VICTOR MASANGU, PWANI
VICTOR MASANGU, PWANI
Polisi wamepata kanda ya CCTV ambayo inaonyesha hatua za mwisho za Afisa Msimamizi wa Uchaguzi wa Embakasi Mashariki Daniel Musyoka, kabla ya kutoweka Alhamisi, Agosti 11.
Zaidi ya saa 48 baada ya Musyoka kuripotiwa kutoweka katika kituo cha kuhesabia kura cha East African School of Aviation (EASA) jijini Nairobi bado hajulikani mahali aliko.
Picha za CCTV kutoka jengo la karibu na kituo hicho zinaonyesha Musyoka, mwenye umri wa miaka 53, akitoka nje siku ambayo aliripotiwa kupotea.
Kulingana na afisa anayefuatilia uchunguzi huo, Musyoka alionekana ametulia alipokuwa akielekea kwenye kituo cha basi kilichokuwa karibu.
"Tumegundua kuwa yeye (Musyoka) hakupiga au kupokea simu wakati alipotoka nje. Uhakiki wetu wa CCTV hauonyeshi mtu yeyote au gari ambalo lingeweza kumfuata mtu huyo," afisa huyo aliambia gazeti la The Standard.
Ripoti za awali zilidai kuwa afisa huyo wa IEBC alijinafasi ili kupokea simu kabla ya kutoweka kwa njia isiyoeleweka.
Uchunguzi zaidi katika akaunti za pesa za simu za Musyoka haukuonyesha jambo lolote la kutiliwa shaka. Kaka yake afisa huyo wa IEBC, Shadrack Musyoka aliambia The Standard kwamba walikuwa wametembelea takriban hospitali zote jijini Nairobi lakini bado hawajampata jamaa wao.
Msako huo pia uliendeshwa hadi kwenye vyumba vya kuhifadhia maiti karibu na jiji la Nairobi lakini haukuzaa matunda.
Binti yake Musyoka, Prudence Mbolu, alisema mara ya mwisho kuzungumza na baba yake ilikuwa Jumanne, Agosti 9, asubuhi ambayo ilikuwa siku ya uchaguzi.
Lakini mazungumzo kati yaoyalikuwa mafupi kwani Musyoka alikuwa akiratibu uchaguzi.
Mke wake naye alieleza kuwa kuwa mumewe ambaye amekuwa akifanya kazi na tume ya uchaguzi tangu 2009, aliondoka nyumbani kwao Nakuru kuelekea Nairobi mnamo Julai 10 baada ya kuhudhuria ibada katika kanisa la AIC Lanet Umoja.
“Nilimpigia simu mnamo Agosti 11 mwendo wa saa nane asubuhi lakini hakupokea simu. Binamu yake ambaye pia anaishi Nairobi alinipigia simu alasiri akiniuliza ikiwa nimezungumza naye. Afisa wa IEBC ambaye alikuwa rafiki yao walimfikia kwa swali sawa,” alisema Tabitha.
Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati alisema kuwa tume hiyo ina hofu kubwa kuhusu tukio hilo la kusikitisha.
Tume hiyo imetoa ripoti katika kituo cha Polisi cha Embakasi kuhusu afisa huyo aliyepotea kwenye daftari la matukio nambari 24/11/8/2022.
Cheukati alisema Musyoka aliondoka nyumbani kwake saa 9.00 alfajiri na kusindikizwa na mlinzi wake hadi ofisini katika kituo cha kujumlisha kura cha East African School of Aviation (EASA) ambako ni mahala pa kuhesabia kura na kujumlisha matokeo ya uchaguzi.
“Afisa huyo aliomba kutoka nje ya chumba cha kuhesabia kura saa 9.45 asubuhi lakini hakurejea afisini,” alisema Chebukati.
TAARIFA ZA KUPATIKANA KWAKE.
Vyombo vya habari
vya Stechitegist vimekusanya kuwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Embakasi Mashariki
aliyetoweka, Daniel Musyoka, alipatikana amekufa kwenye kichaka huko Mariko,
Oloitoktok, Kajiado.
Kifo cha Musyoka
kilitangazwa alfajiri ya Jumanne na mwanablogu maarufu wa Kenya, Robert Alai.
Familia
ilithibitisha kuwa Musyoka alipatikana amefariki katika bustani ya Amboseli,
kaunti ya Kajiado.
Maafisa wa polisi
kutoka Loitoktok, kaunti ndogo ya Kajiado Kusini walithibitisha kupokea arifa
baada ya mwili wa mwanamume wa makamo kupatikana msituni.
Mwili
ulitambuliwa vyema na dada zake; Mary Mwikali na Ann Mboya katika hifadhi ya
maiti ya kaunti ndogo ya Loitokitok.
Afisa wa polisi
wa Loitoktok Kipruto Ruto alithibitisha kuwa familia hiyo iliweza kumtambua
Musyoka na kumaliza msako wa siku 5 wa kumtafuta afisa wa uchaguzi Embakasi
Mashariki aliyetoweka.
Polisi wanaamini
Musyoka aliuawa kwingine na mwili wake kutupwa msituni. Kulingana na maafisa
hao, mwili wake ulikuwa na dalili zinazoonekana za mateso na mapambano lakini
wanasubiri uchunguzi wa maiti.
Uvumi ambao
umekuwa ukienea na kuenea virusi una hivyo
“Daniel Musyoka,
Msimamizi wa Uchaguzi wa IEBC aliyetoweka amepatikana amefariki mahali fulani
Loitoktok.
"Matokeo ya
Embakasi Mashariki yanapaswa kuchunguzwa na kubainishwa ikiwa mbunge
aliyechaguliwa alishinda bila matokeo au kwa vitisho."
“Ni dhahiri kuwa
mwathiriwa aliuawa kwingine na mwili kutupwa bondeni. Mwili una makovu
yanayoashiria kuteswa kabla ya kifo. Huenda alikufa kifo cha uchungu,” Bw Ruto
alisema.
Mwili huo
ulihamishwa hadi katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Kaunti
Ndogo ya Loitokitok ukisubiri kutambuliwa baada ya maafisa wa polisi kukusanya
alama za vidole.
"Tunawasiliana na familia ambazo zimepoteza wapendwa wao ili kuja kutambulishwa tunaposubiri kushughulikiwa kwa alama za vidole," alisema mkuu wa polisi ambaye aliongeza kuwa hawawezi kubashiri juu ya utambulisho wa marehemu.
Kinara wa Azimio Raila Odinga amekataa matokeo ya uchaguzi wa urais yaliyotolewa na mweyekiti wa tume ya uchaguiz nchini IEBC.
Raila alisema uamuzi mzito kama vile kutangazwa kwa kura ni jambo la makamishna wote kuketi na kukubaliana kuhusu litakalotangazwa.
Alizungumzia kesi ya hapo awali ambayo iliwahi kutolewa na mahakama ya Juu kuhusu uamuzi wa IEBC. "Uamuzi wa suala lolote ni lazima liwe la maafisa wote kukubaliana au kwa wingi wa idadi baada ya makamishna kupiga kura," alisema Raila.
Mgombea huyo wa Azimio alisema kutokana na kuwa matokeo ya urais jana yalitolewa na makamishna watatu baada ya wanne kujiondoa, basi hakuna linaloweza kukubalika. "Hatukubali matokeo yaliyotolewa hapo jana.
Na kwa hivyo, tunajua hakuna mshindi aliyetangazwa akiwa amechaguliwa kihalali au Rais Mteule," Raila alisema.
Kiongozi huyo wa Azimio alimkashifu Wafula Chebukati akisema aliendesha shughuli za IEBC kwa njia ya kifua bila kuwahusisha makamishana wengine. "Kama si wafuasi wetu kujizuia kuzua fujo, taifa kwa sasa lingekuwa katika hali baya kama ilivyokuwa 2007.
Hatutakubali mtu mmoja ajaribu kubadilisha yale Wakenya wameamua," alisema Raila huku akiitaka mahakama kubadili kilichotanagzwa na Chebukati.
Kero la kiongozi huyo ni kutokana na mpinzani wake William Ruto kutanagazwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Jumanne Agosti 9.
Ruto alitangazwa mshindi na asilimia 50. 49 ya kura ambazo zilipigwa na hivyo kufikisha vigezo vya kikatiba vinavyohitajika.
Hata hivyo, makamishna wanne walimhepa Chebukati wakisema wao hawawezi kusema wanajua lolote kuhusu matokeo hayo.
Katika kikao na wanahabari Jumanne Agosti 16, naibu mwenyekiti wa IEBC Juliana Cherare, mmoja wa makamishna hao wanne, alisema matokeo ya urais ni ya Chebukati na wala si ya tume ya IEBC.
Na Oscar Assenga,TANGA.
HOSPITALI ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo imepokea msaada wa maabara ya kisasa ya kufanyia uchunguzi wa ugonjwa wa Uviko 19 yenye thamani ya Milioni 225 kutoka kwa Serikali ya Ujerumani kupitia Shirika lake la Maendeleo ya GIZ
Akizungumza mara baada ya kuifungua mara baada ya ukaguzi wa maabara hiyo Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alisema kwamna maabara hiyo ina uwezo wa kutoa majibu ndani ya masaa nane hivyo kuwa mwarobaini wa changamoto zilizokuwepo awali.
Alisema kuwa pia kupitia uwepo wa maabara hiyo utasaidia hata wananchi kutoka nchi jirani ya Kenya ambao wataingia nchini kufanyiwa vipimo kwa haraka na majibu kupatikana kwa wakati.
Alisema uwepo wa maabara hiyo itaondoa changamoto iliyokuwepo ya kusafirtisha sampuli kwenda kwenye maabara nyengine ambapo ilikuwa inasababisha ucheleweshwaji wa majibu na wakati mwengine vipimo vilikuwa vinachelewa.
"Kwa niaba ya serikali tunawashukuru wenzetu wa Ujerumani kwa kutusaidia katika sekta ya Afya kama mnavyofahamu hospitali hii ilijengwa na wajerumani miaka 100 iliyopita lakini bado wanaendelea kutoa fedha nyingi katika kusaidia sekta ya afya nchini ikiwemo hospital yetu ya rufaa ya mkoa wa Tanga Bombo wanatupatia fedha kwaajili ya kuimarisha afya ya uzazi ,mama na mtoto pamoja na mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona "Alisema
Alisema kuzinduliwa kwa kituo hicho cha kupima sampuli za Corona kitasaidia na kuokoa muda kwani awali ilikuwa inawalazimu sampuli zinazochukuliwa hospital Bombo kwenda kupimwa Dar es salaam kwenye maabara ya Taifa na baada ya masaa 48 ndio majibu kupatikana ambapo sasa majibu yatakuwa yanapatikana ndani ya masaa 8 na kuwarahisishia wanaosafiri kwenda nje ya nchi kupata majibu kwa haraka zaidi.
Waziri Ummy alisema pia fedha walizitoa zitatumika kwaajili ya kuimarisha mapambano dhidi ya Uviko -19 na ndio maana katika hospitali ya rufaa ya mkoa Bombo wamefungua kituo cha kupima sampuli za Corona kwa kutumia kipimo hicho.
Awali akizungumza Waziri wa Ushirikiana wa Uchumi na Maendeleo kutok Serikali ya Ujerumani Dkt Barbel Kofler alisema kuwa wakazi wa Tanga pamoja na wageni kutoka nje sasa wataweza kutumia maabara hiyo kwa ajili ya vipimo vya UVIKO.
Alisema wanajisikia furaha kuona kituo hiki cha kupimia sampuli za Covid 19 kinaanza kufanya kazi kwaajili kuimarisha afya ya jamii ya watu wa Tanga na ni muhimu sana kwa serikali ya ujerumani kuendelea kusaidia sekta ya afya katika mapambano dhidi ya magonjwa mbalimbali ya mlipuko.
Alieleza kwa sababu wote hatuko salama muda wowote hivyo wanapaswa kushirikiana kusaidia katika kuimarisha afya ya jamii kwa ujumla kwa Tanzania na ulimwengu mzima pia
Dkt. Kofler alisema mbali na fedha hizo wamesaidia kuwajengea uwezo wataalamu wa afya katika kutoa huduma bora huku wakingia Dolla za kimarekani 15.3 kwaajili ya kusaidia afya ya mama na mtoto na wasichana ili kupambana, kupunguza au kutokomeza kabisa vifo vitokanavyo na uzazi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa maabara kuu ya Taifa ya Afya ya Jamii Medard Beyanga alisema kuwa Serikali inaendelea kuziimarisha maabara zote hapa nchini kwaajili ya kupelekea huduma karibu na wananchi ambapo baadhi ya vituo hapa nchini vimeanza kufunguliwa ikiwemo kilichopo katika hospital ya rufaa mkoa wa Tanga Bombo.
Alisema kwamba hivi sasa wanaendelea na mpango wao wa kuziimarisha maabara za upimaji wa Uviko - 19 na Serikali inafanya jitihada za kuongeza upimaji ili kupeleka huduma karibu na wananchi kuliko kusubiri majibu kutoka Dar es salaam kwenda maabara kuu ya Taifa ,na hii maabara haitakuwa ya kupima Corona bali itapima na magonjwa mengine.
Aidha alieleza pia Serikali ya Ujerumani pia imeendelea kuwa na mchango mkubwa hapa nchini kupitia sekta ya afya ambapo inasaidia kulipia bima ya afya na mtoto inayotambulika kama 'Tumaini la mama', kuchangia mapambano dhidi ya kifua kikuu pamoja na malaria.
“Serikali ya Ujerumani imedhamini miradi ya afya ya Nchini Tanzania kwa gharama ya shilingi dola za kimarekani za zaidi ya shilingi bilioni 7 ikihusisha miradi ya mama na mtoto na Uviko 19”Alisema.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu amempongeza Rais mteule William Ruto kwa ushindi wake katika Uchaguzi Mkuu wa 2022.
Rais Samia Suluhu Ampongeza William Ruto Baada ya Kutangazwa kuwa Rais Mteule. Picha: Samia Suluhu. Chanzo: Twitter Katika taarifa kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii siku ya Jumanne, Agosti 16, Suluhu alimpongeza Ruto kwa ushindi wake na kutangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuwa rais mteule.
Suluhu pia aliwasifu Wakenya kwa kudumisha amani wakati wa mchakat mzima wa uchaguzi na kuahidi kuendelea kufanya kazi na Kenya. "Ninapenda kuwapongeza kwa dhati wananchi wa Kenya kwa kushiriki uchaguzi wao mkuu kwa amani na utulivu, ambapo matokeo yake ni Dkt William Ruto kutangazwa kuwa Rais mteule wa Kenya.
Tanzania itaendeleza undugu na ushirikiano wa Kihistoria na Kenya uliodumu miaka na mikaka," alisema.
Suluhu pia aliahidi kuendelea kufanya kazi na Kenya ili kueneza uhusiano wao kidiplomasia. Rais huyo alibainisha kuwa Kenya na Tanzania zina uhusiano wa kihistoria kama majirani, akiongeza kuwa mataifa hayo mawili yameungana.
Ruto apokea kongole kote duniani Baada ya kutangazwa rais mteule, William Ruto amekuwa akipokea jumbe za kongole kutoka kwa viongozi tofauti ulimwenguni.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa alisema anaamini kuwa Ruto atahudumia Wakenya bila upendeleo.
Rais mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mohamed alisema anatazamia kufanya kazi na Ruto katika kuendeleza maslahi ya pande zote mbili za Nairobi na Mogadishu.
Ubalozi wa Marekani ulitaja kuchaguliwa kwa Ruto kuwa rais wa tano kama hatua muhimu huku ukizitaka pande ambazo hazijaridhika na matokeo kupinga matokeo hayo kupitia mifumo iliyopo ya kutatua mizozo. Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed alimtakia kila la heri Ruto akiahidi kufanya kazi naye kwa karibu ili kuboresha uhusiano baina ya nchi hizo mbili.
PIA SOMA Magazetini Agosti 16: William Ruto Alizungumza na Raila Kabla ya Kutangazwa Rais Mteule Katika salamu zake za pongezi, rais wa Nigeria Muhammadu Buhari alisema anatazamia uhusiano thabiti kati ya Nigeria na Kenya.
Mwenyekiti wa kamati ya Sensa Wilaya ya Iringa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na Makarani, Maudhui na watu wa Tehama wa Sensa ya watu Makazi wilayani humo kutanguliza uzalendo katika utekelezaji wa zoezi la SENSA la kitaifa.
Na Fredy
Mgunda,Iringa.
Mwenyekiti wa kamati ya Sensa Wilaya ya Iringa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo amewataka Makarani, Maudhui na watu wa Tehama wa Sensa ya watu Makazi wilayani humo kutanguliza uzalendo katika utekelezaji wa zoezi la SENSA la kitaifa ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo iliyoyakusudia ya kuwahesabu watu kama ambavyo inatakiwa kuwa Mwaka huu.
Akizungumza na Makarani, Maudhui na watu wa Tehama wa Sensa wanaoendelea na mafunzo katika Manispaa ya Iringa Moyo alisema kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi ili kufanikisha zoezi hilo muhumu litakalosaidia upangaji wa bajeti sahihi ili kuiwezesha kufikisha huduma za msingi katika Kila Kona ya nchi hivyo ni muhumu watu waliopewa dhamana ya kutekeleza zoezi hilo wakalitekeleza kikamilifu na kwa weledi wa hali ya juu.
Moyo aliwataka wahusika wa zoezi la Sensa kuhakikisha wanatunza Siri za taarifa za watu watakaowahesabu ikiwa ni pamoja na utunzaji wa vitendea walivyopatiwa na Serikali katika kutekeleza zoezi Hilo.
Alisema kuwa mhusika yeyeto yule wa zoezi la Sensa atakayepoteva au kuvuruga zoezi la Sensa serikali itamchulia hatua kali za kisheria kwa mujibu wa sheria za nchi,hivyo kila mhusika anatakiwa kuwa makini na zoezi hilo la kitaifa kwa manufaa ya nchi ya Tanzania.
Aidha Mohamed Moyo amewaonya Makarani hao pamoja na Watu Wote watakaobainika kuzembea katika utekelezaji wa jukumu walivyopatiwa na Serikali ikiwemo watu Wote wanakajihusisha na uhujumu Kwa lengo la kukwamisha shughuli za Sensa itakayifanyika Rasmi Agosti 23 mwaa huu.
Akifafanua zaidi amewataka Wananchi kuwa Tayari kwani kuanza Tarehe 21 Hadi 22 Agosti Mwaka huu Karani wa Sensa akiongozwa na kiongozi wa eneo husika atafika kwenye eneo alilopangiwa kujitambulisha na kutambua mipaka ya eneo lake hivyo Kila Mwananchi awe Tayari kutoa ushirikiano Ili kufanikisha zoezi Hilo.
Moyo alimazia kwa
kuwaomba wananchi wa wilaya ya Iringa kuhakikisha wanahamasishana kujitokeza
kuhesabiwa siku ya zoezi la Sensa kwa ajili ya manufaa yao na serikali kujua
namna gani ya kupanga bajeti ya eneo husiku kupitia SENSA hiyo ya mwaka huu.
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na wananchi wa kijiji cha Saadan Kuwa Mwenge wa Uhuru Unaweza Kwenda Kuweka Jiwe la Msingi Katika ujenzi wa Bwawa Hilo
Na Fredy Mgunda,Iringa.
MKUU wa wilaya ya Iringa Mohamed
Hassan Moyo amesema kuwa mwenge wa Uhuru utaweka jiwe la msingi katika mradi wa
ujenzi wa bwawa la kuhifadhia maji ya mvua katika Kijiji cha Sadan kata ya
Masaka unaosimamiwa na uongozi wa Bonde la Rufiji.
Akizungumza wakati wa ziara ya
waziri wa maji Juma Aweso alisema kuwa mradi huo wa ujenzi wa bwawa la
kuhifadhia maji ya mvua ni mradi mkubwa na ambao unasimamiwa kwa ubora
unatakiwa hivyo anaenda kuitarifu kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya
Iringa ili kufanikisha mwenge wa Uhuru utaweka jiwe la msingi.
Moyo alisema kuwa serikali ya
awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kupitia wizara ya maji imetoa fedha nyingi
katika mradi huo hivyo unapaswa kupewa hadhi ya kitaifa kwa kuwa unaenda
kutatua changamoto za wananchi wa kata ya Masaka na kata nyingine za jirani.
Akiwa katika ziara wilaya ya
Iringa waziri waji Juma Aweso ameupongeza uongozi wa wilaya ya Iringa kwa
kusimamia vizuri ujenzi wa bwawa la kuhifadhia maji ya mvua katika bodi ya maji
Bonde la Rufiji kwa kuwa litafanikisha kuleta maendeleo kwa wananchi na kutatua
changamoto ya maji kwa wananchi wa kata ya Masaka.
Aweso alisema kuwa ameridhishwa
na ujenzi wa mradi wa bwawa la kuhifadhia maji ya mvua katika Kijiji cha Sadan
kwa kuwa mmoja ya miradi mingi mikubwa ambayo itakuja kuwa na matokeo ya moja
kwa moja kwa wananchi wanaolizunguka bwawa hilo.
Aweso alisema kuwa serikali ya
awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imeiagiza wizara ya maji kuhakikisha inachimba
mabwawa ya kila wilaya ili kutatua changamoto hiyo na kuongeza njia za kukuza
uchumi wa maeneo husika.
Alisema kuwa kukamilika kwa bwawa
hilo kutaisaidia kuleta maendeleo ya miradi mingine ya maji kutokana na
usimamizi mzuri ambao unafanywa na uongozi wa wilaya na mkoa kwa ujumla kwenye
maendeleo ya miradi ya kijamii.
Alisema mradi huo wa ujenzi wa
bwawa la kuhifadhia maji ya mvua utagharimu kiasi kikubwa cha fedha ambacho ni
900,982,000/= ambazo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amezileta
kutatua changamoto hizo kwa wananchi wa kata ya Masaka.
Aweso alisema kuwa wizara ya maji
musimu huu wa kiangazi inajenga mabwawa kumi (10)ambapo mabwawa manne
(4)yanajengwa katika wilaya ya chemba,mawili wilaya ya Bahi,wawili wilaya ya
Chamwino na wilaya ya Iringa mabwawa mawili na wizara inafanya usanifu wa
mabwawa 51 ambayo yanatarajiwa kujengwa katika mwaka ujao wa fedha
Awali akisoma taarifa ya mradi
kwa waziri,msimamizi wa mradi huo Eng Geofrey Simkonda alisema kuwa mradi wa
ujenzi wa bwawa la kuhifadhia maji ya mvua ni mkakati wa
uendelezaji,utumiaji,uhifadhi na usimamizi wa vyanzo vya maji katika Bonde la
Rufiji.
Alisema kuwa lengo la ujenzi wa
mradi huo wa ujenzi wa bwawa la kuhifadhia maji ya mvua ni kuvunia maji na
kurahisiha upatikanaji wa maji kwa wananchi hususani wenye uhaba wa rasilimali
za maji kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya kibinadamu.
Eng Simkonda alisema kuwa
wananchi wa wilaya ya Iringa,kata ya Masaka inayojumuisha Vijiji vya Makota,
Sadan na Kaning'ombe watanufaika na mradi huo.
Alisema kuwa bwawa la kuhifadhia
maji ya mvua la Masaka lina kimo cha mita 14,urefu mita 260 na litakuwa na
ujazo wa mita 439,803 na ujenzi unatarajiwa kukamilika mwezi wa tisa mwaka 2022
hadi sasa mradi umefikia asilimia 50.
Azma ya mgombea wa Azimio la Umoja One Kenya Alliance Raila Odinga kufika Ikulu ya kwa mara nyingine tena imegonga mwamba.
Raila alibwagwa na mpinzani wake mkuu wa kisiasa wa Muungano wa Kenya Kwanza William Ruto katika uchaguzi wa urais uliokuwa na ushindani mkubwa uliofanyika Jumanne, Agosti 9.
Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Wafula Chebukati, Ruto alipata kura 7,176,141 ikiwa ni asilimia 50.49 ya kura zote zilizojumlishwa za kutangazwa mshindi. Waziri Mkuu huyo wa zamani aliibuka wa pili kwa kura 6,942,930 akiwakilisha 48% ya kura zote zilizojumlishwa.
Hili ilikuwa ni mara ya tano kwa kiongozi huyo wa ODM kupigania kiti hicho cha urais bila kufaulu.
Saitabao Ole Kanchory alisema kuwa Raila hatajitokeza hadi timu yake ihakikishe matokeo rasmi ya uchaguzi ni rasmi.
"Tumepata ripoti za kijasusi kwamba mfumo wao ulidukuliwa na kwamba baadhi ya maafisa wa IEBC walitenda makosa ya uchaguzi na baadhi yao walifaa kukamatwa mara moja," akasema.
Mgombea urais wa Muungano wa Kenya Kwanza William Ruto amewasili Bomas of Kenya kabla ya kutangazwa kwa matokeo ya urais.
Naibu rais aliandamana na mkewe Rachel Ruto, mgombea mwenza Rigathi Gachagua miongoni mwa wanasiasa washirika wa Kenya Kwanza. Tume ya Uhuru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ilisema kuwa itatangaza rasmi matokeo ya urais leo, Jumatatu, Agosti 15, saa tatu usiku.
Hii ni baada ya kuthibitishwa kwa kina na kujumlisha kura katika ukumbi wa Bomas of Kenya ulioanza Jumanne, Agosti 9 Wakenya walipopiga kura.
Mgombea urais wa chama cha Roots George Wajackoyah na mgombea mwenza wa urais wa chama cha Agano David Mwaure walifika katika ukumbi huo mapema mchana.
Kwa sasa, Wakenya ni wajawazito huku wakisubiri mwenyekiti wa IEBC na msimamizi wa uchaguzi wa taifa Wafula Chebukati kumtangaza rais mteule katika ukumbi wa Bomas of Kenya.