ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, February 21, 2023

ORYX GAS YAGAWA BURE MAJIKO NA MITUNGI KWA WANAWAKE WAJASIRIAMALI MKOANI TANGA, MBUNGE UMMY AWASHUKURU KWA KUWAWEZESHA WAKINA MAMA HAO

 

Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Duka la Kuuzia Gesi Kampuni ya Oryxs lililopo barabara ya 7 Jijini Tanga kulia Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Duka la Kuuzia Gesi Kampuni ya Oryxs lililopo barabara ya 7 Jijini Tanga kulia Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kulia akiwa amebeba mtungi wa Gesi ya Oryx 
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kushoto akifurahia jambo wa pili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa akipokea Mitungi ya Gesi ya kampuni ya Oryx


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu katikati akiwa na o na Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite kushoto wakimkabidhi Mtungi wa Gesi mmoja wa wajasiriamali Jijini Tanga leo


Na Oscar Assenga, Tanga

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imekabidhi mitungi ya gesi pamoja na majiko yake 600 kwa wanawake 600 kutoka vikundi mbalimbali vikiwemo vya wajasiriamali katika Mkoa wa Tanga ikiwa ni mkakati wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa yanayoharibu mazingira.

Huku Mbunge wa Jimbo la Tanga ambaye pia ni Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akiishukuru Kampuni ya Oryxs Gas Tanzania kwa kuridhia ombi lake la kukubali kuwasaidia wanawake wajasiriamali kutoka vikundi mbalimbali vilivyopo kwenye Kata zote za Jimbo lake 

Akizungumza wakati wa kukabidhi mitungi hiyo ya gesi mbele ya Waziri wa Afya ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu, Mkurugenzi wa ORYX GAS Araman Benoite amesema kutokana na madhara ya gesi ya ukaa duniani, kampuni ya Oryx Tanzania (OGTL) iko mstari wa mbele kusaidia kuhamasisha matumizi ya gesi safi ya kupikia kwa kutoa mchango mwingine wa vifaa vya gesi mkoani Tanga ambako matumizi ya mkaa ni makubwa.

Amesema matumizi ya mkaa yana athari kubwa kwa mazingira na husababisha jangwa huku akifafanua Tanga ni miongoni mwa mikoa hapa nchini ambayo ina hali ya juu ya ukataji miti kwa ajili ya mkaa, hivyo wao wanaamini mpango huo wa kusaidia vifaa utasaidia wakazi wa Tanga, hasa wanawake ambao wanaathirika na moshi utakanao na kuni na mkaa.

"Kampuni inawekeza kwa kutekeleza miradi ya kutoa elimu juu ya gesi safi ya kupikia, inachangia vifaa vya gesi ya kupikia katika baadhi ya mikoa.Pia tunahamasisha matumizi ya gesi kwa kufanya mauzo makubwa ya mitungi kwa bei nafuu.

"Juhudi zote hizi zinalenga kufanya Watanzania wengi wanaanza kutumia gesi safi ya kupikia kama alivyoahidi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Samia Suluhu Hassan.

Rais Samia ambaye ameweka malengo kuwa ifikapo mwaka 2030 asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia gesi safi ya kupikia.

"Kampuni ya Oryx Gas Tanzania pia imeitikia wito wa kidunia ya kupunguza hewa ukaa kutoka viwandani na shughuli za kibinadamu Kupitia promosheni ya LPGOGTL kampuni is furaha kuungana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika juhudi za kuboresha Maisha ya Watanzania kwa kupunguza hewa ukaa. Tunasikia faraja kusaidia utekelezaji wa ajenda ya LPG ambayo inainufaisha Tanzania,amesema Benoit.

Awali akizungumza Waziri wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu alimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Oryx Tanzania kuwa kuwasaidia kuwezesha majiko ya gesi kwa wanawake wajasiriamali kwenye Jiji hilo.

Alisema kwamba msaada huo umekuja wakati na hivyo kuwa mkombozi mkubwa kwa wana Tanga kutokana na kwamba lazima lifanane na watu na hali halisi hivyo mahitaji ya gesi ni muhimu na hayaweze kukwepeka kwa wananchi.

“Ndugu zangu wana Tanga Oryxs Gas ni Kampuni Bora na nzuri na labda niwaambie kwamba hawapunyi kwenye vipimo vyao lakini niwashukuru kwa kufungua duka hilo na wao kama Tanga Jiji wamepata mlipa kodi mpya “Alisema

Hata hivyo Waziri Ummy alimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Oryxs Gas Tanzania baada ya kumwambia kwamba Tanga kuna wasiriamali na wangependa kuwasadia majiko ya gesi kwa ajili ya kurahisisha shughuli zao kujipatia kipato na kuandaa chakula .

“Hivyo tunamshukuru Mungu kwa kutuwezesha jambo hilo,alisema kwamba yeye anataka kuwasaidia na kuwainua wananchi wa kipato cha chini na kuwaambia kwamba atamsaidia kufanikisha hilo lakini pia matumizi ya gesi yataweza kusaidia kuondokana na matumizi ya mkaa ambayo ni gharama kubwa “Alisema

Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa alisema kitendo kilichofanywa na Mbunge huyo kitaacha alama na wanaona wanakwenda kutibua sehemu ya changamoto kwenye jamii ya ukataji wa miti ambayo mwisho wa siku inapelekea kuharibu mazingira.

“Matumizi ya gesi nchini bado yanakwenda kwa kusuasua kwa hiyo kupitia hili kutakuwa na ushawishi mkubwa kwa kuhakikisha jamii inatumia nishati mbadala ya gesi ambayo itasaidia kutunza mazingira na kuondoa uharibifu wa mazingira” Alisema

Hata hivyo kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Tanga Al- Shaymaa Kweygir alisema kwamba wanashukuru Mbunge Ummy Mwalimu kwa kuwajali wakina mama kwa sababu wao wana mchango mkubwa kwa maendeleo .

Kweygir alisema kwamba kitendo cha kuwezeshwa majiko ya Gesi kwa wajasiriamali wanawake itawasaidia kuwakomboa kichumi kwa sababu wanapokuwa kwenye shughuli zao watakuwa wakitumia muda mchache kuandaa na kuwahuduma wateja wao.

Naye kwa upande wake Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shiloo alimshukuru Mbunge Ummy kwa kuendelea kuwajali wananchi na Baraza la Madiwani linamshukuru kwa kuhakikisha maendeleo kwenye Jimbo hilo yanaendelea kupaa.

Hata hivyo alisema kwamba Mbunge huyo ni wa kipekee kutokea tokea Jimbo hilo lilipoanzishwa ameacha alama na kuvunja rekodi ya wabunge wengine waliowahi kuliongoza Jimbo hilo .

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.