ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, October 27, 2018

"TWENDE KISIWA CHA SAA NANE KUMENOGA"



ZEPHANIA MANDIA/GSENGOtV

Wakati Tanzania inaendelea na jitihada zake za kupanua soko na kuvutia watalii wengi,  wakati ambao mchango wa sekta ya utalii katika uchumi wa Taifa unazidi kupaa kila mwaka, Wananchi wametakiwa kutambua umuhimu wa utalii wa ndani kwa kujenga desturi ya kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Kulingana na takwimu za Wizara ya Maliasili na Utalii, sekta hiyo inachangia takriban asilimia 17.2 ya Pato la Taifa (GDP) na zaidi ya robo (asilimia 25) ya mapato yote ya fedha za kigeni. Pia inachangia zaidi ya asilimia 10 ya ajira zote nchini ambapo ajira za moja kwa moja ni 500,000  na ajira takribani millioni moja zisizo za moja kwa moja.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.