ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, September 29, 2012

SHILATU AUKWAA UENYEKITI CCM NYAMAGANA, MASHA AUKWAA UJUMBE NEC TAIFA


Wakishow love Masha na Mabina.

Mkutano wa uchaguzi ulikuwa na hazina ya wapiga kura wa kutosha.

Wajumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa waliochaguliwa kutoka kulia ni Joseph kahungwa, Saimon Ntabi na Flora Magabe.

Eneo la mkutano huo wa uchaguzi.

Mwenyekiti mpya wa CCM Nyamagana Raphael Shilatu akiwa amebebwa juu kwa juu mara baada ya kutangazwa mshindi kwenye kinyang'anyiro cha ugombea nafasi hiyo.


Mwenyekiti mpya wa CCM Nyamagana Raphael Shilatu akitoa shukurani zake kwa wanachama wenzake sambamba na salaam.

Mwenyekiti mpya wa CCM Nyamagana Raphael Shilatu akiteta na Bw. Mabina ambaye naye anatetea nafasi yake ya  uenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza. 

Ni fursa kuteta bustanini Mjumbe aliyeshinda nafasi NEC Lawrance Masha na Dr. Wangabo 


ILALA NA KINONDONI KESHO KUONYESHANA UBABE FAINALI SAFARI LAGER POOL TAIFA ZINAZOFANYIKA MWANZA.

 Mashindano ya Safari Pool Taifa ambapo jiji la Mwanza kwa mara ya kwanza mwaka huu 2012  limepewa hadhi ya kuwa wenyeji yamefikia hatua ya fainali ambapo kesho jumapili washindi mmoja mmoja yaani Single kwa wanaume na wanawake na mshindi kwa timu watapatikana na kwenda kuzawadiwa medali zao na vitita vyao. 


 Mashindano hayo yaliyoshirikisha timu 16 za mikoa mbalimbali hapa nchini yameshuhudia wenyeji Mwanza wakitolewa kiulaini kwenye hatua za makundi na kuziacha timu za  Dar es salaam,  ziking'ara kwa kuzisambaratisha timu za vilabu toka mikoa mingine kwa makundi hatimaye Kinondoni na Ilala zimefanikiwa kutinga fainali.

Kinondoni imetinga fainali mara baada ya kupata ushindi dhidi ya Morogoro kwa fame 13-10, nayo timu ya Kayumba kutoka Ilala wao wametinga fainali kwa kuinyuka Arusha kwa fame 13-9.


Kwa upande wa Mchezaji mmoja mmoja yaani Single Safari Lager Pool Taifa Wanawake:- Cecilia Kileo wa Kilimanjaro ameingia fainali ambaye atacheza na Betty Sanga wa Mbeya. Kwa upande wa Wanaume:- Solomon Elias kutoka Mbeya ameingia fainali akitarajia kucheza na Athumani Selemani.

Mgeni rasmi katika kufunga Fainali za Safari Lager Pool Taifa hiyo kesho jumapili katika jiji la mwanza ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Wizara ya Habari na utamaduni Leonard Thadeo.
Wadau wakifuatilia kwa makini moja ya michezo ya nusu fainali ya Safari Lager Pool inayofanyika Monarch Holel wilayani Ilemela jijini Mwanza.

 Mchezaji kutoka timu ya mkoa wa Arusha Fayu Stanley akisukuma kipira kwenye mcchezo wa kumtafuta mshindi wa tatu na matokeo Arusha wameinyakuwa nafasi hiyo kwa kuikandamiza Morogoro fame 13-8. 


Aliy Said Aboubakari (kushoto) ambaye ni shabiki mkuu wa Kayumba 'Yeyo' toka Ilala jijini Dar es salaam akishow love na Team Captain wa Kayumba pool club Emanuel Loya.
Sikiliza majigambo ya Ilala na Temekekuelekea fainali ya Safari Lager Pool hapo kesho.

KALAMA NYILAWILA FRANSIC CHEKA USO KWA USO LEO JUMAMOSI


Na. Super D Boxing Coach

Francis Cheka
MIAMBA ya masumbwi nchini, bingwa wa Mabara Francis Cheka [SMG] na aliyekuwa bingwa wa Dunia Karama Nyilawila [Kapten] wanatarajia kupanda ulingoni leo tarehe 29/09/2012 kuoneshana umwamba.

Cheka na Nyilawila walitwangana mbambanmo wao uliofanyika morogoro ata hivyo ulizua utata baada ya mpambano wao kugubikwa na alama za mshangao ambalo cheka aliibuka na ushindi wa point  mashabiki kuhisika wa mabondia hao wanaogopana na kutafutana kwa mda mrefu watapoza kiu yao kwa mpambano huo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, promota wa pambano hilo Oswald Mlay alisema pambano hilo litapigwa katika uwanja wa PTA Sabasaba
.
Alisema pambano hilo litakuwa la raundi 12 uzito wa kg 72 ambapo leo wamepima uzito kwa ajili ya mpambano huo utakaoamua nani zaidi

Katika Mchezo huo kutakua na Uhuzwaji wa DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha wa mchezo huo mkoa wa kimichezo wa Ilala Rajabu Mhamila 'Super D' kwa ajili ya kuwapa mambondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi.

Ndani yake wakiwemo mabondia Floyd Mywether, Manny Paquaio, Amiri Khani, Mohamedi Ali, Mike Tayson David Haye na wengine ambapo kutakuwa na matukio ya mazoezi yao katika mataifa yao ikumbukwe kuwa ni mabingwa wa dunia. na kutakuwa na mapambano makubwa matano ya utangulizi.

Friday, September 28, 2012

TANZANIA INVESTMENT BANK LIMITED (TIB) YAFUNGUA TAWI LAKE LA KANDA YA ZIWA: MWANZA. KUWA KITOVU

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo (mwenye suti ya brown) akifungua rasmi tawi la Tanzania Investment Bank (TIB) mkoani mwake shughuli iliyofanyika leo mchana katika ofisi za huduma za benki hiyo zilizopo ndani ya jengo la PPF Plaza jijini Mwanza.


Hii ndiyo  Benki ya Uwekezaji raslimali nchini Tanzania (TIB)

The inshu..


Mara baada ya kutambulishwa huduma za kibenki zitolewazo na TIB Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo alihamasika kufungua akaunti kama inavyoonekana pichani.


Waalikwa na viongozi kwenye uzinduzi huo. 


Ngoma asili ilihusishwa...


Sehemu ya wadau waliojitokeza kushuhudia uzinduzi huo..


Benki ya TIB tawi la Mwanza itawanufaisha wateja wa mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Simiyu, Kigoma, Mara na Mwanza huku ikiendelea kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu  ambapo imelenga kutoa mikopo ya shilingi bilioni 1,099 kufikia mwaka 2015 ili wananchi wajikwamuwe toka lindi la umaskini.


Wafanyakazi wa Tanzania Investment Bank.


Mkurugenzi mwendeshaji wa Benki ya TIB Bw. Peter Noni ameiomba serikali kuongeza mtaji katika benki hiyo ili iweze kukidhi mahitaji ya wateja ambao mahitaji yao ni makubwa. 


Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akihutubia wananchi ndani ya uzinduzi huo..


Mc wa Uzinduzi huo Ephraim Kibonde wa Jahazi Clouds Fm hapa alitupa kibonzo kwa meza kuu watu....Kwa-kwa-kwa!!


Zawadi kwa mkuu wa mkoa toka benki ya TIB.


Akina dada wateja wa TIB walio alikwakwenye uzinduzi huo.


Picha ya pamoja na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, wafanyakazi wa TIB, uongozi na wageni viongozi meza kuu. 



BREAKING NEWS: CCM YAREJESHA HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA KWA KUSHINDA UMEYA NA NAIBU MEYA, NAO UCHAGUZI WA ILEMELA WAAHIRISHWA KUTOKANA NA PINGAMIZI LA MATATA

Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula kupitia CCM (katikati) akiwa na Naibu Meya John Minja (CCM) wakitambulishwa na Mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe baada ya kutangazwa washindi  kufuatia uchaguzi uliofanyika leo katika ukumbi wa halmashauri ya jiji la Mwanza.

 Kikao cha Uchaguzi cha Halmashauri ya Manispaa ya Nyamagana jijini Mwanza kimemchagua diwani wa Kata ya Mkolani Mh. Stanslaus Mabula wa CCM kuwa Meya wa jiji hilo mara baada ya kumshinda mshindani wake Charles Chinchibela wa CHADEMA aliyepata kura 8 ile hali Mabula akipata kura 11.

Ni picha ya pamoja Meya Mabula, mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga(katikati) na Naibu meya John Minja wakiwa katika ofisi ya Mstahiki Meya 


Diwani wa kata ya Kitangili Henry Matata (aliyevuliwa uanachama CHADEMA) akisalimiana na diwani mwenzake Marietha Chenyenge huku mkononi akiwa na hati ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza iliyozuia kufanyika wa Meya na Naibu Meya mpaka pale kesi iliyofunguliwa na diwani huyo kupinga CHADEMA kuteua wagombea wa nafasi hizo, kwa chati  mbunge wa jimbo la Ilemela Highness Kiwia (aliyesimama) akiwa bize na simu yake ya kiganjani, kabla ya kuahirishwa kwa uchaguzi wa Manispaa ya Ilemela.
Ikumbukwe kuwa leo kulikuwa na chaguzi mbili za Ma- Meya na Ma- Naibu wake wa Halmashauri ya jiji la Mwanza (Nyamagana) na Manispaa ya Ilemela, baada ya uchaguzi wa Nyamagana kumalizika na wajumbe wake kuondoka ukumbini  ili kuwapisha wajumbe wa wilaya ya Ilemela, nao waliketi katika ukumbi wa uchaguzi wakisubiri kushiriki uchaguzi wa kuteuwa Meya na Naibu Meya wao ambapo uchaguzi huo haukufanyika kufuatia diwani wa kata ya Kitangili kufungua kesi katika mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza kupinga kuvuliwa uanachama, kupinga kuenguliwa katika mchakato wa kuwania nafasi ya Meya hadi hapo uamuzi wa kesi yake utakapo tolewa, kutokana na kuwa na hati ya Mahakama inayomruhusu aidha kuruhusiwa kushiriki kupitia chama chake cha zamani (CHADEMA) au chama chake kutofanya uteuzi wa wagombea.

Aliyekuwa mgombea nafasi ya Meya wa Manispaa ya Ilemela Abubakar Kapera diwani kata ya Nyamanoro (kulia)   na kushoto kwake ni diwani wa kata ya Kirumba Danny Kahungu aliyekuwa akiwania nafasi ya Naibu Meya Ilemela  wote kutoka CHADEMA ndani ya ukumbi wa uchaguzi kabla ya uchaguzi wao kuahirishwa kutokana na zuio.

Kutoka kushoto ni aliyekuwa Meya wa jiji la Mwanza kabla ya jiji hilo kugawanywa kuwa Manispaa na Halmashauri, diwani Manyarere akiwa na diwani Rose Brown na diwani wa viti maalum ndani ya ukumbi wa Uchaguzi kutafuta Meya na Naibu wake Nyamagana.

Madiwani wa CCM wilaya ya ilemela kabla ya uchaguzi wao kuahirishwa.

Madiwani wa CHADEMA wakiwa na mbunge wao  wa wilaya ya Ilemela Highness Kiwia (katikati) wakisubiri taratibu za uchaguzi ambao hata hivyo haukufanyika.

Meya wa jiji la Mwanza (wa3kutoka kushoto) Naibu Meya (wa kwanza kushoto) wakiwa pamoja na Madiwani wa CCM wakimsikiliza mbunge wa viti maalum Maria Hewa (wa pili kutoka kulia) aliyekuwa akisema "Chama kimerudisha heshima yake katika jiji la Mwanza"
MAPOKEZI MAKAO MAKUU YA CHAMA MWANZA...
Nje ya ofisi za CCM kulikuwa na makaribisho ya kutosha kwa wanachama mbalimbali kujitokeza kumlaki Meya mpya na naibu wake.

Meya na naibu wake wakiwasili .....

Shangwe zikatawala kwa mtu wao...

Ni full raha, ni full kujiachia kwa wanachama wa CCM Nyamagana jijini Mwanza.

Hapa Meya aklikutana na Mwenyekiti wa Vijana mkoa wa Mwanza.

UPENDO ART EXHIBITION - DAR ES SALAAM



UPENDO Art Exhibition at the Goethe Institut in Dar Es Salaam from Oct 2 - Oct 19, 2012 from 8:00am to 5:00pm, Closed on Saturday and Sunday. Entrance is Free.
Directions: Goethe-Institut Tanzania, Alykhan Road No. 63, ahead of Jamatkhana Mosque, Upanga, Dar es Salaam.

Thursday, September 27, 2012

WANYANG’ANYI WAUAJI WA WALINZI WANASWA NA JESHI LA POLISI MWANZA WAKIWA NA MTUTU WA KIENYEJI

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Liberatus Barlow akionyesha silaha hiyo iliyotengenezwa kienyeji ikiwa na risasi sita za Short-gun inayohusishwa na matukio ya ujambazi ikiwa ni pamoja na tukio la kumuua mlinzi mmoja na kumjeruhi mwingine kwa kumpiga nondo kichwani maeneo ya Busweru kona Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza.


Silaha hiyo iliyotengenezwa kienyeji kwa ukaribu zaidi.

Silaha hiyo iliyotengenezwa kienyeji, risasi zilizokamatwa na RB ya polisi.

JESHI la Polisi Mkoani Mwanza limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu wa tukio la ujambazi wakiwa na silaha moja ya kienyeji ikiwa na risasi sita za Short-gun na kukili kufanya uhalifu na kumuua mlinzi mmoja na kumjeruhi mwingine kwa kumpiga nondo kichwani maeneo ya Busweru kona Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Liberatus Barlow akizungumza ofisini kwake amesema kuwa  jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata majambazi hao wanaohusishwa na tukio lililotokea Septemba 6 mwaka huu majira ya saa 9:00 usiku katika maeneo ya maduka mawili Busweru kona Kata ya Busweru Wilayani Ilemela ambapo watuhumiwa walimuua mlinzi mmoja Mwita Chariya(40) na kumjeruhi mwingine Mwita Wambura wote wakiwa wakazi wa Mabatini Wilayani Nyamagana.


Kamanda Barlow amesema kuwa baada ya tukio hilo jeshi la polisi liliunda kikosi kazi na kuanza msako wa kuwatafuta wahusika wa tukio hilo huku wakipokea ushirikiano wa raia wema kwa kutumia falsafa ya polisi jamii na ulinzi shirikishi ambapo mnamo Septemba 26 mwaka huu majira ya saa 7:30 walianda mtego na kufanikiwa kumkamata  moja kati ya watuhumiwa  Jonathan Fredrick mkazi wa Nyakato jijini Mwanza akiwa nyumbani kwake. 


Mtuhumiwa huyo baada ya kukamatwa aliwataja wenzake nalo jeshi la polisi likaweka mtego mwingine na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine wawili walio salia Mkubwa Rajab na Jonathan Athuman wote wakazi wa Mabatini.


Watuhumiwa hao licha ya kukiri kufanya matukio mbalimbali ya unyang’anyi wa kutumia silaha likiwemo hilo la kuua mlinzi waliwaonyesha mahala walipoficha silaha hiyo iliyotengenezwa kienyeji.  

AIRTEL YAZINDUA MINARA INAYOTUMIA SOLAR VIJIJINI



Wa kwanza ni injinia wa Airtel mkoani Iringa bw Joshua Kadege akitoa ufafafanuzi kwa mwenyekiti wa kijiji cha Kimande tarafa ya Pawaga-Jimbo la Isimani bw Anderson Mpululu jinsi mtambo wa mawasiliano uliowekwa na Airtel kijiji hapo unavyofanya kazi ili kurahisisha mawasiliano katika kijiji hicho.Airtel imeanza kufunga mitambo ya mawasiliano itakayotumia nguvu za  Nishati ya jua (solar) ili kufikisha mawasiliano katika maeneo ya vijijini, kati ni meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania bw Jackson Mmbando wakati wa hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika kijijini Kimande nje ya mji wa Iringa jana.

Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania akisisitiza jambo kwa Mwenyekiti wa kijiji cha Kimande tarafa ya Pawaga-Jimbo la Isimani bw Anderson Mpululu kuhakikisha wanaweka ulinzi shirikishi kulinda mtambo mpya wa mawasiliano unaotumia nishati ya jua uliowekwa na Airtel ili kufikisha  huduma bora ya mawasiliano kijijini hapo, wakwanza kulia ni Meneja Mauzo wa Airtel  Nyanda za juu kusini Bw, Beda Kinunda na kushoto ni Injinia wa Airtel mkoani Iringa bw Joshua Kadege. Hafla ya uzinduzi ilifanyika kijijini Kimande nje ya mji wa Iringa jana.


Kulia ni Meneja Uhusiano wa Airtel Bw Jackson Mmbando na bw Beda Kinunda Meneja wa  Mauzo wa airtel Mkoani Iringa wakiwa nje ya Mnara wa Airtel unaotumia nguvu ya Nishati ya jua (solar)  wakizungumza  na Mwenyekiti  wa kijiji cha Pawaga-Jimbo la Isimani bw Anderson Mpululu (shoto) mara baada ya Airtel kuzindua rasmi mnara wa mawasiliano unaotumia nguvu za Solar katika kijiji cha Kimande tarafa ya Pawaga-Jimbo la Isimani, Airtel imezindua mnara huo unaotumia nishati ya jua kwa lengo la kufikisha mawasiliano katika maeneo ya vijiji ambapo bado hakujafikiwa na umeme wa taifa.

Kulia ni Injinia wa airtel mkoani Iringa akimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa kijiji cha Kimande tarafa ya Pawaga-Jimbo la Isimani bw Anderson Mpululu anaedadisi ili kupata ufafanuzi wa jinsi mnara wa Airtel unaotumia Nishati ya jua (solar) unavyofanya kazi mara baada ya Airtel kuzindua mnara huo kijijini hapo jana

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Airtel yazindua Minara ya Mawasiliano inayotumia umeme wa Jua
. kupunguza changamoto za umeme vijijini
. kurahisisha mawasiliano madhubuti
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inayoongoza kwa kutoa huduma zenye wigo mpana zaidi imezindua minara yake inayotumia  Umeme unao tumia nguvu za nishati ya Jua katika kijiji cha kimande kata ya itunguru mkoani Iringa.  Uzinduzi huo ni moja kati ya mikakati ya Airtel kuhakikisha inaendeleza mipango yake ya kupanua upatikanaji wa mawasiliano katika maeneo mbalimbali nchini kirahisi, kupunguza gharama za uendeshaji na kuhamasisha utunzaji wa mazingira katika maeneo yenye minara yake nchini.
Akiongea wakati wa uzinduzi huo Mwenyekiti wa kijiji cha Kimande kata ya Itunungu Tarafa ya Pawaga Iringa Vijijini Bw, Andason Mpululu ameushukuuru uongozi wa Airtel kwa kuweza kukabili changamoto za mawasiliano kijijini hapo na kuwa sehemu ya uboreshaji wa uendeshaji wa biashara mbalimbali hasa za kilimo cha mpunga ambapo hapo awali upatikanaji wa soko ulikuwa mgumu sana kutokana na kutokua na mawasiliano thabiti kama ilivyo sasa.
“Kwa kupitia Mtandao na huduma ya Airtel money huduma za kifedha zimeboreshwa, zimekua karibu zaidi na kuwawezesha wafanyabiashara kupokea malipo ya bidhaa zao kirahisi, kwa gharama nafuu na bila usumbufu wowote. Nimatumaini yetu kuwa kwa kupitia umeme wa sola gharama za mawasiliano ya simu za mkononi yataaendelea kupungua na kuboreshwa zaidi na kuleta tija kwa wananchi hasa wenye kipato kidogo” alisema bwa Mpululu
Naye mkazi wa kata ya Itunungu bwana Jumanne Zuberi alisema “tunashukuru sana serikali kuwawezesha wawekezaji kuwekeza katika sekta ya mawasiliano na hivyo kufikiwa na mtandao wa Airtel. Hapo zamani upatikanaji wa mawasiliano ulikuwa ni changamoto kubwa hivyo kuwafanya wakazi wa kijiji hapa kutembea umbali mrefu kupata mawasiliano. Tunashukuru kwa sasa huduma za simu kijini hapa zimeweza kuboresha shughuli mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kuboresha usalama wa raia na mali zetu”.
Akiongea kwa niaba ya kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Meneja Uhusiano bw, Jackson Mmbando alisema” nia yetu ni kubadili matumizi ya mafuta ya diesel na generator kuendesha mitambo yetu ya mawasiliano na kutumia umeme wa nishati ya jua ambao utasaidia katika kutunza mazingira na kupunguza gharama za uendeshaji ambazo zitatuwezasha kutoa huduma kwa ufanisi Zaidi na kwa gharama nafuu ili kuwafikia watanzania wengi zaidi na kusogeza huduma mbambali za kijamii karibu na wananchi zikiwemo huduma za Elimu, Afya na Mawasiliano. Kazi kubwa kwa wananchi nikulinda huduma hizi na kuzitumia vizuri kwa shughuli za maendeleo vijijini”.
Mawasiliano ndio chachu ya maendeleo hivyo tunaamini kwa kutumia umeme wa jua hata gharama za uendeshaji zitapungua hivyo kuwezesha ktoa huduma zenye viwango vya juu kwa gharama nafuu kwa watumiaji na wateja wa Airtel nchini nzima aliongeza Mmbando”
Kampuni ya Airtel katika kurahisisha mawasiliano nchini inaendelea kufunga mitambo ya umeme wa sola katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo ya Tanga, Sumbawanga, Kigoma na mikoa mengine mingi. Mpaka sasa Airtel imefanikiwa kufunga mitambo minne inayotumia nguvu za jua katika mkoa wa iringa Iringa vijijini. Mpaka sasa Airtel inaongoza kwa kutoa huduma zenye wigo mpana na ina vijiji na miji 50 zaidi.