
Kuuawa jana kwa mtu ambaye ameiongoza Iran kwa karibu miaka 40 kulithibitishwa usiku na televisheni ya taifa. Hili ni tukio kubwa sana kwa taifa hilo la Kiislamu.
Kulikuwa na sherehe katika baadhi ya mitaa ya miji ya Iran kutoka kwa watu waliopinga utawala wake. Hali hiyo itazitia moyo Israel na Marekani, ambazo zimewahimiza Wairani kutumia fursa hii kuamka na kuiondoa serikali.
Usiku kucha, jeshi la Israel lilifanya wimbi jingine la mashambulizi ya mabomu, likisema lililenga hifadhi na vituo vya kurushia makombora ya masafa marefu ya Iran pamoja na mifumo yake ya ulinzi wa anga.
Zaidi ya watu 200 wameuawa kote Iran, kulingana na Iranian Red Crescent Society, Shirika la misaada ya kibinadamu nchini Iran.
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran limesema litajibu kifo cha Kiongozi Mkuu kwa operesheni yenye uharibifu mkubwa zaidi katika historia yake.
Asubuhi hii nchini Israel, ving’ora vya tahadhari ya mashambulizi ya anga vimesikika tena huku Iran ikiendelea kurusha makombora ya masafa marefu. Karibu yote yamedunguliwa na mfumo wa ulinzi wa anga wa Israel.
Hata hivyo, baadhi yalipenya: mjiniTel Aviv, shambulizi la kombora lilimuua mwanamke mmoja, ambaye ni kifo cha kwanza cha raia wa Israel katika vita hivi. Huduma ya ambulensi imesema watu wengine 120 wamejeruhiwa, wengi wao wakiwa na majeraha madogo.


.jpeg)





.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)




























.jpeg)
.jpeg)