ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, June 23, 2012

CHEREKO LA NDOA YA FRANCO R. & BI. AJUNA R.



Bwana Franco Ruhinda akiwa na mkewe Ajuna Reguza wakionyesha cheti chao cha ndoa mara baada ya kufunga pingu za maisha katika kanisa la KKKT Makuburi jijini Dar es Salaam.


Bwana Franco Ruhinda akiwa na mkewe Ajuna Reguza wakionyesha cheti chao cha ndoa mara baada ya kufunga pingu za maisha katika kanisa la KKKT Makuburi jijini Dar es Salaam.


Bwana Franco Ruhinda na mkewe Ajuna Reguza wakikabidhiwa cheti chao cha ndoa na mchungaji wa kanisa hilo, mara baada ya kufunga pingu za maisha katika kanisa la KKKT Makuburi jijini Dar es Salaam.


Bwana Franco Ruhinda akitia saini cheti cha ndoa yupa yake anayemshuhudia ni mkewe Ajuna Reguza pampja na mchungaji wa kanisa la KKKT Makuburi jijini Dar es Salaam.


Bi. Ajuna Reguza wakisaini cheti cha ndoa mara baada ya kufunga pingu za maisha katika kanisa la KKKT Makuburi jijini Dar es Salaam.


Bi. Ajuna Reguza akisoma kiapo wakati akifunga pingu za maisha na mumewe Bw. Franco Ruhinda katika kanisa la KKKT Makuburi jijini Dar es Salaam.


Bwana Franco Ruhinda akivalisha pete mkewe Ajuna Reguza wakati wakifunga pingu za maisha katika kanisa la KKKT Makuburi jijini Dar es Salaam.


Bi. Ajuna Reguza akivalisha pete mumewe Franco Ruhinda ikiwa ni ishara ya kuwa pamoja wakati wakifunga pingu za maisha katika kanisa la KKKT Makuburi jijini Dar es Salaam.


Bwana Franco Ruhinda akiwa na mkewe Ajuna Reguza wakitoka kanisa. Picha/www.kajunason.blogspot.com

DIWANI MABULA AKABIDHI BAJAJI YA KUBEBEA WAGONJWA KWA ZAHANATI YA SHADI

 Pichani diwani wa kata ya Mkolani Stanslaus Mabula akimkabidhi ufunguo wa bajaji ya  kubebea wagonjwa kwa mwenyekiti wa mtaa wa Shadi bw. Anthony Mabasi. Ni takribani miaka 22 wananchi wa mitaa ya Shadi, Luchelele kati, Luchelele Ziwani na Sweya kata ya Mkolani wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza wamekuwa wakitaabika kupata usafiri kwa nyakati zote (mchana na usiku) kiasi cha kutembea zaidi ya km 14 kupata zingine.

Video diwani Mabula.

 Akipokea msaada huo mwenyekiti wa mtaa wa Shadi, Anthony Mabasi amempongeza diwani huyo kwa kujibidiisha hadi kufanikiwa kulitatua tatizo hilo lililokuwa likikikabili kijiji chake na kuahidi kushirikiana na watumishi wa zahanati hiyo kuitunza Ambullance hiyo ili iweze kutoa huduma kwa muda mrefu.

 Diwani wa kata ya Mkolani Stanslaus Mabula akijaribu Ambulance hiyo ya magurudumu matatu huku akiwa amembeba mwanakijiji wa Shadi aliyehudhuria makabidhiano hayo.

 Changamoto kubwa kwa Zahanati hiyo ilikuwa ni pale ilipokuwa ikipata wagonjwa wakiwemo wanawake wajawazito kufikishwa katika hospitali hiyo hasa nyakati za usiku huku wengine wakihitaji kupelekwa kwenye hospitali ya wilaya iliyoko Butimba umbali wa km 14 kupata tiba zaidi ambazo haziwezi kutatuliwa kwenye zahanati hiyo wengi walikuwa wakipoteza uhai kwa kukosa usafiri.

 Pamoja na kukabidhi Ambulance hiyo ya magurudumu matatu pia diwani huyo ametoa msaada wa mabenchi mawili madhubuti kwaajili ya watu wanao hudhuria kituo hicho cha afya.

 Picha ya pamoja.

Kutokana na msaada huo wagonjwa wote wakiwemo wajawazito watarahisishiwa kupata huduma ya usafiri bure iwapo wataamriwa kupelekwa hospitali ya wilaya kupata tiba zaidi.

MASHALI V/S SAMSON ULINGONI-Friends Corner Hotel jumapili

 Mabondia Thomas Mashali na Maisha Samson wamemaliza zoezi zima la upimaji na tayari kwa ajili ya mpambano wao utakao fanyika katika ukumbi wa Friends corner hotel-manzese siku ya jumapili 24/6/2012.

Mpambano huo wa ubingwa wa taifa wa TPBO uzito wa midle na unaosimamiwa na TPBO chini ya rais wake Yasin Abdallah na katibu mkuu Ibrahim Kamwe umemalizika vizuri na mabondia wote wapo katika hali nzuri na tayari kwa fight.

Zoezi zima la upimaji lilisimamiwa na Ibrahim kamwe na kueleza kuwa mabondia hao wote wawili kwa pamoja wamepata @kilo 71 na watacheza raundi kumi.
Pia kutakuwa na mapambano ya utangulizi kama ifuatavyo;
Juma Fundi (52kg) v/s shaban madilu (49.5kg) - watacheza raundi nane
Mohamed Shaban'ndonga' (61kg) vs Musa hassan (61kgs) - watacheza raundi sita
Jonas godfrey (61.5kgs) vs Venance mponji(59kg) - watacheza raundi sita
Abdalah mohamed'prince naseem'(64kgs) vs Yohana Mathayo(65.5kgs)- raundi sita
Nasoro Hatibu 55kg vs Abdul Athuman 55kgs -watacheza raundi nne
Martin Richard 50kgs vs Hassan Kadenge 49kgs -watacheza raundi nne

Ngumi zitaanza kama kawaida kuanzia saa kumi jioni, na tunarudia tena kusema katika ngumi hakuna kupendelea na TPBO itasimamia kwa haki zote bila kuangalia mtu. tutakachoangalia ni mchezo kuchezwa kwa kanuni za ngumi na utoaji points kulingana na bondia anavyoscore kwa ngumi halali sio kulingana na makelele ya washabiki.


Wako
IBRAHIM ABBAS KAMWE-BigRight
Katibu Mkuu TPBO

SIMBA YAITWANGA TOTO 2-0 DIMBANI CCM KIRUMBA

Kikosi cha Simba leo dimbani CCM Kirumba kutoka kushoto ni Abdullah Juma, Amri Kiemba, Haruna Shamte, Salim Kinje, Hassan Kondo, Haroon Othman, Paul Ngalewa, Abdallah Seseme, Uhuru suleiman, na Obadia Mungusa. Aliyesimama mbele ni golikipa Hamadi Waziri.

Kikosi cha Toto Africans leo dimbani CCM Kirumba.

Waamuzi wakiwa na manahodha wa timu zote mbili.

Benchi la timu ya Simba, Kaseja akiwa kwenye benchi (mwenye head phone).

Mkuu wa mkoa wa Mwanza akisalimiana na wachezaji wa Simba.

Mkuu wa mkoa akitoa nasaha kwa timu za Toto na Simba kabla ya kuanza kwa mpambano wa kirafiki katika uwanja wa CCM Kirumba huku akiwa na viongozi, kushoto kwake ni mwenyekiti wa MZFA Jackson Songora,  mkuu wa wilaya ya Kwimba Suleiman Mzee na kulia kwake ni Omar Juma ambaye ni kamisaa wa mchezo huu na mjumbe wa TFF Samwel Nyala.

Salaam kabla ya mchezo.

 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akiwa na Jack Fish pamoja na Mjumbe wa TFF Samwel Nyala wakifuatilia mpambano wa kirafiki baina ya Simba na Toto Africans ya Mwanza.

Upande wa jukwaa la mashabiki wa wekundu wa Msimbazi wakishangilia baada ya kupata goli kipindi cha kwanza lililofungwa na Uhuru Selemani.

Wadau na pesa zao jukwaa kuu wakiongozwa na Mc Maarufu jijini Mwanza Mc Bonke.  
Goli la pili la Simba limepatikana kipindi cha pili kupitia mchezaji Salim Kinje.

Hadi mwisho Simba 2 Toto 0.

Friday, June 22, 2012

RONARDO AIWEZESHA URENO KUTINGA 1/2 FAINALI Euro 2012


Mshambulizi Cristiano Ronaldo aliwaridhisha mashabiki wa Ureno kwa kucheza vizuri sana usiku wa Alhamisi, na juhudi zake kuiwezesha nchi yake kuishinda Jamhuri ya Czech bao 1-0 katika mechi ya mwanzo ya robo fainali ya Euro 2012, na kufanikiwa kuifikisha hadi nusu fainali.

Ronaldo, ambaye alifunga magoli mawili wakati katika mechi ya awali ya mashindano hayo nchi yako ilipocheza na Uholanzi, aliweza kugonga mwamba katika nusu ya kwanza na ya pili katika mechi dhidi ya Jamhuri ya Czech.

Ureno sasa itakutana aidha na Uhispania au Ufaransa katika juhudi za kufuzu kwa fainali.

PICHA YA WIKI NI KAZI LAKINI SOMETIMES KAMA BURUDANI HIVI

Hii ndiyo style ya ubebaji vyungu kuvihamisha toka eneo la uchomaji kwa ajili ya kuviimarisha hadi sokoni kwamteja. Utamtaka bi dada!!!?

NKABAaaaaa....!!! ..YONDANI ATUA YANGA

Awa kivutio mazoezini" "Gazeti moja laumbuka kwa propaganda za Simba"
"Kisa eti ametekwa na Simba"
Hatimaye aliyekuwa beki wa kutumainiwa wa klabu ya Simba katika msimu uliopita Kevin Yondan "Vidic" leo amekata mzizi wa fitina baada ya kuanza rasmi mazoezi katika uwanja wa Kaunda uliopo Makao Makuu ya klabu ya Yanga na kuwa kivutio katika mazoezi hayo.

Kipenzi hicho cha Yanga kiliwasili majira ya saa tatu kasoro dakika kumi asubuhi, ambapo mara baada ya kushuka katika gari mashabiki waliofurika katika mazoezi hayo walipomuona ghafla walimshangilia kwa vifijo na nderemo huku akielekea uwanjani akiwapungia mashabiki hao mikono.

Vidic ambaye ana mapenzi makubwa na klabu ya Yanga, leo ameripotiwa na chombo kimoja cha habari kuwa eti alitekwa hapo jana na klabu ya Simba na kudaiwa kushiriki katika mazoezi na timu yake hiyo ya zamani.

Kelvin Yondan

Mchezaji huyo ambaye kila kukicha timu yake hiyo ya zamani ikiendelea kumuota kwa mazuri aliyowafanyia amekuwa gumzo kwa kipindi hiki cha usajili ambapo timu yake mpya ya Yanga ikiendelea kufanya kufuru ya usajiri ambao unatarajiwa kumalizika Julai 15 Mwaka huu.

Yondan hivi karibuni aliwashukuru wanachama na wapenzi wa klabu ya Simba kwa ushirikiano aliokuwa akiupata wakati akiitumikia timu hiyo,aliweka bayana mara baada ya kumwaga wino kuichezea Klabu ya Yanga kuwa Simba isihangaike na yeye kwakuwa hana mpango tena wa kuichezea klabu yake ya zamani.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mwanachama mmoja wa klabu ya Simba kwa jina maaraufu (Kobe) muda mfupi uliopita wakati www.youngaficans.co.tz ikiwa mitamboni aliwasili katika mazoezi ya timu ya Yanga yaliyokuwa yakifanyika katika uwanja wa Kaunda kwa ajili ya kutaka kuhakikisha juu ya uvumi wa beki Kevin Yondan kuwa yupo katika mazoezi.

Mara baada ya kumshuhudia mchezaji huyo akifanya mazoezi mwanachama huyo aliangua kilio uwanjani hapo huku mashabiki wa Yanga wakishangilia na kumnunulia maji ya matunda pamoja na uji.
Wachezaji wengine walioanza mazoezi leo ni pamoja na kiungo wa timu ya Taifa Frank Domayo aliyekuwa JKT Ruvu na mshambuliaji wa timu ya Taifa Saimon Msuva aliyekuwa Moro United.

Naye Kocha msaidizi wa Klabu ya Yanga Fredy Felix Minziro amesema kikosi chake chote kinatarajiwa kukamilika mara baada ya wachezaji Haruna Niyonzima aliyekuwa na timu ya Taifa lake(Rwanda) na Rashid Gumbo anayeumwa malaria watakapojiuunga na kikosi hicho.
Habari kwa hisani ya http://www.youngafricans.co.tz

AIRTEL YATOA VIFAA VYA MICHEZO KWA SHULE ZA MSINGI ZA GONGOLAMBOTO

 Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde akikabidhi jezi za mpira kwa Mwalimu wa Taaluma na michezo wa shule ya msingi ya Gongolamboto Jaika Mwl Almasi Shemdoe wakati Airtel ilipotembelea shule za msingi za Gongolamboto za Mwangaza, Maarifa na Gongolamboto Jaika na kugawa vifaa vya michezo hapo Jana

 Walimu wa shule za msingi za Mwangaza, Maarifa na Gongolamboto Jaika wakiwa na jezi zao mara baada ya kukabithi vifaa vya michezo na Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel, makabithiano hayo yalifanyika katika shule ya msingi Maarifa Gongolamboto jijini Dar es Saalam. Pichani (Katikati) ni Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde

 Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde akikabidhi jezi za mpira kwa Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Maarifa Mwl Marietha Mulyalya wakati Airtel ilipotembelea shule za Mwangaza, Maarifa na Gongolamboto Jaika Gongolamboto na kukabidhi vifaa vya michezo hapo Jana

 Afisa uhusiano wa Airtel Jane Matinde akikabidhi jezi za mpira kwa Mwalimu wa Taaluma na michezo wa shule msingi ya Mwangaza Mwl Abdul Mwarami wakati Airtel ilipotembelea shule za Mwangaza, Maarifa na Gongolamboto Jaika Gongolamboto na kukabidhi vifaa vya michezo hapo Jana

Walimu wa shule za msingi za Mwangaza, Maarifa na Gongolamboto Jaika wakiteja jambo mara baada ya kukabithiwa vifaa vya michezo na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel.
 Kikundi cha kwaya cha shule ya msingi ya Maarifa kitumbuiza wakati wa hafla ya kukabithiwa vifaa vya michezo illiyofanywa na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel katika shule ya msingi Maarifa Gongolamboto jijini Dar esa saalam

Na Mwandishi wetu.
Shule za msingi zilizoko Gongolamboto Dar es saalam zimenufaika na vifaa vya michezo vilivyotolewa na kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel jana katika halfa fupi iliyofanyika katika shule ya msingi maarif. Airtel imetoa vifaa vya michezo lengo likiwa ni kuleta hamasa na kuwajenga wanafunzi katika mchezo wa soko wakiwa mashuleni na katika umri mdogo.
Vifaa hivyo vya michezo vimetolewa na Airtel kwa shule za Msingi za Mwangaza, Maarifa na Gongolamboto Jaika ambapo kila shule ilipata seti moja ya jezi na Mipira.

Akiongea mara baada ya kupokea vifaa hivyo mkuu wa shule ya maarifa Bi Marieta Mulyalya alisema “ Natoa shukurani zangu za dhati kwa Airtel kwa kutoa vifaa vya michezo kwa shule za Gongolamboto na kuahidi kuvitumia vizuri kwa manufaa ya shule na wanafunzi na washukuru Airtel kwa msaada wa madawati ambayo walituleate wiki chache zilizopita na tunawaomba Airtel
waendelee kutoa msaada si kwa shule yake tu bali na kwa shule za jirani pia ambazo pia zina mahitaji Mengi”.

Akiongea kwa niaba ya Airtel Afisa Uhusiano wa Airtel Bi Jane Matinde alisema” Airtel inatambua mchango wa michezo mashuleni na katika kuendeleza kuinua kiwango cha soka nchini ndio maana tunaendelea kuwawezesha wanafunzi hawa kuendeleza mchezo wa mpira kwa kuchangia vifaa hivi muhimu. Tunaamini jezi hizi zitatumika katika michuano mbalimbali shule ili kuwawezesha kukuza vipaji vyao ambapo matokeo yake ni kuzalisha kikosi kizuri cha timu ya taifa”

Mwenzi uliopita Airtel ilitoa madawati kwa shule ya Maarifa na kuwawezesha wanafunzi kupata madawati ya kukali ambayo ilikuwa changamoto kubwa shuleni hapa kwasababu shule hzo ni kati ya shule zilizoathiriwa na mlipuko wa mabomu uliotokea katika ghala la kuifadhia silaa la Gongolamboto.

“leo tunayofuraha kuwapatia vifaa vya michezo shule ya maarifa pamoja na shule za jirani za Mwangaza na Gongolamboto Jaika,. Airtel bado inaendelea kutoa vifaa vya michezo ambapo hivi karibuni inategemea kugawa vifaa vya michezo kwa Zaidi ya shule kumi zilizoko Nyanda za juu kusini ikiwemo mikoa ya Iringa, Mbeya, Ruvuma, Songea na Rukwa” alimalizia kusema Bi Matinde.

Airtel imekuwa mstari wa mbele kuchangia katika sekta ya michezo lengo likiwa ni kukuza maendeleo ya michezo hapa nchini, mwaka huu Airtel kwa mara nyingine iimeendelea kuendesha program yake ya kuinua vipaji vya vijana chini ya miaka 17 ijulikanayo kama Airtel Rising Stars ambapo vijana wengi wameweza kufaidika na program hiyo.

SIMBA WAWASILI MWANZA na KESHO KUKIPUTA NA TOTO CCM KIRUMBA

Simba imewasili leo jijini kwa pipa.

 Msafara wa Simba katikati ya jiji la Mwanza hapa ni barabara ya Nyerere.


Ziara ya Simba imeanza leo jijini  Mwanza ambapo kesho (jumamosi) timu hiyo itashuka dimbani kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Toto Africans, kisha mara baada ya hapo siku ya jumapili Simba watakuwa Shinyanga ambapo shughuli itaanza kwa Kombe la Ubingwa kutembezwa tena katika mitaa mbalimbali mjini humo kisha baadaye jioni siku hiyo hiyo Simba itashuka dimbani uwanja wa Kambarage kucheza na mabingwa wa Uganda, The Express.
 Ng'aring'ari ya Simba na kipitashoto katikati ya jiji.

Wapenzi wa soka kanda ya ziwa hii si ya kukosa.

KUTOKA KWA MDAU: KCMC HAWANA TENA KITENGO CHA TIBA KWA MOYO.

Albert,
Salam.

Pongezi kwa first born wako kutimiza miaka 7.

Sasa, baada ya kusoma taarifa ya msaada kwa Yvona, niliiweka pia wavuti.com ambapo mtu mmoja aliisoma kupitia twitter na kushauri mtoto apelekwe Muhimbili kwa kuwa KCMC haina tena kitengo kinachohusika na matatizo ya moyo.

Nikawasiliana na daktari ambaye alinifahamisha kuwa ni kweli daktari aliyekuwa anahusika na kitengo hicho KCMC hayupo tena.

Daktari huyu ameshauri mtoto apelekwe Bugando na siyo Muhimbili kwa kuwa Bugando ndiyo wana kitengo hicho. Yeye mwenyewe alifanya kazi Bugando kwa muda na ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Tiba na Afya Muhimbili hivyo anazifahamu hospitali zote mbili, pia ni mzaliwa wa Kilimanjaro hivyo anao marafiki na anafahamiana na wahusika wa KCMC.
Kwa sasa yupo nje, Japan, masomoni.

---------- message ----------
From: Subi <subi@wavuti.com>

Blogu hii inaahidi kuliwasilisha kwa mzazi, na kuomba wadau waendelee kumsaidia mtoto huyu kwa kuwasiliana na baba wa mtoto kupitia 0754 724278 au 0782 946177

RAMADHANI SHAULI AONESHWA MKANDA WA UBINGWA WA IBF AFRICA ATAKAOGOMBANIA IDDI PILI


Bondia Ramadhani Shauli akiwa ameushika Mkanda wa I.B.F Africa wakati ulipokuwa ukioneshwa mbele ya waandishi wa habari baada ya kuwasili Dar es salaam jana ukitokea USA mkanda huo utakaogombaniwa na Shauli na bondia Sande Kizito kutoka Uganda utafanyika siku ya Iddi pili katika ukumbi wa Diamond Jubilee kushoto ni Makamu wa Rais wa Kamisheni ya Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) Madaraka Nyerere na Promota wa mpambano huoMkurugenzi wa Kitwe General Traders, Lucas Rutainirwa.


Bondia Nassibu Ramadhani kushoto na Ramadhani Shauli wakifungu mkanda wa ubingwa wa IBF Africa utakaogombaniwa na Ramadhani Shauli kushoto na bondia Sande Kizito kutoka Uganda.
 


Ramadhani Shauli akiwa na mkanda wa ubingwa wa IBF Africa.

Thursday, June 21, 2012

MISS UNIVERSE 2012 NATIONAL FINALS

Nani atakayemrithi mrembo Nelly Kamwelu katika fainali za Miss Universe 2012?
Mwaka 2007 alikuwa Flaviana Matata,2008 alikuwa Amanda Ole Sululu,Mwaka 2009 alikuwa Illuminata James,zamu ikawa kwa Hellen Dausen mwaka 2010.
Mwaka 2011 ilikuwa bahati ya Nelly Kamwelu kutoka Dar es Salaam.
Nani kuvikwa taji la Miss Universe baada ya Nelly Kamwelu?

MCHEZA SINEMA WA MAREKANI, DEIDRE LORENZO ATUA MJINI MOSHI NA SHAUKU KUBWA YA KUONA KAMA KWELI MLIMA KILIMANJARO UKO TANZANIA!

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mcheza sinema toka Marekani Deidre Lorenz amewasili mjini Moshi tayari kushiriki kwenye mbio za Mt. Kilimanjaro Marathon zitakazofanyika juni 24. Lorenz amwasili leo na ndege ya Ethiopian Airlines ambao ndio wafadhali wa mbio za Mt. Kilimanjaro Marathon zinazofanyika jumapili ya mwisho ya mwezi wa sita kila mwaka.
Deidre Lorenz na Rais wa IBF-USBA bala la Africa, Masharini ya Kati na Ghuba ya Uajemi Onesmo Ngowi (3)

Ujio wa Lorenz ambaye amecheza sinema nyingi zikiwamo Santorini Bule, Perfect Strangers, The Big Fight umeleta msisimko mkubwa katika mji huu mkuu wa Kilimanjaro. Ujio wake umefuatia matayarisho ya muda mrefu ambayo yanaendana na hadhi yake.

 Akizungumza na waandishi wa habari waliofika kumshuhudia mcheza sinema huyu, Lorenz alisema kuwa ameisikia kuwa mlima wa Kilimanjaro uko Kenya kwa kwa muda mrefu na ana furaha kubwa sana ya kufika ili kushughudia kuwa mlima huu maarufu duniani uko Tanzania. “Nimekuwa nautangaza sana ujio wangu kwenye blog na tovuti yangu, wapenzi wangu pamoja na watu wengi wanangojea kurudi kwangu nikawaambie niliyoyashughudia” alisema Deidre Lorenz ambaye ameshawahi kuteuliwa zaidi ya mara tatu kwa tuzo za Oscar. Lorenz alisema kuwa kwa miaka mingi alifikiri kuwa mlima Kiliamnjaro uko Kenya kwa jinsi nchi hiyo jiraniminavyoutangaza nchini Marekani.

 “Sasa nimeona mwenyewe kwa macho yangu kuwa kweli mlima (Kilimanjaro) huu maarufu duniani uko Tanzania na sio Kenya” alisema Deidre Lorenz ambaye anaishi kwenye jiji la New York City linalofahamika kama jiji la pesa (International Financial Capital) la kimataifa. Lorenz ameshukia katika hoteli ya Bristol Cottages iliyopo karibu na benki ya Standard Chattered mkabala na bustani ya Manispaa ya Uhuru Park.

 Mji wa Moshi na viunga vyake vinarindima kwa ujio wa watalii wengi kutoka Marekani ambao wamekuja kushiriki kwenye mbio hizi zilizojijengea umaarufu mkubwa kwa kuitangaza Tanzania nchini Marekani. Mbio za Mt. Kilimanjaro Marathon zilianzishwa na Marie Frances mwaka 1991 baada ya kuombwa na balozi wa zamania wa Tanzania nchini Misri.

 Mbio hizi zimejijengea umaarufu mkubwa na zimeshawahi kupata tuzo nyingi baadhi zikiwa zimetolewa na Wonders of the World Magazine lenye wasomaji zaidi ya milioni 5 likiwa limezipa nafasi ya 2 kama mbio zenye hadhi ya kukimbiwa duniani wakati jarida la Forbes la Marekani lenye wasomaji wengi duniani limeipa nafasi ya kwanza. Ndio maana Manispaa ya Moshi itampa barabara na kuiita “Marie Frances Boulevard”mwaka 2009.

 Mbio hizi hukimbiwa na watalii wa Warekani wanaokuja Tanzania kupanda mlima Kilimanjaro na kutembelea mbuga za wanyama. Mt. Kilimanjaro Marathon zinajulikana kama 7 continental races zikiwa zinakimbiwa katika mabara 7 ya dunia.

 Ratiba ya Deidre Lorenz inaonyesha kuwa kesho ijumaa atakitemnbelea kituo cha watoto yatima cha Upendo kinachoendeshwa na watawa wa Precious Blood. Lorenz atakaa na watoto hao na kuwasomea hadithi mbalimbali za watoto zilizoandikwa na Waltz Disney mwandishi maarufu wa karne ya ishirini wa Marekani.

 Siku ya jumamosi atatembelea hospitali ya KCMC ambapo atakutana na manesi ili kuwapa shavu kwa kazi yao nzuri wanayoifanyia jamii. Jioni ya jumamosi atahudhuria Pasta Party ambapo atapata nafasi ya kukutana na wakimbiaji wengine na kuchagua namba ya kukimbia kesho yake siku ya jumapili tarehe 24 juni.

Imetumwa na:

Grace Soka

Afisa Uhusiano

MTU MZIMA DAWA KULIPUKA@VILLA PARK MWANZA

NA MWANDISHI WETU

ONYESHO lililopewa jina la Mtu Mzima Dawa ambalo litafanyika Julai 6 (Ijumaa) kwenye Viunga vya Villa Park jijini Mwanza linatarajiwa kuwa bab kubwa.

Akizungumza jana Meneja wa Kundi la TMK Family ambao ndio wandaaji wa onyesho hilo, Said Fella amesema litakuwa onyesho la pekee ambalo halijawahi kutokea Mwanza.

“Onyesho la mtu mzima dawa kwenye Ukumbi wa Villa Park Julai 6, litakuwa bab kubwa sana, yaani itakuwa ni mlipuko,” alisema Fella.

“Tumeandaa wasanii wazuri wenye vyimbo zinazotamba sasa, ambao wamejipanga vyema kwa ajili ya kufanya makamuzi ya kuilipua Villa Park.”

Fella aliwataja wasanii watakaoshiriki kwenye onyesho hilo la usiku wa mtu mzima dawa kuwa ni Bibi Cheka, ambaye ndiye mhusika mkuu wa onyesho hilo.

Wengine watakaomsindikiza ni Chegge, Temba, Aslay kutoka TMK Family, Ommy Dimpoz, Mwana FA na Ferouz. Habari/www.kajunason.blogspot.com