ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 24, 2023

BMH, BOMBO KUENDESHA KAMBI YA HUDUMA MBALIMBALI ZA KIBINGWA JIJINI TANGA

 

 


Na Oscar Assenga, Tanga

HOSPITALI ya Benjamini Mkapa (BMH) ikishirikiana na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo wanatarajia kufanya kambi ya huduma mbalimbali za kibingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kuanzia February 27 hadi Machi 3 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo Dkt Naima Yusuf (Pichani) alisema kwamba maandalizi ya kuelekea kambi hizo yanaendelea vizuri huku akieleza huduma za kibingwa zitakazotolewa.

Dkt Naima alisema huduma zitakazotolewa ni Upasuaji Mishipa ya Fahamu ,Mifupa, Mfumo wa Haja ndogo (Mkojo),Magonjwa ya ndani,Tiba ya Figo,Tiba ya Moyo kwa watoto na watu wazima.

Alizitaja huduma nyengine zitakazotolewa ni Magonjwa ya watoto Magonjwa ya macho,Tiba ya Kinywa na Meno pamoja na Magonjwa ya Uzazi kwa akina Mama.

Hata hivyo Dkt Naima alisema kwamba katika kambi hiyo wateja wa bima ambao watapokelwa ni wa Jubilee Insurance,Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF),Assemble Insurance na Strategis Insurance.

.

WANAUME WANAOPIGA WAKE ZAO VIBAO/MAKOFI CHANZO CHA UKIZIWI - KUELEKEA SIKU YA USIKIVU DUNIANI PT 1

NA ALBERT G. SENGO/MWANZA Tatizo la usikivu linazidi kuongezeka siku hadi siku. Inakadiriwa kuwa zaidi ya asilimia 5 ya watu duniani wana tatizo la usikivu. Kipigo na makofi karibu na maeneo ya sikio imesababisha watu wengi hususani akinamama kuwa viziwi. Kuelekea Maadhimisho ya 'SIKU YA USIKIVU DUNIANI' inayoadhimishwa kila mwaka na kilele chake Tarehe 3 mwezi March, tunazungumza na Dr. Olivia Michael Kimario ambaye ni daktari bingwa wa kichwa, koo, pua, masikio na shingo, kutoka Hospitali ya Rufaa ya Bugando ambaye sanjari na kutoa elimu pia ametoa wito kwa kila mmoja wetu kuchukua hatua kujikinga na vitendo vinavyosababisha changamoto hiyo ikiwemo jamii hususani akinababa kuepuka kuwapiga wapenzi wao vibao au ngumi masikioni. Kuelekea maadhimisho hayo Hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyopo jijini Mwanza imeandaa kliniki kwa wananchi kuonana na wataalamu na fanyiwa uchunguzi bure.

IRINGA DC WAPITISHA BAJETI YA BILIONI 60.24

 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa Stephen Mhapa akiongea wakati wa Baraza la madiwani la kupitisha rasimu ya bajeti ya mwaka 2023/2024

Na Fredy Mgunda, Iringa.


HALMASHAURI ya Wilaya ya Iringa imepitisha rasimu ya mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha wa 2023/2024 wa kiasi Cha shilingi bilion 60.24 ikiwa na ongezeko tofauti na bajeti ya mwaka 2022/2023.

Akizungumza kwenye Baraza la madiwani, mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Stephen Mhapa alisema kuwa wamepitisha rasmi ya bajeti ya shilingi bilioni 60,245,770,237 imepanda Kwa asilimia 2 kutoka asilimia 15 hadi asilimia 17 katika mwaka wa fedha wa 2023/2024. 

Mhapa alisema kuwa Halmashauri imepanga kukusanya na kutumia shilingi 6,592,471,590 Kwa mapato ya ndani ambazo zinajumuisha ukomo wa bajeti kuanzia ngazi ya Halmashauri hadi ngazi ya chini.

Mhapa ameishukuru Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa Dk Samia Suluhu Hassan, akisema imeendelea kupeleka fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika halmashauri hiyo.

Kwa upande wake afisa mipango wa Halmashauri Exavery Luyangaza alisema kuwa mapato ya ndani ya Halmashauri yameongezeka kutoka shilingi 4,269,100,000 mwaka 2022/2023 hadi shilingi 4,995,665,000 sawa na asilimia 17 ya kiasi kilichoongezeka na kusaidia utekelezaji wa majukumu ya Halmashauri.

Luyangaza alisema kuwa rasimu ya bajeti hiyo imekidhi matakwa ya mipango ya maendeleo ya Halmashauri hiyo na kusaidia kukuza uchumi kwa Wananchi.

Kwa upande wao baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa walipongeza bajeti hiyo kuwa itakidhi haja ya kutatua changamoto za Wananchi na kuwaletea maendeleo.


WACHIMBAJI MZINGATIE SHERIA YA USALAMA WA MAZINGIRA NA MATUMIZI SALAMA YA BARUTI-PROFESA KIKULA

Mwenyekiti wa Tume wa Madini Profesa Idris Kikula amewataka Wachimbaji na Wafanyabiashara wa madini nchini kuzingatia Sheria, Usalama, Utunzaji wa Mazingira na Matumizi Salama ya Baruti katika uendeshaji wa shughuli za uchimbaji madini migodini, ambapo kila mchimbaji  ana wajibu wa kusimamia mazingira kwa mujibu wa Sheria zilizowekwa.

Profesa Kikula ameyasema hayo leo Februari 23, 2023 kwenye ufunguzi wa mafunzo ya Usalama, Afya, Utunzaji wa Mazingira na Matumizi Salama ya Baruti kwa Wachimbaji wadogo wa madini, yaliyofanyika Mkoani  Mara ambayo yamekutanisha Wakurugenzi, Mameneja, na Watumishi kutoka Tume ya Madini, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara, Viongozi wa Wachimbaji wadogo na Wachenjuaji wa Madini, pamoja na Wafanyabiashara na Wamiliki wa Migodi wa Mkoa wa Mara.

Profesa Kikula amesema kuwa mafunzo hayo ya siku mbili, yanalenga kuhakikisha kuwa shughuli za uchimbaji, uchenjuaji na biashara ya madini zinafanyika kwa kuzingatia Usalama, Afya na Utunzaji wa Mazingira kwa kufuata Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali iliyowekwa.


Amesema kuwa mafunzo hayo yatazingatia pia utaratibu wa utoaji leseni za uchimbaji, uchenjuaji, biashara ya madini hususan kwenye usimamizi wa masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa madini nchini.


“Kupitia mafunzo haya naamini mna wajibu mkubwa wa kuimarisha mfumo wenu wa utendaji kazi kwa kuangalia usalama katika maeneo mnayochimba ili kuhakiksha kuwa taifa halipotezi nguvu kazi ili tuwe na uchimbaji endelevu wa kuimarisha maisha yetu na jamii inayotuzunguka,” amesema Profesa Kikula.

Thursday, February 23, 2023

MHUDUMU WA AFYA AKALIA KUTIKAVU IRINGA

 

Madiwani,Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa Stephen Mhapa akiongea wakati wa Baraza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa juu ya utovu wa nidham kwa watumishi wa serikali
Diwani wa viti maalum tarafa ya Idodi Wilayani Iringa Shani Msambusi  akitoa taarifa juu ya mhudumu huyo wa afya juu ya utendaji wake wa kazi
Diwani wa kata ya Kising'a Ritha Mlagala akichagia hoja wakati wa Baraza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa


Na Fredy Mgunda, Iringa.



BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Iringa Limeagiza kufanyika uchunguzi wa haraka dhidi ya Mhudumu wa afya katika Zahanati ya Kijiji ya Tungamalenga, anayedaiwa kutumia singano iliyotumika kumtibu mgonjwa

 

Akizungumza wakati wa baraza la Madiwani,Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa Stephen Mhapa alitoa agizo kwa Idara ya afya baada ya hoja ya malalamiko dhidi ya Mhudumu huyo wa afya anayedaiwa kukiuka misingi ya utumishi akijihusisha na vitendo vya utovu wa nidham ikiwemo ulevi wa kupindukia nyakati za kazi.

 

Mhapa alisema Halmashauri hiyo haitovumilia utovu wa nidham unaopelekea ukiukwaji mkubwa wa misingi ya kitaaluma na kuhatarisha afya za wagonjwa wanaopata huduma katika zahanati hiyo kwani kitendo cha kutumia sindano iliyotumika kumtibu mgonjwa mwingine kinaweza kusababisha kusambaa kwa maambukizi ya magonjwa mbalimbali ikiwemo maambukizi ya virusi vya ukimwi

 

"Tumeagiza uchunguzi ufanyike haraka iwezekanavyo kwenye zahanati zote na Mimi kama mwenyekiti napenda kutoa onyo kwa watumishi wote wa Halmashauri hii ninataka kupata taarifa kamili katika Baraza la madiwani lijalo ili tushughulike na hao watendaji"alisema Mhapa


Aliyasema hayo baada ya Diwani wa viti maalum tarafa ya Idodi Wilayani Iringa Shani Msambusi kuwasilisha malalamiko hayo katika baraza la madiwani na kumtaja mhudumu huyo wa afya aliyefahamika kwa jina la Johavina Mjuni kuwa ni kero kwa wananchi wanaopata huduma katika zahanati hiyo kutokana na utovu wa nidham uliokithiri na kushindwa kufanya kazi kwa weledi.

 

Diwani Msambusi alilielezabaraza la Madiwani kuwa Wananchi wanaiomba Serikali kuchukua hatua kwani hawako tayari kuendelea kuhudumiwa na Mhudumu huyo na kusisitiza Serikali kumuhamisha kwa kuwa hawana imani tena na huduma za kiafya anazozitoa.


Msambusi alisema kuwa mhudumu huyo wa afya amekuwa anatumia vilevi kupitiliza kipindi cha kazi hadi kushindwa kufanya kazi kwa weledi wake wa kuhudumia wananchi wagonjwa.

 

Kufuatia malalamiko hayo Kaimu mganga mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa,Luvanda Witson alisema wanaanzisha uchunguzi wa haraka dhidi ya madai hayo na pindi watakapojiridhisha hatua za kinidham zitachukuliwa  na kulijulisha baraza la madiwani kuhusu hatua hizo.

CRDB YAWAPA UBALOZI WACHEZAJI WA SIMBA NA YANGA KAMPENI YA BENKI NI SimBanking

 

Mkurugenzi Mtenndaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (katikati), Afisa Mtendaji Mkuu wa Timu ya Yanga, Andre Mtine (wapili kushoto) na Afisa  Mtendaji Mkuu wa Timu ya Simba, Imani Kajura (wapili kulia) kwa pamoja wakisaini mkataba wa makubaliano wa kuwatumia wachezaji Clatous Chama, Mohammed Hussein, Aziz Ki na Farid Mussa kutoka timu za Simba na Yanga kuwa mabalozi wa Benki ya CRDB katika kufikisha elimu ya fedha kwa jamii kupitia kampeni yake ya “Benki ni SimBanking”, hafla ya kusaini mikataba  hiyo imefanyika leo kwenye makao makuu ya Benki ya  CRDB, jijini Dar es salaam. Wapili kulia waliosimama ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Benki ya  CRDB, Joseline Kamuhanda pamoja na wanasheria Hosea Samba (Timu ya Simba) , Simon Patrick (Yanga) na Danford Kisinda wa Benki ya  CRDB.
Dar es Salaam, Februari 22, 2023 – Benki ya CRDB imesaini mkataba wa makubaliano na wachezaji Clatous Chama, Mohammed Hussein, Aziz Ki na Farid Mussa kutoka Simba na Yanga kuwa mabalozi wake wa kufikisha elimu ya fedha kwa jamii kupitia kampeni yake ya “Benki ni SimBanking.” Mikataba na wachezaji hao imesainiwa katika makao makuu ya Benki ya CRDB na kushuhudiwa na viongozi waandamizi kutoka Benki ya CRDB pamoja na vilabu vya Simba na Yanga.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Mussa Nsekela amesema Benki ya CRDB kwa muda mrefu imekuwa ikishiriki katika kusaidia jitihada mbalimbali za kimichezo kwa kutambua mbali ya kuwa michezo ni burudani, bali pia michezo ni biashara na uchumi pia. 
 
Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita Benki ya CRDB imeanzisha mbio za kimataifa za hisani za CRDB Bank Marathon, mashindano ya taifa ya mpira wa kikapu ya CRDB Bank Taifa Cup pamoja na mashindano ya resi za Ngalawa ya CRDB Bank Ngalawa Race.
“Pamoja na juhudi zetu za kuwekeza katika michezo mingine lakini Benki ya CRDB pia imewekeza katika mchezo wa mpira wa miguu kupitia ufadhili ambao tumekua tukitoa kwa klabu ya Namungo lakini pia mwaka jana tulishirikiana na vilabu hivi vya Simba na Yanga katika maandalizi ya Simba Day pamoja na Wiki ya Mwananchi kama maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu ya soka ya Tanzania bara” aliongeza Nsekela.

Benki ya CRDB imefikia hatua ya kusaini makubaliano na wachezaji hao wa Simba na Yanga ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuongeza wigo wa ufahamu wa elimu ya fedha kwa wachezaji wa soka na jamii kwa ujumla lakini pia ikiwa pia ni sehemu ya kutambua viwango vizuri ambavyo vimeonyeshwa na wachezaji hao katika kusaidia timu zao kupata matokeo mazuri lakini pia nidhamu ambayo wameonyesha katika mchezo jambo ambalo ni muhimu sana kwa mafanikio ya mchezaji.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Yanga, Andre Mtine ameishukuru Benki ya CRDB kwa kutoa ubalozi kwa wachezaji wao jambo ambalo litaleta hamasa kwa wachezaji wengine kuongeza juhudi jambo ambalo litaisadia klabu wakati huu inaposhiriki mashindao ya ndani nan je ya nchi. Mtine alisema Klabu ya Yanga inafarijika pia kuwa sehemu ya familia ya Benki ya CRDB kwa kusaidia kufikisha elimu ya fedha katika jamii, na kuwaletea wananchi maendeleo.

“Tunaishukuru Benki ya CRDB kwa kuwatambua wachezaji wetu na kuwapa heshima hii kubwa ya kuwa mabalozi wao. Kwa kuwa mabalozi wa taasisi kubwa kama Benki ya CRDB kunaleta imani na hamasa hata kwa taasisi nyingine kutaka kushirikiana na wachezaji wetu jambo ambalo litanuifaisha sio tu wachezaji bali vilabu na soka letu kwa ujumla wake” alsema Mtine.
Akizungumza kwa upande wa klabu ya Simba, Afisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Imani Kajula na yeye amepongeza hatua ya Benki ya CRDB kuwatambua wachezaji wao na hasa kwa kuangalia mchango wao katika timu na nidhamu jambo ambalo ni muhimu kwa mafanikio yao na timu kwa ujumla. Aidha, aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa sehemu ya mafanikio ya timu hiyo, na kuahidi kuendelea kushirikiana kupitia kampeni hiyo ya Benki ni SimBanking.

“Pamoja na kuwa mikataba hii inakwenda kuongeza kipato kwa wachezaji lakini kupata nafasi ya kupewa elimu ya fedha ambayo itawasaidia kwenye maisha yao wakati huu wanacheza soka la ushindani na wakati ambao watakua wamestaafu ni jambo kubwa na la kupongezwa kwani wachezaji wengi wameshindwa kunufaika na vipaji vyao kwa kukosa elimu ya fedha” aliongeza Kajula ambae amewahi kufanya kazi katika taasisi mbalimbali za fedha nchini.

Clouts Chama ambae ni mmoja kati ya wachezaji waliosaini mkataba wa ubalozi wa Benki ya CRDB amesema kuwa mkataba huo utakua chachu ya kumfanya aongeze juhudi zaidi kukuza kipaji chake lakini pia kufanya yale yanayotakiwa katika mkataba kwani bila hivo ni ngumu kuendelea kuwapa sababu makampuni mengine kuvutiwa kufanya kazi naye.



KAMPUNI YA TANZANIA, YAKAMILISHA UJENZI WA KIVUKO KIPYA CHA MV PALM CHA NCHI YA UGANDA.

 

Hii tunaiita Mv Palm made in Tanzania, ni ndani ya Ziwa Victoria mara baada ya kujengwa na kushushwa majini.
Hii tunaiita Mv Palm made in Tanzania, ni ndani ya Ziwa Victoria mara baada ya kujengwa na kushushwa majini.
Hii tunaiita Mv Palm made in Tanzania, ni ndani ya Ziwa Victoria mara baada ya kujengwa na kushushwa majini.

KAMPUNI YA SONGORO MARINE  LTD YA TANZANIA, YAKAMILISHA UJENZI WA KIVUKO KIPYA CHA MV PALM CHA NCHI YA UGANDA. MAJOR AMPONGEZA RAIS SAMIA.

Tuesday, February 21, 2023

ORYX GAS YAGAWA BURE MAJIKO NA MITUNGI KWA WANAWAKE WAJASIRIAMALI MKOANI TANGA, MBUNGE UMMY AWASHUKURU KWA KUWAWEZESHA WAKINA MAMA HAO

 

Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Duka la Kuuzia Gesi Kampuni ya Oryxs lililopo barabara ya 7 Jijini Tanga kulia Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Duka la Kuuzia Gesi Kampuni ya Oryxs lililopo barabara ya 7 Jijini Tanga kulia Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kulia akiwa amebeba mtungi wa Gesi ya Oryx 
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kushoto akifurahia jambo wa pili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akipokea Mitungi ya Gesi ya kampuni ya Oryx


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Na Oscar Assenga, Tanga

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imekabidhi mitungi ya gesi pamoja na majiko yake 600 kwa wanawake 600 kutoka vikundi mbalimbali vikiwemo vya wajasiriamali katika Mkoa wa Tanga ikiwa ni mkakati wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa yanayoharibu mazingira.

Huku Mbunge wa Jimbo la Tanga ambaye pia ni Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akiishukuru Kampuni ya Oryxs Gas Tanzania kwa kuridhia ombi lake la kukubali kuwasaidia wanawake wajasiriamali kutoka vikundi mbalimbali vilivyopo kwenye Kata zote za Jimbo lake 

Akizungumza wakati wa kukabidhi mitungi hiyo ya gesi mbele ya Waziri wa Afya ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu, Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite amesema kutokana na madhara ya gesi ya ukaa duniani, kampuni ya Oryx Tanzania (OGTL) iko mstari wa mbele kusaidia kuhamasisha matumizi ya gesi safi ya kupikia kwa kutoa mchango mwingine wa vifaa vya gesi mkoani Tanga ambako matumizi ya mkaa ni makubwa.

Amesema matumizi ya mkaa yana athari kubwa kwa mazingira na husababisha jangwa huku akifafanua Tanga ni miongoni mwa mikoa hapa nchini ambayo ina hali ya juu ya ukataji miti kwa ajili ya mkaa, hivyo wao wanaamini mpango huo wa kusaidia vifaa utasaidia wakazi wa Tanga, hasa wanawake ambao wanaathirika na moshi utakanao na kuni na mkaa.

"Kampuni inawekeza kwa kutekeleza miradi ya kutoa elimu juu ya gesi safi ya kupikia, inachangia vifaa vya gesi ya kupikia katika baadhi ya mikoa.Pia tunahamasisha matumizi ya gesi kwa kufanya mauzo makubwa ya mitungi kwa bei nafuu.

"Juhudi zote hizi zinalenga kufanya Watanzania wengi wanaanza kutumia gesi safi ya kupikia kama alivyoahidi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan.

Rais Samia ambaye ameweka malengo kuwa ifikapo mwaka 2030 asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia gesi safi ya kupikia.

"Kampuni ya Oryx Gas Tanzania pia imeitikia wito wa kidunia ya kupunguza hewa ukaa kutoka viwandani na shughuli za kibinadamu Kupitia promosheni ya LPGOGTL kampuni is furaha kuungana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika juhudi za kuboresha Maisha ya Watanzania kwa kupunguza hewa ukaa. Tunasikia faraja kusaidia utekelezaji wa ajenda ya LPG ambayo inainufaisha Tanzania,amesema Benoit.

Awali akizungumza Waziri wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu alimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Oryx Tanzania kuwa kuwasaidia kuwezesha majiko ya gesi kwa wanawake wajasiriamali kwenye Jiji hilo.

Alisema kwamba msaada huo umekuja wakati na hivyo kuwa mkombozi mkubwa kwa wana Tanga kutokana na kwamba lazima lifanane na watu na hali halisi hivyo mahitaji ya gesi ni muhimu na hayaweze kukwepeka kwa wananchi.

“Ndugu zangu wana Tanga Oryxs Gas ni Kampuni Bora na nzuri na labda niwaambie kwamba hawapunyi kwenye vipimo vyao lakini niwashukuru kwa kufungua duka hilo na wao kama Tanga Jiji wamepata mlipa kodi mpya “Alisema

Hata hivyo Waziri Ummy alimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Oryxs Gas Tanzania baada ya kumwambia kwamba Tanga kuna wasiriamali na wangependa kuwasadia majiko ya gesi kwa ajili ya kurahisisha shughuli zao kujipatia kipato na kuandaa chakula .

“Hivyo tunamshukuru Mungu kwa kutuwezesha jambo hilo,alisema kwamba yeye anataka kuwasaidia na kuwainua wananchi wa kipato cha chini na kuwaambia kwamba atamsaidia kufanikisha hilo lakini pia matumizi ya gesi yataweza kusaidia kuondokana na matumizi ya mkaa ambayo ni gharama kubwa “Alisema

Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa alisema kitendo kilichofanywa na Mbunge huyo kitaacha alama na wanaona wanakwenda kutibua sehemu ya changamoto kwenye jamii ya ukataji wa miti ambayo mwisho wa siku inapelekea kuharibu mazingira.

“Matumizi ya gesi nchini bado yanakwenda kwa kusuasua kwa hiyo kupitia hili kutakuwa na ushawishi mkubwa kwa kuhakikisha jamii inatumia nishati mbadala ya gesi ambayo itasaidia kutunza mazingira na kuondoa uharibifu wa mazingira” Alisema

Hata hivyo kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Tanga Al- Shaymaa Kweygir alisema kwamba wanashukuru Mbunge Ummy Mwalimu kwa kuwajali wakina mama kwa sababu wao wana mchango mkubwa kwa maendeleo .

Kweygir alisema kwamba kitendo cha kuwezeshwa majiko ya Gesi kwa wajasiriamali wanawake itawasaidia kuwakomboa kichumi kwa sababu wanapokuwa kwenye shughuli zao watakuwa wakitumia muda mchache kuandaa na kuwahuduma wateja wao.

Naye kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo alimshukuru Mbunge Ummy kwa kuendelea kuwajali wananchi na Baraza la Madiwani linamshukuru kwa kuhakikisha maendeleo kwenye Jimbo hilo yanaendelea kupaa.

Hata hivyo alisema kwamba Mbunge huyo ni wa kipekee kutokea tokea Jimbo hilo lilipoanzishwa ameacha alama na kuvunja rekodi ya wabunge wengine waliowahi kuliongoza Jimbo hilo .

SIMBA NA AZAM FC ATAKAYECHUKULIA POA MCHEZO HUU AMELIWA

 NA SUZUKI DRUMDRUM

KAZI kubwa inatarajiwa kufanyika jioni ya leo saa moja kamili, Uwanja wa Mkapa kwa Dabi ya Mzizima kati ya Simba v Azam FC unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa jijini Dar es salaam.

Unakuwa ni mchezo wa pili kwa wababe hawa kukutana baada ya ule uliopita wa mzunguko wa kwanza ubao kusoma Azam FC 1-0 Simba na kuwafanya Simba kuyeyusha pointi tatu muhimu. Msafiri Madanya wa Sports Ripoti ya Jembe Fm anafanya uchambuzi wa mchezo huo.

UGANDA: MUUGUZI AKAMATWA KWA KUWABAKA WAGONJWA WAJAWAZITO


Polisi nchini Uganda wamemkamata muuguzi kwa tuhuma za kubaka na jaribio la kuwabaka wagonjwa wawili wajawazito katika Hospitali ya Entebbe Grade B. 

Muuguzi huyo aliye mafunzo alikamatwa Jumamosi, Februari 18, jioni na kwa sasa anashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Entebbe Central. 

Naibu Msemaji wa Polisi wa Jiji la Kampala, Luke Owoyesigire alisema mshukiwa, Kutesa Denis, alikuwa akiwatambua waathiriwa wake kutoka wodi ya Wanawake. 

Kisha aliwawekea dawa ya kuwapoteza fahamu inayoshukiwa kuwa chloroform kabla ya kuwanyanyasa kingono. 

 "Dawa inayoshukiwa kuwa ya chloroform ilipatikana kutoka kwa makazi yake katika hospitali hiyo, na barua ikapatikana ambapo aliomba kuombewa dhidi ya mawazo machafu aliyokuwa nayo," Owoyesigyire alisema kwenye taarifa, akiwataka waathiriwa wengine kujitokeza, akisema kwamba inawezekana mtuhumiwa aliwanyanyasa wanawake wengine. 

Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Peterson Kyebambe alisema kuwa tukio hilo sasa limewachochea kuongeza tahadhari na na kuimarisha usalama kwa kufunga kamera zaidi za CCTV. 

Daktari bandia 

Kwingineko humu nchini, daktari bandia James Mugo Ndichu almaarufu Mugo Wairimu aliongezewa kifungo cha miaka 29 jela. Mugo ambaye tayari alikuwa akitumikia kifungo cha miaka 11 gerezani, alisukumwa jela bila faini baada ya kupatikana na hatia ya kuwadunga wagojwa wanawake dawa za kuwafanya wapoteze fahamu kabla ya kuwadhulumu kimapenzi. 

Akitoa hukumu hiyo Novemba 2022, Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Milimani, Wendy Kagendo Micheni alisema Mugo ni hatari kwa usalama wa wanawake na anastahili kutengwa na jamii ya waungwana wanaopenda amani na haki. 

Kwa shtaka kuwapotezea fahamu wagonjwa na kuwabaka, Micheni amemfunga Mugo miaka 22. 

ZANZIBAR YAIPONGEZA ZIPA.

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar kimesema kimeridhishwa na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM katika eneo la uwekezaji kupitia Mamlaka ya Vitega Uchumi Zanzibar(ZIPA).


Kauli hiyo ameitoa Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi (CCM )Zanzibar Khamis Mbeto Khamis mara baada ya kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji ZIPA,Shariff amesema Shariff ofisini kwake Maruhubi.


Amesema ZIPA imetekeleza kwa kiasi kikubwa azma ya Rais wa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Ali Mwinyi ya kuwavutia wawekezaji ambapo miradi mingi tayari  imekwishawekezwa kwa kipindi kifupi.


"Eneo la uwekezaji ndio uti wa mgongo wa uchumi wa Zanzibar hivyo niwapongeze ZIPA kwa kazi nzuri mnayoifanya na kasi kubwa mnayoitekeleza ya ilani ya chama chetu,"amesema


Katibu huyo ameitaka ZIPA kuendelea kufanya kazi kwa  karibu na CCM ili kufikia malengo ya ilani ya uchaguzi katika kuwaletea maendeleo wazanzibari.


Naye,Mkurugenzi wa ZIPA Sharif Ali Sharif, amesema, mwekezaji anapotaka kuwekeza anapewa masharti kwa kuhakikisha anazingatia mazingira ya uwekezaji yenyewe.

Amesema kwa sasa ZIPA imekuwa na uwekezaji wa miradi mikubwa 226 ambayo inaweza kuzalisha dola za kimarekani bilioni 3.5 ambapo inatengeneza ajira zaidi ya 13000.


"Katika kipindi cha miaka hii miwili ya serikali ya awamu ya nane ZIPA kupitia serikali tumetekeleza ilani kwa vitendo jambo ambalo imeonyesha dhamira kwa serikali kuhakikisha uchumi unaongezeka,"

amesema


Amesema katika kipindi cha miaka miwili wawekezaji wameongezeka kutokana na kupata ushirikiano mkubwa kutoka kwa Rais, Dkt. Mwinyi kutokana na kuwa ametengeneza mazingira mazuri kwa wawekezaji.


"Rais Dkt.Mwinyi ameiimarisha ZIPA kiutendaji kwani Mamlaka hii imekuwa na watendaji wenye uwezo mkubwa wa kitaalamu katika kuwavutia wawekezaji na pia wameweka sheria ambayo ni rafiki zaidi kwa wawekezaji," amesema


Amesema kupitia miradi hiyo zimepatikana ajira mbalimbali kwa wananchi wa Zanzibar na kwamba lengo la serikali ni kuhakikisha uchumi wa unaongezeka kwa asilimia kubwa.


Pia,amesema uwekezaji umeongezeka kutokana na serikali kuanzisha kituo cha pamoja ambacho kinatoa huduma zote kwa wakati mmoja ambapo wawekezaji wamekuwa wakirahisisha upatikanaji wa huduma hizo kwa wakati.


Akizungumzia upande wa visiwa, Mkurugenzi Sharif, amesema,kibali kinachotolewa kwa muwekezaji hupewa masharti ya asilimia 10 ya eneo husika na asilimia iliyobakia hupewa masharti ya kujenga ndani ya eneo la baharini ili kuona visiwa hivyo havihathiriki na uwekezaji huo.


Mkurugenzi huyo alisema katika uwekezaji huo,muwekezaji utanguliza fedha kabla ya kuwekeza ambapo kwa sasa serikali imeshaingiza dola za kimarekani milioni 14 ambapo katika miradi ya visiwa hivyo inatakiwa kuingiza dola za kimarekani milioni 19.


"Wawekezaji hawa wamekuwa wakilipa kwa awamu na fedha zilizoingia zipo na zitatumika kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kulipwa fidia watu waliokuwepo katika bahari ikiwemo wavuvi, na wawekezaji ambao hawakufikia vigezo tunavyovitaka," amesema


Akizungumzia suala la viwanda ndani ya visiwa vidogo amesema, katika uwekezaji huo kutotakiwa uwekezaji wa viwanda vikubwa na kwamba viwanda vinavyotakiwa ni vya kati na vyepesi ambavyo vitakuwa na thamani kubwa.


Mbali na hilo,amesema ZIPA itaendelea kutekeleza ilani ya CCM katika utendaji wao wa kazi wa kila siku na kufuata miongozo ya Rais Dkt.Mwinyi juu ya uwekezaji nchini.