ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, June 4, 2023

RAIS WA YANGA AMPA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MEDALI YAKE

 NA ALBERT G. SENGO

Rais wa Yanga Eng. Hersi Said amesema kuwa atamkabidhi medali yake ya nafasi ya pili Kombe la Shirikisho barani Afrika, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, mara baada ya kutunukiwa jana usiku. #samiasuluhuhassan #yanga #yanganasimba

Saturday, June 3, 2023

NSSF YAMSHUKURU RAIS DKT SAMIA SULUHU KUPANUA WIGO KWA WANACHAMA WAO

 

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga Audrey Claudius akizungumza na waandishi wa habari wakati wa maonyesho ya 10 ya Biashara na Utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
Afisa Mwandamizi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Pangani Haji Sultan kushoto akimpatia kadi kwa mwanachama Grace Poul (kulia)  wakati wa maonyesho ya 10 ya biashara na utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
Afisa Mwandamizi wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Pangani Haji Sultan akitoa elimu kwa wananchi waliofika kwenye banda lao wakati wa maonyesho ya 10 ya biashara na utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga


Na Oscar Assenga,TANGA

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga amesema wanamshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu kwa kutoa sapoti ya kupanua wigo kwa wanachama wao.

Hayo yalisema na Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga Audrey Claudius wakati wa maonyesho ya 10 ya Biashara na Utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga.

Alisema baada ya Serikali kuona wananchi wengi wanafanya biashara lakini hawana mfuko rasmi wa kuweka mafao yao na kutunza fedha zao kwa ajili ya matumizi ya baadae hivyo waliona waanzisha mfumo mpya wa Niss.

Aidha alisema kupitia mfumo huo wanachama wanaweza kujitunzia akiba zao kila mwezi na hivyo kuwa na sifa ya kupata mafao yao baadae lakini ili waweze kuwa mwanachama wa National Informal Sector Scheme (NISS) lazima waandikishwe wapate namba ya uanachama.

Meneja huyo alisema kwamba wakishapata namba ya uanachama naa akishaanza kuchanga kila mwezi kuna mafao wanayotoa kama mafao ya mateniti kwa wakina mama na mafao ya uzee baada kila kazi kuna mwisho wa ajira.

Hata hivyo alisema kwamba wameendelea kuboresha huduma zao na hivyo kuwezesha waajiri kuweza kufanya malipo ya michango ya wafanyakazi wao wakiwa ofisini au majumbani.

Alisema kwa sababu wanaweza kulipa kupitia mifumo ya kieletroniki ikiwa na Portal kufanya malipo kwa wafanyakazi wako pia mwanachama anaweza kuangalia salio lake akiwa nyumbani kwa kutumia simu yake ya mkononi.

“Sio hivyo tu wale waliofungua madai anaweza kuangalia mchakato wa faili lake limefikia wapi”Alisema

Hata hivyo Meneja huyo alisema kwamba wameamua kushiriki kwenye maonyesho hayo ya ili kutoa elimu inayohusiana na hifadhi ya jamii na kutoa huduma kwa wanachama wao.

Alisema kwamba wanatoa elimu kwa wafanyakazi walioajiriwa na waliojiajiri wenyewe kutokana na kwamba mfuko huo wameanzisha huduma kwa wanachama ambao wanajiingizia kipato wao.

Friday, June 2, 2023

KASI YA MAPAMBANO DHIDI YA FISTULA HOSPITALI YA BUGANDO YAKABIDHIWA VIFAA TIBA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Hospitali ya Rufaa Kanda Bugando jijini Mwanza imepokea vifaa tiba vya upasuaji wa ugonjwa wa fistula ya uzazi kutoka shirika la Americares, vyenye thamani ya shilingi milioni 234.2 vitakavyosaidia utoaji huduma ya matibabu ya ugonjwa huo. Akizungumza Juni 01, 2023 kwenye hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi amesema vitasaidia kutoa huduma ya matibabu kwa akina mama wanaougua fistula ya uzazi na hivyo kuzuia vifo vitokanavyo na ugonjwa huo.

Thursday, June 1, 2023

BRELA WATUMIA MAONYESHO YA 10 YA BIASHARA NA UTALII KUTOA ELIMU JUU YA MIFUMO WANAYOISIMAMIA

 

 


Afisa Usajili wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELA) Julieth Kihwelu akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu huduma wanazotoa katika banda lao
Maafisa wa Wakala wa Usajili wa Biasharaa na Lesni nchini (Brela) wakitoa huduma kwa wananchi waliofika kwenye banda lao


Na Oscar Assenga, TANGA.

WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELA) wamesema kwamba wameshiriki kwenye maonyesho ya biashara na utalii ya 10 ili kuweza kutoa elimu juu ya matumizi ya mifumo wanayosimamia kwa sasa ambao ni ORS na Tanzania Nationali Business Portal.

Hayo yalibainishwa na Afisa Usajili wa Wakala huo Julieth Kihwelu wakati akizungumza na waandishi wa habari katika banda lao lililopo eneo la Mwahako Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho hayo ambapo wameamua kushiriki ili kusogeza karibu huduma kwa wakazi wa mkoa wa Tanga na mikoa ya kanda ya kaskazini.

Alisema kwamba mifumo hiyo ni mikuu pendwa ambayo mwombaji anatakiwa kutumia kuwasilisha ombi lake huku akieleza wanatoa huduma ya kuwafundisha namna ya kutumia mfumo huo kuweza kujisajili.

“Katika mifumo hii mwombaji anatakiwa awe na kitambulisho na Taifa,barua pepe aweze kujisaijili na nitoe wito kwa wajasiriamali nchini kuendelea kusajili alama za biashara zao kwa kuwa alama moja inamtumbisla mtu mmoja”Alisema

Afisa usajili huyo alisema kwamba wasiposajili alama zao wanaweza kutegeneza bidhaa ambayo kuna mtu mwengine anayo na amesajili kwa mujibu wa sheria kwa alama za biashara na huduma.

Hata hivyo aliwashauri wakazi wa Tanga na mikoa ya jirani waenda kupata huduma ya papo kwa papo ambapo kwa sasa wanaendelea kutoa huduma hiyo katika maeneo hayo.

“Tokea 28 mei mpaka Mei 31 tumekwisha kuwahudumia wananchi 35 na tukilinganisha mwaka jana na mwaka huu kuna utofauti na tunategemea kufikia watu wengi kwa kuwatembele kwenye mabanda hususani wajasiriamali kuweza kuwapa ushauri namna ya kuweza kusajili alama za biashara “Alisema Afisa huyo.

Hata hivyo aliwataka wajasiriamali na wafanyabiashara kufika kwenda banda lao kupata elimu na kufanyiwa usajili alama zao za bidhaa zao.

TASAC YATOA NENO KWA WASAFIRI WANAOTUMIA VYOMBO VYA MAJINI

 

 

Afisa Mfawidhi wa Shirika la TASAC Mkoani Tanga Kapten Christopher Shalua  (kushoto) akitoa maelezo kwa Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwekezaji,Viwanda na Biashara Conrad Millinga wa kwanza (kulia)ambaye alimwakilisha Waziri wa Wizara hiyo kuhusu namna ya kutumia vifaa vya kujiokolea wakati alipotembelea banda  la TASAC katika maonyesho ya 10 ya biashara na utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
Afisa Mfawidhi wa Shirika la TASAC Mkoani Tanga Kapten Christopher Shalua  (kushoto) akitoa maelezo kwa Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwekezaji,Viwanda na Biashara Conrad Millinga wa kwanza (kulia) ambaye alimwakilisha Waziri wa Viwanda wakati alipotembelea banda lao katika maonyesho ya 10 ya biashara na Utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
Afisa Mfawidhi wa Shirika la TASAC Mkoani Tanga Kapten Christopher Shalua  akizungumza na vyombo vya habari katika Banda lao kwenye  maoanyesho ya 10 ya biashara na utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
Afisa Masoko Mwandamizi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Martha Kelvin (kushoto) akimkabidhi zawadi Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwekezaji,Viwanda na Biashara Conrad Millinga (kulia) wakati alipotembelea Banda lao


Na Oscar Assenga,TANGA

SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limetoa wito kwa wasafiri wanaotumia vyombo vya Usafiri majini kuhakikisha wanatumia vyombo vilivyo ruhusiwa kisheria kubeba abiria na sio kupanda vyombo vya kusafirisha mizigo ikiwemo majahazi.

Wito huo ulitolewa leo na Afisa Mfawidhi wa Shirika hilo Mkoani Tanga Kapten Christopher Shalua wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya 10 ya biashara na utalii yanayoendelea katika viwanja vya Mwahako Jijini Tanga

Aidha, alisema kwa sababu viwango vya vyombo vipo kwenye madaraja tofauti ni vema kila chombo kikatumika kulingana na matumizi huzika yaliyothibitishwa na amewataka  wananchi wa Tanga kwa ujumla kutembelea Banda lao ili kupata elimu zaidi.

Alisema TASAC imeshiriki maonesho hayo kwa ajili ya kuwafikia wananchi hususani wanaoishi maeneo ya fukwe na kuwaelimisha kuhusu Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa Mazingira Majini pamoja na majukumu yanayotekelezwa na Shirika hilo kwa Mujibu wa Sheria. 

Hata hivyo alisema kwamba jukumu lao pia ni kuhakikisha wanasimamia Bandari kuhakikisha wanatoa huduma katika viwango vinavyokubalika kimataifa ili kuweza kuchochea ukuaji wa uchumi nchini .

Wednesday, May 31, 2023

KLABU YA KWANZA YA MKONGE YAZINDULIWA

 

 


Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) kwa kushirikiana na Shule ya Sekondari ya Coastal ya jijini Tanga, zimezindua Klabu ya Mkonge kwa wanafunzi wa shule hiyo ambayo imelenga kuwafundisha vijana kuhusu kilimo cha Mkonge na Sekta ya Mkonge kwa ujumla hatua itakayowawezesha kujiajiri baada ya kumaliza masomo.


Akizindua klabu hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TSB, Saddy Kambona amesema wazo la kuanzisha klabu hiyo lilizaliwa kwenye Mahafali ya kidato ya shule hiyo Machi mwaka huu, lakini baadaye ikaonekana isiwe klabu kwa ajili ya Shule ya Coastal pekee bali ianzishwe klabu itakayoshirikisha shule zote za Tanga na vizazi vinavyokuja kushiriki kwenye uchumi huu wa mkonge.

Amesema kwa muda mrefu imezoelekea kwamba elimu yetu haimuandai mwanafunzi kwenda kujitegemea anapomaliza shule, wengi wamekuwa na mtazamo kuwa kazi ya kuajiririwa ndiyo inafaa.

“Kwa hiyo sisi tulitazama wazo la kuwa na klabu za Mkonge kwa maana kama tunasema Mkonge ni Tanga na Tanga ni Mkonge, basi tunataka mtu akifika Tanga aone kweli kama Mkonge ni Tanga, tunategemea aone kwamba Mkonge ndiyo zao kuu la kibiashara.

“Yaani kuanzia anatua uwanja wa ndege anapotua anaona bidhaa za Mkonge barabarani hadi anapofika hotelini anakutana na mazuria ya Mkonge na bidhaa nyingine. Sasa sehemu ya kuanzia ni kuwa na klabu za kuhamasisha si tu kilimo cha Mkonge bali  pia kuhamasisha matumizi ya bidhaa za Mkonge lakini pia kushiriki kwenye kuzalisha hizo bidhaa.

“Baada ya hayo sasa Bodi inakuwezesha kupata elimu, utaalamu kuanzia shambani kulima Mkonge na uongezaji wa thamani, wataalamu wetu watatoa ujuzi huo kwa vijana wa Tanga na nje ya Tanga ili wanapomaliza shule huko wanakokwenda wakawafundishe na wengine,” amesema.

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Zao la Mkonge na Masoko, Olivo Mtung’e akizungumzia faida za Mkonge na somo la kuhamasisha wanachama wa klabu hiyo alisema mahitaji ya Mkonge kwa sasa yameongezeka ndiyo maana wanahamasisha wakulima kulima zao hilo.

“Nchi nyingi sasa zinahitaji Mkonge lakini kiasi ambacho tunakilima kwa sasa ni kidogo ndiyo maana baada ya kuingia kwenye kilimo cha wakulima wadogo sasa tunahamasisha na sisi kwenye familia zetu wenye mashamba ya eka moja hadi tatu walime Mkonge kwa sababu kwa sasa hali ya hewa inatusukuma kuelekea huko kwani zao la Mkonge linahimili hali za hew azote ili kuimarisha uchumi wa familia,” amesema.

Mkurugenzi Mtung’e anasema kutokana na hali hiyo, wahitimu hawana haja ya kutafuta ajira kwa sababu Mkonge wenyewe ni ajira kwani ukishapanda baada ya miaka mitatu unaanza kuvuna hadi kwa muda wa miaka 18.

Kwa upande wake mwanafunzi wa shule hiyo na mmoja wa wanachama wa klabu hiyo, Fatuma Mshashi amesema klabu hiyo yenye wanachama 50 ambao kati yao wavulana ni 23 na wasichana 27, inatekeleza malengo mbalimbali ikiwamo kufanya tafiti kuhusu kilimo cha zao la Mkonge ili kuona faida zake, kutoa elimu kwa wanafunzi, walimu, wadau wa elimu kuhusu umuhimu wa zao hilo, kuhamasisha jamii kutumia bidhaa za mkonge, kuwaandaa wanafunzi ili kuja kuwa wataalamu wazuri na wabobevu katika zao la Mkonge na nyingine nyingi.

“Ili kufanikisha malengo katika Klabu ya Mkonge katika shule yetu, tunaomba ofisi yako kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwalimu Mkuu itusaidie kukutanishwa na wataalamu wa zao la Mkonge ili kupata elimu na ujuzi wa zao hili, kuwezeshwa klabu kuwa na shamba darasa ambalo litakuwa la kujifunzia hatua zote za uandaaji hadi uvunaji ambapo shamba hilo mlitakuwa mradi wa klabu,” amesema.

Saturday, May 27, 2023

VICTORIA MARATHON 2023 ITAKAYOFANYIKA MWEZI JULY JIJINI MWANZA SAFARI HII 'NI FULL UTALII'

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Mashindano ya riadha ya Transec Lake Victoria marathon kwa msimu wa tatu yanatarajia kufanyika Julai 2 mkoani Mwanza kwa kushirikisha wanariadha zaidi ya 1400 kutoka mikoa ya kanda ya ziwa na maeneo mbalimbali. Hayo yamesemwa na Mratibu wa mbio hizo Halima Chake wakati wa uzinduzi uliofanyika katika uwanja wa Mwanza Yatch Club pembezoni mwa Ziwa Victoria jijini Mwanza. Chake amesema kutakuwa na mashindano ya Kilomita 2.5 kwa watoto chini ya umri wa miaka 10,kilomita 5,kilomita 10 na kilomita 2.1, huku akizitaja gharama za ushiriki kwa kiliomita ni Shilingi 20,000, Kilomita 5 ni shilingi 30,000, Kilomita 10 ni shilingi 35,000 na Kilomita 21.1 ni Shilingi 35,000. Amesema usajili umeshafunguliwa rasmi, nakutoa wito kwa wakimbiaji wote kujisajili kwa wingi tufanikishe lengo lililokusudiwa. Aidha mratibu huyo amewashukuru wadau mbali mbali kwa udhamini wao katika mbizo zao ambapo baadhi ya wadau ni Transec, benki ya KCB,TBL na Konyagi. Mnamo mwaka jana (2022) mashindano hayo yalirejesha kwa jamii kupitia kituo cha watoto wenye uhitaji kwa kuwapatia bima ya afya watoto 85. Naye Katibu Tawala msaidizi wa mkoa wa Mwanza upande wa uwekezaji na Biashara Patrick Karangwa pamoja na kuushukuru uongozi wa Lake Victoria marathon kwa kuandaa mbio hizo pia ameziomba kampuni na mashirika mbalimbali kujitokeza kwa wingi katika kuunga mkono mbio hizo. Ameyataja mashindano kama chachu ya kuutangaza mkoa wa Mwanza kama sehemu ya kuhifadhi Ziwa Victoria na kuchochea biashara kwani kwenye msimu wa mbio hizi biashara zinafanyika na tukio hilo limekuwa likichochea na kukuza utalii Karangwa ameahidi kutoa ushirikiano ili kuhakikisha mbio hizo zinafanyika kwa mafanikio makubwa kama zilivyo mbio za Kilimanjaro na kwingineko. "Matukio kama haya yanawezesha kukuza uchumi, kuainsha na kuzitangaza fursa za mkoa wetu sanjari na kuwakutanisha watu kujenga uhusiano wa kibiashara huku fedha zinazochangwa zikirudi katika kuisaidia jamii. Naye ofisa Mwakilishi wa kampuni ya Transec Victor Okeyo amesema kampuni yake itaendelea kuchangia kwa kile kinachoweza kufanikisha lengo la kuisaidia jamii. "Mbio ni sehemu mojawapo ya vitu vinavyotusaidia kuwa na afya bora, nawaomba wanamichezo washiriki kwa wingi katika mbio hizi" "Kanda ya Ziwa imekuwa sehemu kubwa ya mafanikio yetu, na tunaona ni uamuzi sahihi kurudisha faida kwao" ilisema sehemu ya hotuba ya Victor Okeyo. #mwanza #samiasuluhuhassan #LakeVictoriaMarathon

SHUHUDIA MWANZO MWISHO - MKUU WA MKOA WA MWANZA AKIAGIZA BAR NA KUMBI ZA STAREHE KUFUNGULIWA MWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

KIKAO cha wafanyabiashara wa bara na kumbi za starehe jijini Mwanza kimetamatika kwa maelekezo ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Amos Makalla kuagiza #kaziiendelee kwa baa na kumbi za starehe zilizofungiwa na Baraza la Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) zifunguliwe huku akipiga marufuku kamata kamata ya nguvu na kuvizia inayofanywa na baraza hilo kwa kushirikiana na jeshi la polisi.

Licha ya kuwa anakabidhiwa ofisi Mei 28 mwaka huu, Makalla ambaye aliteuliwa Mei 15 kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza akitokea Dar es Salaam ametoa maagizo hayo jana Mei 26, 2023 baada ya kukutana na kusikiliza kero za wamiliki, mameneja na wafanyakazi wa baa, hoteli, kumbi za starehe na burudani jijini Mwanza. Shuhudia kikao hicho mwanzo mwisho kupitia #JembeFmTz #mwanza #samiasuluhuhassan #kaziiendelee

Thursday, May 25, 2023

RAIS SAMIA AZINDUA MRADI WA KUFUA UMEME NCHINI UGANDA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivuta kamba pamoja na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Umeme wa Kikagati – Murongo, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023. Mradi huo wa umeme utanufaisha nchi zote mbili katika masuala ya Nishati ya umeme.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakati alipotembelea mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo (Megawatt 16), Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.

 


Eneo la mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo pamoja na Mitambo kama linavyoonekana pichani, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakati alipotembelea mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo (Megawatt 16), Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.

Eneo la mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo pamoja na Mitambo kama linavyoonekana pichani, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.

Eneo la mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo pamoja na Mitambo kama linavyoonekana pichani, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.

Eneo la mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo pamoja na Mitambo kama linavyoonekana pichani, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.

.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakati wakisikiliza maelezo ya mradi wa kufua umeme wa Kikagati – Murongo, Mbarara nchini Uganda tarehe 25 Mei, 2023.



KiIBAHA MJI YAJA NA MPANGO KABAMBE WA KUKUSANYA BILIONI 45.8 MAPATO YA NDANI


Na Victor Masangu,Kibaha

Halmashauri ya mji Kibaha kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 imekadiria kukusanya zaidi ya shilingi bilionj 45.8 kutokana na ruzuku, mapato yake ya ndani pamoja na mashirika mbali mbali ya maendeleo.

Hayo yamebainishwa na Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya mji Kibaha Selina Wilson wakati wa kikao cha Baraza la madiwani kwa kipindi Cha robo ya tatu kuanzia mwezi januari hadi machi mwaka 2023.

Makamu huyo alibainisha kwamba kwa upande wa makusanyo kuanzia mwezi julai mwaka 2022 hadi machi 2023 wamefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 29.9 ikiwa sawa na kiwango cha asilimia 65.5.

Aliongeza kuwa halmashauri hiyo kwa kipindi cha kuanzia mwezi julai 2022 hadi kufikia Machi 2023 kiasi cha shilingi mqilioni 587.8 ikiwa sawa na asilimia zipatazo 116 ya makisio ya mwaka.

Akizungumzia kuhusiana na utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2022/2023 imepanga kutumia kiasi cha shilingi bilioni 113 kwa ajili kutumika katika miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya mipango miji na mazingira Hamis Shomari alisema kuwa kwa sasa zoezi la utambuzi wa wananchi waliovamia katika eneo la mtaa wa mkombozi limefanyika na kwamba wananchi 4509 tayari wameshatabuliwa.

"Uuzaji wa viwanja katika mtaa wa mkombozi umeshaanza ramsi tangu tarehe 24 mwaka huu ambapo wananchi walishajulishwa,ambapo jumla ya ankra ya viwanja 168 katika mtaa wa mkombozi zimeshatolewa,"alibainisha Shomari.
Akizungumzia kuhusiana na wananchi ambao wamevamia katika mtaa wa Lumumba tayari kazi ya utambuzi imeshafanyika ambapo wananchi wapatao 6952 wameshatambulika na kazi ya michoro 8 yenye viwanja 7,264 imekamilika.

                  
Kwa upande wake Mwnyekiti wa Halmashauri ya mji Kibaha Mussa Ndomba amewahimiza madiwani kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili iweze kuleta tija kwa maslahi ya wananchi.


Wednesday, May 24, 2023

KAMISHNA WA POLISI JAMII CP SHILOGILE AMEZINDUA JENGO LA DAWATI LA JINSIA NA WATOTO HALMASHAURI YA MSALALA KATA YA BUGARAMA.

Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Nchini, Kamishna Msaidizi wa Polisi DCP, Merry Nzuki akiwasalimia Wananchi (Hawapo Pichani) kabla ya uzinduzi wa Jengo la Dawati na Jinsia na Watoto mkoani Shinyanga, Halmashauri ya Msalala Kata ya Bugarama. (PICHA NA JESHI LA POLISI)


Kamishna wa Jeshi la Polisi Kamisheni ya Polisi Jamii CP Faustine  Shilogile, Mkuu wa Wilaya ya Msalala Mboni Mhita mwenye Suti nyeusi, Naibu Mkurugenzi Mkazi Nchini Tanzania Heo Eun na Melissa Barrett Naibu mwakilishi mkazi  toka UNFPA Tanzania wakiwa katika Picha ya pamoja katika zoezi la kukata utepe katika uzinduzi wa Jengo la Dawati Kata ya Bugarama.(PICHA NA JESHI LA POLISI)

Kamishna wa Jeshi la Polisi Kamisheni ya Polisi Jamii CP Faustine  Shilogile kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Msalala Mboni Mhita, mwenye suti nyeusi upande wa pili ni Naibu Mkurugenzi Mkazi Nchini Tanzania Heo Eun na Melissa Barrett Naibu mwakilishi Mkazi  toka UNFPA Tanzania wakiwa katika Picha ya pamoja katika zoezi la kuvuta kitambaa kuashilia Ufunguzi wa Jengo la Dawati Kata ya Bugarama Halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga.(PICHA NA JESHI LA POLISI)

Pwani kumekucha yapasua mawimbi miradi yote 99 ya maendeleo yapitishwa na mwenge wa uhuru

 Na Victor Masangu,


Jumla ya  miradi  99 ya maendeleo ambayo imetembelewa na mingine kuzinduliwa na kuwekewa mawe ya Asmsingi katika Mkoa wa Pwani imefanikiwa kupitishwa yote bila ya dosari yoyote na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge wakati a awwkimkabidhi rasmi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Robert Chalamila katika eneo la tazara na kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa chama pamoja  na serikali.

Kunenge alibainisha kwamba mbio za Mwenge wa uhuru ukiwa katika mkoa wa Pwani umeweza kukimbizwa umbari wa kilometa zipatazo 1201 katika Wilaya saba na halmashauri zipatazo tisa.


Alifafanua kuwa katika miradi hiyo mbali mbali  ya maendeleo ambayo imeweza imegusa katika sekta mbali imegharimu jumla ya kiasi cha shilingi  tilioni 4.4 ambazo zimetoka serikalini na nyingine kwa wadau wa maendeleo.

Kunenge alibainisha kuwa katika mbio hizo miradi tisa iliweza kufunguliwa na mingine 15 kuzinduliwa huku miradi mingine 20 iliweza kupata fursa ya kuwekewa mawe ya msingi huku miradi 15 imekaguliwa.

"Tunashukuru tumemaliza salama kukimbiza mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wetu wa Pwani na kwamba miradi yetu yote imeweza kupitishwa bila ya kuwa na dosari yoyote Ile kutokana na kuwa na vigezo ambavyo vinatakiwa,"alisema Kunenge.

Kwa Upande wake kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa Abdalah Kaim alisema kwamba ameridhishwa na utekelezaji wa miradi mbali mbali ambayo wameweza kuitembelea.

Alimpongeza kwa dhati mkuu wa .Mkoa wa Pwani kwa kuweza  kusimamia watendaji wake katika suala zima la  kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo itaweza kuwasaidia wananchi.

Nao baahi ya viongozi walioudhulia katika makabidhiano hayo hawakusita kutoa pongezi kwa uongozi mzima wa Mkoa wa Pwani kwa kujitahidi kuibua miradi hiyo ambayo imefanikiwa kupitishwa yote bila kukataliwa.



Walisema kitendo cha miradi yote 99 kupitiwa na mbio za Mwenge na kufanikiwa kupitishwa bila dosari yoyote ni mafaniko makubwa kwani inaonyesha namna ya watendaji wanavyojitahidi kushirikiana bega kwa bega kwa maslahi ya wananchi kwa ujumla.


Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Pwani zimeweza kupita katika miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo kuweka mawe ya msingi.kufunguliwa,kuzinduliwa na mingine kutembelewa katika sekta tofauti.