WENYEJI, JKT Tanzania wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mashujaa FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jana jioni Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar es Salaam.
Bao pekee la JKT Tanzania katika mchezo huo limefungwa na beki Laurian Omar Makame aliyeiadhibu timu yake ya zamani dakika ya 40.
Kwa ushindi huo, JKT Tanzania inafikisha pointi 27 katika mchezo wa 15 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu, wakati Mashujaa inabaki na pointi zake 14 za mechi 14 nafasi ya tisa kwenye msimamo wa ligi yenye timu 16.
Ikumbukwe mwisho wa msimu timu mbili zitashuka Daraja na mbili zitakazomaliza nafasi ya 14 na 13 zitamenyana baina yao kwa mechi mbili za nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla atasalia Ligi Kuu.
Timu itakayofungwa itakwenda kumenyana na timu kutoka Ligi ya Championship katika mechi nyingine mbili za mchujo nyumbani na ugenini na mshindi wa jumla ndiye atacheza Ligi Kuu msimu ujao.


