ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 19, 2014

KARIBU CLUB JEMBE NI ZAIDI YA UTALII MWANZA

Samaki fresh toka ziwa Victoria wakuchoma, wakubanika, wakukaanga, na vyakula vya kila aina lipate jibu ndani  ya kiota kipya cha kitalii cha gharama nafuu mpaka ushangae Jembe ni Jembe aka Skylight Beach Resort Malimbe Mwanza.
Ni muda wa kupiga picha na samaki.
"This is Jembe Club" says Peter Fabian.
Crew ya vijana wa mjini ikiongozwa na mkurugenzi wa Lakairo Investment Co.Ltd Danny Lameck (kulia) ishatia timu hapa.
G akipata bupepo.....
'Represent'
Bustanini....na kaunta yenye full service.
Kama una karanga njoo kuna jiwe la kale la kusagia.
You see?
Jembe ni Jembe. 
On the top.
Vimiminwa vya kila aina.
Nyakati za usiku huu ndiyo muonekano.
Kama ni kuwochi football au matukio mbalimbali basi kaunta kuna bo-bo-booooonge la skrini!!!!!
Kwa mbaaali utaona......
Engo nyingine adimu....
Wenye boti zao kuna shortcut kutoka Malimbe Nyegezi hadi Mwanza town ni mwendo wa dakika 15 tu amini usiamini.
Kwa heriiiii....
Waleeeeeeee!!!!!
Matukio mawili makubwa kufanyika:-
JUMAMOSI :- Tarehe 19 April 2014 Fool Moon Party wasanii Joh Makini, Nikki wa Pili, G. Nako wanaounda kundi la Weusi kukisanukisha na yule mkali mwingine anayetamba na ngoma inayoitwa Kerewa namzugumzia Sheta, kiingilio ni shilingi 10,000/= tu!!

JUMAPILI :-Tarehe 20 April 2014 Easter Bonanza tutakuwa na Skylight Band, mchana watoto sh 3,000/=  wakubwa sh 10,000/= kisha badae usiku tena tukiwa na Skylight Band Part la Nguvu tu kiingilio sh 10,000/=.
nANI aTABaki hOmU?   

Friday, April 18, 2014

ULINZI WAIMARISHWA SIKUKUU YA PASAKA MWANZA.

KAMANDA wa Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza Valentino Mlowola akizungumza na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari jijini hapa (hawapo pichani), kuelezea jinsi jeshi lake lilivyo jipanga kuhakikisha suala la ulinzi na usalama linazingatiwa na kuimarishwa katika kipindi chote cha sherehe za sikukuu ya Pasaka mkoa wa Mwanza.

Pia Kamanda Mlowola alitumia fursa hiyo kuwaasa wananchi kwa kutoa ushirikiano. (BOFYA PLAY KUMSIKILIZA)

Thursday, April 17, 2014

UMESHAWAHI KULIWA KARATA TATU?

 Siku moja nilisimama hapo kwa interest ya kujua kinachoendelea nikajagundua ni wizi mtupu na ushirikina pia kwani muda wote ni udi ubani,baadaye nikatoka pembeni nikauliza vijana wauza karanga hapo njiani nikawaambia mbona Kama kinachofanyika hapo ni wizi? wakaniambia ndo hivyo tunashangaa hata we ulikuwa umeingia mkenge,kwa Hali hiyo ni kwamba jamii inajua kinachoendelea hapo ni wizi kulikoni jeshi letu la polisi wenye jukumu la kulinda usalama wa raia na mali zao?
Hali tete kwa washirika!!
"Twende mbere" sauti zilisikika. Picha na 
Chigiro Jchigiro

FAN CITY YAJIPANGA KUTOA BURUDANI YA KIPEKEE KWA WATANZANIA PASAKA

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Green Stars Industry inayomiliki eneo la FAN CITY Bw. Hasan Rizvi akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani) mashine za michezo mbali mbali itakayotolewa kipindi cha sikukuu ya Pasaka wakati wa mkutano alioufanya katika eneo la Fun City Kigamboni jijini Dar es Salaam. Pia aliongeza kuwa kwa sasa kampuni yake imeeongeza mitambo yenye uwezo wa kutengeneza mawimbi ya aina sita tofauti kwenye bwawa kubwa la kuogelea.
Mitambo ya kisasa iliyofungwa katika eneo la Fun City ambayo itawawezesha wananchi kupata burudani kabambe zenye ubora wa kimataifa kwani hakuna mahali popote Afrika Mashariki mitambo hiyo.
Mawimbi yanayotengenezwa kwa mitambo ya kisasa katika bwawa kubwa la kuogelea lililopo hapa Fun City,
Moja ya Bwawa la kuongelea.
Mkurugenzi Mtendaji wa Fan City, Bw. Hasan Rizvi  akionyesha vigari vya mchezo.
Bembea za kutosha.
Bembea za watoto.
Mapokezi ya Fun City.
Eneo la Fun City linasehemu ya Ibada. 
 Sehemu ya huduma ya kwanza nayo inapatikana hapa.
Sehemu ya moja ya sehemu ya bembea za magari ikiongesha madhari nzuri za kiota cha burudani cha Fun City.
Vigari vya umeme vinavyopita ndani ya maji.
*YAFUNGA MITAMBO YA KISASA KWA AJILI YA MICHEZO YA KWENYE MAJI
Na Mwandishi Wetu, Dares salaam
Wakati Watanzania wakiwa kwenye maandalizi ya sikukuu ya Pasaka kampuni ya Green Stars Industry inayomiliki eneo la FAN CITY limeongeza mitambo yenye uwezo wa kutengeneza mawimbi ya aina sita tofauti kwenye bwawa kubwa la kuogelea.

Mtambo huo wa aina yake utaongeza hamasa kwa waogeleaji kuhisi kama wapo baharini.
Akizungumzia mtambo huo Mkurugenzi Mtendaji wa Fan City, Bw. Hasan Rizvi amesema, lengo la kuoberesha michezo hiyo ni kuwawezesha watanzania kufurahia michezo hiyo pamoja na familia zao wakati huu wa Pasaka.

Ameongeza kuwa mitambo ya kisasa iliyofungwa katika eneo lake itawawezesha wananchi kupata burudani kabambe yenye ubora wa kimataifa kwani hakuna mahali popote Afrika Mashariki mitambo hiyo inapatikana.

“Tumefunga mtambo huu ambao utakua ukitengeneza mawimbi ya aina sita tofauti kwenye bwawa kubwa la kuogelea lililopo hapa Fan City, lengo letu nikutoa burudani zaidi kwa watu wanaotembelea hapa”.Alisema Rizvi.

“Tumefanya uwekezaji wa mashine za kisasa za michezo mbalimbali kwenye eneo letu ili kutoa burudani nzuri na za kipekee kwa wananchi wanaotembelea eneo hili na hasa wakati huu wa Pasaka”. Alisisitiza Rizvi. Fan City iliyopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Fun City imekuwa ikitoa burudani safi ya michezo mbalimbali kwa familia na katika kipindi hiki cha Pasaka imeandaa michezo kama Sarakasi, Mazingaombwe na zawadi kemkem kwa watakaotembelea eneo hilo. Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog