ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, February 16, 2024

BARAZA LA MADIWANI CHALINZE LAPITISHA MAPENDEKEZO YA BL.54.6 KWA MWAKA 2024/2025


NA VICTOR MASANGU CHALINZE 


HALMASHAURI  ya Chalinze Wilayani Bagamoyo mkoani Pwani hatimaye  imepitisha mapendekezo ya bajeti ya kiasi cha shilingi bilioni 54.6 kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2024/2025.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Chalinze Ramadhani Possi wakati wa kikao maalumu cha baraza la madiwani  kwa ajili ya kujadili na kupitisha mapendekezo ya bajeti.

Possi alibainishwa kwamba bajeti hiyo ambayo imeweza kugusa katika nyanja mbali mbali imepitia vikao mbali mbali vya kisheria pamoja na kuwahusisha madiwani kutoka kila kata kwa lengo keleta maendeleo.

Mkurugenzi huyo alifafanua kwamba katika mapendekezo  ya bajeti hiyo fedha za ndani zitakuwa ni shilingi bilioni 17.3 luzuku kutoka serikalini kuu na matumizi ya kawaida ni bilioni 26.01.
"Mwenyekiti ninaomba baraza lako tukufu lipitishe mapendekezo ya bajeti hii ya bilioni 54.6 na kwamba itajumusha na mambo ya mishahara miradi ya maendeleo  pamoja na mahitaji mengine ya kiofisi,"alifafanua Possi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze Mhe.Hassan Mwinyikondo amewapongeza wataalamu pamoja na madiwani wote kwa kuweza kushirikiana kwa pamoja katika kuandaa mapendekezo ya bajeti hiyo.
Alisema kwamba kwamba hawezi kusita kuisifia bajeti hiyo kutokana na kuweza kugusa katika kila nyanja pamoja na kutoa fursa za maoni na mapendekezo ambayo yalikuwa yanatolewa kwa maslahi ya wanannchi.

"Kiukweli hii bajeti yetu imeweza kugusa kila nyanja  maana siku zote sisi madiwani kwa kushirikiana na madiwani tumekaa kuanzia asubuhi mpaka jioni nia na madhumuni kuyachukua mapendekezo yote ambayo yametolewa na kuyaingiza katika bajeti,",alisema Mwinyikondo.
Pia alisema kuwa bajeti hiyo itakwenda kuleta chachu kubwa ya mabadiliko katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo itakuwa ni faida kubwa kwa wananchi wa chalinze.

Mwenyekiti huyo aliongeza kubwa lengo kubwa la kupendekeza bajeti hiyo ni kuhakikisha inakwenda kuokoa maisha ya wananchi wa chalinze pamoja na kuibua miradi mipya ya maendeleo.

"Waandishi wa habari nadhani mnajionea nyinyi wenyewe kwa hivyo yale mazuri yote ambayo tunayatekeleza ni vema mkayaandika kutokana na mambo mazuri ambayo tunayatekeleza,"alisema Mwinyikondo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Halima Okash hakusita kuipongeza Halmashauri ya Chalinze kwa juhudi zake katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo.
Mkuu huyo alisema amefarijika kuona madiwani na wataalamu mbali mbali wanafanya kazi kwa pamoja katika kuhakikisha kwamba wanaweka mipango ya kutekeleza miradi ya maendeleo kupitia fedha za ndani.

Alisema mapendekezo ya bajeti hiyo yanatakiwa kusimamiwa ipasavyo ikiwa sambamba na kumsaidia Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan ili aweze kutimiza majukumu yake ipasavyo.

Nao baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Chalinze wameungana kwa pamoja kupitisha mapendekezo ya bajeti hiyo ambayo wamesema itakuwa ni mkombozi mkubwa kwa wananchi katika sekta mbali mbali.

Wednesday, February 14, 2024

TAHARUKI JESHI LA ZIMAMOTO LIKIZIMA MOTO JENGO LA NSSF TANGA

 

Mmoja wa watumishi wa NSSF Mkoa wa Tanga ambaye alipata majeruhi akibebwa kwa ajili ya kuwahishwa katika Hospitali leo




Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga Nuhu Mmbaga akiteta jambo na baadhi ya wateja wa mfuko huo mara baada ya kutokea tukio hilo

Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga Nuhu Mmbaga kushoto akimsikiliza kwa umakini Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tanga Abrahaman Ntezidyo







Na Oscar Assenga,TANGA.

TAHARUKI kubwa imeibuka kwa wateja na watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoani Tanga baada ya kuibuka kwa moto kwenye moja ya chumba kilichopo kwenye Jengo lao na hivyo kulazimika kuacha shughuli na kukusanyika eneo moja huku Jeshi la Zimamoto na Ukoaji likifika na kufanikiwa kuzima moto huo.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa zoezi la uzimaji wa moto huo Kaimu Makamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tanga,Mrakibu wa Jeshi hilo Abrhaman Ntezidyo alitibitisha kutokea kwa moto huo ambapo alisema ulitokea saa 4.4o asubuhi.

Alisema kwamba walipataa taarifa za uwepo wa moto huo ambao ulianza saa nne na dakika arobaini asubuhi baada ya kupokea taarifa ya wito kutoka Jengo la NSSF kuwepo kwa moto kwenye jengo ambao ulitokea kwenye moja ya chumba cha ofisi.

Alisema kwamba katika jengo hilo kilikuwa na vitu kadhaa ikiwemo thamani za ofisi na waliopata hizo walipofika eneo la tukio kutokana na uwepo wa purukushani kutokana na taharuki hiyo mmoja wa watumishi wa mfuko huo alipata majeruhi kutokana na kupata mshutuko na alipelekwa Hospitalini kwa ajili ya matibabu.

Hata hivyo alisema kwamba chanzo chaa tukio hilo bado hakijafahamika lakini kwa sasa wanaendelea kufanyaa uchunguzi ili kuweza kubaini sabaabu zilizopelekea kutokea kwa moto huo katika moja ya chumba kwenye jengo hilo.

“Tunamshukuru Meneja wa NSSF kwa kutoa taarifa kwa wakati kwa Jeshi letu na tukio hilo kutokana na kuwahi kufika hakuna madhara makubwa kilichohusika ni chumba kimoja cha ofisi ambacho kimeungua vitu vichache kutokana na kuwahi kuzibiti moto usisambae maeneo mengine”Alisema

Alitoa wito kwa wananchi wanapopata matukio ya moto waweze kutoa taarufa kwa mapema ili nao waweze kufika kwa wakati na kuweza kufanya maokozi ambapo pia akitoa pole kwa Meneja na mfanyakazi aliyepata majeruhi apone na kurudi kwenye hali yake ya kawaida.

Awali akizungumza,Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoa wa Tanga Nuhu Mmbaga alilishukuru Jeshi la Zimamoto na Ukoaji na vikosi vinavyohusika na majanga kuwahi kufika kwenye eneo la tukio kweli moto ulitokea na uliweza kudhibitiwsa kikamilifu.

Alisema lakini mfanyakazi mwenzao alipata madhara kidogo na kupelekwa Hospitali natukio hilo limetokea lakini wameweza kulihimili na ni njia mojawapo ya kuweza kuwa na utayari kuweza kuhimili majanga yanapojitokeza.

Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa yazindua promosheni ya Swahiba "Langu Lako"

 

Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa imezindua promosheni ya Swahiba "Langu Lako" inayolenga kuwahamasisha wananchi na wateja wa benki hiyo kunufaika na huduma mbalimbali ikiwemo SimBanking, Lipa Hapa na Hodari Account ambayo ni maalum kwa ajili ya wafanyabiashara.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo uliofanyika Jumanne Februari 13, 2024 jijini Mwanza, Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta amewamasisha wananchi kutumia huduma za benki hiyo ikiwemo Lipa Namba kwa ajili ya kulipia bidhaa malimbali badala ya kutembea na fedha taslimu.

"Tumekuja na akaunti ya Fahari Account kwa ajili ya wafanyabiashara ambapo inawawezesha kuweka na kutoa pesa bila makato huku ikiunganishwa na huduma ya Lipa Hapa ambapo wateja watalipia bidhaa. Pia ukifungua akaunti hiyo, unaweza kupata huduma za mikopo hivyo wafanyabiashara nawasihi kuchangamkia Hodari Account" amesema Sitta na kuongeza;

"Swahiba ni wewe rafiki yangu, ni wewe mteja wa benki ya CRDB hiyo tunataka kila mfanyabiashara ambaye ni Swahiba wa CRDB kufungua Hodari Account ili kunufaika na huduma ya lipa namba, kuweka na kutoa fedha bila makato pamoja na kupata mikopo hadi milioni 50" amesema Sitta.

Meneja Mwandamizi wa CRDB Huduma Mbadala (SimBanking), Mangire Kibanda amesema wateja wanaoendelea kutumia huduma za benki hiyo ikiwemo SimBanking wanayo fursa ya kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo gari, runinga, simu janja pamoja na kompyuta mpakato, ikiwa ni maana halisi ya wateja kuwa Swahiba na benko hiyo.

"Tunaposema Swahiba, Langu Lako tunamaanisha shida za mteja ni shida za benki ya CRDB ambayo ina mazingira sahihi ya kupata usuluhishi wa shida hizo" amesema Meneja wa CRDB Tawi la Mwanza, Medard Kayombo akisisitiza umuhimu wa kutumia huduma za benki hiyo.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akizungumza kwenye uzinduzi wa promosheni ya Swahiba, Langu Lako inayolenga kuhamasisha huduma za benki hiyo ikiwemo Lipa Hapa, Hodari Account na SimBanking.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akizungumza kwenye uzinduzi wa promosheni ya Swahiba, Langu Lako inayolenga kuhamasisha huduma za benki hiyo ikiwemo Lipa Hapa, Hodari Account na SimBanking.
Meneja wa CRDB tawi la Mwanza, Medard Kayombo akizungumza wakati wa uzinduzi wa promosheni ya Swahiba, Langu Lako.
Meneja Mwandamizi wa CRDB Huduma Mbadala (SimBanking), Mangire Kibanda akieleza namna wateja wa benki hiyo wanaweza kujishindia zawadi mbalimbali kwa kutumia huduma zake ikiwemo SimBanking.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (kushoto) akimkabidhi zawadi ya runinga Jackson Kapele (kulia) ambaye ni mtoa huduma aliyesajili wateja wengi wa SimBanking kwa mwaka 2023 jijini Mwanza.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (kushoto) akikabidhi cheti cha utambuzi kwa Jackson Kapele (kulia) ambaye ni mtoa huduma aliyesajili wateja wengi wa SimBanking kwa mwaka 2023 jijini Mwanza. 
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akiwa kwenye picha ya pamoja na watoa huduma wa benki hiyo baada ya uzinduzi wa promosheni ya Swahiba, Langu Lako inayolenga kuhamasisha wananchi na wateja wa benki ya CRDB kutumia huduma za benki hiyo.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akiwa kwenye picha ya pamoja na watoa huduma wa benki hiyo baada ya uzinduzi wa promosheni ya Swahiba, Langu Lako inayolenga kuhamasisha wananchi na wateja wa benki ya CRDB kutumia huduma za benki hiyo.
Benki ya CRDB imejipanga kuwafikia wafanyabiashara jijini Mwanza ili kuwasajili na Hodari Account itakayowawezesha kupokea malipo ya bidhaa wanazouza kupitia Lipa Namba/ Lipa Hapa, kuweka na kutoa fedha bila makato pamoja na kunufaika na mikopo mbalimbali hadi shilingi milioni 50 ili kukuza zaidi biashara zao ambapo promosheni hiyo ilianza mwezi Januari 2024 huku ikizinduliwa rasmi Februari 13, 2023 Kanda ya Ziwa.
SOMA ZAIDI>>> HABARI ZAIDI HAPA

WATAKIWA KUWA NA UTAMADUNI WA KUFANYA UCHUNGUZI WA AFYA YA KINYWA NA MENO MARA KWA MARA

 

 






Na Oscar Assenga, TANGA.


DAKTARI Mwandamizi wa Magonjwa ya Kinywa na Meno katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga, Dkt Onesmo Ezekiel amewashauri wananchi wa mkoa huo kuwa na utamaduni wa kufanya uchunguzi wa kinywa na meno mara bili kwa mwaka ili kuepukana na magonjwa mbalimbali yanayoweza kukutana nayo ikiwemo ya kung’oa jino

Dkt Onesmo ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Kinywa na Meno Katika Hospitali hiyo aliyasema hayo leo wakati akizungumza na mtandao huo ambapo alisema uchunguzi huo wanaweza kufanya bila hata kuumwa kwa sababu magonjwa ya kinywa na meno katika hatua za awali hayana dalili zozote.

Alisema ila dalili zinaanza kujitokeza wakati ugonjwa unakuwa tayari upo kwenye hatua za mbele zaidi hivyo unapokwenda daktari ukiwa na maumivu na kukuangalia kama kuna uwezekano wa kuzuia magonjwa ya kinywa na meno unakuta tayari umeshaathiri eneo kubwa na hivyo kuwa na uchaguzi mmoja wa kung’oa jino.

“Lakini niwaambie kwamba dalili za meno ukiziwahi kwenye hatua za awali inakuwa rahisi kufanya matibabu na gharama zake zinakuwa ni rahisi vyenginevyo utakwenda kwa daktari ukiwa na maumivu makubwa zaidi na hivyo kuwa na uchaguzi wa kungo’a jino”Alisema

Hata hivyo Dkt Onesmo alisema kwamba magonjwa hayo yanaathiri watoto na watu wazima hivyo kuwataka wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanazingatia suala la usafi wa kinywa na meno vizuri wasimamiwe watumie dawa ya mswaki yenye madini ya floride,calcium na karafuu .

“Lakini mswaki wanaoutumia usizidi zaidi ya miezi mitatu kwa sababu baada ya miezi hiyo unashindwa kufanya kazi zake kwa ufanisi huku asisisitiza umuhimu wa jamii kuhakikisha wanatunza vinywa vyao kwa kuzingatia kufanya usafi mara kwa mara”Alisema

Akizungumza kuhusu kitengo cha huduma ya Afya ya Kinywa na Meno katika Hospitali hiyo Dkt Onesmo alisema wanatoa huduma zinazohusiana na magonjwa ya kinywa na meno kila siku za Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa mbili na nusu mpaka saa tisa na nusu mchana.

“Pia wakati mwengine tunatoa huduma siku za wikiendi linapokuwa limejitokeza suala la uhitaji na kitengo chetu kina vitengo kadhaa ndani yake ambapo tunatoa huduma za meno bandia,kuziba meno,kusafisha meno,kufanya matibabu ya mzizi wa jino na kungarisha jino “Alisema

Alisema pia wakati mwengine wanalazimika kwenda chumba cha upasuaji inatpokea kuna mahitaji mfano wanapotokea wagonjwa wenye uvimbe ambao unahitaji kufanyiwa upasuaji mkubwa au wagonjwa wa ajali ambao matibabu yao ili kuweza kuwatibu wanapaswa kwenda chumba cha upasuaji.

“Tunafanya upasuaji mdogo ambao hauhitaji mgonjwa kulazwa bali isipokuwa ikiwekewa ganzi katika eneo husika anaweza kufanyiwa huduma hizo na kuruhusiwa“Alisema.

Hata hivyo alisema kwamba hospitali hiyo inapokea inapokea wagonjwa kutoka wilaya zote za mkoa huo na wanapata matibabu hapo na wachache wanalazimika kuwapa rufaa kwendfa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Akizungumzia magonjwa yanayowatesa wananchi wengi,Dkt Onesmo alisema magonjwa hayo ni kutoboka kwa meno ambao zaidi ya nusu ya wagonjwa ni tatizo kubwa na wengine ni fizi kutoka damu na yamekuwa yakiathiri watu wa umri zote.

“Kuanzia vijana,watoto hadi wazee wa jinsia zote wanakaribiana huku kundi jingine ni wale wanaopata ajali za kuvunjika taya la chini na la juu au yote mawili pamoja au kung’oka meno kwa ajili ya ajali ambazo zinahusisha bodaboda ambao wamekuwa wamelewa”Alisema

Tuesday, February 13, 2024

LOWASSA AAGWA DAR ES SALAAM.

 


Shughuli ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Lowassa inafanyika Jumanne mjini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa akiwamo Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango.

Viongozi mbalimbali wakuu wakiongozi na Rais wa Zanzibar Dr. Hussein Alli Mwinyi.

Picha kutoka maktaba.

Salaam za rambirambi zinaendelea kumiminika katika eneo la Karemjee ambako waombolezaji wamekusanyika kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa mwanasiasa huyo aliyezipamba siasa za Tanzania kuanzia ndani ya chama cha CCM na hata pale alipokwenda chama kikuu cha upinzani Chadema wakati wa harakati za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.


Viongozi wa kitaifa wakiongozwa na makamu wa rais, Dkt Philip Mpango ni sehemu ya waombolezaji hao, wakimlilia Lowassa aliyefariki dunia jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Kila anayepanda jukwaani amekuwa akitoa saalam na kumwelezea kiongozi huyo kuwa mtu aliyeziishi enzi zake na kutenda mambo kwa umakini mkubwa.


Lowassa alikuwa mvumilivu

Waziri Mkuu wa zamani, Joseph Warioba amekumbusha namna alivyokuwa ameshibana na kiongozi huyo akisema Lowassa alikuwa mtu mwenye misimamo na aliyependa kuchapa kazi kwa umakini mkubwa.

"Lowassa alikuwa mvumilivu sana na mimi niliendelea kuwa na uhusiano huo popote alipokuwa, alipokuwa katika CCM, alipokuwa katika serikali alipokuwa katika Chadema, aliporudi hata CCM, uhusiano wetu ulikuwa kama kaka na mdogo wake,"alisema Warioba.

Akizungumza wakati akitoa salamu zake za rambirambi, makamu wa rais Dkt Philip Mpango amesema taifa limempoteza kiongozi aliyekuwa hodari na aliyedhubutu katika kila jambo. Mbali na kutoa pole kwa familia ya kiongozi huyo, makamu wa rais pia alisema hiki siyo kipindi kigumu kwa familia pekee bali kwa taifa zima.

"Kwa kweli ni mmoja wa watoto mahiri sana wa mama Tanzania ambaye alijitoa kwa dhati kulitumikia taifa letu kwa moyo wake wote. Mheshimiwa Lowassa alitumia vyema karama ambazo alijaliwa na mwenyezi Mungu kuwatumikia Watanzania," alisema Mpango.

Wakati wa uhai wake, Lowassa alishika nyadhifa mbalimbalimbalindani ya CCM mpaka serikalini. Aliingia katika baraza la mawaziri wakati wa awamu ya pili ya utawala wa Rais Ally Hassan Mwinyi akiendelea hivyo mpaka wakati wa utawala wa hayati Benjamin Mkapa.

Alijiuzulu kama Waziri Mkuu

Aliteuliwa kuwa waziri mkuu wakati wa utawala wa awamu ya nne wa Jakaya Kikwete nafasi ambayo alidumu nayo kwa kipindi kifupi cha miaka miwili tu, akilazimika kujiuzulu baada ya kuandamwa na kashfa ya Richmond.

"Nadhani tatizo ni uwaziri mkuu kwamba ionekane waziri mkuu ndiye amefanya haya…ionekane kwamba waziri mkuu ndiye amefanya haya tumwondolee heshima au tumwajibishe ..mheshimiwa spika nimetafakari sana kwa niaba ya chama change, kwa niaba ya serikali yangu nimeamua kumwandikia barua rais ya kumwomba niachie ngazi," alisema Lowassa wakati huo.

Lowassa atazikwa mwishoni mwa wiki jimboni kwake Monduli mkoani Arusha, mazishi ambayo yataongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ambaye kwa sasa yuko ziarani Vatican.

"KIFO CHA LOWASSA HAKIWEZI KUSITISHA KUDAI HAKI ZA WATANZANIA" KUELEKEA MAANDAMANO YA CHADEMA MWANZA

 NA ALBERT G. SENGO/MWANZA

KUELEKEA Alhamisi ya tarehe 15 mwezi Februari 2024 siku ambayo Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) imeiteuwa kuwa ya kufanyika maandamano ya amani jijini Mwanza, napata nafasi ya kufanya mahojiano na wadau wa chama hicho waliopo kwenye maandalizi katika viwanja vya Furahisha. 1. Jeh ni ajenda zipi CHADEMA wanakwenda nazo katika maandamano yao jijini Mwanza? 2. Mnafanya Maandamano haya wakati Taifa likiwa kwenye simanzi ya kuondokewa na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Edward Lowassa, ambaye pia mnamo mwaka 2015 alikuwa mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, pengine hamuoni ingekuwa busara kupisha kwanza hilo liishe kisha mkaendeleza ajenda zenu? 3. Pengine inawezekana Maandamano yenu yakaingiza hoja Mpya ya kuenzi Demokrasia kama mnavyosema ama mtabaki na hoja zile zile ambazo mmekuwa mkizinadi?