Saturday, November 4, 2017
ENEO LA PWANI LATOA WITO WA KUJITENGA NA ARDHI YA KENYA.
Gavana wa kaunti ya Mombasa, Ali Hassan Joho na mwenzake wa
Kilifi Amason Jeffa Kingi waliongoza wabunge 12 wa Pwani ya Kenya katika
kutoa mwito huo jana Ijumaa.
Gavana Joho amesema "Huu ndio mwanzo wa kutimiza ndoto ya Wapwani ya kutaka kujitenga na Kenya".
Amesema tayari timu ya mawakili wa ndani na nje ya nchi wameanzisha mazungumzo na mchakato wa kuhakikisha kuwa kanda ya Pwani inajitenga na Kenya.
Ramani ya Kenya.
Gavana wa Kilifi kwa upande wake amesisitiza kuwa, katika safari yao hiyo ya kujitenga, watahakikisha kuwa hawatumii njia zisizo za kisheria na pia wataanza kupokea maoni ya wakazi wa eneo hilo kuhusu kadhia hiyo.
Jopo la wabunge wa Pwani ya Kenya limesema litawasilisha muswada katika Bunge la nchi hiyo, wa kutaka eneo hilo lipewe mamlaka ya kujitawala lenyewe.
Haijabainika iwapo hii ni moja ya mikakati ya mrengo wa upinzani wa NASA ulioapa kuanzisha uasi wa kiraia dhidi ya serikali, sambamba na kutaka wafuasi wao wasusie bidhaa na huduma za kampuni zinazoaminika kumilikiwa na viongozi wa chama tawala cha Jubilee, kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta. CHANZO: PARSTODAY SWAHILI.
Gavana Joho amesema "Huu ndio mwanzo wa kutimiza ndoto ya Wapwani ya kutaka kujitenga na Kenya".
Amesema tayari timu ya mawakili wa ndani na nje ya nchi wameanzisha mazungumzo na mchakato wa kuhakikisha kuwa kanda ya Pwani inajitenga na Kenya.
Gavana wa Kilifi kwa upande wake amesisitiza kuwa, katika safari yao hiyo ya kujitenga, watahakikisha kuwa hawatumii njia zisizo za kisheria na pia wataanza kupokea maoni ya wakazi wa eneo hilo kuhusu kadhia hiyo.
Jopo la wabunge wa Pwani ya Kenya limesema litawasilisha muswada katika Bunge la nchi hiyo, wa kutaka eneo hilo lipewe mamlaka ya kujitawala lenyewe.
Haijabainika iwapo hii ni moja ya mikakati ya mrengo wa upinzani wa NASA ulioapa kuanzisha uasi wa kiraia dhidi ya serikali, sambamba na kutaka wafuasi wao wasusie bidhaa na huduma za kampuni zinazoaminika kumilikiwa na viongozi wa chama tawala cha Jubilee, kinachoongozwa na Rais Uhuru Kenyatta. CHANZO: PARSTODAY SWAHILI.
MONGELA ATEKELEZA AGIZO LA RAIS MAGUFULI ALIYEDHULUMIWA KIWANJA MWANZA.
AGIZO la rais JOHN POMBE MAGUFULI la kumtaka mkuu wa mkoa wa mwanza kushughulikia malalamiko ya mkazi mmoja wa ISAMILO jijini MWANZA, ANNA JOYCE FRANCIS, aliyedai kudhulumiwa kiwanja chake kwa zaidi ya miaka 9 amefika katika eneo la mgogoro na kukutana na wananchi wengi wenye malalamiko kama hayo.
VIDEO : BARAKAH THE PRINCE - SOMETIMES
ARTIST - BARAKAH THE PRINCE
SONG - SOMETIMES
DIRECTED BT - HANSCANA BRAND
VIDEO DIRECTED - LOCATION AT ZANZIBAR
Tunaomba
radhi kwa usumbufu uliojitokeza baada ya video ya kwanza kuondolewa
YOUTUBE hii hapa account mpya ya BARAKA THE PRINCE na link mpya ya video
tunaomba muda wako kwa kushare na kuwajulisha wote account yetu na
video yetu mpya ya SOMETIMES
AJALI MBAYA YATOKEA ARUSHA AKIWAHI MAHAKAMANI.
David Chijana (33) mkazi wa Tabata jijini Dar es Salaam, amefariki
dunia katika ajali ya gari akiwa safarini kuelekea jijini Arusha
kusikiliza kesi ya utakatishaji wa fedha katika benki ya exim
inayokabili mama yake.
Ajali hiyo ilitokea jana Ijumaa, Oktoba 3, majira ya saa 4:00 asubuhi katika eneo la Usa River nje kidogo ya Jiji la Arusha ambapo gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Mark X lenye namba za usajili T 796 DGF lilikuwa lilkiendeshwa na Chijana lilipoteza mwelekeo na kupinduka.
Ajali hiyo ilipelekea pia kifo cha James Alfred (40) mkazi wa Tabata ambaye ilielezwa kuwa alikuwa rafiki kipenzi wa Chijana.
Chijana, ambaye taarifa za uhakika zimesema alikuwa karani mkuu wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Kitengo cha Uhandisi, katika Bandari ya Dar es Salaam, alikuwa katika maandalizi ya mwisho kabla ya kufunga ndoa pia.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, alieleza kuwa ajali hiyo ilisababishwa na mwendokasi wa gari la Chijana wakati akitaka kulipita gari aina ya Toyota Noah yenye namba T841 BVQ, lililokuwa ikiendeshwa na Joseph Bandari mkazi wa Maji ya Chai, Arusha.
“Wakati David (Chijana) akijaribu kuipita Noah, mbele yake kulikuwa na lori linakuja kwa kasi, Sasa akaona ili asikutane nalo uso kwa uso, arudi kushoto. Akaigonga Noah kisha akapoteza mwelekeo na kwenda kugonga miti.” alisema Kamanda Mkumbo.
Aidha, Kamanda Mkumbo alisema watu hao walikufa papo hapo na miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufani ya Mount Meru
mkoani Arusha.
Ajali hiyo ilitokea jana Ijumaa, Oktoba 3, majira ya saa 4:00 asubuhi katika eneo la Usa River nje kidogo ya Jiji la Arusha ambapo gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Mark X lenye namba za usajili T 796 DGF lilikuwa lilkiendeshwa na Chijana lilipoteza mwelekeo na kupinduka.
Ajali hiyo ilipelekea pia kifo cha James Alfred (40) mkazi wa Tabata ambaye ilielezwa kuwa alikuwa rafiki kipenzi wa Chijana.
Chijana, ambaye taarifa za uhakika zimesema alikuwa karani mkuu wa Mamlaka ya Bandari (TPA), Kitengo cha Uhandisi, katika Bandari ya Dar es Salaam, alikuwa katika maandalizi ya mwisho kabla ya kufunga ndoa pia.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, alieleza kuwa ajali hiyo ilisababishwa na mwendokasi wa gari la Chijana wakati akitaka kulipita gari aina ya Toyota Noah yenye namba T841 BVQ, lililokuwa ikiendeshwa na Joseph Bandari mkazi wa Maji ya Chai, Arusha.
“Wakati David (Chijana) akijaribu kuipita Noah, mbele yake kulikuwa na lori linakuja kwa kasi, Sasa akaona ili asikutane nalo uso kwa uso, arudi kushoto. Akaigonga Noah kisha akapoteza mwelekeo na kwenda kugonga miti.” alisema Kamanda Mkumbo.
Aidha, Kamanda Mkumbo alisema watu hao walikufa papo hapo na miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufani ya Mount Meru
mkoani Arusha.
Friday, November 3, 2017
NDUGAI AWAPA BARUA NEC.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai leo Novemba 3, 2017 amemuandikia barua
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC) kumtaarifu kuwa
jimbo la Singida Kaskazini lipo wazi kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa
Mbunge wa jimbo hilo.
Taarifa ya Bunge iliyotolewa leo inasema kuwa jimbo hilo lipo wazi kutokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumfuta Uanachama Lazaro Nyalandu toka Oktoba 30, 2017 siku ambayo Mbunge huyo alitangaza mwenyewe kupitia vyombo vya habari kujivua nafasi zake ndani ya chama hicho na kusema kuwa ameandika barua kwa Spika kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge kupitia CCM.
Taarifa ya Bunge iliyotolewa leo inasema kuwa jimbo hilo lipo wazi kutokana na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumfuta Uanachama Lazaro Nyalandu toka Oktoba 30, 2017 siku ambayo Mbunge huyo alitangaza mwenyewe kupitia vyombo vya habari kujivua nafasi zake ndani ya chama hicho na kusema kuwa ameandika barua kwa Spika kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge kupitia CCM.
TOT PLUS WAJIFUA KUIPUA NYIMBO TATU MPYA UKIWEMO WA KUMUUNGA MKONO JPM KATIKA VITA YA KUTETEA RASILIMALI ZA NCHI
![]() |
Mkurugenzi wa TOT Gasper Tumaini |
Kundi la Tanzania One Theatre (TOT Plus), limo kambini Wanamuziki wake wakijifua vikali katika mazoezi ya nyimbo tatu ambazo kundi hilo litaziipua hivi karibuni.
Akizungumza wakati wa mazoezi ya nyimbo hizo, Mkurugezi wa TOT Plus inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Gasper Tumaini amezitaja nyimbo hizo kuwa ni 'Tumuunge mkono JPM', 'Amani ya Tanzania' na Hongera awamu ya tano'.
Tumaini amsema, wimbo wa 'Tumuunge mkono JPM' ni wa kuwahamasisha Watanzania popote walipo kumuunga mkono Rais Dk John Magufuli katika vita ya uchumi anayoongoza kwa kuhakikisha inaziba mianya inayotishia upotevu au matumizi mabaya ya rasilimali za nchi.
"Kama unavyoona Rais tayari ameshaamua kwa dhati kupigana katika vita ya kubana mianya inayotishia upotevu au matumizi mabaya yanayofanya na baadhi ya watu kutumia rasilimali za nchi vibaya kwa kujinufaisha wao huku taifa likiendelea kuwa masikini
Hii siyo vita ndogo, ni kubwa sana inayohitaji ujasiri na ari kubwa ya kujituma, hivyo ni lazima Watanzania wote tumuunge mkono ili asiyumbishwe na waliokuwa wanajinufaisha na rasilimali hizi", alisema Tumaini wakati wa mazoezi ya nyimbo hizo kwenye ukumbi wa Ofisi ya CCM Mwinjuma, Mwananyamala, Dar es Salaam.
Amesema, wimbo wa 'Amani ya Tanzania' kunahimiza Watanzania ndani na nje ya Nchi kuhakikisha pia wanaienzi amani ya nchi kwa kuunga mkono juhudi za kuiimanrisha zinazofanywa na viongozi wakiongozwa na misingi imara iliyowekwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na pia Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.
Akizungumzia wimbo wa tatu wa 'Hongera awamu ya Tano', Tumaini amesema, wimbo huo ni wa pongezi kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli kwa kutimiza kwa vitendo ahadi zilizotolewa na CCM wakati wa kampeni za kuomba ridhaa ya wananchi katika uchaguzi mkuu uliopita.
"Tumeona ni vizuri kutunga wimbo huu wa kumpongeza kwa sababu utekelezaji wa ilani na ahadi alizokuwa akizitoa kwenye kampeni unaonekana wazi japokuwa sasa ni miaka miwili tu tangu tumchague, kwa kweli Rais Dk. Magufuli amechapa kazi hivyo inastahili kumpongeza", alisema tumaini.
Amesema, nyimbo hizo ambazo ni kwaya tayari zimeshakamilika na sasa wanamuziki wanazifanyia mazoezi ya mwisho mwisho kabla ya kuzirekodi ili zianze kusikika katika maeneo mbalimbali na hasa pale kundi hilo litakapokuwa likitumbuiza.
Mmiliki wa theNkoromoBlog aliyefika kwenye mazoezi ya kundi hilo, alishuhudia wanamuziki wote wakiwajibika kila mmoja katika eneo lake, huku baadhi yao wakitokwa jasho kuliko hata wanapokuwa wakitumbuiza jukwaani katika maonyesho maalum.
Mwanamuziki nguli Juma Abdallah 'Jerry' akikipapasa kinanda kwa mkoni mmoja kuonyesha umahiri wake, Kundi la TOT Plus lilipokuwa katika mazoezi ya nyimbo tatu, leo katika ukumbi wa CCM Mwinjuma, Mwananyamala Dar es Salaam
Waimbaji Neca Twalib aliyechukua nafasi iliyoachwa na aliyekuwa mwimbaji nguli na Mkurugenzi wa TOT Plus Marehemu Kampteni John Komba, akiimba na mwenzake Corobian Mkinga wakati wa mazoezi hayo
Patrick Thomas akizicharaza tumba wakati wa mazoezi hayo
Mkurugenzi wa TOT Plus Gasper Tumaini (mwenye suti) akizungumza na baadhi ya wadau waliofika kushuhudia mazoezi hayo
Jerry akikicharaza kinanda kwa madaha wakati wa mazoezi hayo
Waimbaji Rosemary William, Sharifa Mohammed na Mwasiti Suleimani wakiimba wakati wa mazoezi hayo
Mwimbaji nguli Hadija Kopa na wenzake wakiimba wakati wa mazoezi hayo
Tumaini akiwa na wadau wakati wakifuatilia mazoezi hayo. Kulia ni Jerry
Waimbaji wa TOT Plus wakiwa kwenye mazoezi hayo
Waimbaji wa TOT Plus wakiwa kwenye mazoezi ya wimbo wa 'Amani ya Tanzania'
Jerry na Tumaini wakifuatilia kwa makini mazoezi hayo. Kushoto ni mdau wa TOT Plus
Alen Elias aka Mchungaji akikicharaza kinanda kwa makini
Evans Peter na said Mpiluka wakiyacharaza magita wakati wa mazoezi hayo
Godfrey Kanuti akilicharaza gita wakati wa mazoezi hayo
Neka twalib na Mkinga wakishauriana jambo wakati wa mazoezi hayo
Fundi mitambo akiwajibika wakati wa mazoezi hayo
Tumaini akijadiliana jambo na viongozi wa bendi ya Vijana Jazz ambao walihudhuria mazoezi hayo
Wanamuziki wa TOT Plus wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wakati wa mazoezi hayo.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
DC KIBAHA AUAGIZA UONGOZI WA KAMPUNI YA YAPI MARKEZI KUTATUA KERO ZA WAFANYAKAZI
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama akijadiliana machache na meneja mwajiri wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki wakati alipofanya mkutano wake na vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama akitolea ufafanuzi wa mambo machache kwa vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Asumpter Mshama.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama akaribishwa na uongozi wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki ili aweze kuongea na vijana wasotea ajira walioweka kambi yao kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Mkutano ukiendelea.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama aliyeambatana na viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama wakifanya mkutano wa ndani na vingozi wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki katika mambi yao waliyoiweka kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Kamati ya ulinzi na usalama ikifuatilia kwa karibu.
Mkuu wa wilaya ya Kibaha, Asumpter Mshama (kushoto) na katibu tawala wilaya ya Kibaha Sozi Ng'ate (kulia) wakipata maelezo machache kwa kiongozi wa kampuni ya ujenzi wa reli ya Kisasa ya Yapi Markezi kutoka Uturuki wakati walipotembelea kambi yao iliyopo kijiji cha Soga-Kibaha, Pwani.
Thursday, November 2, 2017
KIKAO CHA MADIWANI HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA CHAVUNJIKA, KITI CHA MSTAHIKI MEYA CHAFICHWA..
Breaking News!
Kikao cha baraza la madiwani Jijini Mwanza kilichokuwa kikiongozwa na yule meya aliyekamatwa na jeshi la polisi asionane na Rais (Mstahiki Meya James Bwire) kimeingia malumbano na mvutano na hata kuvurugika.
Ni takribani miezi miwili sasa hakuna kikao chochote kimeweza kuketi na kujadili namna ya kusukuma shughuli za maendeleo kwa Jimbo la Nyamagana ambako ndiko Halmashauri ya jiji la Mwanza inapatikana.
Leo imeshuhudiwa kikao hicho kuvunjika tena huku kukiwa na giza machoni mwa wananchi wasijue ni lini watapata taarifa zitakazo eleza nini kimefanyika kupitia mipango mbalimbali iliyowekwa awali na hatma kwa mipango ya baadaye..........
VIFARANGA VILIVYO TEKETEZWA KWA MOTO VYAZUA MJADALA.
Watetezi wa haki za wanyama wametoa maoni wakilaani
kuteketezwa vifaranga vya kuku 6,400 vilivyoingizwa nchini kinyume cha
sheria.
Vifaranga hivyo mali ya Mary Matia (23), vyenye thamani ya Sh12.5 milioni vilikamatwa mpakani Namanga vikitokea nchini Kenya.
Kuteketezwa kwa vifaranga hivyo juzi kumeibua mjadala ikielezwa kitendo hicho ni ukiukwaji wa sheria.
Kazi ya kuviteketeza eneo la Namanga wilayani Longido ilifanyika ikishuhudiwa na maofisa wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Wizara ya Mifugo, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na vyombo vingine vya ulinzi na usalama.
Akizungumza wakati wa kuviteketeza vifaranga hivyo, ofisa mfawidhi wa kituo cha udhibiti wa magonjwa ya mifugo Kanda ya Kaskazini, Obedi Nyasebwa alisema kazi hiyo imefanyika kwa kuzingatia Sheria ya Magonjwa ya Wanyama namba 17 ya mwaka 2003.
Pia, alisema Serikali mwaka 2007 ilitoa tangazo kupiga marufuku kuingizwa nchini vifaranga vya kuku na mayai.
Hata hivyo, watu mbalimbali wamehoji ulazima wa kuviteketeza vifaranga hivyo badala ya kuvirudisha vilikotoka kama alivyoomba mmiliki wake Matia.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ustawi wa Wanyama (Taweso), Dk Thomas Kahema akizungumza na Mwananchi jana alisema anatambua dhamira ya Serikali ya kuzuia magonjwa ya kuambukizwa kutoka nchi jirani, lakini kulikuwa na njia mbadala ya kufanikisha suala hilo.
Dk Kahema alisema mamlaka za Serikali zilitakiwa kuvirudisha vifaranga hivyo vilikotoka ili visieneze magonjwa kama inavyohofiwa. Alisema kuviteketeza ni ukatili ambao hauungi mkono na kwamba, wanalaani kitendo hicho ambacho kinatoa taswira mbaya kwa Taifa linaloonekana halijali haki za wanyama.
“Zipo njia nyingi ambazo wangeweza kutumia mbali na kuchoma, mbona wakikamata ng’ombe hawawachomi moto?” alihoji Dk Kahema.
Alisema Sheria ya Ustawi wa Wanyama ya mwaka 2008 inasisitiza kutambuliwa kwa haki za wanyama, kwa hiyo kuteketezwa vifaranga hivyo kunaonyesha jinsi utekelezaji wa sheria unavyoibua utata.
Dk Kahema alisema vifaranga hivyo vingepimwa kubaini kama vina maambukizo na ingebainika havina vingetaifishwa au kugawiwa wajasiriamali, magereza au vituo vya watoto yatima.
Alisema hana uhakika kama sheria iliyotumika kuteketeza vifaranga hivyo inaeleza wazi kwamba viteketezwe.
Mkurugenzi mtendaji huyo amesema mamlaka hazikuweka wazi kama vifaranga hivyo vilikuwa na maambukizo.
Alisema vifaranga havina hatia bali aliyevileta ndiye anayetakiwa kuchukuliwa hatua.
Baadhi ya wananchi kupitia mitandao ya kijamii wameonyesha kutoridhishwa na hatua iliyochukuliwa na mamlaka za Serikali wakieleza ni ukatili dhidi ya wanyama.
Abbas King aliandika kwenye ukurasa wa Facebook wa Mwananchi kuwa, “Hivyo vifaranga vina roho au vinaendeshwa kwa umeme? Kwa nini msivigawe kwa watoto yatima wakafuge vikue wafanye kitoweo, kama vina madhara virejeshwe kwao, walioleta wapigwe faini.”
Tumaini Kyama aliandika katika ukurasa huo kuwa, “Swali langu ni kuwa kama alikuwa kachukua mkopo wa biashara huyo mmiliki wa hivyo vifaranga mkopo ataurudisha na nani sitaki kujua hayo mengine nimewaza kwa sauti tu. Tunapambana na umasikini au tunafurahia umasikini wa baadhi ya watu.”
“Ukiukwaji wa sheria ya wanyama na pia wamerudisha maendeleo nyuma. Vilevile hawajavipima vifaranga na kutufahamisha vina magonjwa gani na hata hivyo si wangevirudisha vilikotoka ili aliyevinunua arejeshewe fedha yake na kama ni faini apigwe ili iwe funzo kwa wafanyabiashara,” aliandika Lightdod Shayo.
Vifaranga hivyo mali ya Mary Matia (23), vyenye thamani ya Sh12.5 milioni vilikamatwa mpakani Namanga vikitokea nchini Kenya.
Kuteketezwa kwa vifaranga hivyo juzi kumeibua mjadala ikielezwa kitendo hicho ni ukiukwaji wa sheria.
Kazi ya kuviteketeza eneo la Namanga wilayani Longido ilifanyika ikishuhudiwa na maofisa wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Wizara ya Mifugo, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na vyombo vingine vya ulinzi na usalama.
Akizungumza wakati wa kuviteketeza vifaranga hivyo, ofisa mfawidhi wa kituo cha udhibiti wa magonjwa ya mifugo Kanda ya Kaskazini, Obedi Nyasebwa alisema kazi hiyo imefanyika kwa kuzingatia Sheria ya Magonjwa ya Wanyama namba 17 ya mwaka 2003.
Pia, alisema Serikali mwaka 2007 ilitoa tangazo kupiga marufuku kuingizwa nchini vifaranga vya kuku na mayai.
Hata hivyo, watu mbalimbali wamehoji ulazima wa kuviteketeza vifaranga hivyo badala ya kuvirudisha vilikotoka kama alivyoomba mmiliki wake Matia.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Ustawi wa Wanyama (Taweso), Dk Thomas Kahema akizungumza na Mwananchi jana alisema anatambua dhamira ya Serikali ya kuzuia magonjwa ya kuambukizwa kutoka nchi jirani, lakini kulikuwa na njia mbadala ya kufanikisha suala hilo.
Dk Kahema alisema mamlaka za Serikali zilitakiwa kuvirudisha vifaranga hivyo vilikotoka ili visieneze magonjwa kama inavyohofiwa. Alisema kuviteketeza ni ukatili ambao hauungi mkono na kwamba, wanalaani kitendo hicho ambacho kinatoa taswira mbaya kwa Taifa linaloonekana halijali haki za wanyama.
“Zipo njia nyingi ambazo wangeweza kutumia mbali na kuchoma, mbona wakikamata ng’ombe hawawachomi moto?” alihoji Dk Kahema.
Alisema Sheria ya Ustawi wa Wanyama ya mwaka 2008 inasisitiza kutambuliwa kwa haki za wanyama, kwa hiyo kuteketezwa vifaranga hivyo kunaonyesha jinsi utekelezaji wa sheria unavyoibua utata.
Dk Kahema alisema vifaranga hivyo vingepimwa kubaini kama vina maambukizo na ingebainika havina vingetaifishwa au kugawiwa wajasiriamali, magereza au vituo vya watoto yatima.
Alisema hana uhakika kama sheria iliyotumika kuteketeza vifaranga hivyo inaeleza wazi kwamba viteketezwe.
Mkurugenzi mtendaji huyo amesema mamlaka hazikuweka wazi kama vifaranga hivyo vilikuwa na maambukizo.
Alisema vifaranga havina hatia bali aliyevileta ndiye anayetakiwa kuchukuliwa hatua.
Baadhi ya wananchi kupitia mitandao ya kijamii wameonyesha kutoridhishwa na hatua iliyochukuliwa na mamlaka za Serikali wakieleza ni ukatili dhidi ya wanyama.
Abbas King aliandika kwenye ukurasa wa Facebook wa Mwananchi kuwa, “Hivyo vifaranga vina roho au vinaendeshwa kwa umeme? Kwa nini msivigawe kwa watoto yatima wakafuge vikue wafanye kitoweo, kama vina madhara virejeshwe kwao, walioleta wapigwe faini.”
Tumaini Kyama aliandika katika ukurasa huo kuwa, “Swali langu ni kuwa kama alikuwa kachukua mkopo wa biashara huyo mmiliki wa hivyo vifaranga mkopo ataurudisha na nani sitaki kujua hayo mengine nimewaza kwa sauti tu. Tunapambana na umasikini au tunafurahia umasikini wa baadhi ya watu.”
“Ukiukwaji wa sheria ya wanyama na pia wamerudisha maendeleo nyuma. Vilevile hawajavipima vifaranga na kutufahamisha vina magonjwa gani na hata hivyo si wangevirudisha vilikotoka ili aliyevinunua arejeshewe fedha yake na kama ni faini apigwe ili iwe funzo kwa wafanyabiashara,” aliandika Lightdod Shayo.
RC GEITA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA LIPA KWA MATOKEO HALMASHAURI YA MJI GEITA.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akitoa maelekezo kwa
Mkuu wa Wilaya ya Geita(Wakwanza kushoto) na Mwalimu Mkuu wa Shule ya
Msingi Nguzombili wakati wa ziara yake katika Shule hiyo.
|
Mkuu wa Mkoa wa Geita akiingia ndani ya moja ya darasa lililojenjwa chini ya mpango wa lipa kwa matokeo shule ya Msingi Nguzo Mbili. |
(PICHA NA JUMAPILI MAGESA)
Mkuu wa Mkoa
wa Geita Mhandisi Robert Lughumbi ameipongeza Halmashauri ya Mji wa Geita kwa
kusimamia vizuri fedha za ujenzi wa vyumba vya madarasa vilivyo chini ya mpango
wa lipa kwa matokeo shule ya msingi Nguzo mbili.
Akizungumza
wakati wa ziara yake katika shule hiyo Mheshimiwa Robert Gabriel alisema kuwa
ameridhishwa na kiasi cha fedha kilichotumika katika ujenzi wa madarasa kwa
ubora wa hali ya juu katika shule hiyo.
" Inashangaza sana kuona maeneo mengine
wanatumia fedha zote kiasi cha shilingi 20 milioni katika ujenzi wa darasa moja
lakini kuna mapungufu mengi hivyo lazima kuwe na nidhamu ya matumizi ya fedha
katika miradi ya Serikali"Alisema Lughumbi.
Akiwa
shuleni hapo Mkuu wa Mkoa ameagiza wakurugenzi kuunda na kutumia vikundi vya
ujenzi vilivyo katika maeneo ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa madarasa pia
kuishirikisha jamii ili kupunguza gharama kwa serikali na hatimaye fedha
zinazobaki ziwezekufanya mambo mengine katika huduma za jamii.
Katika hatua
nyingine Mhandisi Robert Gabriel aliutaka uongozi wa Shule ya Msingi Nguzo
Mbili kusimamia suala la usafi na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa
Geita kuhakikisha anasimamia uimarishaji wa miundombinu hiyo ambayo mingine
imeanza kupasuka.
Aidha, ameagiza shule
hiyo kupelekewa miundombinu ya maji ili vyoo vilivyojengwa vianze kutumika
badala ya kufungwa.Pamoja na kutembelea Shule ya Msingi Nguzo Mbili Mkuu wa
Mkoa pia ameitembelea shule ya Sekondari na kukagua ujenzi wa vyumba vinne vya
madarasa vilivyojengwa kupitia mpango wa lipa kwa matokeo.
Vyumba vya madarasa vilivyojengwa kupitia mpango wa lipa kwa matokeo Halmashauri ya Mji Geita. |
Mkoa wa
Geita una upungufu wa vyumba vya madarasa 8600 hivyo serikali imeandaa mpango
kabambe wa kutokomeza tatizo hili kwa kushirikiana na jamii na wadau wote wa
Mkoa katika ujenzi wa vyumba vya madarasa.
Imeandaliwa na mtandao wa maduka online.
MKUU WA MKOA WA PWANI INJINIA EVARIST NDIKILO AWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA KIWANDA CHA KUTENGENEZEA CHAKI KISARAWE
Thursday, November 02, 2017
No comments
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo
akizungumza na wananachi na baaadhi ya viongozi mbali mbali wa serikali mara
baada ya kuweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho cha chaki cha Mkongoma
kiichopo Wilayani Kisarawe. (PICHA NA VICTOR MASANGU)
Mkurugenzi mtendaji wa kiwanda cha chaki Geofrey
Mkongoma akitoa risala fupi kwa mgeni
rasmi mara baada ya kiwanda hicho kuwekea
jiwe la msingi na Mkuu wa Mkoa wa Pwani .
Mkuu wa
Wilaya ya Kisarawe Happines Seneda akizungumza na wananchi waliofika katika
sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi katika kiwanda hicho cha chaki.
Baadhi ya viongozi wa halmshauri ya Wilaya ya
Kisarawe wakiwa katika halfa hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi katika kiwanda
hicho cha chaki.(PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU)
NA VICTOR MASANGU, KIRASAWE
KATIKA kuunga mkono juhudi za Rais wa serikali ya awamu ya
tano Dk. John Pombe Magufuli katika kuwa na uchumi wa viwanda,Mkuu wa Mkoa wa
Pwani Injinia Evarist Ndikilo amewataka wawekezaji wote kuhakikisha wanaachana
kabisa na tabia ya kukwepa kulipa kodi na
badala yake watimize wajibu wao ipasavyo bila ya kuvunja sheria na taratibu za
nchi ili kuweza kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kwa wananchi.
Injinia Ndikilo ametoa kauli hiyo wakati wa halfa ya uwekaji wa jiwe la msingi katika
kiwanda cha chaki kinachoendelea kujengwa katika awamu ya kwanza katika kijiji
cha Msanga zalala kata ya Msimbu Wilayani Kisarawe na kuhudhuriwa na viongozi
mbali mbali wa , serikali, madhehebu ya dini pamoja na watendaji wa serikali za vijiji na vitongoji.
Pia Mkuu huyo alibainisha kuwa katika uwekezaji wa viwanda
katika Mkoa wa Pwani baadhi ya maeneo bado yanakabiliwa na changamoto ya
kutokuwa ni nishati ya umeme wa uhakika pampja na kuwepo kwa mioundimbinu
mibovu ya barabara hivyo ameagiza mamlaka zote zinazohusika kulifanyia kazi
suala hilo ili kuweza kuwavutia wawekezaji wengine.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Happiness Seneda alitoa wito kwa wananchi
wengine kutumia fursa zilizopo katika kujifunza mambo mbali mbali ya
ujasiriamali na kuanzisha viwanda vidogo
vidogo kwa lengo la kuweza kuunga juhudi za serikali ya awamu ya tano ya kuwa
na uchumi wa kati pamoja na kuwapa nafasi zaidi wawekezaji ambao ni wazawa ili
waweze kutoa fursa za ajira kwa vijana.
Awali Mkurugenzi
mtendaji wa kiwanda hicho cha chaki Geofrey Mkongoma akisoma taarifa yake ameiomba serikali ya
awamu ya tano kuweza kuwapa fursa ya kipekee wazawa wa
Tanzania katika suala zima la
uwekezaji wa ujenzi wa viwanda vidogovidogo huku akitaja akisema changamoto
kubwa ni suaala la umeme wa uhakika.
Alisema kuwa lengo lake kubwa ni kuhakikisha anaunga mkono
juhudi za serikali ya wamu ya tano katika kuwa na uchumi wa viwanda hivyo
ataendelea kushirikiana bega kwa began a wadau wengine kwa lengo la kuweza
kufanikisha malengo aliyojiwekea ya kuweza kutoa fursa za ajira kwa wazawa
pamoja na kuongeza uzalishaji wa chaki.
“Hiki kiwanda kilianza tangu mwaka 2013 na kwa sasa kama
mnavyoona mimi nimeshaajiri wafanyakazi
wapatao 38. Ambao ninawalipa kutokana na kiwanda hiki cha chaki hivyo kitu
kikubwa ninachokiomba kwa serikali ni kutoa sapoti kubwa zaidi kwa wawekezaji
ambao ni wazawa ili waweze kuendelea kujenga viwanda vidogo vidogo ili kuweza
kukuza uchumi wa nchini,”alisema Mkurgenzi Mkongoma.
Nao baadhi ya wakinamama ambao wanafanya kazi katika kiwanda
hicho cha chaki akiwemo Tedy Mzingula na Shoboa Msagasa wamesema kuwa
kipato wanachokipata kinaweza kuwabadilisha kwa kiasi kikubwa katika suala zima
la kujikwmau kimaisha kutokana na kuendesha familia zao ikiwemo kuwasomesha
watoto walionao pamoja na kuwahudumia mahitaji madogo madogo.
“Sisi kwa kwli kama wafanyakazi wa kiwanda hiki tunapenda
kumshukuru Mkurugenzi wetu kwa kuweza kupenda katika hali na mali, na kutokana
na kufanya kazi hii fedha ambayo tunaipata inatusaidia kwa kiasi kikubwa katika
kuendesha familia zetu, kwani wengne tuna watoto ambao tunawasomesha na maisha
yanaendelea lakini kikubwa ni serikali kumsaidia kuweza kupata umeme,”walisema.
KIWANDA hicho cha chaki ambacho kinajulikana kwa jina
la Mkongoma Chalk Factor kilianzishwa
mnamo mwaka 2013 ambapo kwa sasa kina jumla ya wafanyakazi zaidi ya 38 wakiwemo
vijana pamoja na wakinamama kutoka maeneo mbali mbali ya Wilaya hiyo ya
Kisarawe.
WALIMU WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA UJASIRIAMALI KWAAJILI YA KUJIINUA KIUCHUMI.
Walimu wa wilaya ya Geita wakiwa kwenye Kikao cha kujadili maendeleo na changamoto ndani ya chama cha walimu Wilaya ya Geita. |
Katibu wa chama cha Walimu Wilaya ya Geita,John Kifimbi akisoma risala kwa Mgeni rasmi. |
Baadhi ya wageni waalikwa ambao wanatoka taasisi mbali mbali wakifuatilia kikao hicho. |
Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akitoa vyeti kwa walimu ambao wamefanya vizuri ndani ya chama hicho. |
Mwenyekiti wa chama cha walimu(CWT)Wilaya ya Geita,Alfred Alexander akiwasisitiza walimu kuendelea kuwa na mshikamao ndani ya chama hicho. |
Mkuu wa Wilaya ya Geita,Mwl Herman Kapufi akiwasisitiza walimu kujingea tabia ya kuwa na vitega uchumi mbali mbali kwenye mazingira ambayo wanafanyia kazi. |
Walimu
Wilayani Geita wametakiwa kutumia nafasi walizonazo katika kujiinua kiuchumi
kwa kuwekeza kwenye Shughuli za ujasiriamali.
Rai
hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Geita,wakati wa Mkutano mkuu wa chama cha
Walimu (CWT)Wilaya ya Geita ambao umefanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa
halmashauri ya Mji lengo likiwa kuangalini ni kipi chama kimefanya ndani ya
miaka Miwili.
alisema kuwa wakati umefika kwa walimu kuwekeza katika fursa
za ujasiriamali na kutokuogapa kukopa na kwamba kama kuna mtu ambaye anampiga
vita mwalimu kuwekeza na huku anatekeleza majukumu yake ya msingi ni sawa na
kutokumtendea haki.
“Lengo
la kuandaa vitega uchumi kabla ya uzee na manufaa ya uwekezaji ni kwa manufaa
ya jamii kwa hiyo walimu kama kuna mtu anakupiga vita kwa ajili ya uwekezaji na
unafundisha kwa wakati sahihi mtu huyo nipeni taarifa”Alisema Kapufi.
Mwenyekiti
wa chama cha walimu Mkoani Humo,Mwl Lusato Zabron Mashauri ,ameelezea kuwa hali
ya kiuchumi bado ni mbaya kwa walimu hususani wale ambao wanaishi vijijini
wengi wao wamekuwa wakishindwa kufanya biashara kutokana na viongozi wengi wa
kisiasa kutokuwa na uelewa juu ya haki za walimu.
“Hali
ya kiuchumi kwa walimu hairidhishi hususani wale ambao wanaishi vijijini kwani
wengi wao wamekuwa wakipigwa vita na viongozi wa kisiasa mwalimu anapojaribu
kuinuka kiuchumi anapigwa vita na viongozi ao”Alisema Lusato.
Kemilembe
Gerigori ambaye anawawakilisha walimu wanawake Mkoani Humo,alisema hali ya
mazingira ya walimu ni magumu kutokana na namna ambavyo wamebanwa katika suala
la muda wa masomo hivyo wengi wao wamekuwa wakishindwa kujishughulisha na
ujasiriamali kwa kukosa muda.
Subscribe to:
Posts (Atom)