ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 3, 2026

AKINAMAMA CHANGAMKIENI FURSA ZA MIKOPO NAFUU AKIBA COMMERCIAL BANK

 

Na Albert G. Sengo | Mwanza

Katika juhudi za kuimarisha uchumi jumuishi na kukuza ujasiriamali miongoni mwa wanawake, Benki ya Akiba (Akiba Commercial Bank) imeendelea kujenga ukaribu wa karibu na wateja wake kupitia mikutano ya moja kwa moja. Moja ya hatua hizo ni mkutano maalum uliowakutanisha akinamama wajasiriamali wa Mwanza, uliofanyika tarehe 31 Machi 2026 katika ukumbi wa ARCH Mayala, Nyakahoja.


Tukio hilo lilihudhuriwa na zaidi ya washiriki 100, wengi wao wakiwa ni akinamama wanaojishughulisha na biashara ndogo na za kati katika maeneo mbalimbali ya Kanda ya Ziwa Victoria kuanzia biashara za vyakula, usindikaji wa mazao ya kilimo, uuzaji wa samaki, hadi huduma za kijamii kama elimu na urembo.

POLISI MWANZA YASISITIZA MARUFUKU DISKO TOTO

news 

JESHI la Polisi Mkoa wa Mwanza limesisitiza marufuku ya kuandaa burudani za watoto katika kumbi za starehe (disko toto) likisema marufuku hiyo inalenga kulinda rika hilo na vitendo vya uvunjifu wa amani na kupotea.

Marufuku hiyo imesisitizwa leo Aprili 3, 2026 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbrod Mutafungwa, wakati akizungumzia maandalizi ya kuimarisha ulinzi na usalama kuelekea sikukuu hizo.

Pia Mutafungwa amepiga marufuku wazazi kuwaruhusu watoto kwenda kwenye matembezi ama sehemu za burudani bila uangalizi wa watu wazima, huku akisisitiza kila mzazi kuhakikisha anaangalia watoto ili washerehekee wakiwa na ulinzi wa kutosha.

“Niwatake wamiliki wa nyumba za kulala wageni na kumbi za starehe kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia masharti ya leseni zao kwa kutoendesha na kuandaa matamasha ya watoto (disko toto) na kuhakikisha maeneo hayo yamewekewa ulinzi wa kutosha.

“Na tunaelekeza kwa namna yoyote mambo ya kuburudisha watoto disko toto mambo hayo ni marufuku na hatutasita kuchukua hatua za sheria kwa wafanyabiashara watakaofanya hivyo hata kama wana leseni, na tunaomba wazazi wasiwaruhusi kwenda huko,” amesema Mutafungwa.

Hata hivyo, ametoa wito kwa familia zinazosherehekea sikukuu nje ya makazi yao kutoacha nyumba zao zikiwa hazina uangalizi wowote.


“Wanapotoka wahakikishe nyumba ina ulinzi. Pia tunashauri wasitoke wote ndani ya nyumba, wabaki baadhi ya watu wanaoangalia nyumba ili kuepuka kupata changamoto,” amesema.

Amesema jeshi hilo limeimarisha ulinzi maeneo yote kwa kuwapanga askari wanaotumia doria za magari, pikipiki, magari ya wazi, askari wa kiraia, askari wanaotumia wanyama, na limeshaweka mpango kazi wa doria za boti katika visiwa vinavyozungika mkoa huo.

“Tunaomba kila mwananchi awe na utii mkubwa wa sheria na kuepuka mambo ambayo yanaweza kuwaweka kwenye migogoro na vyombo ambavyo vinasimamia sheria,” amesema Mutafungwa.

Vile vile, amewataka viongozi wa makanisa yatakayokuwa na ibada za asubuhi na usiku kuendelea kushirikiana na polisi katika ngazi ya wilaya na vituo ili kuhakikisha katika ibada zote askari wanakuwepo.

MWENYEKITI MANGUNGU NA KAMANDA MULIRO WAGUSA NA KUSIKITISHWA NA KIFO CHA EMMANUEL MACHA

 
NA VICTOR MASANGU, DAR

Maelfu ya wananchi mbali mbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini,  taasisi na mashirika binafsi ,mashabiki wa soka na mziki wa dansi pamoja na wananchi mbali mbali .... wamejitokeza kwa wingi   katika makaburi ya Kinonddoni Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya  kuhudhuria mazishi ya mfanyabiashara maarufu na mshabiki mkubwa  wa klabu ya soka ya Simba Emmanuel  Nderimo almaarufu Macha ambaye alifariki dunia  machi 30 mwaka huu.

Katika mazishi hayo ambayo yalihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na chama cha mapinduzi (CCM) yalikubikwa na  vilio na majonzi makubwa ambayo yalipelekea baadhi ya watu kushindwa kujizuia kwa kutokwa na machozi  wakati wa zoezi la kuuga mwili huo.



Moja kati ya viongozi maarufu ambao walihudhulia katika  msiba huo ni Mwenyekiti wa klabu ya soka ya Simba Murtaza  Mangungu pamoja ambapo aliambatana na viongozi wengine mbali mbali wa klabu hiyo ambapo amesema marehemu Emmanuel alikuwa  na mchango mkubwa sana  katika klabu hiyo kwani alikuwa mstari wa mbela katika kusaidia mambo mbali mbali.


Pia Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya  Dar es Salaam SACP Jumanne Muliro naye alikuwa ni mmoja wa viongozi wa ulinzi na usalama ambaye naye  alifika kwa ajili ya kutoa heshima zake za mwisho  kwa Marehemu Emmaanuel Nderimo.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe,Silvestry  Koka ambaye marehemu ni  shemeji yake hakusita  kumwelezea marehemu jinsi alivyokuwa ni mpambanaji katika mambo mbali nmbali na kwamba alikuwa ni mtu wa kusamehe sana pindi unapomkosea na kwamba alikuwa ni mstari wa mbele katika kutoa ushauri wenye kujenga.

"Kwa kweli mimi nimesimama hapa kwannza kabisa namshukuru mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kutukutanisha hapa katika msiba wa ndugu yetu Emmanuel lakini kitu ambacho nataka kukisema inapaswa tuishi kwa kupendana sana na ndio maana marehemu alikuwa na upendo mkubwa sana  na watu mbali mbali na alikuwa ni mwepesi sana katika suala la kusamehe kwa hivyo inapaswa tujifunze mazuri ambayo ametuachia."amebainisha Mhe. Koka.


Nao baadhi ya  viongozi na mashabiki akiwemo Mama Asha Baraka ambaye pia ni Mbunge wa viti maalumu kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM) amesema kwamba ameguswa na kusikitishwa sana na msiba huo mzito kwani marehemu kwa upande wake alikuwa ni moja ya mtu muhimu sana katika kuleta chachu ya maendeleo katika ttimu pamoja na kuweza kusaidia mtu mmoja mmoja kwa hivyo ni pengo kubwa sana ambalo ameliacha.


Pia mwimbaji maarufu wa mziki wa dansi hapa nchini Ally Choki ni moja kati ya wasanii maarufu ambao walihudhulia katika msiba huo hadi kuweza kufika katika makaburi hayo ya Kinondoni kwa lengo la kumpumzisha ndugu yao na rafiki mkubwa wa burudani ya mziki wa dansi hapa nchini katika bendi mbali mbali.


Mazishi hayo ya marehemu Emmanule Nderimo  ambayo  yamefanyika katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam  yameweza kuhudhuliwa na umati wa  maelfu ya watu kutoka sehemu  mbali mbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa chama, viongozi wa madhehebu ya  dini, taaasisi wezeshi,wasanii maarufu, pamoja na wananchi ambao wamewza kufika na kumuhifadhi katika nyumba yake ya milele.

AKINAMAMA WA KANDA YA ZIWA VICTORIA WANAVYOCHOCHEA UCHUMI KUPITIA UJASILIAMALI NA HUDUMA ZA KIFEDHA

 


Akinamama wa Kanda ya Ziwa Victoria Wanavyochochea Uchumi Kupitia Ujasiriamali na Huduma za Kifedha

Na Albert G. Sengo | Mwanza

Katika juhudi za kuimarisha uchumi jumuishi na kukuza ujasiriamali miongoni mwa wanawake, Benki ya Akiba (Akiba Commercial Bank) imeendelea kujenga ukaribu wa karibu na wateja wake kupitia mikutano ya moja kwa moja. Moja ya hatua hizo ni mkutano maalum uliowakutanisha akinamama wajasiriamali wa Mwanza, uliofanyika tarehe 31 Machi 2026 katika ukumbi wa ARCH Mayala, Nyakahoja.

Tukio hilo lilihudhuriwa na zaidi ya washiriki 100, wengi wao wakiwa ni akinamama wanaojishughulisha na biashara ndogo na za kati katika maeneo mbalimbali ya Kanda ya Ziwa Victoria kuanzia biashara za vyakula, usindikaji wa mazao ya kilimo, uuzaji wa samaki, hadi huduma za kijamii kama elimu na urembo.

Afisa Mkuu wa Biashara wa benki hiyo, Bi. Wezi Mwanzani,


Ni dhahiri kuwa wanawake wa Kanda ya Ziwa wanachangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa eneo hili. Kupitia ujasiriamali, wamekuwa wakitoa ajira, kuongeza thamani ya mazao ya ndani, na kuzungusha mzunguko wa fedha katika jamii.

Hata hivyo, pamoja na juhudi zao, bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa mitaji, elimu ya kifedha, pamoja na ugumu wa kupata huduma rasmi za kifedha. Hapa ndipo nafasi ya taasisi za kifedha kama Benki ya Akiba inakuwa muhimu zaidi.

Jukwaa la Kusikilizana na Kujifunza

Katika mkutano huo, washiriki walipata fursa ya kipekee ya kuzungumza ana kwa ana na viongozi waandamizi wa benki, kutoa maoni yao, na kueleza changamoto wanazokutana nazo katika safari yao ya ujasiriamali.

Afisa Mkuu wa Biashara wa benki hiyo, Bi. Wezi Mwanzani, alieleza kuwa mwitikio mkubwa wa wanawake wa Mwanza unaonyesha wazi imani waliyonayo kwa benki hiyo pamoja na uhitaji mkubwa wa huduma za kifedha zilizo karibu na mahitaji yao halisi.

“Tunaona wazi nguvu ya akinamama katika uchumi wa Mwanza. Kama benki, tunalenga kutoa huduma bunifu zinazomgusa mteja moja kwa moja kwenye uhalisia wa biashara yake,” alisema Bi. Wezi.

Aliongeza kuwa Mwanza ni eneo muhimu katika mkakati wa benki wa kuhakikisha huduma za kifedha zinawafikia wananchi wengi zaidi, hasa wale waliopo katika sekta isiyo rasmi.

Mkurugenzi wa Faith Junior School, Bi. Shiide Nyanda Lugoba.


Miongoni mwa washiriki waliotoa ushuhuda ni Mkurugenzi wa Faith Junior School, Bi. Shiide Nyanda Lugoba, ambaye alieleza namna mkopo kutoka Benki ya Akiba ulivyomsaidia kukuza taasisi yake ya elimu.

“Nimefanikiwa kuendesha shule kwa ufanisi zaidi kutokana na mkopo nilioupata. Leo hii, kupata huduma za kifedha si changamoto tena kama ilivyokuwa awali,” alisema.

Aidha, alibainisha kuwa matumizi ya mifumo ya kidijitali kama Lipa Namba yamerahisisha malipo kwa wateja wake, hasa wazazi, kwa kuwaondolea usumbufu wa foleni benki.

Elimu ya Fedha na Fursa za Mikopo



Mbali na majadiliano, washiriki walipata elimu muhimu kuhusu:

  • Usimamizi wa fedha binafsi na za biashara
  • Matumizi salama ya huduma za kidijitali
  • Njia bora za kukuza biashara kwa uendelevu
  • Fursa za mikopo nafuu kwa wajasiriamali


Elimu hii ni nyenzo muhimu inayoweza kuwasaidia akinamama kubadili biashara zao kutoka kiwango cha kawaida hadi kuwa miradi yenye tija kubwa kiuchumi.




Umuhimu wa Kurasimisha Biashara

Wakili Msomi Rose Ndege.

Kwa upande wake, Wakili Msomi Rose Ndege alisisitiza umuhimu wa kurasimisha biashara kama hatua ya msingi ya kufungua milango ya fursa za kifedha.

“Bila kurasimisha biashara, ni vigumu kupata imani ya taasisi za kifedha. Rasmi ni ufunguo wa kupata mitaji, kujenga uaminifu, na kukuza biashara,” alieleza.


Kwa ujumla, mkutano huu umeonesha wazi kuwa akinamama wa Kanda ya Ziwa si tu washiriki wa uchumi, bali ni injini muhimu ya maendeleo. Kupitia ushirikiano kati yao na taasisi za kifedha, kuna fursa kubwa ya kukuza biashara, kuongeza kipato, na hatimaye kuinua uchumi wa jamii nzima.

Kadri elimu ya kifedha inavyozidi kuenea na huduma za kifedha zinavyokuwa rafiki zaidi, ndivyo ndoto za wanawake wengi wajasiriamali zinavyoweza kutimia—kutoka biashara ndogo hadi kuwa himaya kubwa za kiuchumi.



Picha ya pamoja.

Monday, March 30, 2026

NEMC KUPEWA NGUVU ZAIDI KUDHIBITI MAZINGIRA-MASAUN

 

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Rais (Muungano na Mazingira), Hamad Yusuf Masauni, amesema serikali inatarajia kufanya maboresho ya sheria ili kuipa mamlaka zaidi Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kushughulikia moja kwa moja wanaokiuka sheria za mazingira, bila kujali kama ni taasisi za umma au binafsi.

Akizungumza Machi 30, 2026 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha usimamizi wa taka ili kulinda mazingira na afya za wananchi.

Aidha, Masauni amewataka wananchi kutumia kilele cha maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri kama fursa ya kujifunza namna ya kubadilisha taka kuwa rasilimali yenye tija, hatua itakayosaidia kuongeza kipato na kukuza uchumi wa taifa.

Ameongeza kuwa NEMC inahitaji kupatiwa vitendea kazi vya kisasa, ikiwemo helikopta na droni, ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake na kudhibiti uchafuzi wa mazingira.

Sambamba na hilo, ametoa onyo kali kwa wote wanaochafua mazingira, wakiwemo wazalishaji wa mifuko ya plastiki, wanaotupa taka hovyo, wanaomwaga maji machafu baharini na wanaosababisha kelele mitaani, akisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa bila upendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amesema mkoa wa Dar es Salaam umeanza mpango wa kufundisha somo la uhifadhi wa mazingira kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, ambapo tayari shule 10 zimechaguliwa kuanza utekelezaji wake.

RAIS DKT.SAMIA APOKEA RIPOTI YA CAG, TAKUKURU NA PPRA LEO IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali mara baada ya kupokea Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa Fedha 2024/25, Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye hafla ya kupokea Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa Fedha 2024/25, Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Bw. Charles Kichere akisoma Muhtasri wa Ripoti yake kwa Mwaka wa Fedha 2024/25, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa Fedha 2024/25 kutoka kwa Bw. Charles Kichere, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Bw. Crispin Chalamila akisoma Muhtasari wa Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Taasisi hiyo, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo, Bw. Crispin Chalamila, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 30 Machi, 2026.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) Bw. Dennis Simba akisoma Muhtasari wa Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Taasisi hiyo, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Taarifa ya Mwaka ya Utendaji Kazi wa Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Bw. Dennis Simba, Ikulu jijini Dar es Salaam, tarehe 30 Machi, 2026.

MAFURIKO SIMANJIRO 169,638 WAOMBA MSAADA WA DHARURA

news

TAKRIBANI wananchi 169,638 wa Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara wamekumbwa na mafuriko makubwa yaliyosababisha uharibifu wa makazi, mali na mashamba, hali inayozidi kuongeza ugumu wa maisha kwa wakazi wa eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro, Fakii Lulandala, amesema licha ya idadi hiyo ya wananchi walioathirika lakini pia mafuriko hayo yameharibu zaidi ya ekari 97,429 za mashamba kwa kujaa maji.

Imeelezwa kuwa mafuriko hayo yameathiri kwa kiasi kikubwa kata za Shambalai, Nduruma, Mirerani na Naisinyai, ambako maji yameingia ndani ya nyumba na kusomba mali mbalimbali pamoja na kuharibu vyanzo vya chakula, huku ukihitajika msaada wa dharura.

“Athari hizo zimeacha wananchi wengi bila makazi, chakula na mahitaji muhimu, na wengine wamelazimika kuishi kwa ndugu na jamaa wakati wakisubiri msaada zaidi,” amesema.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, mkazi wa Mererani, Henson Loy, amesema tatizo la mafuriko limekuwepo kwa muda mrefu lakini mwaka huu limeongezeka kwa kiwango kikubwa zaidi.

“Moja ya sababu kuu ya hali hiyo ni miundombinu mibovu ya mifereji ya maji pamoja na barabara kuwa chini, hali inayosababisha maji kushindwa kupita na hivyo kuelekezwa moja kwa moja kwenye makazi ya wananchi,” amesema.

Mkazi wa Utupendana, Jonathan Mkali, amesema mafuriko hayo hujitokeza mara kwa mara kila msimu wa mvua na hudumu kwa muda mrefu, hali inayosababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi ikiwemo kukatika kwa mawasiliano na shughuli za kiuchumi.

Katika juhudi za kusaidia waathirika, kampuni ya Permanent Minerals imetoa msaada wa vifaa mbalimbali ikiwemo chakula vifaa vya shule vya watoto,vyandarua,venye thamani ya takriban Sh. milioni 22, ikiwa ni sehemu ya mchango wa wadau katika kukabiliana na athari za mafuriko hayo.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ameendelea kutoa wito kwa taasisi mbalimbali, mashirika na wananchi kujitokeza kusaidia zaidi, akisisitiza kuwa mahitaji bado ni makubwa kutokana na ukubwa wa janga hilo.

Aidha, wananchi wameiomba serikali kuchukua hatua za kudumu kwa kuboresha miundombinu ya mifereji ya maji, kupanua mitaro na kuinua barabara ili kuzuia kujirudia kwa mafuriko hayo katika siku zijazo.

"HAPAKUWA NA MTU WAKATI AJALI IKITOKEA MGODINI" - RIPOTI YASEMA

 

Taarifa ya Odisi ya Madini Mbogwe, Geita.


OFISI ya Afisa Madini Mkazi Mbogwe imetoa ufafanuzi kuhusu tukio la ajali lililotokea katika Mgodi wa Dhahabu wa Msasa kwamba wakati tukio linatokea hapakuwa na shughuli zozote za uzalishaji katika eneo husika kwakuwa watendakazi wote walikuwa tayari wameondolewa kupisha ukarabati.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na ofisi hiyo ya madini Mbogwe, katika mgodi huo uliopo katika Kijiji cha Msasa, Runzewe, Wilaya ya Bukombe, Mkoa wa Geita, Machi 29, 2026 majira ya saa 4:00 asubuhi, katika eneo la Area A kulitokea mpasuko wa ardhi ulioathiri maduara manne yenye namba KO 46A, 47A, 48A na 49A.

“Hadi sasa, kwa mujibu wa taarifa ya pamoja ya timu ya uokozi, wakaguzi wa migodi na vyombo vya usalama, hakuna mtu aliyeripotiwa kupata majeraha wala kupoteza maisha kutokana na tukio hilo,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

 Imesema maduara hayo yalikuwa yamesimamishwa uzalishaji kufuatia maelekezo ya wakaguzi wa mgodi yaliyotolewa Machi 27, 2026 ili kufanyiwa ukarabati wa kiusalama. Na kwamba mpasuko huo ulisababisha maduara hayo kutitia ardhini, hali inayohusishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini na kusababisha kulegea kwa udongo na miamba.

“Baada ya kubainika dalili za hatari, wakaguzi wa mgodi walichukua hatua za haraka kuwaondoa mafundi waliokuwa chini ya ardhi pamoja na watu waliokuwa jirani na eneo hilo ambapo wote waliweza kutoka salama.

“Vikosi vya uokozi vilivyohusisha Ofisi ya Mgodi, Ofisi ya Madini, Kikosi cha Uokozi na Zimamoto, Jeshi la Polisi pamoja na vyombo vingine vya usalama vilifika mara moja katika eneo la tukio na kusimamisha shughuli zote za mgodi kwa muda, kuweka utepe wa tahadhari katika eneo lililoathirika na kudhibiti wananchi waliokuwa wakijaribu kusogea katika eneo la hatari,” Imesema sehemu ya taarifa hiyo.

 Imeongeza kuwa shughuli za ukaguzi katika mgodi huo hufanyika kila siku kupitia Ofisi ya Ukaguzi wa Mgodi inayoongozwa na Mkaguzi Mkuu wa Mgodi akisaidiwa na takribani wakaguzi 200 waliopo muda wote katika eneo la mgodi, chini ya usimamizi wa karibu wa Ofisi ya Ofisa Madini Mkazi Mbogwe, Mkaguzi Mkuu wa Migodi Tanzania pamoja na taasisi nyingine za serikali kwa mujibu wa sheria.


Friday, March 27, 2026

MATATANI KWA KUJIFANYA BUBU NA KUTAPELI MTWARA.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, SACP Issa Suleiman.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limemkamata Ibrahimu Nzumbi Mugendi (31), mkazi wa Kijiji cha Makere, Wilaya ya Kasulu, kwa tuhuma za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, mtuhumiwa aliwasili mkoani Mtwara Februari 18, 2026 na kufikia katika nyumba ya kulala wageni (jina limehifadhiwa). Februari 26, 2026 alifika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara kupitia Ofisi ya Katibu Tawala wa Wilaya, ambapo aliomba kibali cha kukusanya michango kutoka kwa watu binafsi na taasisi mbalimbali akidai kuwa ana changamoto ya kuongea (bubu).

Alifanikiwa kupatiwa kibali hicho chenye kumbukumbu namba B58/274/03/123, na kuanza kuzunguka katika taasisi za serikali pamoja na kwa watu binafsi akiomba michango.

Hata hivyo, baada ya uchunguzi wa kina, ilibainika kuwa mtuhumiwa hana tatizo lolote la ulemavu wa kuongea, bali alitumia kigezo hicho kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Mtuhumiwa alikamatwa katika nyumba hiyo ya kulala wageni akiwa na kiasi cha Shilingi 1,800,000 alizokuwa amechangiwa na taasisi pamoja na watu binafsi ndani ya Wilaya ya Mtwara.

Uchunguzi wa awali umeonesha kuwa alifanikiwa kufika katika jumla ya taasisi 10 za serikali na binafsi. Polisi wamesema upelelezi unaendelea, na ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa kwenye vyombo vya sheria kwa hatua zaidi.