ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, March 23, 2013

MAANDAMANO YA KUMTAKA WAZIRI WA ELIMU AJIUZURU JESHI LA POLISI MWANZA LAIPIGA STOP CHADEMA.

Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza limepiga marufuku maandamano ya CHADEMA yaliyopangwa kufanyika siku ya jumatatu kumshinikiza Waziri wa Elimu ajiuzuru kufuatia matokeo mabaya ya kidato cha nne kwa mwaka 2012.

Akitoa taarifa leo asubuhi katika ofisi za jeshi hilo mkoani Mwanza Kamanda wa polisi mkoa Ernest Mangu amesema kuwa jeshi lake limeyazuia maandamano hayo kwa sababu za kimsingi za usalama. (Bofya play kumsikiliza)

Akizitaja sababu hizo kamanda Mangu amesema kuwa suala la matokeo ya kidato cha nne kuwa mabaya serikali tayari imeliundia tume ambayo bado inaendelea kukusanya maoni kwa wananchi hivyo haoni sababu za CHADEMA kufanya maandamano na kuwataka viongozi wake kuwasilisha hoja zao wanazodai kuwa za msingi kwenye tume husika na si kufanya maandamano yanayoweza kupelekea uvunjifu wa amani. 

Kwa mkoa wa Mwanza CHADEMA ilitoa taarifa za kufanya maandamano katika wilaya za Sengerema, Misungwi na Magu.

Mangu ameongeza kuwa jumatatu ni moja kati ya siku za kazi na shughuli mbalimbali za biashara hivyo kufanya maandamano kwenye viunga mahali kokote ni chanzo cha kuzuia shughuli za uzalishaji na biashara kufanyika kwa ufanisi kwani wadau watafunga shughuli zao wakihofia uporaji na usalama wa mali zao.

Tayari jeshi la polisi Mwanza limepokea taarifa ya makundi mbalimbali kuibuka na kudai kuyapinga maandamano hayo wakiwemo wafanyabiashara walioko katikati ya jiji wakisema kuwa yatasababisha huduma zao kusimama.

FREDERICK LAWSON KIBOKO YAKE SOWAH


Lile pambanolililokuwa linasubiriwana mashabiki wengi wa ngumi katika jiji la Accra nchini Ghana kati ya bondia kijana anayechipukia Frederick Lawson na mkongwe Isaac Sowah limemalizika muda wa sekunde ya 43 katika raundi ya tatu baada ya referii Shedrack Aquaye kuingilia kati kumwokoa Isaac Sowah asiendelee kupokea mkong’oto kutoka kwa kijana Frederick Lawson.

Wawili hao walikutana kwenye uwanja wa mpira wa Accra katika mpambano ambalo ulirushwa live na Super Sport pamoja na mitandao ya televisheni nyingi duniani. Mpambano mkubwa usiku wa leo ulimshughudia mbabe Joseph Agbeko wa Ghana akimshinda kwa taabu na kuchukua ubingwa wa dunia dhidi ya bondia kutoka nchini Columbia Luis Melendez.

Kwa sasa bondia Frederick Lawson anangojea mapambano mengine ya kuinua kipaji chake na anga ndiyyo tu itakuwa kilele chake katika juhudi zake za kuchanja mbuga kwenye ngumi!

Pambano la wawili hao lilisimamiwa na Rais wa IBF katika bara la Africa, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi ambaye yuko katika jiji la Accra akitokea Windhoek, Namibia!

INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA

KANUNI MPYA ZA MAHAKAMA YA BIASHARA ZATAZAMIWA KUSAIDIA KUPUNGUZA MLUNDIKANO WA KESI


Mgeni rasmi Aishiel Nelson Sumari ambaye ni Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Mwanza akisoma maelezo ya ufunguzi wa semina ya Uhamasishaji kanuni mpya za Mahakama ya Biashara mkoani Mwanza iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya jiji la Mwanza.

Washiriki wa semina hiyo wakisikiliza kinachojiri.
Sheria hizo mpya zimekuja ili kuleta Ufanisi kwa jamii kwa kuharakisha kesi zilizo na migogoro ya kibiashara kwa kuokoa muda na jamii iweze kuendelea na shughuli nyingine za uzalishaji badala ya kushinda mahakamani kuzungushana na mashauri. 
Costantine Mutalemwa wakili wa kujitegemea akitoa mwongozo katika mada mbalimbali zilizowasilishwa kwenye semina ya Uhamasishaji kanuni mpya za Mahakama ya Biashara mkoani Mwanza iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya jiji la Mwanza
Kwa sasa ndani ya kanuni hizo mpya za uendeshaji mashauri ya kesi za madai yenye sura za kibiashara masuala ya kuahirisha kesi bila sababu za msingi hayatopewa nafasi kwani mahakimu watapaswa kulipia gharama za kuahirisha kesi wanapokuwa na sababu zao binafsi.
Washiriki wa semina hiyo pamoja na wawezeshaji wakisikiliza kinachojiri.
Changamoto ya kulazimika kuwa na vitendea kazi vya kiteknolojia kwa uchambuzi wa sheria na kuwasiliana na wateja wenye kesi imeibuka ndani ya semina hiyo kwani mawakili wanapokwenda kwenye kesi mahakama ya biashara watapaswa kuzifahamu vyema kesi zao wanazowakilisha na kuwa tayari kujibu maswali ya kesi husika iwapo mahakama itahitaji ufafanuzi.
Washiriki wa semina hiyo wakisikiliza kinachojiri.


Sehemu nyingine ya washiriki waliohudhuria semina ya Uhamasishaji kanuni mpya za Mahakama ya Biashara mkoani Mwanza iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya jiji la Mwanza.


Washiriki waliohudhuria semina ya Uhamasishaji kanuni mpya za Mahakama ya Biashara mkoani Mwanza iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya jiji la Mwanza wakipiga makofi kuashiria kuafiki moja kati ya mada za wawasilishaji wao.


Katika utangulizi Naibu msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania John Kahyoza  amesema kuwa lengo la mabadiliko hayo ya sheria za maamuzi mahakama ya biashara ni kuokoa muda wa jamii kwa kuhakikisha kesi zinamalizika kwa kipindi kifupi kuanzia mwezi mmoja hadi miezi 10, katika hilo muda huo ukipita na kama hakuna nyongeza inayokubalika kesi itatupwa.


Kwa umakiiii washiriki wa semina hiyo wakisikiliza kinachojiri.




Sikiliza mahojiano yangu na Mwanasheria......>
Jiografia ya kusanyiko la semina ya Uhamasishaji kanuni mpya za Mahakama ya Biashara mkoani Mwanza iliyofanyika leo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya jiji la Mwanza.

Friday, March 22, 2013

CHINUA ACHEBE AFARIKI DUNIA



Mwandishi Maarufu wa vitabu duniani Chinua Achebe amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 82.
Msemaji wa jimbo la Anambra nchini Nigeria Mike Uda ameiambia BBC kuwa wanaomboleza kifo cha wanayemwita mtoto wa taifa la Nigeria na Afrika kwa ujumla.
Chinua Achebe alizaliwa mwaka 1930, miaka 30 kabla ya Nigeria kupata uhuru.
Taarifa iliyotolewa kwa niaba ya familia yake, imemwelezea Chinua Achebe kuwa mmoja wa waandishi wakubwa wa vitabu vya fasihi katika kipindi chake, ambaye busara yake ilikuwa kichocheo cha kumwiga kwa wale wote waliomfahamu.
Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amesema Profesa Achebe ataishi daima katika mioyo ya akili za watu wa kizazi kiliochopo na vijavyo. Alipata umaarufu mkubwa kutokana na utunzi wa kitabu chake cha kwanza cha fasihi kitwaacho 'Things Fall Apart', ambacho alikitunga mwaka 1958 kikizungumzia athari za ukoloni barani Afrika.
Kitabu hiki kiliuza zaidi ya nakala milioni 10. Things Fall Apart kimetafsiriwa katika zaidi ya lugha 50 na kuelekeza mtazamo wake katika jamii ya Wa-Igbo na mgongano wa kimaadili kati ya nchi za mgaharibi na kijadi.
Alipata ngazi ya uprofesa kutoka chuo kikuu cha Boston nchini Marekani mwaka 1970 ambapo katika siku za hivi karibuni alikuwa akikosoa baadhi ya mienendo mibaya ya serikali ya Nigeria.
Amekuwa akiishi nchini Marekani tangu mwaka 1990 kufuatia kujeruhiwa katika ajali ya gari.
Ameandika kazi za kitaaluma zaidi ya 20, baadhi zikikosoa vikali wanasiasa na uongozi mbaya nchini Nigeria.
Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan amesema Profesa Achebe ataishi daima katika mioyo na akili za watu wa kizazi kiliochopo na vijavyo.
CHANZO: BBC SWA.

PAA JUU KWA JUU.

Kulia ni barabara ya Nyerere na kushoto ni barabara ya Rwagasore zikikutana kuelekea barabara ya kelekea Shinyanga.

Tambarare na kilimani.
Shesheni ya Mwanza.

Hoteli ndani ya Ziwa Victoria.

Vikwangua anga vya kale na vya sasa.

Pale katikati ndiko kiwanja cha Sahara aka Kiwanja cha vita vya majukwaa ya siasa.

AIRTEL YAZINDUA GHARAMA NAFUU ZA KUPIGA SIMU MITANDAO MINGINE.




Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano Mallya akiongea wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel Yatosha inayomwenzesha mteja wa Airtel kupata kifurushi cha maongezi, sms na internet na kuwasiliana na mitandao yoyote nchini, huduma hii imebeba ujumbe wa simkadi moja, taifa moja, bei moja.

Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akielezea huduma mpya ya Airtel yatosha yaani Simu kadi moja, taifa moja, bei moja inayomwezeshamteja wa Airtel kuwasiliana na mitandao yoyote nchi na kupata kifurushi cha muda wa maongezi, sms, na internet kwa bei nafuu hadi shiling 349/= pichani (katikati) ni Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Bi, Beatrice Singano Mallya akifatiwa na Meneja masoko Airtel Anethy Muga.




Airtel yazindua gharama nafuu zakupiga simu mitandao mingine
*         Airtel yadhihirisha simu kadi moja, taifa moja, bei moja - Wateja nchini kufaidika na kiwango cha chini cha hadi 75% kupiga simu popote bila kikomo

*          Piga simu muda wowote usiku and mchana

Dar Es Salaam  Jumatano 20 Marchi 2012.  Airtel Tanzania leo imezindua huduma mpya ijulikanayo kama "AIRTEL YATOSHA" itakayowawezesha wateja wake  nchi nzima kupiga simu kwenda mtandao wowote kwa kiwango nafuu cha hadi asilimia 75 bila kuwa na  sababu kubadili simu laini kwa kuhofia gharama.

Huduma ya AIRTEL YATOSHA inadhihirisha simu kadi moja, taifa moja, bei moja  inayoendeleza dhamira ya Airtel ya kutoa huduma bora na nafuu ambapo wateja wa Airtel sasa watapata ofa ya kifurushi kitakacho wapa muda wa maongezi, ujumbe mfupi na kifurushi cha internet ambacho kinaweza kutumika kwa siku au kwa wiki kulingana na mahitaji ya wateja

Akiongea wakati wa hafla maalum ya uzinduzi wa huduma hiyo iliofanyika katika makao makuu ya Airtel Tanzania, Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Bw Sunil Colaso Alisema"  Huduma ya Airtel YATOSHA ni maalum kwa kila mtanzania, hii itawarahisishia watanzania wote kupata mawasilino nafuu kwa kupiga bila kikomo kwenda mitandao mingine nchini. 

Kupitia kifurushi cha Airtel YATOSHA wateja wa Airtel watafurahia kiwango cha chini cha hadi shilingi 349/=, hii inamaana kwamba  mteja atapata dakika 10 za kupiga simu kwenda mtandao wowote muda wowote, pia SMS 100 (ujumbe mfupi wa maneno) pamoja na kifurushi cha intenet cha 25MB ofa itakayotumika masaa 24 kwa siku

Faida za AIRTEL YATOSHA kwa mteja zinadhihirisha dhamira yetu Airtel ya kutoa huduma za mawasiliano bora na nafuu nchini. Airtel tunazingatia kuwa wateja wetu wanamahitaji tofauti na ndio sababu kubwa inayotufanya tuwe wabunifu kwa kuwapatia huduma zinazogusa kila
aina ya wateja na kuleta mabadiliko halisi kwa kuwapa wateja wetu nchi nzima thamani ya pesa zao

Kwa Upande wake  Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel  Bi,i Beatrice Singano Mallya alisema " Airtel YATOSHA  ni huduma inayopatikana kwa SIKU au kwa WIKI hivyo mteja anapewa nafasi ya kuchagua anachokata.
Katika mpango wa WIKI mteja atatozwa shilingi 1,999  na kupata dakika 70, sms 700 na kifurushi cha interneti cha 175MB.

Kujiunga na huduma hii mteja anatakia kupiga *149*99#  na kuunganisha moja kwa moja kwenye orodha ya huduma hii na kuchangua kifurushi anachokipenda na kuweza kujipatia dakika za maongezi, ujumbe mfupi na kifurushi cha internet.  Dakika za maongezi zitatumika kupiga simu kwenda mtando wowote nchini kwa massa 24 na gharama za kupiga simu
zitatozwa kwa sekunde.

Kuhusu muda wa kujiunga na Airtel YATOSHA mteja anaweza kujiunga wakati wowote  kati ya 0500hrs to 2359hrs,

Airtel Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma zenye ubora na ubunifu nchini. Na hii ni njia nyingine ya kudhihirisha jinsi Airtel inavyotoa huduma za mawasiliano yenye ubora na gharama za ushindani kwa watanzania. Airtel itaendelea kuwa chachu ya maendeleo
kwa kutoa huduma  bora zenye gharama nafuu.

MWAUWASA YAZIDAI TAASISI ZA SERIKALI JUMLA YA SHILINGI MILIONI 420: HAYO YABAINIKA KILELE CHA WIKI YA MAJI MWANZA

Diwani wa kata ya Nyamagana Bhiku Kotecha akisoma hotuba kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Maji.
Mamlaka ya maji safi na maji taka jijini Mwanza MWAUWASA inadai Taasisi za Serikali ankara za maji jumla ya Tshs Milioni 420.

Hayo yamethibitishwa leo katika hotuba ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza iliyosomwa kwa niaba yake na Diwani wa Kata ya Nyamagana Bhiku Kotecha wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha wiki ya maji yaliyofanyika viwanja vya Ghand Hall jijini Mwanza.

Amesema kuwa Mamlaka hiyo haiwezi kutekeleza wajibu wake wa kusambaza majisafi na kuondoa majitaka kwa wananchi wapatao 700,000 wa jiji la Mwanza wanaofikiwa na mtandao kama limbikizo la deni hilo na Ankara za kila mwezi havitalipwa kwa wakati muafaka.
Mkurugrnzi wa Mamlaka ya maji safi na maji taka mkoa wa Mwanza (MWAUASA) Eng. Anthony Sanga akihutubia umati wa watu waliofurika viwanja vya Ghand hall hii leo.
Mamlaka imefanikiwa kuhudumia shughuli za uondoaji wa majitaka kwa zaidi ya asilimia 15 katika maeneo ya jiji la Mwanza. MWAUWASA inaendelea kuongeza mtandao wa majisafi katika maeneo ambayo hayajafikiwa kwa wastani wa kilomita 15 kila mwaka kulingana na uwezo wa ndani.

Mahitaji ya kuongeza mtandao wa majisafi katika mji wa Mwanza unaokuwa kwa kasi yanakadiriwa kufikia kilomita 300 kwa gharama ya Tshs. Bilioni 5 kwa ajili ya mabomba, viungio na vituo vya kuongeza msukumo wa maji (Booster stations)
Mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Maji safi na maji taka jijini Mwanza MWAUWASA Mama Lopa akitoa changamoto zinazoikabili Malaka hiyo.
Pamoja na changamoto alizozitaja, Mamlaka imetoa shukurani za dhati kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujenga mradi mkubwa wa Majisafi na Majitaka jijini mwanza kuanzia mwaka 2008 hadi 2011.
Wadau mbalimbali pamoja na wafanyakazi wa Mamlaka ya maji Kusanyikoni.
European investiment Bank (EIB) pamoja na French Development Agency (AFD) ambao kwa pamoja wamekubali kuchangia jumla ya EURO 90 Milioni kwa ajili ya kufadhili miradi ya maji na usafi wa mazingira katika miji ya Mwanza, Musoma, Bukoba, Magu, Misungwi na Lamadi.
Sehemu ya wafanyakazi wa MWAUWASA.
Wananchi nao wameaswa kusimamia vyema suala la ulinzi na usalama kwa miundombinu ya maji kwenye maeneo yote wanayoishi ili kuiwezesha mamlaka hiyo kuwatumikia vyema.
Wiki ya maji pia inaenda na unywaji maji!!

Burudani na Kadogoli.

Burudani na Bujora wazee wa manyoka.


Diwani wa kata ya Nyamagana Bhiku Kotecha akipata maelezo toka kwa wafanyakazi wa MWAUWASA kwenye maonyesho mabandani viwanja vya Ghand Hall Mwanza.


Burudani ikiendelea.


Diwani wa kata ya Nyamagana Bhiku Kotecha akipata maelezo ya Ubora wa Maji toka kwa wafanyakazi wa MWAUWASA kwenye maonyesho mabandani viwanja vya Ghand Hall Mwanza.


Diwani wa kata ya Nyamagana Bhiku Kotecha akisaini kitabu cha wageni  kwenye maonyesho mabandani viwanja vya Ghand Hall Mwanza huku akishuhudiwa na mmoja wa wafanyakazi wa MWAUWASA.

Kaulimbiu ya Wiki ya Maji mwaka huu ni "Mwaka wa Ushirikiano wa Maji Kimataifa" (International Year of Water Co-operation).
Mwaka huu, Wadau mbalimbali wa maendeleo ya chakula na maji duniani wameamua kushirikiana katika kuhifadhi na kutumia rasilimali maji.

Thursday, March 21, 2013

HIKI NDICHO KILICHOSEMWA NA MKUU WA MKOA WA MWANZA, MWAKILISHI WA WAISLAMU MWANZA NA MWAKILISHI WA WAKRISTU MWANZA MARA BAADA YA KUWEKA MIKAKATI KUDHIBITI MIGOGORO YA KIDINI.

Msikilize hapa mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo..
Msikilize hapa mwakilishi wa viongozi wa Kiislamu Shekhe Hassan Kakebe.

Msikilize hapa mwakilishi wa Wakristu Askofu Zenobius Isaya.

TEKNOLOJIA YAZALISHA DUNIA YA WAPUUZI....


Je ni kweli watu wako busy na simu?
Mtaani kwenu? Kwenye shughuli? 
Mkusanyiko wa watu wengi? 
Kwenye vyombo vya usafiri?
Chunguza mjomba utabaini. 

Wednesday, March 20, 2013

UHAMIAJI MKOA WA MWANZA YANASA WATATU.


IDARA ya Uhamiaji Mkoani Mwanza imeendelea kuwanasa Wahamiaji haramu wanaoingia nchini kwa njia za panya baada ya hivi karibuni kuwakamata vijana watatu raia wa Burundi.

Akizungumza ofisini kwake leo Naibu Kamishina Msaidizi na Kaimu Mkuu wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza Bi. Anamaria Yondani alisema kwamba hii inatokana na Idara hiyo kuendelea kupokea taarifa kutoka kwa wananchi na kuzifanyia kazi, huku pia uhamiaji ikiendelea kutekeleza mradi wa Shirika la Kimataifa ambalo linahusika na shughuli za Kiuhamiaji (OIM) kupitia mradi wa Capacity Buiding in Migration Management (CBMM-II)

Bi Yondani aliwataja vijana hao waliokamatwa kuwa ni Akizmana Adamu (15), Gerlad Michael (17) na Boaz Ernest (15) wote wakazi wa Ruingi  raia wa nchi yaBurundi walioingia nchini kwa njia za Panya kupitia Mkoani Kigoma kabla ya kunaswa Mkoani Mwanza wakiwa kwenye harakati za kutafuta kazi ili kuwasaidia kuishi nchini kinyume cha taratibu na sheria za nchi.

Kaimu Mkuu huyo wa Uhamiaji Mkoa  alisema tatizo la wahamiaji haramu limekuwa ni Janga la Kitaifa na Mkoa wa Mwanza ni Kitovu cha Mawasiliano, Biashara ,Elimu na Usafiri kwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Nchi za Maziwa Makuu na wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Akitoa taarifa ya Mkutano wa Kamati ya  National Immigration Inter-regional Steering Committee (NIISC) uliofanyika Mjini Sumbawanga Mkoani Rukwa Machi 11 hadi 12 mwaka kwa lengo la kuendeleza mradi wa CBMM-II, kuongeza Mikoa wanachama wa NIISC na Namna ya kushirikiana na IOM katika kuendeleza mradi wa huo ambayo yalijadiliwa katika mkutano huo.

“Mradi huu wa NIISC awali ulianzisha na Mikoa ya Mwanza, Mara, Kagera na Kigoma mwaka 2012 na kasha kuongeza Mkoa wa Rukwaa hii ikumbukwe ipo katika Kanda ya Ziwa ambapo kuna vivutio  kadhaa vinavyosababisha wahamiaji haramu kuingia na kujipenyeza katika sekta za i Uvuvi, Kilimo, Ufugaji, Madini, Biashara, Elimu na Usafiri  hali ambayo Uhamiaji imekuwa ikizifanyia  doriawavutia ”alisema

Aidha katika mkutano huo  uliweza kuongeza wanachama wapya katika Kamati ya NIISC ambayo ni Mikoa ya Geita, Shinyanga ,Tabora na Katavi ili kuongeza ushirikiano katika kubadilishana taarifa na uzoefu wa utekelezaji wa majukumu ndaji ya kila siku katika kupambana na wimbi kubwa la wahamiaji haramu.

“Tunatambua wahamiaji haramu bado wanaendelea kupitia  nchini mwetu kwa ajili ya kuelekea  nchini Afrika ya Kusini ambapo awali walikuwa wakipita Mpaka wa Sirali kutokea nchi ya Kenya kuingia Wilaya ya Tarime,Musoma kisha Mkoani Mwanza na kuelekea Mikoa ya Kati hadi Mkoani Mbeya kabula ya kuanza safari kuelekea nchi za kusini hadi Afrika Kusini ili kuwa lahisishia kwenda nchi za Ulaya”alisema.

Bi Yondani alisema kwamba baada ya kutekelezwa kwa mradi wa CBMM-II wahamiaji haramu  waliamua kubadili njia pengine kupita mawakala ambao ni raia wa Tanzani wanaowasaidia kuwaingiza kwa njia haramu na sasa kupitia Mikoa ya Kaskazini ya Kilimanjaro,Arusha,Manyara na Tanga na kuelekea mikoa ya Kati kwa ajili nya kuelekea Mkoani Mbeya na kuvuka kuelekea Malawi na Zambia.

“Lengo kuu la wahamiaji haramu ni kwenda Afrika Kusini ni kutafuta maisha bora na kuwa njia lahisi ya kwenda Mataifa ya Bara la Ulaya na Marekani huku wahamiaji wengi wanaoingia kinyume na utaratibu wa kisheria wengi ni kutoka nchi za Ethiopia,Eritrea na Somaliaambao wamekuwa wakinyanyaswa, kuteswa na kufariki wanapokuwa safarini kwenye maroli ya mizigo na watu wanaowasaidia”alisema

“Wanatumia njia za panya kusafiri kupita mipaka isiyo rasimi  na husaidiwa na mawakala  (Maajenti) wao ambao wengine ni watanzania wasio na uzalendo na wamekuwa wakiwapakiza katika maroli ya mizigo,magari ya makontena  na hata wengine kupitishwa kwenye Hifadhi za wanyama wakali na baadhi yao kupitia Ziwa Victoria kwa mitumbwi na kuvuka mito yenye wanyama wakali wakati wa usiku”alieleza

Bi.Yondani ametoa wito kwa wananchi kurejesha uzalendo wa Taifa na kushirikiana na maafisa uhamiaji na polisi kutoa taarifa kwa watu ambao wanawahisi kuwa siyo raia na watu ambao wameingia kwa njia za panya katika maeneo mbalimbali ya Mikoa yao na wanaotafuta kujipenyeza kufanya kazi ambazo zitawasaidia kuonekana kuwa ni raia wakati huu taifa linaelekea kutoa vitambulisho vya uraia .

“Wananchi sasa warudishe uzalendo wao na kuacha kuwasaidia wageni na wahamiaji haramu walioingia nchini kinyume cha taratibu na kuvunja sheria za nchi kwa kuwatolea taarifa kwa ofisi za uhamiaji na vituo vya jeshi la polisi kwa lengo la kupambana na janga hili la kitaifa la kupambanana wahamiaji haramu wanaoingia nchini kila siku kwa kusaidiwa na mawakala na kuhifadhiwa na watu wasiokuwa na uzalendo”alisisitiza

Amevipongeza vyombo vya habari kwa kushirikiana na Idara hiyo kutoa taarifa kwa wananchi ikiwemo Elimu kwa kueleza bayana athari za kuwa na wahamiaji haramu ambao wengi wao wamekuwa wakifanya uhalifu na kuwapora mali na kufanya mauaji kwa wananchi na sasa wananchi katika maeneo yao ya mitaa na kata kuwa kuwatolea watu ambao si raia ili kuwabaini kabla ya kutolewa vitambulisho vya uraia kitaifa.

INGAWA MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA...

Kilichopo juu ya jengo hili lililipo katika kona ya kipitashoto cha barabara ya Posta na Nyerere jijini Mwanza..

Kwa ukaribu zaidi.

Tiketi zinapatika sehemu zifuatazo; JB Belmonte Hotel
Villa Park resort
na Ndege Insuarance opposite Postal Bank.
Kwa booking na maelezo piga
0712480806 au 0789587458.
Uskose!!!!

DJ FETTY + CLOUDS CREW NA ZIARA FUPI ZOO.

Pichani CEO wa K Records Philbert Kabago (mlangoni) akiwapokea wageni wake Dj Fetty, Sebastian Maganga ambaye ni Meneja wa vipindi Clouds Fm na Joff Leah wa Sports Xtra, walipofanya ziara fupi jijini Mwanza.

Dj Fetty akiwa na baadhi ya wasanii wa K Records.

Clouds Crew ikipata  maelezo juu ya kazi mbalimbali zimazofanywa na zilizofanyika ndani ya K Records chini ya Mtayarishaji 'Rolly Mwaaaa'.

Clouds Crew ikipata  maelezo juu ya kazi mbalimbali zimazofanywa na zilizofanyika ndani ya K Records chini ya Mtayarishaji 'Rolly Mwaaaa' aliyeketi kulia, huku mmiliki wa studio hizo zilizopo Kilimahewa jijini Mwanza Philbert Kabago akishuhudia yanayoendelea.
Nini kilichojiri kwenye ziara hiyo? Sikiliza Redio ya Watu.

Tuesday, March 19, 2013

HIKI NDICHO ALICHO SEMA MPENZI MPYA WA TIGER WOODS JUU YA KASHFA ILIYOMKUMBA HATA KUTALIKIANA NA MKEWE.



FacebookKama ilivyosikika siku ya Jumatatu, Tiger Woods na Lindsey Vonn kwa sasa ni wapenzi rasmi. Tiger, the 14-time major winner and tip of the professional athlete summit, announced on his Facebook page that he was dating Vonn, a former gold medal winner in the Winter Olympics and while the two seem obsessed with each other in those pictures, that hasn't always been the case.
Geoff Shackelford dug up this Time Magazine article from three years ago titled, "Lindsey Vonn Makes Fun of Tiger Woods Too!" The article was accompanied by this quote, that shows it wasn't just golf writer, bloggers and fans that had a little fun when Woods came on that stage years ago to give us his statement about what exactly happened in his personal life.
And like millions of Americans, Vonn can't help poking fun at Woods' staged event. When a member of her Vonn-tourage tells her that Woods gave a few friends hugs after ending his statement, she cracks, "They're like, 'Yeah, you're awesome, you go have that sex.' " The room breaks into a laugh. Then she describes a skit she would want to perform if asked to host Saturday Night Live: picture Vonn at Woods' podium, blue backdrop and all. "There's something you don't know about me," Vonn says in a faux solemn, apologetic voice. "Tiger, you're like my idol, and I too have a sex problem." More laughter. "That would be freaking funny."
I guess it isn't true love unless you can laugh at your partner, and hey, time does heal, right?
Also true love is waiting in the car while Woods and his ex-wife Elin Nordegren attend daughter Sam's soccer game. That's what Vonn did following the couple's dating announcement, according to E! News.

AJALI YA BASI NA TIPA LA MCHANGA YAUA WATATU JIJINI MWANZA

Ni bus la Makwizi lililokuwa likitokea Nata maeneo ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara,  lenye namba za usajili T961 AGP limepata ajali mbaya leo katika eneo la Nyamongolo nje kidogo kuingia jijini Mwanza, mara baada ya kugongana na Tipa la mchanga lenye namba za usajili T 971 BYJ na kusababisha ajali hiyo iliyopelekea watu wawili kufariki dunia (wote walikuwa kwenye tipa) na abiria mmoja aliyekuwa amekaa mbele kushoto kwa dereva kwenye  bus hilo, Dereva wa gari hilo amevunjika miguu yuko hoi Hospitali ya Rufaa Bugando. 

Wananchi wakiwa wamelizingira bus la Makwizi lililokuwa likitokea Nata maeneo ya wilaya ya Serengeti mkoani Mara,  lenye namba za usajili T961 AGP limepata ajali mbaya katika eneo la Nyamongolo Igoma nje kidogo kuingia jijini Mwanza, mara baada ya kugongana na Tipa la mchanga lenye namba za usajili T 971 BYJ na kusababisha ajali hiyo iliyopelekea watu wawili kufariki dunia (wote walikuwa kwenye tipa) na abiria mmoja aliyekuwa amekaa mbele kwenye  bus hilo, Dereva wa gari hilo amevunjika miguu yuko hoi katika hospitali ya Rufaa Bugando.