ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, July 23, 2024

VIJANA WAKUMBUSHWA KUJIKITA KATIKA MIDAHALO KUONGEZA UELEWA WA MAISHA.

 


NA VICTOR MASANGU

Vijana wametakiwa kushiriki  katika midahalo mbalimbali itakayowawezesha kuwa na mawazo chanya juu ya mustakabali wa maisha yao.

Hayo yamesemwa na Mwanzilishi wa jukwaa la Power of Sentence ambalo ni jukwaa la uwezeshaji kwa vijana kupitia simulizi za maneno ambapo, jukwaa hilo linatoa nafasi kwa vijana kupata nafasi ya kutambua athari za maneno zinavyoweza kuathiri maamuzi yako na zingine zinazoweza kuwajenga kifikra.

Mwanzilishi wa jukwaa la Power Of Sentence, Jackline Christopher amesema jukwaa hili limewakutanisha vijana mbalimbali na kufanya midahalo juu ya maneno yanavyoweza kuathiri maamuzi yao.

Jackline amesema, huu ni mwaka wa tano toka kuanzishwa kwa jukwaa hilo na limewawezesha vijana wengi kufikia malengo yao baada ya kuweka wazi hisia na fikra zilizopo ndani ya mawazo baada ya kuyawasilisha mbele ya jamii.

“Hii powe of sentence ni namna ambayo mtu anaweza kutumia maneno yake kuweza kumletea mafanikio na muda mwingine yanaweza yakaathiri maisha yake kwa namna moja ama nyingine,” amesema Jackline.

“Unaweza kuwa na mawazo yakawa ni mazuri au mabaya kulingana na utakavyochukulia, zaidi unapokuwa na mawazo usiyaache kuyatumia na kuyaishi kwa sababu maneno hayo yanayopita ndani ya kichwa chako yanaweza kukujenga zaidi na kufikia malengo yako,” amesema


Akizungumzia msimu wa tano wa jukwaa hilo linalotarajia kufanyika Julai 27, mwaka huu Jackline amewaomba vijana wajitokeze kwa wingi kwa kununua tiketi kwani dhamira ya jukwaa hilo ni kuona linafika mbali zaidi katika mikoa mingine ikiwemo Kigoma.

Jackline ni mwandishi wa vitabu mbalimbali ambapo tayari ameshazindua kitabu chake cha 100 Power of Sentence na Amnesia ambavyo vyote kwa sasa vinapatikana.

RC KUNENGE AKABIDHI MAGARI MAPYA YA SERIKALI KWA DC KISARAWE NA BAGAMOYO

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI 


Mkuu wa mkoa wa Pwani Alhaji  Abubakari Kunenge amekabidhi Magari mawili mapya  kwa wakuu wa Wilaya za Kisarawe na Bagamoyo ambayo yataweza  kuwasaidia kwa kiasi kikubwa katika utekelezaji wa kuwahudumia wananchi wao kwa urahisi zaidi.

Akikabidhi Magari hayo kwa wakuu hao wa Wilaya Mkuu huyo wa mkoa wa Pwani amemshukuru kwa dhati  Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa Magari hayo yatakayokuwa ni mkombozi mkubwa katika suala zima la usafiiri kwa wakuu hao wa Wilaya.


Kunenge alisema kupatikana kwa magari hayo mapya kutaweza ni juhudi kubwa ambazo amezifanya Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha anaboresha mazingira ya kazi kwa wakuu wake wa Wilaya.

Alisema katika Mkoa wa Pwani kuna jumla ya Wilaya sana na kwamba Rais kwa awamu hii ameshatoa magari mapya  matatu ambayo mawili yamekabidhiwa leo rasmi na mengine yatakabidhiwa katika awamu nyingine.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti amempongeza kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa  kuwapatia magari hayo ambayo yatakwenda kuwa msaada mkubwa.

Magoti alisema kwamba hapo awali alikuwa anatekeleza majukumu yake kwa kutumia gari nyingine lakini kwa sasa anashukuru kupata gari jipya ambalo litamuwezesha kuwafikia wananchi kwa urahisi zaidi.

"Kwa kweli napenda kumshukuru kwa dhati Mkuu wa Mkoa wa Pwani pamoja na Rais wangu Dkt.Samis Suluhu Hassan kwa kuweza kutupatia magari haya ambayo kwa kweli mm nilikuwa naenda vijijini kwa usafiri wa gari aina ya Pick up,:alisema Magoti.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo  Halima Okash   hakusita kumpongeza Mkuu wa Mkos wa Pwani kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na  Rais Samia  kuwapatia magari mapya kwa ajili ya kurahisisha usafiri na utekelezaji wa majukumu yao ya kuwatumikia wananchi.

Monday, July 22, 2024

NHC YATUMIA ZAIDI YA MILIONI 300 KUBORESHA MAJENGO YAO TANGA

 


Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mkoani Tanga Mhandisi Mussa Kamendu

Na Oscar Assenga, TANGA

SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita 2023/2024 wametumia zaidi ya Milioni 300 kwa ajili ya matengenezo makubwa ya majengo yao katika Jiji la Tanga.

Hayo yalibainishwa leo na Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mkoani Tanga Mhandisi Mussa Kamendu wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema kwamba matengenezo hayo yatahusisha nyumba za Ngamiani, Nguvumali, Bombo mpaka Raskazone.

Mhandisi Kamendu alisema kwamba shirika hilo limefanya mkakati huo maalumu makusudi kuhakikisha majengo yao yanaboreshwa na kuwa na muonekano mzuri ikiwemo kupakwa rangi ili wapangaji wao waishi kwenye mazingira mazuri.

“Katika miji yote ya Tanzania Shirika hilo linamiliki nyumba katikati ya Miji na Majiji kwa hiyo nyumba zinapokuwa kwenye hali mbaya zinafanya miji ionekane vibaya na taswira ya majiji inakuwa haipo vizuri kwa kuliona hilo shirika limekuja na mkakati maalumu wa kuzipaka rangi ili ziweze kuwa na muonekano mzuri na kubadilisha mifumo ya maji taka na maji safi “Alisema

Aidha allisema pia katika matengenezo hayo wamebadilisha pia mifumo ya umeme ambayo imechakaa na kurekebisha miundombinu mbalimbali mingine ikiwemo milango na madirisha ili kuhakikisha wanapangaji wanakuwa kwenye mazingira mazuri.

Katika hatua nyengine Meneja huyo aliwataka wapangaji wao kuhakikisha wanabadilika na kufuata mikataba yao inavyowataka walipe kodi kwa wakati ili waweze kuepukana na usumbufu wanataokumbana nao.

Mhandisi Kamendu alisema kwamba mikataba yao inawataka wapangaji wao kuhakikisha wanalipa kodi kwa wakati na pia waweze kuepukana usumbufu watakaoupata maana pale ambao hawajalipa kodi kufuatia na mikataba yao itafikia wakati watatolewa kwenye nyumba hizo.

“Wapangaji wasumbufu ambao wanasubiri mpaka kufuatwa na madadali kwenye kwenye nyumba sasa wanapotelewa kwenye nyumba ni usumbufu na aibu kwa familia na jamii inaweza kuona ni mtu wa ajabu tusisburi mpaka kufukia hatua hii”Alisema

Katika hatua nyengine Meneja huyo alisema kwamba shirika hilo limejiwekea malengo la kukusanya Sh. Bilioni 2,444,183,556.96 katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 kutokana na makusanyo yao ya Pango la Kodi kutoka katika nyumba zao.

Alisema kwamba hayo ndio malengo yao na mwaka huu wa fedha kwa sababu hiyo kama mkoa wanaendelela kuboresha huduma zao.

Alisema kwamba wanafanya hivyo kama shirika ili kuhakikisha wapangaji wanakuwa kwenye mazingira mazuri na kuwa sawa ili kodi zao wanazolipa ziendane na thamani ya mahali wanapoishi.

Maneja huyo alisema kwamba malengo yao ya Bajeti katika Mwaka wa Fedha wa 2023/2024 waliweza kukusanya kiasi cha Bilioni 2,040,727,435 kutokana na kodi ya pango kutoka kwa wapangaji wao walioishi kwenye nyumba za shirika hilo.

Alisema katika mwaka wa fedha kuanzia Julai 2023 mpaka June 2024 waliweza kukusanya kiasi cha Bilioni 2,040,727,435 na malengo waliokuwa wamejiwekea kwenye bajeti yao ya mwaka 2023/2024 ilikuwa ni kukusanya kodi Bilioni 2,046 ,528,000 .

“Kwa hiyo utaona ukiangalia kiasi tulichokusanya wao Biloni 2,040,727,435 tumekusanya kwa asilimia 99.7 ya malengo ya bajeti yetu ya mwaka 2023/2024 kwa hiyo katika majengo yetu na idadi ya wapangaji wao na kodi tunavyokusanya kwa ufupi tumefikia malengo ya kwa sababu asilimia 99.7 ni sawa asilimia 100 kiasi cha 5,856,400 ndio ambacho hakijaweza kukusanywa”Alisema

Aidha alisema na hivyo inatokana na madeni ya wapangaji wao ambao wanadaiwa na ni wajibu wao kuendelea kuyadai na kuchukua nafasi hiyo kuwapongeza wapangaji ambao wanalipa vizuri huku wakiendelea kuwasisitizia kuendelea kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi.

Sunday, July 21, 2024

UWT KIBAHA MJINI YATEMA CHECHE KWA KATA YA MBWAWA NA MSANGANI JUU YA KUWALINDA WATOTO.


 NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha Elina Mgonja amewahimiza wazazi na walezi kuhakikisha wanaungana kwa pamoja katika kukabiliana na wimbi la vitendo vya utekaji wa watoto.

Mgonja ameyasema hayo wakati akizungumza na wanawake wa UWT katika kata za Mbwawa na Msangani wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuangalia uhai wa chama pamoja na kuhimiza wanawake kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi.

Mwenyekiti huyo alisema kwamba kumekuwepo na matukio mbali mbali ya baadhi ya watoto kufanyiwa vitendo vya kutekwa na wengine kufanyiwa vitendo vya kulawitiwa.


"Wanawake,wazazi pamoja na walezi mnapaswa kuhakikisha kwamba mnawalinda na kuwatunza watoto wao kwani kuna wimbi kubwa la utekaji kwa watoto kwa hivyo inabidi tuwe makini sana,"alisema Mgonja.

Aidha aliwahimiza wanawake kuhakikisha kwamba wanaungana kwa pamoja katika kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu kwa ajili ya kugombea katika uchaguzi wa serikali za mitaa ambao unatarajiwa kufanyika mwaka huu.

Kadhalika aliwakumbusha wanawake kuweka utaratibu wa kuwachunguza kwa kina watoto wao ili kuweza kubaini kama wamefanyiwa vitendo mbali mbali vya ukatili ikiwemo kulawitiwa.


 Kwa upande wake mjumbe wa kamati ya utekelezaji ya UWT Kibaha mjini Dkt.Zainabu Gama amewataka wanawake kutokuwa waoga kabisa na kuchukua maamuzi ya kuwa Jasiri.

Naye Diwani wa viti maalumu wa Halmashauri ya mji Kibaha Lidia Mgaya amewaomba wanawake kuwa na umoja na upendo na kuwa mstari wa mbele hasa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.

Ziara ya Mwenyekiti wa umoja wa wanawake (UWT)  Wilaya ya Kibaha mjini imelenga kupita katika kata zote za 14 kwa lengo la kuwahimiza wanawake kujitokeza kwa wingi katika kugombea nafasi za uongozi.

Friday, July 19, 2024

HAWA HAPA WAKALI WA ACAPELLA THE VOICE NDANI YA JEMBE FM

 NA ALBERT GSENGO/MWANZA

Kuelekea Kongamano la Kwanza la Kikanda kuhusu maandalizi ya Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2050, waimbaji wa kundi la muziki The Voice wamatembelea Jembe Fm na kufanya mahojiano kisha kushare nasi utamu wa sauti zao. Kongamano hilo litaongozwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt Dotto Biteko huku likitarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Kwa Tunza Jumamosi hii, July 20, 2024 kuanzia saa 3:00 asubuhi.

MWENYEKITI UWT KIBAHA MJI AWAKUMBUKA WANAWAKE WAJANE KATIKA FURSA ZA MIKOPO

NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 

Mwenyekiti wa umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini amesema atahakikisha analivalia njuga suala la wanawake wajane kujiunga katika  vikundi vya ujasiriamali ili kupata fursa za mikopo.

Mgonja ameyabainisha hayo wakati akizungumza na  baadhi ya wanawake wa UWT kutoka kata za Visiga pamoja  na Misugusugu akiwa katika mwendelezo wa ziara yake ya kikazi yenye kuwapa ujasiri wanawake kugombea katika nafasi za uongozi.

Mwenyekiti huyo alisema kwamba katika ziara hiyo anatambua uwepo wa baadhi ya wanawake ambao ni wajane hivyo amewahimiza kujiunga katika makundi ya ujasiriamali ambayo itakuwa ni rahisi zaidi katika kupata mikopo.

"Nipo katika ziara ya kikazi katika kutembelea wanawake wa UWT kutoka kata zote 14 za Jimbo la kibaha mjini na leo nimetembelea kata ya Visiga na Misugusugu ikiwa ni kata ya kumi tangu nianze ziara yangu ,"alisema Mgonja.

Aliongeza kuwa ana imani wanawake wajane wakisapotiwa katika kupewa mitaji na mikopo wanaweza kufanya mambo makubwa na kuweza kujikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini.

Aliongeza kuwa kwa sasa lengo la UWT ni kuwa na siasa na uchumi hivyo atahakikisha anapambana kwa hali na mali ili kuwasaidia wajane kupata fursa za mikopo  ya asilimia 10 ambayo inatolewa na serikali.

Katika hatua nyingine alisema atahakikisha kwamba anawalinda na kuwatunza kwa hali na mali  wanawake wajane ambao wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya unyanyasaji na kwamba atashirikiana na vyombo vya dola katika jambo hilo.
Kwa upande wake Katibu wa UWT kata ya Visiga alimpongeza Mwenyekiti wa  Wilaya kwa ziara yake ya kutembelea wanawake kwa ajili ya kuwahimiza kujitokeza kuchukua fomu kwa ajili ya uchaguzi.

Nao baadhi ya waheshimiwa madiwani wa halmashauri ya Kibaha mjini hawakusita kuwapa ujasiri kwa wanawake hao kutoogopa kugombea katika nafasi za uongozi hasa katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Baadhi ya wanawake wajane wamesema kwamba wapo tayari kuwezeshwa mitaji pamoja na mikopo na kwamba wakiwezeshwa wanaweza kuondokana na kuwa tegemezi.



Ziara ya mwenyekiti wa umoja wa wanawake (UWT)     hadi sasa imefanyika katika kata kumi ambapo leo imefanyika katika kata ya Visiga na Viziwaviza.

Thursday, July 18, 2024

KONGAMANO LA KWANZA LA MAANDALIZI YA DIRA YA MAENDELEO YA MWAKA 2050 KUZINDULIWA MWANZA.

 NA ALBERT GSENGO/MWANZA

Kongamano la Kwanza la Kikanda kuhusumaandalizi ya Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka 2050 litazinduliwa 20, mwaka huu jijini Mwanza huku wananchi wakitakiwa kujitokeza kutoa maoni yao.

Akizungumza na wanahabari jijini Mwanza kuhusu Kongamano hilo Mkurugenzi wa Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Thobias Makoba, amesema KOngamano hilo ni sehemu ya kuongeza uelewa kwa umma kuhusu Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050

Naye Mwenyekiti wa Timu Kuu ya Kitaalamu ya Dira ya Taifa 2050 Dkt. Asha Rose Migiro amesema wameweka tahadhari kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi na mazingira kwamba ni masuala ambayo yapo yanayoepukika na yasiyoepukika nao wamejipanga kuhakikisha malengo yatakayowekwa yanatimia kwa asilimia kubwa bila kuathiriwa. ..

Aidha Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Thobias Makoba ameongeza kuwa Kongamano hilo litaongozwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt Dotto Biteko huku likitarajiwa kufanyika katika Ukumbi wa Kwa Tunza Jumamosi hii, July 20, 2024 kuanzia saa 3:00 asubuhi.

UWT KIBAHA MJI YAWAPIGA MSASA WA UCHAGUZI WANAWAKE WA KATA YA KIBAHA NA VIZIWAZIWA

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

 
Umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini imewataka wanawake kuachana na tabia ya kufanya kampeni za chini chini kabla ya muda haujafika wa kampeni  na badala yake wametakiwa kuwapa ushirikiano wa kutosha viongozi ambao wapo madarakani hadi kipindi cha muda wao utakapomalizika bila ubaguzi wowote.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini Selina Mgonja wakati akizungumza na baadhi ya wakinamama wa UWT kata za Kibaha pamoja na viziwaziwa ikiwa ni ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuzungumza na wanachama  sambamba na kuwahimiza wanawake wenye sifa na vigezo kushiriki na kujitokeza katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mgonja alisema kwamba kwa sasa ni vema  viongozi  mbali mbali ambao walichaguliwa na wananchi na wapo madarakani kwa mujibu wa sheria  wanatakiwa kuheshimiwa na kupewa ushirikiano wa kutosha  katika suala zima la utekelezaji wa Ilani ya chama  na sio kuanza kuwabeza na kuwaandaa  watu  mwingine kinyemela  kabla ya muda wake kumalizika kwani amechaguliwa kihalali.

"Katika ziara yangu lengo kubwa ni kutembelea katika kata mbali mbali ambazo zipo katika Jimbo la Kibaha mjini na kuwahimiza wanawake wenzangu kuweza kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi lakini kitu kikubwa wanatakiwa kuwaheshimu viongozi wa chama ambao bado wapo madarakani na kuachana na tabia ya kutengeneza safu ya uongozi kabla ya wakati,"alisema Mgonja.

Aidha Mwenyekiti Mgonja amebainisha kuwa lengo lingine la kufanya ziara hiyo ni kuwajengea uwezo wanawake  ili  wapate fursa ya kujiamini na kugombea katika uchaguzi wa serikali za mitaa bila ya kuwa na uwoga wowote na kwamba wana imani ziara hiyo itaweza kuleta mabadiliko chanya  kwa wanawake kujitokeza kwa wingi.

Katika hatua nyingine aliwataka wanawake wa UWT kuendelea kumpa ushirikiano wa kutosha Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani ameweza kutenga fedha nyingi ambazo zimetumika katika miradi mbali mbali ya kimaendeleo hivyo wanawake wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kumsemea yale mazuri ambayo ameyafanya katika kipindi cha miaka mita.

 
Kwa upande wake Katibu wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini  Cesilia Ndalu alisema kwamba katika kuelekea uchagzui wa serikali za mitaa wanawake wanapaswa kuwa na uthubutu na ujasiri kwa lengo la kuweza kujitosa kuchukua fomu na kushiriki katika uchaguzi huo ambao unatarajiwa kufanyika mwaka huu.

Nao baadhi ya wanawake wa UWT wamempongeza Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja kwa ziara yake hiyo ya kikazi ambayo imeweza kuwapa hamasa zaidi katika kushiriki kugombea katika  uchaguzi wa serikali za mitaa.

 Naye Diwani wa viti maalumu Halmashauri ya mji Kibaha Selina Wilson amewakumbusha wanawake hao kutumia ujuzi na maarifa waliyonayo katika kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kugombea nafasi za uwenyekiti katika uchaguzi wa serikali za mtaa mbao unatarajiwa kufanyika mwaka huu.

Ziara ya Mwenyekiti wa umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Kibaha mjini imelenga kupita katika kata zote 14 za Jimbo la Kibaha mjini ambapo kwa  leo ziara imefanyika katika kata mbili  za Kibaha pamoja na kata ya Viziwaziwa ambayo ni ya nane kufikiwa siku ya leo kwa lengo la kuwahimiza wanawake kujitokeza kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Wednesday, July 17, 2024

WILLIAM RUTO KUBUNI OFISI YA JENERALI MKUU WA KUCHUNGUZA VIFO.


Nairobi - Wizara ya Mambo ya Ndani na Utawala wa Kitaifa imefichua mipango ya kubuniwa kwa Ofisi ya Mkuu wa Uchunguzi wa Vifo. 

Katika taarifa siku ya Jumanne, Julai 16, wizara hiyo ilieleza kuwa ofisi hiyo itabuniwa chini ya Sheria ya Kitaifa ya Huduma ya Wachunguzi wa Vifo 2017. 

Wizara hiyo ilifichua kuwa ilimshauri Rais William Ruto kuunda afisi ambayo itachunguza mauaji yanayohusishwa na ukatili wa polisi. 

Kulingana na wizara hiyo, afisi hiyo itahakikisha uwajibikaji na uwazi katika visa vya vifo vinavyoshukiwa. 

 “Wizara imependekeza kwa Mheshimiwa Rais aanzishe mchakato wa uanzishaji wa Ofisi ya Mchunguzi Mkuu wa Vifo kwa mujibu wa Sheria ya Huduma ya Wachunguzi wa Kitaifa ya mwaka 2017 ili kuchunguza vifo vikiwemo vilivyotokana na polisi, Ofisi ya Mchunguzi Mkuu pia itahakikisha uwajibikaji na uwazi katika visa vya vifo vinavyoshukiwa," ilisoma taarifa hiyo kwa sehemu.

Ni onyo gani ilitolewa kwa polisi? Wizara hiyo pia iliwataka polisi kujizuia wanapokabiliana na waandamanaji kote nchini, ikisisitiza kujitolea kwake kuheshimu utakatifu wa maisha ya binadamu. 

Hata hivyo, polisi wamepewa mwanga wa kijani wa kutumia nguvu zinazofaa wakati vitendo vya uhalifu vinaposhinda maandamano ya amani. 

 “Polisi wanaweza kulazimika kutumia nguvu ya kuridhisha pale wanapojitenga na matukio mahususi ya maandamano yanapofikia vitendo vya uhalifu, vikiwemo fujo, uporaji, uchomaji wa mali, uvunjifu wa magari,” ilisema wizara hiyo. 

Maafisa wa polisi pia wamepewa notisi kwamba kukamatwa kunategemea Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, ambayo inaeleza jinsi ukamataji hutekelezwa na kuwekwa kizuizini na kufikishwa mahakamani kwa washukiwa. 

Serikali ilitoa wito kwa wafanyabiashara na wamiliki wa majengo binafsi wanaolinda mali zao kuwasiliana na mamlaka ili kusimamia usalama kwa utaratibu 

WASHUKIWA WAWILI ZAIDI WAKAMATWA HUKU MSHUKIWA MKUU AKIZUILIWA KWA SIKU 30

Collins Khalusha alizuiliwa kwa siku 30 kutokana na mauaji ya Kware. 

Nairobi - Maafisa wa upelelezi kutoka Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) wamewatia mbaroni washukiwa wawili zaidi wanaohusishwa na mauaji ya kinyama katika eneo la Kware, mtaa wa mabanda wa Mukuru kwa Njenga jijini Nairobi. 

Kwa nini Amos Momanyi Mogusu alikamatwa? Mnamo Jumapili, Julai 14, miili kadhaa iliyokatwakatwa ilipatikana katika eneo la kutupa taka na umma. Katika taarifa, DCI ilifichua kukamatwa kwa Amos Momanyi Mogusu, ambaye alinaswa katika eneo la City Cabanas. 

Kulingana na maafisa hao wa upelelezi, Momanyi alipatikana akiwa na simu ya mmoja wa waathiriwa, Roselyn Akoth Ogongo, ambaye mabaki yake yalitambuliwa na jamaa zake katika Makafani ya Nairobi. 

Ni vitu gani vya waathiriwa wa mauaji ya Kware vilipatikana? Baada ya kuhojiwa, Momanyi aliongoza maafisa wa upelelezi kwa mshukiwa wa tatu aliyejulikana kwa jina la Moses Ogembo ambaye anasemekana alimuuzia simu hiyo ya rununu. 

Katika nyumba ya Ogembo, wapelelezi walipata simu 154 za mitumba, na alikiri kuwa alinunua simu zilizotumika kutoka kwa mshukiwa mkuu, Collins Khalusha. "Baada ya kukamatwa kwa Amos Momanyl Mogusu katika mtaa wa Cabanas na kupatikana kwa simu ya rununu jana, aliongoza wapelelezi hadi kwa nyumba ya Ogembo iliyoko Mukuru kwa Reuben, ambaye alipatikana na jumla ya simu 154 zilizotumika zimefichwa nyumbani kwake," DCI ilisema. 

Wakati huo huo, makachero hao walipewa siku 30 kuendelea kumzuilia Khalusha ili kukamilisha uchunguzi wa madai ya mauaji hayo. 

Je, Collins Khalusha alilazimishwa kukiri makosa ya mauaji ya Kware? Huku hayo yakijiri, Khalusha, mshukiwa wa mauaji ya takriban wanawake 42 na kuwatupa kwenye machimbo eneo la Kware, aliwashutumu polisi kwa ukatili. 

Kupitia kwa wakili wake, John Maina Ndegwa, Khalusha alidai aliteswa hadi kukiri mauaji hayo. Akiwa amefikishwa mbele ya Hakimu Mkuu Irene Gichobi katika Mahakama ya Makadara, Ndegwa aliomba mahakama imruhusu kutafuta matibabu, akiongeza kuwa madai dhidi yake ni ya kuchekesha. 

UWT KIBAHA MJI YAZIDI KUCHANJA MBUGA KUHAMASISHA WANAWAKE KUSHIRIKI UCHAGUZI


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake (UWT) Wilaya ya ya Kibaha mjini Elina Mgonja amewataka wanawake kuachana na tabia ya kukaa vijiweni na badala yake wanapaswa kubadilika na kujiunga na vikundi vya ujasiriamali ili kuweza kujikwamua kiuchumi.

Elina ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na wanawake wa UWT Kata ya picha ya ndege wakati wa mwendelezo wa  ziara yake ya kikazi ya kuweza kujionea uhai wa chama pamoja na kuwahimiza kujitokeza kuchukua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi za uongozi.

Mwenyekiti huyo alibainisha kwamba wanawake wanatakiwa kujituma kwa bidii katika kufanya kazi mbali mbali ambazo zitaweza kuwasaidia kuondokana na wimbi la umasikini na kuondokana na kuwa tegemezi.


"Wanawake mnapaswa kuwa wajasiri katika kushiriki katika kazi mbali mbali ikiwa ni pamoja na kujiunga katika vikundi mbali mbali vya ujasiriamali ili kuweza kujikwamua kiuchumi na kuondokana na kuwa tegemezi,"alisema Mgonga.

Pia aliwataka wanawake kuhakikisha wanatengeneza mahusiano mazuri na viongozi mbali mbali wa chama cha mapinduzi na viongozi wa serikali katika shughuli mbali mbali za utekelezaji wa maendeleo.

Aidha aliwahimiza wanawake kuwa mstari wa mbele katika kumuunga mkono Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku.

Kadhalika Elina alisema kwamba wanawaje wa UWT wanatakiwa kuwa na umoja na mshikamano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa lengo ikiwa ni kushinda katika mitaa yote.

Kwa upande wake Katibu wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini  Cesilia Ndalu amesema wanawake wanatakiwa kuwa na ushirikiano na upendo kwa lengo la kuweza kukijenga na kukiimarisha chama cha mapinduzi.

Ziara ya Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini ina lengo la kutembelea wanawawake wa UWT katika kata mbali mbali ili kuona uhai wa chama sambamba na kuhimiza wanawake kujitokeza kuchukua fomu za kuwania uongozi.

Tuesday, July 16, 2024

UWT KIBAHA MJI YAWAHIMIZA WANAWAKE KATA YA TUMBI NA SOFU KUJITOSA NAFASI ZA UONGOZI

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

Jumuiya  ya umoja wa wanawake  (UWT) Wilaya  ya Kibaha mjini imewahimiza wakinamama  kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi  kuchukua fomu bila ya uwoga wowote  kwa ajili ya kugombea nafasi mbali mbali za uongozi  hasusan katika kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa  ambao unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa UWT Elina Mgonja wakati wa ziara yake ya kikazi  katika Kata ya tumbi na Sofu yenye lengo la kuweza kuangalia uhai wa chama pamoja na kuwahimiza wanawake kushiriki  kikamilifu katika nafasi mbalimbali za uongozi.




Mwenyekiti huyo aliongeza kwamba lengo lake kubwa la  kufanya ziara hiyo ni kuwatembelea wanawake katika kata zote 14 za Jimbo la Kibaha mjini ikiwa sambamba na kuangalia mwenendo mzima wa zoezi la uandikishaji wa wanachama kujisajili  kwa mfumo wa kisasa  kwa njia  ya  kieletroniki.

"Kwa kweli nimefarijika sana nimeamua kufanya ziara yangu ya kikazi ya kutembelea  kata mbali mbali ambazo zipo katika Jimbo la Kibaha mjini na lengo lake kubwa ni kuweza kuangalia uhai wa chama jinsi ulivyo ikiwa sambamba na kuona namna ya zoezi zima la wanachama kujiandikisha kwa njia ya Kieletroniki,"alisema Mgonja.

Kadhalika aliwaomba wanawake wa Kata ya Tumbi  pamoja na kata ya Sofu kuendelea kumpa ushirikiano wa kutosha Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwa sambaamba na kumuheshimisha katika uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kupiga kura kwa wingi ili kushinda kwa kishindo kikubwa na kuchukua mitaa yote bila kupoteza.

Kwa uapnde wake  Diwani wa viti maalumu Selina Wilson amewahimiza wakinamama kutorudi nyuma katika kugombea katika nafasi mbali mbali ikiwa sambamba na kuchukua fomu  kwa ajili ya kuwania nafasi mbali mbali za uongoz ikiwa sambamba na kuchangamkia fursa za mikopo zilizopo ambazo zitawasaidia katika kujikwamua kiuchumi.

Naye Diwani wa viti maalumu Shufaa Bashili amewataka wakina mama pindi wanapopata mikopo kuhakikisha kwamba wanaifanyia kazi pamoja na kuirejesha ikiwa sambamba na kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Diwani wa viti maalumu wa Kibaha mjini Lidya Mgaya alisema kwamba wanawake wanapaswa wasiogope na kwamba wataendelea kumuunga mkono Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika masuala mbali mbali ya kimaendeleo.

 Mwenyekiti wa UWT Wilaya yaKibaha mjini amefanya ziara yake ya kikazi  katika kata mbili za Tumbi pamoja na kata ya Sofu ambapo ameambatana na baadhi ya madiwani wa viti maalumu pamoja na  wajumbe wa  kamati ya utekelezaji sambamba na viongozi wa chama cha mapinduzi CCM. 




Monday, July 15, 2024

MAONI UCHAGUZI MKUU RWANDA

 NA FLORENCIA PETER/ KIGALI/RWANDA

Baada ya Uchaguzi kufanyika Nchini Rwanda je Wananchi niyapi Matarajio yao ? Kama anavyoeleza Bi Nshimimana Tatu Mkaazi wa Wilaya ya Nyamilambo Mkoa wa Nyarugenge Mjini Kigali Nchini Rwanda alipokutana na Mic ya Jembe Fm #rwandaupdate #rwandatoday #uchaguzimkuu_rwanda

UWT KIBAHA MJI YAFANYA KWELI YATEMBELEA MATAWI 14 KUHIMIZA ZOEZI LA KUJISAJILI

 


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Wilaya ya Kibaha mjini (UWT) Elina Mgonja  katika kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa amefanya ziara ya kikazi na kufanikiwa  kuyatembelea jumla ya  matawi 14  kwa lengo la kuweza  kujionea hali halisi ya uandikishaji kwa njia ya kieletroniki.

Ziara hiyo ambayo imefanyika katika kata mbili za Tangini na Maili moja pia ilikuwa na lengo la kuwahimiza wanawake kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi katika kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Akizungumza katika ziara hiyo ya kikazi Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja amesema kwamba ameamua kufanya ziara hiyo akiwa na wajumbe wa kamati ya utekelezaji ili kujionea mwenendo mzima wa zoezi la uandikishaji wa wanachama wa CCM  kwa njia ya kieletroniki.


Pia Mgonja alibainisha kwamba wamebaini kuwepo kwa mwamko mkubwa kwa wanawake kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo la kujisajili kwa njia ya kisasa kwa ajili ya kuweza kujiandaa na uchaguzi wa serikali za mitaa ambao unatarajjwa kufanyika mwaka huu.

"Mimi kama Mwenyekiti nimeambatana na wajumbe wa kamati ya UWT na tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutembelea matawi 14 ambayo yapo katika kata ya Tangini pamoja na kata ya maili moja na tumekuta idadi kubwa ya wanawake wamejisajili kwa mfumo wa kieletroniki,"alisema Mgonja.


Mgonja amesema kwamba lengo ni kuhakikisha wanakuwa na wanachama wengi wa CCM ambao wamesajiliwa kwa njia ya kisasa pamoja na kujiandikisha katika daktari la wapiga kura lengo ikiwa ni kufanya vizuri na kushinda kwa kishindo katika uchaguzi wa serikali za mitaa. 


Kadhalika Mgonja amewahimiza makundi mbali mbali ya wakinamama,vijana,wazee pamoja na wanachama wote kujiandikisha katika daftari la kupiga kura pamoja na kuboresha taarifa zao ili waweze kupata fursa ya kushiriki katika uchaguzi huo.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo amempongeza kwa dhati Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suhuhu Hassan kwa kuweza kutoa fedha kwa ajiili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo  ikiwemo katika  sekta ya afya.maji,elimu,pamoja na miundombinu ya barabara. 


Mgonja amemshukuru kwa dhati Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka pamoja na mke wake Mama Selina Koka  kwa kuweza kushirikiana kwa hali na mali katika kuwasaidia wanawake katika suala zima la kuleta maendeleo chanya katika nyanja mbali mbali.

Kwa upande wake Katibu wa UWT Kibaha mjini Cecilia Ndaru amewahimiza wanachama kuweka misingi mizuri ya kupendana na kuwa na umoja hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguguzi wa serikali za mitaa.

 Katika ziara hiyo ya UWT Mwenyekiti huyo ameambatana na viongozi mbali mbali wa chama cha mapinduzi  wakiwemo baadhi ya madiwani wa kuchaguliwa pamoja na wale madiwani wengine wa viti maalumu sambamba na viongozi wengine wa UWT.

Friday, July 12, 2024

MSIGWA ASIFU 'Zogo Mchongo’ YA BENKI YA CRDB KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA UMMA.

 

Dar es Salaam. Tarehe 11 Julai 2024: Akizindua msimu wa pili wa kipindi maalum cha televisheni cha elimu ya fedha kwa umma cha zogo mchongo kinachoandaliwa na Benki ya CRDB, Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa  na Michezo, Gerson Msigwa amesifu jitihada hizo zinazolenga kuwakomboa wananchi kiuchumi hali itakayowasaidia kuondokana na umasikini.

Msigwa amesema elimu ya fedha itakayotolewa katika kipindi hiki cha Zogo Mchongo kupitia televisheni ya Clouds, itawafungua Watanzania wengi juu ya fursa zilizopo kwenye taasisi za fedha zikiongozwa na Benki ya CRDB. Maarifa watakayoyapata pia yatawasaidia kujikomboa kiuchumi na kuliwezesha taifa kuyafikia malengo ya kuwa na uchumi jumuishi,” amesema Msigwa.
Katibu mkuu huyo amesema kipindi hicho cha elimu ya fedha pia kinakwenda kusaidia kupambana na maadui wawili kati ya watatu waliotajwa na Mwalimu Nyerere ambao ni ujinga na umasikini na hilo likifanyika rahisi jamii kukabiliana na magonjwa. “Ukishapambana na ujinga na umasikini ni rahisi kutafuta maarifa mengine yakiwamo ya kukabiliana na maradhi,” amesema Msigwa.

“Nawapongeza Benki ya CRDB kwa jitihada zenu za kuwaelimisha Watanzania. Kila mmoja akishiriki katika hili itakuwa rahisi kufanikisha malengo ya serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha maisha ya Watanzania,” amesema Msigwa.
Aidha, Msigwa amesema kuwa fedha nyingi nchini zinazunguka kwenye sekta isiyo rasmi kwasababu wananchi wengi hawafahamu faida za matumizi ya huduma za benki. Kutokana na hivyo, Wajasiriamali wengi wamekuwa wakijinyima fursa za kunufaika na mikopo pamoja na huduma nyingine za benki.

“Ni imani yangu kipindi hiki cha Zongo Mchongo kitawafungua macho na kuwawezesha kuchangamkia fursa zitakazosaidia kukuza biashara zao na uchumi wa taifa letu,” ameongezea Msigwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema kipindi hicho cha Zogo Mchongo ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Elimu ya Fedha (2021/22 – 2025/26) unaolenga kuongeza ufahamu na matumizi ya huduma za fedha kwa wananchi.
Mbali na hayo, Nsekela alibainisha kuwa Zogo Mchongo imekuwa jukwaa muhimu la kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa na akaunti za benki, kuwekeza, na kutumia huduma za kifedha kwa usalama na ufanisi. Hii ni hatua muhimu katika kufikia malengo ya kujumuisha kifedha na kuimarisha uchumi wa taifa kwa ujumla.

“Tukiwa Benki kiongozi ya kizalendo tunawajibu wa kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya fedha kwani kwa kufanya hivyo sio tu tunasaidia kuchochea ujumuishi wa kifedha bali pia wa kiuchumi kwani elimu hii itasaidia watu kuchangamkia fursa za kiuchumi kutokana na maarifa waliyonayo ya huduma za fedha ambazo zinatolewa na Benki yao ya CRDB,” amesema Nsekela.
Nsekela aliongeza kuwa kupitia programu mbalimbali za elimu na uwezeshaji kwa jamii, Benki ya CRDB inaendelea kujitolea katika kuleta mabadiliko chanya katika jamii kwa kuhakikisha huduma za kifedha zinawafikia watu wengi zaidi, hususan wale wa vijijini na maeneo yasiyo na huduma za benki.

Joseline Kamuhanda, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Benki ya CRDB, amesema kuwa msimu wa kwanza wa Zogo Mchongo ulikuwa na mafanikio makubwa, na kutokana na mafanikio hayo, wamefanya maboresho makubwa ili kurahisisha uelewa kwa watazamaji wa kipindi hiki kinachorushwa na Clouds TV.
"Msimu huu mpya tumeongeza mada nyingi ambazo zinaelimisha na kuburudisha. Tunataka watazamaji wetu wapate maarifa ya kina kuhusu masuala ya kifedha na waweze kujenga uelewa mzuri zaidi wa jinsi ya kudhibiti na kuwekeza fedha zao. Maboresho haya ni sehemu ya dhamira yetu ya kuendelea kuwahudumia wateja wetu na jamii kwa ujumla." amesema Joseline.

Kipindi cha Zogo Mchongo kinalenga kuongeza ufahamu wa masuala muhimu kama vile bajeti, utunzaji akiba, na namna ya kufanya uwekezaji. Mada zilizoongezwa ni katika msimu huu wa Zogo Mchongo ni pamoja na programu ya IMBEJU ambayo imekuwa kimbilio la vijana na wanawake wajasiriamali kote nchini,  bidhaa kama Hodari kwa wajasiriamali, Huduma zinazofuta misingi ya sharia ‘Al Barakah’,  huduma za Watanzania waishio nje ya nchi ‘Diaspora’, na uwezeshaji kwa biashara.