Baraza Kuu la Waislam Mkoa wa Mwanza limetangaza kuwa Swala ya Eid itafanyika kimkoa katika Uwanja wa Nyamagana uliopo Wilaya ya Nyamagana, Mkoa wa Mwanza.
Katika taarifa hiyo, Waislam wote mkoani Mwanza wanaombwa kuhudhuria swala hilo kwa pamoja ili kushiriki ibada hiyo muhimu ya sikukuu.
Baraza hilo limehimiza umoja, mshikamano na nidhamu wakati wa ibada hiyo, pamoja na kuzingatia maelekezo yatakayotolewa na viongozi wa dini na mamlaka husika.
Tupe maoni yako

0 comments:
Post a Comment