ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, January 10, 2025

HIVI NDIVYO SERIKALI YA TANZANIA ILIVYOJIPANGA KUWA NA UMEME WA UHAKIKA BEI NAFUU.

 NA ALBERT G. SENGO

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko Januari 10, 2025 amesema kuwa ukuaji wa uchumi wa nchi yoyote unategemea upatikanaji wa nishati ya uhakika na yenye gharama nafuu. “Kwa nchi yoyote inayotaka kukua kwa kiasi kikubwa inategemea Nishati inayopatikana kwa hakika na yenye bei nafuu, Bila nishati ya gharama nafuu, uchumi utabadilika na bidhaa zitazalishwa kwa gharama kubwa zaidi,” amesema Dkt. Biteko. Dkt. Biteko amesisitiza kuwa serikali imejipanga kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana kwa gharama nafuu ili kuchochea Maendeleo ya kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi. #samiasuluhuhassan #naibuwazirimkuu

NYAMKA ATEMA CHECHE KWA WENYEVITI WAPYA SERIKALI ZA MITAA KATA YA PANGANI

 


NA VICTOR MASANGU, KIBAHA

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Mwalimu Mwajuma Nyamka  amewataka wenyeviti wote wa serikali za mitaa kupitia tiketi ya CCM ambao wamechaguliwa kwa kishindo katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Novemba 27 mwaka huu kutumia madaraka yao vizuri na  kufanya kazi kwa weledi na  kuwatumikia wananchi kwa  kusikiliza kero na chanagmoto zinazowakabili ili  kuzitafutia ufumbuzi katika maeneo yao.

Nyamka ameyasema hayo  wakati wa halfa fupi ya kuwapongeza wenyeviti wa serikali za mitaa iliyofanyika katika mtaa wa Vikawe Shule kupitia tiketi ya CCM waliopo  katika kata ya Pangani Halmasahuri Kibaha mjini   ambao wameweza kuibuka ushindi wa kishindo na kufanikiwa kuichukua mitaa yote nane iliyopo ndani ya kata ya Pangani.

Nyamka alisema kwamba kwa sasa wenyeviti wa serikali za mitaa ambao wamechaguliwa wanapaswa kutambua kwamba wamechaguliwa kupitia tiketi  ya cahama cha mapinduzi (CCM) hivyo wanawajibu mkubwa wa kuhakikisha kwamba wanatekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kutekeleza ilani ya chama ikiwa pamoja na kuwatumikia wananchi kwa  kuwaletea kasi ya maendeleo na sio vinginevyo.

Aidha Nyamka aliwapongeza kwa dhati wenyeviti wote kutoka mitaa yote nane  iliyopo katika Kata ya Pangani na kuwahimiza kwa sasa wanatakiwa kuungana kwa pamoja na kuweza kujiandaa na uchaguzi mkuu wa mwaka  huu wa 2025 ili wagombea wa CCM katika nafasi za Udiwani, Ubunge, pamoja na Urais waweze kushinda kwa kishindo.

"Ndugu zangu tumemaliza uchaguzi wa serikali za mitaa lakini kitu kikubwa ninawaomba wenyeviti wote katika mitaa  yote 73 ya Kibaha mji ambao wamechaguliwa kwa kishindo ni kujipanga sasa na kuelekeza nguvu zao zote katika uchaguzi mwingine na kupambana kwa hali na mali kama wao walivyopambaniwa mpaka wakaweza kushinda,"aliongeza Nyamka.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti mpya wa serikali ya mtaa wa Vikawe shule Shaban Shaban amewashukuru kwa dhati wanachama wote wa ccm,viongozi pamoja na wananchi kwa ujumla kwa kuweza kumchagua kuwa kiongozi wao pamoja na kuweza  kuwatumikia katika mambo mbali mbali ya kimaendeleo.

Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa ameahidi kuitumia nafasi hiyo ambayo amepatiwa kwa kuweza kuhakikisha kwamba anaweka mikakati madhubuti ya  kuweza kushirikiana bega bega na  wananchi pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini kwa ajili ya kuweza kuleta chacu ya maendeleo katika nyanja mbali mbali.

"Kwa kweli nipende kuchukua fursa hii ya kipekee kwa wanachama wote wa CCM,kwa kuweza kunipa kuranyingi ambazo zimeweza kupelekea ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Vikawe shule na mimi kwa nafasi yangu nitakuwa mstari wa mbele katika kusikiliza changamoto mbali mbali ambzo zinawakabili wananchi ili ziweze kufanyiwa kazi,"alisema Mwenyekiti Shabani.

Naye Diwani wa Kata ya Pangani Agustino Mdachi alisema kwamba atahakikisha anashirikiana na wenyeviti wote ambao wameweza kushinda ili waweze kusikiliza changamoto mbali mbali za wananchi zinazowakabili katika nyanja za afya, elimu,maji pamoja na mambo mengine ya msingi na kuzitafutia ufumbuzi.
Nao baadhi ya viongozi wa CCM mtaa wa Vikawe shule wamepongeza kwa dhati Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kibaha mjini Mwalimu Mwajuma Nyamka pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka kwa kuweza kuwa mstari wa mbele kutekeleza Ilani ya Chama kwa vitendo ikiwa sambamba na kuwaletea maendeleo wananchi katika nyanja mbali mbali.

TUNDU LISSU: "HAKUNA TENA KUIMBIANA MAMBO YA MARIDHIANO YASIYOKUWEPO"

 Katika sehemu hii ya pili ya mazungumzo na BBC, Tundu Lissu anaanza kwa kumueleza Sammy Awami ikiwa atachaguliwa kuwa mwenyekiti wa Chadema, uongozi wake utakuwa wa 'mshike mshike' na uliojaa mapambano ya kudai mabadiliko ya kisiasa nchini

#bbcswahili #siasa #tanzania Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili    / @bbcnewsswahili  

Thursday, January 9, 2025

RAS LINDI:BIL7.8 ZA MTAMA ZIKAMILISHE UJENZI WA SHULE KWA WAKATI

 

Katibu Tawla Mkoa wa Lindi Zuwena Omari ametoa wito kwa Menejimenti ya Halmashauri ya wilaya ya Mtama kuhakikisha wanafunzi wote waliopangiwa na kaundikishwa wanaripoti shule kwa wakati na wanakimilisha ujenzi wa shule kwa muda uliopangwa. 
Katibu Tawla Mkoa wa Lindi Zuwena Omari ametoa wito kwa Menejimenti ya Halmashauri ya wilaya ya Mtama kuhakikisha wanafunzi wote waliopangiwa na kaundikishwa wanaripoti shule kwa wakati na  wanakimilisha ujenzi wa shule kwa muda uliopangwa. 

Na Fredy Mgunda, Lindi.

Katibu Tawla Mkoa wa Lindi Zuwena Omari ametoa wito kwa Menejimenti ya Halmashauri ya wilaya ya Mtama kuhakikisha wanafunzi wote waliopangiwa na kaundikishwa wanaripoti shule kwa wakati na  wanakimilisha ujenzi wa shule kwa muda uliopangwa. 

Wito huo ameutoa leo alipotembelea halmashauri hiyo kuona maandalizi ya uripoti wa wanafunzi wa awali, darasa la kwanza na kidato cha kwanza na ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa shule zenye thamani ya Bil 7.8. 

Akizungumza mbele ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mtama, watalaamu wa halmashauri, Kamati za ujenzi na wawakilishi wa wananchi amesema , halmashauri imepata fedha nyingi ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha anasimamia vema fedha hizo.

“Wito wangu kwa viongozi wa Halmashauri ya Mtama, wakati wote tunapopokea fedha za miradi tuwe tayari kutekeleza na kimsingi serikali imekuwa ikileta fedha za miradi ya maendeleo kila mwaka kwa ajili ya miradi tofauti tupokee fedha hizi tupange utekelezaji na tuwe na usimamizi wa mara kwa mara tuhakikishe ubora na umalizikaji kwa wakati, Mkurugenzi hili ni lakwako kuhakikisha kwamba basi muda tuliokubaliana na wakandarasi wetu miradi hiyo inakamilika kwa wakati “ Zuwena Omari Katibu Tawala Mkoa Lindi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mtama Anderson D Msumba amesema wanamshukuru Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa fedha nyingi kwa mara kwanza kupata fedha hizo na amemuahkikishia Katibu Tawala Mkoa kukamilisha miradi mwezi wa Nne mwishoni.

Mwakilishi wa wenyeviti wa kutoka Halmashauri ya Mtama Juma Omari Salumu wa kijiji cha Kiwalala amemshukuru Mhe. Rais kwa mradi huo na kuahidi kutoa ushirikiano kwa wananchi na viongozi wote.

Brigita John Mponda mkazi wa kijiji hicho kwaniaba ya wananchi amesema miradi hiyo wameipokea vizuri miradi  ujenzi wa shule mpya kwani inakwenda kuwaletea elimu bora kwa watoto wao.

Bil 7.8 ya halmashauri ya Mtama inakwenda kujenga shule ya wavulana kanda ya kiwalala, ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na matundu 6 ya choo shule ya msingi Mahumbika, Ujenzi wa Shule ya mpya ya Msingi –Mtakuja Nyangao, Ujenzi wa Madarasa 5 Shule ya Msingi Simama, Ujenzi wa shule ya sekondari Mtakuja kata ya Nyangao, Ujenzi wa shule mpya ya Amali Mkoa na Ujenzi wa shule ya Sekondari kata ya Pangani.

WALIOKOSA HUDUMA YA MAJI TANGU NCHI IPATE UHURU SASA WACHEKELEA.

 MWANDISHI:- VICTOR MASANGU, PWANI 

IMESOMWA NA ALBERT G.SENGO

Zaidi ya wananchi wapatao laki mbili kutoka maeneo ya kata za Msoga pamoja na Msata Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani hatimaye wameondokana na kilio cha muda mrefu cha kuwepo kwa changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama baada ya kukamilika kwa miradi mipya ya visima pamoja na ujenzi wa tenki kubwa la maji lenye uwezo wa kujaza lita zaidi ya milioni 2.

Baadhi ya wananchi Wilayani Bagamoyo  hususan wakinamama wakizungumza katika nyakati tofauti wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri wa maji Mhandisi kundo Methew ya kutembelea miradi mbali mbali  hawakusita kumshukuru kwa dhati  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuwakomboa na kuwatua ndoo kichwani kwani hapo awali walikuwa wanateseka kutembea umbari mrefu kwa ajili ya kufuata huduma ya maji.
 
Naibu Waziri wa maji Mhandisi Kundo Methew amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani yenye  lengo la kuweza kutembelea miradi mbali mbali ambayo inatekelezwa na Dawasa pamoja na Ruwasa ikiwa pamoja naa kusikiliza kero na  changamoto kutoka kwa wataalamu ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi.

Wednesday, January 8, 2025

IJUWE NYUMBA YA KWANZA YA MWALIMU NYERERE ALIYOJENGA NDIPO AKARUHUSIWA KUOA

 NA ALBERT GSENGO/ BUTIAMA/ MARA

WENGI wanafahamu nyumbani kwa Baba wa Taifa katika eneo la Mwitongo, Kijiji cha Butiama, mahala alipozikwa pia, pale ambapo sasa ni eneo la kivutio cha utalii. Lakini Jeh unaijua nyumba ya kwanza kabisa ya Hayati Baba wa Taifa ambayo kwa mila na desturi za Wazanaki alipaswa kujenga au kumiliki nyumba ili kuwa na sifa ya kuoa? Kwa siku ya leo tunaye mtoto wa sita kati ya watoto nane wa Hayati Baba wa Taifa huyu si mwingine bali ni Madaraka Nyerere. #samiasuluhuhassan #butiama #mwitongo #nyerere

Tuesday, January 7, 2025

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI YA KUMALIZA KABISA KERO YA MAJI NCHINI - NAIBU WAZIRI WA MAJI

 NAVICTOR MASANGU, PWANI 

Naibu waziri wa maji Mhandisi Kundo Mathew amesema kwamba lengo kubwa la serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassana  ni kuendelea  kuhakikisha kwamba inatatua kero na changamoto  ikiwa pamoja na kutafuta ufumbuzi   katika  suala zima la kuboresha  upatikanaji wa maji safi na salama  kwa wananchi bila vikwazo vyovyote.

Hayo ameyabaisha wakati akizungumza katika kikao kazi na wataalamu mbali mbali wa mamlaka za  maji wa Mkoa wa Pwani  ambapo amebasema kwamba lengo la serikali ni kuhakikisha inafikisha huduma ya maji safi na salama kwa kiwango cha asilimi 85 katika maeneo ya vijijini na kwa upande wa maeneo ya mjini ni kwa kiwango cha silimia 95.

Monday, January 6, 2025

MNEC KASESELA,MWAKA 2025 NI MWAKA WA KUTENDA HAKI, UTU NA UPENDO

 

Mjumbe wa Halmshauri kuu ya chama cha Mapinduzi taifa MNEC Richard Kasesela amesema kuwa mwaka wa 2025 utakuwa mwaka wa kutenda haki kwa kila jambo na kwa kila mwananchi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi pamoja upendo na utu kwa kila mwananchi.

Na Fredy Mgunda

Mjumbe wa Halmshauri kuu ya chama cha Mapinduzi taifa MNEC Richard Kasesela amesema kuwa mwaka wa 2025 utakuwa mwaka wa kutenda haki kwa kila jambo na kwa kila mwananchi kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi pamoja upendo na utu kwa kila mwananchi.


MNEC Kasesela alisema kuwa mwaka 2025 ni mwaka wa uchaguzi kwenye vyama vya siasa hadi uchaguzi mkuu wa kuwapata madiwani, wabunge hadi Rais hivyo ni bora ikatumika haki katika chaguzi zote.


Alisema kuwa vyombo vyote vya dola na wananchi wakitenda haki na wakitendewa haki hakutatokea vurugu kama ambavyo zinavyotokea nchi za jirani mara baada ya uchaguzi.


MNEC Kasesela alisema kuwa kila mwananchi akiwa na nidhamu kwenye maamuzi ya kutenda haki na nidhamu ya fedha na muda basi Tanzania itanufaika sana na mwaka 2025 kwa kutenda haki.


Alimalizia kwa kuwaomba viongozi wa dini nchi nzima kuwaombea viongozi wa serikali na vyama vya siasa kudumisha amani, utulivu katika uchaguzi za vyama na uchaguzi mkuu.

UONGOZI WA COREFA WAFANYA MAGEUZI MAKUBWA YA KUKUZA KABUMBU PWANI

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI

Chama cha soko Mkoa wa Pwani (COREFA) katika kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya sita  Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kukuza sekta ya michezo hapa nchini imeamua kuweka mikakati kabambe ambayo itaweza kusaidia kuinua kiwango cha kabumbu kwa kuinua soka la vijana, wanawake, pamoja na soka la ufukweni  sambamba na  ujenzi wa  kiwanja cha kisasa cha mpira wa miguu.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa COREFA Robert Munisi wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano maalumu ambao umefanyika  makao makuu ya ofisi za chama hicho kilichopo eneo la kwa Mathias Wilaya ya Kibaha na kuhudhuliwa na viongozi mbali  wakiwemo viongozi wa  soka la wanawake  kwa lengo la kujadili mambo mbali mbali ya maendeleo ya mchezo huo.

Mwenyekiti huyo amesema kwamba lengo kubwa la kukutana katika mkutano huo ni  kwa ajili ya kuweka mikakati na   mipango  madhubuti katika ya uongozi wa COREFA pamoja na waandishi wa habari wa Mkoa wa Pwani ili kuweza kuona namna nzuri ya kuripoti habari za mchezo wa soka, kusikiliza maoni, changamoto, pamoja na kuelezea mafanikio ambayo yamepatikana kwa Corefa.
Munisi amebaainisha  kwamba lengo lake kubwa ni kuweza kushirikiana na waandishi wote wa Mkoa wa Pwani katika kuhakikisha wanatangaza na kuhabarisha jamii mambo  mbali mbali ambayo ynafanywa na chama ikiwemo kuweka mipango ya kuripoti habari za mchezo wa soka la vijana, wanawake, na soka la ufukweni ikiwa sambamba na kushirikiana katika mambo mbali mbali ambayo yataweza kuletaa tija katika nyanja ya mchezo wa soka ndani ya Mkoa wa Pwani.

"Kimsingi mimi kama Mwenyekiti nimefarijika sana kukutana naa ndugu zangu waandishi w habari ambapo lengo kubwa ni kuzungumza mambo mbali mbali ikiwemo mafanikio ambayo tumeweza kuyapata tangu niweze kuingia madarakani na kitu kikubwa tumeweza kufanya mambo mengi ikiwemo kupata ofisi yetu  eneo la kwa mathiasi japo kwa sasa tumepanga lakini dhumuni etu kubwa ni kujenga ofisi yetu ya Corefa ambaayo itakuwa ni ya kudumu,"alisema Mwenyekiti Munisi.

Aidha alisema kwamba kwa sasa lengo lao kubwa ni kuwa ni uwanja mkubwa wa kisasa wa mpira wa miguu ambao utatarajiwa kujengwa katika kata ya viziwaziwa Wilaya ya Kibaha na kwamba tayari wameshapokea barua ya kupewa eneo kutoka kwa uongozi wa Halmashauri ya mji Kibaha kwa ajili ya kuweza kunegaa uwanja huo ambao kwa upande wao utakuwa ni moja katika ya vitega uchumi vya chama chao.

Kadhalika amesem kwamba  sasa wameshaanza kutekeleza maagizo ambayo yametolewa ba shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) ya kuanzisha ligi ya soka la ufukweni, ikiwa sambamba na kukuza soka la vijana pamoja na soka la wanawake amablo kwa sasa katika Mkoa wa Pwani linafanya vizuri ukilinganisha na miaka ya nyuma iliyopita.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo alitumia mkutano huo kudhamini kwa dhati juhudi za mwandishi wa habari za michezo Mkoa wa Pwani Abdalalah   Zalala kwa kumpogeza na kumkabidhi cheti na kiasi cha shilingi laki moja ikiwa kama ni moja ya motisha katika utekelezaji wa majukumu yake ya kuandika na kuripoti habari za mchezo wa soka kwa kujitolea na weledi.

"COREFA inatambua mchango wa Mwandishi wa Habari za michezo Abdallah Zalala na leo tunamkabidhi zawadi ya fedha lakini tutaendelea kuwashika mkono Waandishi wote ambao watakuwa wanaandika zaidi habari za michezo za Mkoa wa Pwani,"amesema Munisi

Pia Munisi  amebainisha kwamba  Chama cha soka Mkoa wa Pwani  (COREFA)  kimejipanga na kujizatiti zaidi katika  kuhakikisha mpira unachezwa katika Wilaya zote  kwa kuzingatia sheria, taratibu, kanunu, miongozo na katiba ya vyama ngazi ya Wilaya, Mkoa, pamoja na Taifa ili kuepusha migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza na kwamba wataendelea kushirikiana bega kwa bega  na wadau wa mchezo  wa soka  ndani ya Mkoa wa Pwani lengo ikiwa mashindano na ligi zote zifanyike kama ilivyopangwa kwa mujibu wa ratiba ya TFF.