadhalika wameiomba serikakali kupitia Halmashauri ya Kibaha mji kuwawekea mfumo mzuri wazee hao kuwaingia katika vikundi ili waweze kupata fursa ya kukopesheka kwa urahisi zaidi lengo ikiwa ni kuweza kujikwamua kiuchumi na kujiendeleza  kimaisha ikiwa pamoja na kuomba kushirikishwa katika vikao mbali mbali  vya  kimaendeleo.

Tuesday, October 1, 2024

SAO HILL YAKABIDHI VIFAA VYA UJENZI KILOSA MUFINDI

 

 Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Dkt Linda Salekwa amewashukuru TFS kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan katika uendelezaji wa miradi mbalimbali kwa wananchi kwani wamekuwa wakifanya hivyo katika maeneo tofauti tofauti katika Wilaya ya Mufindi.Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Dkt Linda Salekwa amewashukuru TFS kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan katika uendelezaji wa miradi mbalimbali kwa wananchi kwani wamekuwa wakifanya hivyo katika maeneo tofauti tofauti katika Wilaya ya Mufindi.
Naye Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Saohill PCO. Tebby Yoramu amemshukuru Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS Prof Dos Santos Silayo kwa kuridhia ofisi ya Shamba la Miti Saohill kutenga fedha kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Ofisi na ukumbi wa kijiji, madarasa pamoja na jengo la utawala la shule ya msingi Kilosa.

Na Fredy Mgunda, Iringa Mufindi


Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS-kupitia Shamba la Miti Saohill umekabidhi vifaa vya ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo katika Kijiji cha Kilosa Mufindi katika Kata ya Ihanu Wilayani Mufindi.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Dkt Linda Salekwa amewashukuru TFS kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan katika uendelezaji wa miradi mbalimbali kwa wananchi kwani wamekuwa wakifanya hivyo katika maeneo tofauti tofauti katika Wilaya ya Mufindi.

Ameongeza kuwa Kata ya Ihanu ni miongoni mwa kata zinazonufaika sana na uwepo wa Shamba la Miti Saohill kwani awali walijengewa bweni la wanafunzi katika shule ya sekondari ya Ihanu lenye thamani ya zaidi ya Millioni Mia Moja, miondombinu ya barabara pamoja na utunzaji wa mazingira kwa kupata miche bure na kiupanda kwenye hekari 50.

Aidha ameuagiza uongozi wa kata na kijiji cha Kilosa kuhakikisha kuwa vifaa vilivyotolewa vinatumika kwa usahihi katika malengo ambayo yalipangwa kutekelezwa ikiwa ni ukarabati wa ofisi na ukumbi wa mikutano wa kijiji, madarasa pamoja na jengo la utawala katika Shule ya Msingi Kilosa.

Naye Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Saohill PCO. Tebby Yoramu amemshukuru Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania TFS Prof Dos Santos Silayo kwa kuridhia ofisi ya Shamba la Miti Saohill kutenga fedha kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Ofisi na ukumbi wa kijiji, madarasa pamoja na jengo la utawala la shule ya msingi Kilosa.

"Shamba la miti Sao Hill linatambua umuhimu wa mazingira bora ya kutolea huduma kwa wananchi na elimu bora kwa vijana wa kitanzania, kufuatia umuhimu huo, Shamba litakabidhi mifuko 200 ya saruji kutimiza ahadi yake ya kusaidia ujenzi wa ofisi ya Kijiji" alisema PCO Tebby Yoramu

Aidha ameongeza kuwa vifaa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na jengo la utawala viko kwenye mchakato wa kununuliwa na vitawasilishwa mapema ndani ya mwaka huu na ni imani ya Shamba kuwa vitatumika ipasavyo.

Pamoja na hayo ametoa wito kwa wananchi wote kuendelea kutoa ushirikiano katika shughuli za ulinzi wa msitu dhidi ya majanga ya moto hususani katika kipindi hiki cha kiangazi.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Ihanu Michael Kiliwa ameshukuru TFS kupitia Shamba la miti Saohill kwa kuendelea kuwa msaada mkubwa katika kata hiyo kwani wamekuwa wakinufaika na miradi mbalimbali hususani katika sekta ya elimu na utunzaji wa mazingira kwa ujumla.

Makabidhiano hayo yamefanywa na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi na kushuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwepo Afisa Tawala wa Wilaya Robert Kileo, Mwenyekiti wa CCM wilaya George Kavenuke, Wahifadhi kutoka TFS, viongozi na wananchi wa kijiji cha Kilosa Mufindi.

VIONGOZI WA DINI NACHINGWEA KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI

 

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea mhandisi Chionda Kawawa amewaomba viongozi wa dini kuhamasisha wananchi wajitokeze kujiandikisha na kujitokeza kugombea na kupiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa/vijiji na vitongoji unaotakiwa kufanyika 27/11/2024.
Viongozi wa dini na Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea wapata semina ya namna gani ya kuhamasisha wananchi wajitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili waweze kushiriki kikamilifu uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji 
Viongozi wa dini na Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea wapata semina ya namna gani ya kuhamasisha wananchi wajitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili waweze kushiriki kikamilifu uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji 


Na Fredy Mgunda, Nachingwea Lindi.


Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea mhandisi Chionda Kawawa amewaomba viongozi wa dini kuhamasisha wananchi wajitokeze kujiandikisha na kujitokeza kugombea na kupiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa/vijiji na vitongoji unaotakiwa kufanyika 27/11/2024.

Akizungumza na viongozi hao wa dini, mhandisi Kawawa alisema kubwa viongozi wa dini wanaushawishi mkubwa kwa wananchi kuweza kujitokeza kushiriki kikamilifu katika uchanguzi wa mwaka huu.

Mhandisi Kawawa alisema kuwa serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na viongozi wa dini katika Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea hivyo zoezi hilo lipo mikononi mwao tu kwa kushirikiana na serikali.

Alisema kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji unaumhimu mkubwa katika mustakabali wa maendeleo ya wananchi kwa kipindi cha miaka mitano ijayo hivyo ni muhimu kila mwananchi kushiriki kikamilifu uchaguzi huo.

Kwa upande wao viongozi wa dini katika Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea walisema kuwa wapo tayari kushirikiana na serikali kutoa elimu ya umuhimu wa kushiriki zoezi zima la uchaguzi kwa wananchi wote.

Walisema kuwa wananchi wanatakiwa kujitokeza kushiriki kikamilifu uchaguzi wa mwaka huu ili kuweza kuchagua viongozi wapenda maendeleo na wenye nia njema ya kuwatumikia wananchi.

MAMA KOKA ATEKELEZA AHADI KWA VITENDO YA VITI NA MEZA SHULE YA BOKO TIMIZA

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mama Selina Koka ametekeleza ahadi yake kwa vitendo ya kukabidhi viti na meza kwa walimu wa shule ya msingi Boko Timiza iliyopo kata ya Tumbi Halmashauri ya Kibaha mjini waliokuwa wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ukosefu wa viti na meza kwa ajili ya kukalia katika ofisi yao.

Akikabidhi msaada huo wa viti kumi pamoja na meza zake Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini SaidMbecha kwa niaba ya mke wa Mbunge amesema kwamba Mama Koka ameamua kutekeleza ahadi yake kwa vitendo ambayo aliitoa wakati wa halfa ya mahafali ya kuhitimu wanafunzi  wa darasa la saba katika shule hiyo ya msingi Boko Timiza.

Mbecha alisema kwamba Mama Koka ametoa vifaa hivyo kutokana na kupokea risala kutoka kwa walimu hao ambayo ilikuwa inaeleza cahnagamoto mbali mbali walizonazo ikiwemo ya ukosefu wa viti na meza katika ofisi yao hivyo kupelekea kukaa katika mazingira magumu katika suala zima la utekelezaji wa majukumu yao  ya kila sika katika kuwahudumia wanafunzi.

"Shule hii ya msingi Boko Timiza katika halfla ya kumaliza wanafunzi wa darasa la saba ambayo ilifanyika hivi karibuni walimu na wanafunzi walieleza chanagmoto zao mbali mbali na moja ikiwa ni ukosefu wa samani ya viti na meza hivyo kwa kuliona hilo Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mama Selina Koka ametekeleza ahadi ambayo aliitoa na  nimekuja kwa niaba yake kukabidhi viti na meza,"alibainisha Mbecha.

Kadhalika Mbecha alifafanua kwamba mbali na kukabidhi viti na meza ameweza kukabidhi sukari kilo kumi ambazo zitaweza kuwasaidia walimu waweze kupata chai nyakati za asubuhi ili waweze kufundisha walimu wakiwa katika hali nzuri  lengo ikiwa ni kuweza kuongeza kasi ya ufundishaji na kuongeza  kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi.

Kwa upande wake  Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Boko Timiza Rozania Kimate amemshukuru kwa dhati Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mama Selina Koka kwa kuweza kutekeleza ahadi yake  kwa vitendo ambayo aliitoa wakati mahafali ya darasa la saba ya kuwasaidia walimu hao viti na meza ili waondokana na changamoto ambayo walikuwa wanakabiliana nayo ya kukaa katika mazingira magumu.

Mwalimu huyo amebainisha kwamba katika shule hiyo hapo awali walikuwa wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo hiyo ya viti na meza lakini kutokana na kuguswa ameweza kutekeleza ahadi hiyo ya viti na meza ikiwemo pamoja na sukari, bilika kwa ajili ya chai ambayo kwa upande wao ni msaada mkubwa sana katika suala zima la utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku katika ufundishaji wa wanafunzi.

Naye Mwenyekiti kamati ya shule ya msingi Boko Timiza  Michael Mwampashi   hakusita kumpongeza Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe. Silvestry Koka kwa juhudi zake za kushirikiana na wananchi wa Boko Timiza katika kuhakikisha anaboresha na kuweka mazingira mazuri ya kuisaidia kwa hali na mali yeye pamoja na mke wake Mama Selina Koka katika kusaidia mambo mbali mbali ikiwemo viti na meza.

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa Boko Temboni Said Mohamed amesema msaada huo ambao umetolewa na Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini  wa viti na meza utakuwa ni  mkombozi mkubwa kwa walimu  ambao hapo awali walikuwa na adha kubwa ya ofisi yao kukosa vifaa mbali mbali ikiwemo ukosefu wa samani ya viti na meza na kumshukuru Mbunge Koka kwa kushiriki katika juhudi za kuiboresha shule hiyo katika miundombinu ya majengo ya madarasa.

BENKI YA NMB YACHANGIA VIFAA VYENYE THAMANI YA MILIONI 60 KWA SHULE TANO ZA MSINGI WILAYA YA MUHEZA

 

 



Na Oscar Assenga, Muheza


BENKI ya NMB nchini imetoa imechangia vifaa vyenye thamani ya Milioni 60 kwa ajili ya kuboresha mazingira ya elimu kwa shule tano za Msingi katika wilaya ya Muheza mkoani Tanga ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali


Msaada huo ulikabidhiwa kwa Naibu Waziri Mkuu Dkt Doto Biteko na Afisa Mkuu wa Udhibiti wa Benki ya NMB Doreen Joseph katika Halfa iliyofanyika kwenye uwanja wa Jitegemee wilayanu humo katika wakati Juma la Elimu uliokwenda sambamba na uzinduzi wa Kampeni ya Mtoto wa leo Samia wa Kesho.

Alivitaja vifaa hivyo ambavyo benki hiyo imechangia kuwa ni Madawati 200 kwa shule ya Msingi Kwemkamba ,Magusuru,Mdote,Ngomeni na Mwembeni ambapo kila shule itapata madawati 50 ,vifaa yengine ni vitanda 40 vya double deka na magodoro 80 kwa ajili ya shule ya Msingi Ngomeni .

Alisema pia wamekabidhi vitanda 32 na magodoro 64 kwa ajili ya msingi Masuguru ambayo vitakuwa chachu katika kuhakikisha wanatatua changamoto ambazo zilikuwepo awali katika shule hizo.

“Nikushukuru Naibu Waziri Mkuu Mhe Dkt Dotto Biteko pamoja na Serikali kwa kazi kubwa inayofanywa kuendelea kuleta maendeleo nchini na sisi Benki ya NMB tupo tayari kushirikiana na Serikali katika kuendeleza maendeleo”Alisema .

Aidha alisema kwamba utoaji wa vifaa hivyo ni sera ya Benki hiyo kuendelea kurudisha kwa jamii ambayo ni sehemu ya faida wanayoipata kama benki inatoka kwa wadau na jamii hivyo hiyo sehemu yao wanatakiwa kurudisha kwa jamii.

“Benki ya NMB inatambua juhudi za serikali katika kusimamia elimu kwa nguvu zote zilizowekwa ili kuboresha utoaji wa mijini na vijiji ikiwemo utoaji wa elimu bure tunaipongeza Serikali kwa hilo sisi kama wadau furaha yetu ni kuunga mkono juhudi hizo za maendeleo kuisaidia jamii yetu”Alisema

Awali akizungumza wakati wa uzinduzi huo Naibu Waziri Mkuu Dkt Dotto Biteko alisema kampeni hiyo ya Mtoto wa leo ni Samia wa kesho muhimu ambayo inaonyesha walivyoamua kuwekeza kwenye msingi wa muhimu wa watoto kujiamini na hatimaye kuweza kutimiza ndoto ya kuwa viongozi bora wa baadae.

Naibu Waziri Mkuu huyo aliwataka pia wazazi na walimu kushirikiana kuwaandaa wanafunzi wao kuwa viongozi na wazazi bora kwa siku zijazo huku akieleza kwamba Serikali imewekeza katika sekta ya elimu ili kupata matokeo na maendeleo yanayoendana na uwekezaji huo.

Naye kwa upande wake Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Zainabu Katimba alisema Serikali imejipanga kuwaandaa viongozi bora wa kesho kwa kuwekeza zaidi katika sekta ya elimu na miundombinu mbalimballi ikiwemo mazingira bora ya kujifunzia.

Monday, September 30, 2024

TUKAJIANDIKISHE KWENYE DAFTARI LA MKAZI ILI TUPIGE KURA

 

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la Mkazi ambalo linatarajiwa kufanyika Oktoba 11 hadi 20, 2024 na upigaji wa kura 27, Novemba 2024 kuchagua viongozi wa serikali za Mitaa.
Vikundi vya Jogging vikiwa vinafanya mazoezi kwa ajili ya afya ya mwili
Vikundi vya Jogging vikiwa vinafanya mazoezi kwa ajili ya afya ya mwili.
Vikundi vya Jogging vikiwa vinafanya mazoezi kwa ajili ya afya ya mwili.


Na Fredy Mgunda, Lindi.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Telack ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la Mkazi ambalo linatarajiwa kufanyika Oktoba 11 hadi 20, 2024 na upigaji wa kura 27, Novemba 2024 kuchagua viongozi wa serikali za Mitaa.


"Niwaombe vijana wote, niwaombe akina mama, akina Baba tuende tukajiandikishe kwenye daftari la mkazi ili tukaweze kupiga kura " 


Wito huo ameutoa leo katika viwanja vya Kilwa Kivinje ambako kivinje Jogging klabu wameandaa bonanza lakualika klabu mbalimbali kutoka maeneo mikoa mbalimbali kama vile Dodoma, Mtwara, Pwani na Dar Es Salaam lenye lengo la kudumisha afya, ushirikiano, upendo, umoja na hamasa ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa ambao unatarajiwa kufanyika mwezi Novemba 27, 2024.


Mhe. Zainabu Telack ametoa angalizo kwa wananchi ambao hawana taarifa sahihi kuhusu vitambulisho walivbyo navyo na zoezi la kujiandikisha katika daftari la mkazi.


"Wapo wenzetu ambao wanasema tayari wanavitambulisho vya kupiga kura  vitambulisho  kwahiyo hawaoni sababu ya kujiandikisha tena , vile vitambulisho ni kwa ajili ya uchaguzi wa Mwaka kesho lakini kwa uchaguzi huu wa serikali za mitaa, serikali zamitaa ,vijiji na vitongoji tunakwenda kujiandikisha kwenye daftari la mkazi " 


Aidha, amewasihii siku ya kupiga kura wajitokeze mapema kwa ajili ya kutimiza wajibu nahaki ya kupiga kura mapema.


Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Bi. Zuwena Omary amesema kilammojaazishike tarehe hizo muhimu ambazo tarehe 11 hadi 20 Oktoba , 2024 kwa ajili ya kujiandikisha na tarehe 27 siku ya kupiga kura.