ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, April 20, 2024

LEO BARABARA ZOTE ZA JIJI LA DAR ES SA;AAM KUELEKEA MWENGE - TANGAZO ANOINTED MINISTRY 2024

 𝗘𝘄𝗲 𝗺𝘁𝘂 𝘄𝗮 𝗠𝘂𝗻𝗴𝘂 𝗵𝗶𝗶 𝗶𝗻𝗮𝗸𝘂𝗵𝘂𝘀𝘂 𝗻𝗶 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝘁𝗮𝗿𝗲𝗵𝗲 𝟮𝟬𝘁𝗵 𝗔𝗽𝗿𝗶𝗹 𝟮𝟬𝟮𝟰 𝗗𝗮𝗿 𝗲𝘀 𝗦𝗮𝗹𝗮𝗮𝗺 𝗶𝘁𝗮𝘁𝗶𝗸𝗶𝘀𝗶𝗸𝗮....

. . . . . #JEMBEGOSPLE

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI PWANI LAWAFUNDA WANANCHI JUU YA KUJIKINGA NA MAFURIKO NA MAAFA

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI 


Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani Katika kukabiliana na majanga mbali mbali yakiwemo ya  moto na mafuriko ya mvua imetoa elimu kwa zaidi ya wananchi 72862 juu ya kujikinga na majanga pindi yanapotokea.

Hayo yamebainishwa na Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani Mrakibu mwandamizi Jenifa Shirima wakati akizungumzia mipango na mikakati waliyojiwekea katika kupambana na majanga ya aina tofauti.

Kamanda Shirima alisema kwamba lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi juu  ya kujikinga na majanga mbali mbali hasa katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha.

"Sisi kama jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani tumeendelea kutoa elimu kwa wananchi wetu na kwamba tumeshafanikiwa kwa kuwafikia wananchi wapatao 72862 na kimsingi bado tunaendelea,"

"Katika zoezi ili la kutoa elimu kwa wananchi wetu wa Mkoa wa Pwani tangu Julai 2023 hadi kufikia mwezi Aprili mwaka huu tumepiga hatua kubwa ya kutoa elimu hiyo ambayo idadi yake ni 72862,"alisema Kamanda Shirima.

Kadhika Shirima alifafanua kuwa pamoja na kutoa elimu hiyo pia wameweza kupata fursa ya kutoa elimu juu ya tahadhari dhidi ya mafuriko ambayo yanatokea kutokana na mvua.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo alibainisha kuwa wameshapita kutoa elimu katika mikusanyiko ya watu mbali mbali ikiwa sambamba na kuanzisha sehemu maalumu za Fire club ambazo zitasaidia katika kupambana na majanga.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo aliwasisitiza wananchi ambao wamefanikiwa kupatiwa mafunzo hayo kuendelea kuyatumia vizuri ili yaweze kuwa msaada mkubwa katika jamii inayowazunguka.

Friday, April 19, 2024

RFO PWANI-TUMEFANIKIWA KUOKOA WANANCHI 2397 MAFURIKO YA RUFIJI NA KIBITI

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI 


Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani  Mrakibu mwandamizi Jenifa Shirima amesema kwamba hadi kufikia leo Aprili 19 wamefanikiwa kuokoa wananchi wapatao 2397 kutoka Wilaya za Rufiji na Kibiti mkoani Pwani ambao walikubwa na mafuriko ya mvua na makazi yao kuzingirwa na maji.

Akizungumza katika mahojiano maalumu kuhusiana na mwenendo mzima wa hali halisi ilivyo kwa sasa  Kamanda huyo alibainisha hali ya makambi ambayo yametengwa kwa ajili ya wahanga yapo salama.






Kamanda huyo alisema kwamba kutokana na mvua ambazo zinaendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali ziliweza kusababisha baadhi ya wananchi kukosa  makazi yao na hivyo serikali kuamua kuwatafutia maeneo mengine ambayo ni salama zaidi.

Alisema kwamba wameweza kufanikisha zoezi la uokoaji wa wananchi hao kwa kushirikiana bega kwa bega na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kwa lengo la kuwatoa wananchi katika maeneo yaliyozingirwa na maji.

"Kwa sasa wananchi wote ambao tumeweza kufanikiwa kuwaokoa wameifadhiwa na serikali katika makambi maalumu ambayo yapo katika Wilaya ya Rufiji na Kibiti na yapo katika hali salama ", alisema Kamanda Shirima.

Kadhalika alibainisha kuwa tangu zoezi hilo lilipoanza mnano tarehe 9 machi mwaka huu la kuwavusha watu katika maeneo mbali mbali ambayo wanayooshi ili kuwapeleka maeneo salama.

Pia aliongeza kuwa zoezi rasmi kwa ajili ya uokoaji wa watu ambao wanaishi katika maeneo mengine ya mbali lilianza kufanyika kuanzia Aprili 7 mwaka huu hadi kufikia leo hii kufikia idadi ya watu waliookolewa kufikia 2397.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo alitoa rai kwa wananchi wa Wilaya ya Kibiti pamoja na Rufiji kuhakikisha wanaondoka katika maeneo hatarishi na kukubali kwenda katika maeneo salama ambayo yametengwa na serikali.

Nao baadhi ya wananchi wa   Wilaya ya Kibiti na Rufiji wameishukuru kwa dhati serikali pamoja na wadau mbali mbali wa maendeleo kwa kuwapatia misaada ya kibinadamu kutokana na kupata mafuriko hayo.

Pia hawakusita kumshukuru Mkuu wa Mkoa wa Pwani pamoja na Kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani kwa kujituma kwa kipindi chote katika kuwasaidia na  kuokoa maisha yao.

WAZIRI JERRY SILAA KUONGOZA KLINIKI YA ARDHI TANGA

 

Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI wa Ardhi,Nyumba na Mendeleo ya Makazi Jerry Silaa anatarajiwa kuongoza Kliniki ya Ardhi kwa mkoa wa Tanga itakayofanyika kuanzia Aprili 22 mpaka 28 mwaka huu ikifanyika kwenye maeneo mawili Kijiji cha Miaka 21 Chumbageni Tanga na Korogwe.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kamishna Msaidizi wa Ardhi mkoa wa Tanga Tumaini Gwakisa alisema zoezi hilo litafanyika kwenye maeneo mawili ambapo litaanzia Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Tanga eneo la Kijiji cha miaka 21 Chumbageni kuanzia Aprili 22 mpaka 25 mwaka huu.

Alisema baada ya kumaliza kwa Tanga wataelekea wilayani Korogwe ambapo litafanyika kuanzia Aprili 26 mpaka 28 mwaka hu na uendeshwaji wa program hiyo utasimaiwa na itaongozwa na Waziri wa Ardhi Jerry Silaa akiwa na wataalamu wa Wizara hiyo.

“Nichukue nafasi hii kwaalika wananchi wote wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kupata huduma mbalimbali za sekta ya ardhi katika maeneo ambayo kliniki hiyo itafanyika kwani kutakuwa na utatuzi wa migogoro ya ardhi ambapo Waziri atasikiliza kero mbalimbali za Migogoro hiyo”Alisema

Alisema pia kutakuwa na utolewaji wa elimu kuhusu usimamizi wa ardhi pamoja na uwepo wa kituo jumuishi kitakachotoa huduma ya kupokea maoni mbalimbali na utoaji hati miliki ,ukadiriaji wa kodi ya ardhi na ulipaji wa kodi ya ardhi.

Gwakisa aliwataka wananchi wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kushiriki ambapo Waziri atakuwepo na wataalamu kutoka Wizarani

Thursday, April 18, 2024

RAIS SAMIA KUFUNGUA MKUTANO WA ALAT 2024 UTAKAOFANYIKA ZANZIBAR

 𝗥𝗔𝗜𝗦 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔 mgeni rasmi Mkutano wa 38 ALAT utakaofanyika Tarehe 23 - 25 April 2024 #Zanzibar

. . #alat @ortamisemi @samia_suluhu_hassan @dr.hmwinyi @jembenijembe @kikotifredy #samiasuluhuhassan #HUSSEINMWINYI #zanzibar

Wednesday, April 17, 2024

SHIRIKA AMEND,JESHI LA POLISI TANGA WAENDELEA KUTOA ELIMU YA USALAMA BARABARANI

 

 


Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoa elimu kwa Madereva wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda,Bajaji na Madereva wa Daladala katika Stendi ya Pongwe Jijini Tanga
Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoa elimu kwa Madereva wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda,Bajaji na Madereva wa Daladala katika Stendi ya Pongwe Jijini Tanga
Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika
Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika akizungumza na madereva wa bodaboda pikipiki maarufu kama bodaboda,bajaji na daladala






Na Oscar Assenga,TANGA


Shirika la Amend Tanzania kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Switzerland Nchini,wameendesha zoezi la utoaji wa Elimu ya Usalama Barabarani kwa Madereva Daladala na Bodaboda Jiji la Tanga ikiwa ni sehemu ya kupunguza na kutokomeza ajali za barabarani zinazotokana na uzembe wa madereva.

Akizungumza wakati wa utoaji wa Elimu hiyo ya Usalama Barabarani iliyofanyika Aprili 16,2024 katika Stendi ya Pongwe Jijini hapa,Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi, amewaambia waandishi wa habari kuwa lengo ni kuwafikia Madereva 500 na mpaka sasa Madereva 300 tayari wameshafikiwa katika awamu ya kwanza,

Alisema kwamba wamewafikia madereva wa pikipiki maarufu kama (Bodaboda) kuwapa mafunzo ya Usalama Barabarani na waliohitimu wamepewa vyeti huku akieleza wataendelea na kutoa elimu ya usalama barabarani kwa awamu ya pili ambao utaanza mwezi mei mwaka huu na itakuwa endelevu.

Scholastica aliwataka Madereva wa vyombo vyote vya moto kuzingatia sheria za Usalama Barabarani ili kupunguza ajali za barabarani zinazotokana na uzembe wa Madereva,

"Niwaombe Madereva wote hususani wa Bodaboda tuzingatie Usalama Barabarani tusibebe watoto chini ya miaka 9 kwa sababu hawana uwezo wa kuhimili mikikimikiki ya Barabarani na maisha yako ni muhimu zaidi kuliko pesa wanayoitafuta"Alisema


" Tuzingatie Usalama kwanza ili ajali zipungue zibakie zile ambazo haziepukiki ikiwemo kupasuka kwa tairi ,kukatika kwa stelingi au tatizo lolote la kiufundi katika vyombo vyetu vya moto"Alisisitiza Scholastica

Kwa upande wake Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika aliwataka madereva wote kwenda darasani kama sheria inavyowataka kufanya hivyo,


"Tupo hapa kutekeleza wajibu tuliopewa na Serikali ambayo ni nyie wananchi lakini sote tunafahamu kuwa Serikali mwaka jana ilitoa maelekezo ya madereva wote kwenda kusoma pamoja na kuhakiki leseni zenu,wapo baadhi yenu wametekeleza maagizo ya Serikali"Alisema


Hata hivyo alisisitiza umuhimu wao kuhakikisha wanalitekeleza suala la kusoma huku akiwataka wasifanye jambo kwa shuruti kwa sababu elimu wanayoenda kuipata kwa ajili ya manufaa yao hivyo hawana haja yakulazimishana.

Aidha aliwaonya Madereva wa Daladala kuacha tabia ya kusimamisha Daladala zao kwa muda mrefu kwenye maeneo yasiyokuwa na vituo katikati ya Jiji hili lenye mpangilio mzuri wa namba za Barabara za mitaa,

"Kwa Bahati mbaya wakati wanapangilia Jiji hili walisahau kuweka vituo vingi vya Daladala, hivyo sisi tumeona ni busara tu kwa baadhi ya maeneo kwenye Barabara za namba Daladala inaweza ikasimama kwa muda mfupi sana ili kuepusha msongamano unaoweza kujitokeza,unatakiwa utumie muda mfupi sana kupakia au kushusha abiria wako kwenye vituo tulivyoviruhusu" Alisisitiza SP.Mwamasika