NA ALBERT G. SENGO
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko Januari 10, 2025 amesema kuwa ukuaji wa uchumi wa nchi yoyote unategemea upatikanaji wa nishati ya uhakika na yenye gharama nafuu. “Kwa nchi yoyote inayotaka kukua kwa kiasi kikubwa inategemea Nishati inayopatikana kwa hakika na yenye bei nafuu, Bila nishati ya gharama nafuu, uchumi utabadilika na bidhaa zitazalishwa kwa gharama kubwa zaidi,” amesema Dkt. Biteko. Dkt. Biteko amesisitiza kuwa serikali imejipanga kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana kwa gharama nafuu ili kuchochea Maendeleo ya kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi. #samiasuluhuhassan #naibuwazirimkuuFriday, January 10, 2025
NYAMKA ATEMA CHECHE KWA WENYEVITI WAPYA SERIKALI ZA MITAA KATA YA PANGANI
NA VICTOR MASANGU, KIBAHA
Nyamka ameyasema hayo wakati wa halfa fupi ya kuwapongeza wenyeviti wa serikali za mitaa iliyofanyika katika mtaa wa Vikawe Shule kupitia tiketi ya CCM waliopo katika kata ya Pangani Halmasahuri Kibaha mjini ambao wameweza kuibuka ushindi wa kishindo na kufanikiwa kuichukua mitaa yote nane iliyopo ndani ya kata ya Pangani.
Nyamka alisema kwamba kwa sasa wenyeviti wa serikali za mitaa ambao wamechaguliwa wanapaswa kutambua kwamba wamechaguliwa kupitia tiketi ya cahama cha mapinduzi (CCM) hivyo wanawajibu mkubwa wa kuhakikisha kwamba wanatekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kutekeleza ilani ya chama ikiwa pamoja na kuwatumikia wananchi kwa kuwaletea kasi ya maendeleo na sio vinginevyo.
Aidha Nyamka aliwapongeza kwa dhati wenyeviti wote kutoka mitaa yote nane iliyopo katika Kata ya Pangani na kuwahimiza kwa sasa wanatakiwa kuungana kwa pamoja na kuweza kujiandaa na uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa 2025 ili wagombea wa CCM katika nafasi za Udiwani, Ubunge, pamoja na Urais waweze kushinda kwa kishindo.
"Ndugu zangu tumemaliza uchaguzi wa serikali za mitaa lakini kitu kikubwa ninawaomba wenyeviti wote katika mitaa yote 73 ya Kibaha mji ambao wamechaguliwa kwa kishindo ni kujipanga sasa na kuelekeza nguvu zao zote katika uchaguzi mwingine na kupambana kwa hali na mali kama wao walivyopambaniwa mpaka wakaweza kushinda,"aliongeza Nyamka.
Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa serikali ya mtaa wa Vikawe shule Shaban Shaban amewashukuru kwa dhati wanachama wote wa ccm,viongozi pamoja na wananchi kwa ujumla kwa kuweza kumchagua kuwa kiongozi wao pamoja na kuweza kuwatumikia katika mambo mbali mbali ya kimaendeleo.
Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa ameahidi kuitumia nafasi hiyo ambayo amepatiwa kwa kuweza kuhakikisha kwamba anaweka mikakati madhubuti ya kuweza kushirikiana bega bega na wananchi pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini kwa ajili ya kuweza kuleta chacu ya maendeleo katika nyanja mbali mbali.
"Kwa kweli nipende kuchukua fursa hii ya kipekee kwa wanachama wote wa CCM,kwa kuweza kunipa kuranyingi ambazo zimeweza kupelekea ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Vikawe shule na mimi kwa nafasi yangu nitakuwa mstari wa mbele katika kusikiliza changamoto mbali mbali ambzo zinawakabili wananchi ili ziweze kufanyiwa kazi,"alisema Mwenyekiti Shabani.
Naye Diwani wa Kata ya Pangani Agustino Mdachi alisema kwamba atahakikisha anashirikiana na wenyeviti wote ambao wameweza kushinda ili waweze kusikiliza changamoto mbali mbali za wananchi zinazowakabili katika nyanja za afya, elimu,maji pamoja na mambo mengine ya msingi na kuzitafutia ufumbuzi.
Nao baadhi ya viongozi wa CCM mtaa wa Vikawe shule wamepongeza kwa dhati Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kibaha mjini Mwalimu Mwajuma Nyamka pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka kwa kuweza kuwa mstari wa mbele kutekeleza Ilani ya Chama kwa vitendo ikiwa sambamba na kuwaletea maendeleo wananchi katika nyanja mbali mbali.
TUNDU LISSU: "HAKUNA TENA KUIMBIANA MAMBO YA MARIDHIANO YASIYOKUWEPO"
Katika sehemu hii ya pili ya mazungumzo na BBC, Tundu Lissu anaanza kwa kumueleza Sammy Awami ikiwa atachaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chadema, uongozi wake utakuwa wa 'mshike mshike' na uliojaa mapambano ya kudai mabadiliko ya kisiasa nchini
#bbcswahili #siasa #tanzania Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili
Thursday, January 9, 2025
RAS LINDI:BIL7.8 ZA MTAMA ZIKAMILISHE UJENZI WA SHULE KWA WAKATI
WALIOKOSA HUDUMA YA MAJI TANGU NCHI IPATE UHURU SASA WACHEKELEA.
MWANDISHI:- VICTOR MASANGU, PWANI
IMESOMWA NA ALBERT G.SENGO
Baadhi ya wananchi Wilayani Bagamoyo hususan wakinamama wakizungumza katika nyakati tofauti wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri wa maji Mhandisi kundo Methew ya kutembelea miradi mbali mbali hawakusita kumshukuru kwa dhati Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwakomboa na kuwatua ndoo kichwani kwani hapo awali walikuwa wanateseka kutembea umbari mrefu kwa ajili ya kufuata huduma ya maji.
Naibu Waziri wa maji Mhandisi Kundo Methew amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani yenye lengo la kuweza kutembelea miradi mbali mbali ambayo inatekelezwa na Dawasa pamoja na Ruwasa ikiwa pamoja naa kusikiliza kero na changamoto kutoka kwa wataalamu ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi.
Wednesday, January 8, 2025
IJUWE NYUMBA YA KWANZA YA MWALIMU NYERERE ALIYOJENGA NDIPO AKARUHUSIWA KUOA
NA ALBERT GSENGO/ BUTIAMA/ MARA
WENGI wanafahamu nyumbani kwa Baba wa Taifa katika eneo la Mwitongo, Kijiji cha Butiama, mahala alipozikwa pia, pale ambapo sasa ni eneo la kivutio cha utalii. Lakini Jeh unaijua nyumba ya kwanza kabisa ya Hayati Baba wa Taifa ambayo kwa mila na desturi za Wazanaki alipaswa kujenga au kumiliki nyumba ili kuwa na sifa ya kuoa? Kwa siku ya leo tunaye mtoto wa sita kati ya watoto nane wa Hayati Baba wa Taifa huyu si mwingine bali ni Madaraka Nyerere. #samiasuluhuhassan #butiama #mwitongo #nyerereTuesday, January 7, 2025
SERIKALI YAWEKA MIKAKATI YA KUMALIZA KABISA KERO YA MAJI NCHINI - NAIBU WAZIRI WA MAJI
NA. VICTOR MASANGU, PWANI
Hayo ameyabaisha wakati akizungumza katika kikao kazi na wataalamu mbali mbali wa mamlaka za maji wa Mkoa wa Pwani ambapo amebasema kwamba lengo la serikali ni kuhakikisha inafikisha huduma ya maji safi na salama kwa kiwango cha asilimi 85 katika maeneo ya vijijini na kwa upande wa maeneo ya mjini ni kwa kiwango cha silimia 95.
Monday, January 6, 2025
MNEC KASESELA,MWAKA 2025 NI MWAKA WA KUTENDA HAKI, UTU NA UPENDO
Mjumbe wa Halmshauri kuu ya chama cha Mapinduzi taifa MNEC Richard Kasesela amesema kuwa mwaka wa 2025 utakuwa mwaka wa kutenda haki kwa kila jambo na kwa kila mwananchi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi pamoja upendo na utu kwa kila mwananchi.
Mjumbe wa Halmshauri kuu ya chama cha Mapinduzi taifa MNEC Richard Kasesela amesema kuwa mwaka wa 2025 utakuwa mwaka wa kutenda haki kwa kila jambo na kwa kila mwananchi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi pamoja upendo na utu kwa kila mwananchi.
MNEC Kasesela alisema kuwa mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi kwenye vyama vya siasa hadi uchaguzi mkuu wa kuwapata madiwani, wabunge hadi Rais hivyo ni bora ikatumika haki katika chaguzi zote.
Alisema kuwa vyombo vyote vya dola na wananchi wakitenda haki na wakitendewa haki hakutatokea vurugu kama ambavyo zinavyotokea nchi za jirani mara baada ya uchaguzi.
MNEC Kasesela alisema kuwa kila mwananchi akiwa na nidhamu kwenye maamuzi ya kutenda haki na nidhamu ya fedha na muda basi Tanzania itanufaika sana na mwaka 2025 kwa kutenda haki.
Alimalizia kwa kuwaomba viongozi wa dini nchi nzima kuwaombea viongozi wa serikali na vyama vya siasa kudumisha amani, utulivu katika uchaguzi za vyama na uchaguzi mkuu.
UONGOZI WA COREFA WAFANYA MAGEUZI MAKUBWA YA KUKUZA KABUMBU PWANI
NA VICTOR MASANGU,PWANI