ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, October 8, 2024

MAPINDUZI MAKUBWA YAMEFANYIKA TCRA KANDA YA ZIWA - WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA - SEHEMU YA KWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

Katika muendelezo wa Wiki ya Huduma kwa Wateja, Leo Oktoba 08, 2024, Jembe Fm imefika katika ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Kanda ya Ziwa (TCRA) na kuzungumza na meneja wa kanda Mhandisi Imelda Salum, #tcra #samiasuluhuhassan #jembehabari #mwanza

TPA TANGA BILIONI 18 NDANI YA MIEZI 3

 

 

MENEJA wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha akizungumza waandishi wa habari ikiwa ni siku ya wiki ya huduma kwa wateja
Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha kushoto akimkabidhi zawadi Mwandishi Mwandamizi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Mkoa wa Tanga Bertha Mwambela ikiwa ni wiki ya huduma kwa wateja mapema leo



Na Oscar Assenga, TANGA

MAMLAKA ya Bandari (TPA) Tanzania Mkoa wa Tanga kwa kipindi cha miezi mitatu ya robo ya kwanza ya mwaka 2024/2025 wamekusanya Bilioni 18 zilizotokana na ujio wa meli 11 huku asilimia 44.4 ya mapato hayo yakitokana na Meli za Kampuni ya Sea Front Shipping Services kutumia Bandari ya Tanga.

Hayo yalisemwa leo na Meneja wa Bandari ya Tanga Masoud Mrisha wakati akizungumza na waandishi wa habari ikiwa ni siku ya wiki ya huduma kwa wateja ambapo alisema kwamba wanapenda kumshukuru mteja huyo mkubwa na wateja wengine ambao wanaitumia Bandari hiyo.

Alisema kwamba wataendelea kuwashukuru na kushirikiana nao ili wajue changaamoto zinazowakabili ili waweze kuzirekebisha na wahakikishe wanapata huduma bora ya kiwango cha juu kitachowawezeshaa kurudi tena na kupata huduma katika Bandari hiyo na kufikia kwenye lengo walilokusudia.

Akizungumzia kiwango cha shehena ambayo wameihudumia kwa kipindi hicho alisema waliweza kuhudumia shehena ya tani 333,718 na hivyo kuvuka lengo lao waliojiwekea kwa asilimia 17.8 walijiwekea la kuhudumia tani 283,290.

“Utaona ni jinsi gani tumefanikiwa na tusingeweza kufanikiwa bila kutoa huduma bora kwa wateja mwaka jana kwa kipindi cha miezi mitatu kama hii tuliweza kuhudumia tani 200,004 mwaka huu tumehudumia 333,718 utaona namna tumeweza kuvuka lengo ”Alisema

Awali akizungumza Mwakilishi wa Kampuni ya Maersk ofisi ya Tanga Salum Mgaya alisema huduma za bandari ya Tanga hivi sasa zimefanyiwa maboresho makubwa ya vifaa na rasilimali watu na teknolojia imeongezeka ufanisi mkubwa na meli zao zinapoingia zinahudumiwa kwa wakati na makasha ya wateja yanatolewa kwa wakati.

Alisema kwamba hivi sasa meli zinafunga gatini na kuhudumiwa masaa 24 na wamekwisha kuleta meli kubwa yenye kontena 1,000 na imehudumiwa ndani ya wastani wa siku tatu mpaka nne kulingana na vifaa vilivyokuwepo lakini maboresho yaliyofanyika yameongeza ufanisi Bandari ya Tanga.

Naye kwa upande wake Mwakilishi kutoka Kampuni ya Star rock Shipping Vitalis Mokiwa alisema walikuwa wanadili na meli za mafuta na sasa wanadili na meli za mizigo mbalimbali ikiwemo ya kontena na wanaishukuru serikali kwa kuwaboresha bandari ya Tanga.

Alisema kwa sababu mwanzo meli zilipokuwa zinakuja mizigo ilikuwa inashushwa mbali na gatini na hivyo wakijikuta waingia gharama mara mbili lakini sasa kutokana na maboresho ya ujenzi wa gati ambao umewezesha meli kufika gati.


Monday, October 7, 2024

TPA TANGA BILIONI 18 NDANI YA MIEZI 3

 VICTOR MASANGU,PWANI TV

 
Kilio cha walimu wa shule ya  msingi Boko Timiza iliyopo  kata ya Tumbi Halmashauri ya Wilaya ya  Kibaha mji   kilichokuwa kikiwakabiliwa kwa kipindi cha miaka zaidi ya 40  cha kuwepo na  changamoto  sugu ya  ukosefu mkubwa  wa kutokuwa na viti na meza hatimaye kimepatiwa ufumbuzi baada ya baadhi ya wadau wa maendeleo ya elimu kuamua kulivalia njuga suala hilo na kwenda kutoa msaada kutokana na kubaini walimu hao hawana sehemu maalumu ya kukaa.

Hayo yamebainishwa na Kaimu  Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Boko Timiza Rozania Kimate  wakati wa halfa fupi  iliyofanyika shuleni hapo kwa ajili ya kukabidhiwa  msaada huo wa viti na meza kutoka kwa mdau wa maendeleo Selina Koka ambaye pia ni mke wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini na  Mlezi wa Jumuiya ya Umoja wa wanawake (UWT)  Wilaya ya Kibaha mjini na kubainisha  msaada huo utakuwa ni mkombozi mkubwa kwa walimu.

UBIA WA TWIGA WAONGOZA MCHANGO WA TASNIA YA UCHIMBAJI MADINI KATIKA UCHUMI WA TANZANIA

 

Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow akiongea katika mkutano na waandishi wa habari ,viongozi wa serikali na wadau mbalimbali uliofanyika katika mgodi wa bulyanhulu jana,(Kushoto) ni Naibu Waziri wa Madini, Dk.Steven Kiruswa na (kulia) ni Meneja wa Barrick nchini,Melkiory Ngido.
Naibu Waziri wa Madini, Dk.Steven Kiruswa akiongea katika mkutano huo.
Mbunge wa Nyang'hwale,Mh.Hussein Nasor Amar akiongea katika mkutano huo.

Na Mwandishi Wetu.

Naibu Waziri wa Madini, Dk.Steven Kiruswa, amesema ubia kati ya Kampuni ya Dhahabu ya Barrick na Serikali ya Tanzania ni kielelezo cha mafanikio ya ushirikiano wa Serikali na sekta binafsi kwa kuwa unazidi kuleta manufaa nchini na ameomgeza kuwa Serikali itaendelea kuwalinda wawekezaji wenye kuleta mapinduzi chanya katika kukuza uchumi wa nchi .

Akiongea na katika mkutano wa waandishi wa habari wa kupokea taarifa ya utendaji wa migodi ya Barrick na Twiga uliojumuisha wadau mbalimbali uliofanyika katika mgodi wa Bulyanhulu, Dk.Kiruswa, alisema ubia huu umekuwa mfano wa kuigwa kwa kuwa migodi yote inayoendeshwa na Barrick uendeshaji wake umekuwa wa uwazi pia mafanikio yake yanaonekana kutokana na kutoa mchango mkubwa kwa Serikali kupitia kodi mbalimbali, kufanikisha miradi ya kijamii kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR), kupanua wigo kwa ajira kwa Watanzania na kunufaisha wananchi kupitia utekelezwaji wa sera ya maudhui ya ndani (Local content kwa ufanisi mkubwa) sambamba na uwekezaji katika matumizi ya teknolojia za kisasa cha uchimbaji.

Alisema Serikali haitafumbia macho vitendo vya kuwahujumu wawekezaji wanaofanya vizuri katika uwekezaji wao nchini kwa lengo la kuwakatisha tamaa na kurudisha nyuma mkakati wa Serikali wa kukuza uwekezaji nchini yakiwemo mashirikika yasio ya Kiserikali ya nje ya nchi ambayo yamekuwa yakijifanya kiranja wa kutetea haki za binadamu na kusambaza taarifa za uwongo dhidi ya wawekezaji wa hapa nchini zikijifanya kuwatetea watanzania wanyonge wakati zinatafuta mianya ya kujinufaisha kupitia mgongo wa watanzania.

“Serikali ya Tanzania iko imara na madhubuti katika kusimamia wawekezaji kuhakikisha wanafuata kanuni na sheria zake kupitia taasisi zake mbalimbali zilizoanzishwa kisheria ambazo zinafanya vizuri na wanaokiuka sheria wanachukuliwa sheria na kupewa maelekeza na miongozo hivyo hayo mashiriki yasio ya Kiserikali yaache kuchafua taswira ya nchi kama ambavyo yamekuwa yakifanya kwa muda mrefu kupitia mgodi wa North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara” ,alisema.

Aliongeza kuwa kutokana na maombi yaliyokuwa yakitolewa kwa Serikali na viongozi wa wananchi katika maeneo ya migodi ya kuwatengea wachimbaji wadogo maeneo na kuyataka makampuni makubwa yenye teknolojia ya uchimbaji kuwasaidia Serikali imeanza kuyafanyia kazi na imeanza mazungumzo na makampuni makubwa kupitia Wizara ya Madini na taasisi zake zinazosimamia uchimbaji wa madini.

Ubia huo unachangia 51% ya mapato ya Serikali yanayotokana na tasnia ya uchimbaji madini, kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya Mpango wa Uwazi wa Tasnia ya Uchimbaji Madini Tanzania (TEITI). Ubia wa Twiga unajumuisha migodi ya dhahabu ya North Mara na Bulyanhulu.

Migodi yote miwili pia iliongoza katika utendaji wa kiusalama wa tasnia hiyo, huku Bulyanhulu ikishinda Tuzo ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka huu wakati North Mara ikitajwa na Mamlaka ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya Tanzania (OSHA) kuwa kampuni bora katika kuwahudumia wafanyakazi wenye mahitaji maalumu.

Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Barrick, Mark Bristow, alisema katika mkutano huo kuwa utafutaji wa madini unaoendelea katika maeneo yaliyotumika na kuachwa karibu na migodi yake ya Bulyanhulu na North Mara unaendelea. Utafiti huo umebainisha fursa zaidi za kuzihuisha na kuzipanua hifadhi za madini ambapo madini yatakwisha au kupungua, jambo litakalosaidia zaidi katika kuongeza uhai na unyumbufu wa migodi hiyo. Aidha, maendeleo mazuri yameshapatikana katika kuyabainisha maeneo mapya ambapo hapakuwahi kuwa na shughuli za uchimbaji madini, yenye uwezo wa kuongeza migodi mipya kwenye kampuni hiyo.

Aidha, Bristow alisema mpango wa Barrick na Twiga wa Kusongesha Mbele Mustakabali wa Elimu umekamilisha awamu yake ya kwanza, ambapo Barrick ilifadhili upanuzi wa miundombinu ya shule zipatazo 64, yenye thamani ya dola milioni 10, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa vipatavyo 396, mabweni yapatayo 97 na majengo ya maliwato yapatayo 600. Awamu ya pili ya mpango huo umepangwa kuanza katika robo ya nne ya mwaka huu kwa uwekezaji mwingine wa dola milioni 10 ambao utafuatiwa na awamu ya tatu ya dola milioni 10.

Wakati huohuo, Chuo cha Barrick, kilichozinduliwa mwanzoni mwa mwaka na Waziri wa Madini kwenye mgodi uliofungwa wa Buzwagi na ambao hivi sasa ni eneo maalum la uzalishaji (SEZ), tayari kimetoa mafunzo kwa mafomeni, wasimamizi na warakibu zaidi ya 1,000 kutoka katika nchi za Afrika na Mashariki ya Kati. Chuo hiki kiko mbioni kufikia lengo lake la kutoa mafunzo kwa zaidi ya watu 2,000 mwaka huu.

Bristow alisema kulingana na dhamira ya uwazi ya Barrick, kampuni hiyo iliwasilisha taarifa za hivi karibuni za mfululizo wa tuhuma za ukiukwaji wa haki za binadamu zilizokuwa zinatolewa dhidi ya Mgodi wa North Mara kwenye Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tanzania (CHRGG). Baada ya kutembelea mgodi huo na maeneo ya jirani na kufanya uchunguzi wa kina, tume hiyo ilitoa taarifa iliyothibitisha kwamba hapakuwa na ushahidi wa ukiukwaji wa haki za binadamu katika mgodi wa North Mara na hivyo kuuondolea mgodi huo tuhuma hizo zilizotolewa na baadhi ya mashirika yasiyo yasiyo ya kiserikali ya nchi za nje.

Viongozi mbalimbali wa Serikali kutoka wilaya za Kahama, Msalala na Nyang’hwale waliohudhuria mkutano huo, walipongeza mafanikio makubwa yanayoendelea kupatikana kupitia uwekezaji wa Barrick hususani katika kufanikisha miradi mikubwa ya kijamii kupia fedha za uwajibikaji kwa jamii kwenye sekta ya afya na elimu.