ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, September 19, 2023

MAKTABA YABOMOLEWA KUJENGWA MPYA YA KISASA MWANZA NA CHATO


 NA. ALBERT G.SENGO/MWANZA

Huku akionesha na kuelekeza kwa mkono kupitia picha kubwa ya kwenye bango la ukumbi wa mkutano, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (TLSB) Dkt. Mboni A. Ruzegea anasema "Kama umepita sasa hivi eneo ambalo kulikuwa na maktaba ya mkoa wa Mwanza, imebomolewa na ujenzi unaendelea"
"Na hii hapa ndiyo picha ya jinsi jengo litakavyokuwa kwa Maktaba ya Mwanza, pindi litakapokamilika, mnaletewa kitu kizuri sana na Serikali ya awamu ya sita ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, kizuri ni kwamba pesa zake zilishaidhinishwa kwenye Bajeti ya 2023-2024" na kisha Dkt Ruzegea akaendelea kwa kusema. "Vilevile tutakuwa na maktaba kumbukumbu ya aliyekuwa Rais wa awamu ya 5 Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ambayo inajengwa pale Chato, maktaba kubwa nzuri ya mfano itakayobeba kumbukumbu zote za viongozi wa nchi yetu" Taarifa hii imetoka leo Septemba 19 katika Kongamano la Tatu la Kitaifa la Huduma za Maktaba, Tamasha la Vitabu na Usomaji, linalofanyika katika Ukumbi wa Mikutano BOT Kapri Point, Jijini Mwanza. Lengo kuu la Kongamano na Tamasha hili ni kutoa fursa kwa wadau wote wa huduma za maktaba nchini kushiriki, kujadili, kuchangia na kuamua kwa pamoja upatikanaji na utumiaji wa huduma bunifu za maktaba na teknolojia za kisasa nchini kunavyosaidia kujenga ari na utamaduni wa kujisomea. Kongamano hili ni la siku 3, hivyo litadumu kuanzia leo 19 hadi 21 mwezi Septemba 2023. Kauli mbiu ya Kongamano hilo kwa mwaka huu 2023 ni 'Waandishi na Wachapishaji Tukutane Maktaba'

Monday, September 18, 2023

MHE. RAIS SAMIA AKIZUNGUMZA NA WANANCHI WA MTAMA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi wa Mtama leo tarehe 18 Septemba, 2023

KONGAMANO LA HAKI JINAI LAFANYIKA KIBAHA WANANCHI WAELEZA KERO ZAO.

 


Na Victor Masangu,Kibaha 

Wananchi Wilayani Kibaha mkoani Pwani wameiomba serikali kuingilia kati changamoto ya baadhi ya askari wa maliasili kuwakamata na kuwapiga bila sababu za msingi baadhi ya  watu wanaobeba mkaa kwa ajili ya matumizi yao binafsi ya nyumbani kitendo ambacho wamedai ni uonevu.

Wananchi hao wameyasema wakati wa kongamano maalumu kwa ajili ya kujadili haki jinai lililofanyika katika stendi ya zamani maili moja Wilayani Kibaha na kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali taasisi binafsi,wajumbe wa tume iliyoundwa  pamoja na wananchi.

Wamesema kumekuwepo na ukiukwaji wa sheria na taratibu kwa baadhi ya askari hao wa maliasili kuchukua maamuzi ambayo sio sahihi ya kuwakamata watu ambao hawana hatia na kuwachukulia mkaa kitendo ambacho wamekilaani vikali.

Kadhalika Ally Rashid ambaye ni mwananchi alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuunda time hiyo ya haki jinai ambayo itaweza kusaidia kwa kiasi kikubwa changamoto mbali mbali ambazo zinawakabili wananchi hasa katika kupata haki zao za msingi.

Kadhali hawakusita kutoa maoni yao juu ya adhabu kunyonga iwe pale pale na kwamba inatakiwa iundiwe  kitengo chake maalumu  badala ya kuacha jukumu hilo kwa Rais pekee yake na kwamba watu wanaofanya mauaji kwa makusudi adhabu hiyo iwahusu bila ya huruma.

Naye mwananchi mwingine alitejitambulisha kwa jina la  Hawa John alisema kwamba kumekuwepo kwa baadhi ya  polisi jamii nao wamekuwa hawatendi haki pindi wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao katika kuwakamata watuhumiwa.

" Hawa polisi Jamii wako sana kwenye kata unapofika kuelezea tukio lako polisi unaambiwa uwape kwanza hela ili wakamkamate mtuhumiwa hili jambo kwetu ni kero tunaomba takukuru pamoja na  Tume ilifanyie kazi"alisema 

Hawa pia alisema lipo suala la baadhi ya Askari wa Jeshi la Polisi kutowalinda watu wanaotoa taarifa za wahalifu linapaswa kuangaliwa Ili kulinda usalama wao kwani wapo wanaopelekewa taarifa kuhusiana na wahalifu lakini haohao Askari wanawataja watoa taarifa.

Naye Ramadhani Maulidi alieleza katika mkutano huo kwamba  anatamani siku moja angeajiriwa na Serikali Ili akafanye kazi ya kunyonga watu waliohukumiwa kutumikia adhabu hiyo baada ya kukutwa na hatia ya kuhusika na mauaji.

Alisema zipo taarifa zinazoelezwa kwenye  vyombo mbalimbali kuwa ni zaidi ya miaka 10 sasa adhabu hiyo imekuwa haitekelezwi huku matukio ya mauaji yakiendelea ni wakati sasa Serikali  kuliangalia suala hilo sambamba na kuajri watu wenye roho ngumu ambao watatekeleza adhabu ya kunyonga.

"Uanakuta mtu ameuwakwa makusudi halafu anaenda kukaa gerezani muda mrefu bila kunyongwa hilo haliwezekani kama mtu amekutwa na hatia ya kuuwa naye anyongwe, siyo unasikia  wanaanza kusema haki za binadamu kwani yeye alipokuwa anauwa alikuwa hajui kuwa kuna haki za binadamu?" alifafanua .

Mjumbe waTume hiyo Dk Laurean Ndumbaro alisema  kutosainiwa kwa adhabu ya kifo kwa watu wanaohukumiwa kutumikia adhabu hiyo kwa muda mrefu sasa kumesababisha uwepo wa mlundikano wa wafungwa na kwamba  mapendekezo yao ni kuona suala hilo linangaliwa upya.

Prof.  Edward Hosea ambaye ni Mjumbe wa Tume ya Haki Jinai alisema.kuwa katika ufuatiliajj wao walibaini kwamba zipo sheria nyingi zinatakiwa kufanyiwa marekebisho Ili kulinda haki za wananchi ikiwemo utitiri wa majeshi uliopo ambaounapaswa kuangaliwa na kuundiwa sheria upya.

Sunday, September 17, 2023

TASAC YATOA ELIMU KWA UMMA KATIKA MAONESHO YA KONGAMANO LA WIKI YA PILI YA UFUATILIAJI (U&T) 12-15 SEPTEMBA 2023 ARUSHA - AICC

 


Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limefanikiwa kutoa elimu kwa umma ikiwa ni moja ya  ya Taasisi za Kiserikali zinazoshiriki maonesho yanayoendelea katika Kongamano la Wiki ya Pili ya Ufuatiliaji (U&T).

Maonesho hayo yanayofanyika katika Viwanja vya AICC jijini Arusha yalianza tarehe 12 Septemba na kilele chake ni tarehe 15 Septemba, 2023. 

TASAC inashiriki maonesho hayo ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu kazi  na majukumu inayoyatekeleza kwa mujibu wa Sheria ya Uwakala wa Meli Tanzania, Sura 415.

Wadau wote mnaalikwa kutembelea banda la TASAC katika eneo zilipo Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Sekta ya Uchukuzi.

Thursday, September 14, 2023

TRA PWANI YAWAHIMIZA WAFANYABIASHARA KUTUMIA MASHINE ZA EFD

 NA. VICTOR MASANGU,PWANI


Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani katika kupambana na kudhibiti mianya ya ulipaji wa kodi imezindua kampeni maalumu yenye lengo la kutoa elimu kwa wafanyabiashara juu kutumia mashine za kielekroniki (EFD) pindi wanapouza bidhaa zao. Hayo yamebainishwa na Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani, Masawa Masatu wakati akizungumza na waandishi kuhusiana na kampeni hiyo ambayo pia itaenda sambamba na kuwahimiza wananchi kuhakikisha wanasai risiti pindi wanapofanya manunuzi kwani ni haki yao. Nao baadhi ya wafanyabiashara wa Mkoani Pwani hawakusita kuzungumzia juu ya umuhimu wa kutumia mashine hizo za EFD huku wameipongeza TRA kwa hatua ya kwenda kuwatembea na kuwapa elimu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa maslahi ya maendeleo ya Taifa. Jisena Simon na Ramadhani Kassim Wafanyabiashara Mkoa wa Pwani. Kampeni hiyo maalumu ambayo imepewa jina la Tuwajibike itafanyika kwa kipindi cha wiki moja katika Wilaya mbalu mbali za Mkoa wa Pwani ambapo italenha zaidi kutoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara juu ya kutoa risiti halali pamoja na kudai risiti.

Wednesday, September 13, 2023

Rais Mwinyi aipongeza Benki ya CRDB kwa huduma za kibenki zinazozingatia msingi ya Kiislamu

 


Unguja. Tarehe 10 Septemba 2023: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt Hussein Ali Mwinyi ameipongeza Benki ya CRDB kwa kuanzisha huduma za kibenki zinazofuata misingi ya sharia hivyo kuwahamasisha Waislamu wengi kutumia huduma zake jambo linalochochea ujumuishi wa kifedha.

Rais Mwinyi ambaye alikuwa mteja wa kwanza kufungua akaunti ya Al Barakah mwishoni mwa mwaka 2021 huduma hiyo ilipozinduliwa, ametoa pongezi hizo alipokabidhiwa kadi ya akaunti hiyo mwishoni mwa wiki alipotembelewa na ujumbe wa Benki ya CRDB ikulu mjini Zanzibar.
“Tulijua Al Barakah itakuwa na mafanikio lakini hatukutarajia kuwa yangepatikana ndani ya muda mfupi namna hii. Nawapongeza kwa mafanikio mliyoyapata na niwaahidi kwamba Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itaendeleza ushirikiano na benki yenu kuhakikisha huduma hizi zinawafikia Waislamu wengi walipo visiwani humu ili kwa Pamoja tushiriki kulijenga Taifa letu huku tukimwabudu Mwenyezi Mungu bila kukiuka maagizo yake,” amesema Dkt Mwinyi.

Rais Mwinyi pia ameishukuru Benki ya CRDB kwa heshima iliyompa ya kuwa mteja wa kwanza kukabidhiwa kadi ya Akaunti ya Al Barakah na akasema jambo hilo limemhamasisha zaidi hivyo ataangalia namna ya kuongeza amana kwenye akaunti yake ili kufurahia huduma hizo zinazokidhi mahitaji yake ya kifedha na imani ya kiroho.
Akimkabidhi kadi ya Al Barakah, Meneja wa Kanda ya Mashariki wa Benki ya CRDB inayojumuisha Zanzibar na mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, Badru Idd amesema Rais Mwinyi sio tu alihamasisha kuanzishwa kwa huduma hizo bali alionyesha mfano kwa kuwa wa kwanza kufungua akaunti hiyo mwaka 2021 ambayo mpaka sasa ina wateja zaidi ya 70,000 nchini kote.

“Mpaka sasa hivi, tumekopesha zaidi ya shilingi bilioni 90 kwa misingi ya sharia na tumepokea amana za wateja zaidi ya shilingi 85 bilioni ndani ya miaka miwili ya kutoa huduma hizi. Huduma za CRDB Al Barakah Banking zinaendelea kutoa mchango mkubwa sana katika serikali yako ya Zanzibar na wananchi wake kwani tumekopesha zaidi ya shilingi 18 bilioni kwenye uchumi wa buluu na wafanyabiashara wamepata Zaidi ya shilingi bilioni 33,” amesema Idd.

Ili kusogeza huduma kwa wananchi visiwani humu, Benki ya CRDB ilifungua tawi mjini Wete lililozinduliwa na Rais Mwinyi mwaka 2021 alikoiomba benki kuanzisha huduma zenye misingi ya sharia na mpaka sasa, kwenye matawi manne ya Benki ya CRDB yaliyomo Zanzibar, wananchi wameweka amana za zaidi ya shilingi bilioni 28.
Kuhusu kadi za Akaunti ya Al Barakah, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Benki Zinazofuata Sharia (Islamic Bankink) wa Benki ya CRDB, Rashid Rashid amesema zipo za aina nne na zote zinaweza kutumika katika majukwaa yote ikiwamo kwa mawakala zaidi ya 200 waliopo Zanzibar kama ilivyo kwa kadi zinazotumiwa na wateja wengine wote wa Benki ya CRDB.

“Pamoja na mafanikio haya makubwa, CRDB Al Barakah Banking tunaendelea kuboresha huduma zetu ili kuwafikia wateja wetu na kuwapa amani wanayoitegemea kwa kuweka pesa zao katika akaunti za Al Barakah zinazofuatisha misingi ya sharia. Kila mteja mwenye akaunti hii, ana amani kwa kujua kwamba pesa zake ziko mahala salama na zina uangalizi maalum unaoendana na imani na maadili yake,” amesema Rashid.
Akizungumzia umuhimu wa huduma za fedha kwa maendeleo ya Taifa, Mwenyekiti wa Bodi ya Huduma za Fedha Zinazofuata Misingi ya Sharia ya Benki ya CRDB, Abdul van Mohammed amesema kuna fursa nyingi ambazo Zanzibar inaweza kunufaika nazo iwapo itafungua milango.

“Zanzibar ndio yenye matumizi makubwa ya Islamic Banking Afrika Mashariki. Naomba Serikali iangalie uwezekano wa kuifanya kuwa ya kwanza kuuza hatifungani ya Kiislam ili kupata fedha zitakazochangia maendeleo ya watu wetu,” amesema Mohammed.




TPA YAUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS DKT SAMIA KWA KUTOA MSAADA WA VIFAA TIBA HOSPITALI YA WILAYA YA KOROGWE

 

MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo  kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo kushoto akipokea msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe Jokate Mwegelo  kushoto katikati akimkabidhi  msaada wa vifaa tiba wenye thamani ya Milioni 10 Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Korogwe Miriam Cheche mara baada ya kuvipokea kutoka kwa Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kulia  kwa ajili ya Hospitali ya wilaya ya Korogwe ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.
MKUU wa wilaya ya Korogwe     Jokate Mwegelo  kushoto akiwa na Meneja wa Bandari ya Tanga Mrisha Masoud wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo
MKUU wa wilaya ya Korogwe   Jokate Mwegelo    kushoto akiwa na Meneja wa Bandari ya Tanga Mrisha Masoud wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo



Sehemu ya vifaa hivyo





Na Oscar Assenga,KOROGWE

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) wamekabidhi msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya Milioni 10 katika Hospitali ya wilaya ya Korogwe  ikiwa kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu za kuondoa changamoto kwenye sekta ya afya, elimu na mambo mengine kwenye jamii.


Vifaa vilivyotolewa ni viti mwendo 10 vyenye thamani ya milioni 4 na ya mashine ya ECG kwa ajili ya matibabu ya moyo ambavyo vitakwenda kuwasaidia wananchi wanapata huduma kwenye Hospitali hiyo kutoka maeneo vijiji mbalimbali wilayani humo ikiwa  ni kurudisha kwa jamii

Akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo , Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha alisema kwamba wameamua kutoa msaada huo ikiwa leo ni siku yao ya kusheherekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Bandari nchini.

Alisema wao wametoa kwa jamii walichokipata mwaka huu na wameamua kupeleka msaada huo kwenye Hospitali hiyo ili kuweza kuwasaidia kuwapunguzia baadhi ya changamoto zilizokuwa zikiwakabili kwenye Hospitali ya Korogwe.

“Licha ya kutoa msaada huu hapa lakini tutaendelea kusaidia kitakachpatikana ili kuweza kutatua changamoto kwenye hospitali ili kuhakikisha wananchi wanaondokana na vikwazo mbalimbali katika kupata huduma za matibabu”Alisema

Awali akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo Mkuu wa wilaya ya Korogwe  Jokate Mwegelo   aliishukuru Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa msaada huo mkubwa ambao wamewapatia kwa ajili ya hospitali ya wilaya ya Korogwe ambao ni vitindi mwendo ambavyo uhitaji wake ulikuwepo.

Alisema pia msaada huo mashine ya  ECG   kwa ajili ya matibabu ya moyo utawasaidia wananchi katika wilaya hiyo kutokana na idadi ya watu wenye matatizo ya moyo inaongezeka vijijini kutokana na matumizi ya chumvi kuongezeka.

Alisema pia matumizi ya mafuta vinachangia pia na mtindo wa maisha huku akieleza kifaa hicho kitakwenda kuwatibu wananchi na hivyo kuwasaidia kuwa na afya bora kutokana na kwamba Taifa lenye nguvu lazima wananchi wake wawe na afya bila afya hawaweze kufanya kazi na kuweza kushiriki shughuli za kijamii ili kuweza kukuza uchumi.

Naye kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Korogwe Miriam Cheche aliishukuru TPA kwa kugawawia msaada wa vifaa hivyo ikiwemo kifaa cha kisasa ambacho kinagundua matatizo ya moyo kwa mtu anayeugua kabla ya kupelekwa kwenye Hospitali za Rufaa.

“Kwa kweli tunawashukuru sana TPA kwa msaada huu kwa sababu wananchi watafaidika na mashine hii lakini tunamshukuru DC kwa hamasa zake na hivyo kupelekea wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia pia Rais Dkt Samia Suluhu kuendelea kutupatia fedha kuendeleza hospitali yetu ya wilaya hapa Makuyuni”Alisema

MBUNGE KOKA AFANYA KWELI ATEKELEZA AHADI ZAKE SOKO LA MNARANI.


 Na Victor Masangu,Kibaha


Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka ametekeleza ahadi yake kwa vitendo kwa wafanyabiashara wa soko la mnalani kwa kuwakabidhi matenki makubwa matatu kwa ajili ya kuhifadhia maji.

Koka amekabidhi matanki hayo wakati wa ziara yake ya kikazi yenye lengo la kuweza kuwatembelea na kuzungumza na wafanyabiashara wa bidhaa  mbali mbali ikiwa sambamba na kutekeleza ahadi zake ambazo aliziahidi kipindi cha nyuma.

Aidha katika ziara hiyo Mbunge Koka ambaye aliambatana na viongozi mbali mbali wa chama pamoja na viongozi wa serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nikson Saimon pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji wa Kibaha Mussa Ndomba.

Mbunge huyo alisema kwamba ana imani kwamba matanki hayo ya maji yataweza kuwasaidia  kwa kiasi kikubwa kupunguza kero na adha ambayo ilikuwa ikiwakabili wafanyabiashara hao kwa kipindi cha muda mrefu.

Sambamba na hilo Koka amekabidhi televisheni (TV) mbili za kisasa  zenye ukunbwa wa nchi 45 kwa lengo la kuwapa guess ya wafanyabiashara hao kutazama na  kupata  matukio na taarifa  mbali mbali kutoka   ndani na nje ya nchi.

"Kipindi cha nyuma nilipita katika soko hili na niliahidi matanki ya maji makubwa matatu.,Televisheni mbili sambamba na vifaa vya michezo ikiwemo mipira pamoja na jezi na leo hii nimekuja rasmi kwa ajili ya kuvikabidhi,alisema Koka.

Aidha Mbunge huyo aliongeza kwamba lengo lake kubwa ni kuwawekea mazingira mazuri wafanyabiashara hao ili soko liweze kuwa la kisasa zaidi na waweze kufanya biashara zao katika mazingira ambayo ni rafiki.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nikson Saimon alimshukuru kwa dhati Mbunge huyo kwa kuweza kuona umuhimu wa kuwasaidia wafanyabiashara hao na kwamba serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuendelea kuboresha miundombinu ya soko hilo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Kibaha Mussa Ndomba alibainisha kuwa kwa sasa wameshatenga zaidi ya milioni 200 kwa ajili ya kuezeka paaa katika soko hilo ili kuondokana na changamoto hasa katika kipindi cha mvua kwani bidhaa zimekuwa zikilowa.


Nao baadhi ya wafanyabiashara katika soko hilo wamempongeza Mbunge huyo kwa kuweza kutekeleza ahadi yake kwa vitendo na kwamba matanki ya maji waliyopatiwa yatakuwa ni mkombozi mkubwa wa upande wao katika kuhifadhi maji.

TRA PWANI YAZINDUA KAMPENI YA KUWANOA WAFANYABISHARA JUU YA UMUHIMU WA KODI

 


Na Victor Masangu,Pwani 


Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani katika kupambana na kudhibiti mianya ya ulipaji wa kodi imezindua  kampeni maalumu yenye lengo la kutoa elimu kwa wafanyabiashara juu kutumia mashine za kielekroniki (EFD) pindi wanapouza bidhaa zao.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Masawa Masatu  wakati akizungumza na waandishi kuhusiana na  kampeni hiyo ambayo pia itaenda sambamba na kuwahimiza wananchi kuhakikisha wanasai risiti pindi wanapofanya manunuzi kwani ni haki yao ya msingi.

Meneja Masawa alisema kwamba kampeni hiyo itaweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa wafanyabiashara waweze kutimiza wajibu wao katika suala zima la ulipaji wa kodi kwa hiari bila ya kukwepa lengo ikiwa ni kuisaidia serikali kukusanya mapato yake.
"Kikubwa nimewaita kwa ajili ya kampeni hii maalumu ambayo itajulikana kwa jina la Tuwajibike,'kodi yetu maendeleo yetu' na kikubwa ni kutoa elimu katika Wilaya mbali mbali za Mkoa wa Pwani na kikubwa ni wafanyabiashara kulipa kodi ili kuisaidia serikali,"alisema Masawa.

Alifafanua kuwa wananchi wanapaswa kuhakikisha wanasai risiti zao halali pindi wanaponunua bidhaa zao na pia wafanyabiashara watoe risiti za kielectoniki pindi wanapouza bidhaa zao kwani kufanya hivyo kunasaidia serikali kupata mapato yake kihalali.


Aidha Meneja huyo alibainisha kuwa lengo kubwa ni kuweka mikakati madhubuti katika ukusanyaji wa kodi ambayo itaweza kusaidia katika mambo mbali mbali ikiwemo kutekeleza miradi ya maendeleo  kama vile ya elimu,afya,umeme,pamoja maeneo mengine.



Nao baadhi ya wafanyabiashara wa Mkoani Pwani hawakusita kuzungumzia juu ya umuhimu wa kutumia mashine hizo za EFD huku wameipongeza TRA kwa hatua ya kwenda kuwatembea na kuwapa elimu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa maslahi ya maendeleo ya Taifa.

Mmoja wa wafanyabiashara wa eneo la Loliondo alibainisha kuwa kutokana na elimu ambayo wamekuwa wakiipata kutoka kaa TRA Mkoa wa Pwani kumewasaidia wateja wao kusai risiti zao baada ya kumaliza kufanya manunuzi ya bidhaa zao.

Kampeni hiyo maalumu ambayo imepewa jina la Tuwajibike itafanyika kwa kipindi cha wiki moja katika Wilaya mbalu mbali za Mkoa wa Pwani ambapo italenha zaidi kutoa elimu kwa wananchi na wafanyabiashara juu ya kutoa risiti halali pamoja na kudai risiti.

WATATU KUPAMBANA LEO HATUA YA ROBO FAINALI

 


MABONDIA WATATU WA TANZANIA LEO WATINGA ROBO FAINALI YA MASHINDANO KUFUZU KUSHIRIKI OLIMPIKI. 

 Watanzania watatu leo kuanzia saa kumi na moja jioni kwa saa za Senegal, watapanda ulingoni kutafuta tiketi ya kuingia nusu fainali katika mashindano ya kufuzu kushiriki mashindano ya Olimpiki 2024 Paris Ufaransa yanayoendelea Dakar Senegal. Mabondia hao ni, katika uzito wa 66Kg. wanawake Grace Mwakamele (Tanzania) atapambana na Khelif Imane (Algeria), katika uzito wa 51Kg. 

Abdallah Mohamed (Tanzania) atacheza na Mortaji Said (MOROCCO) na katika uzito wa 80Kg. Yusuf Changalawe atacheza na Seydna Konate (Senegal)  

Mabondia waliofuzu kufika hatua hiyo jumla yao ni 104 kutoka katika mataifa 26 ya AFRIKA.  

Jumla ya mabondia walioshiriki mashindano hayo ni 235 kutoka katika mataifa 41 ya Afrika.  

Mabondia wengine wa Tanzania walishindwa katika hatua za awali ni 50Kg. Zulfa Macho, 57Kg. Mwalami Salum na 92 Kg. Mussa Maregesi. 

Viongozi waliombatana na timu ni Lukello Wililo (Raisi na Mkuu wa Msafara),Makore Mashaga (katibu na kocha msaidizi), Samwel Batman (Kocha mkuu) na Aisha George (Matron) Fainali za mashindano hayo zitafanyika ijumaa ya tarehe 15.09.2023. 

Timu itarejea nyumbani Jumapili ya tarehe 17.09.23 saa tisa Alfajiri. 

Naambatanisha na ratiba ya leo.   

Monday, September 4, 2023

KENYA NA CHINA ZAVUTIWA NA FURSA ZA UWEKEZAJI KWENYE MIFUGO NCHINI

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Ranchi ya Mbogo Bw. Naweed Mullah (kulia) akimuongoza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Daniel Mushi (kushoto) na timu ya washiriki wa  Mkutano wa Jukwaa la Mifumo ya Chakula  (AGRF) waliofika shambani kwake Chalinze, Septemba 03,2023 kwa ajili ya kuona namna anavyofanya shughuli zake.
Meneja Uendelezaji biashara kutoka kiwanda cha kusindika nyama cha "TANCHOICE" Bw. Luwungo Hassan (aliyesimama mbele) akielezea kwa ufupi historia ya kiwanda hicho kwa washiriki wa Mkutano wa Jukwa la mifumo ya Chakula (AGRF) waliofika kiwandani hapo Septemba 03, 2023.
Sehemu ya aina ya Ng'ombe waliopo kwenye ranchi ya Mbogo iliyopo Chalinze mkoani Pwani.


 ◾Ni mara baada ya kuwatembelea wadau wa Sekta hiyo..


Nchi za China na Kenya zimeonekana kuvutiwa na fursa za uwekezaji zilizopo kwenye sekta ya Mifugo mara baada ya kuwatembelea wawekezaji wa ndani ambao ni Ranchi ya Mbogo na Kiwanda cha kuchakata nyama cha “Tanchoice” vilivyopo mkoani Pwani Septemba 03, 2023.

Ziara hiyo ambayo ni miongoni mwa shughuli za utangulizi zinazofanyika kabla ya kufanyika kwa mkutano wa Jukwaa la Mifumo ya chakula barani  Afrika (AGRF) iliongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayesimamia sekta ya Mifugo Dkt. Daniel Mushi ambapo alibainisha kuwa Wizara yake imejiandaa kikamilifu kutumia fursa zitakazojitokeza katika pindi chote cha mkutano huo kuiimarisha sekta ya Mifugo nchini.

“Sisi kwa sasa kama nchi tunasema  “flagship” ya wizara yetu ni nyama na samaki ambazo tunazipeleka nje ya nchi na kwa mwaka jana tulifanikiwa kusafirisha tani elfu 14 na malengo yetu ni kuvuka tani elfu 16 kwa mwaka huu wa fedha na hilo tunaweza kufanikiwa kwa kuleta wadau wengi zaidi kama mbogo ranchi” Amesema Dkt. Mushi.

Aidha Dkt. Mushi ameongeza kuwa lengo la mkutano huo ni kupata wawekezaji na masoko mapya ili nyama inayozalishwa nchini iweze kuuzwa kwa wingi nje ya nchi hatua ambayo anaamini itachangia ongezeko la fedha za kigeni kwa kiwango kikubwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa ranchi ya Mbogo Bw. Naweed Mullah amesema kuwa anatarajia kutumia mkutano huo wa kimataifa wa jukwaa la Mifumo ya chakula kuhakikisha anatoa elimu ya kutosha kwa washiriki wa ndani na nje ya nchi kuhusu njia bora za uongezaji thamani wa ng;ombe wa asili waliopo hapa nchini na barani Afrika kwa ujumla.

“Tunajua ulimwengu mzima unakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa chakula hasa nyama na hali ya upatikanaji wa zao hilo imeendelea kushuka kutokana na mabadiliko ya tabia nchi hivyo tunaamini jukwaa hili limelenga kujadili namna bora ya kukabiliana na changamoto hiyo” Ameongeza Bw. Mulllah.

Naye mmoja wa washiriki wa ziara hiyo Bi. Wangari Kurya kutoka nchini Kenya mbali na kukoshwa na uwekezaji mkubwa uliofanyika katika sekta ya Mifugo nchini amevutiwa zaidi na namna Serikali inavyohamasisha aina zote za kilimo ikiwa ni tofauti na kwao ambako kilimo mazao ndio kimekuwa kikisisitizwa zaidi.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya “FAMSUN” kutoka nchini China Bw. Joy Lee amevutiwa na namna Tanzania ilivyobarikiwa kuwa na ardhi kubwa na nzuri kwa ajili ya kufanya shughuli za ufugaji tofauti na hali ilivyo nchini kwao ambako wanalazimika kutumia kiwango kikubwa cha teknolojia ili kutekeleza shughuli hizo kwenye maeneo madogo waliyonayo.

“Ninatoa wito kwa wawekezaji wote kuja Tanzania kuna fursa nyingi sana za uwekezaji kwa upande wa sekta ya Mifugo” Amehitimisha Bw. Lee.

Mkutano wa Jukwaa la kujadili Mifumo ya chakula barani Afrika unatarajiwa kufanyika hapa nchini kuanzia Septemba 05-08, 2023 ambapo takribani 6000 wa ndani na nje ya nchi  wanatarajia kushiriki kwenye mkutano huo.

TANGA UWASA YATUMIA MILIONI 20 KUKARABATI MTANDAO WA MAJI TAKA USAGARA

 

Meneja wa Mazingira wa Tanga Uwasa Nasibu Ramadhani akikagua mtandao wa maji taka katika eneo la Usagara Jijini Tanga ambao wameufanyia ukarabati mkubwa
Meneja wa Mazingira Tanga Uwasa Nasibu Ramadhani akikagua mtandao wa maji taka katika eneo la Usagara Jijini Tanga ambao wameufanyia ukarabati mkubwa
Muonekano wa chemba zilizokarabatiwa
Muonekano wa chemba zilizokarabatiwa

Na Oscar Assenga, TANGA

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) imetumia milioni 20 kwa ajili ya kuukarabati mtandao wa maji taka wa zamani katika eneo la Usagara maarufu kama Bandari Chafu.

Akizungumza Meneja wa Mazingira wa Tanga Uwasa Nasibu Ramadhani alisema uamuzi wa kuukarabati mtandao huo wa maji taka waliufanya baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wakazi wa wa eneo hilo tokea 2018.

Alisema malalamiko hayo yalikuwa yanahusiana na miuondombiu ya maji taka eneo hilo kuwa chakavu na hivyo kuhatarisha afya zao na hivyo kuomba mtandao huo uliojengwa na TPA miaka ya nyuma na hivyo baada ya kubinafishwa nyumba hizo.

Alisema hivyo wanawaomba Tanga Uwasa iwarebishie mfumo huo ambapo awali ulikuwa baada ya kuona changamoto hizo waliamua watenge fedha Milioni 20 kwa ajili ya kuukarabati mtandao huo.

Alisema katika ukarabati wa mtandao huo ulihusisha ukarabati wa chemba kubwa ambazo zinapokea maji taka kutoka kwenye maeneo hayo na ukarabati wa chemba ndogo ndogo ambazo zinaunganisha bomba na bomba na maeneo yenye bomba chakavu .

“Hayo ndio maeneo tuliyoyakarabati na tunatarajia kukarabati na mwaka huu tutakamilisha mpango huo wa ukarabati kukamilisha mfumo hiyo ili kuuwezesha kuishi muda mrefu hiyo itasaidia kuondokana na changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokeza”Alisema

Hata hivyo alitoa wito kwa wakazi wa eneo hilo kuhakikisha miundombinu ya maji taka kuhakikisha hawaweki taka ngumu na wanaitunza ili iweze kukaa muda mrefu