ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 27, 2018

ISAACK GAMBA KUAGWA JIJINI MWANZA SIKU YA JUMA 4.


Ndugu waandishi wa habari,

Mwili wa Marehemu Isaack Gamba, utaagwa ofisi za UTPC zilizopo Isamilo - Mwanza, siku ya Jumanne tarehe 30/10/2018 saa 2:00 asubuhi na kisha kusafirishwa kwenda Bunda mkoani Mara kwa maziko.

Nyote mnakaribishwa kwa ajili ya kumuaga mwenzetu. Ukipata ujumbe huu mtaarifu na mwenzio

Bwana Mungu alitoa na Bwana Mungu ametwaa. Jina lake lihimidiwe

Mary Ngoboko
UTPC - OMS

SAUDI ARABIA YAPEWA RUNGU KUWACHUNGUZA WAHUSIKA WA MAUAJI YA MWANDISHI KHASHOGGI.

Waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia amesema kuwa washukiwa wote wa mauaji ya mwandishi Jamal Khashoggi, mashtaka yao yatasikilizwa nchini Saudi Arabia.

Katika kikao mjini Bahrain, Adel al-Jubeir amevishutumu vyombo vya habari vya magharibi kwa kuongeza chumvi katika kuripoti taarifa ya kesi hiyo.

Kauli yake imekuja siku moja baada ya serikali ya Uturuki kutaka kuwaamisha washukiwa 18 waliohusika na mauaji hayo.

Mwandishi huo aliuwawa nchini Saudi Arabia mjini Istanbul wiki tatu zilizopita.

Mchumba wa Jamal,Riyadh amekanusha madai ya kuhusishwa kwa familia ya kifalme katika mauaji hayo na badala yake amelaumu watu waliowataja kuwa''maajenti wakatili''

Awali Saudi Arabia ilikana kuhusika kwa lolote dhidi ya mwandishi huo lakini mwendesha mashtaka wa serikali sasa ameweza kueleza jinsi mauaji hayo yalivyotokea.

SHIRIKA LA AMREF HEATH AFRIKA WAGAWA PEDI SHULE 15 ZA SEKONDARI

 NA ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV
Wasichana zaidi ya 2300 kutoka shule 15 za sekondari za  wilaya ya Kahama katika halmashauri ya Msalala mkoani Shinyanga wamepewa taulo takriani  (pedi) 2300 na shirika la Amref health Afrika ,ikiwa na lengo la kuhamasisha wanafunzi hao kuhudhuria masomo pindi wawapo katika siku zao.

Katika semina iliyowahusisha taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo madawati ya jinsi,na idara ya ustawi ya jamii ya halmashauri hiyo ,mratibu wa mradi huo kutoka shirika la Amref health Africa Gaspery Misungwi amesema shirika hilo limelenga kutatua changamoto za Afya katika wilaya hiyo pamoja na kuboresha elimu ya wasichana hao kwa kuwapatia taulo hizo.

Hii ni miuongoni mwa jitihada za kuboresha sekta ya Afya katika mikoa ya Kanda ya ziwa hususani mkoa wa Shinyanga  zinazofanywa na shirika la Amref Health Afrika Baada ya lile la BORESHA CHANJO mradi unaotumia teknolojia ya simu za mkononi na kompyuta katika kuratibu maswala ya chanjo katika wilaya mbalimbali za kanda ya ziwa.

 Mratibu wa mradi huo kutoka shirika la Amref health Africa Gaspery Misungwi akiwasilisha dhumuni la kusanyiko, mipango ya baadaye pamoja na malengo ya mradi.

 Kusanyiko la semina kutoka shirika la Amref health Africa.
 Wadau washirika wakifuatilia kwa umakini yanyoendelea kujiri katika Semina hiyo.
 Darasa na umakini.
 Hatua kwa hatua wadau wa semina wakiendelea kuchukuwa pointi.
Wadau toka taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo madawati ya jinsi, na idara ya ustawi ya jamii ya halmashauri ya wilaya ya Misungwi wakiwa wamejumuika na wanafunzi kusikiliza na kuchangia yale yanayowasilishwa.

"TWENDE KISIWA CHA SAA NANE KUMENOGA"



ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

Wakati Tanzania inaendelea na jitihada zake za kupanua soko na kuvutia watalii wengi,  wakati ambao mchango wa sekta ya utalii katika uchumi wa Taifa unazidi kupaa kila mwaka, Wananchi wametakiwa kutambua umuhimu wa utalii wa ndani kwa kujenga desturi ya kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Kulingana na takwimu za Wizara ya Maliasili na Utalii, sekta hiyo inachangia takriban asilimia 17.2 ya Pato la Taifa (GDP) na zaidi ya robo (asilimia 25) ya mapato yote ya fedha za kigeni. Pia inachangia zaidi ya asilimia 10 ya ajira zote nchini ambapo ajira za moja kwa moja ni 500,000  na ajira takribani millioni moja zisizo za moja kwa moja.

Friday, October 26, 2018

SERIKALI YAFANYA MAAMUZI MAGUMU SAKATA LA BEI YA KOROSHO


Na.Ahmad Mmow, Lindi.

SERIKALI imesimamisha mauzo ya korosho hadi tarehe 30 mwezi huu itakapo tangaza tarehe mpya ya kuanza mauzo ya zao hilo kwa msimu wa 2018/2019.

Agizo hilo limetolewa leo na waziri mkuu waJamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa katika manispaa ya Lindi alipozungumza na  viongozi wa vyama vya ushirika,wakuu wa mikoa,warajisi wasaidizi,mameneja wa vyama vikuu ya ushirika wa mikoa ya Lindi,Pwani,Mtwara na Ruvuma.

Waziri mkuu Majaliwa ambaye alifikia uamuzi huo kwaniaba ya serikali kufuatia sintofahamu iliyojitokeza kutokana na mwenendo wa mauzo wa zao hilo ambao umesababisha wakulima kugomea kuuza korosho zao kwa bei zinazopangwa na wanunuzi katika minada yote iliyofanyika katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

Aliwaomba wananchi wawe watulivu kwani nia ya serikali kusimamisha ununuzi huo ni njema.Kwahiyo wavute subira hadi tarehe 30 mwezi huu itakapo watakapotangaziwa tarehe ya kuanza upya ununuzi.Kwani katika kipindi ambacho minada haitafanyika,serikali itakuwa inafanya utafiti kuhusu masoko na utaratibu utakaotumika kununua zao hilo.

Majaliwa alisema awali zao hilo lilikumbwa na matatizo mengi yaliyohusu utaratibu wa mauzo.Ambayo yalitoa mianya kwa wanunuzi kuwadhulumu wakulima.Hata hivyo serikali iliyafanyia kazi.Hali ambayo ilisababisha mwenendo wa mauzo yake kuwa mzuri na wakulima walianza kunufaika na jasho lao.

Alisema serikali ilibaini matatizo ambayo yalisababisha wakulima wengi kuanza kuacha kulima na kuzalisha zao hilo.Hivyo ilifanya marekebisho makubwa.Yakiwamo ya mwaka 2014 ambayo yalisababisha kiwango cha uzalishaji na bei ya zao hilo kuongezeka kila msimu.

Waziri mkuu Majaliwa aliweka wazi kwamba  misimu  ya 2016/2017 na 2017/2018 bei ya korosho ilikuwa mzuri.Hata hivyo alianza kupata mashaka kwa msimu wa 2018/2019.Kwani hata bei iliyotangazwa na bodi ya korosho ya shilingi 1550 ilikuwa ndogo ikilinganishwa na bei ya juu ya sokoni ya msimu uliopita.Ambapo kilo moja ilifikia kununuliwa kwa shilingi 4000.

Majaliwa alihoji sababu zilizosababisha bodi ya korosho kwa kushirikiana na wizara yenye dhamana ya kilimo kuweka bei elekezi ndogo ambayo imetoa mwanya kwa wanunuzi kununua kwa bei ndogo zao hilo tofauti na msimu uliopita.Akiweka wazi kwamba walifanya hivyo kwa nia isiyo njema kwa wakulima kama inavyotokea sasa.

Waziri mkuu alishangazwa na kimya cha wizara ya kilimo kwakitendo cha kutoonesha jitihada zozote za kutafuta na kuwapa majawabu sahihi wakulima ambao nikama wamekosa mtetezi.Kiasi cha kujitetea wenyewe kwa kugoma kuuza korosho zao.Hivyo aliitaka wizara hiyo ijitathimini kuhusiana na yanayoendelea sasa.

Katika hali ya masikitiko waziri mkuu Majaliwa alishangaa kuona mfumo na utaratibu wa ununuzi wa zao hilo nitofauti na misimu iliyopita.Japokuwa yeye alipokutana na wadau wa zao hilo,akiwemo waziri wa kilimo,Charles Tizeba  mjini Mtwara walikubaliana utumike mfumo na utaratibu ulitumika msimu uliopita.

"Lakini nimesikia kwamba waziri na nyinyi watu wabodi mlisema mfumo mpya ambao umeleta matatizo umeridhiwa na mheshimiwa Rais nakwamba hakuna anaweza kupinga agizo la Rais.Huko nikumchafua mheshimiwa Rais,makamo wa Rais na hata mimi msaidizi wao,"alisema Majaliwa.

Alibainisha kwamba Rais hakuagiza utumike mfumo na utaratibu mpya.Kwasababu haujui hata mfumo wa zamani na amekataa kuwa aliagiza.Hivyo jina lake linatumiwa vibaya.Tabia ambayo imeanza kushika kasi kwa watu wachini kutumia majina ya viongozi wa kuu wa nchi kwamba wanayofanya yanabaraka zao.

"Katika hilo mheshimiwa Rais ameniagiza kwamba mtu yeyote atayetumia jina lake kwamba anayofanya yametokana na magizo yake akamatwe.Kwasababu anataka kumchafua,"alisisitiza Majaliwa.

Alisema serikali ilibaini siku za nyuma kulikuwa na mchezo mchafu uliokuwa unafanywa na watu waliopewa dhamana ya kusimamia masilahi ya wakulima.Ndipo ilipoamua kuvunja bodi za mazao zilizokuwepo.Hali ambayo ilisababisha mafanikio ambayo yanataka kuvurugwa na baadhi ya watu waliopewa dhamana ya kusimamia masilahi ya wakulima.Kitendo ambacho hakikubaliki katika serikali ya awamu hii ya tano.

Waziri mkuu alisema sababu za kubadilisha mfumo na utaratibu wa ununuzi wa zao hilo ambao ulitumika misimu iliyopita hazikuwa na ukweli.Kwani miongoni mwa sababu zilizotolewa nikwamba ulikuwa unasababisha kufanyika rushwa baina ya viongozi wa vyama vikuu vya ushirika na wafanyabiashara.Wakati hakuna hata kiongozi mmoja aliyewahi kukamatwa kwa tuhuma hizo.

"Viongozi wanamgapi wa vyama walikamatwa.Wanakataa kuuza kwa bei ndogo mnawatisha kwa mitutu ya bunduki,mfumo mnaolazimisha tulicha kwasababu ulisababisha matatizo.Sasa mnataka kurudisha nyuma,"alisema kwa ukali Majaliwa.

Kaimu mkurugenzi wa bodi ya korosho yamkuta asiyo yatarajia.

Mbali na kutoa agizo hilo na mengine mengi nadani ya kikao hicho.Majaliwa akimgeukia kaimu mkurugenzi mkuu wa hbodi ya korosho(CBT),profesa Wakuru Magii ambae kabla kwenye mkutano huo alishushiwa tuhuma nyingi na wakuu wa mikoa ya Lindi na Mtwara(Godfrey Zambi na Glasious Byakanwa.

Majaliwa alimuuliza kaimu mkugenzi huyo sababu za wakulima kukubali kuuza korosho kwa being ya chini kwenye mnada uliofanyika jana wakati walikataa bei kubwa zaidi ya hizo za Jana.Huku akiwa amenyamaza kimya wakati mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika aliyekuwa kwenye mnada huo akilazimishwa na asikari asaini fomu kuridhia kwamba wakulima waliliridhika kuuza korosho zao.

Lakini pia waziri mkuu alimshangaa kaimu mkurugenzi huyo kwakitendo chake cha kumpigia simu katibu mkuu wa CCM,Dkt Bashiru Alli kwamba alisitisha minada kwasababu anakampuni zake.Lakini pia alimpigia simu mkuu wa jeshi la polisi nchini,Simon Siro nakumueleza tuhuma kama hizo.Jambo ambalo halina ukweli.Bali alifanya hivyo ilikutimiza wajibu wake wakuwasimamia masilahi y wakulima.Tena sio wakorosho peke yake bali wa mazao yote.

Kufuatia tuhuma mbalimbali zilizotolewa na wakuu hao wa mikoa na viongozi wa vyama vikuu vya ushirika vya TANECU na Lindi Mwambao ambazo kaimu mkurugenzi huyo alishindwa kukanusha.Waziri mkuu alifikia uamuzi wa kumrejesha wizarani.

Mkutano huo uliitishwa na waziri mkuu mwenyewe ili kutafuta suluhisho la kudumu kutokana na matatizo yaliyojitokeza katika msimu huu tangu kuanza ununuzi wa zao hilo.

KAULI YA MATAKA BAADA YA KUJIENGUA ALLIANCE.

KOCHA Mkuu wa timu ya Alliance FC ya Mwanza, Mbwana Makata, amesema kuingiliwa majukumu yake ni moja ya sababu iliyomfanya kujiweka pembeni kwenye kikosi cha timu hiyo.

Makata pamoja na msaidiziwake Renatus Shija, hawakuwepo kwenye benchi wakati timu hiyo ilipokuwa ikiumana na Simba kwenye Uwanja wa taifa Dar es Salaam na kukumbana na kipigo cha mabao 5-1.

Alisema imefikia hatua yeye kama kocha hana mamlaka ya kupanga kikosi na kuingiliwa na menejimenti ya timu hiyo.

“"Suala la mchezaji gani anastahili kucheza na mwenye jukumu la kupanga na kufundisha  kikosi ni mwalimu, hivyo unapoingiliwa kwenye majukumu unaonekana kama hufai  na unaharibu taaluma hivyo kufuatia hilo nikaamua kujiengua na ndicho kilichotokea katika mchezo wetu dhidi ya Simba," alisema Makata.

Alisema, Meneja wa timu kimsingi anapaswa kukaa nje ya benchi la ufundi na kushuhudia nini timu yake inafanya  hivyo suala ya kuingilia katika kupanga kikosi siyo jambo jema na mwenye jukumu hilo ni kocha mkuu wa timu pamoja na msaidizi wake.

Makata, alisema kwa sasa wanasubiri hatima yao kutoka kwa menejimenti ya timu hiyo lakini alisisitiza hayupo tayari kufanya kazi kwa kupangiwa na watu ambao hawana taaluma ya ukocha.

Kwa upande wake Meneja wa timu hiyo FC, James Bwire, ambaye anashutumiwa kumuingilia kocha huyo, alisema suala la yeye kuhitafiliana na makocha wake ni jambo geni, kwani yeye kama meneja anatambua majukumu pamoja na mipaka yake hivyo na wao watambue pia.

Bwire alisema hoja ya sasa siyo kutofautiana kimsingi ni kutafuta njia mbadala ya namna ya kusaidia timu kupata matokeo mazuri hayo.

Alisema tuhuma hizo zinazoelekezwa kwake ni kisingizio kwa kuwa mpaka sasa kocha huyo (Makata )amehamisha kila kitu  kwenye nyumba waliompangia.

"Mpango wa kuhama alikuwa nao, hivyo tulimpa mechi mbili za Simba na Yanga kuwa hakipoteza safari yake na timu hiyo itakuwa imeishia hapo, ila yeye amejiwai kuondoka kwa kisingizio cha kuingiliwa majukumu yake, kavunja mkataba mwenyewe hivyo taratibu za kulipwa stahiki zake zitafuatwa kama sheria inavyo elekeza, hata kama kunatofauti kati yetu angesubilia mchezo upite kwanza baada ya hapo tungekaa pamoja kujadiliana lakini yeye akaamua kuitelekeza timu. ", alisema Bwire.

Alliance iliyopanda daraja msimu huu, inaburuza mkia kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi sita baada ya kucheza michezo 11.

WATANZANIA BADO TUKO NYUMA SUALA LA UTALII WA NDANI.

 NA.MANDIA ZEPHANIA MWANZA
Watanzania wametakiwa kutambua umuhimu wa utalii wa ndani kwa kujenga desturi ya kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini ili kuongeza uelewa wa maswala mbalimbali pamoja na kujionea vivutio mbaimbali katika hifadhi hizo.

Mhifadhi mkuu wa hifadhi ya Kisiwa cha Utalii Saa Nane BEATRICE KESSY amesema hifadhi hiyo imelenga kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi hiyo kutoka elfu kumi kwa mwaka hadi kufikia elfu kumi na tatu kwa mwaka kupitia kampeni ya GUDUA HAZINA ZA UTALII MWANZA inayohamasisha wanafunzi kutembelea hifadhi hiyo.


Hifadhi ya taifa ya Saa nane ni hifadhi pekee iliyopo katikati ya jiji la Mwanza ikiwa ni hifadhi pekee iliyopo katikati ya jiji yenye vivutio mbalimbali ikiwemo wanyama  na manthari ya kuvutia.

Mhifadhi mkuu wa hifadhi hiyo BEATRICE KESSY amesema kuanzishwa kwa kampeni ya GUDUA HAZINA ZA UTALII MWANZA, imejikita kuhamasisha utalii wa ndani pamoja na kuongeza idadi ya watalii katika hifadhi hiyo.

GLORIA MWIHAMBO msimamizi wa bodi ya utalii kanda ya ziwa (TTB),amesema ukilinganisha na miaka iliyopita watanzania wamepata muamko wa  kutembelea hifadhi mbalimbali nchini.

Watalii kutoka hao kutoka vyuo mbalimbali vya mkoa wa Mwanza wamesema imekuwa fursa kwa wao kuongeza uelewa katika masomo yao pamoja na kufurahi vivutio mbalimbali katika hifadhi hiyo.

Hifadhi hiyo iliyopo chini ya Shirika la Hifadhi za Taifa nchini (TANAPA) limeanzisha kampeni hiyo itakayodumu kwa siku tatu ambapo pamoja na kutembelea hifadhi hiyo wanafunzi hao watashiriki michezo mbalimbali pamoja na kutoa zawadi kwa mwanafunzi  atakaye  tangaza hifadhi hiyo vyema kupitia mitandao ya kijamii.

CHOO CHA SHULE YA MSINGI SELIAN CHATITIA NA KUZAMISHA WANAFUNZI.

 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Jerry Muro akimpa pole mtoto majeruhi ambae amelazwa katika hospitali ya Seliani na kumjulia hali huku akiongozana na viongozi mbalimbali.








Leo 26/10/2018 Majira ya Saa tatu na nusu asubuhi tumepata changamoto ya kutitia na kuanguka kwa Jengo la choo cha shule ya Msingi ya Seliani katika kijiji cha Olevolosi kata ya kimnyaki Wilaya ya Arumeru ambapo katika tukio hilo tumeweza Kuokoa Mwanafunzi Mmoja wa Kiume aliepata majeraha sehemu na bado tunaendelea na jitahada za kuondoa kifusi kilichochanganyikana na matofali ambacho kimezama katika Shimo la choo kilichokuwa na matundu 20

Katika kukabiliana na Changamoto Iliyotokea Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro akiambatana na Katibu Katibu tawala wa Wilaya na viongozi wa Halmashauri ya Arusha walifika kwenye eneo la tukio na kuanza kazi ya kuratibu jitihada za  uokoaji wakishirkiana na vikosi vya uokoji na Zimamoto pamoja na mamia ya wananchi wa kata ya kimnyaki ambapo walifanikiwa kumuokoa mwananfunzi Mmoja akiwa amejeruhiwa usoni na kukimbizwa katika hospital ya Seliani kwa matibabu zaidi ambapo mpaka sasa vikosi vya uokoaji vinaendelea na jitihada za kufukua kifusi pamoja na matofali yaliyozama katika choo hicho Cha shule chenye matundu 20 ambacho ndio choo pekee Kinachotumiwa na zaidi ya wanafunzi 1,121 wa shule hiyo.

Katika Eneo la tukio kwanza tulilazimika kurejesha hali ya Amani na kutuliza taharuki za wananchi ambao baadhi Wana watoto wanaosoma katika shule hiyo na kutoa nafasi kwa vikosi vya ukoaji kuendelea na zoezi la kutafuta wanafunzi wengine Kutokana na kutokupatikana kwa Taarifa za awali zinazoonyesha idadi ya Wanafunzi ambao huenda walikuwa kwenye choo hicho.

Kutokana na shule hiyo kuwa na choo kimoja chenye matundu ishirini ambacho ndicho kilikuwa pekee kwa shule hiyo ilimlazimu Mkuu wa Wilaya ya Arumeru kuchukua hatua za kuzungumza na Uongozi wa Kanisa la KKKT usharika wa seliani na kuomba shule kutumia vyoo vya Kanisani ombi ambalo lilikubaliwa na *Mkuu wa jimbo la Arusha Magharibi Mchungaji Philemon Joseph Mollel ambae aliungana na Mkuu wa Wilaya katika zoezi a uokoaji na hivyo kuondoa Mashaka ya kufungwa kwa shule.

Kutokana na kadhia hiyo ilimlazimu Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry  Muro kuzungumza na wananchi waliojitokeza ambapo katika mazungumzo yake aliwataka wananchi kutulia na kutoa fursa ya kuendelea kwa zoezi la utoaji wa kifusi ili kujirisha na madhara zaidi ambayo huenda yametokea.

Awali kwa upande wao baadhi ya wananchi waliungana na Mkuu wa Wilaya katika kuchanga Fedha kwa ajili ya kuanza Mikakati ya Ujenzi wa choo kingine ili kutokwamisha masomo ya wanafunzi kazi ambayo ilifanywa na Mkuu wa Wilaya pamoja na viongozi wa Kanisani na halmashauri na kuitikiwa kwa wingi na wananchi waliotoa Fedha zao.

Awali Mhe Muro alilazimika kumtembelea majeruhi ambae amelazwa katika hospitali ya seliani na kumjulia hali huku akiongozana na viongozi mbalimbali.

Imetolewa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru

CHAMA CHA WALIMU TAZANIA CHATINGA MWANZA.

 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella amepokea ugeni kutoka Chama cha Walimu Tanzania ukiongonzwa na Rais wao Comrade Leah H. Ulaya waliofika Mkoani hapa kwa ajili ya maandalizi ya maadhimisho ya siku ya mwalimu duniani pamoja na maadhimisho ya  Jubilei ya Miaka 25 ya kuzaliwa Chama cha Walimu Nchini (CWT) yanayotarajiwa kufanyika Novemba 1 mwaka huu Mkoani hapa.

Kaulimbiu ya Maadhimisho  hayo "Haki ya kupata elimu ni haki ya kuwa na Mwalimu Mahiri."







WAANDISHI WA HABARI WA MITANDAO YA KIJAMII SASA KUHAMIA VIJIJINI



 GSENGOtV

Ni kupitia Mradi wa Data Driven Advocacy (DDA) unaozijengea asasi za kiraia na wanahabari wa vyombo vya habari mbadala kutumia takwimu katika ushawishi na utetezi wa kazi zao, ambapo waandishi wa habari licha ya kupata fursa ya kujadili changamoto wanazokutana nazo, sheria wapi zinawakwamisha pia wanapata fursa ya kufunguka kile walichojifunza na namna watakavyokwenda kukifanyia kazi kwa maslahi ya taifa.