ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, November 4, 2017

ENEO LA PWANI LATOA WITO WA KUJITENGA NA ARDHI YA KENYA.

Eneo la Pwani latoa wito wa kujitenga na ardhi ya KenyaViongozi wa eneo la Pwani nchini Kenya wametoa mwito wa kutaka kujitenga eneo hilo na ardhi ya nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

Gavana wa kaunti ya Mombasa, Ali Hassan Joho na mwenzake wa Kilifi Amason Jeffa Kingi waliongoza wabunge 12 wa Pwani ya Kenya katika kutoa mwito huo jana Ijumaa.

Gavana Joho amesema "Huu ndio mwanzo wa kutimiza ndoto ya Wapwani ya kutaka kujitenga na Kenya".

Amesema tayari timu ya mawakili wa ndani na nje ya nchi wameanzisha mazungumzo na mchakato wa kuhakikisha kuwa kanda ya Pwani inajitenga na Kenya.

Ramani ya Kenya.
Gavana wa Kilifi kwa upande wake amesisitiza kuwa, katika safari yao hiyo ya kujitenga, watahakikisha kuwa hawatumii njia zisizo za kisheria na pia wataanza kupokea maoni ya wakazi wa eneo hilo kuhusu kadhia hiyo.

Jopo la wabunge wa Pwani ya Kenya limesema litawasilisha muswada katika Bunge la nchi hiyo, wa kutaka eneo hilo lipewe mamlaka ya kujitawala lenyewe.

Haijabainika iwapo hii ni moja ya mikakati ya mrengo wa upinzani wa NASA ulioapa kuanzisha uasi wa kiraia dhidi ya serikali, sambamba na kutaka wafuasi wao wasusie bidhaa na huduma za kampuni zinazoaminika kumilikiwa na viongozi wa chama tawala cha Jubilee, kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta. CHANZO: PARSTODAY SWAHILI.

MONGELA ATEKELEZA AGIZO LA RAIS MAGUFULI ALIYEDHULUMIWA KIWANJA MWANZA.


​AGIZO la rais JOHN POMBE  MAGUFULI la kumtaka mkuu wa mkoa wa mwanza kushughulikia malalamiko ya mkazi mmoja wa ISAMILO jijini MWANZA, ANNA JOYCE FRANCIS, aliyedai kudhulumiwa kiwanja chake kwa zaidi ya miaka 9 amefika katika eneo la mgogoro na kukutana na wananchi wengi wenye malalamiko kama hayo.

VIDEO : BARAKAH THE PRINCE - SOMETIMES


ARTIST - BARAKAH THE PRINCE
SONG - SOMETIMES
DIRECTED BT - HANSCANA BRAND
VIDEO DIRECTED - LOCATION AT ZANZIBAR

Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza baada ya video ya kwanza kuondolewa YOUTUBE hii hapa account mpya ya BARAKA THE PRINCE na link mpya ya video tunaomba muda wako kwa kushare na kuwajulisha wote account yetu na video yetu mpya ya SOMETIMES

AJALI MBAYA YATOKEA ARUSHA AKIWAHI MAHAKAMANI.

 David Chijana (33) mkazi wa Tabata jijini Dar es Salaam, amefariki dunia katika ajali ya gari akiwa safarini kuelekea jijini Arusha kusikiliza kesi ya utakatishaji wa fedha katika benki ya exim inayokabili mama yake.

Ajali hiyo ilitokea jana Ijumaa, Oktoba 3, majira ya saa 4:00 asubuhi katika eneo la Usa River nje kidogo ya Jiji la Arusha ambapo gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Mark X lenye namba za usajili T 796 DGF lilikuwa lilkiendeshwa na Chijana lilipoteza mwelekeo na kupinduka.

Ajali hiyo ilipelekea pia kifo cha James Alfred (40) mkazi wa Tabata ambaye ilielezwa kuwa alikuwa rafiki kipenzi wa Chijana.

Chijana, ambaye taarifa za uhakika zimesema alikuwa karani mkuu wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Kitengo cha Uhandisi, katika Bandari ya Dar es Salaam, alikuwa katika maandalizi ya mwisho kabla ya kufunga ndoa pia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, alieleza kuwa ajali hiyo ilisababishwa na mwendokasi wa gari la Chijana wakati akitaka kulipita gari aina ya Toyota Noah yenye namba T841 BVQ, lililokuwa ikiendeshwa na Joseph Bandari mkazi wa Maji ya Chai, Arusha.

“Wakati David (Chijana) akijaribu kuipita Noah, mbele yake kulikuwa na lori linakuja kwa kasi, Sasa akaona ili asikutane nalo uso kwa uso, arudi kushoto. Akaigonga Noah kisha akapoteza mwelekeo na kwenda kugonga miti.” alisema Kamanda Mkumbo.

Aidha, Kamanda Mkumbo alisema watu hao walikufa papo hapo na miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufani ya Mount Meru
mkoani Arusha.

Friday, November 3, 2017

NDUGAI AWAPA BARUA NEC.

 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai leo Novemba 3, 2017 amemuandikia barua Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) kumtaarifu kuwa jimbo la Singida Kaskazini lipo wazi kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo.

Taarifa ya Bunge iliyotolewa leo inasema kuwa jimbo hilo lipo wazi kutokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumfuta Uanachama Lazaro Nyalandu toka Oktoba 30, 2017 siku ambayo Mbunge huyo alitangaza mwenyewe kupitia vyombo vya habari kujivua nafasi zake ndani ya chama hicho na kusema kuwa ameandika barua kwa Spika kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge kupitia CCM.

TOT PLUS WAJIFUA KUIPUA NYIMBO TATU MPYA UKIWEMO WA KUMUUNGA MKONO JPM KATIKA VITA YA KUTETEA RASILIMALI ZA NCHI

Mkurugenzi wa TOT Gasper Tumaini
NA BASHIR NKOROMO
Kundi la Tanzania One Theatre (TOT Plus), limo kambini Wanamuziki wake wakijifua vikali katika mazoezi ya nyimbo tatu ambazo kundi hilo litaziipua hivi karibuni.

Akizungumza wakati wa mazoezi ya nyimbo hizo, Mkurugezi wa TOT Plus inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Gasper Tumaini amezitaja nyimbo hizo kuwa ni 'Tumuunge mkono JPM',  'Amani ya Tanzania' na Hongera awamu ya tano'.

Tumaini amsema, wimbo wa 'Tumuunge mkono JPM' ni wa kuwahamasisha Watanzania popote walipo kumuunga mkono Rais Dk John Magufuli katika vita ya uchumi anayoongoza kwa kuhakikisha inaziba mianya inayotishia upotevu au matumizi mabaya ya rasilimali za nchi.

"Kama unavyoona Rais tayari ameshaamua kwa dhati kupigana katika vita ya kubana mianya inayotishia upotevu au matumizi mabaya yanayofanya na baadhi ya watu kutumia rasilimali za nchi vibaya kwa kujinufaisha wao huku taifa likiendelea kuwa masikini

Hii siyo vita ndogo, ni kubwa sana inayohitaji ujasiri na ari kubwa ya kujituma, hivyo ni lazima Watanzania wote tumuunge mkono ili asiyumbishwe na waliokuwa wanajinufaisha na rasilimali hizi", alisema Tumaini wakati wa mazoezi ya nyimbo hizo kwenye ukumbi wa Ofisi ya CCM Mwinjuma, Mwananyamala, Dar es Salaam.

Amesema, wimbo wa 'Amani ya Tanzania' kunahimiza Watanzania ndani na nje ya Nchi kuhakikisha pia wanaienzi amani ya nchi kwa kuunga mkono juhudi za kuiimanrisha zinazofanywa na viongozi wakiongozwa na misingi imara iliyowekwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na pia Rais wa Kwanza wa Zanzibar  Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

Akizungumzia wimbo wa tatu wa 'Hongera awamu ya Tano', Tumaini amesema, wimbo huo ni wa pongezi kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli kwa kutimiza kwa vitendo ahadi zilizotolewa na CCM wakati wa kampeni za kuomba ridhaa ya wananchi katika uchaguzi mkuu uliopita.

"Tumeona ni vizuri kutunga wimbo huu wa kumpongeza kwa sababu utekelezaji wa ilani na ahadi alizokuwa akizitoa kwenye kampeni unaonekana wazi japokuwa sasa ni miaka miwili tu tangu tumchague, kwa kweli Rais Dk. Magufuli amechapa kazi hivyo inastahili kumpongeza", alisema tumaini.

Amesema, nyimbo hizo ambazo ni kwaya tayari zimeshakamilika na sasa wanamuziki wanazifanyia mazoezi ya mwisho mwisho  kabla ya kuzirekodi ili zianze kusikika katika maeneo mbalimbali na hasa pale kundi hilo litakapokuwa likitumbuiza.

Mmiliki wa theNkoromoBlog aliyefika kwenye mazoezi ya kundi hilo, alishuhudia wanamuziki wote wakiwajibika kila mmoja katika eneo lake, huku baadhi yao wakitokwa jasho kuliko hata wanapokuwa wakitumbuiza jukwaani katika maonyesho maalum.
 Mwanamuziki nguli Juma Abdallah 'Jerry' akikipapasa kinanda kwa mkoni mmoja kuonyesha umahiri wake, Kundi la TOT Plus lilipokuwa katika mazoezi ya nyimbo tatu, leo katika ukumbi wa CCM Mwinjuma, Mwananyamala Dar es Salaam
 Waimbaji Neca Twalib aliyechukua nafasi iliyoachwa na aliyekuwa mwimbaji nguli na Mkurugenzi wa TOT Plus Marehemu Kampteni John Komba, akiimba na mwenzake Corobian Mkinga wakati wa mazoezi hayo
 Patrick Thomas akizicharaza tumba wakati wa mazoezi hayo
 Mkurugenzi wa TOT Plus Gasper Tumaini (mwenye suti) akizungumza na baadhi ya wadau waliofika kushuhudia mazoezi hayo
 Jerry akikicharaza kinanda kwa madaha wakati wa mazoezi hayo
 Waimbaji Rosemary William, Sharifa Mohammed na Mwasiti Suleimani wakiimba wakati wa mazoezi hayo
 Mwimbaji nguli Hadija Kopa na wenzake wakiimba wakati wa mazoezi hayo
 Tumaini akiwa na wadau wakati wakifuatilia mazoezi hayo. Kulia ni Jerry
 Waimbaji wa TOT Plus wakiwa kwenye mazoezi hayo
 Waimbaji wa TOT Plus wakiwa kwenye mazoezi ya wimbo wa 'Amani ya Tanzania'
 Jerry na Tumaini wakifuatilia kwa makini mazoezi hayo. Kushoto ni mdau wa TOT Plus
 Alen Elias aka Mchungaji akikicharaza kinanda kwa makini
 Evans Peter na said Mpiluka wakiyacharaza magita wakati wa mazoezi hayo
 Godfrey Kanuti akilicharaza gita wakati wa mazoezi hayo
 Neka twalib na Mkinga wakishauriana jambo wakati wa mazoezi hayo
 Fundi mitambo akiwajibika wakati wa mazoezi hayo
 Tumaini akijadiliana jambo na viongozi wa bendi ya Vijana Jazz ambao walihudhuria mazoezi hayo
Wanamuziki wa TOT Plus wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wakati wa mazoezi hayo.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

DC KIBAHA AUAGIZA UONGOZI WA KAMPUNI YA YAPI MARKEZI KUTATUA KERO ZA WAFANYAKAZI

Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama akimtambulisha meneja mwajiri wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki kwa vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani wakati akifanya mkutano nao. Mkuu huyo wa wilaya alifanya ziara hiyo kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya. PICHA ZOTE NA CATHBERT KAJUNA - KAJUNASON/MMG - KIBAHA.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama akijadiliana machache na meneja mwajiri wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki wakati alipofanya mkutano wake na vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama akitolea ufafanuzi wa mambo machache kwa vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Asumpter Mshama.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama akaribishwa na uongozi wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki ili aweze kuongea na vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Mkutano ukiendelea.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama aliyeambatana na viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama wakifanya mkutano wa ndani na vingozi wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki  katika mambi yao waliyoiweka kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Kamati ya ulinzi na usalama ikifuatilia kwa karibu.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama (kushoto) na katibu tawala wilaya ya Kibaha Sozi Ng'ate (kulia) wakipata maelezo machache kwa kiongozi wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki wakati walipotembelea kambi yao iliyopo kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.

Thursday, November 2, 2017

KIKAO CHA MADIWANI HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA CHAVUNJIKA, KITI CHA MSTAHIKI MEYA CHAFICHWA..




Breaking News!
Kikao cha baraza la madiwani Jijini Mwanza kilichokuwa kikiongozwa na yule meya aliyekamatwa na jeshi la polisi asionane na Rais (Mstahiki Meya James Bwire) kimeingia malumbano na mvutano na hata kuvurugika.

Ni takribani miezi miwili sasa hakuna kikao chochote kimeweza kuketi na kujadili namna ya kusukuma shughuli za maendeleo kwa Jimbo la Nyamagana ambako ndiko Halmashauri ya jiji la Mwanza inapatikana.

Leo imeshuhudiwa kikao hicho kuvunjika tena huku kukiwa na giza machoni mwa wananchi wasijue ni lini watapata taarifa zitakazo eleza nini kimefanyika kupitia mipango mbalimbali iliyowekwa awali na hatma kwa mipango ya baadaye..........

VIFARANGA VILIVYO TEKETEZWA KWA MOTO VYAZUA MJADALA.

Watetezi wa haki za wanyama wametoa maoni wakilaani kuteketezwa vifaranga vya kuku 6,400 vilivyoingizwa nchini kinyume cha sheria.

Vifaranga hivyo mali ya Mary Matia (23), vyenye thamani ya Sh12.5 milioni vilikamatwa mpakani Namanga vikitokea nchini Kenya.

Kuteketezwa kwa vifaranga hivyo juzi kumeibua mjadala ikielezwa kitendo hicho ni ukiukwaji wa sheria.

Kazi ya kuviteketeza eneo la Namanga wilayani Longido ilifanyika ikishuhudiwa na maofisa wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Wizara ya Mifugo, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na vyombo vingine vya ulinzi na usalama.

Akizungumza wakati wa kuviteketeza vifaranga hivyo, ofisa mfawidhi wa kituo cha udhibiti wa magonjwa ya mifugo Kanda ya Kaskazini, Obedi Nyasebwa alisema kazi hiyo imefanyika kwa kuzingatia Sheria ya Magonjwa ya Wanyama namba 17 ya mwaka 2003.

Pia, alisema Serikali mwaka 2007 ilitoa tangazo kupiga marufuku kuingizwa nchini vifaranga vya kuku na mayai.

Hata hivyo, watu mbalimbali wamehoji ulazima wa kuviteketeza vifaranga hivyo badala ya kuvirudisha vilikotoka kama alivyoomba mmiliki wake Matia.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ustawi wa Wanyama (Taweso), Dk Thomas Kahema akizungumza na Mwananchi jana alisema anatambua dhamira ya Serikali ya kuzuia magonjwa ya kuambukizwa kutoka nchi jirani, lakini kulikuwa na njia mbadala ya kufanikisha suala hilo.

Dk Kahema alisema mamlaka za Serikali zilitakiwa kuvirudisha vifaranga hivyo vilikotoka ili visieneze magonjwa kama inavyohofiwa. Alisema kuviteketeza ni ukatili ambao hauungi mkono na kwamba, wanalaani kitendo hicho ambacho kinatoa taswira mbaya kwa Taifa linaloonekana halijali haki za wanyama.

“Zipo njia nyingi ambazo wangeweza kutumia mbali na kuchoma, mbona wakikamata ng’ombe hawawachomi moto?” alihoji Dk Kahema.

Alisema Sheria ya Ustawi wa Wanyama ya mwaka 2008 inasisitiza kutambuliwa kwa haki za wanyama, kwa hiyo kuteketezwa vifaranga hivyo kunaonyesha jinsi utekelezaji wa sheria unavyoibua utata.

Dk Kahema alisema vifaranga hivyo vingepimwa kubaini kama vina maambukizo na ingebainika havina vingetaifishwa au kugawiwa wajasiriamali, magereza au vituo vya watoto yatima.

Alisema hana uhakika kama sheria iliyotumika kuteketeza vifaranga hivyo inaeleza wazi kwamba viteketezwe.

Mkurugenzi mtendaji huyo amesema mamlaka hazikuweka wazi kama vifaranga hivyo vilikuwa na maambukizo.

Alisema vifaranga havina hatia bali aliyevileta ndiye anayetakiwa kuchukuliwa hatua.

Baadhi ya wananchi kupitia mitandao ya kijamii wameonyesha kutoridhishwa na hatua iliyochukuliwa na mamlaka za Serikali wakieleza ni ukatili dhidi ya wanyama.

Abbas King aliandika kwenye ukurasa wa Facebook wa Mwananchi kuwa, “Hivyo vifaranga vina roho au vinaendeshwa kwa umeme? Kwa nini msivigawe kwa watoto yatima wakafuge vikue wafanye kitoweo, kama vina madhara virejeshwe kwao, walioleta wapigwe faini.”

Tumaini Kyama aliandika katika ukurasa huo kuwa, “Swali langu ni kuwa kama alikuwa kachukua mkopo wa biashara huyo mmiliki wa hivyo vifaranga mkopo ataurudisha na nani sitaki kujua hayo mengine nimewaza kwa sauti tu. Tunapambana na umasikini au tunafurahia umasikini wa baadhi ya watu.”

“Ukiukwaji wa sheria ya wanyama na pia wamerudisha maendeleo nyuma. Vilevile hawajavipima vifaranga na kutufahamisha vina magonjwa gani na hata hivyo si wangevirudisha vilikotoka ili aliyevinunua arejeshewe fedha yake na kama ni faini apigwe ili iwe funzo kwa wafanyabiashara,” aliandika Lightdod Shayo.

RC GEITA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA LIPA KWA MATOKEO HALMASHAURI YA MJI GEITA.

Mhandisi Robert Lughumbi Mkuu wa Mkoa wa Geita pamoja na viongozi wa Mkoa na Wilaya Geita na kamati ya usalama ya Mkoa  wakikagua miundombinu ya shule ya Msingi Nguzombili wakati wa ziara ya Mkuu huyo wa Mkoa Halmashauri ya Mji Geita.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Geita(Wakwanza kushoto) na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nguzombili wakati wa ziara yake katika Shule hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Geita akiingia ndani ya moja ya darasa lililojenjwa chini ya mpango wa lipa kwa matokeo shule ya Msingi Nguzo Mbili.


                                                      (PICHA NA JUMAPILI MAGESA)


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Lughumbi ameipongeza Halmashauri ya Mji wa Geita kwa kusimamia vizuri fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa vilivyo chini ya mpango wa lipa kwa matokeo shule ya msingi Nguzo mbili.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika shule hiyo Mheshimiwa Robert Gabriel alisema kuwa ameridhishwa na kiasi cha fedha kilichotumika katika ujenzi wa madarasa kwa ubora wa hali ya juu katika shule hiyo.  

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Mhandisi  Modest Apolinary  akifafanua jambo kuhusu utekelezaji miradi ya lipa kwa matokeo kwa Mkuu wa Mkoa wakati wa ziara yake shule ya msingi Nguzombili iliyopo Halmashauri ya Mji Geita.

" Inashangaza sana kuona maeneo mengine wanatumia fedha zote kiasi cha shilingi 20 milioni katika ujenzi wa darasa moja lakini kuna mapungufu mengi hivyo lazima kuwe na nidhamu ya matumizi ya fedha katika miradi ya Serikali"Alisema Lughumbi.

Akiwa shuleni hapo Mkuu wa Mkoa ameagiza wakurugenzi kuunda na kutumia vikundi vya ujenzi vilivyo katika maeneo ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa madarasa pia kuishirikisha jamii ili kupunguza gharama kwa serikali na hatimaye fedha zinazobaki ziwezekufanya mambo mengine katika huduma za jamii.

Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akiongozana na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Geita na Wilaya ya Geita wakati wa ukaguzi wa majengo yaliyotekelezwa kwa mpango wa lipa kwa matokeo Halmashauri ya Mji Geita.

Katika hatua nyingine Mhandisi Robert Gabriel aliutaka  uongozi wa Shule ya Msingi Nguzo Mbili kusimamia suala la usafi na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita kuhakikisha anasimamia uimarishaji wa miundombinu hiyo ambayo mingine imeanza kupasuka.  

 Aidha, ameagiza shule hiyo kupelekewa miundombinu ya maji ili vyoo vilivyojengwa vianze kutumika badala ya kufungwa.Pamoja na kutembelea Shule ya Msingi Nguzo Mbili Mkuu wa Mkoa pia ameitembelea shule ya Sekondari na kukagua ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa vilivyojengwa kupitia mpango wa lipa kwa matokeo.

Vyumba vya madarasa vilivyojengwa kupitia mpango wa lipa kwa matokeo Halmashauri ya Mji Geita.

 Shule ya Msingi Nguzo mbili imejenga madarasa nane kwa kutumia shilingi milioni 13 kwa kila darasa, Ofisi 4, kisima cha maji na vyoo vya kisasa pamoja na ukarabati wa madarasa mengine katika shule hiyo kutokana na fedha iliyobaki katika bajeti ya darasa moja.

Mkoa wa Geita una upungufu wa vyumba vya madarasa 8600 hivyo serikali imeandaa mpango kabambe wa kutokomeza tatizo hili kwa kushirikiana na jamii na wadau wote wa Mkoa katika ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Imeandaliwa na mtandao wa maduka online.

MKUU WA MKOA WA PWANI INJINIA EVARIST NDIKILO AWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA KIWANDA CHA KUTENGENEZEA CHAKI KISARAWE

 
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo akizungumza na wananachi na baaadhi ya viongozi mbali mbali wa serikali mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho cha chaki cha Mkongoma kiichopo Wilayani Kisarawe. (PICHA NA VICTOR MASANGU)

Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha chaki Geofrey Mkongoma akitoa risala fupi  kwa mgeni rasmi mara baada ya  kiwanda hicho kuwekea jiwe la msingi na Mkuu wa Mkoa wa Pwani .

 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Happines Seneda akizungumza na wananchi waliofika katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi katika kiwanda hicho cha chaki.

Baadhi ya viongozi wa halmshauri ya Wilaya ya Kisarawe wakiwa katika halfa hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi katika kiwanda hicho cha chaki.(PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)

NA  VICTOR  MASANGU, KIRASAWE

KATIKA kuunga mkono juhudi za Rais wa serikali ya awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli katika kuwa na uchumi wa viwanda,Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wawekezaji wote kuhakikisha wanaachana kabisa na tabia ya kukwepa kulipa kodi  na badala yake watimize wajibu wao ipasavyo bila ya kuvunja sheria na taratibu za nchi ili kuweza kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kwa wananchi.

Injinia Ndikilo ametoa kauli hiyo wakati  wa halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi katika kiwanda cha chaki kinachoendelea kujengwa katika awamu ya kwanza katika kijiji cha Msanga zalala kata ya Msimbu Wilayani Kisarawe na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa , serikali, madhehebu ya dini pamoja na watendaji wa  serikali za vijiji na vitongoji.   

Pia Mkuu huyo alibainisha kuwa katika uwekezaji wa viwanda katika Mkoa wa Pwani baadhi ya maeneo bado yanakabiliwa na changamoto ya kutokuwa ni nishati ya umeme wa uhakika pampja na kuwepo kwa mioundimbinu mibovu ya barabara hivyo ameagiza mamlaka zote zinazohusika kulifanyia kazi suala hilo ili kuweza kuwavutia wawekezaji wengine.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe  Happiness Seneda alitoa wito kwa wananchi wengine kutumia fursa zilizopo katika kujifunza mambo mbali mbali ya ujasiriamali  na kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwa lengo la kuweza kuunga juhudi za serikali ya awamu ya tano ya kuwa na uchumi wa kati pamoja na kuwapa nafasi zaidi wawekezaji ambao ni wazawa ili waweze kutoa fursa za ajira kwa vijana.

Awali  Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda hicho cha chaki Geofrey Mkongoma  akisoma taarifa yake ameiomba serikali ya awamu ya tano  kuweza kuwapa fursa  ya kipekee wazawa  wa  Tanzania katika   suala zima la uwekezaji  wa ujenzi wa viwanda  vidogovidogo huku akitaja akisema changamoto kubwa ni suaala la umeme wa uhakika.

Alisema kuwa lengo lake kubwa ni kuhakikisha anaunga mkono juhudi za serikali ya wamu ya tano katika kuwa na uchumi wa viwanda hivyo ataendelea kushirikiana bega kwa began a wadau wengine kwa lengo la kuweza kufanikisha malengo aliyojiwekea ya kuweza kutoa fursa za ajira kwa wazawa pamoja na kuongeza uzalishaji wa chaki.

“Hiki kiwanda kilianza tangu mwaka 2013 na kwa sasa kama mnavyoona  mimi nimeshaajiri wafanyakazi wapatao 38. Ambao ninawalipa kutokana na kiwanda hiki cha chaki hivyo kitu kikubwa ninachokiomba kwa serikali ni kutoa sapoti kubwa zaidi kwa wawekezaji ambao ni wazawa ili waweze kuendelea kujenga viwanda vidogo vidogo ili kuweza kukuza uchumi wa nchini,”alisema Mkurgenzi Mkongoma.

Nao baadhi ya wakinamama ambao wanafanya kazi katika kiwanda hicho cha chaki  akiwemo  Tedy Mzingula na Shoboa Msagasa wamesema kuwa kipato wanachokipata kinaweza kuwabadilisha kwa kiasi kikubwa katika suala zima la kujikwmau kimaisha kutokana na kuendesha familia zao ikiwemo kuwasomesha watoto walionao pamoja na kuwahudumia mahitaji madogo madogo.

“Sisi kwa kwli kama wafanyakazi wa kiwanda hiki tunapenda kumshukuru Mkurugenzi wetu kwa kuweza kupenda katika hali na mali, na kutokana na kufanya kazi hii fedha ambayo tunaipata inatusaidia kwa kiasi kikubwa katika kuendesha familia zetu, kwani wengne tuna watoto ambao tunawasomesha na maisha yanaendelea lakini kikubwa ni serikali kumsaidia kuweza kupata umeme,”walisema.

KIWANDA hicho cha chaki ambacho kinajulikana kwa jina la  Mkongoma Chalk Factor kilianzishwa mnamo mwaka 2013 ambapo kwa sasa kina jumla ya wafanyakazi zaidi ya 38 wakiwemo vijana pamoja na wakinamama kutoka maeneo mbali mbali ya Wilaya hiyo ya Kisarawe.