ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 3, 2014

WASICHANA 30 JIJINI MWANZA WAPATIWA MAFUNZO YA SIKU TANO KUHUSU ELIMU YA UKATILI WA KIJINSIA MAJUMBANI.

Mkurugenzi wa Shiriki la KIVULINI Bw Ramadhan Masele akisisitiza jambo wakati akifunga mafunzo maalum kwa wasichana 30 walio na umri kati ya miaka 18 mpaka 25 kutoka wilaya ya Ilemela na Nyamagana za jijini Mwanza hapo jana. Wasichana hao wamepewa mafunzo kuhusu ukatili wa kijinsia majumbani pamoja na Kingono lengo likiwa ni kuzalisha waelimisha rika wengi zaidi mitaani na kutengeneza jamii isiyokuwa na ukatili wa kijinsia na kingono kwa kwa watoto wa kike.
Mkufunzi wa Masuala ya Kijinsia Bi. Tumaini Kyola akitoa mafunzo kwa kundi la Wasichana 30 ambao hawako mashuleni juu ya mbinu mbalimbali za kuelemisha jamii kuhusu masuala Ukatili wa Majumbani na wa kingono pia. Wasichana hawa wanategemewa kwenda kuwafundisha wasichana wenzao wa mitaani, kila mmoja amepewa lengo la kufikia wasichana 50. 
Baadhi ya wasichana 30 wakiwa makini kufuatilia mafunzo waliokuwa wakipatiwa na mkufunzi wao (hayupo pichani), hili ni kundi la kwanza kwa wasichana waliokuwa nje ya shule ambapo mafunzo ya kundi la pili kwa wasichana waliopo mashuleni yanatarajiwa kuanza mwezi wa sita kwa kushirikisha shule zipatazo 40 toka wilaya za jiji la Mwanza.

Wasichana thelathini pamoja na Mkufunzi wao na baadhi ya maafisa wa Kivulini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza mafunzo hayo ya siku tano hapo jana katika ukumbi wa VETA jijini Mwanza.


MKURUGENZI wa shirika la kutetea Haki za Wanawake na Wasichana KIVULINI lenye makao yake makuu jijini Mwanza Bw. Ramadhan Masele amefunga rasmi mafunzo ya siku tano yanayolenga  kuwajengea wasichana uwezo wa kutoa elimu juu ya masuala ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia chini ya mradi wa kuwashirikisha vijana kuzui Ukatili wa majumbani ikiwa ni pamoja na ukatili wa  kingono kwa watoto wa kike na wasichana.  

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo Bw. Masele aliwataka washiriki wote kutumia elimu hiyo muhimu waliyoipata kutoa elimu na kuongeza uwelewa zaidi kwa jamii yao kuanzia ngazi ya familia, marafiki na vikundi mbalimbali na kuwa chachu ya mabadiliko  juu ya kupigania haki za wanawake na wasichana wanaonyanyaswa kijinsia katika jamii zao.

“Imani yangu ni kuwa semina hii itakuwa ni kiwanda kizuri cha kuwatengeneza nyinyi wote kuwa mabalozi wazuri katika jamii, baada ya mafunzo haya tunaamini kuwa mtakuwa chachu ya mabadiliko katika kutetea na kulinda haki za wanawake na wasichana kwa kukemea, Kupinga, kuripoti na kuzuia aina zote za ukatili wa majumbani na kingono kwa wasichana na wanawake na kutoa taarifa pindi vitendo hivi vinapotokea” alisema Bw. Masele

“Kila mmoja aliyehudhuria mafunzo haya  kwa nafasi aliyonayo tunaamini anaweza kuwa chachu ya mabadiliko endapo atatimiza wajibu wake kwenye eneo analoishi. Hili suala la ukatili wa kijinsia si suala geni nchini hasa eneo hili la kanda ya ziwa hivyo kuna kila sababu ya kuzidisha mapambano dhidi yake, cha muhimu ni kuzingatia mafunzo mliyopewa na muwezeshaji wenu” aliongeza Bw. Masele.

Mafunzo hayo yamefanyika kwa muda wa siku 5 kwa vijana 30 wa kike wenye umri kati ya miaka 18-24 kutoka wilaya mbili za Nyamagana na Ilemela jijini Mwanza. Lengo la Mafunzo ni kuwajengea vijana uwezo wao binafsi na uwezo wa kuelimisha jamii hasa Vijana wenzao  kupambana na kupinga Ukatili dhidi ya wanawake na wasichana katika maeneo wanayoishi.

Mafunzo yalianza Jumatatu tarehe 28 Aprili, 2014 mpaka tarehe 2 Aprili, 2014 katika Ukumbi wa Chuo cha Ufundi Stadi, VETA kilichopo Nyakato nje kidogo ya jiji la Mwanza.

Takwimu zinaonyesha bado jamii inakabiliwa na ukatili mkubwa wa kijinsia ambapo ubeberu wa wanaume pamoja na mila na desturi potofu zimeonekana kukandamiza jinsi ya kike zaidi kuliko jinsi ya kiume, ukatili huo ni wa kijamii, kiuchumi pamoja na kisaikolojia hivyo kunaitajika juhudi za dhati na makusudi kuweza kukabiliana na tatizo lilopo kwa jamii.

Akimalizia mawaidha yake kwa washiriki Bw. Masele alisema lengo la mafunzo hayo ni kuona mabadiliko katika mfumo juu ya kujali na kuheshimu haki za mwanamke na wasichana, kwani jamii nyingi zinapambana na mifumo miwili mikubwa, ambayo ni mfumo dume ambao umekuwa ukiwakandamiza wanawake katika jamii na mfumo wa kitabaka unaoongeza nafasi kati ya matajiri na masikini.

Shirika la KIVULINI kwa kushirikiana na Asasi ya Vijana  inayojulikana kama Wadada Centre for Solution Focus Approach ndio waandaji wa mafunzo hayo kupitia mradi wa kuwashirikisha vijana kuzui Ukatili majumbani na Ukatili wa Kingono chini ya ufadhili wa Shirika la terre des hommes ch (tdhschweiz) - Fursa kwa Vijana  la nchini Switzerland

Kivulini ni shirika lisilo la kiserikali linalojishughulisha na kutetea pamoja na kulinda Haki za Wanawake na Wasichana. Shiriki la Kivulini linahamasisha jamii (Wanawake, Wanaume na Vijana ) kulinda, kutetea Haki za Wanawake na Wasichana kwa kupinga vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia. Makao makuu ya shirika yapo jijini Mwanza, Wilaya ya Ilemela, Tanzania.

DC BUNDA AZUA MASHINDANO YA ESTHER BULAYA 2014 KWA SABABU ZA KISIASA.

Kunyanyua vipaji ni pamoja na kutoa vifaa kwa vijana washiriki. Jeh! juhudi hizi za msingi za Mhe. Esther Bulaya tunaziruhusu kuteketea kwa matakwa ya wachache wenye ubinafsi? 
Na Augustine Mgendi-BUNDA

Serikali wilaya ya Bunda Mkoani Mara imesitisha Mashindano ya Esther Bulaya ambayo yamekuwa yakifanyika kila Mwaka wilayani humo kwa kile kinachodaiwa baraza la michezo wilayani humo kutoridhishwa na Mazingira ya uwanja wa Sabasaba unatumika kwa Mashindano hayo.

Mwenyekiti wa Mashindano hayo ya Esther Bulaya Bw Flavian Nyamageko alisema Mashindano hayo yamekuwa yakifanyika katika uwanja huo lakini pia wakishirikisha viongozi wa chama cha Soka wilayani humo lakini leo wanashangazwa na kitendo cha chama hicho cha soka kusitisha Mashindano hayo

Mwenyekiti huyo alisema kuwa alipojaribu kuuliza sababu ya kusitishwa kwa Mashindano hayo  viongozi wa Chama cha Soka wilaya ya Bunda wamemweleza ni agizo kutoka kwa mkuu wa wilaya.

 'Tumekuwa tukifanya haya Mashindano kila mwaka tena kwa ufanisi Mkubwa,juzu tumeanza mashindano baada ya kupewa kibali na Chama cha Soka wilaya lakini tunashangaa leo tunaambia tusifanye Mashindano hayo kwa sababu ambazo hazina msingi"alisema Mwenyekiti huyo

Akieleza sababu ambazo zimeainishwa katika barua hiyo Bw Nyamagelo alisema kuwa zipo sababu tatu ambazo zimeelezwa kuwa ni Mazingira kutokuwa rafiki ya kiuchezaji,Chombo kinachotakiwa kuendesha mashindano hayo ni Chama cha Soka na si mwingine,kutokuwepo kwa usalama wa kutosha kulingana na watu wanaohudhuria.

Kiukweli kwetu sisi tunaona hii ni kupingana na ilani ya chama cha Mapinduzi katika kuendeleza Michezo,aliongeza kuwa huu ni mwaka wa nne katika kuandaa mashindano hayo.

Alipotafutwa  Afisa Michezo wilaya ya Bunda mkoani hapa Bw Amos Mtani alisema  ofisi yake bado haijapokea barua yoyote inayoonyesha kusitishwa kwa Mashindano hayo ingawa nakala ya barua hiyo ambayo waandishi wa habari wameipata wilayani hapa inaonyesha  kueleza kutekeleza agizo la Mkuu wa wilaya hiyo lakini afisa michezo huyo hakufika katika kikao hicho.

Wakiongea kwa jazba na waandishi wa habari baadhi ya wadau wa soka wilayani hapa walisema kuwa ni hatari sana kama suala la kisiasa linaingia katika michezo maana kwa hilo inaonekana ni mambo ya kisiasa.

Bw Marwa Juma ambaye alisema kuwa amekuwa mfuatiliaji wa mashindano hayo tangu yameanza amesikitishwa na kusitishwa kwa Mashindano hayo ya Esther Bulaya  Mwaka 2014 kwa kile kinachodai hali ya kiusalama si nzuri lini fujo ilitokea ? alihoji bw Juma

"Tukiendelea kuchanganya chuki na siasa hatutainua michezo katika wilaya yetu" alisema Bw Marwa

Mashindano ya Esther Bulaya yamekuwa yakifanyika kila mwaka kwa misimu minne Mfululizo kwa kuandaliwa na Mbunge wa viti Maalum kupitia vijana ambapo yamekuwa yakiibua vijana  mbalimbali ambapo mwaka huu yanashirikisha timu 72 na wachezaji 1440  katika vituo vya Bunda,Mgeta na kituo cha Nyamswa

Friday, May 2, 2014

JAPO KIDUCHU PICHA ZA MEI MOSI MWANZA NA SENGEREMA.

Askari wa kikosi cha usalama barabarani wilayani Sengerema akiongoza maandamano ya maadhimishio ya siku ya wafanyakazi duniani Mei mosi mjini humo.
Wafanyakazi wa sekta wa mashirika ya serikali, taasisi na makampuni ya watu binafsi walishiriki zoezi hilo. 
Maandamano wilayani Sengerema.
Imependeza.
 "Inapendeza kujumuika japo mara moja kwa mwaka na kujadili changamoto zetu" Kama wanasema wafanyakazi hawa wa wilayani Sengerema.
Ni kutoka Sengerema na sasa tueleke Mwanza mjini (Fuatilia picha zinazo fuata.)
Jijini Mwanza maandamano yafanyika na kuishia Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.
Meza kuu Mkuu wa wilaya ya Ilemela Amina Masenza (Kushoto) akiwa na Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga wakifurahia yanayojiri toka maonyesho ya wafanyakazi kupitia maandamano.
Wakiteta jambo ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nyamagana Raphael Shilatu (kushoto) na Mkuu wa wilaya ya Ilemela Amina Masenza.
Kama sehemu ya kuboresha afya kwa njia ya mazoezi huyu ni mshindi wa mbio za kufukuza kuku upande wa wanawake ni kutoka TANROAD Mwanza Bi. Mariam John.
Mshindi wa mbio za kufukuza kuku wanaume ni Spilian Kaburu kutoka TANESA.
Michezo ya Nyoka ni jadi ya ngoma za Mwanza.


Chezea burudani macho yote ya wanausalama kwenye 'utamu'.

JOSE CHAMELEONE APAGAWISHA MASHABIKI MWANZA NAYE APAGAWA AMWAGAFEDHA KWAO

Ni msanii Dr. Jose Chameleone kutoka nchini Uganda akiwa na mashabiki wake wakishow love na G. Sengo Blog katika usiku wa kuamkia leo ndani ya Villa Park Resort jijini Mwanza, ambapo msanii huyo alipiga show matata ambayo haijawahi kutokea kiasi cha kutii kiu za mashabiki wake waliojitokeza kwa idadi kubwa usiku huo.
Kila mmoja aliyetia timu hapa ndani alimkubali kwa kile alichokuwa akifanya.
Dah sipati picha engo za Ma-Instagram, Face Book na Twitter....zilijaaje mapix ya tukio...!!!!
Wimbo: "Jamila analia bwana wake amemuacha......!!"
Jose ana kwa ana na mashabiki wake!!
Battle hatariii!!
The zoom from behind.
Kutoka stage ilikuwa ni kazi nzito kupata picha, kwani kulikuwa full ile mbayaaaaaa na muvmenti zilikuwa si za kitoto!!!
Sing with me....!!
Lilipigwa Pose kisha track ya Tubonge ikafuatia....!!!
TUBONGE LIVE.
Shabiki huyu alipandwa na mzuka kiasi cha kupanda kwa stage kuonesha mavitu, kilichofuatia mara baada ya hapo ni Chameleone kuanza kumtunza na mihela! 
Hapa zilimwagwa fedha kiasi cha box kadhaa ikawa ni fursa ya kujizolea.
Chameleone na shabiki wake wakichukuwa U-Kodak kwa G. Sengo blog.

Wow oh my my......
Ulipopigwa wimbo wa BADILISHA nyomi ya akinadada ikavamia stage kucheza.
Somo limekubalika.
Hapa akizungumza na shabiki zake kwa lugha mama (Kiswahili)
DjZ'
Jose Chameleone (L) akipata picha ya pamoja na kiongozi wa bendi inayotumbuiza Villa Park, naizungumzia  Super Kamanyola mwanamuziki Roy Mukuna (C).

NYAMA CHOMA FESTIVAL JUMAMOSI HII MWANZA.


PLAY KUSIKILIZA MPANGO MZIMA.

Thursday, May 1, 2014

JOSE CHAMELEONE KUKISANUKISHA USIKU HUU NDANI YA VILLA PARK MWANZA.

Dr. Jose Chameleone akiwakilisha 88.1 Mwanza.
Crew lililo shiba toka kushoto ni Promota maarufu kutoka Geita, Rammadhan Maganga, Dr. Jose Chameleone na Dj Maliz.
Salute!!
Manager Ramma (L), Chemeleone (C) na Dj Maliz (R).
Uskose!!!!

ASASI TANO KANDA YA ZIWA ZINAZOPATA RUZUKU TOKA MFUKO WA MSAADA WA KISHERIA (LSF) ZAMALIZA ZIARA YA SIKU 3 SHIRIKA LA KIVULINI

 Mkurugenzi wa Shirika la KIVULINI Bw Ramadhan Masele akifunga ziara ya kimafunzo ya siku tatu kwa kutoa shukrani kwa maafisa toka mashirika matano ya mikoa ya kanda ya ziwa (hawapopichani) pamoja na maafisa toka Mfuko wa Msaada wa kisheria (LSF) na Foundation for Civil Society kwa ziara hiyo yamafunzo.

Mwana kijiji wa kata ya Mwamala Wilaya ya Kwimba Bi. Grace Masanja akieleza msaada wanaopata juu ya elimu na ushauri wa kisheria toka kwa msaidizi wa kisheria katika kata yao, Bi. Grace alitanaibisha kwamba bado kuna tatizo kubwa la unyanyasaji wa kijansia unaofanywa na wanaume dhidi ya wanawake licha ya elimu ya haki za kilajinsi zinatolewa kila siku na kuwaomba wadau washeria kuzidisha nguvu kuweza kukomesha tabia za wanaume kupiga wanawake.

Mwanakijiji wa kata ya Mwamala Bw. James Ngosha akiwashukuru wageni toka KIVULINI pamoja na washirika wengine kwa msaada wa kuwapatia muelimishaji wa haki na sheria katika kata yao kwani amekuwa akiwasaidia sana katika kutatua migogoro ya ardhi kijijini kwao.

 Baada ya kumaliza ziara ya kutembelea kata za Ngudu, Mwamala na Hungumalwa katika wilaya ya Kwimba maafisa toka Asasi tano za kanda ya ziwa pomoja na wawezeshaji wa KIVULINI, LSF na Foundation for Civil Society wakifanya tathmini ya ziara yao nzima ya siku tatu katika kijiji cha Mwamala.


ASASI TANO KANDA YA ZIWA ZINAZOPATA RUZUKU TOKA MFUKO WA MSAADA WA KISHERIA (LSF) ZAMALIZA ZIARA YA SIKU 3 SHIRIKA LA KIVULINI

Maafisa Miradi pamoja na Maafisa Wakaguzi na Tathmini Miradi toka mashirika matano ya Kiraia yanayopata ruzuku kutoka Mfuko wa Msaada wa Kisheria (LSF) Tanzania, yamemaliza ziara ya kimafunzo ya siku tatu katika Shirika la Kutetea Haki za Wanawake na wasichana Tanzania, KIVULINI la jijini Mwanza, ziara iliyolenga kujifunza na kuboresha ufanyaji kazi wa mashirika hayo kupitia Miradi mbalimbali inayoendeshwa na KIVULINI.

Mashirika hayo matano toka mikoa ya Kagera, Shinyanga, Mara, na Tabora yalianza mafunzo hayo Jumatatu ya tarehe 28 Aprili, 2014 na kumaliza mafunzo hayo tarehe 30 Aprili, 2014 kwa kutembelea Wasaidizi wa Kisheria wanaofanya kazi ya kutoa elimu na ushauri wa kisheria katika vijiji mbalimbali vya Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba chini ya shirika la KIVULINI kupitia mradi wa Msaada wa Kisheria unaofadhiliwa na LSF.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa Ziara hiyo Mkurugenzi wa Shirika la KIVULINI Bw. Ramadhan Masele aliwashukuru maafisa wote toka mikoa hiyo mitano ya kanda ya ziwa kwa kuhudhuria mafunzo hayo lakini pia aliwashukuru Mfuko wa Msaada wa Kisheria kwa heshima waliyowapa KIVULINI kuwa kituo cha mafunzo kwa asasi nyengine.

“Ziara hii imetoa hamasa nzuri hasa kwa upande wa kimahusiano baina ya Asasi zinazotekeleza mradi wa msaada wa kisheria kwa kanda ya ziwa, pia uzoefu tuliobadilishana kwa siku zote tatu za mafunzo naamini utaenda kuimarisha utendaji kazi wa asasi zetu na kuinua hali ya maisha ya Watanzania kupitia sisi” alisema Mkurugenzi wa KIVULINI Bw Ramadhan Masele.

“Lakini pia tuwashukuru wadau wetu wakubwa katika mradii huu wa msaada wa kisheria, LSF, kwa ubunifu waliouleta wa kutuwezesha kukutana pamoja na kubadilishana uzoefu katika utendaji kazi, na hivyo hivyo shukrani zetu ziende kwa Foundation for Civil Society kwa kushirkiana na SLF kuwa pamoja nasi, tunaomba huu uwe ni mwanzo tu na usiwe mwisho” alimalizia Bw Masele

Ziara hiyo imeratibiwa na LSF kwa kushirikiana na Foundation For Civil Society kutoa hamasa na kuinua utendaji kazi wa Asasi za Kiraia nchini katika kuhakikisha asasi hizo zinatoa matokeo bora katika mradi wa Msaada wa kisheria.

Mashirika yaliyohudhuria ziara hiyo ya Kimafunzo ni Jamii Salama Development Volunteers (JSDV) toka Tabora, Centre for Widows and Children Assistance (CWCA) la mkoani Mara, Mama’s Hope Organization for Legal Aid (MHOLA), Paralegal Aid Centre Shinyanga (PACESHI), Sheria na Haki za Binadamu (SHEHABITA) la mkoani Mara.

AJALI YA MAGARI MATANO KWA MPIGO.

Alfajiri hii ajali imetokea ikikusisha magari matano katika eneo la Miseyu baada ya Mikese kuelekea mpakani mwa Pwani na Morogoro. Chanzo cha ajali hiyo kinatajwa kuwa ni dereva wa roli la Nyanya aliyekuwa mbele kusinzia huku akiendesha gari.
Magari matano kwa pamoja yakiwa kwenye msafara mrefu wa malori yamekumbwa na ajali hiyo baada ya kutokea kasoro kwa moja ya magari hayo. Trafiki takriban sita wako eneo la tukio uchunguzi unaendelea kung'amua makosa zaidi yaliyo sababisha ajali hiyo.
Ni magari yenye bidhaa mbalimbali tofauti tofauti.
PICHA NA MDAU WA BLOGU HII: Kimori Ngwasuma.