ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, February 4, 2012

IPATE SASA MADUKANI ALBUM YA PHILBERT KABAGO 'MOYO WANGU' KATIKA CD


Mwonekano kwa mbele..



Ngoma zilizomo.


Mzigo uko madukani sasa
Ili upate ladha ya uhakika:-
Hakikisha unanunua nakala halisi.

KIROBA ORIGINAL CHATINGA KATIKA MAANDALIZI SHEREHE YA MIAKA 35 YA KUZALIWA CCM

Mkuu wa masoko toka Megatrade Investiment Limited James Njuu (wapili kulia) akikabidhi katoni ya K-Vant kwa Katibu Mwenezi wa Mkoa wa Mwanza Simon Mangelepa itumike kama sehemu ya kusherehesha maadhimisho ya miaka 35 ya kuzaliwa Chama cha mapinduzi. Aliyesimama katikati ni Mjumbe kamati ya siasa Ally Mambile na afisa habari CCM Mwanza C. Katulanda.

Mkuu wa masoko wa kampuni ya Megatrade Investment Ltd James Njuu amesema kampuni yake iko kwaajili ya kusherehesha mahali popote na watu wote kwa kuzingatia umri hivyo kwa kutambua kuwa kwenye maadhimisho hayo marafiki watakusanyika toka sehemu mbalimbali basi si hasara kuburudika na kinywaji chenye faida kilicho na nguvu mwanzo mwisho 'KIROBA ORIGINAL'.

Maandalizi nje ya mjengo yanaendelea kama kawa watu wakijinunulia sare.

Hapa biashara inafanyika.

Ni matayarisho tu kwa misafara.

Friday, February 3, 2012

VALLENTINE SPECIAL OFFER FOR THE LADIES

Shop and Brunch together with Cassandra Lingerie invites you to a Valentines Special Shopping event on the 11th of februray 2012, at the thai village 10 am till 5pm.

As usual champagne on the house.
sponsored by:Pearly Bay.

Karibu Sana!
Eugenia.

USIKU WA 'DIVA' LOVENESS LOVE JANA ULIKUWA NOWMA KUPITIA CLOUDS RADIO & CLOUDS TV

Host wa kipindi cha Ala za Roho loveness Love on air clouds Tv...

Music live toka kwa wasanii uling'arisha usiku wa Ala za Roho...

Q. Chief aliachia new track usiku huo akimshirikisha mwanadada huyu pichani...ambapo vilevile kitu kilipigwa live

Best collabo la RnB..

Diva akisain OUT... kwa mujibu wake utamaduni huu wa live kupitia Clouds Tv sanjari na Clouds Tv hufanyika mara moja kila mwezi hivyo next tyme uskoseEee..

MAMA YAKE DROGBA AWAPIKIA MASHABIKI

Wakati mshambuliaji wa Ivory Coast Didier Drogba ambaye ni 'supa staa' wa afrika akiwa uwanjani, mama yake anawapikia chakula mashabiki wa nchi yake katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, hii inadhihirisha wazi kuwa familia hiyo haichagui kazi bali yatumia kila nafasi ya kujipatia kipato inayojitokeza ndani ya jamii kama watu wengine.
Clotilde Drogba amefungua mgahawa karibu na uwanja wa mpira katika viunga vya mji mkuu wa Equatorial Guinea, Malabo, limeripoti shirika la habari la AP. Mama huyo anapika kuku na samaki na wali, ndizi na vyakula vingine kwa ajili ya mashabiki, wakati mwanaye akila chakula cha hoteli aliyofikia pamoja na wachezaji wenzake.

Mama yake Drogba pia alipika chakula kwa ajili ya mashabki wakati wa Kombe la Dunia mwaka 2006 nchini Ujerumani.

Drogba ni mmoja wa watu maarufu sana nchini Ivory Coast, na mwaka jana alijumuishwa katika Tume ya Ukweli na Maridhiano iliyoundwa ili kupunguza mvutano uliotokana na utata wa matokeo ya uchaguzi na miaka mingi ya mgawanyiko.

Kundi la mashabiki wapatao 60 limesafiri kwenda Equatorial Guinea, ambapo Ivory Coast inacheza mechi zake za awali, na kila siku mashabiki hao wanapata chakula chao cha asili kilichopikwa na mama wa mshambuliaji wao mashuhuri.

"Kila mtu anafanya anachopenda kukifanya," Amesema mama yake Drogba, huku akiwa amevalia nguo za rangi ya chungwa ambayo huvaliwa na Ivory Coast.

"Hii sio kwa sababu ya mwanangu, ni kwa sababu ya kuunga mkono taifa langu."

Mama yake Drogba aliiambia AP kuwa alitazama mechi za ufunguzi kupitia televisheni huku akiwa anakata nyanya na vitunguu na kupika kuku.

Amesema ana imani ya kutazama mechi ya nusu fainali kwenye uwanja wa Bata - iwapo Drogba na timu yake watafuzu, anaheshimu sheria, na hiyo ina maana kuwa mwanaye hawezi kula chakula chake wakati huu - anatakiwa kula chakula cha hotelini tu kwa mujibu wa utararibu.
Mama yake Drogba ameiambia AP kuwa ana uhakika atamuona mwanaye akilibeba Kombe la Mataifa ya Afrika

Thursday, February 2, 2012

KINGKIKI KUPEPEA KITAMBAACHEUPE VALENTINE'S DAY NDANI YA GOLD CREST MWANZA

Hakikisha unakuja na kitambaa cheupe ili iwe ishara ya mapenzi ya dhati kwa yule umpendaye.

JESHI LA KENYA LATEKA MJI WA BADHADHE

Jeshi la Kenya limesema limefanikiwa kuuteka mji mmoja muhimu kusini mwa somalia kutoka kwa wapiganaji wa kiislamu wa al-shabaab.

Msemaji wa jeshi la Kenya Major Emmanuel Chirchir ameiambia bbc kuwa majeshi yake yameuteka mji wa Badhadhe, hatua ambayo ameitaja kama pigo kubwa kwa wapiganaji hao wa Kiislamu.

Duru kutoka mji huo zinasema kuwa wanajeshi wa Kenya wakisaidiana na wapiganaji wa kundi la wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya mpito nchini Somalia, waliuteka baada ya mapigano makali.

Msemaji wa jeshi la Kenya, meja Emmanuel Chirchir, amesema kuwa kutekwa kwa mji huo ni pigo kubwa kwa kundi la wanamgambo la al-shabaab.

Hatua hiyo ina maana kuwa njia waliokuwa wakitumia kutoka baharini kuingia nchi kavu sasa imezibwa.

Major Chirchir kadhalika amesema kuwa mji huo wa Badhadhe ulikuwa muhimu sana kwa wanamgambo hao kwa kuwa ulitumiwa kutoa mafunzo ya kivita.

Mara kadhaa serikali ya Kenya imezungumzia ushindi wake wa kuteka miji kadhaa. Mafanikio yao mengi hata hivyo yamekuwa ni kuteka miji midogo tu.

Hata hivyo utekaji wa mji wa Badhadhe ni hatua kubwa kwa sababu ni makao makuu ya wilaya katika eneo la Juba ya chini.

Majeshi ya Kenya yaliingia Somalia Octoba mwaka uliopta na serikali ilisema kuwa lengo lilikuwa ni kupambana na kundi la Al- shabaab ambalo lilidaiwa kutekeleza utekajinyara wa wageni wa kigeni ndani ya Kenya.

Inaaminika lengo kuu la majeshi ya Kenya ni kuuteka mji wa Kismayu ulioko pwani ya Somalia.


CHANZO: bbc swahili

NAPE ATOA TAMKO POSHO ZA WABUNGE

Kuelekea maadhimisho ya miaka 35 ya CCM yaani Tarehe 5 February 2012, Katibu Mkuu wa Uenezi CCM Nape Mnauye atoa tamko la chama juu ya Posho za wabunge akiwa jijini Mwanza.
Taarifa zaidi sikiliza Clouds fm Habari leo jioni saa 18:00, Aplifaya na Dondoo za habari Clouds TV saa 20:00.

VILLA PARK RESORT VALENTINE'S EVE ft KIDUMU & BODA BODA BAND/SUPER KAMANYOLA

Shijani Mtunga meneja Villa Park.
Kusherehekea siku ya wapendanao duniani trh 14feb2012 Club Villa Park imeamua kumleta msanii Kidumu kutoka nchini Burundi kama zawadi kwa wateja wake atakaye burudisha sambamba na bendi ya Super Kamanyola.

Thomas Gikiro Meneja PSI Mwanza.
Uhusiano wetu na tukio hili ni kuhakikisha wapendanao wanatimiza jukumu la kuhakikisha usalama wao kwa kutumia ipasavyo salama kondom kuepuka maambukizi ya virusi vya ukimwi, magonjwa ya zinaa na mimba zisizotarajiwa kwa wale ambao tafsiri yao ya siku hii huitafsiri vibaya.

Abdalah Kijangwa
Zawadi ni kama kawa Tiketi ya ndege kwa wawili wapendanao kwenda na kurudi Mwanza-Dar kupitia Precision Air.

Zawadi nyingine ni Comlimentary ya kuhudhuria matukio muhimu Villa Park na usiku moja uliolipiwa katika hotel ya Gold Crest na mengine kibao... Chini ya Udhamini wa PSI, Tanzania Breweries LTD, Precision Air, Coca Cola NBCL, Gold Crest Hotel na Semira Electronics.

BLOGU MPYA YA RURAL AND URBAN HIYOO HEWANI


Blog mpya ya Rural and Urban
Heshima zenu Wadau wote Nilikuwa napenda Kuwatambulisha Kwenu Blog mpya ya Rural and Urban ambayo itakuwa ikizungumzia maisha hayo zaidi ya mjini na Vijijini. Karibuni sana ukiona Link hii mpatie na mwengine. Natanguliza Shukrani zangu asanteni.

Kutembelea Libeneke hili Bofya hapa:
www.mrs-ca.blogspot.com

Wednesday, February 1, 2012

WAFANYABIASHARA WATOA MATAIRI 50 KWAAJILI YA MAKARANDINGA JESHI LA POLISI MWANZA

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza Liberatus Barlow akikabidhiwa rasmi mchango wa matairi 50 yaliyotolewa asubuhi ya leo na mfanyabiashara maarufu Zuri Nanji kwaajili ya makarandinga ya jeshi hilo.

Mfanyabiashara Zuri Nanji amesema kuwa msaada huo ni kielelezo tosha cha utendaji bora wa jeshi la polisi Mwanza na amesihi jeshi hilo kuendeleza sera yake ya ulinzi shirikishi.

Kamanda Barlow akikagua umadhubuti wa matairi hayo yenye jumla ya thamani ya shilingi milioni 20.

Sehemu ya maafisa wa jeshi la polisi walioshiriki makabidhiano hayo yaliyofanyika mbele ya ofisi za jeshi la polisi Mwanza.

Mfanyabiashara maarufu Josephat Musukuma (anayezungumza) alitoa shilingi milioni moja kwaajili ya mfuko wa magari ya doria ambayo yamekuwa yakikumbwa na kadhia ya kukwama kufika sehemu za matukio kutokana na uhaba wa mafuta sambamba naye Mfanyabiashara Riziki Mbise wa Kampuni ya Mambo ya Chinga Investiment (katikati) akikabidhi mchango wake wa milioni moja taslimu kwa katibu wake wa mfuko wa wafanyabiashara kwenda kwa jeshi la polisi.

Kamanda wa kikosi cha Doria na Ulinzi shirikishi Philip Karage akitoa shukurani kwa mchango huo.

'KITU KASHATA MMmma' ni karandinga lililofungwa tairi zote mpya.

Naye mfanyabiasha Rashid alitoa lita 400 za mafuta kwaajili ya vyombo vya doria, msaada huo utalinusuru jeshi la polisi na aibu ya makarandinga yake na pancha za mara kwa mara wakati wa safari zake pamoja na kukwama kutokana na uhaba wa mafuta.

Tuesday, January 31, 2012

SAFARI YA WANAMABADILIKO KISIWA CHA UTALII RUBONDO

Brogu hii ya jamii http://www.gsengo.blogspot.com/ hivi karibuni ilialikwa kuhudhuria uzinduzi wa jukwaa la Wanamabadiliko, Safari ilianza kuelekea Rubondo National Park mahala palipo chaguliwa kwa tukio.

Kisiwa cha utalii Rubondo kina visiwa vyake vidogovidogo na hiki ni moja wapo yaani ni 'full green' mwaka mzima.

Wanamabadiliko walitia nanga hapa mara baada ya safari yenye misukosuko ya takribani saa mbili.

Kaunta ya bar iliyotengenezwa mithili ya mtumbwi.

Safari ya Wanamabadiliko kuelekea sehemu za mapumziko..

Ajabu-Njiani tulimwokota samaki huyu fresh aina ya sato akiwa ameliwa macho yote na ndege.

Swali ni kwamba kwanini aliliwa macho tu?

Kuna vyumba vya hotel lakini nilichaguwa kujipumzisha humu.

Kutoka kushoto ni Mwanamuziki Ismail, CEO wa blogu hii, Fred Katulanda na Richard Mabala.

Mti ndani ya maji uliojaa vichale vya ndege...

Mwanamabadiliko Wilhelmin aka Masai akiota moto ndani ya night kali'

Nyama choma zilichomeka kinoma noma...

Kisha baadaye msosi hapa ilikuwa mishale ya saa saba hivi mara baada ya uzinduzi wa Jukwaa la Wanamabadiliko.

Msosi na 'fulu sevisi mboga saba kujisevia...'

Niasubuhi tena mapemaaa.. na atuamshaye hapa ni Katibu wa jukwaa F. Katulanda kwa ajili ya safari kurejea 'mAhOmU' nakumbuka Usiku tuliinjoi kweli sauti za Hipopotamus kula nyasi pembezoni mwa tents na ngurumo zao.

Wanamabadiliko wakiongozwa na mr. Katulanda (C) wakipata flash nyuma yao mmeona lakini....

Taswira ndiyo hii...

Safari imeiva, bai bai kisiwa cha Rubondo.

Ni askari wa hifadhi hii aliyetupa eskoti kuhakikisha tunafika salama.