ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, July 28, 2023

Harmonize Ft Spice - Miss Bantu (Official Music Video)

 Harmonize Performing "Miss Bantu" Ft Spice ("Queen of Dancehall", the most prominent dancehall artists in the world.

DC KIBAHA ACHOCHEA UWAJIBIKAJI AMPA MOTISHA YA LAKI 5 DIWANI


Mkuu wa Wilaya ya Kibaha.Nikson Saimon akizungumza na madiwani wa halmashauri ya Kibaha mji katika kikao hicho.

Na Victor Masangu,Kibaha


Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nikson Saimon katika kuhakikisha anachochea zaidi chachu ya kufanya kazi kwa bidii na kuwaletea matokeo chanya ya kimaendeleo wananchi ameamua  kuanzisha mpango wa kuwapa motisha watumishi na madiwani ambao wanatekeleza majukumu yao ipasavyo kwa maslahi ya jamii.


Kwa kulitambua hilo Mkuu wa Wilaya hiyo ameamua kutumia kikao cha Baraza la madiwani wa halmashauri ya Kibaha mji kuwaeleza kwamba atakuwa anatoa zawadi na motisha mbali mbali kwa wafanyakazi ambao watakuwa mstari wa mbele katika kuwatumikia wananchi na kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo.

Katika kikao hicho cha Baraza la madiwani cha robo ya nne aliweza kutumia fursa ya kumtangaza Diwani wa kata ya mail moja Ramadhani Lutambi kuchaguliwa kuwa mshindi kutokana na kuonyesha juhudi zake katika Mambo mbali mbali ambapo amemzawadia kiasi cha shilingi laki tano kama zawadi kwake.

"Kwa sasa nimeweka utaratibu wangu wa kuwa natoa motisha na zawadi mbali mbali na leo hii nimeanza na madiwani na nitafanya hata kwa watumishi na watendaji wengine kwa hiyo diwani Lutambi nampatia zawadi hii ya shilingi laki tano kwa kuwa ndio amechagulia na jopo la watu mbali mbali,"alisema Mkuu huyo.

Aidha alifafanua kwamba kuchaguliwa kwa diwani huyo ni mwanzo tu na kwamba utaratibu huo utaendelea kufanyika na kwamba mpaka jina lake limeweza kupatikana sio Mimi pekee bali kuna jopo la watu wengi ambao wameweza kushiriki katika mchakato mzima wa ziezi hili la kumpata diwani Bora.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya aliwahimiza madiwani wote kuiga mfano wa diwani aliyeshinda na kuwataka kuendelea kuchapa kazi kwa bidii ikiwa sambamba na kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo ili iwe endelevu zaidi kwa maslahi ya wananchi wote.


Pia hakusita kuwakumbusha madiwani kuhakikisha wanakuwa wabunifu katika kutafuta vyanzo vipya vya mapato ikiwa sambamba na kuweka na kutunga sheria ndogo ndogo ambazo zitakuwa ni rafiki na sio kandamizi kwa wafanyabiashara.


Kwa Upande wake diwani huyo wa kata ya maili moja Ramadhani Lutambi alimshukuru kwa dhati mkuu huyo wa Wilaya kwa kutambua mchango wake katika kutimiza wajibu wa kuwatumikia wananchi na mpaka kumpatia motisha ya laki tano.

Lutambi pia aliahidi kuendelea kushirikiana na madiwani wenzake na kwamba hata zawadi ambayo amepatiwa ni kwa ajili ya heshima kubwa ya madiwani wenzake ambao wamekuwa wakishirikiana katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo.

Nao baadhi ya wananchi ambao walihudhulia katika kikao hicho walimpomgeza diwani huyo kwa kuibuka na ushindi pamoja na kumshukuru Mkuu wa Wilaya ya Kibaha kwa kuanzisha utaratibu huo ambao utasaidia zaidi watumishi na madiwani kutimiza majukumu yao kwa bidii.

                           MWISHO


TAASISI YA BILAL MUSLIM YATUMIA KUMBUKIZI YA KIFO CHA MJUKUU WA MTUME (S.A.W) KUCHANGIA DAMU HOSPITALI YA RUFAA BOMBO

 

 




Na Oscar Assenga, TANGA.

WANAFUNZI, walimu pamoja na waumini wa dini ya Kiislamu zaidi ya 130 kutoka Taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania Tawi la Tanga wametumia maadhimisho ya mwaka mpya wa kiislamu ulioambatana na kukumbukizi ya kifo cha Mjuu wa Mtume (S.A.W) Imam Hussein Ally kuchangia damu salama katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo

Mkuu wa shule ya Wasichana katika taasisi hiyo Sheikh Sajad Hassan akizungumza mara baada ya zoezi hilo alisema kuwa uchangiaji wa damu katika hospitali hiyo kawaida yao ya kila mwaka ikiwa ni ishara ya kuonesha moyo wa kujitolea wahitaji mbalimbali hususani watoto na mama wajawazito waliopo hospital wanaohitaji kuongezewa damu.

Mbali na kuchangia damu lakini pia waliwatembelea kwenye wodi ya wakina mama wajawazito na kugawa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa ikiwa ni sehemu ya kuwafariji.

Alisema kusudio la wao kuchangia damuni kujitolea sadaka ambayo wanaifungamanisha na na tukio la kuwawa kwa mjukuu wa bwana mtume (S.A .W) Hussein Bin Ally aliyeuwawa mwaka 61 Hijiria huko Irak aliyekuwa wakiipigania dini kwa lengo la kukemea mabaya na kuamrisha mema, aliyetoka kutetea wanyonge na wale waliodhulumiwa

Aidha alisema wao kama taasisi wamejiwekea utaratibu wa kufanya zoezi hilo kila mwaka katika maeneo tofauti tofauti lengo ni kuonyesha kwamba wamesimama pamoja na mjukuu wa bwana mtume (S.A.W) katika kutetea wanyonge.

“Tunaimani kwamba damu hii itasaidia wanyonge, pia tunasimama na kukemea dhuluma zozote zinazoendelea ulimwenguni" alisema Sheikh Hassan.

Awali akizungumza wakati wa zoezi hilo Mkuu wa Idara ya Maabara katika Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Sinde Ntobu ameishukuru Bilal Muslim kwa kuona kuwa wanayo nafasi kubwa kuokoa maisha ya watu wanaofika hospitalini hapo kupatiwa huduma ikiwemo kuongezewa damu.

Alisema uhitaji wa damu kwa mwezi katika hospital hiyo ni mkubwa tofauti na ile inayochangiwa ambapo uhitaji wao unafikia lita 500 hadi 600 wakiwa na upungufu wa damu kwa Unit 250 hadi 300 hivyo kuziomba taasisi na watu binafsi kuona umuhimu wa kuchangia damu ili kuokoa maisha ya watu.

" Sisi kama hospital kwa wastani kwa mwezi tunatumia chupa za damu 500 mpaka 600 lakini uwezo wa kuchangia damu ambayo inapatikana mara nyingi tunapata unit 250 mpaka 300 kwahiyo uhitaji wa damu kwa wagonjwa ni mkubwa "Alisema Mtobu

Hata hivyo aliiasa jamii kuona umuhimu wa kuchangia damu ili kuweza kuokoa maisha ya wengine wahitaji lakini baadae zinaweza kuwasaidia wanapokuwa wahitaji.

Thursday, July 27, 2023

MCHUNGAJI MUGOGO HUYU HAPA JIJINI MWANZA

 NA ALBERT G.SENGO/MWANZA.

Ile Event yetu pendwa kabisa ya Mwanza Couple’s Night Gala, imekaribia kabisa ni tarehe 12/08/2023 pale Gold Crest Hotel Mwanza. Hii ni bonge moja ya Event hutajuta kuhusika bali utafurahi sana

BARAZA LA MADIWANI KIBAHA MJI LAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUTOA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO




Na Victor Masangu,Kibaha


Baraza la madiwani Halmashauri ya mji Kibaha limeazimia kwa pamoja kumpongeza kwa dhati  serikali ya awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia kiasi cha shilingi bilioni 8.1 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2022/2023.


Akisoma taarifa ya mapokezi na matumizi ya fedha ya mwaka wa fedha 2022/2023 kutoka serikali kuu Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Kibaha Mussa Ndomba amebainisha kuwa fedha hizo zitakwenda kutekekeza miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo itasaidia kusogeza huduma kwa wananchi.

Ndomba alibainisha kwamba katika fedha hizo walizopatiwa zitakwenda kuleta chachu ya maendeleo hususan katika sekta ya elimu,afya,maji,utawala,nishati ya umeme,miundombinu ya barabara,pamoja na suala la uwezeshaji wananchi kiuchumi kupitia asilimia 10 ya makusanyo ya mapato ya ndani.

"Kwa Upande wa halmashauri ya mji kibaha kupitia Ofisi ya mkurugenzi tunamshukuru Sana Rais wetu kutupatia hizi fedha kwa kipindi hiki cha mwaka 2022/2023 kiasi cha zaidi ya bilioni 8.1 hii ni sawa na asilimia 100 kutoka vyanzo mbali mbali.
 

Mwenyekiti huyo alibainisha kuwa vyanzo hivyo ni kutoka serikalini kuu, kiasi cha shilingi bilioni 1,969,958,103,.91 fedha kutoka kwa wahisani na wadau wa maendeleo ni bilioni 2.5,fedha zilizotolewa nje ya bajeti ni bilioni 2.2 huku fedha za mapato ya ndani ni shilingi bilioni 1.4.

Kadhalika alifafanua kuwa kwa Upande wa nishati ya umeme imeendelea kuwa vizuri kutokana na kutekelezwa kwa miradi mikubwa miwili katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023 ambayo itaweza kusaidia upatikanaji wa nishati ya umeme kwa wananchi ambao walikuwa wana changamoto hiyo.


Kuhusiana na uboreshaji wa miundombinu ya barabara kupitia Tarura halmashauri hiyo ina mtandao jumla ya kilometa 504.27 ambapo kati ya hizo kilometa zipatazo 25.33 ni lami,kilometa 89.70 ni changarawe,huku kilometa 389.24 zipo katika hali ya udongo.

Akifafanua kuhusiana Tanroad mtandao wa barabara kuu zinazosimamiwa na Mkoa zina urefu wa kilometa 503.66 ambazo zote ni kiwango cha lami huku barabara nyingine za Mkoa zina jumla ya kilometa 875.75 ambazo zimejumuisha kilometa 49.71 za tabaka la lami na kilometa 826.30 udongo wa changarawe na udongo.


Aidha Baraza hilo la madiwani limetoa ombi maalumu kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuiwezesha halmashauri ya mji Kibaha kupandishwa adhi na kuwa manispaa kutokana na kuwa makao makuu ya Mkoa wa Pwani.



Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nikson Saimon amewataka madiwani hao kuhakikisha wanawatumikia wananchi wao ikiwa sambamba na kuweza kusimamia miradi mbali mbali ya maendeleo katika sekta tofauti.


Pia alilihimiza baraza hilo la .madiwani kutunga sheria ndogo ndogo usheria ndogo ndogo ambazo zitaweza kuwa rafiki zaidi kwa wafanyabiashara wadogo ili wasiwe na vikwazo vyovyote katika utekelezaji wa kujipatia kipato.

JUMUIYA YA WAZAZI CCM WILAYA YA TANGA YAHIMIZA JAMII KUTUNZA MAZINGIRA


KATIBU wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga Urassa Nanyaro kulia akipokea miti kwa ajili ya kuupanda wakati Jumuiya hiyo iliposhiriki kwenye kampeni inayoendeshwa na Taasisi ya Tea inayojishughulisha na mazingira ikiwemo upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali kwenye Jiji hilo ambapo miti hiyo ilipandwa kituo cha Afya Mwakidila
KATIBU wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga Urassa Nanyaro kulia akipanda miti  wakati Jumuiya hiyo iliposhiriki kwenye kampeni inayoendeshwa na Taasisi ya Tea inayojishughulisha na mazingira ikiwemo upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali kwenye Jiji hilo ambapo miti hiyo ilipandwa kituo cha Afya Mwakidila


Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi wakiwa kwenye picha ya pamoja  mara baada ya kumalizika zoezi la kupanda miti wa pili kutoka kulia ni Mjumbe wa Wazazi wilaya ya Tanga Pamela Chaula


Na Oscar Assenga,TANGA.


KATIBU wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga Urassa Nanyaro ameshiriki kwenye kampeni ya upandaji wa miti katika kituo cha Afya Mwakidila Jijiji Tanga huku akiitaka jamii kuendelea kutunza mazingira.

Nanyaro aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati Jumuiya hiyo iliposhiriki kwenye kampeni inayoendeshwa na Taasisi ya Tea inayojishughulisha na mazingira ikiwemo upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali kwenye Jiji hilo.

Alisema kwamba wananchi na jamii kwa ujumla wanapaswa kutunza mazingira kwa mustakabvali wa kuimarisha vyanzo vya maji na uchumi wa Taifa letu kwa sababu maji ndio chanzo kikubwa cha nishati ya umeme.

Aidha alisema na nishati ya umeme inapatikana kutokana na utunzaji mazingira na unapandwaji wa miti na hivyo kupatikana mvua za kutosha zinazopelekea mitambo ya kuzalisha umeme kutokana na uwepo wa mvua za kutosha.

“Niipongeze taasisi ya Tea kwa kuendesha kampeni hii kwani miti inapopandwa inasaidia kupata lishe,kivuli na matunda na kuwasaidia kuwezesha kupata mvua ya kutosha itakayowezesha kuendesha mitambo na kuzalisha nishati ya umeme inayotumika hospital viwanda na kuinua uchumi wa Taifa letu”Alisema Nanyaro.

Akiwa katika shule ya Msingi Mwakidila Katibu huyo aliwapongeza walimu wa shule hiyo kutokana na utunzaji wa mazingira na wana hifadhi ya mazingira ambayo ndio chanzo za utunzaji huo

“Sisi Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga majukumu yetu ni kushrikiana na shule za msingi ,awali,sekondari vyuo Lengo kuhamasisha vijana wapate malezi bora kulingana na tamaduni ya kitanzania tupo hapo leo wanapoanda miti ya matunda na kwa hali hiyo tuliokuta tunaamini miti itakuwa kwa muslakabali wa viumbe hali na kutunza vyanzo vyetu na vya maji “Alisema

Hata hivyo alisema licha ya utunzaji wa vyanzo vya maji lakini pia mwisho wa siku kupitia mazingira mazuri Taifa liweze kusonga mbele kiuchumi likiwa na watu wenye afya na siha njema.

MWENYEKITI WA VIJANA KKKT (KDMs) USHARIKA WA MAKORORA ATOA NENO KWA WAHITIMU WA CHUO CHA AFYA TANGA

 

 



Mwenyekiti wa Vijana KKKT (KDMs) Usharika wa Makorora Jimbo la Pwani Steven Mduma amewataka wahitimu Chuo cha Afya –Bombo kuzingatia upendo na uaminifu kufikia malengo yao waliojiwekea.



Mduma aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati wa akizungumza katika mahafali ya Umoja wa Wanafunzi Wakristo katika chuo hicho ambapo alisema kwamba hayo ndio mambo muhimu ya msingi ya kuzingatia baada ya kumaliza chuo ili waweze kufikia ndoto zao walizojiwekea wanapokuwa kazini.

Mduma aliwataka pia wahitimu hao kujiepusha na vitendo vya rushwa kwani vinakwamisha juhudi za kimaendeleo na kupelekea kushindwa kutimiza malengo yao hivyo wahakikishe wanaachana navyo.

“Ndugu zangu leo hii mnatarajiwa kumaliza hapa chuoni na kwenda kwa jamii hivyo niwaase mhakikishe mnakwenda kuishi kwa, uaminifu, upendo mkiwa kama vijana leo mnahitimu kutoka hatua moja kwenda nyengine”Alisema

Hata hivyo aliwataka pia wanaohitimu kwenda kufanya kazi kwa ujasiri, nguvu na uaminifu ambao utakuwa chachu yao kuweza kufikia mafanikio.

Aidha katika Halfa hiyo Mwenyekiti huyo alihaidi kutoa laki tano kwa ajili ya kuchangia vyombo vya mziki na kutunisha mfuko wa umoja huo ili kuhakikisha wanapiga hatua ,kubwa za kimaendeleo










Wednesday, July 26, 2023

ZAIDI YA MAKAMPUNI NA TAASISI 420 KUSHIRIKI MAONESHO YA BIASHARA AFRIKA MASHARIKI

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

TCCIA yapania kutumia maonesho kutatua changanmoto za wawekezaji wajasiliamali na viwanda vidogo. Maonesho kufanyika katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza.

Sunday, July 23, 2023

Yanga SC 1-0 Kaizer Chiefs | Highlights | Friendly Match - 22/07/2023

 Highlights: hapa chuma cha Kennedy Musonda assist saafi kutoka kwa Maxi Mpia akiwaadhibu Kaizer Chiefs kwenye mechi ya kirafiki ilivyochezwa kwenye kilele cha Wiki ya Mwananchi Julai 22, 2023.