ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, August 20, 2016

STAND UNITED YAIKARIBISHA LIGI KUU MBAO FC KWA SARE 0-0

Kocha Mkuu wa Mbao Fc Echien Ndelgije raia wa Burundi akitoa maelekezo kwa mmoja wa wachezaji wa timu yake katika mchezo wa Ligi kuu soka Tanzania Bara kati ya Stand United ya mjini Shinyanga iliyoikaribisha Mbao Fc ya Mwanza, Hadi mwisho timu izo zilitoka sare 0-0.
 BOFYA HAPA KUPATA KILICHOJIRI.
Mchezo ukiendelea ndani ya dimba la CCM Kambarage mjini Shinyanga baina ya Stand United V mbao Fc.
Timu zote zilicheza mchezo wa kukamiana, nao mabeki wakifanya kila liwezekanalo kuweka ukuta wa nguvu kuhakikisha hakuna makosa yanayoweza kuleta madhara.
Licha ya uchanga wao Mbao Fc wamecheza soka tamu na la kuvutia lenye pasi fupifupi kiasi cha kuwastaajabisha wengi kwamba hii  ndiyo mara yake ya kwanza kutinga Ligi kuu soka Tanzania Bara.
Ndni ya dimba la CCM Kambarage.
Mshambuliaji wa Mbao Fc mbele ya ukuta wa Stand United.
Kasi ya mchezo na umakini.
Kachomoka huyo....
Kosakosa langoni mwa Stand United V Mbao Fc.
Jukwaa kuu macho kwenye kandanda.
Hata hivyo kwa mabadiliko ya Stand United, yaiyofanyika kipindi cha pili hayakuleta matokeo ya ziada.
Kocha Mkuu wa Mbao Fc Echien Ndelgije raia wa Burundi akitoa maelekezo kwa wachezaji wa timu yake katika mchezo wa Ligi kuu soka Tanzania Bara kati ya Stand United ya mjini Shinyanga iliyoikaribisha Mbao Fc ya Mwanza, Hadi mwisho timu izo zilitoka sare 0-0.
Mbao Fc.
Toka Mwanza hawa ni mashabiki wa Mbao Fc na hii ndiyo kona yao.
Utawala wa soka na hisia za wapenzi wa soka.
Hadi dakika 90 za mchezo zinamalizika.

KAMANDA MPINGA AHITIMISHA KILELE CHA SHINDANO LA UCHORAJI KWA AJILI YA KUHAMASISHA USALAMA BARABARANI KATIKA SHULE ZA MSINGI JIJINI DAR

Hii ni zawadi ya heshima (tuzo) iliyotolewa na kampuni ya Puma Energy Tanzania na kukabidhiwa kwa mshindi wa kwanza,Mwanafunzi wa darasa la sita kutoka shule ya Msingi Bunge,Veronika Inocent.


Mkurugenzi Mkuu kutoka kampeni ya Puma Energy Tanzania Ltd,Philippe Corsaletti akimkabidhi tuzo/zawadi ya Begi na cheti mwanafuzi wa darasa la sita kutoka shule ya Msingi Bunge,Veronika Inocent baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika Kilele cha shindano la Uchoraji kwa ajili ya kuhamasisha usalama barabarani katika shule za msingi jijini Dar Es Salaam kwa mwaka 2016,hafla hiyo fupi iliyoandaliwa na Kampuni ya Puma Energy Tanzania ilifanyika mapema leo katika viunga vya shue ya msingi Bunge.

Mashindano hayo yalihusisha shule kumi kwa upande wa Dar Es Salaam ambazo ni    Mwananyamala,Kisutu,Bunge,Kisiwani,Mchangani,Mnazini,Mwananyamala B,Mikocheni,Mtendeni,Kisutu,Kisiwani na Ugindoni,Shule nyingine tatu ni kutoa mkoa wa Geita ambazo zitashiriki na mchakato wa kuwapata washindi,matokeo ya washindi wa mwisho yatatangazwa wakati wa kilele cha cha wiki ya Usalama barabarani ambayo inatarajia kufanyika hivi karibuni 
Mwanafuzi wa darasa la sita kutoka shule ya Msingi Bunge,Veronika Inocent akilia kwa furaha mara baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika Kilele cha shindano la Uchoraji kwa ajili ya kuhamasisha usalama barabarani katika shule za msingi jijini Dar Es Salaam kwa mwaka 2016,hafla hiyo fupi iliyoandaliwa na Kampuni ya Puma Energy Tanzania ilifanyika mapema leo katika viunga vya shue ya msingi Bunge.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamanda Mohamed Mpinga pamoja na Waandaji kutoka kampuni ya Puma Energy Tanzania na AMEND wakitafuta washindi watatu wa shindano la uchoraji katika masuala mazima ya kuhamasisha usalama barabarani 2016.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamanda Mohamed Mpinga akimkabidhi Mwanafunzi wa darasa la sita,Shaaban zawadi ya Begi na Cheti,kutoka shule ya msingi Bunge baada ya kuibuka mshindi wa tatu katika Kilele cha shindano la Uchoraji kwa ajili ya kuhamasisha usalama barabarani katika shule za msingi jijini Dar Es Salaam kwa mwaka 2016,hafla hiyo fupi iliyoandaliwa na Kampuni ya Puma Energy Tanzania ilifanyika mapema leo katika viunga vya shue ya msingi Bunge.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamanda Mohamed Mpinga akimkabidhi Mwanafunzi wa darasa la sita Antonia Anthony zawadi ya Begi na Cheti,kutoka shule ya msingi Mwananyamala baada ya kuibuka mshindi wa pili katika Kilele cha shindano la Uchoraji kwa ajili ya kuhamasisha usalama barabarani katika shule za msingi jijini Dar Es Salaam kwa mwaka 2016,hafla hiyo fupi iliyoandaliwa na Kampuni ya Puma Energy Tanzania ilifanyika mapema leo katika viunga vya shue ya msingi Bunge.
Picha ya Pamoja na Washindi watatu shindano la Uchoraji kwa ajili ya kuhamasisha usalama barabarani katika shule za msingi jijini Dar Es Salaam kwa mwaka 2016.

Baadhi ya Wanafunzi walioshiriki na kuibuka na zawadi kutoka Kampuni ya Puma Energy Tanzania . 
Mkurugenzi Mkuu kutoka kampeni ya Puma Energy Tanzania Ltd,Philippe Corsaletti alisema kuwa shindano hilo linalenga kusaidia kuelimisha Wanafunzi wa shule za msingi katika masuala ya Usalama barabarani."Mpangp wetu wa usalama barabarani kwa mashule hapa Tanzania ulianza toka mwaka 2013 na mpaka sasa shule za msingi zipatazo 30 zimeshiriki,ikiwa ni jumla ya wanafunzi 38,638",alisema Philippe.Alisema kuwa shindano hilo pia linalenga kumpatia Mwanafunzi nafasi ya kushiriki mawazo

Friday, August 19, 2016

MISS MWANZA KUPIGWA USIKU HUU (LEO IJUMAA TRH 19) GOLD CREST HOTEL

#Hakunaaaa caption maelezo yanajieleza.

USIKU WA JESTINA.

 Bi harusi Mtarajiwa, Jestina Julius akiwa katika pozi kabla ya kuanza kupambwa, ambapo anatarajiwa kuagwa katika ukumbi wa Unenamwa uliopo Kimara Jijini Dar es Salaam hivi punde na kufatiwa na Hafla ya Sherehe ya Harusi inayotarajiwa kufungwa Agosti 21, 2016. katika kanisa la Waebrania (E.A.G.T) lililopo kimara Dar es Salaam. (PICHA NA KHAMISI MUSSA)
 Biharusi katika muonekano wake
 Bi harusi Mtarajiwa, Jestina Julius akiwa atika tabasam



 Bi harusi Mtarajiwa, Jestina Julius akipambwa na Domitila Mbawala ambaye ni Mmiliki wa Clara Beauty Salooni  liyopo Kimara Suka Dar es Salaam ,ambapo Sherehe ya hafla hiyo itafanyika katika Ukumbi wa Unenamwa na kufatiwa na Ndoa inayo tarajiwa kufungwa Agosti 21, 2016 Dar es Salaam  katika kanisa la Waebrania (E.A.G.T) lililopo kimara . (PICHA NA KHAMISI MUSSA)
Mpambe wa bi harusi mtarajiwa Mrs Shija, Upendo Shija akipambwa na Domitila Mbawala ambaye ni Mmiliki wa Clara Beauty Salooni  liyopo Kimara Suka Dar es Salaam.

SOKA NI AJIRA, DC MORO AWAMBIA VIJANA RISING STARS.

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mheshimiwa Regina Chonjo akipiga mpira kuashiria ufunguzi Airtel Rising Stars mkoa wa Morogoro kwenye uwanja wa Jamhuri jana. 
 Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mheshimiwa Regina Chonjo akikagua timu wakati wa ufunguzi wa Airtel Rising Stars mkoa wa Morogoro kwenye uwanja wa Jamhuri jana.
Soka ni ajira, DC Moro awambia vijana Airtel Rising stars

Morogoro, Jumatano Agosti 17 2016 … Mkuu wa wilaya ya Morogoro Mheshimiwa Regina Chonjo amewataka vijana kuonyesha vipaji vyao vya soka na kutambua kuwa mchezo huo ni fursa nzuri inayoweza kuwapa maisha bora na kusaidia ukuaji wa uchumi wa nchi.

Mheshimiwa Chonjo aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mashindano ya soka ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars kwa mkoa wa Morogoro uliofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa mchezo huo.

“Napenda kutumia fursa hii kutoa rai kwa wazazi na walezi kuwahamasisha vijana kushiriki michuano hii ili kuendeleza vipaji vyao na kusaidia juhudi za serikali za kuinua kiwango cha mchezo wa soka hapa nchini”, alisema. Zaidi ya wachezaji  120 walihudhuria uzinduzi huo

Alisema mbali ya kuwa burudani, mpira wa miguu pia hudumisha amani, umoja, urafiki, udugu miongoni mwa viongozi na wachezaji na kuwafanya vijana kuwa wakakamavu, wachangamfu na wenye afya bora. “Lakini muhimu zaidi mpira wa miguu ni chanzo cha ajira kwa vijana wengi duniani”, alisema .

Aliwataka viongozi wa soka mkoa wa Morogoro kufuatilia kwa karibu michuano hiyo na kuchagua wachezaji wenye vipaji ili kuuwezesha mkoa huo kufanya vizuri katika fainali za Taifa za Airtel Rising Stars zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 6 hadi 11.

Alisema michuano ya Airtel Rising Stars imekuwa ni jukwaa la kusaidia kubaini wachezaji wenye vipaji kutoka sehemu mbalimbali ambao bila mashindano haya wangeweza kupotea hivi hivi. Aliwataka viongozi wa soka mkoa humo kushirikiana na shirikisho la soka nchini (TFF) kuwalea na kuwaendeleza vijana wanaopatikana kupitia Airtel Rising Stars.

Akiongea katika hafla hiyo ya ufunguzi, mwenyekiti wa wa chama cha Soka mkoani Morogoro Pascal Kihanga ambaye pia ni Mustahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro aliwataka vijana kucheza kwa kujituma ili kuweza kuchaguliwa kuunda timu ya mkoa.

Kwa upande wake, Meneja wa Airtel mkoa wa Morogoro Omar Bongo alisema kuwa kampuni ya Airtel inajivunia kuweza kupata fursa ya kutoa mchango katika soka la Tanzania. “Airtel Rising Stars imekuwa chimbuko la wachezaji wa timu za Taifa na klabu hapa nchini”. Tunaona fahari kuweza kupata fursa ya kudhamini soka nchini Tanzania“alisema Bongo.


Hafla hiyo ya ufunguzi ilishuhudia mchezo wa ufunguzi kati ya Moro Kids na Techforty ambapo Moro Kids waliibuka na ushindi wa 2-0. Katika mchezo mwingine, Mwere Kids iliishinda Kizuka 2-1.

PICHA:- HARUSI YA MR & MRS MODECAI ILIVYOFANA.

Bustanini...
Maharusi wakiingia kanisani.
Ibada ya ndoa takatifu kwa Mr. na  Mrs Modecai.
Pete zikibarikiwa.
Na sasa ni ndoa, pete kwa Bi harusi.
Pete kwa Bi. Harusi.
Pete kwa Bwana Harusi.
Ishara ya mapendo.
Mchungaji akibariki ndoa.
Vazi na pendeza ya Bi. Harusi.
Bwana Harusi na mpambe wake.
Maua.
The area kwa bustani.
Na frendZ...!!
Another angle na wapambe.
Ukumbini.
Ufunguzi wa sherehe.
Kata utepe kuashiria, sherehe sasa ni kule kunywa na kucheza.
Aksanteni kwa kuja.