Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza , Amir Mkalipa, amevitaka vikundi vilivyopata mikopo ya asilimia 10 katika wilaya hiyo kuhakikisha vinarejesha fedha hizo kwa wakati ili kutoa fursa kwa vikundi vingine kunufaika na mpango huo.
Akizungumza hii leo wakati wa hafla ya utoaji wa mikopo hiyo iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Mkalipa amesema kuwa halmashauri itafuatilia kwa karibu vikundi vyote vilivyopata mikopo ili kuhakikisha vinarejesha kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa.
Aidha, Mkalipa amewataka maafisa maendeleo wa kata kutoa elimu mara kwa mara kwa vikundi hivyo pamoja na kuvitembelea ili kubaini mapema vikundi vinavyosuasua katika marejesho, na kuchukua hatua stahiki kwa wakati.
Kwa upande wake, Meya wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela, Bi. Salah Ngw'ani, ameishukuru halmashauri hiyo kwa utoaji wa mikopo hiyo, akisema kuwa itakuwa chachu ya maendeleo kwa wakazi wa wilaya hiyo.
Jumla ya vikundi 41 vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu katika wilaya ya ilemela vimenufaika na mikopo hiyo ya alimia 10 yenye thamani ya shilingi milioni 463.
Tupe maoni yako
.jpeg)



0 comments:
Post a Comment