ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, January 1, 2011

MLIPUKO WA VODACOM NA MAKARIBISHO YA 2011 ILIVYOFANA NDANI YA JIJI LA MIAMBA.

'Haya sasa ugomvi huo' na anaye utaka ni Mnyamwezi' Mr. Hills-So-GooD wa Passion fm ndani ya kitaa cha eneo la tukio.

Mwamba wa kaskazini Joe Makini juu ya Red Capet la Milipuko ya VODACOM.

Watu toka mataifa mbalimbali nao walijumuika kulipuka.

Ni wadada watatu wanaounda kundi linaloitwa 'FAGIO' kutoka nchini uganda, askwambie mtu watamu ile kinyama.

Hapa ngoma sambamba na dance zilipigwaaaaaa', kisha wakaganda hivi kwa style, then chezo likaendelea.

Wanadada wa kundi la FAGIO wakivuma kwao zaidi, Kundi hili Ni mara ya kwanza kufanya show Tanzania na kutokana na ubora waliouonesha wananchi hawakusita kuwapa shangwe.

Producer Q.toka MO Record akiwa na mkewe (walioketi) pamoja na ma-member wa MO Record, wakifuatilia show kwa umakini.

Juma Nature 'wacha awalipue watu'

Raha ya utamu!!

Burudani ilinogeshwa na mpambano baina ya vijana hawa wa VHT (Victoria House of Talent) kutoka Zoo' (Mwanza) pamoja nao THT (Tanzania House of Talent)ktoka Dizim' (Dar es salaam). "Mashabiki walijitenga"

Mavijana ya THT...

Street ili shine ile mbayaaaaaaa!!

THT...Take 2

Dj Chriss (kulia) along side meneja wa FAGIO toka nchini Uganda.

Inspector Haroun aka 'BABU' naye alikuwepo siyo kwa show bali kula maisha.

Watu walifunga mtaa kisha lkapigwa burudani NZURI isiyo kifani, Humo ndani kila kitu kikipatikana, kuanzia burudani, vinywaji, vyakula aina zote, Flowerz nzuri tena zenye kunukia, usalama full yaani kila kitu. aaaaaaaah MILIPUKooooooo!!

Thursday, December 30, 2010

POLISI MWANZA WAINUSURU BENKI YA BOA NA UVAMIZI. WANASA MMOJA BAADA YA MWINGINE.

Jeshi la polisi mkoani Mwanza linafanikiwa kuwanasa watu wanne waliokuwa katika mpango wakufanya uvamizi katika benki ya BOA iliyopo mtaa wa Kaluta jijini hapa.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Mwanza Simon Sirro amesema kuwa mara baada ya jeshi lake kupata taarifa kutoka kwa wasiri wake kuwa kuna watu wamejipanga kuvamia benki hiyo, waliweka mtego na hatimaye kufanikiwa kumkamata mtu mmoja aliyetajwa kwa jina la Donard Charles (28) mfanyakazi wa zamani wa benki hiyo aliyetimuliwa kazi.

Baada ya kuhojiwa na maafisa wa polisi, Charles alikiri kuhusika na mpango huo wa uvamizi na kusema kuwa kabla ya kukamatwa, yeye pamoja na wenzake wengine watatu walipanga uvamizi huo ufanyike mnamo tarehe 21 disemba 2010.

Ndani ya maelezo yake mtuhumiwa huyo amesimulia kuwa mara baada ya kufukuzwa kazi alifanya mpango wa kutafuta watu wengine watatu ili apate kushirikiana nao katika mpango huo haramu ambao nao tayari wamekwisha kamatwa.

Kamanda amewataja watu hao wanaoshikiliwa kuwa ni Henry Juma Salehe (32) ambaye ni shoe shine jijini Mwanza, Emanuel Masamilo (27) anayejihusisha na udalali pamoja na Wachu Kaloboka mkazi wa Kahama mkoani Shinyanga ambaye ndiye mwenye siraha ambayo ilikuwa itumike kutekeleza uvamizi huo.

TRENI LA KWENDA KIGOMA KULA SIKUKUU LAANZA .......

WAZIRI wa Uchukuzi, Omary Nundu amezindua safari ya treni ya pili inayosimamiwa na Kampuni ya Reli nchini (TRL) Kwenda Mkoa wa Kigoma kufuatia shida ya usafiri inayowakabili wakazi wa mkoa huo. Kuzinduliwa kwa treni hiyo kunatarajiwa kupunguza adha ya usafiri inayowakabili wakazi wa mkoa huo kwa kipindi kirefu sasa.
JE HUDUMA HII NI KWA SIKUKUU TU?
Akizungumza na baadhi ya abiria waliokuwa ndani ya treni hiyo jana,Waziri Nundu alisema kuzinduliwa kwa treni hiyo kutawasaidia wananchi kwenda kusheherekea sikukuu ya mwaka mpya ambapo Serikali imeamua kuruhusu treni hiyo ianze kazi ili kusafirisha abiria wanaopenda kwenda kula sikukuu ya mwaka mpya katika mikoa ambayo treni hiyo inapita.
STESHENI YA MWANZA, ZAIDI YA KUSAFIRISHA MIZIGO, KITUO HIKI HAKIJATOA HUDUMA YA USAFIRI KWA ABIRIA TANGU ZILIPOSITISHWA HUDUMA ZA TREN.
Hata hivyo wakati Nundu akizindua safari ya treni hiyo ilibainikia kwamba menejimenti ya Shirika la Reli nchini (TRL) inayongozwa na wawekezaji kutoka India hawakufurahishwa na hatua ya waziri huyo kuzindua safari hiyo. “Hii safari ni kiini macho kwa sababu wawekezaji hawaipendi na wameahidi kuisitisha baada ya sikukuu ya mwaka mpya” alisema mmoja wa wafanyakazi wa TRL huku akiomba jina lake lihifadhiwe.

Usafiri wa treni umezidi kudorora kila kukicha huku msongamano wa abiria ukizidi kuongezeka ndani ya treni kiasi cha kusababisha kero kwa abiria.

Wednesday, December 29, 2010

MWANZA KUUAGA MWAKA KWA STYLE YAKE : NI KATIKA USIKU WA MLIPUKO WA VODACOM.

Huu ndiyo mpango mzima!
Hawa ndiyo FAGIO kundi muziki wa ragga toka nchini Uganda wanaotegemewa kushuka, kukamua na kufanya mchuano FULANI HIVI kwani siku hiyo THT toka dar, VHT toka rock city wote watapanda stage HILO-HILO katika siku tutakapofunga mtaa wa posta na Nyamagana jijini Mwanza, na kisha pale kati MAKAMUZzzz ya BURUDANI zilizoshiba jicho lako likisaidiwa na KITU cha BIG SCREEN na maDVJ toka Uganda, INSHU NZIMA ni tarehe 31 mkesha wa kuuga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka mpya 2011.

USIKU WA TAREHE 31DECEMBER SAA SITA KAMILI WANGOJEWA KWA HAMU.........!!!!

Tumeisikia sana, tumeitamani sana na sasa twaenda... Kuiona Kupitia king'amuzi cha Star Times channel namba 8. "Ni kama kufungua mwaka na thamani mpya ndani ya nyumba"

ARUSHA - MWANZA - DODOMA

AAaaaaaaaa YUUUUUUUU REDeeeeeeeeee!!!....................!!!!!

!!...........................KITU HEWANI............................!!

HAWA NDIYO BORA KWA 2010.

Kwa kutambua mchango unaotolewa na wasanii wetu katika tasnia ya filamu mtandao huu umeguswa na kazi za wasanii hawa na kuwatambua kwa kuwatangaza, kulingana na zoezi tulilokuwa tunaliendesha la BORA ZA 2010, wadau hawa wamechaguliwa na wapenzi wa filamu hapa nchini kupitia tovuti ya www.filamucentral.co.tz kuanzia mwanzo wa mwezi december katika mtandao huu wa habari za filamu kutoka Swahiliwood.

Tunawapongeza wale wote walioshinda na kuibuka washindi katika nafasi walizoshiriki, kila aliyeingia katika mtanange huu alikuwa ni bora lakini siku ya siku tuliitaji mshindi mmoja ambaye ndiye tunamtngaza leo hii, tumefarijika sana kwa ushirikiano mlioonyesha wadau wa tasnia hii toka mwazo wa zoezi hili hadi mwisho, tunapenda kuwatambua waliotikisa mwaka 2010 na kusema Hongera.
BORA ZA 2010


1. Msanii chipukizi bora za 2010 – HANIFA DAUDI (Jenifer)
2. Muigizaji bora wa kike — YVONNE CHERRYL (Monalisa)
3. Muigizaji bora wa kiume — STEVEN KANUMBA (The Great)
4. Mwandishi bora wa mswaada – ALI YAKUTI
5. Mchekeshaji bora – ATHUMAN MUSSA ( KING MWALUBADU)
6. Filamu yenye kava bora – DANGER ZONE
7. Mtayarishaji bora wa filamu – STEVEN KANUMBA
8. Kampuni bora ya utengenezaji filamu – RJ Company
9. Msambazaji bora – Game 1st Quality
10. Muongozaji bora – VICENT KIGOSI (Ray The Greatest)

Matokeo haya ni kwa mujibu wa watembeleaji wa mtandao huu ndani na nje ya nchi.

ZAIDI TEMBELEA filamucentral.co.tz

LIGI KUU YA ENGLAND SHUGHULI PEVU KILELENI.

Meneja wa Chelsea, Carlo Ancelotti, amewatonya wachezaji wake, hawana budi kuzinduka usingizini kabla matumaini yao ya kuutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya England hayajayeyuka. Chelsea walikubali kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Arsenal na sasa wamecheza michezo sita ya ligi bila chereko na wameporomoka hadi nafasi ya nne ya msimamo wa ligi.Ushindi wa mwisho kwa Chelsea msimu huu wa ligi, ilikuwa tarehe 10 mwezi wa Novemba dhidi ya Fulham. Alipoulizwa ni kwa muda gani mmiliki wa Chelsea, Roman Abramovich, ataendelea kuwa mvumilivu, Ancelotti alijibu: "Sijui. Kwa vyovyote vile hatakuwa mwenye furaha wakati huu."

Mechi za jana Manchester City ilipojisogeza hadi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Soka ya England kwa ushindi wa bao 4-0, wakati Mario Balotelli alifunga mabao matatu dhidi ya Aston Villa, mawili yakiwa kwa mikwaju ya penalti.

Katika game nyingine iliyovuta macho na hisia za mashabiki wengi kufahamu matokeo yake ni ile iliyochezwa baina ya Birmingham na Man U'.

Lee Bowyer wa Birmingham City alipachika bao katika dakika ya tisini na kuifanikisha klabu yake kuibana mbavu Manchester United kwa droo ya 1-1. Hata Hivyo licha ya sare hiyo United wamerejea kileleni.

Tuesday, December 28, 2010

MKUTANO WA BENKI YA DUNIA MWANZA.

KUTOKA KUSHOTO NI MATIA LEVI AMBAYE NI AFISA MIPANGO OFISI YA MKUU WA MKOA MWANZA, MWENYEKITI WA KUSANYIKO HILO BW. WAMBURA SABURA (KATIBU TAWALA MSAIDIZI SEKSHENI YA MIUNDOMBINU, OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA) PAMOJA NA WARATIBU TOKA BENKI YA DUNIA CHIYO KANDA NA ADAM.

Mkutano wa kujadili Mpango wa miaka 5 wa Benki ya Dunia wa kusaidia Tanzania umekamilika na mkutano ulifanyika tarehe 13/12/2010, Hoteli ya Nyumbani jijini Mwanza, Washiriki wa mafunzo hayo walikuwa wakuu wa Seksheni,idara na vitengo toka Serikali kuu, Serikali za Mitaa na taasisi zisizo za Serikali.
Tofauti iliyopo katika ukuaji wa sekta na miradi mbalimbali inayofadhiliwa na benki ya dunia kati ya mwaka 2007 na 2010.

Mmoja kati ya washiriki akichangia katika kuainisha changamoto zinazo kwamisha mipango ya maendeleo kwa miradi inayofadhiliwa na benki ya dunia.

Je! maendeleo kiasi gani yamepatikana?
Je! Juhudi za kuondoa umaskini zimefanikiwa?
Je! Miradi imelenga Vipaumbele sahihi?
Meneja wa uhusiano jiji la Mwanza mr. Joseph Mlinzi akichangia kwenye mkutano huo.


Country Assistance Strategy (CAS)(1)
World Bank Group’s business plan in support of a country’s development strategy and poverty reduction goals. Provide a framework for areas of Bank support and modalities/approaches, based on country’s priorities, other partners’ support and Bank’s comparative advantages. Normally prepared on a four-year cycle.


New CAS (Country Assistance Strategy): Overall Approach Starting point was MKUKUTA II(mkakati wa kukuza uchumi na kupunguza umaskini Tanzania/Poverty Reduction Strategy for mainland Tanzania) & MKUZA II(mkakati wa kupunguza umaskini Zanzibar/Poverty Reduction Strategy for Zanzibar).

TUAGE&TUUKARIBISHE STONE CLUB NDIYO PLACE!!

WELCOME KATIKA EVENT YA KUIKARIBISHA 'NYUIYA'
NI MAWE TU MA HIP HOP ZA UKWELI, BONGOFLAVA, HOUSE, RAGGA NA MA R&B FLANI HIVI.
HUKU TUKIOGA MASHAMPENI

Aaaaaah YA rahaaa!!..!!.

Monday, December 27, 2010

BARIDI YAZIDI KULETA KIZAAZAA MICHEZONI UINGEREZA, WAPENZI WA LIGI KUU AGHhh!..!!.

Hali iko hivi nje ya dimba la Emirates nyumbani kwa washika bunduki Arsenal ambao leo majira ya usiku wataumana na Chelsea kiwanjani hapa, kocha Arsene Wenger akikitaka kikosi chake kupata ushindi ili kujiweka ktk nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu .

Hali ya hewa ya baridi kali inaendelea kuleta bugudha kubwa katika michezo nchini Uingereza, hasa wakati huu wa sikukuu.

Jana Michezo ya Ligi Kuu ya soka ya England kati ya Blackpool na Liverpool na kati ya Everton na Birmingham ilifutwa.

Ipswich ambao walikuwa wawakaribishe nyumbani Watford katika mechi za Championship jana, mchezo huo nao umeahirishwa, wakati mechi ya Ligi Kuu ya Scotland kati ya Kilmarnock na Dundee United nao umeahirishwa.

Michezo ya rugby, pambano baina ya Gloucester na Northampton limeahirishwa kutokana na baridi kali. Pia michezo mingine ya rugby ya ligi kuu kati ya Bath na Exeter ilifutwa na ule mpambano baina ya Newcastle dhidi ya Leeds umesogezwa mbele, badala ya kufanyika Jumapili jana, sasa utachezwa leo Jumatatu.

Katika soka tena, michezo ya Championship ya Crystal Palace, Derby, Ipswich, Scunthorpe na Middlesbrough pia ilifutwa; michezo 22 ya Ligi daraja la kwanza na la pili pia iliahirishwa. Mechi ya ligi daraja la kwanza pekee iliyochezwa jana ni kati ya Huddersfield na Hartlepool, wakati ya ligi daraja la pili, kati ya Wycombe na Hereford ulinusurika kutochezwa na hatimaye ukachezwa kama ulivyopangwa.

HUYU HAPA MSHINDI WA UNIQ MODEL

Mshindi wa Giraffe Unique Model, Asia Dachi (katikati) akiwa na furaha mara baada ya kutangazwa mshindi wa shindano hilo (unique model of the year 2010). Kulia ni mshindi wa pili, Diana Mainanson na mshindi wa tatu Mariam Rabii. Shindano hilo lilidhaminiwa na Giraffe ocean view hotel, Channel ten, Magic fm, Global pubishers, Mohammed enterprises, Truworths, mtaakwamtaablog na uniqueentertz blog.

“Nawashukuru wote, vyombo vya habari, wadau na kila mmoja kwa ushirikiano mzuri na sapoti kubwa mliyonipa, Bwana CHARLES BEKON kwa UDHAMINI NA HATIMAYE NIMEFANIKIWA KUFIKISHA JAHAZI UKINGONI, kisha kufanikiwa zoezi la kuwatangaza wanamitindo kumi katika soko la mitindo Tanzania. Hakika ni fahari kubwa.” By Magese.

KRISMASI ILIKUWA SAFI!!...!!BADO MWAKA MPYA.

Inamhusu kila mmoja aliyezaliwa siku moja na maadhimisho haya ya kuzaliwa masia yaani tarehe 25/Disemba. Ilikuwa tamu sanaaaaaa! Aksante kwa aliyeitwaa kwetu sisi.

Derick Nyathi na 'wazeeeya' mchezoni katika fukwe za malaika.

Mwonekano wa Mjengo na x.mass.

Sports na watoto.

Run..na fukwe ya malaika.

Swimming pool iliyo juu ya maji.

Cathbert A.G.

Dogoooo...Jeremiah from A.city na Cathbert.