ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Monday, October 27, 2025

SERIKALI MKOA WA PWANI YAJIIMARISHA KWA ULINZI NA USALAMA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

 VICTOR MASANGU, PWANI ... HABARI ..OCTOBA 27 /2025

SERIKALI Mkoa wa Pwani imesema kwamba imejiandaa  vya kutosha hususan katika hali ya ulinzi na usalama  katika kuelekea katika uchagzuo mkuu wa mwaka 2025 ambaop unatarajiwa kufanyika  octoba 29 mwaka huu ambayo itakuwa ni siku ya jumatano ya wiki hii.

Hayo yamebaishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge wakati akizunhgumza na waandishi wa habari  ofisini kwake kuhusiana na maandalizi ya kuelekea katika uchagzuzi huo ambapo amewaahimiza wanananchi wote wenye sifa  kujitokeza kwa wingi kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo.